Machapisho

Karia kufuta Ligi Kuu ya vijana

Picha
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia, amesema hana hofu na vilabu vikubwa kama Simba na Yanga katika kufanya maamuzi yenye maslahi ya soka la Tanzania. Karia amesisitiza kuwa anaongozwa na kanuni badala ya busara au shinikizo kutoka kwa wadau. Kiongozi huyo amesema moja ya mipango yake ni kuifuta Ligi ya U-20 kutokana na kile alichodai kuwa wachezaji wengi wanaoshiriki hawachezi katika umri unaostahili. Badala yake, amependekeza ligi hiyo ibadilishwe na kuitwa ligi ya wachezaji wa akiba ili kuondoa changamoto zinazohusiana na udanganyifu wa umri. Karia pia amesema atakutana na wadhamini wa mashindano hayo kujadili hatma ya ligi hiyo na kuona namna bora ya kuiboresha. Kauli yake tayari imeibua mjadala mkubwa miongoni mwa wadau wa soka, huku wengi wakisubiri kuona uamuzi rasmi kuhusu mustakabali wa Ligi ya U-20 nchini

Simba yaonesha jeuri ya pesa, yagomea hoteli

Picha
Wakati vilabu vingine ambavyo vinashiriki michuano ya CECAFA Kagame Cup 2026 vikifikia kwenye hoteli ambazo zinalipiwa na CECAFA zenye hadhi ya nyota tatu. Simba iliwajulisha CECAFA kwamba itafikia kwenye hoteli yenye hadhi ya juu zaidi na italipa gharama zote za ziada ili kuendana na hadhi na ukubwa wa klabu yao baada ya Raisi wa heshima wa klabu hiyo Mohammed Dewji kuagiza kwamba wanastahili kuhukua hotel ya hadhi ya nyota 5 na atalipia kila kitu yeye! Hivyo Simba wamefikia hoteli ya nyota 5 ya Mövenpick yenye hadhi ya juu zaidi jijini Kigali ambayo Gharama ya chini ya chumba ambacho kinachotumiwa na staff wa Simba ni Tsh. 450,000 kwa siku moja ikihusisha chai ya asubuhi pekee. Simba wamesafiri na chakula chao kutoka Tanzania ambacho watatumia muda wote ambao kikosi kitakuwepo nchini Rwanda.

MO Dewji akutana na Ibra Doumbia

Picha
Rais wa Simba SC, Mohammed Dewji alipokutana na mshambuliaji mpya, Ibrahim Doumbia kuzungumza nae kuhusu malengo ya klabu na matarajio ambayo Wanasimba wanayo juu yake.

Dili la Ahoua kujiunga Singida lapaa

Picha
kwenye soko la usajili baada ya dili la kiungo mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Jean-Charles Ahoua, kujiunga na klabu hiyo ya hapa nchini kuvunjika rasmi. ​Taarifa za ndani zinaeleza kuwa pande hizo mbili zimeshindwa kufikia makubaliano ya mwisho kufuatia kutoelewana kati ya upande wa mchezaji na mmoja wa vigogo wakubwa wa klabu hiyo. Kutokana na kukwama kwa mazungumzo hayo, usajili huo uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu sasa umefutwa rasmi. ​Baada ya dili hilo kufungwa, mchezaji huyo wa zamani wa Simba SC na CR Belouizdad sasa anaendelea kuchakata na kupitia ofa mbalimbali zilizopo mezani kwake kutoka katika mataifa ya Afrika Kusini, Libya, na Misri ili kuamua hatima ya klabu yake mpya kuelekea msimu ujao. ​Mdau wa soka, unadhani nini kimesababisha kiongozi huyo kushindwa kuelewana na Ahoua? Na unaona ni nchi gani itafaa zaidi kwa kiungo huyo kutua msimu huu? Dondosha maoni yako!

Simba yaja na Ibrahim Doumbia

Picha
Simba SC imemsajili mshambuliaji Ibrahim Doumbia kwa mkataba wa muda mrefu na sio kufanya majaribio kwenye CECAFA KAGAME CUP 2026 akitokea AS Kôrôfina Ibrahim Doumbia ni mchezaji hatari sana akiwa amehusika kwenye magoli 22 kwenye mechi 24 za Ligi Kuu ya Mali.

Singida Black Stars yaja na mzungu

Picha
Klabu ya Singida Black Stars imemtambulisha rasmi kiungo mshambuliaji Marcel Canad kuwa sehemu ya kikosi kitakachoiwakilisha klabu hiyo katika msimu wa 2026/27.Marcel, mwenye umri wa miaka 28, anatajwa kuwa miongoni mwa wachezaji wanaotarajiwa kuongeza nguvu na ubunifu katika eneo la kiungo cha ushambuliaji la Singida Black Stars. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa, Marcel amewahi kuwa sehemu ya mfumo wa Borussia Mönchengladbach, klabu inayoshiriki Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga), katika kipindi cha mwaka 2014 hadi 2017.Usajili wake unaongeza hamasa kwa mashabiki wa Singida Black Stars, ambao sasa wanaanza kuona picha ya kikosi kitakachopambana kwenye msimu mpya.

Peter Shalulile rasmi Yanga

Picha
Taarifa kuhusu uwezekano wa Peter Shalulile kujiunga na Young Africans SC (Yanga) zimezidi kushika kasi, huku mashabiki wa klabu hiyo wakianza kuhusisha dokezo lililotolewa na Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe, kupitia ukurasa wake wa Instagram. Ally Kamwe aliandika ujumbe wenye mafumbo, jambo lililoibua hisia na kuzua mjadala miongoni mwa mashabiki wa Wananchi, ambao baadhi yao wamehusisha ujumbe huo na nyota huyo wa Namibia. Shalulile, ambaye ametengeneza jina kubwa akiwa na Mamelodi Sundowns, kwa sasa ni mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na klabu hiyo. Yanga inaendelea na harakati za kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu mpya, huku ikijiandaa kwa mashindano mbalimbali, ikiwemo CAF Champions League.Endapo usajili wa Shalulile utathibitishwa, atakuwa mmoja wa washambuliaji wenye uzoefu mkubwa wanaoweza kuongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji ya Wananchi.