Nilimfahamu King Kinya tangu mwaka 1998
Nilimfahamu King Kinya katika ofisi za gazeti la Majira nakumbuka ilikuwa mwaka 1998, nadhani nilipeleka hadithi yangu itokee gazetini. Kinya alikuwa anachora katuni tena enzi hizo alikuwa na umri wa miaka 14, mimi pia nilikuwa na umri kama wake, nilimfahamu King Kinya akiwa na wenzake Masoud Kipanya, Bondaboy, Nathan Mpangala, Noah Yongolo na wengineo. Kifo chake kimenisikitisha ila kazi yake mola aina makosa, hayo ni maneno ya Prince Hoza ambaye anamuelezea marehemu kwamba alifanya naye kazi kuanzia gazeti la Majira ingawa yeye alipita tu na kutimkia magazeti mengine Enzi za uhai wake King Kinya akichora katuni zake Miongoni mwa michoro yake Alikuwa anachora katuni Sanaa za King Kinya