Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

CECAFA yapata Rais mpya

Machapisho ya hivi karibuni

Salum Mayanga akalia kuti klabu Mashujaa FC

Mashujaa FC inayonolewa na Kocha Salum Mayanga haijashinda mchezo wowote kwenye michezo 5 ya karibuni ya Ligi Kuu bara. Kwa mwenendo huo wa kocha Mayanga, kwa vyovyote anaataharisha nafasi yake kwani muda wowote uongozi wa Mashujaa FC unaweza kusitisha mkataba wake. Mayanga anaheshimika sana kwakuwa amewahi kufundisha timu ya taifa, Taifa Stars, lakini pia amewahi kuzifundisha Mtibwa Sugar na Tanzania Prisons. Rekodi zake za hivi karibuni katika mechi 5 zilizopita ni kama ifuatavyo. 0-0 V Dodoma Jiji sare 0-0 V Coastal Union sare 6-0 V Yanga SC kufungwa 2-0 V Simba SC kufungwa 1-0 V KMC kufungwa, ni dalili mbaya sana kwa upande wake. Pia hawajafunga goli lolote kwenye michezo hiyo 5

JKT Tanzania yaendelea kukaa kileleni Ligi Kuu bara

WENYEJI, JKT Tanzania wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Mbweni Jijini Dar es Salaam. Bao pekee la JKT Tanzania katika mchezo huo limefungwa na beki Laurian Omar Makame aliyeiadhibu timu yake ya zamani dakika ya 40. Kwa ushindi huo, JKT Tanzania inafikisha pointi 27 katika mchezo wa 15 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu, wakati Mashujaa inabaki na pointi zake 14 za mechi 14 nafasi ya tisa kwenye ligi ya timu 16. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.

Stephanie Aziz Ki anarudi tena Jangwani

Kiungo mshambuliaji raia wa Burkina Faso, Stephanie Aziz Ki, huenda akarejea tena katika klabu yake ya zamani ya Yanga SC kufuatia taarifa zinazozagaa kwamba Yanga wanamrudisha. Habari za uhakika kabisa kutoka viunga vya Jangwani, Aziz Ki aliyeuzwa kwa klabu ya Wydad Athletic ya Morocco kisha na wao kumuuza Al Ittihad ya Libya, uongozi wa Yanga umeona biashara ya mchezaji huyo haikuwapa amani kwani pengo lake linaonekana dhahiri. Hivyo kwenye usajili wa dirisha kubwa la Agosti mwaka huu, jina la Aziz Ki litakuwa miongoni mwa wachezaji wapya wa mabingwa hao wa Tanzania bara.

William Edgar awa mchezaji bora Ligi Kuu bara mwezi Januari

MSHAMBULIAJI wa Dodoma Jiji FC, William Edgar amechaguliwa Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara mwezi Januari 2026, huku Mreno Pedro Valdemar Soares Gonçalves wa Yanga SC akichaguliwa Kocha Bora wa mwezi huo.

Samatta afikisha siku 343 bila kufumania nyavu

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania na klabu ya Le Havre, Mbwana Samatta ameendelea kuandamwa na ukame wa mabao akiwa na siku 343 bila kuzifumania nyavu tangu alipofunga kwa mara ya mwisho mnamo March 2 mwaka jana kwenye mchezo wa Greek Super League wakati akiitumikia PAOK . Takwimu zake za klabu na timu ya taifa tangu alipofunga kwa mara ya mwisho mnamo March 2, 2025. 1303 - Minutes 23 - Games played 00 - Goals 01 - Assists Kati ya washambuliaji wa kati waliopiga mashuti 20+ yanayojumuisha yaliyolenga goli na yasiyo lenga goli katika ligi kuu ya Ufaransa (Ligue 1) msimu huu, ni Samatta pekee ambaye bado hajafunga bao mpaka sasa . Samatta akiwa na Le Havre katika Ligue 1 msimu huu hadi sasa . ◉ 14 - Games ◉ 43 - Touches in opp. box ◉ 21 - Shots ◉ 07 - Shots on target ◉ 00 - Goals ◉ 00 - Assists

Droo ya kombe la CRDB hadharani, Yanga kuanza na mabingwa wa zamani bara

DROO ya Hatua ya Timu 64 Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB imefanyika leo Studio za Azam TV, Tabata TIOT Jijini Dar es Salaam na vigogo wote, Simba na Yanga wataanzia nyumbani dhidi ya timu za madaraja ya chini. Mabingwa watetezi, Yanga watacheza na Cosmopolitan, zote za Dar es Salaam, Simba Sports Club na Greenland ya Kagera, Azam FC na Endument ya Kilimanjaro na Singida Black Stars dhidi ya Copco FC ya Mwanza. MECHI ZOTE ZA 64 BORA Tanzania Prisons V Moro Kids Mbeya City V Bishara United Coastal Union V Nyumbu FC TRA United V Rhino Rangers JKT Tanzania V Pan Africa Mtibwa Sugar V IAA SC Fountain Gate V Mapinduzi FC Namungo V Magnet FC Pamba Jiji V Alliance FC Dodoma Jiji V Kilimanjaro Wonders KMC FC V Bandari Tanzania Mashujaa FC V NKIM FC