Na Abdul Makambo KOCHA Sebastian Nkoma ni mmoja wa makocha wazawa waliotoa mchango mkubwa katika maendeleo ya soka hapa nchini Tanzania .Pamoja na nchi yetu wamepita makocha wengi wazawa wenye uwezo na majina makubwa kama Mansour Magram, Joel Bendera, Ray Gama, Ayoub Mohamed, Zacharia Kinanda na Elijah Kategile. Wengine ni Iddi Machupa, Pius Nyamko, Edmund Thomas, Mohamed Msomali, Salum Madadi, Abdalah Kibaden, Omary Mahadhi, Abdurahman Juma, Athuman Juma Kalomba, Silylelsaid Mziray, Kenny Mwaisabula, Hamim Mawazo na hao ni baadhi. Nkoma alipokuwa Yanga Princess (kulia) Nkoma ni mmoja wa makocha wetu wazawa mwenye moyo Nkoma amezifundisha timu nyingi hapa Tanzania na baadhi ni kama Rhino ya Tabora. Soka la wanawake ndio lililomtoa kocha huyo, lakini kwa wanaume pia alianza kufanya mabalaa kwani aliifundisha timu ya taifa ya vijana ya Tanzania yeye na Bakari Shime aliipeleka katika AFCON ndogo kule nchini Gabon, akiwa na wanasoka vijana kama Ramadhan Kabwili, Kibwana Shomari, Dickson J...