Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2014

GEORGE BUSH ALAZWA MAREKANI

Picha
Aliyekuwa rais wa Marekani George H.W Bush amekimbizwa katika hospitali moja ya Houston nchini Marekani baada ya kupatikana na tatizo la kupumua. Kulingana na madaktari,Bush mwenye umri wa miaka 90 anachunguzwa katika hospitali ya Methodist. Alipelekwa katika hospitali hiyo na ambalensi jumanne usiku. Wawakilishi wa Bush wanasema kuwa hatua hiyo ya kupelekwa hospitali ni kama tahadhari.

RA,OS AMALIZA MWAKA BORA KWA TUZO YA CWC

Picha
Sergio Ramos Difenda wa Real Madrid aliyeshinda mataji mengi Sergio Ramos ametaja mwaka 2014 "mwaka bora zaidi maishani mwangu” baada ya kuchangia sana ufanisi wa miamba hao wa Uhispania waliposhinda mataji manne ikiwa ni pamoja na kutwaa kombe la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mara ya 10. Mkabaji huyo wa kati ambaye nguvu zake angani mara nyingi huzalisha mabao alishinda tuzo ya mchezaji wa dimba katika Kombe la Dunia la Klabu baada ya kufunga wakati wa ushindi nusufainali dhidi ya Cruz Azul na ushindi dhidi ya San Lorenzo kwenye fainali Jumamosi. Tukio kuu zaidi uwanjani katika mwaka ambao pia alikuwa baba kwa mara ya kwanza lilikuwa kusawazisha dakiak za mwisho dhidi ya Atletico Madrid fainali ya Kombe la Klabu Bingwa Ulaya Mei kabla ya Real kushinda mahasimu hao wao wa jiji 4-1 baada ya muda wa ziada kuongezwa.

MESSI ATOSWA CHELSEA

Picha
Kocha wa Timu ya Chelsea Jose Mourinho amesema kwa sasa hawana nafasi ya kumsaini mchezaji Lionel Messi kwa kuwa hakuna Fedha ya kutosha kumsajili mchezaji huyo .

MOURINHO AFURAHISHWA SANA NA VIJANA WAKE

Picha
Jose Mourinho Meneja wa Chelsea Jose Mourinho alisifu sana ushindi wa vijana wake wa 2-0 Ligi ya Premia ugenini Stoke City Jumatatu na kuutaja kuwa mojawapo ya ushindi muhimu zaidi wao msimu huu. Bao la kichwa dakika ya pili kutoka kwa John Terry na la Cesc Fabregas kipindi cha pili, yaliwezesha vijana hao wa London kurejesha mwanya wa alama tatu kileleni mwa jedwali kati yao na Manchester City klabu zikielekea Krismasi. Lakini ni jinsi ushindi huo ulivyopatikana iliyomfurahisha Mourinho sana huku Chelsea wakipigana kushinda vita vikali vya kimwili. “Kushinda hapa lazima ucheze mchezo mzuri sana na tulifanya hivyo kwa sababu tulibadilika na mtindo wao wa uchezaji,” akasema. “Tulipokuwa na mpira, tulijaribu kutopoteza sifa zetu na kucheza mchezo wetu. “Huwa wakali sana uwanja huu, na mashabiki huwaunga mkono sana. Wana wachezaji wazuri na benchi zuri pia. Ulikuwa ushindi mgumu.

MAJANGA YANGA, MLIBERIA WAKE ASAKWA ULAYA

Picha
WAKATI Yanga ikiwa katika maandalizi ya mwisho kuwavaa Azam FC katika mechi ya Ligi Kuu Bara, jambo jipya limeibuka kuwa yule mshambuliaji wake hatari, Kpah Sherman raia wa Liberia, anatuhumiwa kutoroka kazini nchini Cyprus Kaskazini. Taarifa kutoka Cyprus Kaskazini barani Ulaya kwa mmoja wa Watanzania wanaoishi nchini humo zimeeleza vyombo vya habari nchini humo, vimeripoti kuwa Mliberia huyo atafunguliwa mashitaka baada ya kutorokea Tanzania. “Nimesikia huyo mchezaji yuko huko nyumbani, ila huku vyombo vya habari vya hapa vimeripoti timu yake ina mpango wa kufungua kesi Fifa kuelezea kuhusiana na kutoroka kwake,” alisema Mtanzania huyo anayeishi nchini humo. Juhudi za kuwapata viongozi wa Yanga ilikuwa ni ‘sheedaa’, imeelezwa Mwenyekiti Yusuf Manji yuko nje ya nchi na katibu mkuu mpya, hajaingia ofisini rasmi. Uongozi wa Klabu ya Centikaya TSK ya Cyprus, umethibitisha kushitushwa na taarifa za Sherman kuondoka nchini humo akidai ana matatizo ya kifamilia.

MAKALA: YAJUE MAISHA YA JONAS MKUDE WA SIMBA SC

Picha
TANZANIA ina jumla ya watu milioni 45 kulingana na sensa ya watu ya mwaka 2012, kati yao kuna wanandinga lukuki, lakini ina kiungo mmoja tu mkabaji anayeaminiwa na wengi ambaye si mwingine ni Jonas Gerald Mkude utotoni alikuwa akiitwa Jonas Mwakindagi. Wengi hawaijui historia ya Mkude lakini gazeti la Msimbazi limefanikisha kuipata na hatimaye leo inawajuza, alipokuwa mdogo akicheza mpira wa chandimu, Mkude alianzia golini. Timu ya mtaani kwake iliyoanzia kucheza barabarani na kupelekea usumbufu mkubwa kwa wapita njia, hasa watembea kwa miguu, baiskeli au magari na pikipiki, Mkude na akiwa na umri wa miaka minne alisimama imara katika lango la timu yake. Kipindi hicho alipata usumbufu mkubwa kutoka kwa mama yake ambaye hakutaka mwanaye acheze soka, lakini alijiiba mara kwa mara na kuendelea nao.

PHIRI ASEMASIMBA SASA IMEIVA, ANAYEKATIZA MBELE HALALI YAO

Picha
Baada ya kuichapa Yanga mabao 2-0 na kufanikiwa kunasa saini za nyota watatu wapya kutoka Uganda, kocha wa Simba, Mzambia Patrick Phiri alisema kikosi chake sasa kimeiva na anaamini kitafanya kazi nzuri msimu huu. Simba iliinyanyasa bila huruma Yanga kwa kuipa kipigo cha pili katika mechi ya Nani Mtani Jembe 2 iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi. Katika mechi hiyo, Simba iliwatumia wachezaji wawili kutoka Uganda waliokuwa wametua nchini kwa ajili ya kufanya majaribio, beki Juuko Murshid na mshambuliaji Simon Sserunkuma kabla ya juzi kuwasanisha mikataba baada ya kuridhika na viwango vyao. Katika mahojiano na NIPASHE jijini jana, Phiri alisema kikosi chake kimeimarika na kinampa matumaini ya kufanya vizuri katika mechi zinazofuata za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu baada ya kuanza vibaya katika mechi sita za awali walizoambulia sare. "Kesho (leo) tutaanika wachezaji wote walioingia na kutoka Simba kabla ya timu yetu kuingia kambini Ndege

HAKUNA MAKOSA KUMWACHIA LAMPARD- MOURINHO

Picha
Frank Lampard  Meneja wa Chelsea Jose Mourinho hajuti kumwachilia kiungo nyota mkongwe Frank Lampard kuondoka licha ya kubobea kwake akichezea mabingwa wa ligi ya Premier Manchester City. Vingozi Chelsea na City wanashindania vikali taji hilo wakitenganishwa na alama tatu pekee huku Manchester United wakiwa point inane nyuma ya vinara katika nafasi ya tatu. Lampard, 36, aliondoka Chelsea Juni baada ya miaka 11 ya ufanisi kama kiungo kigezo cha kati ambapo alivunja rekodi ya mabao ya klabu hicho na kujiunga na timu ya Marekani, New York City. Klabu hicho kilimwazima kwa mkopo kwa wamiliki wao Manchester City na amewafungia magoli sita ikiwemo bao la kipekee na la ushindi Jumamosi dhidi ya wavuta mkia Leicester City.

KAZI KWAMAGIWJI CHELSEA, LIVERPOOL.

Picha
Vinara wa ligi ya Premier ya Uingereza Chelsea na miamba wenzao Liverpool waliotatizika watakuwa miongoni mwa vilabu vitakavyo wania kukaribia Wembley kwenye robo fainali za Kombe la Ligi wiki hii. Chelsea watatembelea Derby County wanaocheza daraja la kwanza Jumanne huku Liverpool wakichuana na vingozi wapya wa ngazi hiyo, Bournemouth Jumatano. Kwenye kivumbi cha timu za Premier, Tottenham Hotspurs watatoana jasho na Newcastle United huku Sheffield United wa daraja la tatu watachuana na Southampton ambao wamekosa mwelekeo. “Timu hii ina ahadi kubwa na mambo yameenda vyema musimu huu lakini hatujashinda lolote kwa sasa na hakuna haja ya kulinganisha kikosi cha sasa na vile vilivyotangulia hadi mwisho wa musimu,” golikipa Petr Cech alisema.

BABU PLUIJM ATUA YANGA, MWENYEWE ASEMA NDOTO ZAKE ZIMETIMIA.

Picha
Aliyekuwa kocha mkuu wa Yanga Hans Van der Pluijm 'Babu' amewasili jana usiku tayari kabisa kwa kuanza kazi ya kuinoa timu hiyo, Pluijm ataanza kazi ya ukocha mara tu atakapokuwa amesaini mkataba mpya.

MAN UNITED SASA YAPIGIWA HESABU ZA UBINGWA ENGLAND

Picha
Manchester United moja ya timu vigogo wa ligi kuu ya England ambayo kabla ya ushindi wa sita mfululizo ilikuwa na wakati mgumu, sasa imeanza kupewa nafasi ya kutwaa ubingwa wa ligi hiyo maarufu duniani. Manchester United Jumapili waliiangushia kipigo Liverpool kwa kuwacharaza magoli matatu kwa bila na kupanda hadi nafasi ya tatu wakiwa na pointi 31 nyuma ya Chelsea vinara wenye pointi 39 na Manchester City wakiwa na pointi 36. Kocha msaidizi wa zamani wa Manchester United, Phil Neville akizungumza na BBC Radio 5, alisema, Manchester United inaweza kutwaa taji la ligi hiyo.

REAL MADRID YAENDELEZA REKODI YAKE YA USHINDI

Picha
Karim Benzema Cristiano Ronaldo alifunga mawili na kusaidia viongozi wa La Liga Real Madrid kutwanga Almeria 4-1 na kuongeza mkimbio wao wa kushinda hadi mechi 20 Ijumaa. Ronaldo alifunga dakika 10 za mwisho na kufikisha idadi ya mabao aliyofunga ligini hadi 25 alipofikia mpira wa Karim Benzema uliokuwa umezimwa na kisha akafunga kutoka kwa pasi ya Isco kutoka katikati ya eneo la hatari na kukamilisha ushindi huo. Real wanaongoza jedwali la ligi na alama 39 kutoka kwa mechi 15, alama tano mbele ya Barcelona watakaotembelea Getafe Jumamosi. Kiungo wa kati Isco alikuwa ameweka Real kifua mbele kwa kombora kali la kujipinda kutoka nje ya eneo la hatari dakika ya 15 kabla ya Almeria kusawazisha kwa kombora la mbali lililotoka kwa Verza. Gareth Bale kisha alifunga kwa kichwa kutokana na krosi ya Toni Kroos na kuweka Real 2-1 mbele wakati wa mapumziko.

Di Maria kukosa mechi ya Liverpool

Picha
Angel Di Maria Mchezaji aliyenunuliwa pesa nyingi zaidi na Manchester United Angel Di Maria atakosa mechi dhidi ya mahasimu hao wao wa jadi Ligi ya Premia Jumapili lakini mzozo wa majeraha Old Trafford kwa sasa unapungua, meneja Louis van Gaal alisema Ijumaa. Winga huyo wa Argentina, aliyenunuliwa £59.7 milioni kutoka Real Madrid, ambayo ni rekodi Uingereza, atakosa mechi yake ya tatu mfululizo baada yake kukosa kupona jeraha la misuli ya paja. Mabingwa hao mara 20 wa Uingereza pia watakuwa bila madifenda Luke Shaw na Chris Smalling waliojeruhiwa, sawa na kiungo wa kati Daley Blind. vLakini meneja wa United Van Gaal alibaki mwenye matumaini Ijumaa, akisema mzozo wake wa majeraha utaisha karibuni. Mzozo huo ulikuwa umemkosesha raha mwanzo wa maisha yake Old Trafford, wakati mwingine akiwa bila wachezaji hadi 12 wakati mmoja. 

MAKALA: NI SIMBA AU YANGA ATAKAYECHEKA TAIFA LEO?

Picha
Amisi Tambwe alifunga mara mbili katika muda wa dakika 45 za kipindi cha kwanza katika mchezo wa Nani Mtani Jembe, mwishoni mwa Disemba ,2013 kisha kiungo, Awadh Juma akafunga bao lingine na kutengeneza ushindi wa aina yake kwa timu yao ya Simba SC dhidi ya mahasimu wao wa soka nchini Yanga SC. Emmanuel Okwi alifunga ‘ bao kali’ katika mchezo huo dakika za mwishoni mwa mchezo ambao ulikuwa ni wa kwanza kwake katika timu ya Yanga ambao walimsaini kwa usajili uliozua utata mkubwa kutoka SC Villa ya Uganda.