Muda wowote kuanzia sasa, Simba itakamilisha makubaliano ya kumuuza mshambuliaji Kibu Denis kwenda Al Nasr ya Libya. Chanzo kutoka ndani ya klabu hiyo kimeithibitishia Mwananchi Digital kuwa mshambuliaji huyo anajiandaa kukamilisha mchakato wa kujiunga na miamba hiyo ya Libya. “Kibu anaenda Libya. Klabu imeshafikia makubaliano ya kumuuza na kuna mambo machache tu yamesalia ili uhamisho huo ukamilike,” kimefichua chanzo hicho. Hii ni mara ya pili kwa Al Nasr kumhitaji Kibu kwani mara ya kwanza ilikuwa katika dirisha kubwa la usajili kabla ya kuanza kwa msimu huu ambapo nia yao haikufanikiwa. Lakini awamu hii Al Nasr wameonekana kuja na nguvu mpya ambayo imewafanya wafanikiwe kumuachia Kibu ili kukwepa nyota huyo kuondoka bure baada ya msimu kumalizika. Ifahamike kwamba mkataba wa Simba na Kibu Denis utafikia tamati mwishoni mwa msimu huu hivyo klabu hiyo imeonekana haiko tayari kuziachia noti za Walibya hao kwa sasa. {Via @mwananchi
MAMBO UWANJANI
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com