Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Yanga na Simba kupigwa New Amaan, Zanzibar- Kamwe

Machapisho ya hivi karibuni

Azam FC chali kombe la Shirikisho Afrika

TIMU ya Azam FC imechapwa mabao 2-0 na wenyeji, Wydad AC katika mchezo wa mwisho wa Kundi B Kombe la Shirikisho Afrika jioni ya leo Uwanja wa Mohammed V Jijini Casablanca nchini Morocco. Mabao ya Wydad Athletics Club yamefungwa na beki Paschal Gaudence Msindo aliyejifunga dakika ya 64‎ na mshambuliaji Mfaransa, Nassi Ouled Bentle dakika ya 90‎’+‎4‎’. Mechi nyingine ya mwisho ya Kundi B Kombe la Shirikisho, AS Maniema Union imeichapa Nairobi United FC mabao 3-0 Uwanjawa TP Mazembe Jijini Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Kwa matokeo hayo Wydad inamaliza kileleni na pointi zake 15, ikifuatiwa na AS Maniema Union yenye pointi 12 na zote zinakwenda Robo Fainali, wakati Azam FC inamaliza na pointi tisa mbele ya Nairobi United ambayo imefungwa mechi zote na zote safari yao inaishia hapa. Wakati huo huo timu ya Singida Black Stars nayo imeilazimisha sare tasa 0-0 dhidi ya Stellenbosch ya Afrika Kusini katika mchezo wa kombe la Shirikisho Afrika 

Yanga fungu la kukosa, yatupwa nje Ligi ya mabingwa Afrika

NDOTO za Yanga SC kwenda Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika zimeyeyuka leo licha ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya JS Kabylie katika mchezo wa mwisho wa Kundi B usiku huu Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Yanga imezidiwa kete na AS FAR Rabat ya Morocco iliyomaliza na pointi tisa katika nafasi ya pili ya Kundi B, moja zaidi ya Yanga baada ya sare ya bila mabao na wenyeji, Al Ahly usiku huu Uwanja wa Cairo International Jijini Cairo, Misri. Mabao ya Yanga katika mchezo wa leo yamefungwa na mshambuliaji Muangola, Laurindo Dilson Maria Aurélio ‘Depu’ la kwanza kwa penalti dakika ya 36 na la pili dakika ya 63, kabla ya beki Mkongo Chadrack Issaka Boka kufunga la tatu dakika ya 65. Baada ya matokeo hayo, Al Ahly inamaliza kileleni mwa Kundi C na pointi zake 10, ikifuatiwa na AS FAR Rabat tisa na Yanga nane — wakati JS Kabylie inamaliza mkiani na pointi zake tatu.

Simba ya msimu ujao itafika nusu fainali

Uongozi wa klabu ya Simba SC umejidhatiti kwamba msimu ujao lazima kikosi chao kirejee kimataifa na kitafika hatua ya robo fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika na ikiwezekana kitafika nusu fainali au fainali yenyewe. Hayo yote yametokana na mabadiliko waliyoyafanya msimu huu hasa katika dirisha dogo baada ya kufanya sajili nzuri, uongozi huo kwa nyakati tofauti wameridhishwa na kikosi chao kilichocheza mechi zote za mzunguko wa pili wa hatua ya makundi Ligi ya mabingwa Afrika. Kuanzia mchezo marudiano dhidi ya Esperance uliomalizika kwa sare ya 2-2 uwanja wa Mkapa na ule dhidi ya Petro Luanda ulioisha kwa sare ya 1-1 mjini Luanda na huu wa Jumamosi iliyopita Simba ikishinda 1-0 uwanja wa Mkapa. Simba imeambulia pointi 5 hivyo ni hatua nzuri kwao tofauti na walivyoanza ambapo walipoteza mechi 3 mfululizo, pia uongozi huo wa Simba umeridhishwa na benchi lao la ufundi linaloongozwa na Steve Barker na pia wachezaji wao wapya waliowasajili kwenye dirisha dogo

Wananchi pekee wanaosubiriwa kutinga robo fainali leo

Meneja Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Shaban Kamwe anasema katika orodha ya timu saba ambazo tayari zimefuzu robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), ni Wananchi pekee ndio wanaosubiriwa kukamilisha ile idadi ya timu nane ambazo zinatakiwa kwenye hatua hiyo. Yanga leo itakuwa nyumbani kucheza mechi ya mwisho ya hatua ya makundi saa 1:00 usiku

Tunajenga uwanja wa kucheza robo fainali Ligi ya mabingwa Afrika - Injinia Hersi

“Tumewasilisha kwa GSM mahitaji uwanja tunaohitaji. Tunatambua yapo madaraja manne ya viwango vya viwanja vya CAF. Daraja la tatu ni uwanja ambao unaweza kuchezewa mpaka hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa Afrika. Daraja la nne linaweza kuandaa mpaka hatua ya fainali. Tunalenga kuwa kati ya daraja la tatu na la nne la ubora wa viwanja. Tunahitaji uwanja bora wa kisasa ambayo utamudu mahitaji yote ya kitaifa na kimataifa” alisema Hersi Ally Said na kuendelea. “Tunaenda kujenga uwanja ambao sio tu unahudumu mpira wa miguu pekee bali ni mradi ambao utakwenda kubeba majukumu mengine ya kijamii. Uwanja huu utakuwa na uwezo wa kutumika kwa ajili hafla na shughuli mbalimbali. Nawahakikisha tunakwenda kujenga uwanja ambayo unaakisi mandhari ya ubunifu utakao mudu mahitaji mbalimbali ya kijamii, sanaa, burudani na michezo” Hersi Ally Said alimaliza

Simba yapata ushindi wake wa kwanza Ligi ya mabingwa Afrika

Timu ya Simba SC ya Tanzania usiku huu imepata ushindi wake wa kwanza kwenye michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika hatua ya makundi, baada ya kuilaza Stade Malien ya Mali bao 1-0 uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam. Goli pekee la ushindi limefungwa na kiungo mshambuliaji Anicet Oura dakika ya pili ya mchezo, ushindi ambao unaifanya Simba kufikisha pointi 5 lakini ikisalia nafasi ya mwisho. Wakati huo huo timu ya Esperance inaungana na Stade Malien baada ya kushinda mabao 2-0 dhidi ya Petro de Luanda na kufikisha pointi 9 huku Malien licha ya kufungwa imefikisha pointi 11 na kukwea nafasi ya kwanza.