Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2016

#MAONI: TFF IMEHODHI LIGI KWA AZAM

Picha
Na Prince Hoza KITENDO kilichofanywa na shirikisho la kandanda nchini TFF kuiruhusu Azam Fc kwenda Zambia kucheza mechi za kirafiki na kuikacha ligi kiu ya Vodacom Tanzania bata huku ikisababisha kupangua ratiba ya ligi hiyo si cha kuzoeleka hata siku moja. TFF imefanya kosa kubwa ambalo linaanza kuharibu sifa ya shirikisho hilo pamoja na Bodi yake ya ligi TPLB, Licha kwamba raisi wa shirikisho hilo Jamal Malinzi kuomba radhi lakini bado ni sawa na kazi bure, kwani kosa limeshafanyika. Bora ruhusa hiyo ingepewa Mwadui Fc au Kagera Sugar sidhani kama wadau wa soka wangelalamika sana, huenda wangelisifu shirikisho hilo kwani timu hizo hazipo kwenye mbio za ubingwa, kitendo cha kuiruhusu Azam Fc kinaonekana kama cha kuipendelea. Tunafahamu kwamba Azam Fc ni timu inayomilikiwa na bilionea Said Salim Bakhressa ambaye pia ndiye mmiliki wa Azam Tv yeye na familia yake. Azam Tv ni wadhamini wenza wa ligi kuu bara hivyo ina nguvu ndani ya shirikisho hilo, matajiri hao pia wanadhamini michu

KIONGERA BASI TENA, AFIKIRIA KUREJEA KWAO

Picha
Na Saida Fikiri Hali si nzuri kwa kiungo mshambuliaji wa Simba Sc Paul Kiongera kufuatia mwenendo wake mbaya ndani ya klabu hiyo. Simba ilifikia maamuzi ya kumrejesha mshambuliaji huyo baada ya kuridhishwa na kiwango chake alichokionyesha kwenye ligi kuu ya Kenya (KPL). Mshambuliaji huyo aliyekuwa akiichezea timu ya KCB kwa mkopo aliibuka mfungaji bora kwenye ligi hiyo na ndipo Simba ilipoamua kumrejesha ikiamini atawasaidia. Lakini hali iko tofauti kwani mchezaji huyo amezidi kushuka kiwango kila kukicha na tangia aanze kutumikia Simba hajafunga hata goli la kuotea. Rafiki yake wa karibu ambaye naye ni raia wa Kenya ameitonya blogu hii kuwa mara baada ya kumalizika msimu huu jamaa anaweza kuchapa mwendo na kurejea kwao Kenya huku akiwa amekata tamaa

COASTAL YAILOWESHA YANGA MKWAKWANI TANGA, AZAM MILANGO IKO WAZI KUSHIKA USUKANI

Picha
Na Alex Jonas Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania bara Yanga Sc jioni ya leo katika uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga imekiona cha moto baada ya kulala mabao 2-0 na Coastal Union "Wagosi wa kaya". Yanga leo imepotezwa kabisa na vijana wa Ally Jangalu na kujikuta inashindwa kuchomoza na ushindi kwenye mchezo huo. Licha ya mchezo huo kutawaliwa na vurugu za hapa na pale zilizopelekea beki wa Yanga Kevin Yondan kupewa kadi nyekundu, magoli ya Wagosi wa kaya yaliwekwa kimiani na Miraji Adam na Juma Mahadhi. Licha ya Yanga kulala mabao hayo mawili, Yanga inaendelea kuongoza ligi hiyo lakini imewapa nafasi kubwa Azam Fc kukamata usukani endapo itashinda mechi yake

HASSAN KESSY AIONGOZA SIMBA KUIUA AFRICAN SPORTS 4-0

Picha
Na Prince Hoza Wekundu wa msimbazi Simba Sc jioni ya leo katika uwanja wa Taifa Dar es salaam imeishushia kipigo kitakatifu African Sports ya Tanga mabao 4-0 mchezo wa ligi kuu bara. Chachu ya ushindi wa Simba katika mchezo wa leo ni beki wake wa upande wa kulia Hassan Ramadhan Kessy ambaye alicheza vizuri na kusaidia ushindi mnono wa timu hiyo ambayo imefikisha pointi 36. Simba ilijipatia mabao yake matatu katika kipindi cha kwanza yakifungwa na Mganda Hamisi Kiiza "Diego" aliyetupia mawili na moja likifungwa na Kessy. Kipindi cha pili Simba waliongeza juhudi na kupata bao la nne lililofungwa na mshambuliaji wake chipukizi Hajji Ugando

PETER MANYIKA AMSHANGAA MAYANJA KUMWEKA BENCHI

Picha
Na Mrisho Hassan Mlinda mlango wa Simba Peter Manyika anaendelea kushangazwa na kitendo cha kocha wake Jackson Mayanja cha kumwanzishia benchi wakati bado kiwango chake ni cha juu. Akizungumza na mwandishi wa blogu hii, Manyika alisema yeye bado kipa mahiri na anastahili kukaa langoni. Anashangaa kuona anakalishwa benchi bila sababu yoyote, "Mimi ni kipa mahiri lakini sianzishwi katika kikosi cha kwanza, uwezo ninao ila ni matakwa ya kocha na wala siwezi kuamua", alisema. Simba leo jioni inashuka katika uwanja wa Taifa kuvaana na African Sports ya Tanga uwanja wa Taifa Dar es salaam mchezo wa ligi kuu bara. Tangia kumalizika kwa michuano ya kombe la Mapinduzi huko Zanzibar Simba ilikuwa ikimpanga golini Peter Manyika tena ikiwa chini ya kocha Muingereza Dylan Kerr ambaye baadaye akatimuliwa na kukabidhiwa jahazi Jackson Mayanja. Hata hivyo Mayanja amekuwa akimtumia Vincent Angban

RASMI: SAMATTA ASAINI GENK MIAKA MINNE

Picha
Na Prince Hoza Mtanzania Mbwana Samatta amesaini mkataba wa miaka minne kuanzia 2016 hadi 2020 kuitumikia timu yake mpya ya KRC Genk ya Ubelgiji. Samatta amemalizana na vinara hao wa ligi kuu ya Ubelgiji na sasa si mchezaji wa TP Mazembe ya DRC ambapo aliiwezesha kutwaa ubingwa wa vilabu Afrika. Mshambuliaji huyo aliyeshinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani. Bosi wa TP Mazembe Moise Katumbi amesaini fomu za kumuidhinisha mshambuliaji huyo aliyewahi kuzichezea Simba Sc, African Lyon na Kimbangulile zote za Tanzania

MBWANA SAMATTA KUCHEZA LIGI YA MABINGWA MSIMU UJAO

Picha
Na Alex Jonas LEO klabu ya KRS Genk ya Ubelgiji inamtambulisha mchezaji wake mpya raia wa Tanzania Mbwana Ali Samatta. Samatta aliondoka usiku wa kuamkia jana kuelekea jijini Brussers Ubelgiji kujiunga na timu yake mpya. Mwanasoka huyo bora wa Afrika kwa wanaocheza ligi ya ndani, ameitwa kujiunga na timu hiyo inayoshiriki ligi kuu nchini humo akitokea TP Mazembe ya DRC ambapo aliiwezesha kutwaa ubingwa wa Afrika. Kwa maana hiyo Samatta atacheza ligi ya mabingwa barani ulaya msimu ujao kwani hadi sasa timu yake mpya ya Genk inaongoza ligi ya nchi hiyo

UCHAGUZI YANGA WANUKIA, SAM MAPANDE AWA MWENYEKITI WA KAMATI

Picha
Na Prince Hoza UNAWEZA kusema sasa kimeeleweka. Uongozi wa mabingwa wa soka nchini Yanga Sc umemteua mwanasheria Sam Mapamde kuwa mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ya klabu hiyo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkurugenzi wa idara ya habari na mawasiliano wa klabu hiyo Jerry Muro imedai kuwa Mapande anakuwa mwenyekiti wa kamati hiyo akichukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa mwenyekiti wa kamati hiyo Alex Gaitani Mgongolwa. Mgongolwa alijiuzuru wadhifa huo akidai ni kubanwa na majukumu ya kifamilia. Yanga imetakiwa kufanya uchaguzi jana na raisi wa shirikisho la kandanda nchini TFF Jamal Malinzi. Hata hivyo muda wa kukaa madarakani kwa viongozi wa klabu hiyo umekwisha kisheria. Tayari mwenyekiti wa timu hiyo Yusuf Mehbood Manji ametangaza kutetea kiti chake, awali Manji aliwaomba Wanayanga kutowania tena kiti hicho na walimuongezea mwaka mmoja kuendelea kuiongoza, mwaka mmoja aliopewa imekwisha kisheria

PICHA YA MANJI NA MANARA YAZUA UTATA MTANDAONI

Picha
Na Prince Hoza Picha inayowaonyesha msemaji wa klabu ya Simba Hajji Sunday Manara na mwenyekiti wa klabu ya Yanga Yusuf Mehbood Manji inazidi kuwaacha hoi wapenzi wa soka nchini, Picha hiyo ilianza kuenea katika mitandao ya kijamii na sasa imekuwa gumzo kila kulicha. Vigogo hao wanatola timu mahasimu na zimekuwa zikichukiana lakini wameonyesha kwamba nje ya soka ni marafiki

Yanga yaichimba mkwara Coastal

Picha
Mabingwa watetezi wa ligi kuu Yanga Sc wameipiga mkwara mzito Coastal Union ya Tanga ambao watakutana jumamosi ijayo katika iwanja wa CCM Mkwakwani.