Machapisho

Bendera ya Marekani kupepea nusu mlingoni siku 7 kumlilia Dolly Parton

Picha
Rais Donald Trump ameagiza bendera ya Marekani kushushwa nusu mlingoti nchini humo kwa muda wa siku 7 kuanzia jana Jumanne jioni, kufuatia kifo cha nguli wa muziki wa country Dolly Parton kilichotokea mapema siku ya jana. "Hajawahi kutokea mtu kama yeye, na hatatokea tena," ameandika Trump. Mpwa wa Parton, Bryan Seaver, alitangaza kifo cha Dolly Parton kupitia video iliyorekodiwa mapema na kuchapishwa kwenye mitandao ya kijamii, amefariki akiwa na umri wa miaka 80, siku 4 baada ya kulazwa hospitali. Dolly alikuwa mmoja wa wanamuziki pendwa zaidi wa nyakati zote, akiwa na nyimbo kama “Jolene,” “9 to 5,” na “I Will Always Love You” zilizompa umaarufu zaidi enzi za uhai wake.

Simba Queens yatupwa nje CECAFA

Picha
Simba Queens imeondolewa katika mashindano ya CECAFA yanayoendelea Kigali, Rwanda, baada ya kushika nafasi ya pili Kundi C ikiwa na pointi tatu. Timu hiyo ilishinda mchezo mmoja na kupoteza mmoja, hivyo kushindwa kufuzu hatua ya nusu fainali. Kenya Police Bullets ya Kenya imeongoza kundi hilo kwa pointi sita baada ya kuichapa Top Girls Academy ya Burundi mabao 3-1 na kutinga nusu fainali. Kwa Simba Queens, matokeo hayo ni pigo katika harakati za kurejesha taji linaloshikiliwa na JKT Queens ya Tanzania. Timu hiyo imeendelea kukosa mafanikio makubwa katika miaka ya hivi karibuni. Baada ya kufika nusu fainali mwaka 2022, ilishiriki tena mwaka 2024 na kumaliza nafasi ya nne. Matokeo ya mwaka huu yanaongeza changamoto kwa Simba Queens katika kurejesha ubabe wake kwenye soka la wanawake Afrika Mashariki na ‎kati.

Masikini Kibabage!!

Picha
Simba SC imepata pigo baada ya beki wake, Nickson Kibabage, kupata majeraha yatakayomuweka nje ya uwanja kwa takribani wiki 3–4. Tunamtakia Kibabage ahueni ya haraka na tunatarajia kumuona ak irejea uwanjani akiwa fiti zaidi.

Mayele aibukia Al Ahli Tripoli

Picha
Mshambuliaji wa kimataifa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Fiston Kalala Mayele, amejiunga rasmi na klabu ya Al Ahli Tripoli ya Libya akitokea Pyramids FC ya Misri kama mchezaji huru. Mayele amesaini mkataba wa miaka miwili, utakaomuweka klabuni hapo hadi Juni 2028. Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na vyanzo mbalimbali vya michezo, thamani ya jumla ya kifurushi cha mkataba wake inakadiriwa kufikia Dola Milioni 5 kwa miaka miwili. Mshahara wa milioni 550 kwa mwezi pale Al Ahly Tripoli SC ambao ukiugawanya unapata around 19.7 m kwa siku  Fiston Kalala Mayele amegonga jackpot baada ya kipaji na juhudi zake,19.7m kwa siku pungufu ya 1.3m mshahara wa mwezi aliokuwa akipokea Young Africans SC (21m monthly)

Injinia Hersi amkabidhi gari mbunifu idara ya habari

Picha
Rais wa Yanga, Eng. Hersi Said, amemkabidhi zawadi ya gari Willy Shemoka @shemokawilly kama pongezi kwa kutokana na jitihada zake na ubunifu mkubwa alionesha kwenye idara ya habari. Mafanikio haya yanaenda sambamba na ubunifu, bidii na maboresho makubwa katika uzalishaji wa maudhui ya Yanga. Kama muandaa maudhui , Willy amekuwa sehemu muhimu ya safari hii, huku YouTube ya Yanga ikifikia hadhi ya kuwa namba moja Afrika kwa watazamaji. Hongera Willy Shemoka

Shalulile azua balaa Mamelodi

Picha
Mashabiki wa Mamelod Sundowns ya Afrika Kusini wameanza kutoa milio na wakionekana kuushutumu uongozi wa timu kumuachia aondoke. Mashabiki hao wa Mamelod ya wameanza kuulamu uongozi wao pamoja na kocha wa timu yao Miguel Cardozo kwa kumuacha Peter Shalulile kutimkia Young Africans Sports Club ya Tanzania na kubaki na Mothiba ambae kiwango chake hawajaridhishwa nacho.

Coastal wagumu lakini tutashinda- Matola

Picha
Kocha Msaidizi wa Simba SC, Seleman Matola, amesema mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Coastal Union utakuwa mgumu, lakini kikosi chake kimejiandaa kuhakikisha kinapata alama tatu. Matola amesema licha ya Coastal Union kutokuwa na matokeo mazuri katika michezo yake ya mwanzo, timu hiyo imekuwa ikionesha ushindani mkubwa inapokutana na Simba SC. Akizungumzia matumizi ya Video Support (FVS), Matola amesema teknolojia hiyo imeongeza kitu katika ligi, huku benchi la ufundi likiwataka wachezaji kuongeza umakini na kuepuka makosa yanayoweza kuonekana kupitia mfumo huo. Kwa upande wake, golikipa wa Simba SC, Hussein Abel, amewahakikishia Wanasimba kuwa wataingia uwanjani kupambana kupata alama tatu na kulinda lango lao bila kufungwa. Simba SC itakutana na Coastal Union kesho, Agosti 27, 2026, saa 1:00 usiku katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam. Taarifa rasmi ya Simba SC pia inaonesha kuwa mchezo huo utaanza saa 1:00 usiku.