TIMU ya Simba SC imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Mabao ya Simba SC leo yamefungwa na mshambuliaji mzawa, Suleiman Abdallah Mwalimu dakika ya 19 na beki wa kati raia wa Afrika Kusini, Rushine De Reuck kwa penalti dakika ya 45. Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 22 katika mchezo wa tisa na kusogea nafasi ya nne, wakati Tanzania Prisons inabaki na pointi zake 12 za mechi 14 sasa nafasi ya 14 kwenye ligi ya timu 16. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.
MAMBO UWANJANI
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com