Klabu ya Young Africans (Yanga SC) imefanya uzinduzi wa kipekee wa jezi zao mpya zitakazotumika katika michuano ya kimataifa ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika (CAF Champions League) kwa kumtumia mwandishi nguli wa habari za usajili duniani, Fabrizio Romano. Uzinduzi huo wa aina yake umefanyika kupitia video iliyochapishwa kwenye ukurasa wa Instagram wa @liveherewego unaomilikiwa na mwandishi huyo. Katika video hiyo, Fabrizio Romano anaonekana akifungua kisanduku maalum chenye jezi tatu mpya za Yanga zilizotengenezwa kwa ajili ya ushindani wa barani Afrika. Mwandishi huyo maarufu alitumia fursa hiyo kuitambua na kuipongeza klabu hiyo, huku akiitaja rasmi Yanga kama klabu kubwa zaidi nchini Tanzania. Pamoja na kuzionyesha jezi hizo kwa mashabiki wa soka ulimwenguni, Romano alihitimisha ujumbe wake kwa kutumia msemo maarufu unaotumiwa na Wana-Yanga pamoja na mdhamini wao GSM wa "Yanga Bingwa". Hatua hii ya masoko imepokelewa kwa hisia kubwa na mashabiki wa soka nchini, ikio...