Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Viongozi Bodi ya Ligi Tanzania na Rwanda zaenda kujifunza uendeshaji Yanga

Machapisho ya hivi karibuni

TFF yavifungulia viwanja vya Sokoine na Ali Hassan Mwinyi

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imevifungulia viwanja vya Sokoine Mbeya pamoja na Ali Hassan Mwinyi, Tabora kutumika kwa michezo ya Ligi baada ya kufanya marekebisho yaliyokidhi vigezo vya kikanuni na sheria za mpira wa miguu. Viwanja vyote vipo tayari kutumika kwenye mechi zijazo za Ligi Kuu ya NBC. Aidha, TFF inaendelea kuzikumbusha klabu kuendelea kuboresha na kutunza miundombinu ya viwanja vyao vya nyumbani ili michezo ya Ligi ichezwe kwenye viwanja bora vinavyosaidia kuongeza ushindani na thamani ya Ligi.

Simba kususia dabi

Uongozi wa Simba SC umeiandikia barua Bodi ya Ligi (TPLB) kutaka kujua kwanini taarifa ya kuhamisha uwanja kutoka Benjamin Mkapa kwenda Amaan Complex ilitolewa kwanza na Afisa Habari wa Yanga SC, Ali Kamwe badala ya Bodi ya Ligi TPLB na Bodi ikaja kutangaza siku yake ya pili ya Februari 16, 2026 baada ya Ali Kamwe kutangazwa jana yake Februari 15, 2026. Katika barua hiyo pia Simba Sports Club imehoji kanuni ipi imetumika kuhamisha uwanja maana ilitakiwa taarifa ya kuhamishwa kwa uwanja itoke kabla ya siku 21 kama kanuni inavyosema, taarifa ya kuhamishwa uwanja ilipaswa kutoka siku 21 kabla ya siku ya mechi husika.

SAJILI ZA GUEYE NA OURA ZINAWEZA KUWALIPA SIMBA

Na Prince Hoza Matua DIRISHA dogo la Januari mwaka huu, Simba SC imefanya sajili mpya za wachezaji takribani saba ambazo zinalenga kuibadili timu hiyo katika mashindano mbalimbali inayoshiriki hapa nchini. Miongoni mwa mashindano ambayo Simba inashiriki kikamilifu msimu huu ni pamoja na michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika ambapo timu hiyo ilikuwa inamalizia mechi zake kadhaa za hatua ya makundi ambapo msimu huu Simba iliangukia pua. Wekundu hao wa Msimbazi, hawakuwa na msimu mzuri baada ya kupoteza mechi tatu mfululizo, Simba iliyopangwa na timu za Esperance ya Tunisia, Petro de Luanda ya Angola na Stade Malien ya Mali. Katika mechi za mzunguko wa kwanza, Simba ilijikuta inafungwa mechi zote, ikifungwa 1-0 na Petro de Luanda, 1-0 na Esperance na 2-1 na Stade Malien. Wekundu hao wakaamua kufanya usajili mwingine baada ya ule wa Agosti mwaka jana kushindwa na kuleta mabadiliko, Simba imefanya usajili Ili angalau ifufue matumaini yake ya kutinga robo fainali kama ilivyozoea kufanya hivyo ...

Simba nilifuata kazi tu na si ushabiki- Haji Manara

Msemaji wa zamani wa klabu za Simba SC na Young Africans SC ambaye kwa sasa ni Diwani wa Kata ya Kariakoo Ndugu Haji S Manara amesema kwa kipindi alichoitumikia klabu ya Simba kama Msemaji wa timu hiyo hakuwa na ushabiki zaidi ya kazi. Manara ameyasema hayo wakati wa mahojiano maalum na kituo cha Crown FM ambapo amesema, "Yaani Mimi sio Yanga wa kubabaisha, Toka nazaliwa. Simba nlienda sababu ya kazi, hapa nina kadi za wana CCM wenzangu lakini nina kadi ya Young Africans" Alisema Manara akiongeza kuwa mashabiki wa Simba awali waliamini kuwa ni shabiki wa timu yao. "Nina bahati moja, watu wa Simba wakati sijawa msemaji wa Simba, waliamini mimi ni mshabiki wao. Hali kadhalika na watu wa Yanga. Kabla sijawa msemaji wa Simba wala Yanga, walikuwa wanaamini mimi ni mtu wao kwasababu ya taaluma yangu" Alisema Manara akielezea taaluma ya baadhi ya waandishi wanaoonyesha mapenzi yao kwenye timu. "Mi niko mwandishi ulikuwa hunikuti nafanya uchawa wa baadhi ya waandishi, ...

TFF yaziingiza vitani Yanga na Simba

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeziingiza kwenye ushindani mkali kampuni za michezo ya kubashiri baada ya kutangaza rasmi zabuni ya haki ya kubashiri mchezo wa watani wa jadi wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kati ya Yanga na Simba. Mchezo huo unaotarajiwa kuvuta hisia za mashabiki wengi umepangwa kuchezwa Machi Mosi katika Uwanja wa Amaan, Zanzibar, na tayari umeanza kuonekana kama fursa muhimu ya kibiashara kwa sekta ya michezo ya kubashiri. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Cliford Ndimbo, shirikisho limesema kuwa haki zote za kubashiri michezo ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara ni mali ya TFF pamoja na washirika wake waliotambuliwa kisheria. TFF imeeleza wazi kuwa kampuni yoyote ya kubashiri itakayojihusisha na kubashiri mchezo huo au michezo mingine ya ligi bila kuwa mshirika halali wa shirikisho hilo itakuwa imekiuka taratibu na sheria zilizopo. Katika taarifa hiyo, shirikisho limetoa onyo kali kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi...

Pedro humwambii kitu kwa Boka

Kwa hali jinsk ilivyo inaonekana wazi kocha mkuu wa Yanga SC Pedro Goncalves raia wa Ureno ameonyesha wazi wazi kuridhishwa na uchezaji wa beki wa kushoto wa klabu hiyo Chadrack Boka na amekuwa akimpanga kwenye baadhi ya mechi za timu hiyo. Ingawa wapenzi na mashabiki wa timu hiyo wanampenda sana beki wao mwingine Mohamed Hussein "Tshabalala" na wamekuwa akishinikiza aanzishwe kwenye kikosi chao, lakini Pedro amekuwa akimpanga Boka kwakuwa mapenzi yake yapo kwa beki huyo raia wa DR Congo. Yanga ilikuwa na kocha mkuu aitwaye Roman Folz ambaye alipoanza kuinoa Yanga alikuta timu ina kikosi kilichoenea viungo mahiri akiwemo Duke Abuye ambaye alikuwa panga pangua, lakini kocha huyo alianza kumuamini Aziz Andabwile na akawa kwenye kikosi cha kwanza. Mashabiki wa Yanga walianza kulalama wakitaka Andabwile akae benchi huku Duke Abuye pamoja na kiungo mpya Mousa Balla Conte waanze, lakini Folz humwambii kitu kwa Andabwile hivyo ndivyo kwa Pedro kumwamini Boka.