Machapisho

Nilimfahamu King Kinya tangu mwaka 1998

Picha
Nilimfahamu King Kinya katika ofisi za gazeti la Majira nakumbuka ilikuwa mwaka 1998, nadhani nilipeleka hadithi yangu itokee gazetini. Kinya alikuwa anachora katuni tena enzi hizo alikuwa na umri wa miaka 14, mimi pia nilikuwa na umri kama wake, nilimfahamu King Kinya akiwa na wenzake Masoud Kipanya, Bondaboy, Nathan Mpangala, Noah Yongolo na wengineo. Kifo chake kimenisikitisha ila kazi yake mola aina makosa, hayo ni maneno ya Prince Hoza ambaye anamuelezea marehemu kwamba alifanya naye kazi kuanzia gazeti la Majira ingawa yeye alipita tu na kutimkia magazeti mengine Enzi za uhai wake King Kinya akichora katuni zake Miongoni mwa michoro yake Alikuwa anachora katuni Sanaa za King Kinya

King Kinya afariki dunia

Picha
Tasnia ya uchoraji katuni nchini imepata pigo baada ya kifo cha Kinyagulo Tuzo, maarufu King Kinya, aliyefariki dunia Septemba 17, 2026 baada ya kuugua kwa kipindi kifupi. Kifo cha King Kinya kimethibitishwa na Ofisi ya Rasilimali Watu ya Kampuni ya MCL, aliyokuwa akiifanyia kazi kama mchora katuni wa magazeti. Kaka wa marehemu, Kiondo Mjema, amesema King Kinya alianza kuugua akiwa nyumbani Tabata mwanzoni mwa Julai mwaka huu, kabla ya kupelekwa Morogoro baada ya hali yake kuzidi kuwa mbaya. Amesema akiwa Morogoro, marehemu alipelekwa hospitalini na kulazwa kwa takriban wiki moja, kabla ya kuruhusiwa kurejea nyumbani huku akielekezwa kurejea hospitalini kwa ajili ya ufuatiliaji. Kwa mujibu wa Kiondo, King Kinya alirejea hospitalini juzi baada ya kusumbuliwa na tumbo, kuharisha na kutapika, lakini hali yake ilizidi kuwa mbaya usiku wa kuamkia jana, Septemba 15, akilalamikia maumivu makali ya tumbo na kichwa. Amesema msiba upo Kimara Kona.

MO Dewji atoa neno ushindi wa Azam FC

Picha
Mo Dewji, ambaye ni rais wa klabu ya Simba SC, ameandika ujumbe baada ya timu yake kufanya vizuri dhidi ya Azam FC. Kwa taarifa za ndani, inasemekana kuwa kiongozi huyo alitoa tena mshiko mrefu akiwapa wachezaji, huku akisema, “Mkiendelea kufanya vizuri, itakuwa zaidi ya hapo.” Kupitia uclas wake wa Instagram, ameandika maneno machache juu ya wachezaji wake pamoja na benchi zima la ufundi: “Hongereni sana wachezaji wetu, benchi la ufundi na mashabiki wote wa Simba SC kwa matokeo mazuri. Tuendelee kupambana, kuamini na kusimama pamoja na timu yetu. Umoja na mshikamano wetu ndio nguvu yetu.”

Yanga na ST George kumenyana kesho

Picha
Baada ya mikiki ya Ligi Kuu, Wananchi Yanga SC Septemba 18, 2026 watakuwa na kibarua kingine katika mchezo wa kirafiki dhidi ya St. George ya Ethiopia. Mchezo huo utachezwa kesho Ijumaa kuanzia saa 12 00 jioni huku mechi hiyo ikirushws live na Azam Tv

CAF yasisitiza AFCON 2027 ni Tanzania, Kenya na Uganda

Picha
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Dkt. Patrice Motsepe amesema AFCON 2027 haitaondolewa Tanzania, Kenya na Uganda, akisisitiza kuwa Mataifa hayo yataendelea kuwa wenyeji wa mashindano hayo. Rais Akizungumza leo Septemba 17, 2026 baada ya kuwasili Tanzania kwa ajili ya kukagua maendeleo ya maandalizi, Motsepe amesema amekuwa akisikia taarifa zinazodai kuwa CAF inaweza kuanza kufikiria mpango mbadala wa kuondoa mashindano hayo katika Nchi hizo tatu. “Baadhi ya Watu, kutokana na yale ambayo tayari yameripotiwa na baadhi ya Vyombo vya Habari barani Afrika na sehemu nyingine duniani, wanasema Rais wa CAF anapaswa kuanza kufikiria mpango B na mpango C na kuiondoa AFCON Tanzania, Kenya na Uganda, hilo halitatokea,” amesema Motsepe. “Ninajivunia sana kazi nzuri inayoendelea kufanyika Tanzania, tuna miezi tisa, na moja ya mambo ninayosisitiza ni kwamba tunapaswa kuongeza kasi, tupo hapa kufanya kazi pamoja, kusaidia na kutoa ushirikiano, hii ni AFCON yetu,”

KOCHA WA YANGA NAYE ANAJIWEKA MTEGONI MWENYEWE

Picha
Na Prince Hoza Matua JUMANNE iliyopita katika uwanja wa KMC Complex Mwenge jijini Dar es Salaam kulichezwa mchezo wa soka wa Ligi Kuu bara wenyeji Yanga SC na Geita Gold toka mkoani Geita uliomalizika kwa Yanga kushinda 1-0. Mchezo ulikuwa mgumu kwa Yanga kwani ilijaribu kufanya mashambulizi mara kadhaa lakini vijana wa Geita walikuwa makini kuondoa hatari zote golini kwake, Yanga iliwachukua dakika ya 60 kuandika bao likifungwa na mlinzi wake wa kati Farouk Komara. Kuelekea mchezo huo, kocha mkuu wa Yanga Manqoba Mngqoithi raia wa Afrika Kusini akiuzungumzia mchezo huo siku ya Jumatatu katika press na waandishi wa habari alidai kwamba Geita haimtii presha. Maanake mechi itakuwa nyepesi na atalazimika kutumia wachezaji wake wasiopata nafasi ya kucheza na kwa upande mwingine atawapumzisha nyota wake wanaoanza kikosi cha kwanza. Ni kweli siku ya mchezo Yanga iliwakosa nyota wake Peter Shalulile na Kouassi Yao Attohoula na jujaribu wachezaji wengine na mchezo waliuchukulia rahisi. Sio sir...

Makonda azigomea jezi mpya Taifa Stars

Picha
Makonda akataa jezi alizozivaa Naibu Waziri wake FA asema “ofisi yangu haina taarifa,tuheshimiane” Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amezikataa jezi mpya za Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, zilizozinduliwa rasmi leo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Makonda ameposti picha za jezi hizo na kueleza kuwa hazikidhi kiwango anachokitarajia kwa timu ya taifa, huku akisema ofisi yake haikuwa na taarifa kuhusu matumizi ya picha za Naibu Waziri katika suala hilo. "Hii sio jezi ya Taifa Stars. Taifa Stars kwa ubora wake hatuwezi kuwa na jezi za kiwango cha chini hivi. Acheni kutumia picha za Naibu wangu huku ofisi yangu haina taarifa. Tuheshimiane," ameandika Makonda.