Machapisho

Yanga mwendo mdundo ikiilalua Pamba Jiji

Picha
Timu ya Yanga SC usiku huu imeendelea kuchanja mbuga kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Pamba Jiji ya Mwanza katika mchezo wa Ligi Kuu bara uwanja wa KMC Complex Mwenge jijini Dar es Salaam. Kwa ushindi huo Yanga inaendeles kukaa kileleni ikifikisha pointi 12 huku ikiwa imefunga mabao 13 huku ikicheza mechi 4. Yanga ilianza kupata bao kupitia kwa Maxi Nzengeli assist ya Sheikh Ibrahim Toure dakika ya 17 kabla ya Toure kufunga la pili assist ya Peter Shalulile dakika ya 23. Yanga sasa itasafiri tarehe 1, Septemba kuwafuata Fountain Gate wanaotumia uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha.

Wachezaji 15 Afrika wanaolipwa zaidi, Girumugisha ashika ya 3

Picha
Jean Claude Girumugisha amekuwa mchezaji wa tatu anayelipwa mshahara mkubwa zaidi katika historia ya soka barani Afrika, ikiwa tunazingatia mishahara inayolipwa katika mashindano ya ndani ya Afrika pekee. Kwa mujibu wa orodha iliyotolewa na Story Africa, hawa ndio wachezaji wanaodaiwa kulipwa mishahara mikubwa zaidi katika historia ya soka la ndani barani Afrika: 1. Fiston Mayele — analipwa dola milioni 5 kwa mwaka na Al Ahli Tripoli. 2. Mohamed Tougai — analipwa dola milioni 3.7 kwa mwaka na Al Ahli Tripoli. 3. Jean Claude Girumugisha — analipwa dola milioni 2.4 kwa mwaka na Al Ahli Tripoli . 4. Ferjani Sassi — aliwahi kulipwa dola milioni 2.2 kwa mwaka na Zamalek kati ya 2018 na 2021. 5. Ali Maaloul — aliwahi kulipwa dola milioni 1.5 kwa mwaka na Al Ahly kati ya 2021 na 2025. 6. Anthony Modeste — aliwahi kulipwa dola milioni 1.5 kwa mwaka na Al Ahly kati ya 2023 na 2024. 7. Ramadan Sobhi — analipwa dola milioni 1.446 kwa mwaka na Pyramids FC tangu 2020. 8. Youcef Belaïli — aliwahi k...

Enzo aondolewa Chelsea

Picha
Kiungo wa Chelsea, Enzo Fernández, ameondolewa rasmi kwenye kikosi cha Chelsea usiku wa leo Agosti 27, katika mchezo wa Carabao Cup dhidi ya Luton Town, baada ya kukubali maslahi binafsi na kutoa "Green Light" kuhamia Manchester City. Enzo Fernández amevutiwa sana na mradi wa Manchester City na amewaambia mawakala wake kuwa anataka kuhamia Etihad. Kocha mpya wa Man City, Enzo Maresca, amemtaja Enzo kama shabaha yake namba moja ili kuziba pengo la Rodri aliyetimkia Barcelona. Wawili hao walifanya kazi kwa mafanikio makubwa hapo awali ndani ya Chelsea.

Mwamuzi wa kwanza mwanamke Afrika Kusini atajwa FIFA

Picha
Akhona Zennith Makalima (aliyezaliwa tarehe 27 Machi 1988, mwenye umri wa miaka 37) ni mwamuzi wa kimataifa wa soka kutoka Afrika Kusini, ambaye amekuwa kwenye orodha ya waamuzi wa kimataifa wa FIFA tangu mwaka 2014. Anachezesha mechi chini ya FIFA, CAF, COSAFA, Premier Soccer League (PSL), pamoja na Shirikisho la Soka la Afrika Kusini (SAFA). Alikuwa mwanamke wa kwanza kuwa mwamuzi katika Premier Soccer League. Ana Diploma ya Kitaifa ya Usimamizi wa Rasilimali Watu kutoka King Hintsa FET College, na kwa sasa anafanya kazi kama msimamizi katika Idara ya Michezo. Tarehe 9 Januari 2023, FIFA ilimteua kuwa sehemu ya kundi la waamuzi kwa Kombe la Dunia la Wanawake la FIFA 2023 lililofanyika Australia. Pia alikuwa mwamuzi wa VAR katika AFCON 2023, na alifanya kazi kama mwamuzi wa VAR katika CAF Super Cup 2024.

Sele Gomez aja na muonekano mpya

Picha
Straika mpya wa Yanga SC, Selemani Mwalimu ‘Gomez’, akiwa mazoezini na mwonekano mpya. Kwa mujibu wa taarifa ya Yanga, kesho mshambuliaji huyu atakuwa uwanjani wakati Yanga wakikipiga dhidi ya Pamba Jiji FC. “Chuma kipo tayari kwa ajili ya kuwapa furaha Wananchi Kesho,” taarifa ya Yanga SC.

Simba yapata ushindi kiduchu

Picha
Timu ya Simba SC usiku huu imepata ushindi kiduchu baada ya kuifunga Coastal Union ya Tanga bao 1-0 katika uwanja wa Meja Isamuhyo Mbweni jijini Dar es Salaam. Mchezo huo wa Ligi Kuu bara ulikuwa wa upande mmoja kwa Simba kufanya mara kwa mara, bao pekee la Simba limefungwa na Ismail Toure baada ya kutokea nyuma.

Bodi ya Ligi Tanzania na Mali waenda kujifunza Yanga

Picha
Uongozi wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania ukiambatana na wageni wao kutoka Bodi ya Ligi ya Mali, umefika katika Klabu ya Yanga kwa ziara yenye lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu namna klabu inavyojiendesha. Katika ziara hiyo, wageni hao wamepata fursa ya kufahamu mifumo ya uendeshaji wa klabu, usimamizi wa shughuli za kila siku, maendeleo ya biashara na masoko, matumizi ya teknolojia, pamoja na namna Yanga inavyosimamia chapa yake na kuwahudumia mashabiki Wageni hao wamepokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Yanga SC, Andre Mtine