Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Nani yupo nyuma ya mpango wa Mangungu kushambuliwa?

Machapisho ya hivi karibuni

GSM yashinda zabuni ya kutengeneza uwanja wa Yanga SC

Rasmi kampuni ya GSM Tanzania Limited imeshinda tenda ya kujenga Uwanja wa klabu ya Yanga kwa kushirikiana na klabu hiyo. Rais wa klabu ya Yanga Sc, Eng. Hersi Said ndiye Mwenyekiti wa kamati maalum iliyoundwa kusimamia ujenzi wa uwanja huo, huku Wajumbe wa kamati hiyo watakuwa ni Wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji ya Yanga SC. Kamati hiyo itakutana na GSM Tanzania Limited kujadili kuanza kwa mradi huo.

Shafih Dauda aishangaa Simba kutowaheshimu Esperance

Mchambuzi wa soka nchini Shafih Dauda amewaambia mashabiki wa Simba waliomzonga na kumshambulia mwenyekiti wa klabu hiyo Murtaza Mangungu jioni ya leo uwanja wa Mkapa wakati Simba inacheza na Esperance, watamuomba radhi kwani Mangungu ahusiki la lolote kuhusu Simba isipokuwa wakiwajua wahusika watagundua kwamba Mangungu hana kosa lolote. Dauda ameyasema hayo akizungumza na Sports Extra ya Clouds FM ambapo amedai kwamba mashabiki hao wa Simba hawajatumia hekima na pia dharau kwa timu ya Esperance. "Mashabiki wa Simba hawajaiheshimu Esperance kwani ni miongoni mwa timu kubwa na bora barani Afrika, wenzao Yanga jana wameiheshimu Al Ahly na ndio maana sijaona mashabiki wa Yanga wakiijia juu timu yao kwa sare ya 1-1 wakiiua fika Ahly ni timu kubwa, lakini Simba leo heshima haijawekwa kwa Esperance, sare ya 2-2 licha ya kuongoza 2-0 kipindi cha kwanza, mashabiki wametaka kumpiga mwenyekiti wa klabu", alisema Dauda. Shafih Dauda

Azam FC yafufua matumaini ya kutinga robo fainali kombe la Shirikisho Afrika

Timu ya Azam FC usiku huu imepata ushindi kiduchu wa bao 1-0 dhidi ya Nairobi United ya Kenya mchezo wa kombe la Shirikisho Afrika uwanja wa New Amaan Stadium, Zanzibar. Bao pekee lililowapa ushindi Azam FC limefungwa na kiungo mshambuliaji Feisal Salum "Feitoto" dakika ya 11. Kwa matokeo hayo Azam FC imefikisha pointi 6 ikicheza mechi 4 huku ikiwa imefufua matumaini ya kuingia robo fainali.

Andiko la Ahmed Ally linatia simanzi

Umekua msimu mbaya kwetu kwenye michuano ya kimataifa, inauma lakin hatuna budi kukubali kuwa msimu huu umekua mgumu kwetu Kama ambavyo misimu mingine tunafuzu kwenda Robo Fainali na wengine wanashindwa basi msimu imekua zamu yetu kuanguka Hatuna sababu ya kuvurugana wala kutafuta mchawi itoshe kusema msimu huu haukuwa wetu au haikua rizki yetu Tumalizie mechi mbili zilizobaki baada ya hapo tuwekeze nguvu kwenye mashindano ya ndani huku bado tuna nafasi kubwa ya kufanya vizuri Poleni ndugu zangu Wana Simba, Tulichozea kufanya tumeshindwa kufanya safari hii, Tukubali kuwa huu ni msimu mbaya kwetu na hutokea kwa timu yeyote Duniani Asanteni na poleni wale wote waliotoa nguvu zao kuipambania Simba ishinde hii leo, Asanteni wale wote waliokuja Uwanjani hii leo, Tanatambua na kuthamini mchango wenu kwenye kuipambania Simba yetu Itoshe kusema Asante Mungu wewe ndio mpangaji wa yote Hadi wakati mwingine Wanyama, Hakuna kukataa tamaa maisha ya mpira bado yanaendelea

Singida Black Stars yachapwa 2-1 huko Brazzavile

WENYEJI, AS Otohô wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Singida Black Stars katika mchezo wa Kundi C Kombe la Shirikisho Afrika jioni ya leo Uwanja wa Alphonse Massemba-Débat Jijini Brazzaville, Jamhuri ya Kongo. Mabao yote ya Association Sportive Otohô yenye maskani yake mjini Oyo yamefungwa na mshambuliaji chipukizi wa miaka 22, Pomi Sagesse Exaucé Nzaou dakika ya 52 na 80, huku bao pekee la Singida Black Stars likifungwa na mshambuliaji Muivory Coast, Joseph Guédé Gnadou dakika ya 90. Singida Black Stars ilipata pigo la mapema kufuatia kipa wake, Metacha Borniphace Mnata kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 27‎. Kwa matokeo hayo, AS Otohô inafikisha pointi sita na kusogea nafasi ya pili nyuma ya CR Belouizdad yenye pointi tisa, wakati Singida Black Stars inabaki na pointi zake nne sawa na Stellenbosch ya Afrika Kusini kufuatia timu zote kucheza mechi nne. Mchezo mwingine wa Kundi C leo CR Belouizdad imeitandika Stellenbosch 3-0 Uwanja wa Athlone Jijini Cape Town, Afrika Kusi...

Yanga kuwafuata Simba uwanja wa Meja Isamuyo

Huenda mabingwa wa soka Tanzania bara, Yanga SC, wanahamia uwanja wa Meja Isamuyo Mbweni jijini Dar es Salaam baada ya uwanja wao wa KMC Complex kufungiwa na Shirikisho la soka nchini, TFF. Taarifa za ndani zinasema kwamba viongozi wa Yanga SC wamekubaliana wahamie uwanja wa Meja Isamuyo licha kwamba kuna wengine wamependekeza wahamie uwanja wa Uhuru ambao tayari umekamilika. Uwanja wa Uhuru zamani Taifa, ulikuwa unafanyiwa marekebisho, na sasa uwanja huo uko tayari kwa mitanange mbalimbali ya ligi na Yanga inakaribishwa kuutumia uwanja huo ingawa wenyewe wanataka kuwang' ang' ania watani zao Simba kuwafuata uwanja wa Meja Isamuyo