Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Nabi ndiye kocha aliyeleta mabadiliko makubwa Yanga

Machapisho ya hivi karibuni

Al Ahly wakiri kuboronga msimu huu

Klabu ya Al Ahly imetoa taarifa rasmi kufuatia kikao cha dharura kati ya Rais wa klabu, Mahmoud El Khatib, na viongozi waandamizi baada ya kutoridhishwa na mwenendo wa timu. Katika taarifa hiyo, klabu inakiri na kuelewa kusononeka na hasira za mashabiki kutokana na matokeo mabaya, huku uongozi ukichukua dhima kamili kwa yale yanayotokea. Uongozi umekiri kuwepo kwa makosa ya kiufundi na kiutawala, ukiahidi kuwa hatua madhubuti za kurekebisha hali hiyo zinaandaliwa na zitahitaji muda kiasi ili kuleta tija. Tayari maamuzi kadhaa ya dharura yamefanyika na yatatangazwa hivi karibuni, huku tathmini ya kina na mabadiliko ya kimfumo ndani ya idara ya mpira wa miguu yakianza kufanyiwa kazi ili kuendana na hadhi ya klabu. Mwisho, uongozi umewashukuru mashabiki kwa uaminifu wao na kuahidi kufanya kila liwezekanalo kurudisha timu katika mstari uliozoeleka. Maana ya Taarifa hii kuwa tayari kuna watu washaliwa vichwa ...Faini zimetembea na wenye kuajibishwa wamewajibishwa

Vinara wa Assist Ligi Kuu bara hawa hapa

Vinara wa pasi saidizi (assists) kwenye Ligi kuu ya NBC Tanzania bara mpaka sasa msimu huu. 1. Elie Mpanzu (Simba Sc)— 5 2. Feisal Salum (Azam FC) — 5 3. Duke Abuya (Yanga Sc) — 4 4. Ibrahim Imoro (Singida BS) — 4 5. Baraka Maranyingi (Mbeya City) — 3 6. Israel Mwenda (Yanga Sc) — 3 7. Maxi Nzengeli (Yanga Sc) — 3 8. Lamine Jarjou (Singida BS) — 3 9. Andrew Raymond (Namungo FC) —3 10. Mathew Tegisi (Pamba Jiji) — 2

Mpanzu awashukuru mashabiki Simba

Mshambuliaji wa Simba SC, Elie Mpanzu, amewaandikia mashabiki wa klabu hiyo ujumbe mzito na wa kugusa hisia akishukuru kwa mapenzi na msaada mkubwa waliompa katika kipindi kigumu alichopitia. Mpanzu amebainisha kuwa ni kutokana na maombi, simu, na jumbe za kutia moyo kutoka kwa mashabiki ndiko kumempa nguvu ya kurejea kwenye mstari na kufanya uamuzi wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo badala ya kuondoka, akiahidi kuwalipa fadhila hizo kwa mambo mema uwanjani katika siku zijazo. ​ ​"Nikiwa na machozi machoni mwangu ninawaandikia, wapenzi mashabiki wa Simba. Ninyi ndio wafuasi bora zaidi ambao nimewahi kukutana nao. Nataka kuwashukuru kutoka moyoni mwangu kwa msaada wenu usioyumba, licha ya nyakati ngumu ambazo nimepitia. Mmekuwa mkiniamini kila wakati. ​Ni kutokana na maombi yenu, simu, ujumbe, kutia moyo kwenu, na ushauri wenu kwamba ninaanza kurudi kwenye mstari. Ndiyo maana nimeamua kutowasaliti na kuendelea na klabu. Ninawapenda nyote sana na ninawaahidi mambo mema katika siku z...

Kocha wa Zambia atamba kuwalaza Argentina ya Messj

Kocha wa timu ya taifa ya Zambia Chipolopolo George Lwandamina amesema mchezo wa kirafiki dhidi ya Argentina utakuwa mgumu lakini wamejiandaa kupambana vizuri na kuleta ushindani wa hali ya juu. Akizungumza baada ya mazoezi ya timu hiyo katika chuo kikuu cha Lusaka, Lwandamina alisema kucheza na mabingwa hao wa dunia itakuwa kazi kubwa. Chipolopolo watakuwa ugenini nchini Argentina Machi 31 mjini Buenos Aires katika mechi ya kihistoria ya kirafiki ambayo inawakutanisha Zambia dhidi ya mabingwa hao wa dunia. Hata hivyo wachezaji wakubwa hawakuweza kujumuishwa katika kikosi hicho cha timu ya taifa kutokana na majukumu kwenye timu zao.

KUUMBWA KWA DUNIA

Inaandikwa na Fikiri Salum DUNIA (kutoka neno la Kiarabu) wakati mwingine pia Ardhi na Kwa neno la asili la Kibantu nchi, ni Gimba la angani ambapo juu yake tunaishi sisi binadamu na viumbe hai wengine wengi, tukipata mahitaji yetu, kuanzia hewa ya kutufaa na maji. Dunia ni mojawapo ya sayari zinazoelea katika anga la ulimwengu, kuna sayari nane zinazolizunguka jua, dunia yetu ikiwa sayari ya tatu katika mfumo wa juavna sayari zake. Masafa baina yake na jua ni kilomita milioni 150 au kizio Astronomia 1, dunia huchukua siku 365, 256 kulizunguka jua, na masaa 23,9345 kuuzunguka mhimili wake na upana wake ni kilomita 12,756. Dunia huwa na mwezi mmoja 1. Umri wa dunia hukadiriwa kuwa na miaka bilioni 4,5 (1/2) Ni mahari pekee katika ulimwengu panapojulikana kuna uhai ulioaminiwa kuanza miaka bilioni 3.5, hivi iliyopita, uhai unapatikana kwa spishi milioni 10-14 za viumbe hai pamoja na  wanadamu waliokadiriwa kuwa sasa bilioni 7, 2 (4). UMBO LA DUNIA Umbo la dunia linafanana na tufe au mpir...

Rasmi, Pedro Goncalves kusalia Jangwani hadi mwisho wa msimu

Uongozi wa Klabu ya Yanga umethibitishwa kwamba Kocha wake Mkuu,Pedro Goncalves ataendelea kusalia Yanga SC mpaka mwishoni mwa msimu.