Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2024

SIMBA, AZAM ZAMGOMBEA LAMECK LAWI WA COASTAL UNION

Picha
Taarifa nilizozipata kutokea Mkoani Tanga ni kwamba mlinzi kitasa wa Coastal Union, Lameck Lawi ana mkataba wa miaka miwili na mabingwa hao wa zamani wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara. Kwa maana hiyo Azam FC na Simba SC zimeonyesha nia ya kumhitaji nyota huyo watalazimika kuvunja mkataba wa nyota huyo jambo ambalo Coastal Union wanajiandaa kuvuta mkwanja mrefu kwelikweli kama ilivyokuwa Kwa Bakari Nondo na Abdul Sopu.

KAMBOLE AIPONZA YANGA, YAFUNGIWA NA FIFA

Picha
FIFA imewafungia Yanga ya Tanzwnia kufanya usajili wa Kimataifa hadi watakapomlipa Lazarus Kambole ambae anadai fidia ya kuvunjiwa mkataba wake na malimbikizo ya mshahara TFF nao wameifungia Yanga kufanya usajili wa ndani kutokana na kosa hilo

KITUNDA AKABIDHIWA STAND UNITED

Picha
Na Prince Hoza Kocha wa zamani wa timu ya Korosho ya Tunduru mkoani Ruvuma, Seleman Kitunda amekabidhiwa kikosi cha Stand United ya Shinyanga na sasa amepewa majukumu ya kuipandisha daraja msimu ujao. Kocha huyo anasaidiwa na Kitwana Tambwe ambao wote wamepewa majukumu ya kuhakikisha timu hiyo inarejea Ligi Kuu bara msimu ujao. Kitunda na Tambwe wameanza kazi hivi karibuni lakini wote kwa pamoja wanahakikisha timu hiyo inamaliza Ligi kwenye nafasi nzuri Seleman Kitunda (kushoto) akiwa na mwandishi wa habari hizi

MGUNDA AKARIBISHWA NA SARE YA 2-2

Picha
Timu ya Namungo FC ya Ruangwa mkoani Lindi imeilazimisha sare ya mabao 2-2 Wekundu wa Msimbazi, Simba SC mchezo wa Ligi Kuu bara uliofanyika uwanja wa Majaliwa mjini Ruangwa. Simba walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia Willy Onana dakika ya 33 kabla ya Namungo kisawazisha kupitia Kevin Sabato dakika ya 39, hadi mapumziko timu hizo zilifungana 1-1. Kipindi cha pili Simba waliandika bao la pili kupitia Edwin Balua dakika ya 70 kabla ya Namungo kisawazisha dakika ya 89 hasa baada ya kipa wa Simba kujifunga. Kwa matokeo hayo Simba inaendelea kusalia nafasi ya tatu ikiwa na pointi 47 ikicheza mechi 22, matumaini ya kukwea nafasi ya pili ili ipate tiketi ya kushiriki Ligi ya mabingwa Afrika msimu ujao ni ngumu kwani Yanga na Azam zipo juu yake. Hii ni mechi ya Kwanza kwa kocha Juma Mgunda aliyechukua nafasi ya Abdelhak Benchikha aliyetangaza kuachana na klabu hiyo

LOMALISA AOMBA KUONDOKA YANGA

Picha
Beki wa kushoto klabu ya Yanga, Joyce Lomalisa ameupa taarifa Uongozi wa klabu ya Yanga kuwa anahitaji kuondoka klabuni hapo mwishoni mwa msimu huu ambapo atakuwa Mchezaji huru ( Free agent ). Licha ya kupewa ofa na klabu ya Yanga ya mkataba wa mwaka mmoja kuendelea kuwatumikia Wananchi, amesisitiza kuondoka na ana ofa 3 rasmi kubwa zaidi kutokana klabu za Morocco, Libya na Tanzania. Kutokana na hilo klabu ya Yanga itaingia sokoni hivi karibuni katika dirisha lijalo la uhamisho ili kupata mchezaji ambaye atajiunga na klabu hiyo kuongeza nguvu eneo la pembeni.

RASMI PACOME KUWAVAA TABORA UNITED KESHO

Picha
Baada ya Kukaa nje ya uwanja kwa muda mrefu kutokana na majeraha ni rasmi Kiungo Pacome Zouzoua amefanya mazoezi jana pamoja na wachezaji wenzake kujiandaa na mchezo dhidi ya Tabora United siku ya Jumatano. Pacome aliumia katika mchezo was Ligi Kuu bara dhidi ya Azam FC ambapo Yanga ililala kwa mabao 2-1 na tangu alipoumia hajaonekana tena huku kukiwa na kila aina ya fununu zinazovuma juu yake

SIMBA QUEENS YASHUSHA VIPIGO LIGI YA WANAWAKE

Picha
JKT Queens imekubali kichapo cha kizalendo cha 2-0 kutoka Kwa Simba Queens katika mchezo wa lIgi Kuu ya Wanawake Tanzania bara uliopigwa Leo na kuifanya Simba Queens kufikisha alama 37 na kuwaacha mbali zaidi JKT Queens wenye alama 28. Hapo awali JKT Queens ilikumbana na adhabu ya kupokwa alama Tano mara baada ya kutopeleka Timu Uwanjani hapo ndipo paliopanzia kuwepo na ugumu Kwa JKT Queens kutetea ubingwa. Ikiwa ni raundi ya 13 ya Ligi mpaka sasa matumaini ni madogo Kwa JKT Queens kutetea ubingwa wao huku ukilinganisha na kasi ambayo Simba Queens wamekuwa nayo.

GAMONDI ASEMA HAWAENDI UWANJANI KUSHINDA MABAO MATANO

Picha
Kocha wa Yanga SC Miguel Angel Gamondi amesema hawajawahi kutoka Avic Town na wakasema wanaenda kushinda mabao matano isipokuwa inategemeana na makosa ya mpinzani wao. “Hatujawahi kutoka kambini tukasema tunakwenda kuwafunga wapinzani mabao matano, kushinda mabao mengi inategemea na makosa gani mpinzani ameyafanya dhidi yetu, tuna staili ya soka letu namna ya kutafuta ushindi, kitu muhimu kwetu ni kushinda kwa kupata pointi tatu na kucheza soka la kuvutia,” . “Angalia mechi ya juzi ingewezekana kushinda mabao mengi, wapinzani wetu walijua wanakuja kukutana na timu gani wakaamua wote kucheza nyuma ya mpira bado haikuwa shida tulitawala mchezo na kutengeneza nafasi nyingi za kufunga.” Miguel Gamondi kocha wa Yanga

KOCHA WA FULHAM KUMRITHI BENCHIKHA

Picha
Kocha Omar Najhi anatazamiwa kuteuliwa kuwa kocha mkuu mpya wa Simba SC mkataba umekamilika. Makubaliano yametiwa muhuri usiku wa kuamkia leo kwa mkataba wa miaka miwili - na atahudumu hapo hadi Juni 2026 kama Omar Najhi alivyokubali. Simba SC imechukua hatua hiyo ya kuziba pengo la Abdelhack Benchikha aliyeondoka klabauni hapo siku ya jana. Mazungumzo na kocha aliyekuwa kocha wa vijana wa Fulham na kocha msaidizi wa Wydad casablanca ya Morocco ambaye atasaini mkataba baadaye wiki hii. Mrithi wa Abdelhak Benchikha

AMAZULU YAMFUATA SKUDU MAKULUBELA

Picha
Timu ya Amazulu ya Afrika Kusini inamfuatilia kwa karibu Mchezaji wa Young Africans Skudu Makudubela mwenye miaka 34 Ili kuipata Huduma yake msimu ujao. Mchezaji huyo wa zamani wa Club ya Marumo Gallants mkataba wake na Young SC unatamatika mwishoni mwa msimu huu. Amazulu Kwa sasa inanolewa na Kocha wa zamani wa Club ya Simba Pablo Franko Martin.

SIMBA YAMWEKEA MKATABA WA MWAKA MMOJA SIMBA

Picha
Klabu ya Simba ilimuwekea mkataba wa mwaka mmoja Kiungo wao Mshambuliaji, Clatous Chama kuendelea kuitumikia klabu hiyo hadi June 2025 kwakuwa mkataba wake na Wekundu wa Msimbazi unamalizika mwishoni mwa msimu huu. Clatous Chama ana ofa rasmi 3 zilizopo kwenye Menejiment yake, ofa zilizopo ni kutoka klabu ya Simba, Yanga na Red Arrows na ofa anayoipa kipaumbele zaidi ni ofa kutoka Yanga kuanzia vipengele vya kimkataba zaidi ya Simba. Menejiment ya Clatous Chama itakaa mezani na mteja wao ili kuangalia ni ofa ipi anastahili kuipokea na kusaini kandarasi kuelekea msimu ujao, bado Menejiment haifanya maamuzi ya mwisho pia maamuzi ya mwisho yatafanyika hivi karibuni.

PYRAMIDS YAPIGA HODI TENA YANGA

Picha
" Pyramid FC itatuma ofa yake ya Pili ya kumuhitaji Nyota wa Yanga na Burkina Faso Ki Aziz Stephane (28) ambaye kwa sasa ni Mwiba kwa wapinzani wa Yanga Ofa ya Kwanza ya Pyramid FC ilikuwa na thamani ya Billion 1.498.670.000 Yanga waliipiga Chini ofa hiyo na kumpa Ki Aziz Stephane Mkataba Mpya ambao utamuweka Yanga Mpaka 2026 Mpaka sas Ofa za Kumuhitaji Ki Aziz. Zimefika sita (6) ✺ Pyramid FC ─ 1.4 Billions ✺ Orlando Pirates ─ 800 Millions ✺ Super Sports Club ─ 700 Millions ✺ Far Rabat ─ 980 Millions ✺ Azam FC ─ 700 Millions ✺ Cape Town City ─ 770 Millions "Yanga imezikusanya Ofa izo na kuanza kuzipitia moja Baada ya Nyingine huku Tayari wakiwa wamempa Mkataba Mpya kiungo huyo . (Top Score wa Ligi Kuu)

Usilolijua kaka yake Mbwana Samatta kumbe kwipandisha Ligi Kuu Kengold

Picha
Kaka wa Mbwana Samatta, Mohamed Samatta amesaidia kuipandisha Daraja la Ligi Kuu Bara msimu ujao timu ya Ken Gold ya Mbeya. Mohamed Samatta anayecheza nafasi ya kiungo mshambuliaji alikuwa na msimu bora na kikosi hicho katika Mashindano ya Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) msimu huu. Kabla ya kiungo huyo hajajiunga na timu hiyo amewahi kuzitumikia timu za Mbeya City, KMC, Mbagala Market na African Lyon.

INJINIA HERSI AZUNGUMZIA SAKATA LA PACOME

Picha
"Jana nimeulizwa na Mzee wangu Jakaya vipi kuhusu Pacome? Yaani imetengenezwa stori moja ya uongo uongo tu" "Wanasema ni kwasababu kuna kesi FIFA, sijui Yanga wasimtumie mchezaji kwasababu watakatwa point, ni vitu vya kipuuzi tu" "Kuna vitu vingine ukivisikia havi-make sense, mara sijui hana vibali vya kukaa nchini" "Huyu mchezaji anacho kibali cha kukaa nchini, huyu mchezaji amepata leseni ya TFF, huyu mchezaji amepata leseni ya CAF, amecheza mechi za Ligi na mashindano ya CAF na akapata majeraha" "Alivyoitwa timu ya Taifa ya Ivory Coast tulikubaliana kwamba huyu mchezaji aende kwasababu ya kulinda nafasi yake, lile taifa lina wachezaji wengi sana duniani kote"

SIMBA YAANZA NA MOHAMED CAMARA

Picha
Taarifa zilizonifikia zinaeleza kuwa tayari Simba SC imefikia makubaliano na Hafia FC ya nchini Guinea juu ya kumsajili kiungo Mohamed Damaro Camara raia wa Guinea. Nyota huyo atajiunga na Simba SC kwenye dirisha kubwa la usajili na anatajwa kuwa anakuja kutibu tatizo la eneo la kiungo wa chini ndani ya Msimbazi. Na tayari Hafia wamekamilisha usajili wa kiungo mwengine Ibrahima Sory Camara kwa ajijili ya kuziba pengo la Mohamed Damaro Camara.

MAPYA: KOCHA WA KMC KUINOA SIMBA MSIMU UJAO

Picha
Licha ya kudaiwa Juma Mgunda anaweza kumrithi kocha Benchikha aliyevunja mkataba. Simba SC inaangalia uwezekano wa kumpata Kocha Mkuu wa KMC, Abdi Himid Moalin kwenda kocha wa Mkuu wa timu hiyo mpaka mwisho wa msimu huu. Na uongozi tayari upo kwenye mazungumzo ya kumshawishi msomali huyo kuchukua mikoba ya Abdelhak Benchikha ambae anajiandaa kuachana na timu hiyo muda wowote kuanzia sasa. Inaelezwa kuwa Abdelhak Benchikha hatokuwa sehemu ya timu itakayosafiri kuelekea Ruangwa kwenye mchezo wao dhidi ya Namungo FC.

HANS PLUIJM KUIBUKIA KENGOLD

Picha
Kocha wa Zamani wa Yanga na Singida Big stars Hans Van Der Pluijm ameonyesha hamu ya kutaka Kurejea Tanzania na kuhudumu kama mkurugenzi wa Ufundi kwenye klabu ya Ken Gold FC ambayo Imejihakikishia kushiriki ligi kuu ya Tanzania Bara msimu ujao wa 2024/25. Kupitia chapisho lake kwenye ukurasa wake wa kijamiii wa Facebook Kocha Pluijm aliandika "Nawapa pongezi klabu ya Ken Gold FC , Ndio naweza kufanya kazi lakini kama mkurugenzi wa Ufundi kusaidia walimu"Ameandika Pluijm akijibu moja ya swali alipoulizwa kama anaweza Kurejea Tanzania kufundisha soka. Pluijm ni Mwalimu wa Soka mwenye Uzoefu mkubwa na Soka la Tanzania Kwa zaidi ya Miaka 5 amehudumu kwenye Vilabu tofauti kuanzia kama kocha mkuuu akiwa Yanga, lakini aliwahi kuhudumu kama Mkurugenzi wa Benchi la Ufundi akiwa na Singida Big stars.

PACOME KUIPONZA YANGA

Picha
Hii ngoma ni nzito sana matarajia yao kesi hii itafufuka baada ya ligi kuisha,kinachofanyika ni kukausha kimyakimya ili wadau wasijue.According to FIFA Young Africans Sports Club wanamtumia Mchezaji bila kufata taratibu za Uhamisho. Kwamujibu Wa Sheria za FIFA Yanga anatakiwa kupokwa points au kushushwa daraja kabisa.Mchezaji anayefichwa hapa ni Pacome Zouzou,na baada ya hii Taarifa kutolewa Sasa Hivi Yanga wanaogopa kumtumia Tena.Hapa ilikuwa inatakiwa TFF walishughulikie hilo swala haraka lakini nao wamekaa kimya kuwalinda Yanga. Viongozi wa Vilabu Vyote walikuwa wadai point zao kwakufatilia huko @tanzania football federation kama itashindikana basi waende FIFA. Maajabu ni Kwamba Viongozi wa Vilabu nao wamekaa kimya. Wakina Popat, Try Again wamekaa kimya hawaoni kuwa hii Fursa kwao kama watapokwa point wanaweza kuwa mabingwa. Hii kesi ya Yanga ni kubwa sana itakapokuja kufufuka watakuwa katika Wakati mgumu sana.Time will tell

PAMBA YAREJEA LIGI KUU BARA

Picha
-Hatimaye baada ya miaka 23 timu ya Pamba Jiji FC ya Mwanza imefanikiwa kupanda Ligi Kuu ya NBC baada ya leo kushinda kwa magoli 3-1 dhidi ya Mbuni FC ya Arusha. Pamba wameungana na Kengold FC ya Mbeya kupanda Ligi Kuu bara msimu huu moja moja . huku Mbeya Kwanza na Biashara United ya Mara zitacheza play off ya kutafuta nafasi ya kupanda Ligi Kuu bara .

MGUNDA KUMRITHI BENCHIKHA

Picha
Kocha wa timu ya wanawake ya Simba Queens Juma Mgunda anatajwa kuchukua mikoba ya kocha wa timu ya wanaume ya Simba SC Abdelhak Benchikha raia wa Algeria. Mapema leo kocha Benchikha amedaiwa kuachana na Simba na ametangaza kurejea kwao Algeria. Kocha huyo hana furaha akiwa na kikosi hicho hivyo anataka kuachana na timu hiyo, Mgunda anatajwa kuchukua nafasi kwani kuna ukweli kwamba Benchikha amevunja mkataba. Mgunda sasa atasaidiwa na Seleman Matola na tayari viongozi wa klabu hiyo wameshafanya mazungumzo na Mgunda

SIMBA MABINGWA WA MUUNGANO

Picha
Hatimaye Simba SC imefanikiwa kutwaa ubingwa wa kombe la Muungano baada ya usiku huu kuifunga Azam FC bao 1-0 katika mchezo wa fainali uliofanyika uwanja wa New Amaan mjini Zanzibar. Hilo litakuwa taji la pili kwa Simba msimu huu baada ya kutwaa Ngao ya Jamii lakini ni taji la kwanza kwa kocha Abdelhak Benchikha. Bao pekee la Wekundu hao wa Msimbazi limefungwa dakika ya 78 na kiungo mkabaji Babacar Sall, Simba iliutawala mchezo huo na kama si bahati mbaya ingeweza kupata ushindi mkubwa tangu mapema. Kitendo cha Azam kumkosa mshambuliaji wake hatari Mzimbabwe Prince Dube kuliifanya timu hiyo kuwa dhaifu na kuwafanya Simba kutokuwa kwenye hatari kubwa

GUEDE AISOGEZA YANGA KARIBU NA UBINGWA

Picha
Bao pekee lililofungwa kipindi cha pili na mshambuliaji wa kati Joseph Guede raia wa Ivory Coast limeiwezesha klabu ya Yanga kuondoka na pointi zote tatu baada ya kuifunga bao 1-0 Coastal Union ya Tanga mchezo wa Ligi Kuu bara uwanja wa Azam Complex jijini Dar ea Salaam. Kwa ushindi huo Yanga inaendelea kuongoza ligi hiyo ikifikisha pointi 62 na michezo 24 ikizidi kuziacha nyuma wapinzani wake Azam FC na Simba SC ambazo zinakutana kwenye mchezo wa fainali ya kombe la Muungano huko Zanzibar usiku huu. Hata hivyo Coastal Union imefungwa bao kipindi cha pili tena ni baada ya kutolewa kwa kadi nyekundu beki wake Lameck Lawi baada ya kumshika Stephanie Aziz Ki

EDO KUMWEMBE AWASHANGAA SIMBA KUCHEKELEA KUFUNGWA NA YANGA GOLI CHACHE

Picha
Mchambuzi wa masuala ya soka nchini, Edo Kumwembe awechana klabu ya Simba akisema ni aibu kubwa kufurahia kufungwa bao chache na watani zao Yanga Sc. Edo amesema hayo baada ya Simba kukubali kichapo cha bao 2-1 huku hofu yao ilikuwa ni kufungwa bao nyingi kama ilivyokuwa duru ya kwanza kutokana na ubovu qa kikosi chao. “Sasa msimu umemalizika dhahiri kwa Simba. Sioni namna gani Simba wakichukua ubingwa kwa pengo la pointi lililopo. Baada ya Azam kucheza dakika 90 na za nyongeza dhidi ya Mashujaa bila ya kufunga bao lolote Ijumaa usiku sioni namna gani Yanga wanaweza kuzuiwa wasitwae ubingwa. “Swali ni namna gani Simba watarudi msimu ujao. Wamejifunza kitu au wataendelea kumdharau Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said? Watafumua kikosi chao cha utawala wa timu? Watarekebisha mipango yao ya usajili wa timu na kuleta wachezaji wenye hadhi ya Simba katika kikosi? Ni suala la kusubiri kwa sasa.. “Tupo Aprili. Mvua zinanyesha. Tusubiri Aprili ya mwakani kuona Simba itakuwa wapi. Kuona itakuwa im

CHAMA AWATULIZA WANASIMBA

Picha
Kiungo Mshambuliaji wa Simba SC, Clatous Chama, amewasihi mashabiki wa timu hiyo kuendelea kuwapa moyo wachezaji licha ya kikosi chao kupitia wakati mgumu. Simba SC hivi sasa imekuwa ikipitia kipindi kigumu, ambapo imeshatolewa katika michuano miwili mikubwa huku katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara ikiwa imepitwa Pointi kadhaa na kinara Young Africans. “Hata sisi tunaumia kutokana na kipindi hiki tunachopitia kwa sasa. Ni kipindi cha mpito kwetu, tutakaa sawa na kuendelea kuwapa furaha (mashabiki), kikubwa ni kuhakikisha mashabiki wanatusapoti vya kutosha tuweze kufanya vizuri,” amesema CHAMA. Leo Simba itajitupa uwanjani kusaka Kombe la Muungano mbele ya Azam uwanja wa New Amaan Stadium Zanzibar

KENGOLD YABISHA HODI JANGWANI

Picha
Klabu ya Kengold iko kwenye rada za kuwania saini ya kiungo mshambuliaji Farid Mussa ambaye amekuwa hapati nafasi mara kwa mara ndani ya Yanga SC. Farid Mussa anatarajiwa kusaini Mkataba wa miaka miwili na miamba hao waliopanda ligi kuu kwa Msimu ujao. Ikumbukwe Farid Mussa Malik yuko chini ya management ya Oscar Oscar.

TUMEJIPANGA KUSHINDA- MATOLA

Picha
Kocha msaidizi wa Simba SC Seleman Matola amejinasibu kushinda kwenye mchezo wa fainali ya kombe la Muungano utakaofanyika uwanja wa Amaan Zanzibar Jumamosi. Simba itacheza na Azam ambapo Mstola amedai itakuwa mechi ngumu ambapo lolote linaweza kutokea, lakini Simba itaibuka na ushindi. "“Itakuwa mechi ngumu, Azam ni timu bora lakini tumejipanga kuhakikisha tunashinda. Hii ni fainali na siku zote haiwezi kuwa nyepesi kwahiyo tumejipanga kuwakabili.”- amesema kocha Msaidizi, Seleman Matola.

BARBARA HATIHATI KURUDI SIMBA

Picha
Klabu ya Simba SC imeanza mchakato wa kumtafuta CEO mpya baada ya Iman Kajula kujiuzulu siku chache zilizopita. Barbara Gonzalez amekataa kurudi ndani ya klabu ya Simba baada ya Mangungu kukataa kujiuzulu. Mangungu amesema hawezi kujiuzulu sababu yeye amechaguliwa na wanachama na amesema wasubirie mpaka mkutano mkuu wa Wanachama Simba imepanga kutangaza mabadiliko ya safu ya uongozi baada ya msimu huu kumalizika. Viongozi wa Klabu ya Simba bado wanaimani na kocha wao Benchikha na wamemuahidi kumpa ushirikiano kwa mechi zilizobaki na kuanzia msimu ujao

KINACHOMWONDOA BENCHIKHA SIMBA HIKI HAPA

Picha
"Nimeomba kuondoka klabu mwishoni mwa msimu huu kutokana na sababu zangu binafsi (kifamilia) nahitaji kuwa nyumbani Algeria." "Ligi ya hapa sidhani kama itaweza kunipa thamani pia nahitaji kubeba ubingwa wa afrika kitu ambacho hakiwezekani kutokana na aina ya timu niliyonayo." Kocha Abdelhak Benchikha

CHAMA AHUSISHWA KUSAINI MKATABA WA AWALI YANGA

Picha
Hii baada ya ukimya wa Viongozi wa Simba wa mda mrefu kuhusu kuongeza mkataba wake Simba, Kuna kiongozi wa Yanga ambaye anapambana kulifanikisha dili hili.. Taarifa za kusaini mkataba wa awali na Yanga zimevuja hadi kwa Uongozi wa simba na Sasa wanapambana ku extend mkataba wake. Hata hivyo bado hawajakaa mezani na Mchezaji ili kujadili vipaumbele vya Mchezaji anavyohitaji katika mkataba mpya. Wakati huo huo Chama stakosekana kwenye mchezo wa fainali ya kombe la Muungano dhidi ya Azam FC

MPIGA PICHA MILLARD AYO AFARIKI DUNIA

Picha
Mpiga Picha na Mwandishi wa Habari wa Emillardayo Bayotv_ Noel Mwingila (Zuchy) amefariki dunia Alfajiri ya leo Baada ya Kupata ajali ya Pikipikii Maeneo ya Makonde - Mbezi, Dar es salaam. Zuchy ni mmoja mwa wapigapicha Mahili kwenye Tasnia ya Habari na alifanikiwa kufanya kazi na watu mbalimbali. Kwa taarifa iliyotolewa na mtu wa karibu ameeleza kuwa ajali hiyo imetokea majira ya saa tisa usiku Zuchy enzi za uhai wake

PACOME KUONDOKA YANGA

Picha
Sasa hizi ni zandaaani kabisa, taarifa zinasema Mwamba alipona kabla ya Yao Kouassi na angeweza kucheza mechi ya Marudiano dhidi ya Mamelodi kule kwa Madiba. Hivi tayari wakala wake Zambro Traore yupo dar kutatua mgogoro, kama mambo yataenda vizuri Mwamba atabaki ila ikiwa tofauti basi msimu ujao sio Mwananchi tena.

WATANO WAPYA WA GAMONDI HAWA HAPA

Picha
Baada ya Miguel Gamondi kukabithi ripoti kwa uongozi wa klabu ya Yanga kuhitaji kusajiliwa wachezaji 5 katika msimu ujao na baadhi ya wachezaji wanaomaliza mikataba yao waongezewe mikataba na mpaka sasa Uongozi wa klabu ya Yanga ya imeanza mazungumzo na wachezaji hawa. 1. Beno Kakolanya-Singida Fountain Gate 2. Yusuph Kagoma- Singida Fountain Gate 3. Frank Carlos Zouzou- Asec Mimosas 4. Serge poku- Asec Mimosas 5. Khanyisa Mayo- Cape Town. Mpaka sasa klabu ya Yanga itawaongezea wachezaji hawa wanaomaliza mikataba yao. 1. Djigui Diarra 2. Bakari Mwamnyeto 3. Clement Mzize. 4 . Stephanie Aziz Ki. Na wengine wataboreshewa mikataba yao kutokana na kiwango nzuri walichokionyesha,Yanga imepanga kumaliza usajili mapema ili kuruhusu utambulisho ufanyike mapema kabla ya Ligi Kuu kuanza.

AZAM YAIFUATA SIMBA FAINALI YA LIGI YA MUUNGANO

Picha
Timu ya Azam FC usiku huu imetinga fainali ya michuano ya Ligi ya muungano baada ya kuilaza KMKM mabao 5-2 katika uwanja wa New Amaan Zanzibar. Kwa ushindi huo sasa Azan itacheza fainali na Simba SC ambao katika mchezo wake jana iliifunga KVZ mabao 2-0, kwa vyovyote mchezo huo wa fainali utakuwa wa aina yake kutokana na timu hizo kukamiana vikali. Mabao ya Azam yamefungwa na Abdul Sopu (mawili), Nathaniel Chilambo, Iddi Nado na Iddi Kishindo

TAKWIMU ZA JKT QUEENS BALAA

Picha
Kuna Namna Hawa Jkt Queens Wanatoa Alarm Ya Hatari Kwamba Ukikutana Nao Yeyote Anakudhuru Yeeees Mfano Wa Timu Nne Wafungaji Hatari Wenye Muendelezo Hadi Sasa ... Jkt Queens 1. Stumai Abdallah 17 Goals 2. Winfrida Gerald 8 Goals 3. Donisia Minja 4 Goals 4. Amina Bilali 4 Goals 5. Jamila Rajab       4  Goals  6. Aliya Fikiri                2  Goals Jumla = 39 Hao Ndio Wafungaji Wa Jkt Queens Na Orodha Ya Magoli Waliyofunga Hadi Sasa Na Wote Bado Wanamuendelezo Mzuri Wa Kufunga ... Na Hapa Bado Ukizubaa Hata Beki Anakufunga Kama Fatuma Makusanya Leo,Anastazia Katunzi,Janeth Pangamwene,Lidya Maximilian Hawa Wote Wana Goli Msimu Huu ... Simba Queens  1. Aisha Mnunka            13 Goals 2. Asha Djafari               8  Goals 3. Jentrix Shikangwa    4  Goals 4. Viviane Corazone     3  Goals 5. Joan Ainambambazi 2 Goals Jumla = 30 Katika Orodha Hii Ya Simba Queens Wafunga Wenye Muendelezo Mzuri Ni Wawili Tu Aisha Mnunka Na Asha Djafari Tu Hao Wengine

YANGA PRINCESS YAKUBALI TENA KICHAPO KWA SIMBA QUEENS

Picha
Simba Queens imeendeleza ubabe wa Ligi Kuu ya wanawake (WPL) mbele ya Yanga Princess kwa kuifunga tena mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi. Mabao ya Simba Queens yaliwekwa kimiani na Asha Mnunka katika dakika ya 49 na 90 kumfanya afikishe mabao 15 kwenye ligi nyuma ya kinara Stumai Abdallah mwenye mabao 17, huku bao la tatu leo likifungwa na Jentrix Shikangwa katika dakika ya 66 na kumfanya afikishe mabao matano. Bao la kufutia machozi la Yanga limefungwa na Mmarekani Kaeda Wilson.  Simba imeifunga Yanga mara mbili kwenye ligi msimu huu ikiipiga kwa idadi ya mabao hayo hayo ambayo straika wake Mnunka aliwafunga mabao mawili-mawili katika kila mechi na hivyo kuiwezesha Queens kuifunga Princess jumla ya mabao 6-2. Timu hizo mbili kwenye dakika 10 za mwanzo kipindi cha kwanza na pili zilionyesha ushindani wa aina yake na kila timu ilifika langoni kwa mwenzie lakini Simba ilikuwa bora zaidi katika dakika 30 za mwisho.

BIL 19.7 KUKARABATI UWANJA WA UHURU "SHAMBA LA BIBI"

Picha
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia wizara ya utamaduni Sanaa na michezo imesaini mkataba wa ukarabati na kampuni ya CRCEG ya China kwa ajili ya ukarabati wa uwanja wa Uhuru uliopo jijini Dar es salaam. Katika hafla ya utiaji wa saini za mkataba huo Serikali imeweka wazi gharama itakayotumika kukarabati uwanja huo ni bilioni 19.7 za Kitanzania na ukarabati huo utachukua miezi 12 sawa na mwaka mmoja. Hongera Serikali kwa hatua hii ambayo inatoa mwanga kuelekea michuano ya Kombe la mataifa Ya Afrika 2027 ambayo Tanzania,Kenya na Uganda ndio watakuwa wenyeji kwa pamoja.

BENCHIKHA KIKAANGONI SIMBA

Picha
kocha mkuu Wa Simba SC ameitwa kwenye kamati ya nidhamu ya Simba Sc na anapaswa kujibu juu ya kauli yake aliyoitoa kwenye press anatarajiwa kufanya kikao Baada tu ya mechi za Muungano kutamatika. Aprili 20/4 Baada ya mchezo wa Watani Wa jadi na Simba kupoteza Kwa Magoli 2-1 kocha alitoa maneno yaliyotafsriwa ayakuwa maneno ya kiuungwana Kwa Wachezaji. Benchikha alisema “Toka nimeanza kufundisha mpira sijawahi kufundisha Wachezaji wenye vichwa vigumu kama hawa, CV yangu inashuka Kila siku.”

FREDDIE MICHAEL ATAWAUMBUA WATU HUMU!

Picha
Na Prince Hoza 0652-626627 KWA hakika kabisa hali inavyoelekea mwishoni mwa msimu huu, kuna watu watakuja kuumbuka, kuanzia wachambuzi mpaka mashabiki watakaatana wenyewe kwa wenyewe. Hiyo yote inatokana na kauli zao wanazozitoa kwa mshambuliaji Freddie Michael Koblas raia wa Ivory Coast anayeichezea klabu ya Simba. Mshambuliaji huyo aliyesajiliwa kwenye dirisha dogo la Januari mwaka huu sambamba na mshambuliaji mwenzake Jobe Omari raia wa Gambia. Kwasasa Freddie na Jobe ni gumzo kubwa kwenye medani ya michezo hasa soka, wapo baadhi ya wadau tena wana majina makubwa wamefikia kuwabeza Freddie na Jobe huku wakiuponda uongozi wa Simba kwa kufanya usajili mbaya zaidi. Kitendo cha Simba kuwatema washambuliaji Jean Baleke na Moses Phiri ambao walikuwa na rekodi nzuri za kufunga, kuliwaudhi wengi walioamini kwamba Jobe na Freddie wanaweza kuwazidi uwezo nyota hao. Baleke raia wa DR Congo alijiunga na Simba akitokea TP Mazembe ya mjini Lubumbashi na Phiri raia wa Zambia aliyekuwa anaichezea t

Alikiba achekelea Crown Fm kucheza nyimbo za Diamond Platinumz

Picha
Mmiliki wa redio ya Crown Fm Alikiba amefurahishwa na kitendo cha redio yake kucheza nyimbo za hasimu wake Diamond Platinumz, Kiba ambaye naye ni msanii wa bongofleva amefurahishwa na maamuzi hayo na kuandika katika kurasa wake. "Nimefurahishwa sana baada ya kuona radio yangu ikicheza nyimbo za Diamond Platnumz. Ndio maana nilipokuwa nikiifungua media yangu nikasema hii ni ya kila mtu na si ya familia." "Crown Fm itacheza nyimbo za Diamond na Harmonize bila kubagua. Natamani pia Wasafi Media wafanye hivyo kwa wasanii wengine." Alikiba akieleza jinsi alivyofurahishwa na kuchezwa kwa nyimbo za Diamond Platnumz na Harmonize kwenye radio yake.

SIMBA YAAMKIA MUUNGANO

Picha
Wekundu wa Msimbazi, Simba SC usiku huu wametakata baada ya kuifunga KVZ mabao 2-0 katika michuano ya Ligi ya Muungano kwenye uwanja wa Amaan, Zanzibar. Mabao ya Simba yamefungwa na Freddy Michael dakika ya 25 na Israel Mwenda dakika ya 90 aliyefunga kwa mkwaju wa penalti. Kwa maana hiyo Simba imeingia fainali na emdapo itafanikiwa kushinda ubingwa itakuwa rasmi bingwa mpya wa muungano na kuambulia shilingi milioni 50

BINGWA LIGI YA MUUNGANO KUAMBULIA MIL 50

Picha
Wakati KVZ ikiialika Simba katika mchezo wa kwanza wa Ligi ya Muungano leo kuanzia saa 2:15 usiku katika Uwanja wa Amaan, timu zinazoshiriki zimetangaziwa zawadi ya Sh50 milioni kwa itakayobeba ubingwa. Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Mipango ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF), Awadh Maulid Mwita alisema jana kuwa bingwa wa mashindano hayo itaondoka na Sh50 milioni ilhali washindi wa pili watapata Sh30 milioni. “Mwaka huu tumeanza na timu nne, lakini mwakani mipango yetu ni kuwa na timu nane nne Zanzibar na nne Bara. Kwa hiyo ndio maana tumeweka kiasi hicho cha fedha kwa mshindi,” alisema na kuongeza kwamba mwakani bingwa ataondoka na Sh100 milioni.

JKT TANZANIA NA YANGA HAKUNA MBABE

Picha
Timu ya JKT Tanzania jioni ya leo imeibana mbavu Yanga SC baada ya kuilazimisha sare ya bila kufungana 0-0 katika uwanja wake wa nyumbani wa Meja Isamuya nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Bahati haikuwa yao vijana wa JKT Tanzania kwani tangu kipindi cha kwanza waliutawala mchezo lakini washambuliaji wake wakiongozwa na Matheo Antony, Sixtus Sabilo na Shiza Kichuya wakishindwa wenyewe. Yanga ambayo katika mzunguko wa kwanza waliifunga mabao 5-0, leo imeshindwa kabisa kuonesha kiwango chao kwani haijafanya lolote na zaidi ingepoteza mchezo

YANGA NA AIR TANZANIA WAINGIA MKATABA

Picha
Timu ya wananchiii Yanga rasmi imeingia mkataba wa miaka miwili na shirika la ndege Air Tanzania.Mkataba huu wa Yanga na Air Tanzania utakwenda kugusa.. Yanga watapata punguzo la Bei Kwa safari zao zote za ndani ya nchi na nje ya nchi.

EDO KUMWEMBE AMSHANGAA KELVIN YONDANI

Picha
Nilimuona Kelvin Yondani akiwa na kitambaa cha unahodha wa timu yake Geita Gold. Ilikuwa siku chache zilizopita. Nikakimbilia katika mtandao wa Wikipedia kutazama umri wake. Msela Kevin yupo uwanjani mpaka leo. Nadhani hata msimu ujao atakuwepo uwanjani. Jina? Kelvin Yondani. Tarehe ya kuzaliwa? Oktoba 9, 1984. Umri? Miaka 39. Bado Kelvin anadunda katika nafasi ngumu ya ulinzi wa kati. Akiwa katika umri huu amekumbana na kina Fiston Mayele, Prince Dube, Jean Baleke na wengineo. . Kwa mujibu wa mtandao huo huo wa Wikipedia inaonyesha kwamba John Bocco ambaye jina lake lipo katika usajili wa Simba msimu huu ana umri wa miaka 34. Amepitwa miaka mitano na Yondani. Kwanini Bocco hayupo uwanjani? Kwa sasa nasikia anasomea ukocha huku akifundisha timu ya Simba chini ya umri wa miaka 17. Ni baada ya kumfukuza na kumwambia amezeeka katika soka letu. . Ni kitu ambacho tumekuwa tukifanya mara nyingi baada ya kumchoka mchezaji. Mchezaji mwenye roho ndogo huwa anakimbia akiambiwa hivi. Sana sana ka

Wadau walaani kitendo cha Maxi Nzengeli

Picha
Nalaani kitendo hichi alichofanya Maxi Nzengeli kwa Azizi Ki na Aziz Ki akiwa ametulia tuu eti aise anasikilizia Kiss 🤮? mpigaji wa hii picha amekosea kuipiga na kuiweka hadharani Je? waafrika tumeacha tamuduni zetu kama wa Afrika mwanaume kabisa unakubali kupigwa busu na mwanaume mweinzako aise mimi napigana aise hayo mambo ni watu wa Ulaya huko wameruhusu hayo mambo...ya kishwaitwani....

BENCHIKHA KUACHIA NGAZI MWISHONI MWA MSIMU HUU

Picha
Inaarifiwa kwamba kocha mkuu was Simba SC Muargeria Abdelhak Benchikha yuko mbioni kuachana na klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu ikidaiwa anataka kutunza heshima yake. Tangu kocha huyo ajiunge na Simba, hadhi yake inazidi kuporomoka na hasa kutokana na matokeo mabaya inayopata klabu hiyo. Mpaka sasa Simba imeshatolewa katika michuano ya Ligi ya mabingwa, kombe la FA na pia kuondoka kwenye mbio za kuwania ubingwa wa Tanzania bara Michuano pekee ambayo Simba inaweza kuambulia kombe ni ligi ya Muungano ambayo imetangazwacm kuanza na TFF

MDAKA MISHALE WA ZESCO KUTUA AZAM FC

Picha
Inaelezwa kuwa Azam FC inamfuatilia Kwa karibu kipa wa Zesco United ya Zambia Ian Otieno raia wa Kenya mwenye umri wa miaka 30. Mlinda mlango huyo ndiye atakaenda kuchukua ya mlinda mlango wa sasa wa Azam FC, Mohamed Mustafa. Mostafa Mohamed anadaiwa kurejea kwenye klabu yake ya El Merreikh mwishoni mwa msimu baada ya kumaliza mkataba wake mkopo ndani ya Chamazi.

PRINCE DUBE AANDALIWA MKATABA WA MIAKA MITATU YANGA

Picha
Taarifa zilizopatikana jijini Dar es Salaam zinasema kuwa mshambuliaji anayejiandaa kuachana na klabu yake ya Azam, ameandaliwa mkataba mnono na klabu moja ya kariakoo kwa ajili ya kuitumikia msimu ujao. Taarifa za uhakika ni kuwa mshambuliaji huyo ataendelea kusalia nchini na ataendelea kuuwasha katika ligi kuu NBC Tanzania akiwa na kigogo mmoja wa kariakoo. Prince Dube ameandaliwa mkataba wa miaka mitatu na vigogo hao wa kariakoo na muda wowote atalipa faini kwa klabu yake ya Azam ili awe huru kusaini katika klabu anayoipenda. Vigogo hao ambao wamepania kufanya vizuri zaidi katika michuano ya kimataifa na kuvuka hatua ambayo wamekwama kuvuka ya robo fainali ya ligi ya Mabingwa Afrika.