Machapisho

Yanga, Sportpesa wateta

Picha
Mapema asubuhi ya leo, Uongozi wa YANGA SC ukiongozwa na Rais Eng. Hersi Said ulifanya kikao na Mdhamini Mkuu wa Klabu yetu, Kampuni ya SportPesa na kujadili mambo mbalimbali ya kimkataba na mahusiano ya pande zote mbili. Upande wa Kampuni ya SportPesa uliwakilishwa na Tarimba Abbas, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Allan McTavish, Mkuu wa Kimataifa wa Udhamini na Sabrina Msuya ambaye ni Mshauri wa Udhamini Mahusiano na Serikali.

Simba yapindua meza

Picha
Simba wanataka kupindua meza kwa Yona Amos (27). Yona ni mcheza huru baada ya kumalizana na Pamba Jiji. Mwezi uliopita Yona alikubaliana kila kitu (Sign on fee,mshahara) na Singida Black stars ila dili hilo limechelewa kukamilika coz Singida bado hawajaingiza hela kwenye Account ya Yona. Baada ya Simba kugundua hilo wameingilia kati na sasa wanataka kupita na kipa huyo. Mazungumzo ya Simba na Yona yanaendelea.

Prince Dube atambulishwa Zimbabwe

Picha
Mshambuliaji wa kimataifa wa Zimbabwe, Prince Dube, ametambulishwa rasmi kama mchezaji mpya wa Hard Rock FC ya nchini Zimbabwe, akianza rasmi safari mpya ya soka katika taifa lake. Kwa mujibu wa taarifa hizo, Dube ameamua kujiunga na Hard Rock FC licha ya kuripotiwa kuvutiwa na klabu kadhaa, zikiwemo Young Africans SC (Yanga), Al Ahly Benghazi ya Libya na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini. Uamuzi huo unahitimisha uvumi wa muda mrefu kuhusu hatma ya mshambuliaji huyo baada ya kumalizika kwa mkataba wake na Yanga SC.Tunamtakia Prince Dube kila la heri katika changamoto mpya ya maisha yake ya soka.

Mamelodi yamtaka Lucas kurudi klabuni

Picha
Klabu ya Mamelodi Sundowns  imempa taarifa kiungo mshambuliaji Lucas Ribeiro (27) kuwa arudi klabuni hapo ili kuwatumikia kuelekea msimu ujao wa 2026-27. Lucas Ribeiro mpaka sasa yupo nyumbani kwao nchini Brazil  baada ya kuachana na Curtural Leonesa ya Spain na ashafanya makubaliano ya awali na Al Ittihad SC ya Libya ili kujiunga nao kwa msimu mpya kwa ushawishi wa kocha Rhulani Mokwena. Lucas Ribeiro anasubiri maamuzi ya FIFA ili afanye maamuzi ya mwisho kama atarudi Mamelodi Sundowns au atasaini mkataba wa Al Ittihad SC baada ya Sundowns kushitaki kuwa Lucas Ribeiro alivunja mkataba kimakosa bila kufuata taratibu zote hadi kujiunga na Curtural Leonesa. 

JKT Tanzania yamng' oa Sure Boy Yanga

Picha
Mazungumzo baina ya pande zote mbili kwa maana upande wa Salum Abubakar Sure boy na JKT Tanzania yamekamilika na kilichosalia kwasasa ni kusaini kandarasi tu. Licha ya vilabu kama Dodoma Jiji na Mashujaa kuonesha nia ya kuipata huduma yake ila Maafande, Jkt Tanzania ndio wapo karibu zaidi kukamilisha usajili wake Sure (36) anaondoka Young Africans baada ya iandarasi yake kuisha

Akaminko njia nyeupe kwenda Yanga

Picha
Yanga SC wameanza mazungumzo rasmi na kambi ya James Akaminko wakipania kuimarisha safu yao ya kiungo kabla ya msimu mpya. Mkataba wa sasa wa kiungo huyo wa kimataifa wa Ghana unatarajiwa kumalizika Julai 5, na Kwa sasa akamiko anaweza kuzungumza na timu yeyote Yanga SC sasa wanatathimini uwezekano wa kumleta klabuni hapo,lakini mazungumzo bado yanaendelea na hakuna makubaliano ya mwisho ambayo yamefikiwa katika hatua hii

Chris Mugalu huyoo Caps United

Picha
Mshambuliaji Chris Mugalu (35) amejiunga na klabu ya CAPS United kwaajili ya msimu ujao wa 2026-27 kutoka Forest Rangers Chris Mugalu aliwahi kucheza Simba SC kabla ya kujiunga na CAPS United ambayo mkataba wake na klabu hiyo kumalizika.