Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Wachezaji 7 Yanga kuikosa Namungo FC

Machapisho ya hivi karibuni

Simba SC tayari kuimaliza Tanzania Prisons kesho

Kikosi cha timu ya Simba SC kimeendelea kufanya mazoezi makali Ili kuwakabili wanajeshi wa Magereza, Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu bara utakaopigwa kesho.

Yanga kamili kuivaa Namungo FC kesho

Kikosi cha Yanga SC kimefanya mazoezi yake ya mwisho jioni ya leo kabla ya kuwakabili Namungo FC hapo kesho. Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu bara watashuka dimbani wakitaka kuendeleza rekodi Yao ya ushindi dhidi ya timu hiyo licha ya kucheza kwenye ardhi ya ugenini.

Kocha wa Saudi Arabia anajua maamuzi yake ya kuitosa Morocco

Kocha wa timu ya Taifa ya Saudi Arabia, Herve Renard amedai kuwa anajutia uamuzi wake wa kuitosa timu ya Taifa ya Morocco mwaka 2019 licha ya kuwa na mkataba mrefu. Na kisha timu hiyo kufanya makubwa chini ya Kocha Walid Regragui ambaye alichukua nafasi yake. "Sikupaswa kuondoka, nilikuwa na mkataba wa kuinoa Morocco hadi mwaka 2022, nikaondoka mwaka 2019 lakini hiyo ni sehemu ya makosa unayoweza kuyafanya kazini". -Herve Renard, kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Saudi Arabia. Herve Renard

Yanga tumefeli- Haji Manara

Aliyekuwa Afisa Habari wa klabu ya Yanga SC, Haji Manara "Computer" amesema bila kuogopa kwamba klabu yake ya Yanga imefeli. "Yanga msimu huu tumefeli haiwezekani misimu minne robo fainali moja tu, halafu kila msimu kila dirisha tunasajili wachezaji wapya sita saba kila dirisha na kila msimu kocha mpya, hesabu makocha wangapi wamepita baada ya Nabi isitoshe na nimewaambia ukweli hadi Rais unaenda kusajili Mchezaji wa Kimataifa anakaa benchi na wakati mwingine hapenyi hata kwenye Wachezaji 18 wa mechi yaani tunakaa nae Jukwaani sasa kusajili Mchezaji Kimataifa hana uwezo si ni UCHALE huu?” - Haji Manara, Diwani wa Kata ya Kariakoo na aliyekuwa Msemaji wa Yanga.

JUMA SAID NYOSO: BEKI MTUKUTU UWANJANI ALIYEPITA ASHANTI, SIMBA SC, MBEYA CITY NA KAGERA SUGAR

Na Abdul Makambo 0787905328. JINA la Juma Said Nyoso si geni kwa wapenda soka hapa nchini pi ni jina maarufu katika masuala haya ya mchezo wa soka. Nyoso ni beki au mlinzi wa kati akizimudu namba 4 na 5, miaka ya katikati ya miaka ya 2000 aliibukia kwenye Ligi Kuu bara akiwa kwenye klabu ya Ashanti ya Ilala jijini Dar es Salaam. Akiwa Ashanti ndipo alipoonekana na kocha wa timu ya taifa, Taifa Stars miaka ile Mbrazil Marcio Maximo na kumuita kwenye kikosi cha National team. Juma Nyoso Nyoso ni beki makini wa kati na ana ball control na mtulivu wakati mwingine anacheza soka la kistaarabu kutegemea na mechi lakini kama mechi kubwa kubwa anakua ni mtu hatari na asiependa masihara kiwanjani. Kuna kipindi fulani akiwa Simba alikua pacha wake ni Kelvin Yondan "Vidic"' na hata kwenye timu ya taifa, Taifa Stars pia alikua anasimama na Yondan. Washambuliaji wengi hapa nchini wamekua wanamhofia Nyoso, hata John Bocco na Meddy Kagere walikua wanapata wakati mgumu wakikutana na Nyoso...

Francis Ngoy kinara wa mabao Ligi Kuu bara

Vita ya ufungaji bora Ligi Kuu bara inayodhaminiwa na benki ya NBC, inaweza kuwa mbichi kwani nyota wa timu kubwa na kongwe hapa nchini, Yanga na Simba hawapo kwenye kinyang' anyiro. Lakini sasa mshambuliaji wa timu ya Namungo FC ya Ruangwa mkoani Lindi, Francis Ngoy anaongoza kwa mabao mpaka sasa akiwa amepachika mabao 7. Wanaomfuatia ni Saleh Karabaka ana mabao 6 na Paul Peter wote wa JKT Tanzania ana mabao 5, nyota wa Yanga ambaye ana mabao mengi zaidi ni Prince Dube ana mabao 4. Francis Ngoy kinara wa mabao Ligi Kuu bara