Seleman Mwalimu aisawazishia Yanga
Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika Dar Young Africans maarufu Yanga, usiku huu wamenusurika kulala baada ya kutoka sare ya 1-1 na Gaborone United uwanja wa Taifa nchini Botswana. Gaborone United walikuwa wa kwanza kupata bao kipindi cha kwanza lililofungwa na Obry Amseb dakika ya 33 kwa mpira wa kutenga, iliwachukua Yanga dakika ya 90 kusawazisha goli hilo likifungwa na Seleman Mwalimu Gomez. Yanga wanapata sare muhimu ya 1-1 ugenini baada ya bao la dakika za mwisho