Machapisho

Makonda amteua Leodgal Tenga kamati ya AFCON

Picha
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Christian Makonda amemteua Nahodha wa zamani wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Leodegar Chilla Tenga kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ndani ya Maandalizi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 ambazo Tanzania inaandaa kwa ushirikianona majirani, Kenya na Uganda.

Simba yaendeleza vipigo Sheikh Amri Abeid

Picha
TIMU ya Simba SC imeibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Fountain Gate katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha. Mabao ya Simba SC yamefungwa na kiungo Mzambia, Clatous Chotta Chama dakika ya 45’+7, winga Msenegal Libasse Gueye dakika ya 53 na kiungo mzawa, Shaaban Mgunda aliyejifunga dakika ya 71 wakati akijaribu kuokoa. Kwa matokeo hayo, Simba SC inafikisha pointi 39, ingawa inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi tano na mabingwa watetezi, Yanga SC baada ya timu zote kucheza mechi 18. Kwa upande wao Fountain Gate baada ya kupoteza mchezo wa 10 leo kati ya michezo 18 iliyocheza hadi sasa, mingine minne ikitoaa sare na kushinda minne pia – inabaki na pointi zake 16 nafasi ya 14 katika ligi ya timu 16. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda...

Uwanja wa Yanga wafikia pazuri

Picha
Rais wa klabu ya Yanga SC, Eng Hersi Said ameweka bayana suala la ujenzi wa uwanja wa Yanga SC utakaojengwa Jangwani, umefikia pazuri. "Kwenye ujenzi wa uwanja tumefika kwenye eneo zuri sana. Tunafanya mchakato wetu kwa umakini mkubwa na kwa usahihi. "Tuliwatangaza GSM kuwa washindi wa tenda ya ujenzi wa uwanja. Tayari tumepata mchoro wa awali wa uwanja.  Klabu imeshatoa maoni kuhusu mchoro huo. Jana tumekamilisha michoro yote na gharama za ujenzi” Eng Hersi Said @caamil_88, Rais wa Klabu ya Yanga SC

Muhibu Kanu kuendelea kuwa kocha mkuu Singida Black Stars

Picha
Uongozi wa Klabu ya Singida Black Stars umefikia makubaliano ya kumuajiri aliyekuwa Kocha wa AS Maniema, Papy Kimoto kuwa Meneja Mkuu wa Timu, pamoja na Kapiten Ngoyi Dora kuwa Kocha Msaidizi, wote wakisaini mikataba ya mwaka mmoja na miezi mitatu. Aidha, Muhibu Kanu ataendelea kushika nafasi ya Kocha Mkuu hadi mwisho wa msimu huu, akisimamia kikamilifu majukumu ya kiufundi kwa kushirikiana na safu mpya ya Benchi la Ufundi.

UKRISTO NI CHIMBUKO LA UYAHUDI - 13

Picha
Inaandikwa na Fikiri Salum Ilipoishia  KUHUSU maeneo ambako Wakristo wanapungua ni kwamba kutokana na historia ya kanisa kuwa na mchanganyiko wa mazuri na mabaya, wengine wanahisi kuwa halina maana tena. Endelea Pia Kuna makundi kama Wakomunisti na Wamasoni ambayo yanakusudia kabisa kufuta Ukristo kwa kutangaza kasoro za waumini na viongozi wao, pamoja na kuhimiza watu kwenda kinyume cha maadili. Hali hii inajionyesha hasa pale ambapo waamini wengi, hasa Ulaya, wameacha kwenda kanisani isipokuwa siku ya Krismasi na Pasaka au kwenye harusi na msiba. Pia kutokana na mgawanyiko wa madhehebu kumekuwa na mkanganyiko kuhusu kazi ambazo zinaipasa kanisa la leo. SALA NA IBADA Mafundisho ya Yesu kuhusu sala hayatii maanani taratibu maalum, badala yake yeye alisisitiza msimamo wa ndani wa kumuendea Mungu kwa imani na unyofu kama vitoto vinavyohusiana na baba zao. Ndivyo mwenyewe alivyosali katika roho mtakatifu aliyewaahidia wafuasi atawaongoza badala yake. Kwa msingi huo, katika historia ya kan...

Dkt Mwinyi atembelea mradi wa AFCON mkoa Mjini Magharibi

Picha
Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameutembelea mradi wa Mji wa AFCON Fumba uliopo Mkoa wa Mjini Magharibi. Ziara hiyo imefanyika leo Aprili 14, 2026, akiambatana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Riziki Pembe Juma, pamoja na wadau wa mradi wa AFCON Fumba Zanzibar. Katika ziara hiyo, Rais Dkt. Mwinyi amekagua maeneo mbalimbali ya uwanja huo wa kisasa wa AFCON unaojengwa na kampuni ya ORKUN GROUP ya Uturuki, ambao unaotarajiwa kutumika kwa michuano ya #AFCON2027 itakayofanyika kwa ushirikiano wa nchi tatu za Afrika Mashariki za Kenya, Uganda na Tanzania. Aidha Dkt. Mwinyi ametembelea na kukagua miundombinu inayotarajiwa kujengwa kuzunguka uwanja huo, ikiwemo hospitali, barabara, migahawa, maduka makubwa (mall) pamoja na huduma nyingine muhimu zitakazouzunguka mji huo wa kisasa. Uwanja huo unakadiriwa kuchukua watazamaji elfu 35, ukiwa na viwango vya ubora vinavyokubalika na Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF).

Magori aungana na Simba kula nyama choma Arusha

Picha
Mwenyekiti wa Bodi, Crescentius Magori na Mjumbe wa Bodi, Dr. Seif Muba wamefika hapa katika Simba Nyama Choma Festival hapa Arusha.