Aliyekuwa Waziri na Mwanachama wa Simba SC, Dr. Hamisi Kigwangalla, ameibua mtafaruku mpya Msimbazi baada ya kuweka wazi nia yake ya kuvunja kile alichokiita "utawala wa mtu mmoja". Huku akitangaza kuwa yuko tayari kuweka fedha taslimu (cash) mezani kununua hisa za mwekezaji mkuu wa sasa, Mohammed 'Mo' Dewji. Kigwangalla ameyasema hayo huku akijibu shinikizo la baadhi ya wanasimba wanaomtaka agombee nafasi ya Uwenyekiti wa Simba SC kwenye uchaguzi ujao. Sina Hamu na Siasa za Mpira, Tatizo ni Mfumo" Akieleza sababu za kukataa kuingia kwenye kinyang'anyiro cha Uwenyekiti kwa sasa, Dr. Kigwangalla amebainisha kuwa tatizo la Simba silo uongozi wa mtu mmoja, bali ni muundo mbovu wa uendeshaji (governance) na umiliki wa klabu (ownership). "Kwanza, sijioni nikijikita kwenye siasa za mpira wa miguu wa klabu kubwa kama Simba. Pili, naamini tatizo la Simba si mtu mmoja. Tatizo kubwa ni mfumo wa uongozi na umiliki," alisema Kigwangalla. Mpango wa Kuondoa '...