Machapisho

Simba yatupwa nje Kagame Cup

Picha
Simba SC imehitimisha rasmi safari yake katika michuano ya CECAFA Kagame Cup 2026 baada ya kushindwa kufuzu hatua ya nusu fainali kufuatia matokeo ya michezo ya hatua ya makundi. Baada ya kukusanya pointi mbili pekee katika michezo yake miwili ya kwanza, Simba ilijikuta katika nafasi ngumu ya kusonga mbele. Hata kama itaibuka na ushindi katika mchezo wake wa mwisho dhidi ya Singida Black Stars na kufikisha pointi tano, idadi hiyo haitatosha kuiwezesha kuwa miongoni mwa timu bora zilizomaliza katika nafasi ya pili zitakazofuzu hatua inayofuata. Hali hiyo imechangiwa na matokeo ya makundi mengine, ambapo Al Hilal na Rayon Sports tayari zimekusanya pointi sita kila moja, na hivyo kuondoa uwezekano wa Simba kuingia katika orodha ya timu zitakazofuzu nusu fainali. Kutokana na matokeo hayo, Simba SC inaaga rasmi michuano ya CECAFA Kagame Cup 2026 na sasa itaelekeza nguvu zake katika kujiandaa na msimu mpya wa mashindano ya ndani na kimataifa.

Wydad yamrejesha kundini Seleman Mwalimu "Gomez"

Picha
Selemani Mwalimu yupo jijini Dar Es Salaam akishughulikia safari yake ya kuelekea Morocco kwaajili ya maandalizi ya msimu mpya. Kocha mpya wa Wydad, Paulo Sergio anataka kuwaona wachezaji wote kambini kabla ya kufanya maamuzi.

Yanga yazima tetesi za Feitoto kutua Yanga'

Picha
Baada ya kuzagaa kwa tetesi zinazomhusisha kiungo wa Azam FC, Feisal Salum, na kujiunga na Yanga, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Ally Kamwe, amesema hakuna mazungumzo yoyote yanayoendelea kati ya pande hizo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Kamwe amesema Yanga tayari imekamilisha usajili wa wachezaji wa ndani, hivyo Feisal si sehemu ya mipango ya klabu hiyo. "Feisal Salum ni mchezaji mzuri sana, lakini Yanga SC tumeshafunga usajili wetu wa ndani. Hakuna mazungumzo yoyote kati ya Yanga na Fei/Azam," ameandika Kamwe. Aidha, ameeleza kuwa nafasi mbili za usajili zilizobaki klabuni hapo ni kwa ajili ya wachezaji wa kimataifa pekee.

Al Hilal yaitoa mashindanoni KVZ

Picha
Al Hilal imepata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya KVZ katika mchezo wa mzunguko wa pili wa kundi C la CECAFA Kagame cup 2026. Ushindi huu unawafanya Al Hilal wapande kwenye kilele cha msimamo wa kundi C wakiwa na points zao 6. Mchezo wa kundi C unaofuata hivi punde ni kati ya Rayon Sports dhidi ya Tusker FC.

Arajiga aweka historia Kagame Cup

Picha
Ahmed Arajigga anakua mwamuzi wa kwanza kutoka Tanzania kuchezesha michezo miwili mfululizo ya kombe la CECAFA. Muda huu anasimamia mchezo wa hatua ya makundi kati ya Tusker dhidi ya Rayon Sports. Mashindano hayo yanafanyika ndani ya Rwanda.

Sakata la Seleman Mwalimu lafikia pabaya

Picha
Mshambuliaji wa Simba SC Seleman Mwalimu ameondoka kambini kwa timu hiyo mjini Kigali, Rwanda, na kurejea Dar es Salaam huku hatma yake ndani ya kikosi hicho ikiendelea kujadiliwa. Taarifa zinaeleza kuwa uongozi wa Simba unatarajia kuanza mazungumzo na klabu ya Wydad Athletic Club ya Morocco kwa lengo la kufikia makubaliano yatakayomwezesha mshambuliaji huyo kuendelea kuitumikia Simba kwa msimu mmoja zaidi kwa mkopo. Hata hivyo, endapo pande hizo mbili hazitafikia mwafaka, mchezaji huyo atalazimika kurejea Wydad, ambayo bado inamiliki haki za kimkataba za mshambuliaji huyo. Hatua hiyo inatajwa kuwa sehemu ya jitihada za Simba kuhakikisha inaendelea kuwa na kikosi imara kuelekea msimu mpya wa mashindano.

Mbegu wa Simba kupaa Czech

Picha
Muda wowote kuanzia sasa kinda wa Simba,Hussein Ally Mbegu (17) atapaa kwenda Czechia ili kufanya majaribio ya wiki mbili na klabu ya Slavia Prague. Simba wametoa ruhusa ya Mchezaji huyo kwenda Czechia ili kujaribu baati yake na kama atafuzu biashara itafanyika. Kwa sasa Mchezaji huyo anahangaikia Viza na muda siyo mrefu ataondoka nchini. Kama biashara hiyo itafanikiwa Simba wataweka kipengele cha “sell-on clause” kama walivyofanya kwa Mbwana Samatta siku za karibuni.