Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2015

PLUIJM AKIRI YANGA KUBANWA NA STAND UTD

Picha
Licha ya timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 juzi, kocha wa Yanga, Hans van der Pluijm, amesema kuwa wapinzani wao Stand United kutoka Shinyanga waliwazidi uwezo katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Wageni Stand ndiyo walikuwa wa kwanza kuliona lao la Yanga lakini baadaye wenyeji walisawazisha na kuongeza la pili lililodumu hadi mapumziko. Stand walisawazisha mapema kipindi cha pili, kabla ya Yanga kupata penalti iliyowapa ushindi wa 3-2 katika dakika za lalasalama. Akizungumza juzi baada ya mechi hiyo, Pluijm alisema kwamba kikosi chake hakikucheza vizuri, wachezaji hawakuwa na maelewano katika mchezo huo licha ya kushinda.

HATA KAMA KUNA MACHAFUKO, NAKWENDA TU SAUZI- NGASSA

Picha
Winga wa Yanga ya jijini Dar es Salaam, Mrisho Ngasa, amesema kwamba licha ya hali ya machafuko inayoendelea nchini Afrika Kusini ya wazawa dhidi ya wageni, hatasita kwenda huko endapo atapokea mwaliko wa kujiunga na klabu yoyote  itakayomuhitaji. Ngasa ambaye alirejea Yanga akitokea Simba kwa mkopo, anatarajia kumaliza mkataba wake Jangwani mwezi ujao. Ngasa ambaye mwaka jana alikwenda Afrika Kusini kufanya majaribio 'kinyemela', anatajwa kuwa kwenye mipango ya kuhamia Free State Stars ya huko na ndio inayofanya achelewe kusaini mkataba mpya na Yanga.

NNE ZAFUZU NUSU FAINALI ULAYA

Picha
Timu nne zimetinga hatua ya nusu fainali katika ligi ya mabingwa barani Ulaya iliyokamilika hapo jana, baada ya Real Madrid ya Hispania na Juventus ya Uitaliano kufanikiwa kuingia nusu fainali. Wakicheza katika uwanja wao wa nyumbani wa Santiago Bernabeu, Madrid walilazimika kusubiri hadi dakika ya 88, walipopata bao lao la pekee lililotiwa kimia Javier Hernandez almaarufu kama Chicharito,na hivyo kuhitimisha safari ya Atletico Madrid.

Gervinho kukaa nje wiki tatu

Picha
Gervinho   Straika matata wa Roma Gervinho atakaa nje wiki tatu baada ya kuumia misuli ya paja, hilo likiwa pigo kuu kwa matumaini ya klabu hiyo ya Serie A kumaliza nambari mbili msimu huu. Taarifa kutoka kwa klabu hiyo ilisema: "Gervinho alichunguzwa mara kadha na imebainika ana jeraha la ngazi ya kwanza paja lake la kulia. Kuna uwezekano atakaa nje wiki tatu. “Kuanzia kesho ataanza kuponya jeraha.” Gervinho, ambayea meshindwa kufungia vijana hao wa Rudi Garcia ligini tangu Novemba, atakosa mechi zijazo za ligi dhidi ya Napoli, Torino, Atalanta nap engine Inter Milan Aprili 25. Roma wamo nambari mbili Serie A, alama 14 nyuma ya viongozi Juventus lakini alama moja pekee dhdii ya wapinzani wao wa jiji Lazio kukiwa na mechi 10 zilizosalia msimu huu.

Ureno wacharazwa na Cape Verde

Picha
Odair Fortes  Ureno walihangaishwa na wanyonge Cape Verde kwenye mechi ya kirafiki iliyochezwa Jumanne, vijana hao wa visiwa hivyo vya Afrika wakiwalaza 2-0. Ureno, ambao hawakutumia hata mchezaji mmoja kutoka kwa waliolaza Serbia mechi ya kfuuzu kwa Euro 2016 Jumapili waliumbuliwa na mabao mawili ya kipindi cha kwanza ambayo yalifungwa katika kipindi cha dakika sita. Masaibu ya Ureno yalizidishwa na kufukuzwa uwanjani wa Andre Pinto kipindi cha pili. Odair Fortes alifungua ukurasa wa mabao upande wa Cape Verde dakika ya 37 kwa ustadi mkubwa baada ya krosi yake kutoka kulia kuonekana kushika kasi angani na kumbwaga kipa wa Ureno Anthony Lopes. Mkabaji wa kati Gege alifunga la pili kwa kufunga kwa stadi kutoka mlingoti wa mbali kufuatia frikiki iliyochapwa na nahodha wa Cape Verde Heldon ambayo ilihepa miguu mingi kabla ya kumfikia.

BUHARI: ASEMA USHINDI WAKE NI WA KIDEMOKRASIA

Picha
Mshindi wa uchaguzi wa urais nchini Nigeria Muhammadu Buhari anasema kuwa ushindi wake unamaanisha kuwa taifa hilo linafuata mfumo wa kidemokrasi. Buhari alimshinda mpinzani wake Goodluck Jonathan,kwa kura millioni 2 idadi ambayo wachanganuzi wanasema kuwa itazuia harakati zozote za kuanzisha kesi.

MALINZI AKIRI KUVURUNDA

Picha
Rais wa TFF, Jamal Malinzi, amesema panguapangua ya ovyo ya ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu huu imelichafua shirikisho hilo la soka nchini, hivyo wanajipanga kuhakikisha fedheha hiyo haijirudii. Malinzi, kiongozi wa zamani wa Yanga, aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juzi kuwa mara tu baada ya kumalizika kwa msimu huu wa VPL Mei 9, mwaka huu, vyombo vya TFF vitakutana na kupanga ratiba makini ya msimu ujao. "Ratiba ya VPL msimu huu imetia doa. Tulifanya makosa katika michuano ya Kombe la Mapinduzi. Ratiba yetu haikujali michuano hiyo. Msimu ujao tutahakikisha tunakuja na ratiba itakayojali matukio yote ya soka yakiwamo mashindano ya Kombe la Mapinduzi, ratiba ya Taifa Stars na Taifa Stars Maboresho maana programu ya maboresho ni ya kudumu," alisema Malinzi.

WADAU WAMPONDA KOCHA STARS, WADAI BORA YA KIM POULSEN

Picha
Wachambuzi wa soka wamesema timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ haina kiwango cha kuvutia uwanjani na imepoteza mvuto. Wakizungumza baada ya kuishuhudia Taifa Stars ikilazimishwa sare ya bao 1-1 na Malawi katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika Mwanza juzi, walisema wanauona mwisho mbaya wa kocha Mholanzi, Mart Nooij. Kocha Joseph Kanakamfumu aliliambia gazeti hili kuwa Nooij hajaibadilisha Stars na inacheza ili mradi tu tofauti na mtangulizi wake, Kim Poulsen. Kanakamfumu alisema jambo kubwa analokosea Mholanzi huyo ni uteuzi wa kikosi chake, hasa aina ya wachezaji anaowaita kwani wengi wao hawako fiti.