Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

NABII MUSA KIONGOZI WA WANAISRAEL

Machapisho ya hivi karibuni

Simba yambakiza nahodha wake Kwa kumpa mkataba

Nahodha wa Klabu ya Simba SC, Rushine De Reuck ameongeza mkataba wa mwaka mmoja wa kuendelea kuitumikia Klabu ya Simba SC mpaka June 2027. . Rushine mwenye umri wa miaka 29 amesinya mkataba huo jana .

Yanga yatishia kujitoa Ligi Kuu bara

Klabu ya Yanga SC imeripotiwa kuwa tayari kususia Ligi Kuu Tanzania Bara iwapo hatua kali hazitachukuliwa dhidi ya Simba SC, huku wakidai kuwepo kwa upendeleo katika maamuzi mbalimbali ya ligi. Taarifa zinaeleza kuwa viongozi wa Yanga hawaridhishwi na namna baadhi ya matukio yanavyoshughulikiwa na mamlaka za soka nchini, wakisisitiza kuwa wanahitaji usawa na haki kwa klabu zote zinazoshiriki ligi. Inadaiwa kuwa endapo Simba haitachukuliwa hatua stahiki kulingana na kanuni za ligi, Yanga wanaweza kuchukua uamuzi wa kususia baadhi ya mechi kama njia ya kuonesha kutoridhishwa kwao. Hata hivyo, hadi sasa mamlaka zinazosimamia ligi bado hazijatoa tamko rasmi kuhusu suala hilo.

Mbuni yaitupa nje Mtibwa Sugar kombe la CRDB

TIMU ya Mtibwa Sugar imetupwa nje ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Hatua ya 32 Bora michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya kufungwa 1-0 na Mbuni jioni ya leo Uwanja wa Jamhuri, Dodoma. Bao pekee la Mbuni inayoshiriki Ligi ya ya Championship lililoitupa nje Mtibwa Sugar inayocheza Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara limefungwa na Omary Athumani dakika ya 33. Mchezo mwingine wa Hatua ya 32 Bora Kombe la CRDB leo, timu nyingine ya Championship, TMA Stars ya Arusha imeitoa Tanzania Prisons ya Ligi Kuu kwa kuichapa 1-0 bao la Ernest Baltazari dakika ya 39 Uwanja wa Halmashauri ya Wilaya Chunya Jijini Mbeya. Nayo Mbeya City imeitoa Bandari FC kwa kuichapa 3-0 mabao ya Vitalis Mayanga dakika ya 16 na 55 na Riphat Msuya dakika ya 76 Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.

Yusuph Kagoma aongeza miwili tena

Klabu ya Simba imefanikiwa kumuongezea mkataba miaka miwili (2) mchezaji wao Yusuph Kagoma ambapo utatamatika 2028 mwezi June. Simba inajiimarisha vyema kuelekea msimu ujao kwaajili ya michuano ya kimataifa

Yanga yaipiga Polisi Tanzania 7-1, Depu aondoka na mpira wake

Timu ya Yanga SC usiku huu imepata ushindi mnono wa mabao 7-1 dhidi ya Polisi Tanzania uwanja wa KMC Complex jijini Dar es Salaam mchezo wa kombe la CRDB. Kwa matokeo hayo Yanga SC inaungana na Simba SC kutinga hatua ya 16 bora, mabao ya Yanga yamefungwa na Mudathir Yahya dakika ya 01, Laurindo Depu 22, ambaye pia alifunga mabao mengine mawili dakika ya 32 na 59, mabao mengine yamefungwa  na Joseph Majagi dakika ya 38, Bubah Jammeh dakika ya 76 na Abdulnassir Mohamed "Casemilo". Goli la Polisi Tanzania limefungwa na beki wa Yanga, Frank Assink dakika ya 81. Hata hivyo mshambuliaji wa Yanga, Laurindo Depu ameondoka na mpira wake baada ya kufunga mabao matatu.

Ahoua afunga bonge la goli CR Belouizdad

Kiungo Mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Jean Charles Ahoua hapo jana aliifungia bao Klabu yake ya CR Belouizdad kwenye ushindi wa bao 3-0 dhidi ya MB Rouisat kwenye mchezo wa Ligi Kuu Nchini Algeria. . Ahoua mwenye umri wa miaka 24 alisajiliwa na Klabu hiyo akitokea Simba SC ya Tanzania.