Timu ya Yanga SC usiku huu imepata ushindi mnono wa mabao 7-1 dhidi ya Polisi Tanzania uwanja wa KMC Complex jijini Dar es Salaam mchezo wa kombe la CRDB. Kwa matokeo hayo Yanga SC inaungana na Simba SC kutinga hatua ya 16 bora, mabao ya Yanga yamefungwa na Mudathir Yahya dakika ya 01, Laurindo Depu 22, ambaye pia alifunga mabao mengine mawili dakika ya 32 na 59, mabao mengine yamefungwa na Joseph Majagi dakika ya 38, Bubah Jammeh dakika ya 76 na Abdulnassir Mohamed "Casemilo". Goli la Polisi Tanzania limefungwa na beki wa Yanga, Frank Assink dakika ya 81. Hata hivyo mshambuliaji wa Yanga, Laurindo Depu ameondoka na mpira wake baada ya kufunga mabao matatu.