Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2026

Ally Kiba kupamba Simba Day

Picha
Klabu ya Simba SC imemtangaza rasmi mwanamuziki Alikiba kuwa msanii mkuu atakayetumbuiza katika tamasha la Simba Day mwaka huu. ​Hatua hii inalenga kuongeza thamani ya burudani na hamasa kwa mashabiki na wadau wa soka kuelekea utambulisho wa kikosi cha msimu ujao.

Yanga mwendo wa 7

Picha
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya NBC, Young Africans (Yanga SC), wameendelea kuonyesha utulivu na uwezo mkubwa wa ushambuliaji baada ya kuibuka na ushindi mnono wa magoli 7-0 dhidi ya klabu ya Kigamboni United (B-19) inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza (Championship). ​Katika mchezo huo wa kujiandaa na msimu mpya, safu ya ushambuliaji na viungo wa Yanga ilionyesha utofauti mkubwa kupitia mchanganyiko wa wachezaji wapya na wa zamani waliopachika mabao hayo: ​⚽ Wafungaji wa Magoli ya Yanga SC: ​Erick Mwijage ⚽ (Assist: Mihambo) ​Cheikh Ibrahima Touré ⚽ (Penati) ​Cheikh Ibrahima Touré ⚽ (Assist: Mohamed Hussein 'Zimbwe') ​Kazimoto ⚽ ​Kazimoto ⚽ (Assist: Hussein Zakuani) ​Hussein Zakuani ⚽ (Assist: Cheikh Touré) ​Maxi Nzengeli ⚽ (Assist: Chadrack Boka) ​Ushindi huu wa magoli saba unakuwa wa pili mtawalia katika mechi za majaribio, ukionyesha kuwa kikosi hicho kinaendelea kuimarika kwa kasi kuelekea mchezo wa Ngao ya Jamii pamoja na msimu mpya wa mashindano.

Karia aahidi kuwadhibiti wanaotumia gesi vyumba vya kubadilishia

Picha
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia, amesema TFF inanunua vifaa maalum vitakavyotumika kuthibitisha uwepo wa gesi katika maeneo ya vyumba vya kubadilishia nguo. Karia amesema matukio hayo yanaripotiwa kufanyika, lakini TFF inataka kupata ushahidi wa kitaalamu kabla ya kuchukua hatua dhidi ya timu husika. Wallace Karia: "Tunanunua vifaa maalum vya kuthibitisha uwepo wa gesi na ni kweli hayo mambo yanafanyika. Lakini ikiwa tutajiridhisha timu imevalia nje ya vyumba na tukabaini hakuna sumu au harufu hizo, itapokwa pointi 5. "Kauli hiyo imekuja wakati TFF ikiweka msisitizo wa kuhakikisha matukio yanayodaiwa kutokea kwenye vyumba vya kubadilishia nguo yanathibitishwa kwa ushahidi kabla ya hatua za kinidhamu kuchukuliwa.

Haroub awashukuru viongozi Simba

Picha
“Viongozi wamenituma kuja kueleza machache kubwa zaidi ni kuwashukuru wenzetu wa Ngorongoro kwa ushirikiano huu, lakini pia kuwashukuru wadhamini wetu wanaowezesha klabu hii kuwa kubwa. Tuunge mkono timu yetu, tumesajili vizuri, tuna malengo ya kufika mbali kwenye michuano ya Afrika na michuano ya ndani. Huu ni mwaka wetu Wanasimba na sherehe hizi zinakwenda sambamba na sherehe za miaka 90 tangu kuanzishwa kwa Klabu ya Simba.”- Mjumbe wa Bodi, Selemani Haroub kwenye uzinduzi wa Simba Week 2026.

Simba yazindua jezi mpya

Picha
Klabu ya Simba SC hii leo imetambulisha jezi zake mpya kwa ajili ya msimu ujao, Simba imetambulisha jezi hizo ambazo watazitumia kwenye mashindano ya ligi za ndani na mechi za kirafiki.