Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Moallin kurejea tena nchini

Machapisho ya hivi karibuni

Simba yailaza Tanzania Prisons

TIMU ya Simba SC imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Mabao ya Simba SC leo yamefungwa na mshambuliaji mzawa, Suleiman Abdallah Mwalimu dakika ya 19 na beki wa kati raia wa Afrika Kusini, Rushine De Reuck kwa penalti dakika ya 45. Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 22 katika mchezo wa tisa na kusogea nafasi ya nne, wakati Tanzania Prisons inabaki na pointi zake 12 za mechi 14 sasa nafasi ya 14 kwenye ligi ya timu 16. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.

Depu aendelea kutupia Ligi Kuu bara

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu bara inayodhaminiwa na benki ya NBC, Yanga SC usiku huu imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Namungo FC katika uwanja wa Majaliwa Stadium, Ruangwa mkoani Lindi. Bao pekee lililowapa pointi 3 Yanga SC limefungwa na mshambuliaji wao hatari raia wa Angola, Laurindo Dilson Maria Aurelio Depu dakika ya 26 kwa changamoto ya penalti. Kwa matokeo hayo sasa Yanga SC imefikisha alama 25 ilipanda hadi nafasi ya pili nyuma ya JKT Tanzania inayoongoza ikiwa na alama 28, kwa mwenendo wa Yanga inaweza kutetea taji lake msimu huu ikiwa ni kwa mara ya Tano mfululizo. Depu

Azam FC yaizamisha KMC

TIMU ya Azam FC imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji, KMC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa KMC Complex, Complex, Mwenge, Dar es Salaam. Mabao yote ya Azam FC leo yamefungwa na winga Idii Suleiman Ali – maarufu tu kama Iddi Nado dakika ya 55 na 65 na kwa ushindi huo wanafikisha pointi 19 katika mchezo wa tisa na kupanda kwa nafasi moja hadi ya nane. Hali inazidi kuwa mbaya kwa KMC baada ya mchezo wa 12 wa msimu leo – nyingine nne ikishinda mbili na kutoa sare mbili hivyo kuendelea kushika mkia katika Ligi Kuu inayoshirikisha timu 16. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.

Singida Black Stars yaiua Mtibwa Sugar

TIMU ya Singida Black Stars imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara mchana wa leo Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na winga Mrundi, Ndumumwe Mossi dakika ya sita, mshambuliaji Mkongo, Malanga Horso Mwaku dakika ya 17 na beki Kennedy Wilson Juma dakika ya 59, wakati bao pekee la Mtibwa Sugar limefungwa na kiungo Raizin Hafidh dakika ya 88. Kwa ushindi huo, Singida Black Stars inafikisha pointi 15 katika mchezo wa tisa na kusogea nafasi ya 10 kutoka ya 13, wakati Mtibwa Sugar inabaki na pointi zake 21 za mechi 15 sasa nafasi ya nne.

Mwamnyeto kizungumkuti kuongeza mkataba mpya Yanga

Hakuna mazungumzo ya mkataba mpya mpaka sasa kwa kapteni wa Yanga, beki Bakari Mwamnyeto ambaye mkataba wake umebakisha miezi Minne kumalizika. Mwamnyeto alitua Yanga tangu Mwaka 2020 akitokea Coastal Union, kisha Mwaka 2024 akaongeza miaka miwili mkataba unaoisha Mwaka huu. Ikumbukwe Simba SC ni timu iliyowahi kuvutiwa na Mwamnyeto, inawezekana Yanga wakichelewa kumbakisha, msimu ujao tukamshuhudia tena beki huyo akivaa uzi mwekundu.

Mwanariadha mwingine wa Tanzania ashinda medali ya dhahabu Korea Kusini

Mwanariadha wa Tanzania, Gabriel Geay, ameibuka mshindi katika mbio za Daegu Marathon zilizofanyika Korea Kusini, na kutwaa medali ya dhahabu. Geay alimaliza mbio hizo kwa muda wa saa 2:08:09, akimshinda mpinzani wake wa karibu kutoka Ethiopia, Chimdesa Gudeta. Geay amefanikiwa kutetea ubingwa wake, kwani mwaka 2025 alishinda mbio hizo zilizofanyika huko huko Korea Kusini. Mwanariadha mwingine wa Tanzania, Josephat Gisemo, alimaliza nafasi ya tatu na kutwaa medali ya fedha baada ya kutumia muda wa saa 2:08:17. Ushindi wa wanariadha hao unaendelea kuthibitisha nafasi ya Tanzania katika mbio za kimataifa na nguvu ya wanariadha wake mashuhuri.