Machapisho

Bao 6 za Simba zaondoka na kigogo wa Mighty Wonderers-

Picha
Kipigo kizito walichokipata miamba ya Malawi, Mighty Wanderers, kwenye michuano ya CAF Champions League mikononi mwa Simba SC kimeleta mtafaruku mkubwa uliomfanya Rais na Mdhamini Mkuu wa klabu hiyo, Dr Thomson Mpinganjira, kutangaza kujiuzulu rasmi. Matokeo hayo mabaya uwanjani yameonekana kuwa chanzo kikuu cha maamuzi hayo ya ghafla, yakionyesha jinsi dozi ya Mnyama Simba ilivyoingia hadi kwenye korido za uongozi wa Wanderers. Kuondoka kwa Dr Mpinganjira, ambaye pia ndiye alikuwa mwekezaji na mdhamini mkuu, kunaiweka klabu hiyo ya Malawi kwenye utata mkubwa wa kifedha kuelekea michezo inayofuata.

Niffer atangaza kudata kwa Libasse Gueye

Picha
Mfanyabiashara na mrembo maarufu nchini, Niffer, ameshangaza watu kwa maranyingine baada ya kuanza kuonyesha hadharani mahaba na ukaribu wake kwa winga hatari wa Simba SC raia wa Senegal , Libasse Gueye. Licha ya Niffer kufahamika kama shabiki lialia wa Yanga SC, mrembo huyo amezua mshtuko kwa mashabiki baada ya ku-repost post mbili za Gueye siku ya leo pekee. Huku akiweka comments zilizozua maswali mengi ikiwemo kumwita "Top Simba SC treasure" akimaanisha "Hazina kuu ya Simba SC" na kuandika kuwa anamkubali popote alipo huku akimuombea afike mbali zaidi. Gueye anaendelea kuthibitisha kuwa yeye ni X-Factor wa Simba SC msimu huu, baada ya kutangazwa Mchezaji Bora wa Agosti kwa kuhusika kwenye mabao 6 ya Ligi Kuu, leo amefunga mabao mawili dhidi ya Mighty Wanderers kwenye ushindi wa 6-1.

Kutoitwa timu ya taifa, Chama alitangaza kustaafu kitambo

Picha
Nyota wa klabu ya Simba raia wa Zambia Clatous Chota Chama "Triple C" ametangaza rasmi kustaafu kuitumikia timu ya taifa ya Zambia "Chipopolo". Na hiki ndicho alichokisema Chama JR,kwa nini amefanya Maamuzi ya kustaafu kipindi hiki:- "Muda wangu umeisha,sasa hivi Zambia kuna wachezaji wengine wengi wana nguvu.Kwahiyo hao wanaweza kuipambania bendera ya Chipopolo" -Clatous Chama, Aliyekuwa Mchezaji wa timu ya taifa ya Zambia.

Kangwanda aitwa timu ya taifa

Picha
Kocha wa Zambia, George Lwandamina, ameitangaza orodha ya wachezaji kwa ajili ya michezo ya kufuzu AFCON. Albert Kangwanda wa Yanga SC ameitwa kwenye kikosi cha Chipolopolo, huku Clatous Chama wa Simba SC akikosa nafasi. Hii ni habari kubwa kwa Kangwanda ambaye anaendelea kujenga nafasi yake kwenye timu ya taifa. Kwa upande wa Chama, kuachwa nje ni pigo jingine na sasa itakuwa juu yake kuendelea kufanya kazi ili kurejea kwenye mipango ya kocha.

Anuary Jabir kinara wa mabao Ligi Kuu bara

Picha
Likija swala la kufunga magoli msimu huu 2026/2027 Ligi Kuu Tanzania bara kuna huyu Mwamba Anuary Jabiry kutokea Polisi Tanzania amekua wa moto sana mpaka sasa yeye ndiye kinara wa magoli akiwa kashafunga magoli matano (5) kwenye michezo Sita(6) ambayo amecheza. Wanao mfuatia Anuary Jabiry, • Obrey Chilwa ( Geita Gold FC ) 4 • Abdul Sopu ( Azam FC ) 4 • Clatous Chama ( Simba SC ) 3 • Peter Shalulile ( Yanga SC ) 3 • Maxi Nzengeli ( Yanga SC ) 3 • Maabad Maabad ( Coastal Union) 3

Yanga hawana presha na Geita Gold kesho

Picha
Kocha wa Yanga, Manqoba Mngqithi, amesema hana presha kuelekea mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Geita Gold, akisema yuko kwenye nafasi ambayo alitamani kuwa. Akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mchezo huo utakaochezwa kesho, Septemba 15, 2026, Manqoba amesema Yanga inapaswa kufurahia ushindani na kuchukua mchezo mmoja baada ya mwingine, huku akisifu uwezo wa Kocha wa Geita Gold, Zuberi Katwila. “Sina presha, niko kwenye nafasi ambayo nilitamani kuwa. Tunapaswa kufurahia ushindani na kuona mapambano yataishia wapi. Hii ni ligi yenye ushindani mkubwa na bado hatujacheza dhidi ya baadhi ya timu kubwa, hivyo tunapaswa kuchukua mchezo mmoja baada ya mwingine,” amesema Manqoba. Amesema Geita Gold ni timu yenye wachezaji wenye uwezo mkubwa kiufundi, mpangilio mzuri, ulinzi ulioshikamana na uwezo wa kufanya mashambulizi ya kushtukiza, hivyo wanafahamu kuwa hawatacheza dhidi ya wapinzani wepesi. “Tunakwenda kukutana na timu nzuri sana. Ina wachezaji wenye uwezo mkubwa kiufundi, ni tim...

CAF kutoa milioni 270 kwa klabu itakayotolewa Afrika

Picha
Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) limetangaza kutoa kitita cha dola za Marekani 100,000, sawa na takribani shilingi milioni 270 za Tanzania, kwa kila klabu itakayoondolewa katika hatua ya kwanza ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika au Kombe la Shirikisho Afrika. Hatua hiyo inalenga kuzisaidia klabu, hususan zile zenye uwezo mdogo kifedha, kumudu gharama mbalimbali zinazohusiana na ushiriki wao katika mashindano ya kimataifa, ikiwemo usafiri, malazi na uendeshaji wa mechi. Kiasi hicho ni ongezeko kubwa ikilinganishwa na msimu uliopita, ambapo CAF ilikuwa ikitoa dola 50,000, huku msimu huu malipo hayo yakiongezwa hadi kufikia dola 100,000.