Machapisho

Mchora ramani hatari Simba

Picha
Kristopher Bergman huyu naye ni mchora ramani hatari sana kwenye mpango wa kocha Steven Barker, haimbwi lakini pale Simba kuna shughuli anaifanya ni balaa Video Analyst lakini huyu pia ni Kocha, kuna muda haonekani kwenye benchi, anakaa juu kabisa kwenye paa la uwanja, anautazama mchezo kwa juu. Kuna utaalam upo Simba SC ni hatari nawaambia ! Nyie mfatilieni tu huyu Kristopher Bergman, mtajua ninachomaanisha.

Gor Mahia yasimamisha wachezaji kisa kipigo cha Pyramids

Picha
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Kenya, Gor Mahia, wamewasimamisha baadhi ya wachezaji kufuatia kipigo cha mabao 5-1 dhidi ya Pyramids katika mchezo wa hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Gor Mahia walitolewa kwenye mashindano hayo kwa jumla ya mabao 7-1 baada ya michezo miwili dhidi ya Pyramids. Kwa mujibu wa taarifa za ndani, uamuzi huo umefikiwa na uongozi wa klabu hiyo kutokana na wasiwasi kuhusu kiwango na mwenendo wa baadhi ya wachezaji kufuatia kipigo hicho.

Albert Kangwanda aendeleza ushindi kwa Yanga

Picha
Mabingwa wa Tanzania bara Yanga SC jioni ya leo imetoka na ushindi wa bao 1-0.dhidi ya ST George mchezo wa kirafiki wa kimataifa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Bao pekee la Yanga limefungwa na kiungo mshambuliaji wa kimataifa raia wa Zambia Albert Kangwanda aliyepokea assist toka kwa Erick Mwijage. Yanga imeamua kucheza mechi za kirafiki baada ya Ligi Kuu bara kusimama kupisha timu ya taifa, Taifa Stars itakayocheza mechi mbili za kirafiki za kimataifa.

Mechi ya Tanzania na Ghana yaota mbawa

Picha
Mchezo wa kirafiki kati ya Tanzania vs Ghana uliopangwa kuchezwa siku ya Oktoba 4, 2026 umefutwa. Badala ya mchezo huo, Ghana sasa itacheza dhidi ya Morocco siku hiyo ya Oktoba 4 na mchezo utapigwa kwenye uwanja wa Grande Stade de Tangier.

Ostaz Juma amuangukia Sheikh Kishki

Picha
Ostaz Juma Namusoma amemuomba radhi Sheikh Nurdeen Kishki, familia yake na Waislamu kwa ujumla, akisema amejutia kwa dhati kauli alizowahi kutoa dhidi ya Sheikh huyo. Amesema baada ya kutafakari na kupokea nasaha kutoka kwa watu mbalimbali, ameona ni vyema kuomba msamaha kwa unyenyekevu. “Leo natamka wazi kuwa nilimkosea ndugu yangu katika Imani, Muislamu mwenzangu Sheikh Kishki. Ninakuomba radhi na unisamehe pamoja na familia yako. Pia nawaomba radhi Waislamu wote walioathirika na jambo hili. Mwenyezi Mungu atusamehe makosa yetu na atujaalie mwisho mwema,” amesema Ostaz Juma. Hatua hiyo inakuja baada ya Sheikh Kishki kufungua kesi mahakamani akidai fidia ya Shilingi bilioni 5.

Madee kuanzisha redio ya kupiga nyimbo za zamani

Picha
Msafara wa Wakongwe wa Muziki wa Bongo Fleva upo njiani kuelekea Arusha kwa ajili ya Tamasha la Miaka 30 ya Bongo Fleva linalotarajiwa kufanyika Septemba 19, 2026 katika Viwanja vya General Tyre. Akizungumza akiwa njiani kuelekea Arusha, Mratibu wa Tamasha hilo, Madee Ali amesema baada ya tamasha kumalizika, mpango unaofuata ni kufungua redio maalumu itakayokuwa ikipiga nyimbo za zamani (Old School). Aidha, Madee amewataka Wakazi wa Arusha kujiandaa kwa tamasha hilo, akisema wamewaletea burudani yenye kila kitu ikiwa ni sehemu ya kusherehekea safari ya miaka 30 ya Bongo Fleva.

Sandaland Fashion Wear kumburuza mahakamani Makonda kisa kuzikataa jezi za taifa

Picha
Kampuni ya Sandaland Fashion Wear Limited imetangaza kuchukua hatua za kisheria dhidi ya kauli iliyotolewa hadharani na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, kuhusu jezi za Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars. Hatua hiyo imetangazwa kupitia tamko rasmi la kampuni hiyo, iliyosema kauli ya Makonda iliyotolewa Septemba 16, 2026 kupitia akaunti yake ya Instagram imeathiri jina, chapa, hadhi na uhalali wa bidhaa za Sandaland katika soko. Katika ujumbe huo, Makonda alinukuliwa akisema: “Hii sio jezi ya Taifa Stars, Taifa Stars kwa ubora wake hatuwezi kuwa na jezi za kiwango chini hivi. Acheni kutumia picha za Naibu wangu huku ofisi yangu haina taarifa.” Ujumbe huo uliambatana na picha ya Naibu Waziri Hamis Mwinjuma, maarufu Mwana FA, akiwa amevalia jezi yenye mchanganyiko wa rangi ya njano, bluu, nyeusi iliyochanganyika na kijani. Sandaland imesema kauli hiyo imezua taharuki na sintofahamu, huku ikidai kuwa tayari imesababisha madhara ya kiuchumi na kwa hadhi ya kam...