Machapisho

Singida Black Stars balaa, yamrudisha mfungaji bora msimu uliopita

Picha
Singida Black Stars imekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Jean-Charles Ahoua, kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kuondoka CR Belouizdad ya Algeria kama mchezaji huru. Taarifa za usajili huo zinaeleza kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 atakuwa sehemu ya kikosi cha Singida kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Kagame. Ahoua anarudi Tanzania miezi michache baada ya kuondoka Simba SC, ambako aling'ara kwa kiwango bora na kuwa mmoja wa viungo waliovutia zaidi katika Ligi Kuu Bara kabla ya kuhamia CR Belouizdad mapema mwaka huu. Usajili huo unatajwa kuwa nyongeza kubwa kwa Singida Black Stars, ambao wanaendelea kuimarisha kikosi chao kwa ajili ya mashindano ya ndani na kimataifa. Mashabiki sasa wanasubiri kumuona Ahoua akianza rasmi maisha mapya akiwa na jezi ya Singida Black Stars kwenye michuano ya Kagame Cup.

Seleman Mwalimu aongeza mmoja Simba

Picha
Mshambuliaji wa Simba Selemani Mwalimu atakuwa sehemu ya kikosi hicho msimu ujao baada ya kuongeza mwaka mwingine mmoja.  Mwalimu amekuwa na msimu mzuri baada ya kufanikiwa kuongoza kwa mabao kwenye kombe la CRDB Cup ambapo Simba ndio mabingwa.

Wiki ya Wananchi ni Agosti 9

Picha
Mabingwa watetezi wa Ligi kuu soka Tanzania bara (NBC Premier League 2025/26) klabu ya Yanga imethibitisha kuwa Sherehe ya kilele cha "WIKI YA MWANANCHI" itafanyika Agosti 09,2026 kwenye uwanja wa Uhuru Jijini Dar Es Salaam. Aidha, tukio la uzinduzi kuelekea kilele cha tamasha hilo litafanyika Jijini Mwanza  kati ya Agosti 03 au 04,2026.

Neo Maema mguu pande Simba

Picha
Kiungo Neo Maema bado hajafikia makubaliano na Simba SC ya kuongeza mkataba mpya ili kuendelea kuitumikia klabu hiyo kwa msimu ujao baada ya mkataba wake kumalizika! Neo Maema anahitaji mshahara mkubwa ili kubaki Simba SC na hilo ndio jambo linaloleta ugumu sana kuweza kupewa mkataba wa muda mrefu,na Simba SC bado wanamuhitaji Neo Maema abaki kutokana na uzoefu wake kwenye Klabu Bingwa Afrika. Bado mazungumzo yanaendelea baina ya pande zote mbili ili kufikia muafaka wa mwisho kama atabaki Msimbazi au ataondoka mapema sana na kabla ya msimu wa 2025-26 haujamalizika Neo Maema tayari alikuwa na machaguo yake kwa klabu za Afrika Kusini

Injinia Hersi amkaribisha kocha mkuu mpya Yanga

Picha
Rais wa Klabu ya Yanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Shirikisho la Vilabu Afrika (ACA) na Mjumbe wa Kamati ya Mashindano ya Vilabu FIFA, Eng. Hersi Said amemkaribisha rasmi Kocha Mkuu wa Klabu yetu, Manqoba Mngqithi pamoja na benchi lake la ufundi nyumbani kwa Mabingwa wa kihistoria. Tunawatakia kila la heri katika safari hii mpya ya kuendelea kuijenga na kuipeleka Klabu yetu kwenye mafanikio makubwa zaidi

Adolf Mtasigwa mbioni kutua Kaizer Chief

Picha
Kaizer Chiefs anakaribia kukamilisha usajili wa kiungo wa ulinzi Adolf Mtasingwa Bikego (27) kutoka Azam FC kwaajili ya kuitumikia klabu hiyo kwa msimu ujao! Kaizer Chiefs wanamalizia baadhi ya vitu kadhaa vya kimaslahi baina yao na Matajiri wa Chamazi ili kukamilisha kila kitu na mchezaji kusaini mkataba wa Amakhosi.

MO Dewji uso kwa uso na wachezaji wapya Simba

Picha
Rais wa Simba SC, Mohammed Dewji amekutana na kufanya mazungumzo na wachezaji wapya watatu ambao tayari wametambulishwa Kelvin Nashon, Nathaniel Chilambo na Bakari Msimu. Mo Dewji amewakaribisha wachezaji hao kwenye familia ya Simba na kuwaeleza malengo ya Simba ya ndani na kimataifa na hivyo kuwataka kujituma wakati wote wanapokuwa kwenye majukumu ya kuipambania nembo ya klabu. Mwenyekiti wa Bodi, Crescentius Magori alikuwepo pia katika kikao hicho.