Machapisho

Lupini Mawuku ajiunga Azam FC

Picha
KLABU ya Azam FC imemtambulisha beki wa kati, Lupini Mawuku Dieumerci (20) kutoka AS Maniema Union ya kwao, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Anakuwa mchezaji mpya wa tatu pamoja na beki mwingine, Henri Braham Stanic Mbelgiji mwenye asili ya DRC kutoka Stellenbosch FC ya Afrika Kusini. Mwingine ni winga Muivory Coast, Kipré Tiagori Emmanuel Junior Zunon ‘Kipre Junior’ aliyejiunga tena na Azam FC akitokea MC Algiers ya Algeria. Kipre Junior amerejea Azam FC ambako awali alicheza kuanzia msimu wa 2022-2023 akitokea SOL FC d’Abobo ya kwao, Ivory Coast hadi 2024-2025 alipohamia MC Algiers.

Henoc Molia straika mpya Azam FC

Picha
Azam FC imefikia makubaliano na St Eloi Lupopo ya kumsajili mshambuliaji Henoc Molia (22) kwaajili ya kuitumikia klabu hiyo kwa msimu ujao wa 2026-27. Henoc Molia amesajiliwa kwa kuchukua nafasi ya Bola Kitambala aliyeondoka klabuni hapo na Henoc Molia ni pendekezo la kocha wao Florent Ibenge.

Yanga yakamilisha usajili wa straika wa Mashujaa

Picha
Jioni ya leo Yanga wamekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Mashujaa,Raia wa Tanzania,Hussein Juma Mihambo (19). Hussein Juma Mihambo amesinya mkataba wa miaka minne Yanga. Yanga wametoa tsh 200m kumpata namba 9 huyo. Hussein Juma Mihambo ni Balaa jipya Jangwani.

Azam FC inasajili kibingwa

Picha
Azam FC imekamilisha usajili wa beki wa kati Lupini Dieumerci (20) kutoka AS Maniema Union kwaajili ya msimu ujao! Kila kitu kimekamilika na atatambulisha hivi karibuni na Matajiri wa Chamazi na atachukua nafasi ya Yoro Diaby waliyeachana nae.

Betway yaishikisha Simba milioni 78 za ubingwa CRDB

Picha
KLABU ya Simba SC imepewa Bakhshishi ya Sh. Milioni 78.5 na Wadhamini wao, Kampuni ya Betway kwa kutwaa Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB.

Polisi Tanzania yapanda Ligi Kuu

Picha
TIMU ya Polisi Tanzania imefanikiwa kurejea Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara licha ya kufungwa 1-0 na wenyeji, Tanzania Prisons bao la Neva Kapoma dakika ya 86 jioni ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Polisi Tanzania inanufaika na ushindi wa 4-0 kwenye mchezo wa kwanza wa Mchujo wa mwisho wa kuwania kucheza Ligi Kuu Julai 12 Uwanjan wa Chuo cha Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, mabao yake yakifungwa na Juhudi Philemon kwa penalti dakika ya sita, Tariq Seif dakika ya 46, Tatizo Shem dakika ya 54 na Emanuel Mpuka kwa penalti pia dakika ya 73. Tanzania Prisons ilifikia kwenye mchujo huo baada ya kufungwa na Mbeya City kwa jumla ya mabao 2-0 katika mchujo wa awali wa timu za igi Kuu tupu – wakati Polisi Tanzania iliitoa Mbeya Kwanza kwa jumla ya mabao 7-1 katika mchujo wa timu za Champonship tupu. Kwa mujibu wa kanuni za Ligi Kuu inayoshirikisha timu 16, baada ya timu mbili za mwisho kuteremka, zinazofuatia katika nafasi ya 13 na 14 humenyana katika michezo miwili ya nyumbani na ug...

Simba yamnasa nyota wa Taifa Stars

Picha
Klabu ya Simba Sports Club imekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji na winga wa kimataifa wa Tanzania, Tarryn Allarakhia, baada ya kumsajili kama mchezaji huru (Free Agent), hatua inayotajwa kuwa sehemu ya mkakati wa klabu hiyo kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu mpya wa mashindano ya ndani na kimataifa. Allarakhia, ambaye alizaliwa jijini London nchini England lakini anaitumikia Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, anajiunga na Simba akiwa na uzoefu mkubwa wa kucheza katika soka la Uingereza. Katika safari yake ya soka amewahi kuzichezea klabu mbalimbali zikiwemo Aveley, Maldon & Tiptree, Colchester United, Crawley Town, Woking, Wealdstone pamoja na Rochdale, ambapo alijijengea sifa kutokana na uwezo wake wa kucheza nafasi zaidi ya moja katika eneo la ushambuliaji. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 ana uwezo wa kucheza kama winga wa kushoto, winga wa kulia pamoja na kiungo mshambuliaji. Kasi yake, ubunifu wa kutengeneza nafasi, uwezo wa kupiga chenga na kutoa pasi za ...