Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

CAS yathibitisha kupokea rufaa ya Senegal

Machapisho ya hivi karibuni

Diarra atemwa timu ya taifa ya Mali

Golikipa wa Yanga Djigui Diarra hajaitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Mali kwaajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Russia Machi 31. Diarra ni miongoni mwa wachezaji 20 muhimu ambao hawajaitwa kutokana na sababu za kupewa mapumziko na majeraha.

Edward Songo achekelea kukipiga JKT Tanzania na kupewa ajira

Mshambuliaji wa timu ya JKT Tanzania, Edward Songo, amesema kwamba mchezo wa mpira wa miguu umempa ajira kwenye Jeshi la Kujenga Taifa, JKT na anajivunia kucheza soka akiwa muajiriwa wa jeshi hilo. Akizungumza na Sports Extra ya Clouds FM, Songo aliyeibukia vilabu vya Majimaji FC na JKT Mlale zote za mkoani Ruvuma, amesema kujituma na kuwa na nidhamu nzuri vimepelekea yeye kunyakuliwa na JKT Tanzania na baadaye muajiriwa. Amewaasa vijana wenye vipaji kama yeye kuzingatia nidhamu na kujituma kwani yeye anafurahia mafanikio aliyonayo sasa. Edward Songo

Mke wa Rais avamiwa Marekani

Msemaji wa Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo anasema kuwa baadhi ya watu walijaribu kupenya kwenye hoteli anakoishi Mke wa Rais wa nchi hiyo mjini Washington ambaye yuko kwenye ziara kwa mwaliko wa mwenzake wa Marekani,lakini hawakufanikiwa kumdhuru. Katika mkutano na Waandishi wa habari Patrick Muyaya alisema kwamba Serikali ya DRC inashirikiana kwa karibu na mamlaka za Marekani ili kubaini undani wa tukio hilo. Muyaya hakusema iwapo watu hao walifanikiwa kuingia katika chumba alichokuwa akiishi Denise Tshisekedi. Bila kutoa ushahidi, Muyaya alisema kuwa Serikali ya Rwanda inaweza kuwa muhusika.Serikali ya Rwanda haijazungumzia madai hayo mapya yaliyotolewa na Serikali ya DRC. Wataalamu wa Umoja wa Mataifa, DRC na nchi nyingi za Magharibi zinaishutumu Rwanda kwa kuunga mkono kundi la waasi la M23 linalopambana na serikali ya DRC, kwa kuwapatia wanajeshi silaha. Serikali ya Rwanda inakanusha kuunga mkono M23, ikisema kuwa imeweka hatua za kujilinda kiusalama. Denise Nyakeru...

Haruna Niyonzima akiwa kazini Rwanda

Afisa utambuzi wa vipaji wa Shirikisho la soka Rwanda,Haruna Niyonzima tayari ameanza majukumu yake mapya wakati huu akiwa na kikosi cha Rwanda kinachojiandaa na michezo ya FIFA Series. Haruna ni miongoni mwa nyota waliofanya vyema wakiwa na jezi ya amavubi na klabu kadhaa ndani na nje y Rwanda.

Mohamed Salah atangaza kuondoka Liverpool

MSHAMBULIAJI wa Kimataifa wa Misri, Mohamed Salah ametangaza ataondoka Liverpool FC mwishoni mwa msimu huu wa 2025/26 baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa miaka tisa

Jean Charles Ahoua aweka bonge la rekodi

Jean Charles Ahoua ameingia kwenye rekodi ya aina yake baada ya kuingia nusu fainali ya kombe la Shirikisho Afrika mara mbili mfululizo akiwa na timu mbili tofauti Simba SC na CR Belouizdad. Huku akikutana na timu ile ile moja katika Robo fainali mbili za Cafcc na amefanikiwa kuitoa timu hiyo katika hizo robo fainali mbili Al Masry. Msimu Jana Al Masry alikutana na Simba SC katika hatua ya robo fainali na alitolewa na Simba SC Ahoua akiwa sehemu ya kikosi cha wekundu hao wa msimbazi Msimu huu Al Masry ametolewa na Cr Belouizdad katika hatua ya Robo fainali huku Ahoua akiwa sehemu ya kikosi hicho cha Ligue 1 pale Algeria Ahoua amekuwa na Bahati na Al Masry