Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2017

Chirwa mambo safi Yanga

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Kamati ya nidhamu, sheria na haki za wachezaji ya Shirikisho la mpira wa miguu nchini, (TFF) imemaliza utata uliokuwa ukiwaandama wachezaji wa Yanga, Obrey Chirwa raia wa Zambia na Simon Msuva ambao walisimamishwa kutokana na makosa waliyofanya msimu uliopita. Nyota hao wawili walisimamishwa kucheza Ligi Kuu ya Vodacom msimu huu baada ya kudaiwa kumsukuma mwamuzi aliochezesha mechi kati ya Yanga na Mbao FC mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu Bara. Msuva yeye tayari ameshaachana na Yanga ambapo amesajiliwa na Difaa El Jajida ya Morocco wakati Chirwa bado anakipiga Yanga na amekosa mechi mbili moja ikiwa ya Ngao ya Jamii dhidi ya Simba na nyingine ya Ligi Kuu Bara. Lakini leo hii kamati hiyo imetangaza kuwaachia huru nyota hao, kwa maana hiyo Chirwa sasa ataichezea Yanga katika mechi zijazo za Ligi Kuu Bara wakati Msuva ataitumikia timu ya taifa, Taifa Stars ambayo mwishoni mwa wiki itacheza na Botswana mchezo unaotambuliwa na Fifa Obrey Chirwa yuko huru sas

Joseph Kimwaga ndio basi tena

Picha
Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam Nadhani mnamkumbuka vema Joseph Kimwaga yule kiungo mshambuliaji wa Azam FC aliyewahi pia kusajiliwa na Simba, Kimwaga aliibuliwa kutoka Azam Academy ambapo alipangwa kwenye mchezo dhidi ya Yanga na kufunga bao la ushindi. Katika mchezo huo Azam iliifunga mabao 3-2 mchezo wa Ligi Kuu Bara, kwa taarifa yako Kimwaga aliingia dakika za lala salama lakini alifumua bonge la shuti mpira ukaingia nyavuni na kuwalaza Yanga mchana kweupee, kuanzia hapo jina lake lilianza kujulikana. Akaanza kupata sifa hadi akaitwa timu ya taifa, Taifa Stars, lakini aliumia na kupoteza namba kwenye kikosi cha Azam, akapotea taratibu kisha kutemwa kwenye kikosi hicho, lakini Simba wakamchukua bhana, akatua na kuanza kurudisha heshima yake iliyopotea. Akiwa na Simba pia akapotea baada ya kuumia, Simba nao wakamtema, kijana huyo akapotea tena na hakuna aliyejua taarifa zake, ndipo alipoibuka tena baada ya Azam kumrejesha kikosini, lakini dogo kaumia tena mazoezini huko Mtwara wa

NDUDA KUTIBIWA INDIA

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Mlinda mlango namba mbili wa mabingwa wa Ngao ya Jamii, Simba SC, Said Mohamed Nduda amatazamiwa kupelekwa nchini India kufanyiwa upasuaji wa goti. Kipa huyo aliumia akiwa mazoezini huko Zanzibar wakati klabu yake ya Simba ikijiandaa na mchezo wa kuwania Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga SC mchezo ambao ulipigwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Taarifa iliyotolewa jana na uongozi wa Simba umesema wanampeleka India kipa huyo bora wa michuano ya Cosafa iliyofanyika nchinj Afrika Kusini Nduda (Kushoto) akipokea zawadi yake ya kipa bora wa Cosafa

Ishu ya kukutwa fuvu la binadamu Uwanja wa Taifa iko hivi

Picha
Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam Kumeibuka wasiwasi kwa mafundi wanaokarabati uwanja wa Taifa Dar es Salaam baada ya kuliona fuvu linalodaiwa kuwa la binadamu ambalo lilifukiwa chini ya uwanja huo. Haijajulikana kama fuvu hilo lilizikwa lini na watu gani, lakini imani za kishirikina zimetajwa, mafundi hao wa moja ya kampuni iliyopewa kandarasi ya kukarabati uwanja huo imeanza kuingia shaka. Watani wa jadi Simba na Yanga wanatajwa kuhusika na fuvu hilo kwakuwa waliutumia uwanja huo Jumatano iliyopita walipokutana katika mchezo wa kuwania Ngao ya Jamii ambapo Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 baada ya sare tasa 0-0. Vitendo vya imani ya kishirikina vimekuwa vikilaaniwa vikali kwani vimehusisha roho za watu ikiwemo fuvu hilo la binadamu, hata hivyo vilabu vya Simba na Yanga vimegoma kuzungumzia ishu hiyo vikidai havitambui kuwepo kwa ushu hiyo kwani wao wanajihusisha na soka Mafundi wa Uwanja wa Taifa wamelifukua fuvu la binadamu

HAMOSNOTA AACHIA BONGE LA SINGO

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Mwanamuziki wa kizazi kipya Hashim Momba "Hamosnota"  ambaye kwa sasa anakuja juu na wimbo wake uitwao "Pole", ameachia bonge la singo linalokwenda kwa jina la "Uwezo sina" ambao ameurekodi katika studio za Jean Records chini ya prodyuza machachari Naroh Wings. Akizungumza na Mambo Uwanjani, Hamosnota amesema ameamua kuachia wimbo mpya kwakuwa mashabiki wake wanataka radha, anasema baada ya kuachia wimbo wa Pole ambao ulipata wafuasi wengi, sasa amekuja kivingine. "Wimbo wangu huu tofauti na ule wa Pole ambao ulikuwa wa kutulia, lakini wimbo huu mpya unachezeka na si wa taratibu kama ule", alisema Hamosnota ambaye amewataka mashabiki wake kujiandaa na video ya wimbo huo atakairekodi hivi karibuni. Msanii huyo amedai alikwama kutengeneza video baada ya kufuatia kufiwa na baba wa mke wake hivyo kumeweza kumfanya asimamishe shughuri zake, wimbo huo tayari ameshausambaza mitandaoni bado kwenye vituo vya redio na

YANGA YAANZA KWA SARE LIGI KUU BARA

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga SC imeanza vibaya Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kulazimishwa sare na wageni wa ligi hiyo Lipuli FC ya Iringa kwa kufungana bao 1-1 katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Yanga leo hawakucheza kama walivyokutana na Simba na hata kiungo wake mpya Mkongoman Papy Tshishimbi hakufanya yale aliyofanya dhidi ya Simba, Seif Abdallah Kalihe alianza kuifungia Lipuli bao la kwanza katika dakika ya 44 kipindi cha kwanza. Yanga wakasawazisha dakika ya 45 kabla ya kuelekea mapumziko goli lililofungwa na Mzimbabwe Donald Dombo Ngoma, hata hivyo Lipuli walimaliza wakiwa pungufu baada ya nahodha wao Asante Kwasi kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kuonyesha utovu wa nidhamu. Kipindi cha pili nacho hakikuwa na magoli kwani timu zote zilishambuliana kwa zamu ingawa Yanga walionekana kuutawala mchezo licha ya Lipuli kurudi nyuma na wachezaji kujiangushaangusha hovyo ili kupoteza muda, kwa matokeo hayo Y

Yanga na udambwidambwi wa Tshishimbi leo

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga SC wanashuka uwanja wa Uhuru jioni ya leo kuwakaribisha Lipuli FC ya Iringa mchezo wa Ligi Kuu Bara. Mabingwa hao wametoka kufungwa na watani wao wa jadi Simba SC mabao 5-4 yaliyopatikana kwa matuta kufuatia sare tasa ya 0-0 mchezo wa kuwania Ngao ya Jamii uliofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Lakini licha ya Yanga kupoteza kwa matuta, wameibuka kidedea kutokana na mchezaji wao Papy Tshishimbi kupiga mpira mkubwa kiasi kwamba aliweza kuwafunika nyota wote wa Simba, Emmanuel Okwi na Haruna Niyonzima. Hivyo mashabiki wa Yanga watajitokeza kwa wingi kumuona tena akifanya vitu vyake adimu mbele ya vijana wa Lipuli wanaonolewa na Seleman Matola, Lipuli nao wametamba kuonyesha soka safi kwani nao wana wachezaji mahiri kama vile ilivyo Yanga Papy Tshishimbi akifanya yake

Simba yaanza na kifurushi cha wiki, Okwi akamatiki

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Mabingwa wa Ngao ya Jamii, Simba SC jioni ya leo wameanza vema Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Baada ya kuichakaza vibaya Ruvu Shooting ya Mlandizi mkoani Pwani mabao 7-0 Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Mchezo ulikuwa wa upande mmoja ambapo Simba walianza kuutawala huku viungo wake James  Kotei na Mzamiru Yassin wakicheza vizuri, Emmanuel Okwi amefunga magoli manne peke yake huku akisaidia kuseti lingine moja ambalo lilifungwa na Erasto Edward Nyoni. Magoli mengine ya Simba yamefungwa na Juma Luizio Ndanda na Shiza Kichuya, kwa matokeo hayo Simba imekalia kiti cha uongozi wa ligi. Matokeo mengine kama ifuatavyo. Kule mjini Mtwara katima uwanja wa Nangwanda Sijaona, Azam FC imewalaza wenyeji Ndanda FC bao 1-0, mjini Shinyanga, Mwadui imeifunga Singida United mabao 2-1 uwanja wa Mwadui Complex. Mtibwa Sugar imeutumia vema uwanja wake wa nyumbani wa Manungu Complex baada ya kuilaza Stand United bao 1-0, Mbao FC imeichapa Kagera Sugar pia bao 1-0 kati

MAYANGA ATANGAZA KIKOSI CHA STARS NA KUWARUDISHA WAKONGWE

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Kocha mkuu wa timu ya taifa, Taifa Stars, Salum Shaaban Mayanga, leo ametangaza majina ya wachezaji wa timu ya taifa, Taifa Stars watakaoingia kambini kujiandaa na mchezo wa kirafiki unaotambuliwa na Fifa. Katika kikosi hicho, Mayanga amewarudisha tena wakongwe Mwadini Ally na Kevin Yondan huku akimtema kipa bora wa michuano ya Cosafa Castle Cup, Said Mohamed Nduda ambaye ni majeruhi. Kikosi kamili hiki hapa: Makipa: Aishi Manula (Simba SC) Mwadini Ally (Azam FC) Ramadhan Kabwili (Yanga SC) Mabeki: Gardiel Michael (Yanga SC) Boniface Maganga (Mbao FC) Kevin Yondan (Yanga SC) Salim Mbonde (Simba SC) na Erasto Nyoni (Simba SC). Viungo: Himid Mao (Azam FC) Hamisi Abdallah (Sony Sugar ya Kenya) Mzamiru Yassin (Simba SC) Said Ndemla (Simba SC) Simon Msuva (Difaa El Jadida ya Morocco) Shiza Kichuya (Simba) Farid Musa (Tennerife ya Hispania) Morel Ergenes (Famalicao ya Ureno) Washambuliaji: Raphael Daudi (Yanga SC) Kevin Sabato (Mtibwa Sug

Simba kuendeleza mauaji kwa Ruvu Shooting leo!

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Mabingwa wa Ngao ya Jamii, Simba SC jioni ya leo inashuka katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kuchuana na masarange wa Ruvu Shooting ya Mlandizi Pwani mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.. Simba ambao Jumatano iliyopita iliifunga Yanga mabao 5-4 kwa changamoto ya penalti, baada ya kutoka sare tasa 0-0 ndani ya dakika 90 na kutwaa Ngao ya Jamii, leo itataka kuendeleza mauaji ili kuzidi kuwafurahisha mashabiki wake. Mkuu wa kitengo cha Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba, Haji Sunday Manara amesema ni lazima Simba leo ishinde kwakuwa wanataka kuwathibitishia mashabiki wake kuwa msimu huu watabeba ubingwa wa VPL. "Mashabiki njooni kwa wingi uwanjani mushuhudie kikosi chenu kinavyoanza ligi kwa kishindo na msimu tutabeba ubingwa", alisema Manara ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Yanga SC, Sunday Manara "Computer" Wachezaji wa Simba

Fifa yaipongeza Tff kwa kupata uongozi mpya

Picha
Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam Shirikisho la soka duniani,(Fifa) limewapongeza viongozi wote wapya waliochaguliwa kuliongoza tena kwa miaka minne ijayo. Fifa kupitia kwa rais wake, Gian Ifontinho amewatumia salamu za pongezi viongozi hao ambao walishinda katika uchaguzi uliofanyika mjini Dodoma. Wallace Karia alichaguliwa kuwa rais wa shirikisho hilo wakati Michael Wambura alichaguliwa kuwa makamu wa rais huku wajumbe wa kamati ya utendaji nao wakiingia katika shirikisho hilo. Uongozi wa Jamal Malinzi ulimaliza muda wake lakini ukashindwa kusimama imara baada ya Malinzj na watendaji wake kushikiliwa na Jeshi la polisi kwa kukutwa na makosa mbalimbali ikjwemo kughushi nyaraka na utakatishaji fedha Rais wa Fifa,Gian Infotinho akiipongeza Tff kwa kupata viongozi wapya

PAZIA LA LIGI KUU BARA KUFUNGULIWA KESHO

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Pazia la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara linafunguliwa kesho kwa viwanja saba kutimua vumbi, katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona, wenyeji Ndanda FC watawaalika wauza lambalamba wa Azam FC wakati Kagera Sugar watawakaribisha Mbao FC katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba. Mabingwa wa Ngao ya Jamii, Simba SC wao watawakaribisha Ruvu Shooting katika Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam wakati Mwadui ya Shinyanga itaawalika Singida United ya pale Singida, Mtibwa Sugar watakipiga na Stand United katika Uwanja wa Manungu. Mji Njombe ya mkoani Njombe yenyewe itawakaribisha Prisons katika Uwanja wa Sabasaba Njombe huku Mbeya City ikiwaalika Majimaji ya Songea, ligi hiyo itaendelea tena Jumapili ambapo mabingwa watetezi Yanga SC watawakaribisha Lipuli ya Iringa katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam Pazia la Ligi Kuu linafunguliwa kesho

Kesho ni Simba na Ruvu Shooting Taifa

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajia kuanza rasmi kesho ambapo viwanja saba vinatatimua vumbi kwa timu 14 kushuka uwanjani. Lakini mechi ambayo itakuwa balaa ni kati ya Wekundu wa Msimbazi, Simba SC na Ruvu Shooting katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Tayari vijana wa Ruvu Shooting wanaotokea kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Ruvu Mlandizi mkoani Pwani wapo Dar es Salaam kujiandaa na mchezo huo. Simba ambao wametoka kutwaa Ngao ya Jamii Jumatano iliyopita baada ya kumfunga mtani wao wa jadi Yanga mabao 5-4 kwa changamoto ya penalti baada ya sare tasa 0-0 Uwanja wa Taifa, wapo kamili kuwavaa wanajeshi hao na Msemaji wa Simba Haji Sunday Manara amesema ushindi kwao ni kama uji kwa mgonjwa. Lakini msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire amejinadi kuibuka na ushindi kwa kudai Simba ni sawa na toi la Kichina kwani Kariakoo hakuna Simba Kikosi cha Ruvu Shooting

Shamte aja na Tanzania ya usafi

Picha
Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam Tangia kuingia madarakani kwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli, Watanzania wamekuwa wakifanya usafi kila ifikapo Jumamosi na kwa msisitizo mkubwa kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi imekuwa ikichukuliwa mkazo. Msanii Shukuru Nassoro "Shamte" anayeimba muziki wa kizazi kipya ameamua kuja na wimbo unaosisitiza ufanyaji usafi, wimbo huo unaitwa "Tanzania ya Usafi" ambapo amewashirikisha wasanii wa kundi la Hisia Soul Band lenye maskani ya Temeke. Ndani ya wimbo huo zimesikika aauti za vijana Y. Handsome na Rubians ambapo wameutendea haki wimbo huo ambapo umeanza kuteka hisia katika vituo mbalimbali vya redio pamoja na kwenye mitandao ya kijamii. Kufanya vizuri kwa wimbo huo, kunamrudisha tena hewani Shamte ambaye siku za hivi karibuni alipotea kidogo kutokana na ubize aliokuwa nao, msanii huyo amesema ndio kwanza moto umeanza kuwaka hivyo mashabiki wake wakae mkao wa kula kwani ngoma zinaanza kutoka Sh

CCM YAIGALAGAZA CHADEMA KWENYE DRAFT

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Wakati jana kukipigwa pambano la watani wa jadi wa soka la Tanzania Bara Simba na Yanga katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam kuwania Ngao ya Jamii, maeneo ya Tabata pia Dar es Salaam kulipigwa mechi ya mchezo wa draft kati ya Steven Mruge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Thadeo Kirufi "Ted" wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Katika mchezo huo Steven Mruge wa CCM alimshinda Ted wa CHADEMA kwa mabao 3-2, washindani hao wawili walianza kwa kupaniana kabla ya kuanza kuchuana na walipoanza kucheza Mruge alikuwa akimnyanyasa Ted na kumfunga mabao hayo matatu. Ingwe ya pili Ted alicharuka na kuanza kukomboa mabao hayo lakini mwisho mchezo huo ukawa umemalizika hasa baada ya kuanza kwa penalti Uwanja wa Taifa mchezo wa Simba na Yanga, Wakati huo huo ile michuano ya draft kuwania mchele kilo kumi itaendelea tena mwishoni mwa wiki kwa mechi nne za hatua ya robo fainali Ted aliyevaa fulana ya CHADEMA akichuana na Mruge aliyevalia fulana

WOLPER AGEUKIA MUZIKI

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Video queen wa bongofleva, Leonarda Wolper ameamua kujikita kwenye muziki wa bongofleva na sasa anatarajia kutengeneza wimbo wake mwenyewe, ambapo amedai utazungumzia mahaba. Wolper ameyasema hayo leo alipozungumza na Mambo Uwanjani asubuhi ya leo ambapo alidai tayari ameshaanza maandalizi ya kuachia wimbo huo atakaourekodi katika studio za Jini Records zilizopo Tabata Shule. Hata hivyo Wolper amedai si kwamba ataacha uigizaji isipokuwa ataendelea kuwa video queen kwani ndio fani iliyomtambulisha, Wolper ameanza kujipatia umaarufu mkubwa kupitia kazi zake zikiwemo filamu alizoigiza kama Lovennes Leonarda Wolper, amegeukia muziki

Licha ya kufungwa, Yanga yang' ara na Tshishimbi wake, apiga mpira mkubwa jana

Picha
Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam Yanga jana licha ya kufungwa kwa mikwaju ya penalti 5-4 na watani zao wa jadi Simba SC katika mchezo wa Ngao ya Jamii katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, lakini imeondoka na faida kuu mbili ikiwemo nyota wake wawili kupiga mpira mkubwa ile mbaya. Mchezo huo uliomalizika kwa sare isiyo na mabao yaani 0-0, Yanga ilionekana kuizidi Simba kwenye eneo la katikati kiasi kwamba kiungo wake James Kotei akishindwa kumpandishia mipira Mzamiru Yassin ambaye alishindwa kung' ara. Huku Emmanuel Okwi ambaye alikuwa akitegemewa kwenye eneo la ushambuliaji naye akishindwa kufanya yale aliyozoea kuyafanya, lakini unaambiwa mtu aliyeikata umeme Simba katikati si mwingine ni Papy Kabamba Tshishimbi raia wa DRC ambaye gumzo kwa sasa hapa mjini. Kwa upande wa ulinzi, mtu aliyemnyima raha Okwi si mwingine ni Gardiel Michael Mbaga ambaye alikuwa na kazi ya kuhakikisha anafuta makosa yote yaliyokuwa yakifanywa na Kevin Yondan, Andrew Vincent  "Dante"

MO AWAPA NGAO YA JAMII SIMBA, MAHADHI AWAAMGUSHA YANGA

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Mabingwa wa kombe la FA, Simba SC ama Wekundu wa Msimbazi usiku huu wameongeza taji lingine baada ya kutwaa Ngao ya Jamii kwa kuichapa Yanga SC kwa mikwaju ya penalti 5-4 kufuatia sare tasa ya 0-0 ndani ya dakika 90. Hiki kinakuwa kipigo cha tatu mfululizo kwa Yanga dhidi ya Simba, Ikifungwa kwa mikwaju ya penalti 4-2 katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la Mapinduzi Zanzibar pia ikaambulia tena kipigo cha mabao 2-1 mjini Dar es Salaam mchezo wa Ligi Kuu Bara. Mchezo wa leo Yanga walianza vizuri kulitia msukosuko lango la Simba lakini washambuliaji wake Ibrahim Ajibu na Donald Ngoma wakishindwa kumalizia, kiungo wa Yanga, Papy Kabamba Tshishimbi na Raphael Daudi walionekana kuwamudu viungo wa Simba. Simba nao walikuja juu na kulisakama lango la Yanga lakini nao washambuliaji wake Emmanuel Okwi, Haruna Niyonzima na Laudit Mavugo nao hawakuwa imara, hadi mapumziko timu hizo zilikuwa hazijafungana. Kipindi cha pili nacho kilikuwa kigumu kwani timu hizo

YANGA YAPATA PIGO KUFUNGIWA KWA KIUNGO WAKE

Picha
Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam Mabingwa wa soka nchini Yanga wamepata pigo kufuatia kufungiwa kwa kiungo wake Pius Buswita na Shirikisho la mpira wa miguu nchini,(TFF) kwa kipindi cha mwaka mmoja. Buswita amekutwa na makosa hayo na Kamati ya Sheria, Nidhamu na Hadhi za wachezaji ya shirikisho la soka nchini akiwa amesaini vilabu viwili vya Simba na Yanga. Mchezaji huyo ambaye msimu uliopita alikuwa anaichezea Mbao ya Mwanza, ameiachia pigo klabu yake ambayo ilimsajili msimu huu kwa mkataba wa miaka miwili kwa lengo la kuitumikia timu yao. Shirikisho la soka nchini limekuwa likitoa adhabu kwa wachezaji wanaokutwa wamesaini timu mbili kwani kufanya hivyo ni kosa kubwa sana Pius Buswita (Aliyevaa jezi ya bluu) amefungiwa na TFF

Simba na Yanga hakuna kuremba

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Watani wa jadi wa soka la Tanzania Simba SC na Yanga SC leo jioni zinaumana katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuwania Ngao ya Jamii, miamba hiyo inakutana kila mmoja ikiwa imetokea Visiwani Zanzibar ambako ilikwenda kuweka kambi. Kwa upande wa Yanga, walielekea katika kisiwa cha Pemba lakini walianza kufikia Unguja ambapo walicheza mechi moja ya kirafiki na Mlandege na kushinda mabao 2-0, kisha wakaelekea Pemba ambapo pia walicheza mechi mbili za kirafiki. Yanga ilicheza na Chipukizi na kushinda bao 1-0 kisha ikainyoa Jamhuri pia bao 1-0, itashuka uwanjani leo ikimtegemea zaidi mshambuliaji wake mpya Ibrahim Ajibu ambaye katika mechi hizo aliweza kufunga. Simba nao walifikia Unguja ambapo wao walicheza mechi mbili za kirafiki ambapo walilazimishwa sare na Mlandege 0-0 kisha wakaichapa Gulioni mabao 5-0, Laudit Mavugo anapewa nafasi kubwa ya kuiongoza Simba kutokana na kuifungia mabao mawili Simba ilikuwa Zanzibar, ingawa kutakuwa na kivutio t

YANGA YATUA KIMAFIA, KAZI IPO KESHO

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Kikosi cha mabingwa wa soka Tanzania Bara Yanga SC kimewasili muda huu kikitokea Pemba ambako kiliweka kambi kujiandaa na mchezo wa kesho wa kuwania Ngao ya Jamii dhidi ya mtani wake wa jadi Simba katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Mabingwa hao wa Bara wametua kimafia kwani hawakutaka kuzungumza na mtu yoyote na moja kwa moja waliekelekea kambini ambapo pia wamefanya siri. Kesho Yanga itakutana na Simba katika mchezo unaotajwa utakuwa mkali na utakaotoa mshindi kwakuwa hakutakuwa na sare kwani hata zikimaliza dakika 90 bila kufungana zitapigwa penalti, Yanga itawakosa nyota wake watatu ambao ni Beno Kakolanya, Obrey Chirwa na Geofrey Mwashiuya ambao ni majeruhi huku Simba ikimkosa John Bocco "Adebayor" Yanga wakiwasili

Simba wapo tayari kuiua Yanga kesho

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Homa ya mpambano wa watani wa jadi kesho kati ya Simba na Yanga imezidi kupanda ambapo kila timu ikiwa imejiandaa kumkabili mwenzie, Simba leo wamemaliza mazoezi yao kabla jioni ya kesho hawajaivaa Yanga Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Kocha mkuu wa kikosi hicho Mcameroon Joseph Omog  amesema kikosi chake kipo tayari kwa vita hiyo ila amewaambia mashabiki wa Simba, kwamba kesho Yanga anakufa atake asitake. Kiungo mwenye udambwidambwi mwingi, Mnyarwanda Haruna Niyonzima ametamba kuwalaza mapema mashabiki wa Yanga, amesema mashabiki wa Simba wajitokeze kushuhudia kalamu ya mabao wakiwafunga Yanga ambao aliwahi kuwatumikia. Simba ilirejea juzi ikitokea Zanzibar ambako iliweka kambi yake kujiandaa na mchezo huo, Yanga nao walikuwa Pemba ambapo inasemekana wametua leo Wachezaji wa Simba wakiwa mazoezini

SOPHIA ABDUL "KIBENA": NYOTA MPYA KWENYE FILAMU, AAPA KUMFIKIA WEMA SEPETU

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam TANZANIA ni miongoni mwa nchi zinazopiga hatua kwenye tasnia ya filamu Duniani, tofauti na miaka iliyopita ambapo kulikuwa na wasanii wachache kwenye fani hiyo. Lakini sasa kila kona kumetapakaa vikundi vya sanaa huku kampuni za kutengeneza filamu zikizidi kuongezeka, vijana wa kike na kiume nao wanajikita kwa wingi kwenye tasnia hiyo, tofauti na miaka ya nyuma ambapo ilikuwa vigumu kuwaona vijana wakiigiza. Miaka hiyo wazee pekee ndio waliotawala kama mzee Jangala, mzee Jongo (Marehemu), Bi Hambiliki (Naye marehemu), mzee Kagunga, mzee Janja, Bi Hindu, mzee Kipara, mzee Mahoka, mzee Pwagu, mzee Panda, mzee Majuto, mzee Small na wengineo waliweza kushiriki maigizo. King Majuto ama mzee Majuto na mzee Small wao ndio walifungua milango kwa kufanikiwa kutengeneza filamu ambazo zilisisimua wengi na kuanza kuwavutia vijana ambao nao walianza kujiingiza kwenye tasnia hiyo, marehemu Steven Kanumba, Elizabeth Michael "Lulu", Aunt Ezekiel, Irene Uwoya

Simba yawasili Dar kuiwahi Yanga

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Simba SC mchana wa leo imewasili ikitokea Zanzibar ambapo ilikwenda kuweka kambi kwa ajili ya kujiandaa na pambano lake la Jumatano ijayo na mtani wake wa jadi Yanga SC katika uwanja wa Taifa kuwania Ngao ya Jamii. Simba ilikaa Unguja ambapo pia ilicheza mechi mbili za kirafiki, Wekundu hao wa Msimbazi walicheza na Mlandege katika uwanja wa Amaan na kulazimishwa sare tasa 0-0 kisha ikaiduwaza Gulioni mabao 5-0. Kocha wa Simba, Mcameroon Joseph Omog amesema kikosi chake kipo tayari kwa mchezo wao na Yanga na wamemuahidi ushindi, Yanga nao wapo Zanzibar katika kisiwa cha Pemba ambapo nao walicheza mechi mbili ingawa walicheza tatu ikiwemo moja waliyoicheza Unguja na Mlandege na kushinda 2-0, mechi nyingine Yanga ilizifunga Chipukizi na Jamhuri zote bao 1-0 Kikosi cha Simba kimewasili leo

Mwinyi Haji aitumia Simba salamu

Picha
Na Ikram Khamees. Pemba Bao pekee lililofungwa kipindi cha kwanza na beki wa upande wa kushoto Mwinyi Haji Mngwali, limeipa ushindi wa bao 1-0 Yanga SC dhidi ya Jamhuri ya Pemba katika uwanja wa Gombani mjini hapa. Kocha wa Yanga, Mzambia George Lwandamina alilazimika kupanga vikosi viwili ili kutesti silaha zake vizuri kabla ya Jumatano ijayo kumenyana na watani wao wa jadi Simba katika mchezo wa kuwania Ngao ya Jamii Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Huo ni ushindi wa pili mfululizo lakini ni wa tatu kwao tangu watue visiwani Zanzibar, Yanga iliifunga Mlandege mabao 2-0, Chipukizi 1-0 na Jamhuri pia kwa bao hilo, Simba nao jana waliichapa timu ya Gulioni mabao 5-0 Mwinyi Haji mfungajj wa goli la Yanga leo

Wanachama Simba wapitisha mabadiliko

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Wanachama wa klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam leo wamepitisha mabadiliko na sasa Simba imeingia katika mfumo mpya wa uhuzaji hisa. Hata hivyo klabu imeridhia kubaki kumilikiwa na wanachama badala ya mwekezaji, mwekezaji ameruhusiwa kununua hisa asilimia 50 na wanachama watabakiwa na asilimia 50. Hisa zote 50 zitauzwa kwa Bilioni 20 na nyingine zitauzwa kwa wanachama ambao wamepunguziwa bei, katika zoezi hilo mwanachama mmoja amekataa Simba kuingia kwenye mfumo huo Wanachama wa Simba wamepitisha mabadiliko

KMC YAMWEKEA NGUMU RONALDO, MBEYA CITY

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Timu ya KMC ya Kinondoni jijini Dar es Salaam ambayo inashiriki Ligi Daraja la kwanza Tanzania Bara imemwekea pingamizi kiungo wake Iddi Seleman maarufu Ronaldo ambaye amesajiliwa na Mbeya City. Uongozi wa KMC umesema hautakubali kuona nyota wao anaichezea Mbeya City pasipo wao kulipwa chao, Mbeya City imekiuka taratibu kwa kumpa kandarasi mchezaji wao bila kuwasiliana nao. Ronaldo ni mchezaji wa KMC na bado ana mkataba na timu hiyo hivyo Mbeya City ya mkoani Mbeya ilipaswa kuwafuata, kwa sasa KMC wanataka walipwe chao ama sivyo mchezaji huyo hatoichezea timu hiyo msimu ujao Iddi Seleman "Ronaldo" amewekewa ngumu na timu yake

Kilomoni asema ajafutwa uanachama, na afuti kesi

Picha
Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam Aliyekuwa Mdhamini wa klabu ya Simba, mzee Hamisi Kilomoni amesema atambui kufutwa uanachama kama ilivyotangazwa na klabu hiyo na pia hawezi kwenda kuondoa kesi yake akiyoifungua mahakamani. Akizungumza na mtandao huu, Kilomoni amesema yeye bado kiongozi wa bodi ya wadhamini wa klabu ya Simba na amedai maamuzi ya kumsimamisha uanachama wameyafanya wao tu ili kudanganyana na kamwe hakuna atakayeweza kumsimamisha wala kumfuta uanachama. Kilomoni amedai hawezi kwenda kuifuta kesi aliyoifungua katika mahakama ya mkazi ya Kisutu na amesema ataendelea kuushinikiza uongozi juu ya mpango wake wa kutaka kumuuzia klabu mfanyabiashara Mohamed Dewji Hamisi Kilomoni, amesema afuti kesi na hakuna wa kumfuta uanachama

KABWILI KUANZA LANGONI NA SIMBA

Picha
Na Ikram Khamees. Pemba Kuna kila dalili mlinda mlango chipukizi wa mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga SC, Ramadhan Kabwili akaanza langoni katika mchezo wa kuwania Ngao ya Jamii dhidi ya mahasimu wao Simba mchezo utakaofanyika Jumatano ijayo Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kocha mkuu wa Yanga, Mzambia George Lwandamina, huenda akamuanzisha kipa huyo kwakuwa Beno Kakolanya hayupo fiti kuanza katika mchezo huo huku mlinda mlango anayemuamini kuanza kwenye mchezo huo Mcameroon, Youthe Rostand Jehu amewekewa pingamizi na klabu yake ya African Lyon na ikizingatiwa huo ni mchezo unaosimamiwa na shirikisho la soka nchini, (TFF). Kabwili anapewa nafasi kubwa ya kuanza katika mchezo huo na huenda akavunja rekodi ya Peter Manyika Jr ambaye naye aliaminiwa kucheza mechi ya watani baada ya makipa namba moja na mbili kukosekana, Lwandamina alikuwa skimpanga Kabwili katika mechi za kirafiki Kipa Ramadhan Kabwili ataanza langoni na Simba Jumatano ijayo

Mbaraka Yusuf kimeeleweka Azam

Picha
Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam Hatimaye klabu ya Kagera Sugar imeridhia Mbaraka Yusuf kukipiga Azam FC msimu ujao baada ya kumwekea pingamizi katika shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) ambalo wameliondoa rasmi. Afisa Habari wa Azam FC,Jaffar Idd Maganga amesema leo kuwa, Kagera Sugar wamekubali Mbaraka kukipiga Azam na hilo ni jambo jema kwao kwani tayari walishakamilisha taratibu zote za kumsaini. Mbaraka ameitumikia Kagera Sugar kwa misimu miwili na alitambulishwa na Azam kama mchezaji mpya kitendo ambacho kiliwachefua viongozi wa Kagera Sugar na kuamua kumwekea pingamizi, lakini Azam wakaamua kukaa chini na Kagera Sugar hatimaye kulimaliza suala hilo na sasa Mbaraka ni mali ya Azam Mbaraka Yusuf Abeid, sasa mali ya Azam FC

Tshishimbi awasili Pemba kuiwahi Simba

Picha
Na Ikram Khamees. Pemba Kiungo mpya wa mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga SC, Papy Tshishimbi Kabamba raia wa DRC amewasili leo nchini akitokea nyumbani kwao DRC. Tshishimbi moja kwa moja ameelekea kisiwani Pemba ambako Yanga imeweka kambi kujiandaa na kucheza na mtani wake wa jadi Simba Jumatano ijayo katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam kuwania Ngao ya Jamii. Kutua kwa kiungo huyo kunapunguza presha kwa mashabiki wa mabingwa hao wa Bara ambao jana waliichapa Chipukizi bao 1-0 bao lililofungwa na Ibrahim Ajibu mchezo ukiwa ni wa kirafiki, Tshishimbi amejiunga na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Mbabane Swallows ya Swaziland Papy Tshishimbi Kabamba (Katikati) amejiunga na wenzake Pemba leo

Simba butu, washikwa na wachovu wa Yanga

Picha
Na Mwandishi Wetu. Unguja Mabingwa wa kombe la FA, Simba SC imeshindwa kuondoka na ushindi baada ya kulazimishwa sare tasa 0-0 na wachovu wa Yanga, Mlandege FC mchezo wa kirafiki uliofanyika usiku katika Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Mlandege ambao juzi walipokea kichapo cha mabao 2-0 dhidi ya Yanga ambao kwa sasa wameenda Pemba, waliweza kuwadhibiti vilivyo Simba ambao walichezesha kikosi chao chote lakini kikashindwa kufurukuta. Simba wameweka kambi yao kisiwani hapa wakijiandaa kucheza na Yanga hapo Jumatano ijayo katika Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam kuwania Ngao ya Jamii, matokeo hayo yanawashangaza wengi kwani baada ya Mlandege kufungwa na Yanga washabiki wa Simba walikuwa wakiibeza Mlandege wakidai ni vibonde Simba imelazimishwa sare tasa leo na Mlandege

AJIBU AWATUMIA SALAMU SIMBA

Picha
Na Mwandishi Wetu. Pemba Klabu bingwa ya soka Tanzania Bara Yanga SC imeifunga timu ya Chipukizi ya Wete Pemba bao 1-0 mchezo wa kirafiki uliofanyika katika Uwanja wa Gombani mjini hapa. Mabingwa hao wa Bara wametua Pemba tangu majuzi wakitokea Dar es Salaam wakipitia Unguja ambapo waliweza kucheza na Mlandege na kushinda mabao 2-0, na ujio wao Pemba ni kwa ajili ya kuweka kambi kujiandaa na mchezo wake dhidi ya Simba jumatano ijayo kuwania Ngao ya Jamii uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Vijana hao wa Yanga wamecheza mpira mzuri na kuwazidi maarifa Chipukizi ambao nao walionyesha kuwamudu Yanga lakini mshambuliaji Ibrahim Ajibu Migomba akaifungia Yanga bao pekee la ushindi ambalo ni kama salamu kwa timu yake ya zamani Simba ambao watakutana Jumatano ijayo Ibrahim Ajibu Migomba,amefunga bao la ushindi dhidi ya Chipukizi

BOSSOU KUIBURUZA YANGA FIFA

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Beki wa zamani wa mabingwa wa soka nchini, Yanga, Vincent Bossou ametishia kuiburuza FIFA klabu yake ya zamani ya Yanga endapo itashindwa kumlipa mishahara yake ya miezi miwili. Bossou amesema anaidai Yanga na imeshindwa kumlipa kwani alianza kudai fedha zake tangia Yanga ikiwa chini ya kaimu katibu mkuu, Baraka Deusdetit na sasa Charles Boniface Mkwasa na wote wamekuwa wakimpiga danadana. Katika taarifa yake aliyoitoa, beki huyo amedai mashabiki wa Yanga wasimlaumu pale atakapowasilisha madai yake FIFA, wakala wa mchezaji huyo Mganda, Gibby Kalule amesema Yanga watalazimika kumlipa pesa zake za mishahara ama sivyo watafikishwa FIFA Vincent Bossou, anaipeleka Yanga, FIFA

JENGO LA YANGA KUPIGWA MNADA KESHO

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Jengo la makao makuu ya klabu ya Yanga lililopo Jangwani mtaa wa Twiga, kesho litapigwa mnada na kampuni ya udalali ya Msolopa kuanzia saa 4:00, asubuhi. Taarifa za kudaiwa Yanga zimeanza kusambaa leo ambapo Wizara ya Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi imetangaza kuidai Yanga mamilioni ya shilingi baada ya kesi iliyofunguliwa na Baraza la Ardhi la wilaya ya Temeke na Ilala. Katibu mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa amekiri kweli Yanga inadaiwa Ardhi lakini walishafanya mazungumzo na wizara na walikubaliana kulipa deni hilo, lakini anashangaa kusikia tangazo la kupigwa mnada kwa jengo lao. Hata hivyo Mkwasa amesema suala hilo anamfikishia kaimu mwenyekiti Clement Sanga ili aweke zuio Jengo la Yanga kupigwa mnada kesho

SOPHIA KIBENA ALIACHA SHULE KISA MIMBA

Picha
Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam Agizo la Rais wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli la kuzuia wasichana wanaopata mimba mashuleni kutoendelea tena na masomo kama wadau wa elimu walivyotaka waendelee, msanii wa filamu anayekuja juu kwa sasa, Sophia Abdul Kinyogoli "Kibena" amesema hata yeye yalimkuta. Akizungumza na Mambo Uwanjani, Kibena amesema alilazimika kukatisha masomo ya sekondari kidato cha pili kwakuwa alipewa ujauzito, anasema ujauzito huo alipewa na mume wa mtu na hatosahau kwa kuacha masomo kwani huenda sasa hivi angekuwa mbali. Kibena kwa sasa anafanya vizuri katika tamthilia yao inayoitwa "Msitu wa Ndendemba" nayorushwa kwenye kituo cha runinga cha Sibuka kila siku ya Jumamosi saa 6:30 mchana na ikirudiwa Jumapili kuanzia saa 2:30 asubuhi ,  akiigiza katika kikundi cha New Hope maskani yake Tandale jijini Dar es Salaam. Kibena anadai aliachishwa shule ili kuficha yale yaliyomkuta lakini ujauzito huo uliharibika ingawa watu wanazus

SIMBA KUTESTI MITAMBO NA MLANDEGE

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Unguja Simba SC jioni ya leo inatelemka katika Uwanja wa Amaan,Zanzibar kucheza na timu ya Mlandege mchezo wa kirafiki kujiandaa na mchezo wa kuwania Ngao ya Jamii dhidi ya mahasimu wao Yanga, Jumatano ijayo. Mechi hiyo ya watani itachezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivyo vigogo vyote vimetoka nje ya Dar es Salaam kusaka uchawi visiwani Zanzibar, Yanga wao wapo Pemba ambapo kabla walicheza na Mlandege na kushinda mabao 2-0. Mchezo wa leo kati ya Simba na Mlandege utatoa taswira kuelekea mpambano huo, Simba leo itashusha silaha zake zote ikiongozwa na Emmanuel Okwi, Haruna Niyonzima, John Bocco na Shiza Kichuya na kocha msaidizi wa Simba Jackson Mayanja amesema leo watapata ushindi wa mabao mengi kwakuwa ameinoa vema safu yake ya ushambuliaji

Mwambusi atajwa kurejea Mbeya City

Picha
Na Exipedito Mataruma. Mbeya Aliyekuwa kocha msaidizi wa mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga SC, Juma Mwambusi anahusishwa kurejea timu yake ya zamani ya Mbeya City kama kocha mkuu kuchukua nafasi ya Mmalawi Kinah Phiri. Taarifa ambazo zimezagaa jijini Mbeya zinasema mazungumzo kati ya Mwambusi na viongozi wa Mbeya City yanaendelea vizuri na kila dalili zinaonekana kocha huyo aliyeipa mafanikio makubwa timu hiyo anarejea kazini. Lakini Mwambusi ameweka sharti la kupumzika kwa sasa kama alivyotamka awali wakati akiwaaga Wanayanga kwamba anaachana na klabu hiyo aliyoitumikia kwa misimu miwili yote akiisaidia kutwaa ubingwa wa Bara. Mwambusi huenda akaanza kukinoa kikosi hicho katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara, kocha huyo pia amewahi kuinoa Tanzania Prisons pia ya jijini Mbeya Kocha, Juma Mwambusi kurejea Mbeya City

Tff yaishitukia Kagera Sugar kwa Mbaraka Yusuf

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Shirikisho la mpira wa miguu nchini, (Tff) limeishitukia klabu ya Kagera Sugar ya mkoani Kagera juu ya kumwekea pingamizi mchezaji mpya wa Azam FC, Mbaraka Yusuf ikisema ni mali yao na Azam FC walikiuka taratibu kwa kumsainisha mkataba wa miaka miwili. Katika malalamiko yao Kagera Sugar walidai Mbaraka Yusuf wana mkataba nae wa miaka mitatu na alitumikia miaka miwili hivyo bado ni wao na Azam walitakiwa wawafuate ili kutamgaza ofa ya kumuhitaji lakini hawakufanya hivyo. Azam nao wamesema wao wamemsajili kihalali Mbaraka kwani mkataba wake na Kagera ulikuwa umemalizika na ndio maana wakampa mkataba wa miaka miwili, Lakini nao Tff kupitia kwa Afisa Habari wake Alfred Lucas ameshangazwa na madai ya Kagera Sugar dhidi ya Azam kuhusu mchezaji Mbaraka Yusuf. Lucas amesema kama Kagera inasema ukweli kuwa Mbaraka ni mali yao mbona hawakumuorodhesha katika kikosi chao cha msimu ujao na hofu ya Tff kwamba endapo Kagera itashinda kesi yake hiyo ina maana Mbaraka

Simba yahofia kichapo kwa Yanga

Picha
Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam. Simba tayari wameanza kuingja hofu ya kupoteza pambano na watani wao Yanga SC litakalopigwa Jumatano ijayo katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa kamati ya usajili wa Simba, Zacharia Hanspoppe amewaweka kitimoto wachezaji wao kuelekea mchezo huo hasa akiamini kabisa watabweteka siku hiyo wakiamini wao ni bora kuliko wenzao. Hanspoppe amesema kwa sasa Simba inaonekana ni timu bora kuliko Yanga hivyo wachezaji wataingia uwanjani wakiidharau Yanga na mwishowe watapoteza mchezo, amesema hata wao msimu uliopita waliifunga Yanga mabao 2-1 wakiwa hawapewi nafasi yoyote ya kushinda kutokana na kikosi cha Yanga kuwa bora. Na ndivyo itakavyotokea Jumatano ijayo watakapocheza na Yanga ambao kwa sasa wanaonekana si lolote si chochote, Yanga wameweka kambi yao Pemba wakati Simba wapo Unguja Wachezaji wa Simba waambiwa wasiidharau Yanga watafungwa

TSHISHIMBI AMWAGA WINO YANGA, AENDA PEMBA

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Kiungo nyota wa Mbabane Swallows ya Swaziland, Papy Tshishimbi Kabamba raia wa DRC, amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga SC na tayari ameshawasili kisiwani Pemba kuungana na wenzake. Mwenyekiti wa kamati ya usajili wa Yanga,Hussein Nyika amesema kuwa tayari wameshamalizana na Tshishimbi na wameshampeleka Pemba kuungana na wachezaji wenzake ambao walienda huko tangia jana wakitokea Unguja ambapo walicheza juzi na Mlandege na kushinda 2-0. Yanga imekwenda Pemba kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wake wa Ngao ya Jamii dhidi ya mtani wake wa jadi Simba, huo utakuwa mchezo wake wa nne kabla ya kuingia kwenye msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara 2017/18 ikiwa kama bingwa mtetezi Papy Tshishimbi Kabamba akisaini

MO AWEKEWA KAUZIBE SIMBA

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Kuna uwezekano mkubwa mfanyabiashara kijana barani Afrika, Mohamed Dewji "Mo" akashindwa kuwekeza bilioni 20 yake katika klabu ya Simba kwa lengo la kununua Asilimia 51 ya Hisa baada ya klabu hiyo kuja na mkakati mpya wa masharti ya wawekezaji. Mmoja kati ya viongozi wa Simba waliopewa dhamana ya kuipeleka klabu hiyo kuwa kampuni, Mulamu Ng' ambi amesema ni marufuku kwa mwanachama  yeyote wa Simba kununua Hisa zaidi ya 50 katika klabu hiyo. Akizungumza leo Ng' ambi amesema wamekubaliana kuwa endapo hisa zitaanza kuuzwa basi mwisho wa kumiliki ni 50 ili kusiwe na mtu mwenye kumzidi mwenzake kati ya klabu na mwekezaji, pia amesema klabu ndiyo itakayokuwa na kauli tofauti na mwanzo ambapo ilisemekana kuwa kama bilionea Mo Dewji angeinunua Simba kwa bilioni 20 angekuwa na kauli ya mwisho. Lakini sasa hata kama Mo Dewji atainunua Simba bado atabaki kama mwanachama wa kawaida na wala hatokuwa na sauti, hii ni sawa na kuwekewa kauzibe na kun

Msanii Viso anusurika kifo Handeni

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Msanii wa muziki wa kizazi kipya Vincent Patrick "Viso" amenusurika kifo baada ya kupata ajali ya gari akiwa safarini mjini Tanga juzi Jumamosi. Akizungumza na Mambo Uwanjani kwa njia ya simu leo, Viso amesema alipata ajali ya gari na kuumia kifuani pamoja na mgongoni, Viso amedai alipokuwa mjini Tanga ambapo ni kwao, alienda eneo moja linaloitwa Kwa Msisi na wenzake walipanda roli aina ya Fuso. Anasema wakiwa njiani roli hilo lilishindwa kupanda kilima na kujikuta likirudi kinyumenyume na kuanguka ambapo yeye aliumia kifuani na mgongoni huku abiria wengine waliokuwemo kwenye roli hilo walivunjika mikono, miguu na viuno. Hata hivyo amesema yeye anaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu kutoka katika hospitali ya Handeni, roli hilo lilikuwa linatokea Kwa Msisi likielekea Mkata ambapo kulikuwa na gulio, kwa sasa Viso amerejea Dar es Salaam na anaendelea na matibabu, msanii huyo tayari ametambulisha wimbo wake mpya uitwao "Kipendacho r

Yanga yaikalisha Mlandege, Ajibu atisha

Picha
Na Mwandishi Wetu. Zanzibar Mabingwa wa Tanzania Bara Yanga SC, jana usiku waliweza kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika Uwanja wa Amaan, Zanzibar mchezo wa kirafiki. Yanga iliwasili asubuhi ya jana ikitokea jijini Dar es Salaam ambapo juzi ilipokea kichapo cha bao 1-0 toka kwa masarange wa Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo mwingine wa kirafiki uliofanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi. Ibrahim Ajibu alifungua akaunti yake ya mabao akifunga bao lake la kwanza tangia ajiunge na Yanga akitokea Simba lakini pia lilikuwa bao la kwanza kwa Yanga kisha akaseti lingine la pili lililofungwa na winga Emmanuel Martin. Yanga wanajiandaa na mchezo wao wa Ngao ya Jamii dhidi ya mahasimu wao Simba SC utakaopigwa Agosti 23 katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam Emmanuel Martin, alifunga bao la pili jana

Nasikia sikia, Mark Dallarz amekuja kuwashika

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Ngoma mpya ya mkali wa Hip Hop tangia kitambo, Salum Rashid A K A Mark Dallarz mwenyewe anapenda kujiita Ukuni au Cannavaro tayari imeshatoka na mashabiki wake wameanza kuchizika nayo. Ngoma hiyo inakwenda kwa jina la "Nasikia sikia" na ameirekodi katika studio za Jini Record chini ya prodyuza anayekuja juu kwa sasa hapa mjini Naroh Wing. Dallarz muasisi wa kundi la TBT Crew lililokuwa likimshirikisha memba KG Soon ambao walitamba na ngoma yao Segerea, amesema wimbo wake huu wa sasa :Nasikia sikia' ni bomba ile mbaya na lazima ukubalike na kushika namba moja kwenye Top Ten za radio hapa nchini. Dallarz ambaye kwa sasa maskani yake ni Morogoro mji kasoro bahari amekuwa akionekana jijini Dar es Salaam kwa shughuri maalum kama za usambazaji wa kazi zake Cover ya wimbo mpya wa Dallarz Dallarz Ukuni akiwa katika pozi

Okwi aanza balaa lake, apiga bonge la bao

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Mabingwa wa kombe la FA, Simba SC jioni ya leo imechomoza na ushindi wa bao 1-0 mchezo wa kirafiki Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Goli la ushindi limefungwa na Mganda, Emmanuel Okwi aliyepokea pasi murua kutoka kwa John Bocco "Adebayor", huo ni ushindi wa pili mfululizo baada ya Jumanne iliyopita kuichapa Rayon Sports bao 1-0. Okwi alitoa pasi nzuri ambapo Mohamed Ibrahim "Mo" aliifungia Simba bao la ushindi, Simba inaendelea kukisuka kikosi chake ambapo itacheza na Ruvu Shooting kabla haijaivaa Yanga Agosti 23 mwaka huu kuwanjia Ngao ya Hisani katika Uwanja hup huo wa Taifa Emmanuel Okwi (Kushoto) akishangilia sambamba na Shiza Kichuya

Mzee Kilomoni apigwa dundo Simba

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Klabu ya Simba leo imefanya mkutano wake wa wanachama katika ukumbi wa kisasa wa Mwl Nyerere (Mnicc) uliopo Osterbay jijini Dar es Salaam, Kaimu Rais wa Simba Salim Abdallah "Try Again" aliongoza mkutano huo uliohudhuriwa na maelfu ya wanachama wa klabu hiyo. Klabu hiyo mbali ya kutangaza maazimio mbalimbali kwanza ilianza kutoa takwimu za fedha ambapo ilitangaza jumla ya shilingi Bilioni 1.3 kutumika katika usajili. Kisha ikatangaza kumsimamisha uanachama aliyekuwa mchezaji na kiongozi wa zamani wa klabu hiyo Hamisi Kilomoni na kumvua udhamini mkuu na nafasi yake akipewa Adam Mgoyi. Mzee Kilomoni pia ametishiwa kufukuzwa endapo asipoenda kufuta kesi aliyoifungua mahakamani, Kilomoni amesimamishwa uanachama kwa kosa la kupeleka masuala ya mpira mahakamani, pia Simba imemuongezea Prof Juma Kapuya katika Bodi ya wadhamini Mzee Hamjsi Kilomoni amesimamishwa uanachama