Machapisho

Eto'o atuhumiwa kulamba bilioni 1.7

Picha
Samuel Eto’o yuko kikaangoni baada ya kupewa tuhuma za matumizi ya pesa hovyo. kwa taarifa kutoka vyanzo vya habari, vinaeleza kuwa nyota wa Barcelona, ambaye pia ni Rais wa Shirikisho la Soka la Cameroon (FECAFOOT), Kuna kiasi cha pesa fulani hakionekani, na kiwango hicho si chini ya takribani dola 665,000 [TZS bilioni 1.7], zilizohusishwa na malipo ya mchezo wa kirafiki kati ya Cameroon na Urusi mwaka 2023. Kufuatia sakata hilo, Eto’o, ambaye amekuwa akiongoza FECAFOOT tangu mwaka 2021, wataanza zoezi la uchunguzi dhidi ya jambo hilo linalomkabili. Kwa upande wa mshitakiwa ambaye ni Eto’o, amesema kuwa upande wake uko wazi kwa uchunguzi zaidi ili kuona wapi amekosea. Pia, nyaraka zake zote zitaanza kuchunguzwa, na kuripotiwa kuonyesha kuwa fedha hizo ziliagizwa kutumwa kwenye akaunti yake binafsi katika benki nchini Qatar.

Clara Luvanga atinga makao makuu Yanga

Picha
Mchezaji wa zamani wa Yanga Princess Clara Luvanga ambaye kwa sasa anacheza Ligi kuu nchini Marekani amemtembelea Rais wa Yanga SC Injinia Hersi Said ofisini na kuzungumza mambo mbali mbali kuhusu maendeleo ya mchezaji huyo siku hadi siku

Libasse Gueye ashinda tuzo ya mwezi NBC Primier League

Picha
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) kupitia Kamati ya Tuzo za TFF imemtangaza kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Libasse Gueye, kuwa Mchezaji Bora wa Mwezi Agosti wa Ligi Kuu ya NBC (2026/27), huku kocha mkuu wa Yanga SC, Manqoba Mngqithi, akitwaa tuzo ya Kocha Bora wa Mwezi huo. Kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Libasse Gueye, ametwaa tuzo hiyo baada ya kuonyesha kiwango bora na kutoa mchango mkubwa katika michezo mitano ambayo Simba ilishinda yote. Akifunga bao moja na kuhusika kwenye mabao mengine matano (Assist 5) hivyo amehusika kwenye Magoli 6, Amewashinda Maxi Nzengeli (Young Africans) na Oscar Mwajanga (Mbeya City) walioingia naye fainali. Kocha wa Young Africans, Manqoba Mngqithi, amechaguliwa kuwa kocha bora baada ya kuiongoza timu yake kushinda michezo yote mitano na kukaa kileleni mwa msimamo wa ligi. Amewabwaga Steve Barker (Simba SC) na Florent Ibenge (Azam FC).

AS Maniema ziarani Tanzania

Picha
Jioni hii klabu ya AS Maniema Union,ya Congo DR imeanza safari ya kuja Tanzania. AS Maniema Union Wamealikwa na Azam Fc na watatua usiku wa leo. Lengo la timu hiyo kuja Tanzania ni kucheza mechi ya kirafiki na Azam FC.

Simba SC, MO Dewji yatoa msaada kwa watoto Mbweni

Picha
Kwa kushirikiana na Taasisi ya Mo Dewji klabu ya Simba SC imetoa zawadi kwa watoto wanaoishi katika Kituo cha Kutunza Watoto Yatima cha Mwandaliwa kilichopo Mbweni, Dar es Salaam kama sehemu ya kurudisha kwa jamii yenye uhitaji lakini pia kujikabidhi kwa Mwenyezi Mungu kuelekea katika mchezo wa Jumapili wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Ajali ya bodaboda yaondoa uhai kipa wa Azam FC U20

Picha
MCHEZAJI wa Azam FC U-20, Iddy Salim, amefariki dunia baada ya kupata ajali ya pikipiki jana Alhamisi, Septemba 10, 2026. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Klabu ya Azam FC, marehemu alikuwa akicheza nafasi ya kipa katika timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 (U-20). Mwili wa marehemu kwa sasa umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwananyamala (MRRH), ambapo unafanyiwa taratibu za mwisho kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Tanga kwa ajili ya maziko. Azam FC pia imetuma salamu za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu kufuatia msiba huo.

Kocha wa Yanga ashinda tuzo ya mwezi

Picha
Kocha wa Young Africans, Manqoba Mngqithi, ametangazwa kuwa Kocha Bora wa mwezi Agosti katika Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2026/27, baada ya kuiongoza timu hiyo kufanya vizuri katika michezo ya mwezi huo. Mngqithi aliiongoza Yanga kushinda michezo yote mitano iliyocheza mwezi Agosti, matokeo yaliyoiwezesha timu hiyo kukaa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu. Katika mchakato wa kuwania tuzo hiyo, Mngqithi aliwashinda Steve Barker wa Simba na Florent Ibenge wa Azam FC, ambao pia walikuwa wameingia hatua ya mwisho ya kinyang’anyiro hicho.