Milio ya risasi ilisikika nyumbani kwa Rihanna huko Beverly Hills, California, Polisi wakisema kuwa hakuna aliyejeruhiwa katika tukio hilo. Polisi wanasema mshukiwa, Mwanamke mwenye umri wa miaka 30, alisimama mbele ya Nyumba kutoka kwenye gari na kufyatua risasi saba kabla ya kukimbia. Kwa mujibu wa Polisi Mwanamke huyo ambaye bado hajatajwa utambulisho wake alikamatwa na Maafisa usalama Kilomita 12 kutoka kwenye makazi ya mwimbaji huyo. Mnamo Septemba (9), Rihanna alijifungua mtoto wake wa tatu, binti, na mpenzi wake A$AP Rocky. Wanandoa hao tayari wana watoto wengine wawili wa kiume, Riot na RZA. Mzaliwa wa Barbados, Rihanna, ambaye jina lake halisi ni Robyn Fenty, alipata umaarufu miaka ya 2000 kwa vibao kama vile Pon de Replay na Umbrella.