Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2015

Drogba naye awafuata akina Henry, Gerrald Marekani

Picha
Mchezaji wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba amekamilisha usajili wake kwenye klabu ya Ligi Kuu ya Marekani (MLS), Montreal Impact ya Canada. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 ambaye alikuwa nahodha wa Ivory Coast ametua Montreal kama mchezaji huru baada ya kumaliza maisha yake katika klabu ya Chelsea alikorejea akitokea China alikocheza kwa msimu mmoja. Aliichezea Chelsea kwa mafanikio na kufunga mabao 164 kwa misimu tisa. Awali, Drogba alivumishwa kuwa angetua Inter Milan na klabu nyingine la MLS ,Chicago Fire ambayo zilikuwa zikimtaka. Hata hivyo, Drogba aliichagua Montreal Impact ambayo amesaini mkataba wa kuichezea msimu ujao.

Simba yaendeleza mauaji Zanzibar, yaipiga Black Sailor 4-0

Picha
Simba imetoa mafunzo ya soka kwa tiku ya Black Sailor  kwa kuichapa kwa mabao 4-0.Black Sailor ambayo imepanda Ligi Kuu Zanzibar msimu huu ilikiona cha moto, kwani hadi mapumziko Simba ilikuwa ba mabao mawili. Abdi Banda ndiye alianza kuifungia timu yake bao dakika ya nne tu baada ya kupokea pasi nzuri ya Dani Alves au Hassan Kessy na Kadabra Ibrahim Ajib akaongeza la pili katika dakika ya 23. Simba ilipata mabao yake mengine katika dakika dakika 80 na 90 wafungaji wakiwa ni Elius Maguli na Boniface Maganga.

MAKALA: SHUKURU NASSORO 'SHAMTA' MSANII ANAYEICHIPUKIA, ADAI YOUNG D NDIYE ALIYEMFANYA AIMBE HIP HOP

Picha
Na Mwandishi Wetu ANAFAHAMIKA zaidi kama Shukuru Nassoro jina ambalo alipewa na wazazi wake wawili baba na mama, lakini vijana wenzake wa mtaani wakampachika jina la utani Shamta ambalo ndilo analolitumia kwenye sanaa yake ya muziki wa hip hop. Shamta alizaliwa Machi 27 mwaka 1996 Mdaula Chalinze mkoani Pwani, na ni mtoto wa sita kuzaliwa katika familia ya mzee Nassoro, elimu yake ya msingi aliianzia hapo hapo Mdaula na mwaka 2012 akabahatika kufaulu na kujiunga na sekondari. Msanii huyo wa muziki wa kizazi kipya alichaguliwa kujiunga na sekondari ya Handeni mkoani Tanga ambapo mwaka huu anatarajia kumaliza kidato cha nne na kujikita kisawa sawa kwenye muziki. Akielezea muziki, Shamta anasema alianza kuupenda muziki tangia anasoma shule ya mdingi na alizidi kuupenda kila alivyozidi kukua, Shamta anadai Young D ndiye aliyemsukuma zaidi kuingia kwenye tasnia hiyo inayopendwa na vijana wengi hapa nchini, hivyo naye aliamua kuingia rasmi kwenye gemu.

Hii ndiyo historia kamili ya Yanga SC iliyotimiza miaka 80 ya kuzaliwa kwake.

Picha
YANGA SC siku ya Idd pili itasherehekea miaka ya 80 ya kuzaliwa kwake, pia itasherehekea ubingwa wake wa 25 iliyoutwaa msimu uliomalizika mwaka huu. Katibu mkuu wa Yanga Dk Jonas Toboroha aliiambia Afrika Soka kuwa sherehe hizo sasa zitafanyika siku ya Idd pili baada ya kukubali kuzisogeza mbele, awali sherehe hizo zilikuwa zifanyike jumamosi iliyopita ya tarehe 27 Juni mwaka huu. Siku hiyo kulipangwa kufanyika kwa burudani kadhaa kutoka kwa wanamuziki wetu, pia mgeni wa heshima ilikuwa awe rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete ambaye pia ni mpenzi mkubwa wa Yanga.

Khalfan Ngasa 'Babu': Unafahamu kwamba amemfunika mwanaye Mrisho Ngasa kwa rekodi Simba?

Picha
Na Prince Hoza NAFURAHI umzima na unaendelea na majukumu yako ya kila siku huku ukiendelea kufuatilia safu yako pendwa ya 'Anayekumbukwa', kwa sasa habari ya mjini ni kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura kwa kutumia BVR, nadhani ewe ndugu msomaji umejiandikisha. Na kama ulikuwa haujajiandikisha ni vema ukaenda kupanga foleni ili ujiandikishe na utumie haki yako ya kidemokrasia kumchagua rais, mbunge na diwani wako katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu. Na huneda uchaguzi wa mwaka huu ukawa wa kihistoria hasa kutokana na Chama Cha Mapinduzi CCM kumpitisha ndugu John Pombe Magufuli kuwa mgombea wake wa urais, na aliyekuwa waziri mkuu Edward Lowassa kuhamia Chadema ambapo naye huenda akasimishwa kuwa mgombea wa urais kupitia chama hicho kinachounda UKAWA.

Simba itacheza Caf mwakani- Kiiza

Picha
Mshambuliaji mpya wa Simba SC Hamis Friday Kiiza ambaye jana alisaini mkataba wa miaka miwli ametamba kuwa klabu hiyo msimu ujao itapata tiketi ya kushiriki michuano ya Caf kwa kumaliza katika nafasi za juu ya msimamo wa ligi kuu bara. Akizungumza hayo na mwandhishi wa habari hizi, Kiiza amesema Simba ina kila nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa kutokana na kuimariika kwa kikosi chake, Kiiza amedai uwepo wake katika safu ya ushambuliaji sambamba na Mussa Hassan Mgosi, Emmanuel Okwi, Laudit Mavugo kutawapa jeuri na kutwaa ubingwa wa bara.

Barcelona kumsajili Pogba

Picha
Mgombea wa wadhfa wa urais katika klabu ya Barcelona Joan Laporta anasema kuwa mabingwa hao wa Ulaya watajaribu kumsajili kiungo wa kati wa Juventus Paul Pogba iwapo atachaguliwa. Ripoti zinasema kuwa kilabu ya Barcelona ilijaribu kumsajili raia huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 22 ambaye aliisaidia Juventus kushinda ligi ya Serie A na kufika fainali ya kombe la vilabu bingwa Ulaya. ''Kuna mchezaji tunayempenda sana -Paul Pogba. Tunamjua ajenti wa mchezaji huyo na hilo na swala muhimu katika oparesheni zetu. Tutajadiliana na wakala wake pamoja na klabu ya Juventus'',. Alisema Laporta.

KIMONDO YAZIDI KUIWEKA ROHO JUU YANGA

Picha
Wakati uongozi wa Yanga umedai kuwa ulimsajili kiungo Geofrey Mwashiuya akiwa huru, uongozi wa Kimondo umesema una mkataba na mchezaji huyo na utawashtaki mabingwa hao wa Bara ikiwa wataendelea kumtumia. Mwanzoni mwa wiki Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga, Jerry Muro aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18, alisaini nayo mkataba wa miaka mitatu akiwa huru. Hata hivyo, mkurugenzi wa Kimondo, Elick Ambakisye aliuambia mkutano na waandishi wa habari jijini hapa jana kuwa Mwashiuya ana mkataba wa miaka minne aliousaini Agosti 30 mwaka jana.

Chelsea yamsajili Radamel Falcao

Picha
Chelsea imemsajili mshambuliaji wa klabu ya Monaco Radamel Falcao kwa makubaliano ya mkopo lakini kuna uwezekano wa kuongeza kandarasi hiyo na kuwa ya kudumu. Falcao mwenye umri wa miaka 29 alicheza kama mchezaji wa mkopo katika klabu ya Manchester United na kufanikiwa kufunga mabao manne katika mechi 29. Anakutana na wachezaji wenza wa zamani katika kilabu ya Athletico Thibaut Courtois,Filipe Luis na Diego Costa.

KOCHA SIMBA AZIOGOPA YANGA, AZAM

Picha
Kocha wa Simba, Dylan Kerr amesema anahitaji mechi tano za kirafiki kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu Bara, lakini si dhidi ya Yanga na Azam. Kocha huyo Mwingereza alianza kibarua chake juzi aliliambia gazeti hili kuwa anahitaji mechi hizo za kirafiki dhidi ya timu yoyote inayoshiriki Ligi Kuu, lakini isiwe Azam wala Yanga kwani anajua hao ni wapinzani wake katika mbio za kusaka ubingwa. Simba iliyoanza mazoezi ya viungo gym wiki iliyopita, juzi ilianza mazoezi ya uwanjani chini ya kocha Kerr na wasaidizi wake, Selemani Matola, Mserbia Dusan Momcilovic kocha wa viungo na kocha wa kipa, Mkenya Abdul Iddi Salim.