Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Azam FC yanusurika kichapo mbele ya Pamba Jiji

Machapisho ya hivi karibuni

Uwanja wa Mkapa wafungwa tena

Serikali imetangaza rasmi kuufunga Uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia Machi 2026 kwa ajili ya awamu ya mwisho ya ukarabati mkubwa kuelekea AFCON 2027. Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amethibitisha kuwa ukarabati huo utachukua kati ya miezi 6 hadi mwaka mmoja, ukilenga zaidi kuboresha: Eneo la kuchezea (Pitch). Miundombinu muhimu ya uwanja. Nini kitatokea? Hakutakuwa na mechi yoyote itakayochezwa pindi kazi itakapoanza. Timu zote zitalazimika kutafuta viwanja mbadala kwa mechi za ndani na kimataifa. Huu ni uamuzi muhimu kuhakikisha Tanzania inatoa burudani ya kiwango cha dunia mwaka 2027

Singida Black Stars yailaza Coastal Union

WENYEJI, Singida Black Stars wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Airtel mjini Singida. Bao pekee la Singida Black Stars katika mchezo huo limefungwa na mshambuliaji Muivory Coast, Joseph Guédé Gnadou dakika ya 71. Kwa ushindi huo, Singida Black Stars inafikisha pointi 19 katika mchezo wa 11 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya tisa, wakati Coastal Union inabaki na pointi zake 15 za mechi 16 sasa nafasi ya 12.

HISTORIA YA MTUME MUHAMMAD NA UISLAMU-1

Inaandikwa na Fikiri Salum  MUHAMMAD kwa Kiarabu (mwenye kusifika) jina kamili ni Muhammad bin Abd Allah bin Abd Al-:Muttalib Al Hashim anaashiriwa katika dini ya Uislamu kuwa ni MTUME wa mwisho wa mwenyezi Mungu (Allah) kwa binadamu. UTOTO WAKE Muhammad alizaliwa yatima, kwani baba yake alifariki kabla yeye hajazaliwa, hakuishi sana na mama yake (Amina) kwa kuwa naye alifariki dunia, Muhammad akiwa na umri wa miaka sita. Baadaye akachukuliwa na babu yake Abdul Muttalib na kuishi naye kwa muda wa miaka miwili, kisha babu yake naye alifariki. Kazi ya kumlea Muhammad ilimwangukia ami yake Abu Talib ambaye ndiye aliyeishi naye mpaka ukubwa na kumuoza na kumpa himaya wakati alipoanza kazi ya kufikisha ujumbe wa mwenyezi Mungu kwa watu. Kadiri ya hadithi za Kiislamu, ilipokuwa karibu atadhihiri mtume, mapadri wa kinasara na makuhani wa Kiyahudi waliokuwa wakikaa Bara Arabu walikuwa wakiwatayarisha majirani wao wa Kiarabu waliokuwa wakiabudu sanamu, wakiwaambia "karibu ataletwa mtume ka...

Mpinzani wa Yanga, hashikiki Championship

Polisi Tanzania FC inayonolewa na kocha Mbwana Makata haijapoteza mchezo wowote kwenye michezo 5 ya karibuni kwenye ligi ya Championship Tanzania Bara 4-0 V Gunners 1-1 V B19 1-2 V Hausung 2-0 V Stand United 2-0 V Geita Gold FC Michezo 3 inayofuata watacheza dhidi ya BigMan FC , Transit Camp na Kagera Sugar

Ally Kamwe afunguka makubwa Simba kufanya ushirikina, adai goli ni offside

Afisa Habari wa Young Africans, Ally Kamwe, ametoa malalamiko mazito dhidi ya wapinzani wao Simba SC, akidai kuwa mambo mengi yasiyo ya michezo yalitawala kuelekea kupatikana kwa sare ya 0-0 katika dabi iliyopita. Kamwe amedai kuwa kulikuwa na matukio ya utata ya uamuzi pamoja na vitendo vya ushirikina ambavyo viliisaidia Simba kupata alama hiyo moja. ​Katika andiko lake, Ally Kamwe amefunguka yafuatayo: ​"Kwanza ilikuwa OFFSIDE.. Pili, AKASHIKA. Move ikaruhusiwa kuendelea kama hakijatokea kitu. Sitaki kabisa kukumbusha kuwa Mchezaji huyu alitakiwa kufungiwa MECHI 5 kwa kosa la kumpiga kiwiko mchezaji wa Dodoma Jiji ... Sitaki kuwakumbusha, kuwa Waamuzi walishatishiwa kufungiwa Maisha kimpira na kupelekwa JELA kuhusu mechi hii. ​Turidi uwanjani, Watu hawa baada ya mazoezi ya mwisho siku moja kabla ya mchezo, wakagoma kuondoka uwanjani Usiku.. Wakafanya Ushirikina na vurugu za kila aina.. Wakaja kutolewa kwa msaada wa Polisi. ​Hawakumaliza, Siku ya mechi wametumia mlango wa VVIP ku...

Iran kujitoa kombe la Dunia

Iran inafikiria kujiondoa kwenye kombe la Dunia la 2026 huko USA, Canada na Mexico. Kulingana na chapisho la mamlaka la Marca, nchi haijafurahishwa na hali ya wasiwasi inayoongezeka baada ya shambulio la jana la kijeshi na Marekani na Israel. Iran ilifuzu mwezi Machi mwaka uliopita kwa kuongoza Kundi A katika mchujo wa Asia, na hivyo kujihakikishia nafasi ya kucheza Kombe la Dunia kwa mara ya saba. Wamepangwa Kundi G pamoja na Ubelgiji, Misri na New Zealand, huku mechi zao zote zikiwa kwenye ardhi ya Marekani.