Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Tunajenga uwanja wa kucheza robo fainali Ligi ya mabingwa Afrika - Injinia Hersi

Machapisho ya hivi karibuni

Simba yapata ushindi wake wa kwanza Ligi ya mabingwa Afrika

Timu ya Simba SC ya Tanzania usiku huu imepata ushindi wake wa kwanza kwenye michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika hatua ya makundi, baada ya kuilaza Stade Malien ya Mali bao 1-0 uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam. Goli pekee la ushindi limefungwa na kiungo mshambuliaji Anicet Oura dakika ya pili ya mchezo, ushindi ambao unaifanya Simba kufikisha pointi 5 lakini ikisalia nafasi ya mwisho. Wakati huo huo timu ya Esperance inaungana na Stade Malien baada ya kushinda mabao 2-0 dhidi ya Petro de Luanda na kufikisha pointi 9 huku Malien licha ya kufungwa imefikisha pointi 11 na kukwea nafasi ya kwanza.

Mamadou Lamine Camara achukua nafasi ya Feitoto, Al Ahli Tripoli

Baada ya kumkosa Fei Toto klabu ya Al Ahli Tripoli ya Libya,imekamilisha usajili wa kiungo hatari wa RS Berkane na timu ya taifa ya Senegal,Mamadou Lamine Camara (23) Camara alisaini mkataba jana Changamoto iliyopo ni kwamba Berkane walichelewesha baadhi ya nyalaka mpaka dirisha la usajili Libya likafungwa ila tayari Tripoli wameomba FIFA ipitishe usajili huo kwani mchezajili anataka kucheza Libya.

Tanzania Prisons yafanya comeback ya kibabe kwa Namungo

Tanzania Prisons yapindua meza kibabe, yaishona Namungo 3-2 Mchezo wa Ligi Kuu ya NBC kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Namungo FC umetamatika ambao umekuwa wakusisimua baada ya Tanzania Prisons, kufanya comeback ya kishujaa kipindi cha pili na kuibuka na ushindi wa magoli 3-2. Namungo FC walionekana kuumiliki mchezo mapema baada ya kupata mabao mawili ya haraka kipindi cha kwanza kupitia kwa Cyprian Kipenye aliyefunga dakika ya 36 kwa mkwaju wa penalti huku chuma cha pili kikiwekwa kambani na Fabrice Ngoy dakika ya 43. Hata hivyo, Tanzania Prisons walirejea kwa nguvu kipindi cha pili na kubadili kabisa mwelekeo wa mchezo baada ya Lambert Sabiyanka alipoanza kupunguza mlima wa magoli dakika ya 49 huku George Mpole akasawazisha dakika ya 71 kwa mkwaju wa penalti na Oscar Mwajanga akafunga bao la tatu la ushindi. Ushindi huu unaipa Tanzania Prisons alama tatu muhimu katika msimamo wa Ligi hiyo.

GSM na MO wote msaada kwa timu zao, ila mmoja ana nidhamu, mwingine mhuni...

Nimewafuatilia GSM na Mo ni matajiri wakubwa Tanzania, wote wana mchango mkubwa sana kwa timu zao Huwezi kutaja maendeleo ya Yanga bila GSM huwezi kutaja maendeleo ya Simba bila Mo Kinachoifanya Yanga kutamba sa hivi ni busara za GSM anajua mipaka yake na anaijua kazi yake vizuri sana Sijawahi kumuona akitoa tamko lolote au kuingilia jambo lolote pale Yanga sababu kuna mtu wake anamuamini ambaye ni Eng Hersi Njoo kwa Mo sasa suala la kuingilia utendaji wa timu na kutoa matamko yanayo zua taharuki kwake ni kitu cha kawaida Tajiri Mo kuna muda aliandika tamko la kususa hadharani, kuna muda pia aliandika tamko kusema kuwa kufungwa goli tano na yanga kuna wachezaji wana hujumu timu bila kuwa na ushahidi wowote, tajiri mo kuna muda aliandika hadharani kuwa simba inahitaji kipa mpya na akamsajili na sijui kipa wake aliishia wapi, juzi hapa kaandika kuulizia mabadiliko ya simba wakati anajua kila kitu kuhusu simba. Shida ya watu wengi wanafikiri mtu kuwa tajiri ndo kujua kila kitu matokeo yak...

688 watuma maombi ya kuinoa timu ya taifa ya Rwanda

Makocha 688 wametuma maombi ya kuifundisha timu ya Taifa ya Rwanda ‘Amavubi’ ambayo imekaa mwezi mmoja bila Kocha Mkuu. Shirikisho la soka la Rwanda (FERWAFA) liliachana na aliyekuwa Kocha wa timu hiyo Adel Amrouche Januari 14, 2026 baada ya kuhudumu kwa mwaka mmoja. Wakati mchakato wa kutafuta mbadala wake ukiendelea, FERWAFA ilitangaza kupokea maombi ya Makocha 688 wenye sifa, ambayo yatafuatiwa na hatua ya mchujo kwa kuzingatia sifa na uzoefu wa kufundisha timu za taifa na ushiriki wao katika michuano mikubwa ikiwemo Kombe la Mataifa ya Afrika na Kombe la Dunia. Rwanda itaandaa mechi za kirafiki za FIFA huko Kigali Machi 2026. Katika michezo hiyo, Rwanda ipo Kundi A pamoja na Estonia, Grenada na Kenya, huku Kundi B likiwa na timu za Aruba, Liechtenstein, Macau na Tanzania.

Ni mechi ya heshima Stellenbosch na Singida Black Stars kwa Madiba

Kocha Othmen Najjar na mchezaji Obasogie Amas wa Singida Black Stars wanasema ni lazima wamalize kwa heshima michuano ya CAF na imekuwa chachu kwao kutamani kurudi tena msimu ujao. Singida BS ipo Afrika Kusini kucheza mechi ya mwisho ya hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC) dhidi ya Stellenbosch. Mechi ni kesho Februari 15, saa 1:00 usiku