Machapisho

Beki aliyetambulishwa Yanga kutemwa

Picha
Yanga wana mpango wa kumkata beki wao wa kati Oumar Farouk Comara,ili kupata nafasi ya kumuingiza kwenye mfumo namba 10 wao mpya ajaye. Comara alisaini mkataba wa miaka miwili wenye kipengele cha kutazamwa ndani ya miezi sita ila hadi sasa bado hajawashawishi. Awali Yanga walitaka kumuuza Okello ili wapate nafasi ya namba 10 wao mpya ila hadi sasa hakuna timu iliyofika bei $1.5m hivyo Comara yuko kwenye hatari ya kukatwa.

Kigwangala aliamsha tena Simba

Picha
Aliyekuwa Waziri na Mwanachama wa Simba SC, Dr. Hamisi Kigwangalla, ameibua mtafaruku mpya Msimbazi baada ya kuweka wazi nia yake ya kuvunja kile alichokiita "utawala wa mtu mmoja". Huku akitangaza kuwa yuko tayari kuweka fedha taslimu (cash) mezani kununua hisa za mwekezaji mkuu wa sasa, Mohammed 'Mo' Dewji. Kigwangalla ameyasema hayo huku akijibu shinikizo la baadhi ya wanasimba wanaomtaka agombee nafasi ya Uwenyekiti wa Simba SC kwenye uchaguzi ujao. Sina Hamu na Siasa za Mpira, Tatizo ni Mfumo" Akieleza sababu za kukataa kuingia kwenye kinyang'anyiro cha Uwenyekiti kwa sasa, Dr. Kigwangalla amebainisha kuwa tatizo la Simba silo uongozi wa mtu mmoja, bali ni muundo mbovu wa uendeshaji (governance) na umiliki wa klabu (ownership). "Kwanza, sijioni nikijikita kwenye siasa za mpira wa miguu wa klabu kubwa kama Simba. Pili, naamini tatizo la Simba si mtu mmoja. Tatizo kubwa ni mfumo wa uongozi na umiliki," alisema Kigwangalla. Mpango wa Kuondoa '...

Allan Okello ahitajika FAR Rabat

Picha
Jioni hii Klabu ya FAR Rabat ya Morocco imetuka ofa ya pili yenye thamani ya $1,000,000 (tsh 2.6b) kwenda Yanga ili kumpata Allan Okello. Hii ni ofa ya pili kutoka Rabat baada ya jana Yanga kukataa ofa ya $700,000. Yanga wanataka $1.5m (tsh 3.9b) ili kumuachia Okello.

Yanga yawasili Ruangwa

Picha
Kikosi cha Yanga SC kimewasili Ruangwa, mkoani Lindi tayari kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu ya NBC msimu mpya wa 2026/27 Agosti 15, 2026 Yanga watakua ugenini katika Dimba la Majaliwa kukiwasha na Wauaji wa Kusini, Namungo FC, mchezo utakaopigwa saa tatu usiku.

DABI IMEHARIBU MATAMASHA

Picha
Na Prince Hoza Matua WIKI iliyopita ilikuwa siku muhimu kwa timu zote mbili hasimu kuweza kusherehekea matamasha yake na kutambulisha vikosi vyao, ilianza Simba SC tarehe 8, Agosti ambapo iliadhimisha Simba Day. Na kufuatiwa na Yanga SC tarehe 9 Agosti waliadhimisha Wiki ya Wananchi, kwa kifupi matamasha yote yalifana sana hasa kwenye matukio mengine mambo yalienda safi ila katika suala la mchezo kwa upande wa timu kubwa ya wanaume mambo hayakuwa mazuri. Kwa upande wa Simba timu yao tegemezi haikufanya vizuri ingawa ilitambulisha wachezaji wake wapya, Simba ilicheza na timu ya Police FC ya Kenya na ilikubali kichapo cha bao 1-0. Mashabiki wa timu hiyo hawakuwa na furaha baada ya kushindwa kuwaona nyota wake wapya wakionesha viwango vyao, ndivyo hivyo kwa Yanga nako walikutana na kipigo. Yanga ilicheza na Les Aigle De Congo ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC  ambapo mwisho wa mchezo ilichalazwa mabao 2-1, kipigo cha Yanga nacho kimewauma mashabiki wake ambapo hawakuona viwango vya...

Rais Samia azitakia kila kheri Simba na Yanga

Picha
Tumeshuhudia burudani katika Dabi nyingine ya Kariakoo kupitia mchezo wa Ngao ya Jamii. Pongezi kwa Klabu ya Yanga kwa ubingwa wa 10 wa Ngao ya Jamii. Ninazitakia kila la heri timu zote katika msimu mpya wa Ligi Kuu, pamoja na mashindano mengine ya kitaifa na kimataifa.

Yanga yatwaa tena Ngao ya Jamii

Picha
Yanga SC imeanza vema msimu mpya wa 2026/2027 baada ya kushinda Ngao ya Jamii kufuatia ushindi wa bao 1-0 dhidi ya mtani wake wa jadi Simba SC katika uwanja wa New Amaan Stadium Zanzibar. Bao pekee lilifungwa na Mzambia Albert Kingwanda aliyeunganisha krosi ya Mkongoman Chadrack Boka dakika ya 32 kipindi cha kwanza. Yanga sasa imekabidhiwa Ngao ya Jamii na kuashiria msimu mzuri kwao