Machapisho

Simba yashikws shati na Mogadishu

Picha
Wawakilishi wa Tanzania bara katika michusno ya Kagame Cup, Simba usiku huu wameanza vibaya baada ya kutoka sare ya 0-0 na timu ya Mogadishu City Club ya Somalia. Mashindano hayo yanafanyika nchini Rwanda na kudhaminiwa na klabu ya Al Hilal ya Sudan, tumeshuhudia Simba na Mogadishu wakicheza soka zuri na lenye ufundi. Almanusura Simba ipate bao dakika za mwisho mwisho kupitia mshambuliaji wake mpya Ibrahim Doumbia baada ya kugongesha mwamba. ​Katika mchezo mwingine wa kundi hilo, Jamus SC kutoka Sudan Kusini imeilaza Singida Black Stars kwa mabao 2-0 na kushika usukani wa kundi hilo.

Ibraheem Jabaar amalizana na mnyama

Picha
Klabu ya Simba imeendelea kutambulisha wachezaji wapya na safari hii imemleta Ibraheem Jabaar raia wa Nigeria aliyekuwa anacheza Stellenbosch FC Ujio wa Jabaar ni kuondoa tetesi zilizokuwa midomoni mwa watu kwamba Simba inaleta watu wa maana msimu ujao.

Mpishi wa mabao Afrika Kusini atambulishwa Simba

Picha
Klabu ya Simba imemtambulisha rasmi kiungo mshambuliaji wa Sekhukhune United Keletso Makgalwa, ambaye ameonekana kuwa mmoja wa wachezaji hatari zaidi wa kutengeneza nafasi za mabao katika Ligi Kuu ya Afrika Kusini ndani ya misimu miwili iliyopita. Makgalwa, mwenye umri wa miaka 29 amejijengea sifa kubwa Sekhukhune United kutokana na kasi yake, uwezo wa kupiga chenga na hasa ubora wake wa kutoa pasi za mwisho zinazozaa mabao. Msimu wa 2024/25 Makgalwa alikuwa mchezaji aliyeongoza kwa pasi za mabao (assists) kwenye ligi kuu ya Afrika Kusini baada ya kutoa asisti 11 katika mechi 28 za ligi na alifunga mabao sita katika mashindano yote na kumaliza msimu akiwa miongoni mwa wachezaji walioteuliwa kuwania tuzo ya Mchezaji Bora wa Msimu wa Ligi Kuu ya Afrika Kusini. Ubora wake haukuishia hapo katika msimu wa 2025/26, Makgalwa aliendelea kuwa miongoni mwa wachezaji wanaotengeneza nafasi nyingi za mabao, akichangia asisti saba kwenye ligi, huku akiendelea kuwa silaha muhimu ya Sekhukhune United ...

Alphonce Mabula ni Yanga

Picha
Yanga wako kwenye hatua za mwisho za kukamilisha usajili wa kiungo Raia wa Tanzania,Alphonce Mabula Msanga. Kambi ya Mabula imekubaliana na ofa ya mwisho ambayo imetumwa na Yanga na sasa wanajadili namna ya ulipaji wa pesa hiyo. Mkataba wa miaka mitatu utasainiwa pale ambapo kila kitu kitakamilika. Mabula ana ofa tatu za Ulaya ila sasa ni kama anaelekea Yanga

Simba yawaashia taa ya kijani Slavia Prague

Picha
SIMBA rasmi wamewajibu Mabingwa wa Jamhuri ya Czech, Slavia Praha kuwa wanawapa siku 14 tu za majaribio pamoja na vipimo vya afya kwa Beki wao Hussein Ally Mbegu na sio miezi mitatu kama ambavyo Praha walitaka hapo awali kwakuwa wana mipango nae kuelekea msimu mpya endapo majaribio hayatofanikiwa. Praha wanaoshiriki UEFA Champions League wamekubaliana na masharti ya Simba na tayari Kijana na Menejiment yake wameanza mchakato wa VISA ili asafiri haraka iwezekanavyo kuelekea barani Ulaya.

Karia kufuta Ligi Kuu ya vijana

Picha
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia, amesema hana hofu na vilabu vikubwa kama Simba na Yanga katika kufanya maamuzi yenye maslahi ya soka la Tanzania. Karia amesisitiza kuwa anaongozwa na kanuni badala ya busara au shinikizo kutoka kwa wadau. Kiongozi huyo amesema moja ya mipango yake ni kuifuta Ligi ya U-20 kutokana na kile alichodai kuwa wachezaji wengi wanaoshiriki hawachezi katika umri unaostahili. Badala yake, amependekeza ligi hiyo ibadilishwe na kuitwa ligi ya wachezaji wa akiba ili kuondoa changamoto zinazohusiana na udanganyifu wa umri. Karia pia amesema atakutana na wadhamini wa mashindano hayo kujadili hatma ya ligi hiyo na kuona namna bora ya kuiboresha. Kauli yake tayari imeibua mjadala mkubwa miongoni mwa wadau wa soka, huku wengi wakisubiri kuona uamuzi rasmi kuhusu mustakabali wa Ligi ya U-20 nchini

Simba yaonesha jeuri ya pesa, yagomea hoteli

Picha
Wakati vilabu vingine ambavyo vinashiriki michuano ya CECAFA Kagame Cup 2026 vikifikia kwenye hoteli ambazo zinalipiwa na CECAFA zenye hadhi ya nyota tatu. Simba iliwajulisha CECAFA kwamba itafikia kwenye hoteli yenye hadhi ya juu zaidi na italipa gharama zote za ziada ili kuendana na hadhi na ukubwa wa klabu yao baada ya Raisi wa heshima wa klabu hiyo Mohammed Dewji kuagiza kwamba wanastahili kuhukua hotel ya hadhi ya nyota 5 na atalipia kila kitu yeye! Hivyo Simba wamefikia hoteli ya nyota 5 ya Mövenpick yenye hadhi ya juu zaidi jijini Kigali ambayo Gharama ya chini ya chumba ambacho kinachotumiwa na staff wa Simba ni Tsh. 450,000 kwa siku moja ikihusisha chai ya asubuhi pekee. Simba wamesafiri na chakula chao kutoka Tanzania ambacho watatumia muda wote ambao kikosi kitakuwepo nchini Rwanda.