Machapisho

Kipre Jr arejea Azam FC

Picha
Azam Fc wamekamilisha usajili wa winga wa Ivory Coast,Kipre Zunon Jr kutoka MC alger Kwenye mauziano hayo MC wameweka kipengele cha “Sell on” 30% kama Azam watamuuza Kipre basi 30% ya pesa itakwenda MC Alger.

Job kulipua bomu

Picha
Beki wa kati na nahodha msaidizi wa Young Africans SC, Dickson Job, ameibua mjadala mkubwa baada ya kuchapisha ujumbe kwenye ukurasa wake rasmi wa Instagram (@jobdick05) akidokeza kuwa atazungumza hadharani kuhusu jambo alilolieleza kuwa ni muhimu. Kuna mtu nna ujumbe wake, Job aliandika:"Kama Nahodha, jukumu langu ni timu. Nidhamu ni bora kuliko kipaji. Hivyo nitazungumza kesho (Jumatatu). Sio busara mchezaji kurubuniwa." Kauli hiyo imeibua hisia na maswali mengi miongoni mwa mashabiki wa Yanga na wadau wa soka, huku wengi wakisubiri kwa hamu kufahamu kile ambacho nahodha huyo msaidizi amesema atakiweka hadharani. Uj umbe huo tayari umeanza kusambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii, ukiibua mijadala kuhusu kile kinachoweza kuwa kiini cha kauli yake.

Yanga, Sportpesa wateta

Picha
Mapema asubuhi ya leo, Uongozi wa YANGA SC ukiongozwa na Rais Eng. Hersi Said ulifanya kikao na Mdhamini Mkuu wa Klabu yetu, Kampuni ya SportPesa na kujadili mambo mbalimbali ya kimkataba na mahusiano ya pande zote mbili. Upande wa Kampuni ya SportPesa uliwakilishwa na Tarimba Abbas, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Allan McTavish, Mkuu wa Kimataifa wa Udhamini na Sabrina Msuya ambaye ni Mshauri wa Udhamini Mahusiano na Serikali.

Simba yapindua meza

Picha
Simba wanataka kupindua meza kwa Yona Amos (27). Yona ni mcheza huru baada ya kumalizana na Pamba Jiji. Mwezi uliopita Yona alikubaliana kila kitu (Sign on fee,mshahara) na Singida Black stars ila dili hilo limechelewa kukamilika coz Singida bado hawajaingiza hela kwenye Account ya Yona. Baada ya Simba kugundua hilo wameingilia kati na sasa wanataka kupita na kipa huyo. Mazungumzo ya Simba na Yona yanaendelea.

Prince Dube atambulishwa Zimbabwe

Picha
Mshambuliaji wa kimataifa wa Zimbabwe, Prince Dube, ametambulishwa rasmi kama mchezaji mpya wa Hard Rock FC ya nchini Zimbabwe, akianza rasmi safari mpya ya soka katika taifa lake. Kwa mujibu wa taarifa hizo, Dube ameamua kujiunga na Hard Rock FC licha ya kuripotiwa kuvutiwa na klabu kadhaa, zikiwemo Young Africans SC (Yanga), Al Ahly Benghazi ya Libya na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini. Uamuzi huo unahitimisha uvumi wa muda mrefu kuhusu hatma ya mshambuliaji huyo baada ya kumalizika kwa mkataba wake na Yanga SC.Tunamtakia Prince Dube kila la heri katika changamoto mpya ya maisha yake ya soka.

Mamelodi yamtaka Lucas kurudi klabuni

Picha
Klabu ya Mamelodi Sundowns  imempa taarifa kiungo mshambuliaji Lucas Ribeiro (27) kuwa arudi klabuni hapo ili kuwatumikia kuelekea msimu ujao wa 2026-27. Lucas Ribeiro mpaka sasa yupo nyumbani kwao nchini Brazil  baada ya kuachana na Curtural Leonesa ya Spain na ashafanya makubaliano ya awali na Al Ittihad SC ya Libya ili kujiunga nao kwa msimu mpya kwa ushawishi wa kocha Rhulani Mokwena. Lucas Ribeiro anasubiri maamuzi ya FIFA ili afanye maamuzi ya mwisho kama atarudi Mamelodi Sundowns au atasaini mkataba wa Al Ittihad SC baada ya Sundowns kushitaki kuwa Lucas Ribeiro alivunja mkataba kimakosa bila kufuata taratibu zote hadi kujiunga na Curtural Leonesa. 

JKT Tanzania yamng' oa Sure Boy Yanga

Picha
Mazungumzo baina ya pande zote mbili kwa maana upande wa Salum Abubakar Sure boy na JKT Tanzania yamekamilika na kilichosalia kwasasa ni kusaini kandarasi tu. Licha ya vilabu kama Dodoma Jiji na Mashujaa kuonesha nia ya kuipata huduma yake ila Maafande, Jkt Tanzania ndio wapo karibu zaidi kukamilisha usajili wake Sure (36) anaondoka Young Africans baada ya iandarasi yake kuisha