Tshabalala kuongoza parade la ubingwa Jumamosi
Afisa Habari wa Young Africans SC, Ally Kamwe, ameendelea kuchanja mbuga na utani wa jadi mara baada ya timu yake kutwaa ubingwa, safari hii akimfanyia dhihaka nahodha wa Simba SC, Mohamed Hussein 'Zimbwe Jr'. Kamwe amedai kwa utani kuwa Zimbwe Jr ndiye atakayeongoza gwaride lao la ubingwa Jumamosi akiwa juu ya basi la wazi la Yanga, akijumuisha kijembe kuwa mara ya mwisho kwa beki huyo kufanya gwaride la ubingwa alipanda gari la mizigo aina ya kenta. Ujumbe wa Ally Kamwe ulisikika hivi: "Mohamed Hussein ndiye atakayeongoza parade letu Jumamosi, atakaa juu pale kwenye lile bus la ubingwa. Mara yake ya mwisho kufanya parade alipanda kenta. Jana alinionyesha kivideo cha miaka sijui elfu moja mia nane na ngapi huko, yupo kwenye kikenta anachungulia".