Machapisho

Salah atambulishwa Trabzonsor

Picha
Mohhamed Salah sasa ni rasmi mchezaji wa Trabzonspor, akijiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili unaoripotiwa kuwa na thamani ya €17 milioni kwa mwaka, sawa na takribani TSh bilioni 51 kwa mwaka. Mkataba huo unatajwa kuwa na: €10 milioni mshahara — takribani TSh bilioni 30 kwa mwaka. €7 milioni bonasi ya kusaini — takribani TSh bilioni 21. 20% ya mapato yatokanayo na mauzo ya bidhaa zenye chapa ya Salah. Hivyo Kwa miaka miwili, thamani ya mshahara na bonasi pekee inaweza kufikia takribani TSh bilioni 102.

Yanga yapatwa pigo, Mzee Motisha aaga dunia

Picha
Familia ya Yanga imepata pigo kubwa kufuatia kifo cha mwanachama wake maarufu, Mzee Said “Motisha”, aliyefariki dunia jioni ya leo. Mzee Said Motisha alikuwa mmoja wa mashabiki na wanachama wa muda mrefu wa Yanga SC, akijulikana kwa mapenzi yake ya dhati kwa klabu hiyo. Alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakihudhuria mechi nyingi za Yanga nyumbani na ugenini, akitoa hamasa kwa wachezaji na mashabiki wenzake bila kuchoka. Kwa miaka mingi, jina la “Motisha” lilikuwa sehemu ya utambulisho wa Yanga, huku uwepo wake ukiwa chanzo cha ari na mshikamano kwa Wananchi. Wengi walimfahamu kama shabiki wa kweli, aliyeishi na kuipenda Yanga katika nyakati za ushindi na changamoto. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na familia, maziko ya marehemu yatafanyika kesho, Ijumaa, baada ya Swala ya Alasiri. Ibada ya mazishi itafanyika katika Msikiti wa Mwinyimkuu, kabla ya mwili wake kuzikwa katika Makaburi ya Mwinyimkuu. Hakika mchango wake kwa familia ya Yanga utakumbukwa kwa muda mrefu. Mwenyezi Mungu am...

Singida, KMKM kazi kwao

Picha
Hizi ndio mechi za Kombe la Shirikisho raundi ya kwanza ya awali, ambapo timu za Tanzania, SINGIDA BS, Kmkm SC Zanzibar zitakuwa na kazi ya kuisaka hatua ya makundi.

Azam FC kupepetana na Zed au ASAS

Picha
Hizi ndio mechi za Kombe la Shirikisho raundi ya pili ya awali, ambapo Azam Football Club atakuwa anasubiri mshindi kati ya Zed FC ya Misri dhidi ya ASAS Djibouti ili kutafuta nafasi ya kutinga hatua ya makundi.

Simba Queens ziarani Kenya

Picha
Mabingwa wa Ligi Kuu Wanawake Tanzania Tanzania Women's Premier League 2025-2026 Simba Queens wanatarajia Kusafiri Hadi Nchini Kenya August 11,2026 kwa Ajili ya Kuweka Kambi. Simba Queens wanatarajia Kuweka Kambi ya Siku 7 Nchini Humo na Kupata Michezo ya Kirafiki kabla ya Kusafiri Kuelekea Nchini Rwanda kwenye Mashindano ya CAF Women's Champions League CECAFA Zonal Qualifies yanayotarajia Kuanza August 21,2026 Mpaka August 29,2026 Simba Queens imepangwa kwenye Kundi C na Timu Za Kenya Police Bullets (Kenya) pamoja na Top Girls (Burundi) Kila la Kheri Mnyama Simba Sports Club (Queens)

Yanga itakutana na Gaborone United

Picha
Wawakilishi wa Tanzania katika CAF Champions League, Young Africans SC, wamepangwa dhidi ya Gaborone United ya Botswana katika raundi ya kwanza ya hatua ya awali ya michuano hiyo. Yanga itahitaji kupata matokeo mazuri katika michezo hiyo ili kusonga mbele na kuendelea na safari ya kusaka nafasi ya kufuzu hatua ya makundi ya CAF Champions League. Iwapo Yanga itafanikiwa kuiondoa Gaborone United, hatua inayofuata itawakutanisha na mshindi kati ya CFFA ya Madagascar na Lijabatho FC ya Lesotho. Hivyo, safari ya Yanga kuelekea Group Stage ya CAF Champions League inaanza rasmi, huku klabu hiyo ikiwa na lengo la kuendelea kuiwakilisha Tanzania kwenye jukwaa la juu la soka la Afrika.

Seleman Mwalimu aanza mszoezi Wydad

Picha
Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania, Selemani Mwalimu 'Gomez' ameanza mazoezi ya maandalizi ya msimu mpya wa 2026/27 akiwa na waajiri wake, Wydad Casablanca ya Morocco baada ya kumalizika kwa mkataba wake wa mkopo kunako klabu ya Simba SC