Machapisho

Omari Omari rasmi Singida Black Stars

Picha
Singida Black Stars FC imekamilisha usajili wa kiungo Omary Omary kutoka Mashujaa FC ambayo anaitumikia kwa mkopo akitokea Simba SC. Omary Jr alikuwa na mkataba wa miaka mitatu na Simba SC na mpaka sasa Singida Black Stars ilishamalizana na Simba SC kwa uhamisho huo kwa kila kitu!

Dkt Nchinbi atembelea uwanja wa Samia Arusha

Picha
Makamu wa Rais Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Uwanja wa Arusha, utakaotumika katika fainali za AFCON 2027, unaojengwa jijini Arusha. Dkt. Nchimbi amepongeza maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo, ambapo amesema ni faraja kuona ahadi ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa ili kuvutia michuano hiyo kufanyika nchini Tanzania, inatakelezwa kikamilifu. Makamu wa Rais amemshukuru Rais kwa kuendelea kutoa fedha ili kuhakikisha uwanja huo unakamilika kwa wakati. Dkt. Nchimbi ameishukuru Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na mkoa wa Arusha, wakandarasi na mshauri Elekezi kwa kazi waliyofanya katika Uwanja huo. Makamu wa Rais amewataka viongozi wa wizara pamoja na Mkoa wa Arusha kusimamia vema agizo la Rais Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha barabara zinazotumika katika kufika uwanjani hapo zinakamilika kwa wakati.

Kagere amkosoa Ibrahim Doumbia

Picha
Aliyekuwa mshambuliaji hatari wa Simba SC na timu ya taifa ya Rwanda, Medie Kagere, amefunguka na kueleza kusikitishwa kwake na nafasi ya goli aliyokosa mshambuliaji mpya wa Wekundu wa Msimbazi, Ibrahim Doumbia raia wa Mali. ​Akizungumzia tukio hilo lililokea katika mchezo wao wa CECAFA Kagame Cup, Kagere amesema: ​🗣️ "Kwangu binafsi, ile naichukulia kama ni nafasi ya dhahabu kwa mshambuliaji. Sijui ni kwa nini alichagua kufunga kwa namna ile; angechagua namna nzuri ya kufunga, lingekuwa ni goli rahisi." ​Unadhani Doumbia alikosa umakini au presha ya mechi za mwanzo imemshika ndani ya Simba SC? Dondosha maoni yako!

Bodi ya Ligi kuanzisha sheria mpya kwa wachezaji wa kigeni

Picha
Bodi ya Ligi Tanzania inatarajiwa kuanzisha kanuni mpya ya usajili wa wachezaji wa kigeni itakayoanza kutumika kuanzia msimu wa 2026/27 wa Ligi Kuu ya NBC. Kwa mujibu wa kanuni hiyo mpya, mchezaji wa kigeni atakayehitaji kusajiliwa na klabu yoyote ya Ligi Kuu ya NBC atalazimika kuwa ameiwakilisha nchi yake katika timu ya taifa ya U-17, U-20 au timu ya taifa ya wakubwa, kuanzia mwaka 2024 na kuendelea, ili aweze kustahili kusajiliwa. Hata hivyo, sheria hiyo haitawahusu wachezaji wa kigeni ambao tayari walikuwa wakicheza Ligi Kuu ya NBC katika msimu wa 2025/26 au misimu iliyotangulia. Hivyo, wachezaji hao wataendelea kustahili kucheza bila kulazimika kutimiza sharti hilo jipya.

Libasse Gueye anauzwa

Picha
Klabu ya Simba SC inadaiwa kupokea ofa mbili kutoka nje ya Tanzania kwa ajili ya winga wake wa Senegal, Libasse Gueye.OFA ya kwanza imetoka kwa klabu ya Morocco yenye thamani ya $500,000 (takribani Sh bilioni 1.3), wakati ofa ya pili kutoka klabu ya Qatar inatajwa kuwa na thamani ya $700,000 (takribani Sh bilioni 1.8). Hata hivyo, Simba inadaiwa kuwa tayari kumuuza nyota huyo endapo italetewa ofa ya $1,000,000 (takribani Sh bilioni 2.6).Endapo Libasse Gueye ataondoka Msimbazi, Simba inatarajiwa kuelekeza nguvu zake kwenye usajili wa winga mwingine wa kigeni ili kuziba nafasi yake katika kikosi.

Seleman Mwalimu Simba haina mamlaka ya kumtumia

Picha
Klabu ya Simba SC bado haina mamlaka ya kumtumia mshambuliaji Seleman Mwalimu Kwenye mchezo wowote ule bila idhini ya klabu yake mama ya Wydad AC, Katika mchezo wa leo wa CECAFA KAGAME CUP dhidi ya klab ya Mogadishu City Club Seleman Mwalimu hakujumuishwa, Klab ya Simba inapambana kuhakikisha inampata mshambuliaji huyo kwa mkataba wa mkopo kama ilivyokuwa hapo awali,

Simba yashikws shati na Mogadishu

Picha
Wawakilishi wa Tanzania bara katika michusno ya Kagame Cup, Simba usiku huu wameanza vibaya baada ya kutoka sare ya 0-0 na timu ya Mogadishu City Club ya Somalia. Mashindano hayo yanafanyika nchini Rwanda na kudhaminiwa na klabu ya Al Hilal ya Sudan, tumeshuhudia Simba na Mogadishu wakicheza soka zuri na lenye ufundi. Almanusura Simba ipate bao dakika za mwisho mwisho kupitia mshambuliaji wake mpya Ibrahim Doumbia baada ya kugongesha mwamba. ​Katika mchezo mwingine wa kundi hilo, Jamus SC kutoka Sudan Kusini imeilaza Singida Black Stars kwa mabao 2-0 na kushika usukani wa kundi hilo.