Machapisho

Naby Camara aachwa Simba

Picha
Klabu ya Simba SC imeingia kwenye mabadiliko makubwa ya kikosi chake kuelekea msimu mpya baada ya kukamilisha taratibu za kuachana na kiungo wao, Naby Camara.  Pande zote mbili zimefikia makubaliano ya kirafiki ya kuvunja mkataba uliokuwa unawaunganisha, hatua inayohitimisha rasmi safari ya mchezaji huyo ndani ya uwanja wa Mo Simba Arena baada ya kuitumikia timu hiyo kwa msimu mmoja pekee. ​Kuondoka kwa kiungo huyo hakujashtukiza uongozi kwani tayari alishafunganya virago na kuondoka nchini tangu Juni 25, 2026, huku akiiacha Simba ikiendelea na mikakati mingine ya kusuka safu yake ya kiungo. Camara kwa sasa anatajwa kuwa mchezaji huru (free agent), jambo linalompa fursa ya kukaa mezani na timu yoyote ndani au nje ya Afrika inayohitaji huduma yake kwa ajili ya changamoto mpya za kisoka. ​Hatua hii ya Simba SC ni mwendelezo wa mpango wao wa kupunguza wachezaji wa kigeni ambao hawakuwa na mchango mkubwa wa moja kwa moja kwenye kikosi cha kwanza msimu uliopita. Mashabiki wa Wekundu wa Msim...

Rais wa nchi amtembelea Pacome

Picha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na MWANANCHI NAMBA MOJA Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na leo alimtembelea na kumpa pole mchezaji wa timu ya wananchi Pacome Zouzoua, ambaye anaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam kufuatia majeraha aliyoyapata wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya JKT Tanzania.

Al Ittihad SC yanasa kocha wa fitness wa Yanga

Picha
Al Ittihad SC imeanza mazungumzo na Tshephang "Chyna" Mokaila ambaye ni kocha wa fitness wa Young Africans SC kwaajili ya kuitumikia klabu hiyo kwa msimu ujao! Mazungumzo yanaendelea vizuri sana baina ya Tshephang "Chyna" Mokaila na Al Ittihad SC na Libya na ikiwa watafikia makubaliano chanya atahamia Libya kwasababu amepewa ofa kubwa zaidi ya Wananchi kuanzia mshahara hadi vipengele vingine vya kimkataba.

Kipre Jr arejea Azam FC

Picha
Azam Fc wamekamilisha usajili wa winga wa Ivory Coast,Kipre Zunon Jr kutoka MC alger Kwenye mauziano hayo MC wameweka kipengele cha “Sell on” 30% kama Azam watamuuza Kipre basi 30% ya pesa itakwenda MC Alger.

Job kulipua bomu

Picha
Beki wa kati na nahodha msaidizi wa Young Africans SC, Dickson Job, ameibua mjadala mkubwa baada ya kuchapisha ujumbe kwenye ukurasa wake rasmi wa Instagram (@jobdick05) akidokeza kuwa atazungumza hadharani kuhusu jambo alilolieleza kuwa ni muhimu. Kuna mtu nna ujumbe wake, Job aliandika:"Kama Nahodha, jukumu langu ni timu. Nidhamu ni bora kuliko kipaji. Hivyo nitazungumza kesho (Jumatatu). Sio busara mchezaji kurubuniwa." Kauli hiyo imeibua hisia na maswali mengi miongoni mwa mashabiki wa Yanga na wadau wa soka, huku wengi wakisubiri kwa hamu kufahamu kile ambacho nahodha huyo msaidizi amesema atakiweka hadharani. Uj umbe huo tayari umeanza kusambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii, ukiibua mijadala kuhusu kile kinachoweza kuwa kiini cha kauli yake.

Yanga, Sportpesa wateta

Picha
Mapema asubuhi ya leo, Uongozi wa YANGA SC ukiongozwa na Rais Eng. Hersi Said ulifanya kikao na Mdhamini Mkuu wa Klabu yetu, Kampuni ya SportPesa na kujadili mambo mbalimbali ya kimkataba na mahusiano ya pande zote mbili. Upande wa Kampuni ya SportPesa uliwakilishwa na Tarimba Abbas, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Allan McTavish, Mkuu wa Kimataifa wa Udhamini na Sabrina Msuya ambaye ni Mshauri wa Udhamini Mahusiano na Serikali.

Simba yapindua meza

Picha
Simba wanataka kupindua meza kwa Yona Amos (27). Yona ni mcheza huru baada ya kumalizana na Pamba Jiji. Mwezi uliopita Yona alikubaliana kila kitu (Sign on fee,mshahara) na Singida Black stars ila dili hilo limechelewa kukamilika coz Singida bado hawajaingiza hela kwenye Account ya Yona. Baada ya Simba kugundua hilo wameingilia kati na sasa wanataka kupita na kipa huyo. Mazungumzo ya Simba na Yona yanaendelea.