Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

AFCON 2027 itapigwa hapa hapa Tanzania, Kenya na Uganda na si vinginevyo- Motsepe

Machapisho ya hivi karibuni

JKT Tanzania yashikwa shati na Coastal Union

TIMU ya JKT Tanzania imelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Meja Jenerali Charles Isamuhyo, Mbweni, Dar es Salaam. Mshambuliaji Valentino Mashaka Kusengama alianza kuifungia JKT Tanzania kwa penalti dakika ya tatu, kabla ya winga mkongwe Shiza Ramadhani Kichuya kuisawazishia Coastal Union dakika ya 13. Kwa matokeo hayo, JKT Tanzania inafikisha pointi 28 katika mchezo wa 16 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu, wakati Coastal Union imefikisha pointi 15 katika mchezo wa 15 ingawa inabaki nafasi ya tisa kwenye ligi ya timu 16.

Mchambuzi Crown amjibu Ahmed Ally kuhusu Mpanzu

Kisipika punguza maneno mengi subiri muda utaongea,mimi ni mwandishi ambe nafanya uchunguzi kabla ya kuzungumza….nakumbuka hata kwenye issue ya Chama ulisema vile kama unavyosema leo kwa Mpanzu.. Hans Raphael leo amejiwa juu na msemaji wa Simba SC, Ahmed Ally "Semaji la CAF" kumjia juu Hans Raphael akishangaa maneno ya mchambuzi huyo wa Crown FM kudai kwamba mchezaji Elie Mpanzu licha kwamba anaichezea Simba lakini mapenzi yake yapo kwa Yanga. Hata hivyo mchambuzi huyo kupitia ukurasa wa facebook, amemjibu akiandika maneno hayo katika utangulizi wa habari hizi. Elie Mpanzu anaichezea Simba lakini mapenzi yake yapo kwa Yanga

Walter Bwalya naye atimkia Libya

Mshambuliaji wa kimataifa wa DR Congo Walter Bwalya, amejiunga na klabu ya Al-Qadisiyah Bani Walid ya Libya kama mchezaji huru. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Nkana pamoja na Al Ahly SC anamerejea Afrika Kaskazini baada ya kuwa na kipindi kifupi katika klabu ya Cape Town City FC ya Afrika Kusini .

Semaji la CAF amjia juu mchambuzi Crown FM kisa Mpanzu

MENEJA Habari wa Simba SC, Ahmed Ally, ameshangazwa na kauli ya mchambuzi Hans Raphael aliyedai kuwa Elie Mpanzu ana mapenzi na Yanga SC licha ya kucheza Simba. “Nilimsikia mchambuzi wenu akisema mchezaji wetu anacheza tu Simba, lakini ana mapenzi na Yanga. Unawezaje kuthibitisha hilo?” Ahmed amesema kauli hiyo si sahihi na imemkosea mchezaji, hasa kwa kipindi anachopitia. “Amemkosea sana mchezaji, ile sio sentensi ya kuzungumza hadharani. Mpanzu ametoka kufiwa na mtoto wake hivi karibuni, sio rahisi kwake. Anapitia nyakati ngumu.”

Yanga wamkataa refa wa JS Kabylie

Yanga wamewasilisha barua kwa Shirikisho la mpira wa miguu Afrika CAF kuomba kubadilishiwa mwamuzi atakaechezesha mchezo wa Ligi ya mabingwa dhidi ya JS Kabylie katika uwanja wa New Aman Complex Zanzibar.. Mwamuzi Jaque Ndala( 34) kutoka DR Congo ndiyo mwamuzi aliyeteuliwa na CAF kusimamia mchezo huo. Ikumbukwe tu huyu ndiyo mwamuzi aliyewachinja Tanzania dhidi Morocco katika michuano ya AFCON yaliyofanyika nchini Morocco msimu huu .! Mchezo wa Yanga na JS Kabylie utatoa taarifa kwa umma kuwa Yanga amesonga robo fainali au amesalia Ligi Kuu NBC.. Kama ombi lao litajibiwa basi furaha ya wananchi itarejea kutokana na Jaque Ndala kutokuwa na Imani naye.

Dodoma Jiji yaishusha Simba

Timu ya Dodoma Jiji imeendelea kutakata kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania bara inayodhaminiwa na benki ya NBC, baada ya usiku huu kuilaza TRA United mabao 3-0. Kwa matokeo hayo Dodoma Jiji iliyokuwa nyumbani, imeishusha Simba kwenye nafasi ya sita ikifikisha pointi 20 huku Simba ikiangulia nafasi ya saba na pointi 19. Mabao ya Dodoma Jiji yamefungwa na Faraji Kayanda dakika ya 15, Gadiel Michael dakika ya 40 na William Edgar dakika ya 55. Edgar amekuwa na mwendelezo mzuri wa kufunga mabao tangu alipoanza kufanya hivyo dhidi ya Yanga na kupelekea kupewa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Januari wa Ligi Kuu bara.