Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Duke Abuye ang' ara Harambee Stars, FIFA Series

Machapisho ya hivi karibuni

FIFA Series yamng' arisha Ahmed Arajiga

Mwamuzi wa kimataifa, Ahmed Arajiga, ameendelea kuonyesha kiwango bora kwa kuamua mchezo wa FIFA Series 2026 kati ya Kenya national football team na Grenada national football team uliopigwa Amahoro, Rwanda Arajiga anaendelea kuthibitisha ubora wake kwenye majukwaa ya kimataifa, akiipeperusha vyema bendera ya Tanzania. Wengi wanaamini ni miongoni mwa waamuzi bora nchini, licha ya changamoto za ndani zinazoweza kuathiri maendeleo yake

Allan Okello akwama Uganda

Siku kadhaa zilizopita niliwataarifu hapa kuwa Allan Okello ataichezea timu yake ya mkoa wa Lango kwenye mchezo wa robo fainali ya mashindano ya FUFA Drum dhidi ya mkoa wa Teso. Mchezo wenyewe ulichezwa jana na Allan Okello alishindwa kucheza kwenye mchezo huo ambao ulimalizika kwa timu ya mkoa wake kupata ushindi wa bao 1-0. Sababu za kutocheza kwake ni zuio kutoka kwa viongozi wa klabu yake, Young Africans. Okello alifanya mazoezi na wachezaji wenzake wa timu yake ya mkoa hadi dakika za mwisho, lakini klabu yake ya Yanga SC haikumruhusu kucheza mchezo huo. Yanga kwa sasa inakabiliwa na wimbi kubwa la majeruhi kwa wachezaji wake, hivyo hawakutaka kuchukua hatari yoyote ile. Walihofia kwamba anaweza kuumia, hivyo wakamtaka arejee Dar Es Salaam Jumapili asubuhi. Hata hivyo, Allan aliweza kuwashawishi wamruhusu kubaki na kuangalia mechi kama shabiki, lakini hawakumpa ruhusa ya kucheza. Kwa hiyo Allan Okello hakucheza mchezo huo kutokana klabu ilitaka kumlinda ili abaki fiti kwa ajili ya ...

Fukwe ya Coco Beach yafungwa

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule amesema Coco Beach haijauzwa, bali serikali inaboresha ili kulipa hadhi eneo hilo na kudhibiti shughuli zisizokubalika kisheria. "Vijana wengi waliopo pale Coco Beach hawana kazi hawana biashara wanazurura tu na wengine ni walevi wengine wanatumia bangi na wengine wanajiuza sasa tunaishukuru jeshi la polisi kwa kufanya upembuzi yakinifu na kutusanua juu ya hili jambo hivyo sisi kama manispaa ya kinondoni tumeamua kuifanya hili eneo liwe la kistaarabu kwa kuleta wawekezaji wapya ili kuwe na usalama zaidi"

Damaro kuigharimu Yanga, kukatwa pointi tatu za Simba

Klabu ya Simba SC imeweka wazi mpango wake wa kukata rufaa dhidi ya mchezaji wa Yanga SC, Mohamed Damaro ikitaka ipewe alama tatu huku pia iliitaka TFF kuipoka Yanga alama zaidi kutokana na mchezaji huyo kushiriki katika mechi nyingine. Simba SC wameorodhesha hatua 6 ambazo zinafuatwa katika mchakato wa kuhama Shirikisho kwa mchezaji kwa mujibu wa FIFA, ambazo hazikufuatwa. Kwa mujibu wa Regulations Governing the Application of the Statutes (RGAS), maombi ya kubadilisha Shirikisho lazima yapelekwe kwa Players’ Status Committee (PSC) Kuna aina 4, lakini nimechukua hii ambayo Damaro inamhusu tu. b) Kwa wachezaji wanaotaka kubadili chama cha soka (association) baada ya tayari kushiriki katika mashindano rasmi, katika ngazi yoyote au aina yoyote ya mpira wa miguu, kwa niaba ya chama kingine (Kifungu cha 9 aya ya 2 ya RGAS) Mohamedi Damaro Camara ana angukia kipengele (b), kwani akiwa Guinea alishacheza vilabu vya HAFIA FC na MILO FC, lakini mwaka 2019 alikuwemo kwenye kikosi cha Guinea ch...

Dkt Kikwete aipongeza Dar City

Rais mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jopo la Wazee la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, amekutana na timu ya mpira wa kikapu ya Dar City inayoshiriki Michuano ya Ligi ya Mpira wa Kikapu Afrika 2026, inayoendelea jijini Pretoria, Afrika Kusini. Katika mazungumzo hayo, yaliyoihusisha pia timu hiyo pamoja na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF), Hasheem Thabit, na viongozi wengine wa Serikali, Dkt. Kikwete ameipongeza Dar City kwa kufikia hatua hiyo muhimu, akieleza kuwa mafanikio hayo yanaashiria kukua kwa kiwango cha mpira wa kikapu nchini Tanzania. Aidha, amewatia moyo wachezaji wa Dar City kupambana katika mchezo wao unaofuata Machi 31, 2026, akisisitiza umuhimu wa nidhamu, kujituma na kujiamini wanapoingia uwanjani. “Kwa hatua mliyofikia, nina imani kabisa mnaweza kutinga fainali na hatimaye kubeba kombe hili,” amesema Dkt. Kikwete. Dkt. Kikwete yupo nchini Afrika Kusini kwa ziara ya kikazi, ambapo pia amekutana na Rais Cyril Ramaphosa, ...

Makonda aja na ligi yake ya wazawa

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema Wizara hiyo ina mpango wa kuanzisha ligi ya wachezaji wa ndani ili kukuza uwezo wa wachezaji hao. Waziri Makonda ameyasema hayo Mkoani Arusha wakati akifungua kikao kazi cha 16 cha Maafisa Utamaduni na Maafisa Maendeleo ya michezo kinachoendelea mkoani humo. . Mfano kwa sasa ikianzishwa Ligi ya wazawa,klabu ipi itachukua ubingwa asubuhi na mapema?