Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2013

'WAASI WA M23' WAIBUKIA SHEREHE DAR.

Picha
Hali si shwari hasa kwa wakazi wa maeneo ya Tabata na Kigogo jijini Dar es Salaam kufuatia kutokea kwa kikundi cha vijana wadogo wenye umri wa miaka 12-17 wanaojiita 'Waasi wa M23' kuvamia sherehe mbalimbali na kufanya vurugu huku wakiwa na silaha za jadi yakiwemo mapanga, visu na bisibisi. Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na mtandao wa Mambo Uwanjani Leo ambao huko jirani na maeneo hayo umebaini kuwa kikundi cha vijana hao wanajitokeza nyakati za usiku kwenye sherehe za aina mbalimbali zinazohusisha muziki.

MAN CITY, MAN UNITED, CHELSEA JINO KWA JINO CAPITAL ONE.

Picha
KLABU ya Tottenham itamenyana na West Ham katika Robo Fainali za Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One wakitakiwa kulipa kisasi cha kufungwa mabao 3-0 katika Ligi Kuu  mwezi huu. Spurs ilipigana na kutoka nyuma kwa mabao 2-1 katika dakika za nyongeza na kuipiga Hull Jumatano mabao 8-7 kwa mikwaju ya penalti. Katika mechi nyingine za hatua hiyo ya michuano hiyo, Manchester United itasafiri hadi Stoke wakati Manchester City itamenyana na Leicester.

BRANDTS NAYE KUTUPIWA VIRAGO YANGA.

Picha
UONGOZI wa Yanga SC unafuatilia mwenendo wa timu kwa ujumla na utendaji wa kocha wake, Mholanzi Ernstus ‘Ernie’ Wilhelmus Johannes Brandts kwa mechi zilizobaki za mzunguko wa kwanza na baada ya hapo itaamua kumuongeza Mkataba au kuachana naye mwalimu huyo. Brandts ametimiza mwaka mmoja wa Mkataba wake Yanga mwezi huu, lakini kuhusu Mkataba mpya ametakiwa kusubiri hadi mwisho wa mzunguko wa kwanza wa ligi mwezi ujao. Yanga SC hawajaonyesha wasiwasi juu ya uwezo wa Brandts katika kufundisha, lakini wanatilia shaka mambo matatu; sera zake, usimamiaji wake wa nidhamu ya wachezaji na kutokuwa na maamuzi ya haraka. Brandts analaumiwa kwa kitendo cha kuruhusu wachezaji wasikae kambini muda mrefu, akidai wachezaji si wafungwa wanatakiwa huru na mara nyingi Yanga imekuwa ikiingia kambini siku mbili kabla ya mechi. Kwa kuzingatia wapinzani wao wa jadi, Simba SC wako kambini muda wote Bamba Beach, Kigamboni, Dar es Salaam, Yanga nao wanaona hata kwao inawezekana, lakini Brandts amekuwa akikataa

ZILIZOTUFIKIA: ANNE MAKINDA KUVULIWA USPIKA

Picha
Mbunge wa Nzega, Dk Khamis Kigwangalla, (CCM), leo anatarajiwa kuanza kukusanya saini za wabunge akitafuta kuungwa mkono katika hoja ya kutokuwa na imani na Spika wa Bunge, Anne Makinda kwa madai kwamba amekuwa akikiuka kanuni za Bunge. Dk Kigwangalla aliibua hoja ya kutokuwa na imani na Spika katika kikao cha wabunge wote cha kuelezea shughuli zitakazofanywa na Bunge katika mkutano wa 13, kilichofanyika juzi jioni kwenye ukumbi wa Pius Msekwa.

HAMISI KIIZA AMGWAYA TAMBWE, UFUNGAJI BORA

Picha
Mshambuliaji  Mganda Hamis Kiiza wa Yanga amesema kuwa kwa sasa hawazii kiatu cha dhahabu cha mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu, bali mawazo yake yamejikita katika kuhakikisha anaisaidia timu yake kutetea ubingwa wa ligi hiyo. Kiiza alisema baada ya mazoezi ya Yanga kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Loyola uliopo Mabibo jijini Dar es Salaam jana kuwa hashindani na wachezaji wengine kusaka zawadi ya mfungaji bora bali anasaka mafanikio ya kikosi cha 'Wanajangwani'.

KAGERA SUGAR WAPANIA KUISHUSHA SIMBA NAFASI YA NNE

Picha
Wakati  mshambuliaji mpya wa Simba Mrundi Amisi Tambwe akirejea uwanjani na kuanza mazoezi, uongozi wa klabu ya Kagera Sugar umetamba kuwa timu yao itaendeleza ubabe dhidi ya 'Wanamsimbazi' kwa kuhakikisha inaibuka na ushindi katika mchezo wao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara utakaopigwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Katika mechi ya mwisho baina ya timu hizo, Kagera Sugar iliyokuwa ikifundishwa na kocha wa sasa wa Simba, Abdallah Kibadeni, iliwafunga Wekundu wa Msimbazi 1-0 kwenye Uwanja wa Kaitaba Machi 27, 2013 baada ya timu hizo kutoka sare ya 2-2 jijini Dar es Salaam Oktoba 17, 2012.

YAYA AZURU KENYA, HOFU YATANDA.

Picha
Yaya Toure Mchezaji maarufu wa timu ya Manchester City Yaya Toure, amewasili mjini Nairobi Kenya kwa uzinduzi wa muungano mpya wa kukabiliana na uwindaji haramu kwa ushirikiano na shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia mazingira (UNEP). Muungano huo umeanzishwa ili kukabiliana na uwindaji haramu wa wanyama pori haswa Ndovu ambao wanakabiliwa na tisho la kudidimia kutokana na uwindaji haramu barani Afrika . Toure, mshindi wa tuzo la mchezaji soka bora zaidi Mwafrika kwa miaka miwili mfululizo, 2011 na 2012 ataeleza kwanini amekubali kushirikiana na muungano huo kupambana dhidi ya uwindaji haramu na nini hasa jukumu lake.

IVO MAPUNDA ACHEKELEA KUITWA STARS.

Picha
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen alitangaza kumjumuisha kwa mara ya kwanza kipa Ivo Mapunda katika kikosi cha wachezaji 30 watakaoingia kambini kujiandaa na Michuano ya Chalenji itakayofanyika Nairobi, Kenya kuanzia Novemba 27 hadi Desemba 12. Mapunda aliwahi kuwa kipa tegemeo wa Taifa Stars iliyokuwa chini ya kocha Mbrazil, Marcio Maximo na kuisaidia kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) zilizofanyika Ivory Coast 2009. Mapunda akizungumza na kwa simu kutoka Kenya alisema:  “Nimesoma taarifa za kuitwa katika kikosi cha Kilimanjaro Stars leo asubuhi kupitia mitandao ya kijamii, hakika nilishtuka.

KIBADENI APEWA MECHI MBILI KABLA YA KUTIMULIWA.

Picha
Kuna taarifa zimeenea ambapo Mambo Uwanjani Leo imezipata kwamba kocha mkuu wa Simba SC Abdallah Kibadeni, amepewa mechi mbili za mwisho kabla ya kutimuliwa na uongozi wa timu hiyo baada ya kushindwa kuifikisha Simba kwenye kilele cha mafanikio. Kwa mujibu wa chanzo cha habari hizi ambacho ni rafiki wa karibu na klabu ya Simba kinasema kuwa uongozi wa Simba umechoshwa na hali iliyopo kwa sasa katika klabu hiyo ambapo nidhamu ya wachezaji imeshuka mno. Uongozi huo unadai ni tofauti kubwa kati ya Simba inayonolewa na Kibadeni na ile iliyokuwa ikinolewa na Mfaransa Patrick Liewig ambayo ilionekana kuwa na nidhamu ya hali ya juu iliyopelekea kukamata nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi msimu uliopita. Chanzo hicho kinadai kuwa Simba kwa sasa imepoteza mwelekeo na lawama zota anabebeshwa Kibadeni ambaye ndiye kocha mkuu, chanzo hicho kinaongeza kuwa Kibadeni ameshindwa kusimamia nidhamu ya wachezaji iliyowapelekea kucheza chini ya kiwango katika mechi zake mbili dhidi ya Coastal Unio

MOYES AANZA NGEBE MAN UNITED IKIUA 4-0

Picha
MSHAMBULIAJI Javier Hernandez 'Chicharito' ameendeleza takwimu zake nzuri ndani ya Manchester United, licha ya kupewa nafasi chache za kucheza kwenye timu hiyo. Nyota huyo wa Mexico usiku wa jana amefunga mabao mawili katika ushindi wa 4-0 wa Manchester United dhidi ya Norwich katika Kombe la Ligi. Nyota huyo mwenye kipaji cha kufunga, alitikisa nyavu katika dakikaa 20 na 54 kwa penalti jana, wakati mabao mengine yalifungwa na Jones dakika ya 87 na Fabio dakika ya 90 na ushei.

JAMAL MALINZI AULA CAF.

Picha
RAIS wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Issa Hayatou amempongeza Jamal Malinzi kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 27 mwaka huu. Katika salamu zake kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya CAF na familia ya mpira wa miguu Afrika, Rais Hayatou amesema uchaguzi huo unampa Rais Malinzi fursa ya kuupeleka mbele mpira wa miguu nchini Tanzania. Jamal Malinzi kulia akiwa na Tenga Amesema CAF ina imani uwezo wake katika uongozi, uzoefu na ujuzi katika mpira wa miguu havitausaidia mpira wa miguu Tanzania pekee bali Afrika kwa ujumla, na kuongeza kuwa ataendeleza ushirikiano uliopo ili kuwanufaisha zaidi vijana wa bara hili.

YANGA, MGAMBO WAVUNA MIL 37.

Picha
MECHI ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Mgambo Shooting lililochezwa jana (Oktoba 29 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 37,915,000. Washabiki waliohudhuria mechi hiyo namba 46 iliyomalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 walikuwa 6,515 ambapo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000. Mgawo wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 5,783,644.07, gharama za kuchapa tiketi sh. 3,145,790 wakati kila klabu ilipata sh. 8,550,741.95. Wamiliki wa uwanja walipata sh. 4,347,834.89, gharama za mchezo sh. 2,608,700.93, Bodi ya Ligi sh. 2,608,700.93, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,304,350.47, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,014,494.81.

WACHEZAJI WA CHELSEA MATATANI ULAYA

Picha
KWA pamoja wanawekewa ulinzi na mabeki wa timu pinzani, na sasa imketokea wote wawili wanakamatwa na trafiki akiwa na mchezaji mwenzake wa Chelsea, Juan Mata. Nyota huyo wa Hispania alikwenda kula chakula cha mchana katikati ya London akiwa na mchezaji mwenzake wa klabu hiyo na timu ya taifa, Fernando Torres wakati wanakutwa na kasheshe hilo kutoka na kupaki vibaya gari lao.

KIPA WA SIMBA APELEKWA JESHINI

Picha
KIPA namba moja wa Simba SC, Abbel Dhaira amekwenda kufanyiwa uchunguzi asubuhi hii katika hospitali Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kitengo cha wanamaji kutokana na matatizo ya msuli wa nyuma ya shingo. Daktari wa Simba SC, Yassin Gembe amesema leo kwamba Dhaira amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya msuli wa nyuma ya shingo tangu kwenye mechi dhidi ya Yanga Jumapili ambayo alifungwa mabao matatu katika sare ya 3-3. Abbel Dhaira “Kama utakumbuka katika mechi dhidi ya Yanga alitibiwa tibiwa wakati mchezo unaendelea, ni kutokana na matatizo hayo hayo, kwa hivyo sasa hivi nakwenda naye akafanyiwe uchunguzi,”amesema Gembe asubuhi hii. Dhaira alitoka dakika ya 35 juzi katika mchezo dhidi ya Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga baada ya kugongana na mshambuliaji wa Coastal Union, Haruna Moshi ‘Boban’, timu hizo zikitoka sare ya 0-0.

YANGA YAZITEGA SIMBA, AZAM NA MBEYA CITY

Picha
Unaweza kushangaa lakini ndivyo itakavyokuwa kuwa mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara Yanga inaweza kukamata usukani wa ligi kuu Tanzania bara inayoelekea ukingoni endapo tu vinara wa ligi hiyo Simba, Azam na Mbeya City zitafanya makosa katika mechi zao za wao kwa wao. Yanga kwa sasa iko katika nafasi ya nne na inaweza kukamata usukani wa ligi endapo itamaliza mechi zake za mwisho vizuri kwani inacheza na timu dhaifu, Lakini Simba Sc wiki ijayo inakutana na Azam FC kwenye uwanja wa Taifa ambapo kama timu hizo zitatoka sare nasi Yanga inaweza kuzivuka kirahisi.

BARTHEZ AREJESHWA YANGA........

Picha
Benchi la ufundi la Yanga limemsafisha kipa wake namba moja, Ally Mustapha ‘Barthez’ dhidi ya shutuma anazotupiwa na mashabiki wa timu hiyo tangu siku ya Jumapili baada ya kumalizika kwa mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Simba. Mashabiki hao wanamshutumu Barthez kuwa alichangia timu hiyo ishindwe kuibuka na ushindi katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya bao 3-3 ikiwa ni baada ya Yanga iliyokuwa ikiongoza kwa mabao 3-0 katika kipindi cha kwanza kuruhusu wapinzani wao hao wa jadi Simba kusawazisha mabao yote kipindi cha pili cha mchezo huo.

NYAMLANI KUENDELEZA SERA ZA TENGA TFF

Picha
Mgombea Urais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Jumanne Nyamlani amesema endapo atachaguliwa kuliongoza shirikisho hilo lenye mamlaka ya juu kisoka nchini, ataendeleza mambo yote mazuri yaliyofanywa na utawala unaoondoka madarakani chini ya Rais wa sasa, Leodegar Tenga. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Nyamlani ambaye kwa sasa ni makamu wa kwanza wa rais wa TFF, alisema uongozi wa Tenga (58), umefanya mambo mengi mazuri ambayo amepanga kuyaendeleza kwa maslahi ya soka la Tanzania.

NGASA, KIIZA WAUNDA BENDI YAO............

Picha
Winga  hatari wa Yanga na timu ya Taifa (Taifa Stars), Mrisho Ngasa amesema ushirikiano mzuri wanaouonyesha wakicheza sambamba na Mganda Hamisi Kiiza, umewafanya waunde bendi  yao ya uwanjani inayokwenda kwa jina la 'Danger Zone'. Ngasa ambaye ameifungia Yanga mabao matatu katika mechi tano alizocheza msimu huu tangu atoke kifungoni huku akitoa pasi tano za mwisho, anaamini kujituma kwake mazoezini na kwenye mechi ndiko kunakomfanya ang'are katika kikosi cha klabu yake msimu huu wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

FERGUSON AMUUMBUA BECKHAM

Picha
Aliyekuwa meneja wa klabu ya Manchester United ya Uingereza Sir Alex Ferguson amesema David Beckham alilazimika kuondoka katika klabu hiyo kutokana na tabia yake ya kujiona ni mkubwa kuliko meneja wake. Katika kitabu kipya kuhusu historia ya maisha yake Ferguson amesema enzi za uongozi wake walitofautiana na Beckham kutokana na kumkosoa kuhusiana na kiwango chake katika matokeo ya ligi ya FA 2003.

KIBADENI AWEKWA NJIA PANDA SIMBA.......YADAIWA ANAWAGAWA WACHEZAJI

Picha
Uongozi wa Simba umetupilia mbali madai ya kocha wao, Abdallah Kibadeni aliyewatuhumu baadhi ya wachezaji wake kuihujumu timu hiyo katika mchezo dhidi ya Yanga uliofanyika Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Baada ya mechi hiyo iliyomalizika kwa sare ya mabao 3-3, Kibadeni aliwashushia lawama baadhi ya wachezaji wake kwamba waliihujumu timu hiyo kwa kucheza chini ya kiwango. Kutokana na hali hiyo Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang’are alisema mambo hayo hayana nafasi kwa sasa wanachoangalia ni mechi zao zilizobakia katika mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu. Alisema baada ya mechi hizo ndipo watakapokaa na kufanyia  kazi shutuma hizo, lakini kwa sasa hawana nafasi hiyo.

SIMBA KUKALIA USUKANI LEO?

Picha
Wakati  Simba na Yanga zikiwa katika viwanja tofauti leo kwa ajili ya mechi zao kukamilisha raundi ya 10 ya Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara, makocha wa timu hizo, Jamhuri Kihwelu 'Julio' na Mholanzi Ernie Brandts wametamba kupata matokeo mazuri leo. Simba yenye pointi 19 katika nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi, itajaribu kurejea kileleni wakati watakapocheza dhidi ya Coastal Union ugenini Tanga, huku mabingwa Yanga waliopoteza uongozi wao wa magoli 3-0 katika sare 3-3 dhidi ya Simba Jumapili, watawakaribisha Rhino Rangers kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

LEWANDOWSKI AISAMBARATISHA ARSENAL

Picha
BAO la dakika za lala salama la Robert Lewandowski limeipa ushindi wa 2-1 Borussia Dortmund dhidi ya Arsenal katika Ligi ya Mabingwa Uwanja wa Emirates usiku huu. Henrikh Mkhitaryan aliifungia bao la kuongoza Borussia Dortmund, lakini Olivier Giroud akasawazisha ikawa 1-1. Lakini katika dakika 10 za mwisho, Arsenal ikatepeta na kumruhusu mshambuliaji Lewandowski kuwamaliza nyumbani.

ROBINHO AMZIDI KWA KILA KITU NEYMAR, WOTE WANG'ARA.....

Picha
 WASHAMBULIAJI Neymar na Robinho walionekana kutaka sana kubadilishana jezi katika mechi baina ya timu zao, AC Milan na Barcelona Ligi ya Mabingwa jana usiku... na wakafanya hivyo wakati wa mapumziko! Licha ya kuchezea wote timu ya taifa ya Brazil, Robinho anabakia kuwa shujaa mkubwa wa Neymar na wawili hao walibadilishana jezi wakati refa anamaliza kipindi cha kwanza. Neymar alitoa heshima zake kwa winga wa Milan, anayemzidi miaka nane, kabla ya mchezo wa jana, lakini akamuonyesha kazi uwanjani. Neymar aliposti picha yake akiwa mdogo pamoja na nyota huyo wa zamani wa Man City katika Instagram akisema: "Leo ni siku maalum kwangu...kwa kucheza kwa mara ya kwanza dhidi ya mkali wangu,

HAIJAPATA KUTOKEA BARANI AFRIKA...............

Picha
Furaha ya kupita kiasi ndiyo iliyosababisha zaidi ya watu 20 kuzimia uwanjani wakati walipokuwa wakishuhudia mchezo wa Ligi Kuu kati ya Simba na Yanga uliofanyika juzi Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Katika mchezo huo uliokuwa umejaa na presha kubwa kuanzia kwa wachezaji hadi kwa mashabiki wa pande zote mbili ulimalizika kwa timu hizo kufungana mabao 3-3.

AL AHLY USO KWA USO NA ORLANDO PIRATES

Picha
Al ahly wanajiandaa kumenyana na Orlando Pirates Klabu ya soka ya Misri, Al-Ahly iko kifua mbele katika kutetea ubingwa wao wa ligi ya klabu bingwa Afrika baada ya kuicharaza klabu ya Cameroon ya Coton Sport katika penalty ili kuweza kufika fainali. Klabu hiyo ya Cairo ilishinda kwa ujumla wa mabao sita saba kwenye mechi iliyochezwa katika eneo la El-Gouna baada ya mechi ukamilia kwa sare ya bao maoja kwa moja. Matokeo sawa na hayo yalishuhudiwa kwenye mechi ya mkondo wa kwanza, iliyomalizika kwa mabao mawili kwa mawili.

MAGOLI YALIYOSABABISHA VIFO VYA MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA HAYA HAPA............

Picha
Goli la pili la Yanga lililofungwa na mshambuliaji Mganda Hamis Kiiza limedaiwa kusababisha kifo cha shabiki wa Simba Ramadhani Mbande, mkazi wa mtaa wa Matokeo kata ya Mabibo, Kinondoni jijini Dar es Salaam. Mapema jana kulienea taarifa kuwa mmoja wa mashabiki wa Simba (Mbande) alipoteza maisha wakati kikosi cha Yanga kinachonolewa na kocha Mholanzi Ernie Brandts kilipokuwa kikikifunga mabao mfululizo kikosi cha Simba kinachonolewa na kocha mzawa Abdallah Kibadeni 'King' katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara iliyomazika kwa sare ya 3-3 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam juzi.

MAN CITY WAWASIRI URUSI BILA NAHODHA WAO

Picha
KLABU ya Manchester City itamkosa Nahodha wake Vincent Kompany katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya CSKA Moscow kesho. Kikosi cha Manuel Pellegrini kitamenyana na jkabu ya Urusi wiki hii, kikitarajia kuzinduka baada ya kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Bayern Munich katika mchezo uliopita. Lakini Kompany, sambamba na Martin Demichellis na Jack Rodwell, hawajasafiri na timu. Beki mshirika wa kudumu Kompany pale katikati Matija Nastasic alianza pamoja na Javi Garcia, ambaye kwa kawaida hucheza kama kiungo mkabaji.Kompany alirejea uwanjani wiki za karibuni baada ya kukosa mechi kibao za mwanzo wa msimu, lakini akaumia tena na kukosa mechi ya Jumamosi timu hiyo ikishinda dhidi ya West Ham.

BARTHEZ, CANNAVARO OUT YANGA..............

Picha
KIPA Ally Mustafa ‘Barthez’ anaweza kupumzishwa katika mchezo wa kesho wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baina a timu yake na Rhino Rangers ya Tabora, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Katika mechi tisa alizodaka Barthez hadi sasa, amefungwa mabao 11 na inaonekana kudaka mfululizo tangu msimu uliopita kunamchosha na bila shaka Deo Munishi ‘Dida’ atasimama langoni kwa mara ya kwanza kesho katika Ligi Kuu tangu asajiliwe na Yanga msimu huu kutoka Azam. Kwa ujumla, kocha Mholanzi Ernstus ‘Ernie’ Wilhelmus Johannes Brandts anatarajiwa kufanya marekebisho makubwa katika safu yake ya ulinzi kesho baada ya matokeo ya sare ya 3-3 na wapinzani wa jadi Simba SC Jumapili, Uwanja wa Taifa, wakitoka kuongoza 3-0 hadi mapumziko.

MAGAIDI WAWILI WA 'WESTGATE' WAPATIKANA KENYA........

Picha
Miili miwili iliyoungua vibaya aliyoopolewa katika eneo la kituo cha biashara cha Westgate nchini Kenya siku ya Alhamisi inawezekana kwa kiasi kikubwa ikiwa ni ya magaidi walioshambulia kituo hicho, Mbunge mmoja wa Kenya ameiambia BBC.

LEWANDOWSKI ATUA BAYERN MUNICH

Picha
MSHAMBULIAJI Robert Lewandowski atapokea dau la usajili la karibu Pauni Milioni 10 atakapojiunga na Bayern Munich kama mchezaji huru mwishoni mwa msimu.

SIMBA YATAMBIA REKODI YA KUIFUNGA YANGA MARA NYINGI JUMAPILI

Picha
Huku zikiwa zimesalia siku mbili, rekodi za miaka 13 iliyopita, zinaonyesha Simba imeibuka na ushindi mara nyingi zaidi ya Yanga katika mapambano baina ya timu hizo iliyopigwa siku ya Jumapili.

MWOMBEKI AREJEA KUIVAA YANGA KESHOKUTWA

Picha
Klabu ya soka ya Simba imepumua na kuwa na matumaini makubwa ya kumtumia mshambuliaji wake mrefu na mwenye nguvu, Betram Mombeki aliyekuwa akitajwa huenda asiwapo kwenye pambano lao la watani dhidi ya Yanga.

YANGA WAITANGAZIA KIAMA SIMBA JUMAPILI

Picha
Mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga wamesema wamejipanga kuhakikisha wanaibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya watani wao wa jadi, Simba katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara utakaopigwa keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

MKOLA MAN AJA NA KILEVI CHAKE........

Picha
Msanii mkongwe wa miondoko ya muziki wa kizazi kipya nchini Christopher Mhenga aka Mkolaman mwenye maskani yake mkoani Tanga anaomba mashabiki wake wampokee tena kama walivyompokea mwanzo.

KUMUONA TAMBWE, KAVUMBAGU 5000 TAIFA......

Picha
Kiingilio cha chini cha mechi ya watani wa jadi, Simba na Yanga itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kitakuwa ni Sh.5,000 kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Shirikisho la Soka (TFF).

KUMBE BRANDTS ANARINGIA UBABE WAKE KWA SIMBA.......

Picha
NYASI za Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam zinatarajiwa kuwaka moto Jumapili kwa mpambano wa watani wa jadi katika soka ya Tanzania, Simba na Yanga.

NDONDI ZA DUNIA ZAPAMBA MOTO KAZAKHSTAN

Picha
Mashindano ya ndondi ya ubingwa wa dunia yanazidi kupamba moto mjini Almaty, Kazakhstan.

TP MAZEMBE YAIUMBUA ZAMBIA KUHUSU NYOTA WATATU

Picha
Zambia imetoa vibali vya kukamatwa kwa wachezaji wake watatu waliokosa mechi ya kirafiki dhidi ya Brazil mjini Beijing China. Hata hivyo Zambia ilishindwa na Brazil mabao mawili kwa nunge.

BRANDTS AHOFIA KAMBI YA PEMBA......

Picha
Wakati  mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngasa anaugua malaria na yuko hatarini kuikosa mechi ya Ligi Kuu ya Bara dhidi ya watani wa jadi Simba Jumapili, kocha wa mabingwa hao watetezi Mholanzi Ernie Brandts amesema hajui kwanini wameenda kuweka kambi Pemba.

ENGLAND YATINGA BRAZIL KWA KISHINDO

Picha
MABAO ya Wayne Rooney na Nahodha Steven Gerrard yameihakikishia England nafasi ya kucheza Kombe la Dunia usiku huu baada ya kuifunga Polnd 2-0 usiku huu kwenye Uwanja wa Wembley.

KAMPUNI YANUKIA YANGA

Picha
KLABU ya Yanga ya Dar es Salaam imepiga hatua katika mchakato wa kuanzisha kampuni kwa kuanza rasmi mchakato wa kupigisha kura wanachamwa wake kuunga mkono au kupinga wazo hilo.

JONAS MKUDE AAPA KUTOKA NA BAO JUMAPILI

Picha
Wakati homa ya mpambano wa watani wa jadi Yanga na Simba ukiwa unazidi kupamba moto, kiungo wa Simba Jonas Gerrard Mkude ameahidi na bao.

MCHEZAJI WA NIGERIA AJERUHIWA VIBAYA..........

Picha
Mchezaji soka wa Nigeria , Nosa Igiebor alijeruhiwa vibaya wakati timu yao iliposhambuliwa mjini Addis Ababa baada ya mchuano wao wa mchujo dhidi ya Ethiopia katika kutafuta nafasi ya kushirki kombe la dunia mwaka ujao nchini Brazil.

JEURI YA PESA, RAIS REAL MADRID KUVUNJA REKODI NYINGINE YA USAJILI ULAYA

Picha
RAIS wa Real Madrid, Florentino Perez amesema kwamba mapato ya klabu yake tajiri zaidi duniani yanaweza kumnunua mshambuliaji wa Monaco, raia Colombia, Radamel Falcao mwakani.

KIBADENI AANZA VISINGIZIO, ADAI HAJAPATA FIRST ELEVEN......

Picha
Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah Kibaden ameweka wazi kuwa bado hajapata kikosi cha kwanza na kudai amebakisha mechi mbili za majaribio ili kupata ‘first eleven’ yake ambapo mechi yao na Yanga Jumapili itakuwa miongoni mwa mechi hizo.

HOFU YA KIPIGO DHIDI YA YANGA J,PILI, SIMBA WALIKIMBIA JIJI.......

Picha
Wakati   mabingwa wa ligi kuu ya Bara, Yanga jana walitua kisiwani Pemba kwa ajili ya maandalizi ya mechi yao dhidi ya Simba itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa Jumapili, Wekundu wa Msimbazi wakihamisha kambi kutoka Bamba Beach na kwenda Bagamoyo.

PINDA AMWEKA MATATANI MAGUFULI

Picha
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ametengua maamuzi yaliyofanywa na Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuli ya kuongeza tozo ya asilimia tano kwa wasafirishaji wa malori na mabasi kwa uzito unaozidi.

BOATENG AONDOLEWA GHANA

Picha
Mchezaji wa kiungo cha kati wa timu ya taifa ya Ghana, Kevin-Prince Boateng atakosa mechi ya mkondo wa kwanza ya kujitafutia nafasi kwenye dimba la kombe la dunia dhidi ya Misri, kutokana na jeraha la goti.