Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2013

WENGER AICHEKELEA CARDIFF ISIYO NA KOCHA.

Picha
Arsenal wana nafasi ya kuimarisha uongozi wao wa Ligi ya Premier ya Uingereza ikiwa watawachakaza Cardiff City, ambao hawana meneja, kwa mara ya pili katika kipindi kichache wakati shindano hilo litakapo rejea siku ya kuadhimisha Mwaka Mpya. Ligi ya Premier iko katika pilika pilika za mechi ya nne ndani ya siku kumi wakati ambao wachezaji na vilabu vya nchi zingine barani Uropa viko kwenye mapumziko ya sherehe za Krismasi. Huku ligi hiyo ikiwa imefikia kati musimu huu baada ya raundi 19 kusakatwa, Arsenal wanamiliki uongozi na alama 42, ikiwa ni mara ya kwanza kilabu hicho kuanza mwaka kileleni tangu kampeni ya 2007-08.

HATIMAYE TANGANYIKA IMEREJEA, CCM YAANGUKA.

Picha
Tume ya Mabadiliko ya Katiba imetoa Rasimu ya Pili ya Katiba ikiwa na mambo sita mapya, huku ikiendelea kupendekeza Muungano wa Serikali tatu na kurejea kwa nchi ya Tanganyika. Rasimu hiyo ya Pili ambayo imetolewa miezi saba baada ya Rasimu ya Kwanza, ilikabidhiwa jana kwa Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam. Akizungumza kabla ya kukabidhi rasimu hiyo, Jaji Warioba alisema ina Ibara 271, tofauti na ile ya kwanza iliyokuwa na Ibara 240.

KUNANI YANGA! NGASA, MSUVA WATIMKA.

Picha
Yanga imepata pigo baada ya winga wake, Mrisho Ngasa, Simon Msuva na beki wa kati Nadir Haroub 'Cannavaro' kuugua jambo litakalowafanya kuwa nje ya uwanja kwa siku kadhaa, hivyo kuzikosa mechi za mwanzo za michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoanza kesho visiwani Zanzibar. Katika ratiba iliyotolewa na waandaaji wa michuano hiyo, inaonyesha Yanga itaanza kwa kucheza dhidi ya Tusker ya Kenya keshokutwa. Ngasa anasumbuliwa na homa ya matumbo wakati Cannavaro ni majeruhi wa goti huku Simon Msuva akisumbuliwa na malaria. Hali hiyo ilimfanya Ngasa kuyakosa mazoezi ya Yanga yaliyofanyika kwa saa mbili jana kuanzia saa 3:00 - 5:00 asubuhi chini ya Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Felix Minziro. Wachezaji wengine ambao hawakuwapo jana ni pamoja na washambuliaji Waganda, Emmanuel Okwi na Hamis Kiiza, winga Msuva na kiungo Salum Tetela.

SIMBA SASA KAMILI GADO LIGI KUU.

Picha
KLABU ya Simba SC ya Dars Salaam, imesema kwamba imekwisharekebisha dosari zilizokuwapo kwenye usajili wake na sasa haitakuwa na sababu ya kupunguza mchezaji yeyote kwenye kikosi chake. Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba SC, Swedi Nkwabi amesema jana kwamba, wachezaji wote wapya waliosajiliwa katika dirisha dogo wataendelea kuitumikia timu hiyo baada ya kurekebishwa kwa dosari hizo. Alisema dosari yenyewe ilikuwa ni kutopeleka fomu za kuvunjiana Mkataba na mchezaji Sino Augustino, hivyo Ikaonekana klabu hiyo imesajili wachezaji zaidi tofauti na nafasi yake.

MAN UNITED YAMTOSA MOYES KATIKA USAJILI WA DIRISHA DOGO

Picha
KLABU ya Manchester United inahofia jitihada zake za beki mpya wa kushoto katika usajili wa dirisha dogo Januari hauwezi kuvunja matunda, kwa Everton na Southampton kutokuwa na mpango wa kuwaachia wachezaji wake Leighton Baines na Luke Shaw. Kocha wa United, David Moyes alijaribu bila mafanikio kutaka kumsaini Baines kutoka klabu yake ya zamani mapema msimu huu, baada ya Patrice Evra kusema anahitaji ushindani wa maana wa namba katika nafasi yake. Lakini juhudi za United zimezimwa na Mwenyekiti wa Everton, Bill Kenwright na pamoja na hayo Moyes ameambiwa na Mtendaji Mkuu wa klabu yake, Ed Woodward kwamba hana fedha za kutoa kwa ajili ya usajili wa mwezi ujao.

SUAREZ AFURAHIA KUIWEKA LIVERPOOL KILELENI.

Picha
Luis Suarez alisherehekea mkataba wake mpya kwa kuiweka Liverpool kileleni Ligi ya Premia kwa kufunga mabao mawili na kutamba uwanjani wakati wa ushindi wa 3-1 Jumamosi dhidi ya klabu ya Cardiff City inayokabiliwa na mzozo. Manchester City walisonga hadi nambari mbili licha ya bao la kujifunga la Vincent Kompany wakati wa ushindi wa 4-2 dhidi ya wanyonge Fulham nao mabingwa Manchester United, walio nambari saba, wakacharaza West Ham United 3-1 kupitia magoli ya Danny Welbeck, Adnan Januzaj na Ashley Young. Suarez ambaye kwa sasa hashikiki, na aliyekuwa ameonekana kama ataondoka Anfield kipindi cha kuhama wachezaji kilichopita baada ya kupigwa marufuku kwa kumuuma mchezaji mwingine, alifunga bao la kwanza kwa ustadi mkali kasha akamwandalia Raheem Sterling la pili baada ya kupokea mpira mzuri kutoka kwa Jordan Henderson ambaye sasa ameamka.

PATA PICHA YA MECHI YA NANI MTANI JEMBE SIMBA NA YANGA.

Picha
 Kikosi cha Simba.

BREKING NEWS: YANGA YAACHANA NA BRANDTS.

Picha
RASMI, Yanga SC imetangaza kuachana na kocha Mholanzi, Ernie Brandts siku mbili baada ya kufungwa mabao 3-1 na wapinzani wao wa jadi, Simba SC juzi katika mechi ya Nani Mtani Jembe Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Abdallah Ahmed Bin Kleb amewaambia Waandishi wa Habari leo asubuhi makao makuu ya klabu, Jangwani mjini Dar es Salaam kwamba Brandts amepewa notisi ya mwezi mmoja kwa mujibu wa taratibu za ajira na baada ya hapo ataondoka. Bin Kleb (katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari makao makuu ya klabu leo Jangwani. Wengine kulia ni Ofisa Habari, Baraka Kizuguto na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano, Mussa Katabaro

MZUNGU WA SIMBA ATOWEKA.

Picha
Baada ya kuipa timu yake ushindi wa mabao 3-1 katika mechi ya kirafiki dhidi ya Yanga (Nani Mtani Jembe), Kocha Mkuu wa Simba, Zdravok Logarusic 'Loga', aliondoka nchini jana usiku na kwenda kwao Croatia kwa ajili ya mapumziko ya Sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya huku akiahidi makubwa zaidi atakaporejea. Mcroatia huyo atakosa mechi mbili za hatua ya makundi katika mashindano ya Kombe la Mapinduzi yatakayofanyika kuanzia Januari Mosi mwakani. Logarusic aliyewahi kuifundisha Gor Mahia ya Kenya, Jumamosi aliiongoza Simba kwa mara ya kwanza wakati ikiibuka na ushindi huo mnono dhidi ya watani zao Yanga.

MASIKINI DALLARS, MAISHA YA MUZIKI YAMEMSHINDA.

Picha
MUZIKI ni bahati ya mtu, Diamond Plutinum anaendesha gari la kifahari sawa na Nay wa Mitego, huwezi kumkuta akibeba zege au kusukuma mkokoteni, lakini maisha yamekuwa magumu kwa staa muziki wa kizazi kipya aliyegeukia upande wa hip hop Mark Dallars aliyepata kutamba na wimbo wake wa Mtaani kwetu . Mambo uwanjani ilimshuhudia nyota huyo akisukuma mkokoteni ili kupa ujira mdogo kufuatia maisha ya muziki kumwendea kombo, Dallars alitupia katika ukurasa wake wa facebook ambapo alisema 'Natafuta ela ya sikukuu kwa mtindo wowote bishoo endelea kusubiri uletewe', ulisema ujumbe wake. Aidha maneno hayo ya msanii huyo anayesota kwa sasa kutokana na nyimbo zake mpya anazotoa kutopokelewa vema na mashabiki wake, ujumbe wake umekuwa na maana kubwa kwa watu maarufu ambao wengi wao hujifanya mabishoo.

JUMA KASEJA AJIONDOA YANGA.

Picha
KIPA wa Yanga, Juma Kaseja amesema kukaa nje ya uwanja kwa zaidi ya miezi minne kulichangia kupunguza ufanisi wake uwanjani wakati wa mechi dhidi ya Simba Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam juzi iliyomalizika kwa Yanga kubugizwa mabao 3-1. Akizungumza na mwandishi wetu, Kaseja amesema kwamba kukaa kwake benchi kwa kipindi kirefu kumechangia yeye kufanya vibaya na kuruhusu goli mbili za kizembe, Kaseja anasema haikuwa makusudi yeye kufungwa magoli hayo ila uwezo wake ulianza kumpotea. 'Mchezaji yeyote yule duniani akikaa nje miezi minne na zaidi kunaweza kuathli kiwango chake, mimi sikuhujumu mechi ile, kwanza mnakumbuka wenyewe jinsi Simba ilivyochangia kuharibu kiwango changu kwa kunitema na kuniharibia nisipate timu', alisema na kuongeza.

CHELSEA WAMEKOSA MAKALI YA KUUA- MOURINHO

Picha
Meneja wa Chelsea Jose Mourinho alilazimika kurudia tena hadithi yake ya kawaida huku akiomboleza kushindwa kwa timu yake kufunga baada ya kubanduliwa kwa kulazwa 2-1 muda wa ziada na Sunderland katika League Cup Jumanne. "Kiwango cha uchezaji soka ambacho tulionyesha ni kizuri sana. Hatushindwi kwenye mechi kwa sababu eti hatuchezi au kwamba mpinzani anatuzidi, ni kutokana na hali kwamba hatuui wapinzani wetu na tunawapa uhai,” Mourinho aliambia Sky Sports baada ya timu yake kubanduliwa katika robofainali. “Kila mpinzani anajua kwamba anaweza kutufunga bao. Tulipata nafasi nyingi nzuri za kufunga na hatukufunga.” Ingawa Chelsea wako nambari tatu kwenye Ligi ya Premia na wako awamu ya muondoano katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, matokeo ya kushangaza majuzi yamefanya Mourinho kutahadhari zaidi kuhusu uwezekano wa timu yake kushinda mataji.

AZAM FC WAFUNGA 'SOFA ZA HATARI' CHAMAZI, KOMBE LA SHIRIKISHO PALE PALE MWAKANI

Picha
Mafundi wakiendelea na zoezi la uwekaji wa viti vya kisasa katika majukwaa ya Uwanja wa Azam Complex, uliopo Chamazi, Dar es Salaam. Klabu ya Azam inataka kuutumia Uwanja huo kwa michuano ya Afrika pia mwakani na inapambana na muda kuhakikisha uboreshaji unakamilika mapema ili mechi zake za Kombe la Shirikisho icheze hapo mwakani.

REAL MADRID WATAMBAA HADI 16 BORA KOMBE LA MFALME

Picha
KLABU ya Real Madrid imefanikiwa kutinga hatua ya 16 Bora ya Kombe la Mfalme Hispania baada ya kuifunga Olimpic Xativa mabao 2-0 Uwanja wa Bernabeu.   Kikosi cha Carlo Ancelotti walijiweka kwenye nafasi ngumu awali baada ya awali kutoa sare ya bila kufungana na timu hiyo ya Daraja la Kwanza.   Lakini mabeki wa Real wakafanya kazi nzuri ya kutoruhusu mabao jana, huku Asier Illarramendi akiifungia timu hiyo bao la kwanza dakika ya 16 kabla ya Angel Di Maria kufunga la pili dakika ya 28 kwa penalti. Real sasa itakutana na Osasuna.   B iashara imeisha: Carlos Casemiro na Angel di Maria wakipongezana kwa kuipa ushindi Real Madrid dhidi ya Olimpic de Xativa

FUFA YAMRUDISHA OKWI SIMBA.

Picha
Shirikisho la Soka Uganda (Fufa) limeandika barua kwenda Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) likitaka ufafanuzi juu ya uhamisho wa mshambuliaji hatari Emmanuel Okwi aliyeuzwa kutoka SC Villa kwenda Yanga mwishoni mwa wiki. Uongozi wa Yanga Jumapili ulithibitisha kumsajili kwa miaka miwili na nusu mshambuliaji huyo wa zamani wa watani wao wa jadi, Simba kwa dau kubwa linalotajwa kuwa dola za Marekani 150,000 (Sh. milioni 240 za Tanzania) huku huko nyuma Fifa ilimuidhinisha Okwi kujiunga kwa mkopo SC Villa ya Ligi Kuu ya Uganda akitokea Klabu ya Etoile du Sahel (ESS) ya Tunisia. “Tumeiandikia barua FIFA kwa sababu tunahitaji watueleze kama uhamisho huo ni sahihi," amekaririwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Fufa, Edgar Watson na mtandao wa MTNFootball. Okwi, ambaye aliuzwa kwa mali kauli ya dola za Marekani 300,00 (Sh. milioni 480) na uongozi wa Simba kwa Klabu ya ESS mwaka jana, ameichezea SC Villa katika Ligi Kuu ya Uganda kwa kipindi cha takriban miezi miwili na kuifungia mabao

MAKALA: NI NDOTO VIJANA KUPATA NAFASI YANGA, SIMBA AU TAIFA STARS.

Picha
Na Prince Hoza AKILI za wapenda soka walio wengi hapa nchini ni kuona soka la vijana likipewa nafasi, vijana wanapewa nafasi ili waweze kuisaidia nchi katika siku za usoni baada ya kaka zao kutundika daruga, lakini pia vijana ni mchango mkubwa kwenye maendeleo ya nchi. Lakini jitihada zake zinashindikana, sioni kama kuna dalili za kuwaamini vijana, katika siku za hivi karibuni neno vijana limegeuka siasa kwenye vilabu vyetu vya soka hasa Yanga, Simba na Azam pia limehamia kwenye timu ya taifa, Taifa Stars. Nimeamua kuandika ili kila Mtanzania ashuhudie mwenyewe jinsi mipango ya kutokomeza soka la vijana inavyozidi kuchukua kasi, mashabiki wa soka nchini nao wanahusika kwa namna moja ama nyingine kutokomeza maendeleo ya soka la vijana.

RONALDO ATWAA TUZO YA MCHEZAJI BORA MBELE YA MESSI.

Picha
Gwiji Cristiano Ronaldo, ametajwa kama mshindi wa tuzo ya mchezaji wa mwaka wa World Soccer mbele ya mtani wake wa jadi, Lionel Messi na kiungo machachari wa Bayern Munich, Franck Ribery, jarida hilo lilitangaza Alhamisi. Tuzo hiyo inayoamuliwa na kikao cha wanahabari na wafafanuzi wa mchezo huo kutoka sehemu mbali mbali duniani, lilitambua juhudi zake za kustaajabisha zilizotekelezwa na nyota huyo katika klabu chake Real Madrid pamoja na kuongoza taifa lake Ureno kufuzu Dimba la Dunia la 2014 Brazil. Mara yake ya mwisho kunyakua ilikuwa ni 2008, mwaka ambao pia alitunukiwa lile la mchezaji bora duniani la Fifa Ballon d' Or ambalo anawania dhidi ya wawili hao wakati huu, mshindi akizinduliwa Januari.

MESSI HATOENDA KOKOTE-ROSELL.

Picha
Staa matata wa Barcelona, Lionel Messi, hataenda popote katika utawala wa rais Sandro Rosell kiongozi huyo alitangaza Alhamisi. "Kwa muda wote nitakuwa rais, lolote liwezekanalo au lisilowezekana litatendwa kuhakikisha Messi anasalia kitako hapa," Rosell alihimiza katika hafla ya kuwasilisha mkataba wa ushirikiano baina ya Barca na kampuni kuu ya elektroniki ya Marekani, Intel. "Ni vigumu sana, au tuseme haitowezekana, kuwa Messi ataondoka timu hapa." Mshindi mara nne wa tuzo la Ballon d' Or anauguza jeraha na anatarajiwa kurudi uwanjani Januari huku kandarasi yake Barcelona ikidumu hadi 2018 karibu na wakati nyota huyo atakuwa karibu kuadhimisha miaka 31 tangu kuzaliwa kwake.

BRANDTS AKACHA MAZOEZI YANGA.

Picha
Kocha wa Yanga, Mdachi Ernie Brandts amelazimika kukatisha ratiba ya mazoezi ya kikosi chake kwenye Uwanja wa Bora uliopo Kijitonyama, Dar es Salaam baada ya kubaini wachezaji wake wanasumbuliwa na uchovu wa mazoezi magumu ya juzi. Juzi Timu ya Yanga ilifaya mazoezi kwa takriban saa tatu kwenye uwanja huo huku kukiwa na kali kujiandaa kwa mchezo wa 'Nani Mtani Jembe' dhidi ya watani wao wa jadi, Simba utakaopigwa Uwanja wa Taifa jijini Desemba 21, mwaka huu. Lakini, Kikosi cha Yanga jana kilifanya mazoezi kwa dakika 90 tu kwenye huo tofauti na ilivyozoeleka 'Wanajangwani' kujifua kwa saa mbili.

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA KUJIUZURU.

Picha
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amevunja ukimya na kusema yuko tayari kuachia ngazi endapo tu Rais Jakaya Kikwete ataamua kumwondoa na kama itatokea hivyo, atamshukuru Rais kwa kumwambia, ahsante. Pinda aliliambia Bunge mjini Dodoma jana kwamba endapo Rais hatafanya hivyo, bado wabunge wanayo mamlaka ya kikatiba ya kumwondoa kwa njia ya kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye. Ibara ya 53 A(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977, Bunge linaweza kupitisha azimio la kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu endapo itatolewa hoja kupendekeza hivyo.

HARAMBEE MABINGWA CHALLENGE 2013

Picha
KENYA ‘Harambee Stars’ ndiyo mabingwa wapya wa Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge baada ya jana usiku kuifunga Sudan ‘Mwewe wa Jangwani’ mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya. Shukrani kwake, Nahodha wa timu hiyo, Alan Wanga aliyefunga mabao yote hayo katika mchezo wa leo uliokwenda sambamba na sherehe za miaka 50 ya Uhuru wa Kenya. Wanga alifunga bao la kwanza dakika ya 35 kwa kichwa akiunganisha krosi ya David Ochieng Owino kutoka kushoto na la pili dakika ya 69 akiunganisha kwa guu la kulia krosi ya chini ya James Situma kutoka kulia pia. Hilo linakuwa taji la sita la Challenge kwa Kenya, baada ya awali kutwaa katika miaka ya 1975, 1981, 1982, 1983 na 2002.

IVO MAPUNDA AMWAGA WINO RASMI SIMBA MIAKA MIWILI.

Picha
KIPA namba moja wa Tanzania, Ivo Philip Mapunda, jana usiku amesaini Mkataba wa mwaka mmoja na nusu kujiunga na klabu ya Simba SC ya Dar es Salaam, akitokea Gor Mahia ya Kenya. Ivo anasaini Simba SC, baada ya kung’ara akiwa na kikosi cha Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’ katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge mwaka huu. Ivo aliiongoza Kilimanjaro Stars kufika Nusu Fainali ya Challenge baada ya kuwatoa waliokuwa mabingwa watetezi Uganda ‘The Cranes’ kwa penalti 3-2 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90, kipa huyo akicheza mikwaju miwili. Akizungumza baada ya kusaini Simba SC, Ivo alisema kwamba ameamua kusaini timu hiyo Mtaa wa Msimbazi baada ya kuridhishwa na maslahi aliyopewa.

HULL CITY SASA KUITWA HULL TIGERS.

Picha
Klabu ya Ligi ya Premia Hull City imewasilisha ombi kwa FA ya Uingereza kutaka kubadilisha jina lake hadi Hull Tigers kuanzia msimu ujao, BBC waliripoti Jumatano. Mmiliki wa klabu hiyo Assem Allam anataka kubadilisha jina klabu hiyo ya umri wa miaka 109 kutoka Yorkshire lakini hatua hiyo imepingwa vikali na mashabiki. Mfanyabiashara huyo mzaliwa wa Misri tayari alibadilisha jina la kampuni inayomiliki klabu hiyo kutoka Hull City Association Football Club hadi Hull City Tigers mwezi Agosti. Allam anaamini kwamba nembo ya 'Tigers' “itauza zaidi ulimwenguni”.

STARS KUMKOSA ULIMWENGU DHIDI YA ZAMBIA LEO, SURE BOY AREJEA KIKOSINI

Picha
MSHAMBULIAJI tegemeo wa Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’, Thomas Ulimwengu atakosekana kwenye kikosi cha leo wakati timu hiyo ikimenyana na Zambia katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu wa Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge 2013 Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya. Uli amesema jana kwamba anasumbuliwa na maumivu ya nyama na hali ni mbaya kiasi kwamba hawezi kucheza leo. Uli alicheza vizuri mechi zote, za Robo Fainali Stars ikiitoa Uganda ‘The Cranes’ kwa penalti 3-2 baada ya sare ya 2-2 ndani ya dakika 90 na Nusu Fainali wakifungwa 1-0 na Kenya. Kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’ aliyekosa mechi dhidi ya Kenya kutokana na kuwa anatumikia kadi nyekundu aliyopewa dhidi ya Uganda, leo anatarajiwa kurejea kikosini. Mchezo huo wa mshindi wa tatu, utafuatiwa na Fainali kati ya Sudan ‘Mwewe wa Jangwani’ dhidi ya wenyeji, Kenya ‘Harambee Stars’ jioni, Uwanja huo huo wa Nyayo.

PELLEGRINI SASA AIGEUKIA ARSENAL.

Picha
Manuel Pellegrini wa Manchester City amekiri kwamba hatua yake ya kuweka freshi wachezaji wake kwa ajili ya mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza dhidi ya viongozi Arsenal Jumamosi ilisaidia kwenye ushindi wao wa kushangaza wa 3-2 wakiwa Bayern Munich. Usiku huo wa kihistoria kwa klabu hiyo, City walipambana kutoka mabao mawili chini na kufikisha kikomo mkimbio wa ushindi wa mechi 10 mfululizo za Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya wa mabingwa hao huku kocha wa Bayern Pep Guardiola akikabidhiwa kichapo chake cha kwanza katika dimba kuu akiwa na timu hiyo ya Ujerumani. Bayern pia walishindwa mara ya kwanza nyumbani – baada ya kushinda mara 18 Munich – tangu washindwe na Arsenal 2-0 wakiwa nyumbani mikononi mwa Arsenal wakati wa awamu ya muondoano ya msimu uliopita katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mwezi Machi.

DORTMUND, MILAN WACHECHEMEA HADI 16 BORA .

Picha
Borussia Dortmund ambao walimaliza wa pili msimu uliopita waliepusha aibu ya kubanduliwa mapema Ligi ya Klabu Bingwa na bao la dakika za lala salama lake Kevin Grosskreutz ambalo liliwafikisha Wajerumani hao hadi kwenye 16 bora Jumatano. Dortmund, ambao waliilaza Olympique Marseille 2-1, Arsenal na Napoli wote walimaliza wakiwa na alama 12 huku timu hiyo ya Bundesliga ikimaliza ya kwanza Kundi F na Wataliano hao kuibuka wasio na bahati na kutemwa kutokana na mechi za moja kwa moja licha ya ushindi wa 2-0 dhidi ya viongozi hao wa Ligi ya Premia Uingereza. AC Milan watakuwa ndio wawakilishi pekee wa Italia katika awamu ya muondoano. Galatasaray, Zenit St Petersburg na Schalke 04 walijaza nafasi zilizosalia katika 16 bora na watakuwa kwenye droo ya Jumatatu ambayo itakuwa na wawakilishi wane kutoka Ligi ya Premia na kutoka Bundesliga.

IVO MAPUNDA AIGEUKA SIMBA MWISHONI, AMWAGA WINO MWAKA MMOJA GOR MAHIA.

Picha
Wakati Simba ikieleza kuwa wameshamalizana na kipa chaguo la kwanza la timu ya Kilimanjaro Stars, Ivo Mapunda, na kilichobaki ni kusaini tu, mlinda mlango huyo amekanusha vikali na kuweka wazi kuwa anasaini mkataba mpya wa kuitumikia Gor Mahia. Ivo, ambaye ni kipa namba mbili katika klabu hiyo mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Kenya na akiwa ameonyesha uwezo wa hali ya juu akiwa na timu yake ya Kilimanjaro Stars, amesema anatarajia kusaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuichezea Gor Mahia. Akizungumza jana, Ivo alisema tayari viongozi wake wa Gor Mahia wamemfuata na kumueleza wanataka kumpa mkataba mpya.

PATA PICHA MBALIMBALI ZA KUUAGA MWILI WA NELSON MANDELA.

Picha
 Neslon Mandela's widow Graca Machel bids farewell to South African former president Nelson Mandela lying in state

HOTUBA YA OBAMA 'SAUZ' YAITIKISA DUNIA.

Picha
Licha ya kuwa ni siku ya huzuni kwa dunia nzima, hotuba ya Rais wa Marekani, Barack Obama imewagusa maelfu ya watu waliokuwa kwenye Uwanja wa FNB katika ibada ya kitaifa kumuaga Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela. Obama aliyetumia dakika 20 katika hotuba yake iliyokuwa ikikatizwa na kelele za kumshangilia, aliwataka vijana wa Afrika na dunia nzima kuiga maisha aliyoishi Mandela kama yeye alivyojifunza mambo mengi kutoka kwa mzalendo huyo. “Miaka 30 iliyopita nikiwa mwanafunzi, nilisoma Kitabu cha Mandela na tangu siku hiyo nilijifunza, nikajenga roho ya uthabiti. Iliamsha uwajibikaji kwa ajili yangu na kwa ajili ya watu wangu... hakika Mandela amenifanya niwe hivi nilivyo leo. Michelle na mimi tumenufaika sana na Mandela,” alisema Obama na kuongeza:

HAKUNA KAMA CRISTIANO RONALDO TUZO YA MWANASOKA BORA WA DUNIA.

Picha
Kwa nini asiwe bora duniani? Bao alilofunga jana katika ushindi wa 2-0 dhidi ya FC Copenhagen limemfanya Cristiano Ronaldo awe mchezaji wa kwanza kufunga mabao tisa katika hatua ya makundi kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya. Mreno huyo alirejea uwanjani baada ya kukosa mechi iliyopita ya makundi ya Real Madrid dhidi ya Galatasaray na kufunga dakika ya 58. Sasa amefikisha mabao 59 katika mechi 96 kwenye michuano hiyo, akiwa amefunga katika kila mechi kati ya tano alizocheza msimu huu.

MAN UNITED YAICHAPA SHAKHTAR NA KUMALIZA KILELENI KUNDI A, RONALDO AREJEA NA MOTO WAKE REAL

Picha
BAO pekee la Phil Jones dakika ya 67, limeipa ushindi mwembamba nyumbani wa 1-0 Manchester United dhidi ya Shakhtar Donetsk Uwanja wa Old Trafford na kumpa ahueni kocha David Moyes. Ushindi huo unaipandisha kileleni mwa Kundi A Manchester United, baada ya kumaliza na pointi 14 katika mechi sita ilizocheza. Bayer Leverkursen inashika nafasi ya pili kwa pointi zake 10, Shakhtar ya tatu kwa pointi zake nane na Real Sociedad imeshika mkia kwa pointi yake moja. Katika mechi nyingine, mshambuliaji Cristiano Ronaldo amerejea kutoka kwenye maumivu ya nyama na kufunga bao katika ushindi wa 2-0 ugenini dhidi ya FC Copenhagen.

KILL STARS YATUPWA NJE CHALENJI, SAMATTA ASHINDWA KUIBEBA TENA.

Picha
TANZANIA Bara ‘Kilimanjaro Stars’, imefungwa 1-0 na Kenya ‘Harambee Stars’ katika Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge Uwanja wa Nyayo, Nairobi, ikisindikizwa na mvua. Kwa matokeo hayo, sasa Stars itamenyana na Zambia katika mechi ya kusaka mshindi wa tatu keshokutwa mchana Uwanja wa Nyayo tena, wakati Kenya itamenyana na Sudan katika Fainali jioni yake. Katika mchezo huo, uliochezeshwa na refa Thiery Nkurunziza wa Burundi, aliyesaidiwa na Idam Hamid wa Sudan na Mussie Kinde wa Ethiopia, hadi mapumziko, tayari wenyeji walikuwa mbele kwa bao hilo 1-0, lililowekwa kimiani na mshambuliaji wa Thika United, Clifton Miheso dakika ya nne kwa shuti la umbali wa mita 20, baada ya kupokea pasi fupi ya Alan Wanga na kumchungulia kipa Ivo Mapunda.

SIRI YAGUNDULIKA KINACHOMUONDOA MANJI YANGA.

Picha
Na Salum Fikiri Jr HATIMAYE siri imegundulika kwamba kinachomuondoa mwenyekiti wa mabingwa wa soka Tanzania bara Yanga Yusuf Manji kufuatia kauli yake aliyoitoa jana wakati viongozi wa timu hiyo walipokutana na kujadili mambo mbalimbali ikiwemo kuteua wajumbe wengine katika kamati mbalimbali zilizoundwa. Siri iliyogundulika na kuelezwa Mambo Uwanjani kuwa mwenyekiti huyo atogombea tena Uenyekiti katika uchaguzi ujao na kuwapisha wengine wenye nia ya kutaka kuiongoza Yanga, lakini inasemekana Manji amekimbia kivuli chake huku suala la mheshimiwa Rage na klabu yake ya Simba moja kati ya sababu zinazomuondoa mapema Yanga. Mbali na hilo msimamo wa baraza la wazee la klabu hiyo linaloongozwa na mzee Ibrahim Akilimali ambalo lilipinga waziwazi ajira ya Mkenya kuwa katibu mkuu wa Yanga pamoja na mtunza fedha ambaye alikuwa Mhindi, wazee hao waliendelea na msimamo wao na kupinga wazo la kuanzishwa kwa kampuni.

MWALUSAKO AKUMBWA NA KIMBUNGA JANGWANI, NJOVU AMRITHI.

Picha
Uongozi wa Yanga umemtambulisha Beno Njovu kuwa Katibu Mkuu mpya wa klabu hiyo akichukua nafasi ya Lawrence Mwalusako aliyekuwa akiikaimu kwa mwaka mmoja baada ya Celestine Mwesigwa kufukuzwa Septemba mwaka jana. Kamati ya Utendaji ya Yanga, ilimtambulisha rasmi Njovu ambaye wameingia naye mkataba wa mwaka mmoja, mbele ya waandishi wa habari, wajumbe wa Baraza la Wazee la Yanga na Baraza la Wenyeviti wa Matawi wa klabu hiyo kwenye makao makuu ya Yanga jijini Dar es Salaam jana. Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto alisema, Njovu alianza kuitumikia nafasi hiyo kuanzia jana na Mwalusako atakuwa naye kwa kipindi cha mwezi mmoja mpaka atakapokabidhi kazi rasmi Januari mwakani.

MECHI YA KILI STARS, HARAMBEE YAOTA MBAWA, UWANJA WAJAA MAJI SASA KUPIGWA NYAYO STADIUM.

Picha
MECHI ya Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge kati ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’ na Kenya ‘Harambee Stars’ iliyopangwa kuanza Saa 7:00 mchana huu Uwanja wa Kenyatta, Machakos, imeahirishwa na sasa itachezwa Saa 12:00 jioni Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya. Katibu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholas Musonye amesema kwamba sababu ya kufikia hatua hiyo ni hali mbaya ya Uwanja wa Kenyatta kufuatia mvua kubwa iliyonyesha leo. Makocha wa timu zote, Kim Poulsen wa Tanzania Bara na Adel Amrouche wa Kenya wamekagua Uwanja na kujiridhisha haufai kuchezewa, ingawa Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka Kenya (FKF) alikuwa anashinikiza mechi hiyo ichezwe hapo hapo

MKOLA MAN AHUSISHWA NA FREEMASON, NEMBO YAMPONZA.

Picha
Na Exipedito Mataluma MWANAMUZIKI wa kizazi kipya anayetokea Hale mkoani Tanga Christopher Mhenga maarufu Mkola Man anatajwa kuwemo katika orodha ya wasanii wanaotajwa kuwemo kwenye imani ya kishetani inayoenea kwa kasi nchini ya 'Freemason' huku ikidaiwa nembo anayotumia ndio imemponza. Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari vinasema kuwa msanii huyo kwa sasa ameanza kujipatia umaarufu mkubwa na kupata mialiko kadhaa ndani na nje ya Tanzania kiasi kwamba kinawachanganya wengi, pia kuongezeka kwa mashabiki na kupendwa kwa nyimbo zake ukiwemo huu mpya wa 'Kilevi changu' ni sehemu nyingine inayotajwa kuwemo katika imani hiyo. Pia chanzp chetu kimefichua siri ya msanii huyo kuwa anatumia nembo maarufu ya '5LAMABAD ' ambayo ni moja kati ya alama za imani hiyo, kitu kingine kilichoibua tetesi za msanii huyo kujihusisha na freemason ni pale alipopiga picha akifanya tambiko kwenye makaburi ambapo inasemekana watu wenye imani hiyo hupendelea kufanya hivyo.

SHEREHE ZA UHURU ZAFANA JANA, KIKWETE AMUELEZEA MANDELA NA NYERERE.

Picha
Rais Jakaya Kikwete jana aliongoza maelfu ya Watanzania katika maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru wa Tanganyika (sasa Tanzania), kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam na kulihutubia taifa, akiwataka wananchi kuwa na moyo wa kusamehe kama aliokuwa nao Rais wa Kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela. Tanganyika ilipata uhuru wake kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza Desemba 9, mwaka 1961. Katika maadhimisho hayo, mbali na karibu asilimia 90 ya hotuba ya Rais Kikwete kumzungumzia marehemu Mandela, aliamuru kusitishwa kwa shamrashamra za ngoma za asili kama ilivyozoeleka na badala yake ilikuwapo halaiki pekee.

JAKAYA KIKWETE KAMA OBAMA 'SAUZI' KUMUAGA ,MANDELA.

Picha
Serikali ya Afrika Kusini, imetoa orodha ya majina ya wakuu wa nchi na Serikali 91 ambao wamethibitisha kushiriki katika shughuli zinazohusiana na safari ya mwisho ya Rais wa kwanza mzalendo wa taifa hilo, Nelson Mandela. Jina la Rais Jakaya Kikwete ni la kwanza katika orodha hiyo inayowaweka viongozi hao katika makundi kutokana na mabara wanakotoka. Rais Kikwete alitarajiwa kuwasili jana usiku tayari kuhudhuria Ibada ya Kitaifa ya Mandela ambayo imepangwa kufanyika leo kwenye Uwanja wa FNB (Soccer City). Kabla ya Serikali kutoa orodha hiyo, Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa wa Afrika Kusini, Maite Nkoana-Mashabane alisema wakuu wa nchi na Serikali 53 walikuwa wamethibitisha lakini jana mchana idadi hiyo ilikuwa imeongezeka na kufikia 91. Kulikuwa na wasiwasi kwamba huenda idadi hiyo ikaongezeka na kuzidi 100. Msemaji wa Wizara ya Uhusiano wa Kimataifa ya Afrika Kusini, Clayson Monyela aliwataja marais wengine kutoka Afrika kuwa ni kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC), Joseph K

IVO MAPUNDA ASAINI SIMBA MIAKA MIWILI.

Picha
Uongozi wa Simba umesema upo katika hatua za mwisho kukamilisha usajili wa kipa mkali wa kupangua mikwaju ya penalti Mtanzania Ivo Mapunda. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hanspope alisema uongozi wa 'Wanamsimbazi' hao umekubaliana kumpa mkataba wa miaka miwili kipa huyo wa zamani wa watani wao wa jadi, Yanga. "Kwa sasa tunamsikiliza kocha (Mcroatia Zdravok Logarusic) kama kuna mchezaji mwingine anayemhitaji baada ya kumpata Ivo. Tumekubaliana tumpe mkatana wa miaka miwili ambao atausaini mara tu baada ya mashindano ya Kombe la Chalenji," alisema Hanspope. Alisema wametenga fungu nono ambalo limemshawishi nyota huyo kujiunga nao.

MESSI, RONALDO NA RIBBERY WAINGIA FAINALI BALLON D'OR

Picha
FIFA imethibitisha orodha ya majina ya wachezaji watatu walioingia Fainali ya kuwania tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia wa mwaka 2013, Ballon d'Or ambao ni mtetezi Lionel Messi, Cristiano Ronaldo na Franck Ribery. Messi ameshinda mfululizo mara nne tuzo zilizopita, lakini safari hii ni Ronaldo anayepewa nafasi kubwa ya kutwaa mpira wa dhahabu. Mtu wa tuzo: Lionel Messi aliposhinda tuzo ya 2012 ya Ballon d'Or Watatu wa Fainali: Mwaka jana walioingia fainali walikuwa Cristiano Ronaldo, Andres Iniesta na Messi

STARS DHIDI YA KENYA ‘INAYOBEBWA VIBAYA’ NA MAREFA CHALLENGE 2013, PATACHIMBIKA MACHAKOS LEO

Picha
TANZANIA Bara ‘Kilimanjaro Stars’, leo inashuka dimbani kwenye Uwanja wa Kenyatta, Machakos, kumenyana na wenyeji, Kenya ‘Harambee Stars’ katika Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge kuanzia saa 7:00 mchana. Hii ni mara ya pili mfululizo kwa Stars chini ya kocha Mdenmark, Kim Poulsen kufika Nusu Fainali ya michuano hiyo, baada ya mwaka jana pia mjini Kampala, Uganda ambako ilitolewa na wenyeji, Uganda ‘The Cranes’ kwa kufungwa mabao 3-0. Lakini Kim, amelipa kisasi kwa The Cranes, baada ya Stars kuivua ubingwa Uganda Jumamosi kwa kuitoa kwenye Robo Fainali, Uwanja wa County ya Mombasa, zamani Manispaa kwa penalti 3-2, kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90. Baada ya kumaliza shughuli hiyo pevu, Kim anakabiliwa na jukumu lingine zito mbele yake, ambalo ni Nusu Fainali dhidi ya Kenya, ambayo imeonekana ‘kubebwa’ mno na marefa hadi sasa katika mashindano haya.

MAKALA: MGOGORO SIMBA UMEPANDIKIZWA.

Picha
Na Prince Hoza KWA sasa hawakai kiti kimoja, wamegombana, ni mgogoro mkubwa unafukuta katika klabu ya Simba unaowahusisha viongozi wa juu wa timu hiyo, mgogoro huo umesababisha kutimuliwa kwa makocha Abdallah Kibadeni na msaidizi wake Jamhuri Kihwelo 'Julio'. Pia umesababisha kuajiliwa kocha mpya Zdravkos Lugarusic, pia umesababisha wapenzi na wanachama wa timu hiyo kugawanyika, katika sehemu ya mgogoro wa klabu ya Simba chanzo inasemekana ni mwenyekiti wao Ismail Aden Rage. Baadhi ya viongozi wa klabu hiyo kongwe Afrika mashariki na kati kupitia kamati ya utendaji waliitisha mkutano kwa lengo la kumjadili mwenyekiti wao ambaye alikuwa safarini nje ya nchi kikazi, katika mkutano huo waliamua kumsimamisha mpaka mkutano mkuu wa wanachama utakapoamua hatma yake. Ndipo ulipoibuka mgogoro mkubwa uliopelekea mwenyekiti wa klabu hiyo aliyesimamishwa kupinga uamuzi wa kamati kumsimamisha na kuwasilisha malalamiko yake TFF, Lakini kamati ya utendaji ya klabu hiyo iliendelea na

MBEYA CITY YAMPONZA PRINCE HOZA.

Picha
Na Mwandishi Wetu Majanga yameanza kumpata aliyekuwa mkurugenzi wa promosheni katika kampuni ya Modern Publishers Prince Hoza ( Pichani) ambao pia ni watoaji wa gazeti maarufu la michezo la Mwanasoka ambalo linasomwa na wapenzi na mashabiki wa klabu ya Simba maarufu wekundu wa msimbazi. Kwa mujibu wa chanzo cha habari hizi kinasema kuwa  Hoza ambaye ni kiongozi upande wa promosheni katika kampuni hiyo inayomilikiwa na mdau na mwanachama maarufu wa Simba SC Majuto Mbiligenda, taarifa hizo zinadai kuwa ujumbe alioutuma Hoza katika ukurasa wake wa facebook ndio chanzo kilichopelekea kuondoshwa katika kampuni hiyo na kusimamishwa kazi. Inaemekana kuwa Hoza aliandika katika ukurasa wake wa facebook kuwa yeye si shabiki wa Simba na ameamua kujiunga na Mbeya City inayotokea mkoani Mbeya, Hoza aliamua kufanya hivyo kutokana na mgogoro unaoendelea kufukuta katika klabu hiyo iliyopelekea kusimamishwa kwa mwenyekiti wa klabu hiyo Alhaj Ismail Aden Rage. Chanzo kilichosababishwa Hoza af

NI KIFO TU BRAZIL, GHANA YAPANGWA NA WABABE....

Picha
Hapana shaka wapenzi wa soka barani Afrika pamoja na kuomboleza kifo cha Nelson Mandela wamekuwa wanafuatilia Droo ya kombe la dunia kufahamu nani wapinzani wa timu tano zinazowakilisha bara hilo. Cameroon wamejikuta katika kundi gumu la A pamoja na wenyeji Brazil, Mexico na Croatia. Mabingwa watetezi Uhispania watakuwa katika kundi B pamoja na Netherlands waliokutana nayo fainali kombe lililopita, na timu zingine ni Chile na Australia. Dua ya Ivory Coast ya kuepuka kundi gumu sana wakati huu inaonekana imesikika, wako katika kundi C pamoja na Colomboa, Japan na Ugiriki.England watakuwa na kibarua kigumu kwenye kundi D ambapo wapinzani wao ni Italia, Uruguay na Costa Rica.

MAZISHI WA NELSON MANDELA YAIDI YA PAPA JOHN PAUL 11.

Picha
Afrika na dunia inatarajiwa kushuhudia kitu kipya katika maziko ya Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela (95) aliyefariki dunia juzi, baada ya kuugua kwa zaidi ya miezi sita. Serikali ya Afrika Kusini imesema kiongozi huyo ambaye atazikwa Desemba 15, imeandaa mazishi ya kihistoria yanayosemekana yatazidi yale ya Papa John 11. Matukio ya shughuli mbalimbali zinazohusu mipango ya maziko ya kiongozi huyo maarufu yanatarajiwa kushuhudiwa sehemu mbalimbali duniani, tofauti na tukio jingine lililowahi kutokea barani Afrika mbali na kombe la dunia.

UGANDA YATISHWA NA MAKALI YA SAMATTA, ULIMWENGU, POULSEN ATAMBA USHINDI LEO.

Picha
ROBO Fainali za kwanza za Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Chalenge zinatarajiwa kuchezwa leo Uwanja wa Manispaa, Mombasa, Kenya. Mechi inayotarajiwa kuteka hisia za wengi ni kati ya mabingwa watetezi, Uganda The Cranes dhidi ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars itakayoanza saa 8:00 mchana, ingawa kutakuwa na mchezo mwingine kati ya Kenya na Rwanda saa 10:00 jioni. Stars wanaingia katika sura ya unyonge kumenyana na The Cranes inayofundishwa na kocha hodari Afrika, Mserbia Milutin Sredojevic ‘Micho’ kutokana na kufungwa mfululizo na wapinzani wao hao siku za karibuni. Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inayoundwa na idadi kubwa ya wachezaji wa Bara ilifungwa nyumbani na ugenini na Uganda katika mechi za kuwania tiketi ya kucheza Fainali za CHAN.