Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2023

MAKALA. YANGA IKAFIE UWANJANI NA KUPINDUA MEZA ALGERIA

Picha
WAWAKILISHI wa Afrika mashariki na kati Dar Young Africans, maarufu Yanga SC ilianza vibaya kwenye mchezo wake wa kwanza wa fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika, baada ya kufungwa mabao 2-1 katika uwanja wake wa nyumbani wa Mkapa uliopo jijini Dar es Salaam.  Yanga ilipokea kipigo hicho kutoka kwa USM Alger ya Algeria, hivyo itakuwa na kazi ngumu kwenye mchezo wa marudiano utakaofanyika Jumamosi ijayo mjini Algiers nchini Algeria.  Mimi binafsi sina wasiwasi na Yanga hasa inapofikia kwenye hatua kama hii ambapo Yanga inahitaji kufia uwanjani na mwisho wa siku kuibuka na ushindi ikiwezekana wa mabao 2-0 au zaidi.  Yanga inapewa sapoti kubwa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye amejitolea ndege ya serikali kusafirisha wachezaji wote wa timu hiyo, viongozi na mashabiki ili warudi na kombe na kuwafurahisha Watanzania.  Ingawa mechi hiyo itakuwa ngumu na ya ushindani wa aina yake na hasa kutokana na USM Alger kuonyesha uwezo mkubwa uwanjani na in

3000 KWENDA ALGERIA KUISHANGILIA YANGA

Picha
Ndege aina ya Boeing 787-8 Dreamliner yenye uwezo wa kubeba abiria 260 ndiyo itakayowabeba wachezaji wa Yanga na mashabiki kwenda Algiers nchini Algeria kwa ajili ya mchezo wao wa fainali dhidi ya USM Alger. Yanga wanaondoka kesho Juni Mosi, 2023 kwenye mchezo kwa ajili ya mchezo wao wa marudiano na USM Alger utakaochezwa Juni 3, 2023. Akimzungumza na waandishi wa habari leo Jumatano ya Mei 31, 2023, Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa amesema Rais Samia Suluhu Hassan ametimiza ahadi yake ya kuipa ndege Yanga kwa ajili ya kwenda kuipeperusha bendera ya Taifa kwenye mchezo wa fainali dhidi ya USM Alger. Msigwa amesema zaidi ya mashabiki 3,000 wamejitokeza kwa kupeleka majina yao kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni na Michezo. "Katibu Mkuu amekuwa na kazi kwa siku mbili kwa kuwa ndege inabeba zaidi ya watu 260, huku timu ya Yanga na maofisa wake wakiwa 90," amesema Msigwa "Kwanza kabla ya kutua Algeria itazunguka pale kama mara tatu hivi na huo ni ushindi wa kurudi na ko

Neymar Jr huyooo Man United

Picha
Imeripotiwa kuwa Neymar anataka kujiunga na Manchester United msimu huu wa majira ya joto na sio timu nyingine yoyote. Ripoti kutoka Ufaransa zinadai staa huyo moyo wake wote upo Man United atakapoondoka Paris Saint-Germain na si vinginevyo. Staa huyo mwenye umri wa miaka 31 anapitia wakati mgumu kutoka kwa mashabiki wa PSG kwa miaka kadhaa sasa ukichanganya na majeraha ya mara kwa mara hivyo anatarajiwa kuondoka dirisha hili.

MATOLA AREJESHWA TENA SIMBA

Picha
Leo tumemtambulisha rasmi Kocha Selemani Matola kuwa Kocha mkuu wa timu zetu za vijana chini ya miaka 17 na 20 Pia tumemtambulisha Patrick Rweyemamu kuwa Mkuu wa Programs za vijana za Simba Kwanini Patrick na Matola, wawili hawa wana uzoefu mkubwa kwenye eneo hili la vijana, tunaaamini watafanya makubwa kama ambavyo walifanya hapo awali

ALIYEIUA YANGA KUCHEZA TIMU MOJA NA MAHREZ

Picha
Aymen Mahious wa USM Alger aliyefunga goli la kwanza dhidi ya Yanga katika fainali ya kwanza Kombe la Shirikisho Afrika ameitwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya Algeria kitakachocheza mechi za kufuzu AFCON 2023 dhidi ya Uganda na ya kirafiki dhidi ya Tunisia. Kwa kifupi, huyu bwana wanapasiana na Riyad Mahrez ambaye huwa anampa assist Haaland.

YANGA KUKABIDHIWA UBINGWA WAO SUMBAWANGA JUNI 9

Picha
Bodi ya ligi kupitia kwa afisa hahari wake, Karim Boimanda imesema kuwa, Klabu ya Yanga watakabidhiwa Ubingwa wao wa ligi kuu Juni (9) Mjini Sumbawanga. » Watakabidhiwa kwenye Mchezo wa ligi kuu dhidi ya klabu ya Tanzania Prisons ambao wamechagua kamalizia mechi zao katika dimba la Nelson Mandela Sumbawanga. » Pia bodi imeeleza kusikia ushauri wa baadhi ya wadau wa soka kuhusu ratiba ngumu inayoikabiri klabu ya Yanga. Bodi hiyo imesema muda ni mfinyu ligi inatakiwa kumalizika Juni (9) hivyo ratiba itabaki vilevile, hakuta kuwa na mabadiliko. » Mchezo wa fainali ya (FA) baina ya Azam dhidi ya Yanga utachezwa tarehe ileile Juni (12) katika uwanja wa Mkwakwani Tanga.

PILATO WA USM ALGER NA YANGA HADHARANI

Picha
Shirikisho la Soka barani Afrika CAF limemtangaza mwamuzi Dahane Beida kutoka nchini Mauritania kuchezesha mchezo wa fainali ya pili ya kombe la Shirikisho Afrika kati ya USM Alger dhidi ya Yanga SC mchezo ambao utachezwa uwanja wa Julliet 5, Jijini Algers nchini Algeria, Mwamuzi huyo atasaidiwa na Jarson Dos Santos kutoka Angola na Arsenio Marngol kutoka Nchini Msumbiji.

PAUL NONGA KUSTAAFU SOKA MBELE YA YANGA

Picha
Wakati ligi ikitaraji kufika ukomo June 9, 2023 kwa upande wa mshambuliaji Paul Nonga wa Mbeya City amesema atahitimisha safari yake ya kusakata kabumbu katika mechi ya mzunguko wa 29 ya ligi kuu wakati timu yake ya Mbeya City FC @officialmbeyacityfc itakapoikaribisha Young Africans sports club June 6,2023. Nje ya soka Nonga ambae jina la utani huitwa 'Baba Paroko' tofauti na kucheza mpira kitaaluma yeye ana taaluma ya kupasua miamba migodini (Blaster). Nonga amesema amelazimika kupumzika rasmi kucheza kutokana na kuandamwa na majeraha ya muda mrefu, licha ya kupumzika bado ataendelea kuutumikia mpira wa miguu kwa upande mwingine kama kocha msaidizi wa timu yake ya Mbeya City FC kwa sasa. Ikumbukwe Nonga ana leseni C ya ukocha ya CAF Klabu alizopita ni Yanga SC, Mwadui FC, Lipuli FC, Gwambina FC, JKT Oljoro na Mbeya City FC ambayo anaitumikia kwa mara ya pili hapo. Pongezi kwake miaka karibia 13 ya soka sio haba kwake.

HAALAND AMFUNIKA KWA MABAO KANE

Picha
Erling Haaland amefunga magoli 36 kwenye Ligi Kuu ya England msimu huu, yaliyochangia Manchester City kutwaa ubingwa wa tatu mfululizo. Kwa upande mwingine Harry Kane amefunga magoli 30, Tottenham Hotspur ikimaliza katika nafasi ya nane. Baadhi ya wachambuzi wanaamini kuwa endapo Kane angekuwa na na timu bora kama Man City huenda angefunga magoli zaidi ya Halaand.

YANGA YAIPORA MCHEZAJI SIMBA

Picha
Mabosi wa Klabu Bingwa Tanzania Bara Young Africans wanadaiwa kuifanyia umafia Simba SC kwa kupanda dau kwenye kuipata saini ya beki wa Ihefu FC, Yahaya Mbegu, ambaye taarifa zinasema amemalizana na Singida Big Stars. Sasa baada ya taarifa hizo kuwepo, Young Africans wenyewe wametua huko Singida kuhamisha usajili huo kabla ya jina lake kuingizwa kwenye mfumo wa usajili wa Shirikisho la Soka Tanzania ‘TFF’. Mbegu alijiunga na Ihefu FC msimu huu, na kujihakikishia namba katika kikosi cha kwanza, jambo ambalo timu nyingi zimeanza kumpigia hesabu.

NAIBU WAZIRI WA MICHEZO MWANAFA AKIISAPOTI YANGA

Picha
Naibu waziri wa Michezo, Sanaa na Utamaduni, Mhe Khamis Mwinjuma maarufu MwanaFA alipoudhuria uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam akiwa amevalia jezi ya Yanga kuisapoti timu hiyo wakati ilipocheza na USM Alger katika mchezo wa fainali mkondo wa kwanza. Kwenye mchezo huo Yanga ikiwa nyumbani ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-1, timu hizo zitarudiana Jumamosi ijayo ya tarehe 3., Juni ambapo Yanga inatakiwa kushinda mabao 2-0 ili kurejea na kombe

MASHUJAA YANUSA LIGI KUU

Picha
Klabu ya Mashujaa ya mkoani Kigoma imeipiga klabu ya Pamba ya Mwanza Kwa ushindi wa jumla Kwa mabao 5-4. Mchezo wa Kwanza Mashujaa waliibuka na ushindi wa 4-0, Mchezo wa pili Pamba walishinda 4-1 bao moja la Mashujaa likatoa nafasi Kwa kuweka mguu mmoja mbele. Mashujaa Sasa wanasubiri Mchezo mmoja Dhidi ya timu itakayo cheza PlayOff Kutoka Ligi kuu ya NBC Premier league ili Kujua hatima yao ya kupanda Ligi Kuu.

SIMBA WAMLILIA SHABIKI ALIYEFARIKI UWANJA WA MKAPA JANA

Picha
Uongozi wa klabu ya Simba umetoa salamu za pole kwa familia ya shabiki aliyefariki dunia katika msongamano wa kuingia uwanjani kwa Mkapa jijini Dar es Salaam kushuhudia fainali ya kwanza Kombe la Shirikisho Afrika baina ya Yanga dhidi ya USM Alger jana Jumapili. “Kwa masikitiko makubwa Klabu ya Simba inatoa pole kwa familia ya shabiki aliyefariki Uwanja wa Benjamin Mkapa wakati akiwa katika jitihada za kuingia kushuhudia mechi ya fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Yanga dhidi ya USM Alger ya Algeria leo (jana) Mei 28, 2023,” ilisema taarifa hiyo. Shabiki huyo alikuwa miongoni mwa watu 30 waliojeruhiwa na kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya Temeke ambapo alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu.

KOCHA USM ALGER AINGIA MCHECHETO KWA YANGA

Picha
“ Tunarudi Algeria lakini bado mechi haijaisha, ni asilimia 50 kwa 50. Bado tuna kazi ya kufanya Algeria kwa sababu katika mechi ya marudiano Yanga hawana cha kupoteza. Watacheza wanavyojua ili wapate matokeo. ” Kocha wa USM Alger Benchikha Abdelhak baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Yanga

YANGA KUSHUSHIWA RUNGU NA CAF

Picha
Huenda klabu ya Yanga ikakutana na adhabu kutoka Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) baadaya siku ya Jana mashabiki kupata kadhia ya kuingia uwanjani Hali iliyopelekea Zaidi ya mashabiki 30 Kujeruhiwa na Kukimbizwa Hospitali Huku Shabiki mmoja Akifariki duniani. Tukio kama hili liliwahi kuikuta Klabu ya ES TUNISIA , Baada ya vurugu za mashabiki Katika Mchezo wao dhidi ya JS Kabylie na shabiki mmoja kupoteza maisha, Es Tunis walifungiwa kucheza mechi zao bila mashabiki Raja Casablanca nao kutoka Morocco Baada ya vurugu Kutokea kwenye mechi yao dhidi ya Al Ahly CAF Waliwafungia na kutakiwa kucheza nje ya Morocco michezo yao miwili ya mkondo wa kwanza endapo watashiriki msimu ujao.

NCHIMBI KUTUA KITAYOSCE

Picha
Kitayose FC iko mbioni kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa zamani wa Azam FC, Yanga na Geita gold Ditram Nchimbi (30, Tayari makubaliano ya mtu binafsi yamefikiwa na siku chache zijazo Ditram Nchimbi atasaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Kitayosce inaweza kuthibitisha.

NABI AIKATIA TAMAA YANGA

Picha
“Kwa sasa siwezi kutoa ahadi ya uongo lakini bado nina matumaini mechi haijaisha. Ninajua timu yangu ina uwezo wa kwenda kupata magoli ugenini. Leo tumemiliki mpira kwa asilimia 65, kwa hiyo inaonesha tuna ubora utakaotufanya tupate matokeo ya ushindi ugenini" “Siwezi kuahidi 100 kwa 100 tutarudi na kombe, lakini tutajitolea kwa kadri ya uwezo wetu kwa sababu hatuna tena cha kupoteza” -Kocha wa Yanga SC Nasreddine Nabi baada ya kufungwa goli 2-1 nyumbani na USM Alger kwenye mchezo wa kwanza wa Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika. Mechi ya marudiano itapigwa Juni 03 Algeria.

MWAKALEBELA ALIGOMEA GOLI LA PILI LA USM ALGER

Picha
Aliyekuwa makamu wa Rais wa Yanga SC, Fredrick Mwakalebela amesema bao la pili walilofungwa na USM Alger ilikuwa ni 'offside' kwa mujibu wa jicho lake la kitaalam hata hivyo wameyapokea matokeo anaamini benchi la ufundi watajipanga vyema katika mchezo wa marudiano nchini Algeria Juni 3, 2023. “Haya ni mashindano makubwa Afrika hivyo mechi ilikuwa nzuri dakika zote tisini na Yanga imecheza vyema kuanzia kipindi cha kwanza hadi cha pili hivyo haikuwa bahati“ amesema Mwakalebela.

SAIDO NTIBANZOKIZA ATEMWA BURUNDI

Picha
Kikosi cha timu ya taifa ya Burundi kimetangazwa kwa ajiri ya kujiandaa kuwakabili Namibia. ◾Ndikumana Justin ◾Mutombo Fabien ◾Onesime Rukundo ◾Bizimana Aladin ◾Ndayishimiye Youssouf Nyange ◾Christophe Nduwarugira ◾Derrick Mukombozi ◾Harerimana Rashid Léon ◾Nshimirimana David ◾Marco Weymans ◾Nshimirimana Ismail Pitchou ◾Muhindo Collins ◾Nshimirimana Jospin ◾Jordi Liongola ◾Musore Aaron ◾Bigirimana Abedi ◾Mvuyekure Emmanuel ◾Nahimana Shassir ◾Irakoze Donasiyano ◾Girumugisha Jean Claude ◾Niyongabire Pacifique ◾Bimenyimana Bonfils Caleb ◾Hussein Tchabalala ◾Saido Berahino ◾Kanakimana Bienvenue ◾ B. Richard ◾Crispaldinho Saido Ntibanzokiza hajaitwa katika kikosi hicho kwa sabbau za utovu wa nidhani katika Timu ya Taifa, ikumbukwe kuwa yeye ndio captain katika kikosi hicho.

Makala: NI DHARAU KUBWA KUMLINGANISHA NA KAGERE

Picha
NIMETEMBELEA baadhi ya kurasa za mitandao ya kijamii hasa kwenye Facebook, Instagram na magroup ya Whatsaap ambapo baadhi ya wadau wakafikia hatua ya kuwafananisha Fiston Kalala Mayele na Meddie Kagere.  Kilichonishangaza na kuona ni dharau kubwa waliyomfanyia mshambuliaji wa kimataifa wa DR Congo Fiston Mayele ambaye pia ni mshambuliaji tegemeo wa Yanga SC, kumfananisha Mayele na Kagere ni dharau.  Watu walioleta ushindani huo wa Mayele na Kagere ulitokana na Kagere wa misimu minne iliyopita na Mayele wa sasa, ushindani huo wa Mayele sio na Kagere wa sasa anayeichezea Singida Big Stars kwa mheshimiwa Mwigulu Nchemba.  Na pia simdharau Kagere, kwani ni mmoja kati ya washambuliaji hatari waliowahi kung' ara kwenye Ligi Kuu bara na kuweza kuibuka mfungaji bora misimu miwili mfululizo. Kagere alisajiliwa na Simba msimu wa 2018/2019 akitokea Gor Mahia ya Kenya na alifanikiwa kuibuka mfungaji bora ndani ya msimu wake wa kwanza.  Mshambuliaji huyo wa kati alivunja rekodi za Amissi Tambwe

YANGA YAFA KIUME KWA MKAPA

Picha
Na Ikram Khamees. Mabingwa wa soka Tanzania bara na wawakilishi pekee wa Afrika mashariki na kati katika michuano ya kimataifa Dar Young Africans, maarufu Yanga SC jioni ya leo imeanza vibaya fainali yake ya kwanza ya kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya kufungwa mabao 2-1 na timu ya USM Alger ya Algeria. Mchezo huo wa mkondo wa kwanza ulifanyika katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, timu hizo zitarudiana Jumamosi ijayo huko jijini Algiers nchini Algeria ambapo ili Yanga iweze kutwaa ubingwa inatakiwa kushinda mabao 2-0. Aymen Mahious aliisaidia USM Alger kuongoza kwa bao la kwanza kunako dakika ya 32 kipindi cha kwanza kabla ya Fiston Mayele wa Yanga kuisawazishia timu yake bao dakika ya 82, wakati mashabiki wa Yanga wakiendelea kushangilia goli la Mayele. USM Alger waliongeza goli la pili dakika ya 84 kupitia kwa Islam Meriji na kumaliza mchezo ikiwa mshindi, Yanga bado ina nafasi ya kushinda ugenini na kurudi na kombe, katika mchezo wa leo timu zote zilishambuliana kwa

NYOTA BARCELONA AMPATA MAMA YAKE MZAZI BAADA YA KUPOTEZANA

Picha
Mama huyu kutoka katika nchi ya Liberia aitwaye Nancy Pyne amesema Frenkie Kessie ni mtoto wake na wamepotezana baada ya mme wake kuwaomba awapeleke shule katika nchi ya Ivory Coast na baada ya hapo hawajawahi kumuona tena zaidi ya kuishia kwenye vyombo vya habari. Mama huyo amesema waliondoka nyumbani wakiwa watoto wadogo wakiwa na kaka ake ambao wote walikuwa wadogo na baada hapo alisikia wameenda Ulaya na baba huyo alikataa mawasiliano ili wasiwasiliane tena na huku kwakua mama huyo hakuwa na uwezo wowote hakufanya kitu chochote zaidi ya miaka yote hakuwa na usingizi mzuri "Alisema hivyo" Baba ake Frenkie na kaka ake aliwambia hawana mama ndiyo maana Frenkie Kessie alikuwa anaulizwa mama mzazi yupo wapi??? Alikaa kimya na kuwajibu kwamba hana mama, baba ndiyo aliwakuza . Baada ya kusikia taarifa hizo Frenkie Kessie amepewa ruhusa na klabu yake ya Barcelona na ametumia usafiri wake binafsi kusafiri mpaka ufaransa kwaajiri ya kuonana na kaka yake ili kumtafuta mama huyo ili

IBRAHIM CLASS ATWAA MKANDA WA SUPER FEATHER

Picha
Ibrahim Class ameshinda Mkanda wa uzito wa kati (Super Feather) katika pambano hilo baada majaji wote watatu kumpa ushindi wa pointi 98-91, 97-92, 97-92 Akizungumza baada ya pambano hilo la Raundi 10 lililofanyika Masaki, Dar es Salaam, Class amesema “Nilijua nitampiga mpinzani wangu kwa kuwa nilishasema tangu awali kuwa huyu si Bondia bali ni mpiga debe.” Upande wa #SaidChino amesema “Nataka nirudiane naye, Class sio mkali, ameshinda kwa kuwa kuna mambo yametokea lakini uwezo wake bado na ndio maana huwa anapewa mabondia wa mchongo kupigana nao."

SANDALAND WADHAMINI WAPYA WA JEZI SIMBA SC

Picha
Taarifa zilizotufikia zinasema kwamba huenda duka kubwa la kuuza mavazi ikiwemo vifaa vya michezo la Sandaland muda wowote linaweza kuchukua nafasi ya Vunjabei na kuwa wadhamini wa jezi wa klabu ya Simba SC. Sandaland ndiye atakuwa mzalishaji mpya na msambazaji wa jezi za Simba msimu ujao na tayari alikuwa China akifyatua uzi wa mnyama.

MOHAMED KACHUMARI AFARIKI DUNIA

Picha
Beki wa zamani wa timu ya Kikwajuni, Small Simba, Mlandege na Mafunzo, Moh'd Kachumbari amefariki Dunia asubuhi ya leo Jijini Dar es Salam. Mwili wa marehemu unatarajiwa kusafirishwa mchana huu kutoka Dar kwenda kuzikwa nyumbani kwao Zanzibar. Marehemu Kachumbari pia aliwahi kucheza timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) na Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars). Inallillah Wainailah Rajiun, Mwenyezi Mungu amsamehe makosa yake 🤲.

MASHABIKI YANGA WALALAMIKIA UTARATIBU WA KUINGIA UWANJANI

Picha
Mashabiki na wanachama wa Yanga SC wanaonekana kulalamika na kukerwa na mfumo wa kuingia uwanjani kutokuwa na ufanyaji kazi vizuri, wengi wa mashabiki wanasema kuwa kadi zao za malipo za mfumo wa N-Card zimekuwa zikikataa kusoma ilihali wamelipia tiketi siku nne zilizopita. Pia wamedai kuwa wamekua wakiambiwa watoe fedha (10,000/= hadi 20,000/=) ili waruhusiwe kuingia uwanjani ,ilihali tayari wamelipia tiketi.

MASHUJAA KAMA LUTON TOWN CITY, NAYO KUPANDA LIGI KUU

Picha
Timu ya Luton Town FC Imepanda Ligi Kuu ya Uingereza Kwa Mara ya kwanza Katika Historia Timu Hiyo Ilikuwa Inashika Nafasi ya 5 Katika Msimamo wa Ligi ya Championship na Kwenda Kucheza Playoff na Timu ya Coventry City Ambayo ilikuwa kwenye Msimamo lakini Wamefanikiwa Kuwashangaza wengi Kupata Ushindi Kwa Mikwaju ya Penalty na Kupanda Daraja Hivyo Hivyo Historia ya Luton Town haipishani na Timu ya Mashujaa FC kutoka Kigoma ambayo inapambana Kuuheshimisha Mkoa huo Baada ya Kukosa Kushuhudia Ligi Kuu Kwa Miaka zaidi ya 20 sasa Mashujaa Ilimaliza Katika Nafasi ya 4 Katika Ligi ya Championship na kupangiwa Kucheza Playoff na Timu ya Pamba Ambayo ilikuwa Inashika Nafasi ya 3, Mchezo wa Mkondo wa kwanza Mashujaa walishinda 4-0 Nyumbani kwao Leo ni Mechi ya Mwisho itapigwa Pale Jijini Mwanza

PAMBA YAIKATIA RUFAA KITAYOSCE FIFA

Picha
(FIFA) wamepokea barua ya Pamba FC kuhusu sakata la Upangaji wa matokeo. Katibu mkuu wa klabu ya Pamba, Jonson James amethibitisha kuwa, shirikisho la soka Duniani (FIFA) limewajibu kuwa wamepokea malalamiko yao na watayafanyia kazi. Klabu ya Pamba kupitia mawakili (4) waliandika barua kwenda katika kamati ya maadili ya (FIFA) kuitaka itoe adhabu kwa klabu ya Kitayosce ambao mwenyekiti wao alikutwa na hatia ya upangaji wa matokeo akafungiwa maisha na (TFF) kujihusisha na soka huku klabu ya Kitayosce ikiachwa bila kupewa adhabu. "Sakata la upangaji wa matokeo Championship baina ya klabu za Kitayosce na Fountain gate limefika rasmi (FIFA) kupitia Pamba FC.

YACOUBA SOGNE KUTUA KITAYOSCE

Picha
Uongozi wa Klabu ya Kitayosce FC (Tabora united) umedhamiria kumsajili Mshambuliaji wa Ihefu FC Yacouba Sogne pamoja na Mshambuliaji wa zamani wa Young Africans Herietier Makambo ili kuboresha kikosi cha klabu hiyo ambayo itashiriki kwa mara ya kwanza Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao 2023/24. Kitayosce FC itashiriki Ligi Kuu msimu ujao ikitokea Ligi ya Championship sambamba na Mabingwa wa ligi hiyo JKT Tanzania, na sasa imeanza kujipanga kufanya usajili wa wachezaji wenye uzoefu na Mshike Mshike wa michuano hiyo mikubwa nchini Tanzania. Katibu Mkuu wa timu hiyo, Adam Simba amesema wanataka kuwasajili Yacouba Sogne pamoja na Herietier Makambo ambao anaamini kuwa watawasaidia kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao wa mwaka 2023/24.

BAYERN MUNICH MABINGWA TENA UJERUMANI

Picha
BAYERN MUNICH wametwaa Ubingwa wa Ligi Kuu Ujerumani kwa mara ya 11 Mfululizo baada ya kushinda kwa goli 2-1 dhidi ya FC Koln huku Borussia Dortmund wakisare kwao 2-2 dhidi ya Mainz 05.

USM ALGER WAPASHA KWA MARA YA MWISHO KABLA YA KUIVAA YANGA KESHO

Picha
Kikosi cha USM Alger kimefanya mazoezi yake ya mwisho jioni ya leo kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa kabla ya kuwavaa Yanga hapo kesho.