Machapisho

Raja Casablanca yanasa kiungo wa Yanga

Picha
Klabu ya Raja Casablanca inafikiria kumrudisha kiungo wao Moussa Balla Conte katika klabu yake ya Young Africans SC baada ya kuwatumikia kwa mkopo! Raja AC hawaridhishwi na kiwango chake na atakutana na Fadlu Davids ikiwa atamalizana na Young Africans SC kwa makubaliano ya mwisho pia Raja AC wanatarajia kuwasiliana na Young Africans SC ili kuwapa taarifa kuwa hawatamuongezea mkataba wa muda mrefu kiungo huyo.

Ajitokeza kugombea na Injinia, Yanga

Picha
Mfanyabiashara mkubwa nchini katika sekta ya simu, Zahoro Matelephone, ameripotiwa kuchukua fomu katika makao makuu ya Klabu ya Yanga kwa ajili ya kuwania nafasi ya ujumbe kwenye uongozi wa klabu hiyo. Hatua hiyo inaongeza ushindani katika mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa Yanga, huku wadau na mashabiki wakifuatilia kwa karibu majina yanayojitokeza kuwania nafasi mbalimbali. Iwapo atafanikiwa kuchaguliwa, Zahoro atakuwa sehemu ya uongozi utakaosimamia maendeleo ya klabu kuelekea misimu ijayo.

Top scorer wa Simba Queens atimka

Picha
Mshambuliaji wa Simba Queens, Jetrix Shikangwa, ameondoka rasmi klabuni hapo na kujiunga na FC Masar ya Misri. Jetrix anaondoka baada ya msimu bora, akifunga mabao 16 na kuwa mmoja wa nyota walioisaidia Simba Queens kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania. Anatarajiwa kuungana na Mtanzania, Hasnath Ubamba, anayekipiga FC Masar.

Seleman Mwalimu atabaki Simba

Picha
Kocha Steve Barker amemtaja Selemani Mwalimu kuwa mmoja wa washambuliaji anaotaka kubaki nao Simba SC kuelekea msimu wa 2026/27 Mkataba wa sasa wa mkopo wa Selemani Mwalimu na Simba SC hauna kipengele chochote cha kuongeza muda wa mkopo au kumnunua moja kwa moja Hii ina maana kuwa Mwalimu anatakiwa kurejea Wydad AC mara baada ya mkopo wake kumalizika, then Simba SC na Wydad AC wafungue mazungumzo mapya(kama wanahitaji kubaki naye) Taarifa zinaeleza kuwa Wydad AC wako tayari kumruhusu Mwalimu aondoke kwa uhamisho wa moja kwa moja(kuuzwa), na si kwa mkopo mwingine Hata hivyo, ada inayotarajiwa kuhitajika inaweza kuwa changamoto kwa Simba SC Licha ya kuvutiwa na vilabu kadhaa, Selemani Mwalimu ameipa Simba SC kipaumbele na yuko tayari kusubiri uamuzi wa Simba sc kabla ya kusikiliza ofa nyingine Kwa sasa, mchezaji anaitaka Simba kwanza... lakini uamuzi wa mwisho utategemea kama Simba SC na Wydad AC watafikiana

Barker amng' ang' ania Ibraheem Jabaar

Picha
Kocha mkuu wa Simba Steve Barker,ana-push sana Simba wakamilishe usajili wa kiungo wa Stellenbosch raia wa Nigeria, Ibraheem Jabaar (23). Personal terms Siyo ishu kwani mchezaji huyo yuko huru. Kocha anamtaka Jaabar kwani anamfahamu vizuri ila viongozi wa Simba wanamtaka namba 10 wa Chile,Diego Mauricio ambae nae ni mchezaji huru. Simba wanamuona Diego ni Top Top Number 10 ambae atakuju kumpa changamoto Chota Chama….na Simba wako tayari kumlipa mshahara wa $20,000 (52,646,460) kila mwezi. Wiki ijayo itakuwa muhimu sana kufanya maamuzi ya nani aje kati ya Diego Mauricio au Jabaar.

Azam FC yamkomalia Iddi Nado kwenda Yanga

Picha
Azam FC imeanza mazungumzo na kiungo wake Nado kwa lengo la kuongeza mkataba wake, kufuatia kiwango bora alichoonyesha tangu aliporejea kikosini mwezi Julai 2025. Nado, ambaye alijiunga na Azam FC mwaka 2019 akitokea Mbeya City, ameendelea kuwa mmoja wa wachezaji muhimu ndani ya kikosi hicho kutokana na mchango wake mkubwa katika safu ya kiungo. Taarifa zinaeleza kuwa hatua ya Azam FC kumuita mezani inalenga kuhakikisha inamdumisha nyota huyo, hasa baada ya kuvutia macho ya watani wa jadi, Yanga SC na Simba SC, ambao wanatajwa kuwa na nia ya kupata saini yake. Hatma ya Nado sasa inategemewa kuamuliwa na mazungumzo kati yake na Azam FC huku dirisha la usajili likiendelea kushika kasi. 

Rasmi, Yanga wanamleta Fadlu

Picha
Inaripotiwa nchini Afrika Kusini mchana huu kwamba, Yanga Afrika wameweka ofa mezani na wako kwenye mazungumzo kumsaini Kocha Fadlu Davids kama kocha wake mpya mkuu kuelekea msimu ujao. Fadlu Davids aliitumikia Simba Sports msimu huu, hapa Tanzania kabla ya kutimkia Raja Club huko Morocco ambako baada ya matokeo mabovu dhdi ya vilabu vikubwa na kuukosa Ubingwa wa Botola Pro alifutwa kazi jijjni Casablanca wiki chache zilizopita.