Rayon Sports mabingwa kombe la Kagame Cup
Timu ya Rayon Sports ya Rwanda imefanikiwa kulibakiza kombe nyumbani baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo mkali uliochezwa dakika 120. Dakika 90 za kawaida timu hizo zilitoka sare ya 1-1 na kupelekea kuongezwa muda wa ziada, Rayon walianza kupata bao dakika ya 28 kupitia kwa Herman Kameni kabla ya Gor Mahia kusawazisha kupitia kwa Sharrif Mussa dakika ya 53. Muhoza Daniel aliiandikia bao la pili Rayon katika dakika ya 97, sasa ni rasmi Rayon inaivua ubingwa Singida Black Stars ya Tanzania iliyotolewa mwanzoni mwa mashindano hayo.