Machapisho

Aisha Masaka arejea Brighton

Picha
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Aisha Masaka, amerejea rasmi kikosini na kuanza mazoezi na wachezaji wenzake wa klabu ya Brighton & Hove Albion ya nchini Uingereza kufuatia kupona majeraha makubwa ya goti yaliyomweka nje ya uwanja kwa muda mrefu tangu mwaka 2025. ​Mshambuliaji huyo tayari yupo nchini Uingereza akifanya programu za uwanjani zinazolenga kumpa utimamu wa mwili na kurejesha kiwango chake cha ushindani kabla ya kurejea rasmi kwenye michezo ya kimashindano. Kurejea kwake kumeleta matumaini makubwa kwa benchi la ufundi la Brighton pamoja na timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania, Twiga Stars, ambazo zote zinanufaika na uwezo wake wa kupachika mabao. ​Hatua hii ni pigo lililogeuka kuwa furaha, ikizingatiwa kuwa majeraha hayo ya goti yalimnyima fursa ya kushiriki mashindano makubwa ikiwa ni pamoja na Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON). Kurejea kwake uwanjani kunatajwa kuwa msukumo mpya katika ushindani wa nafasi ya kikosi cha kwanza ndani ya k...

Dudubaya mbaroni

Picha
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, ametoa agizo kwa Jeshi la Polisi kumtafuta na kumfikisha mbele ya vyombo vya sheria msanii Godfrey Tumaini maarufu Dudubaya, baada ya kushindwa kuitikia wito wa Wizara hiyo. Aidha, Katambi amesema Dudubaya alikuwa ametakiwa kufika Wizara ya Mambo ya Ndani baada ya kutajwa katika tuhuma za makosa ya jinai, lakini licha ya kuitwa kwa mara ya pili, bado hakufika. Waziri amesema Dudubaya ameonekana kwenye mitandao ya kijamii akitoa kauli ambayo Waziri ameielezea kuwa ni kukaidi wito wa Serikali.

Kadi nyekundu ya Sillah yafutwa

Picha
Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imefuta adhabu ya kadi nyekundu aliyooneshwa mchezaji wa Azam FC, Gibril Sillah, katika mechi dhidi ya Kagera Sugar, baada ya kujiridhisha kupitia picha jongeo na taarifa ya wataalamu kuwa mchezaji huyo hakustahili adhabu hiyo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TPLB, uamuzi huo umefikiwa kwa kuzingatia Kanuni ya 12:8 ya Ligi Kuu kuhusu usimamizi wa ligi. Aidha, mwamuzi wa akiba wa mchezo huo, Greyson Buchard kutoka Kagera, amepewa onyo kali kwa kosa la kuonyesha mapungufu ya kiuchezaji yaliyotokana na kushindwa kutafsiri vema sheria za mpira wa miguu. Kwa upande mwingine, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Singida Black Stars, Hussein Massanza, ametozwa faini ya shilingi milioni 10 kwa kosa la kumshutumu na kumtolea lugha ya matusi mwamuzi wa kati wa mchezo kati ya Singida BS na Simba SC kupitia chapisho moja la mtandaoni, kinyume na kanuni za Ligi Kuu.

Simfuatilii kocha wa Gaborone United - Manqoba

Picha
Kocha wa Yanga SC, Manqoba Mngqithi ameibua hisia za wengi kwa kusema amekuwa akimfuatilia Sean Connor, kocha wa Gaborone tangu ametua klabuni hapo. Kwa upande wangu mimi nimeona mwenzangu yuko vizuri lakini hakuna namna ni lazima tupate ubingwa kivyovyote vile. Nimesoma nyakati zake zote pia nimeangalia wachezaji alio nao, ambao mimi ninawafahamu vizuri na kuweka mkazo juu ya wachezaji hao. Kipindi cha kwanza nitasoma michezo kwa maana na yeye atakuja kwa nguvu ili asipoteze mchezo wa nyumbani. “Kwa upande wa ulinzi ni timu imara. Hairuhusu mabao mengi na pia ni hatari sana inapofanya mashambulizi ya kushtukiza pamoja na mipira iliyokufa (set pieces). Sijui kutokuwepo kwa Mothusi Johnson na Mpho Kgwaswane kutakuwa na athari gani kwa timu yao kwa sababu wote walikuwa wachezaji muhimu sana. Hata hivyo bado wana kipa mwenye uzoefu pamoja na wafungaji wawili wazuri na kipa kutoka Namibia. Pia wana beki wa kulia mwenye uwezo mkubwa” Manqoba Mngqithi.

Gamondi atangaza kikosi, Mwalimu wa Yanga ndani

Picha
Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Miguel Ángel Gamondi, ametangaza kikosi cha awali cha wachezaji watakaoingia kambini kujiandaa na michezo ya kufuzu Ligi ya Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 dhidi ya Guinea Bissau na Madagascar, pamoja na mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Ghana. Makipa: Zuberi Foba (Azam FC), Aishi Manula (Azam FC), Yona Amos (Singida BS), Metacha Mnata (Singida BS), Hussein Masalanga (Young Africans). Mabeki: Ibrahim Bacca (Young Africans), Bakari Mwamnyeto (Young Africans), Lameck Lawi (Azam FC), Twalib Nuru (Azam FC), Vedastus Masinde (Simba SC), Mohammed Mussa (Young Africans), Danillo Maino (FK Panevezys, Lithuania), Haji Mnoga (Patro Eisden, Ubelgiji), Bakari Msimu (Simba SC), Nickson Kibabage (Simba SC), Mohammed Hussein (Young Africans), Anthony Mligo (Simba SC), Pascal Msindo (Azam FC), Nathaniel Chilambo (Simba SC). Viungo: Novatus Miroshi (Göztepe, Uturuki), Himid Mao (Azam FC), Adolph Mtasingwa (Kaizer Chiefs, Afrika Kusini), Yusuf...

Massanza wa Singida Black Stars apigwa faini Mil 10

Picha
Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imepitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi na kutoa maamuzi kadhaa katika kikao chake kilichofanyika Septemba 3, 2026. Miongoni mwa maamuzi yaliyotolewa ni kumtoza Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Singida Black Stars, Hussein Massanza, faini ya Sh. milioni 10. Massanza ameadhibiwa kwa kosa la kushutumu na kutumia lugha ya matusi dhidi ya mwamuzi kupitia moja ya machapisho yake kwenye mtandao. Kwa mujibu wa TPLB, kitendo hicho ni kinyume na Kanuni ya 49:3 na 49:4 ya Ligi Kuu Tanzania, zinazohusu udhibiti na mwenendo wa Maofisa Habari wa Klabu. Kamati imesisitiza kuwa maofisa wa klabu wanapaswa kuzingatia kanuni na taratibu za mashindano katika matumizi ya majukwaa ya mawasiliano, ikiwemo mitandao ya kijamii.

Mimi sijawahi kufikiria suala la kwenda Yanga - Chama

Picha
Kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Zambia, Clatous Chama wa Simba ya Tanzania, amefunguka yafuatayo kwamba hakuwahi kuwaza wala kuota kucheza Yanga ila ilitokea tu. "Nashukuru Mungu sikuchukua muda mrefu pale kwasababu sijawahi kufikiria suala la kwenda Yanga, ilitokea tu” “Nilikuwa kwenye wakati mgumu lakini ninachoweza kusema ni kwamba, nimerudi Simba na siku niliyosaini Simba nilifurahi sana hata familia yangu ilifurahi”