Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2026

Tshabalala kuongoza parade la ubingwa Jumamosi

Picha
Afisa Habari wa Young Africans SC, Ally Kamwe, ameendelea kuchanja mbuga na utani wa jadi mara baada ya timu yake kutwaa ubingwa, safari hii akimfanyia dhihaka nahodha wa Simba SC, Mohamed Hussein 'Zimbwe Jr'. Kamwe amedai kwa utani kuwa Zimbwe Jr ndiye atakayeongoza gwaride lao la ubingwa Jumamosi akiwa juu ya basi la wazi la Yanga, akijumuisha kijembe kuwa mara ya mwisho kwa beki huyo kufanya gwaride la ubingwa alipanda gari la mizigo aina ya kenta. ​Ujumbe wa Ally Kamwe ulisikika hivi: ​"Mohamed Hussein ndiye atakayeongoza parade letu Jumamosi, atakaa juu pale kwenye lile bus la ubingwa. Mara yake ya mwisho kufanya parade alipanda kenta. ​Jana alinionyesha kivideo cha miaka sijui elfu moja mia nane na ngapi huko, yupo kwenye kikenta anachungulia".

Al Ittihad Iko tayari kumuuza Aziz Ki

Picha
Klabu ya Al Ittihad SC ya Libya ipo tayari kumuuza kiungo wao mshambuliaji Stephane Aziz Ki ikiwa ofa itafika mezani kwao itakayowaridhisha kuelekea msimu ujao wa 2026-27. Al Ittihad SC imeshamlipa ada ya usajili na mishahara yote kwa Aziz Ki na imekanusha taarifa zilizovuma kuwa hawajalipa pesa hizo baada ya Young Africans SC umuhitaji kiungo Aziz Ki arudi klabuni kwao, Al Ittihad SC wanaheshimu mkataba wao na Aziz Ki na washalipa kila mchezaji ada yake ya usajili na mishahara.

Simba yaiomba Bodi ya Ligi ilete waamuzi wa nje ya nchi

Picha
Uongozi wa klabu ya Simba SC umeandika barua kwenda Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) na TFF kuwataka wachague Waamuzi ambao hawana maamuzi mabaya ya kujirudia. Simba SC ipo tayari kughalimikia Bodi ya Ligi na TFF kuleta Marefa kutoka nje ya nchi ikiwa humu ndani itashindikana