Machapisho

Tshabalala kuongoza parade la ubingwa Jumamosi

Picha
Afisa Habari wa Young Africans SC, Ally Kamwe, ameendelea kuchanja mbuga na utani wa jadi mara baada ya timu yake kutwaa ubingwa, safari hii akimfanyia dhihaka nahodha wa Simba SC, Mohamed Hussein 'Zimbwe Jr'. Kamwe amedai kwa utani kuwa Zimbwe Jr ndiye atakayeongoza gwaride lao la ubingwa Jumamosi akiwa juu ya basi la wazi la Yanga, akijumuisha kijembe kuwa mara ya mwisho kwa beki huyo kufanya gwaride la ubingwa alipanda gari la mizigo aina ya kenta. ​Ujumbe wa Ally Kamwe ulisikika hivi: ​"Mohamed Hussein ndiye atakayeongoza parade letu Jumamosi, atakaa juu pale kwenye lile bus la ubingwa. Mara yake ya mwisho kufanya parade alipanda kenta. ​Jana alinionyesha kivideo cha miaka sijui elfu moja mia nane na ngapi huko, yupo kwenye kikenta anachungulia".

Al Ittihad Iko tayari kumuuza Aziz Ki

Picha
Klabu ya Al Ittihad SC ya Libya ipo tayari kumuuza kiungo wao mshambuliaji Stephane Aziz Ki ikiwa ofa itafika mezani kwao itakayowaridhisha kuelekea msimu ujao wa 2026-27. Al Ittihad SC imeshamlipa ada ya usajili na mishahara yote kwa Aziz Ki na imekanusha taarifa zilizovuma kuwa hawajalipa pesa hizo baada ya Young Africans SC umuhitaji kiungo Aziz Ki arudi klabuni kwao, Al Ittihad SC wanaheshimu mkataba wao na Aziz Ki na washalipa kila mchezaji ada yake ya usajili na mishahara.

Simba yaiomba Bodi ya Ligi ilete waamuzi wa nje ya nchi

Picha
Uongozi wa klabu ya Simba SC umeandika barua kwenda Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) na TFF kuwataka wachague Waamuzi ambao hawana maamuzi mabaya ya kujirudia. Simba SC ipo tayari kughalimikia Bodi ya Ligi na TFF kuleta Marefa kutoka nje ya nchi ikiwa humu ndani itashindikana

Hatuna habari na Fadlu- AliKamwe

Picha
Klabu ya Young Africans SC kupitia kwa Afisa Habari wake, Ally Kamwe, imetolea ufafanuzi wa haraka uvumi unaoendelea mitandaoni kuhusu mchakato wa kusaka kocha mpya. Kamwe ameweka wazi kuwa uongozi haujafanya mazungumzo yoyote na kocha Fadlu Davids na kuwataka mashabiki kupuuza taarifa zote za usajili zinazosambazwa kwa sasa, kwani nguvu zao zote zimeelekezwa kwenye mchezo wa kesho wa kusaka ubingwa. ​Ujumbe wake kamili unasomeka hivi:​"Uongozi wa YANGA SC haujafanya mazungumzo Yoyote wala hauna mpango wa kumuajiri Kocha Fadlu Davis .. ​Ni vile tu watu wanapitia kipindi kigumu kupata Breaking News za YANGA ndio maana wanaanzisha jambo la kulimaliza wenyewe juu kwa juu ​Kwenu Wananchi, Habari sahihi za YANGA SC mtazipata kupitia YANGA APP na Kurasa zetu za Mitandao ya Kijamii za klabu ya YANGA ​Kipindi hiki, Habari yoyote ya Usajili wa Wachezaji au Kocha utakaousoma huku Mitandaoni, Ni UZUSHI na UONGO. ​Kwa sasa, Focus yetu Yote iko kesho. Twendeni Uwanjani Tukapambanie UBINGWA wet...

Rais Samia aipongeza Yanga kutwaa ubingwa

Picha
Ninaipongeza Klabu ya Yanga kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa mara ya tano mfululizo. Mafanikio haya ni ushahidi wa juhudi, nidhamu na kujituma kwa wachezaji, benchi la ufundi, uongozi pamoja na mashabiki. Aidha, ninazipongeza klabu zote zilizoshiriki Ligi Kuu msimu huu kwa ushindani mzuri uliofanya mchezo wa mpira wa miguu nchini Tanzania kuendelea kukua, kuvutia na kuongeza hamasa kwa mashabiki pamoja na wadau wa mchezo huu.

Mangungu afunguka baada ya kukosa ubingwa

Picha
Niwaambie tu kuwa Bingwa wa Ligi Kuu msimu huu amepatikana kwa kupendelewa na kila mtu anajua na Waandishi mnaelewa.. hakuna fair competition na makosa ya kibinadamu yalikuwa ya kutosha kwa marefa waliochezesha mechi za Bingwa (Yanga) ". - Mwenyekiti wa Simba akiongea baada ya mchezo wa Simba SC dhidi ya KMC kumalizika.. akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Young Africans SC kuwa Bingwa wa Ligi kuu msimu huu.

Yanga bingwa Ligi Kuu bara, yarudia historia ya mwaka 1968-1972

Picha
TIMU ya Yanga imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Tanzania jioni ya leo Uwanja wa Meja Jenerali Charles Isamuhyo, Mbweni, Dar es Salaam. Mabao ya Yanga SC leo yamefungwa na mshambuliaji Mzimbabwe, Prince Mpumelelo Dube dakika ya nane, kiungo Maxi Mpia Nzengeli kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na mshambuliaji Laurindo Dilson Maria AurĂ©lio ‘Depu’ kutoka Angola dakika ya 66. Kwa ushindi huo, Yanga SC inamaliza Ligi Kuu msimu wa 2025 – 2026 ikiwa na pointi 75, mbili Zaidi ya watani wao, Simba SC waliomaliza nafasi ya pili baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, KMC FC jioni ya leo Uwanja wa KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam. Hilo linakuwa taji la tano mfululizo la Ligi Kuu kwa Yanga kuanzia msimu wa 2021–2022, 2022–2023, 2023–2024 na 2024–2025 na hiyo inakuwa mara ya pili kwa wana Jangwani hao kutwaa mataji ya Ligi Kuu mara tano mfululizo baada ya kufanya hivyo misimu ya 1968, 1969, 1970, 1971 na 1972. Kwa u...