Machapisho

Mecky Mexime alikataa masharti ya TRA United

Picha
Inasemekana Miongoni mwa vitu vilivyopelekea kocha Mecky Mexime kuachana na TRA united licha ya makubaliano kufikiwa na kusimamia mazoezi ya timu hio ni sharti la kutakiwa kushinda mechi nne. Mechi hizo nne za TRA united ni dhidi ya Pamba Jiji, Namungo, Yanga, Singida Black Stars, kama atashinda mechi hizo basi atapewa mkataba wa kudumu kutoka kwenye mkataba wake wa kua kocha wa muda (Interim Coach ).

Feitoto aichambua Simba

Picha
Kiungo mshambuliaji mahiri wa Azam FC, Feisal Salum Abdallah “Feitoto”, amefunguka kuhusu mchezo ujao wa Ligi Kuu dhidi ya Simba SC, akionya kuwa pambano hilo litakuwa na ushindani mkubwa sana uwanjani. Feitoto amekiri kuwa mchezo huo utakuwa mgumu kutokana na kikosi cha Simba kusheheni wachezaji wakubwa na wenye uzoefu mkubwa wa michuano ya ushindani. Amesisitiza kuwa timu zote mbili zitaingia uwanjani zikiwa na azma moja tu ya kusaka ushindi, jambo ambalo linafanya mchezo huo kuwa wa aina yake.

Yanga imenipa thamani kubwa- Mwalimu

Picha
Mchezaji wa Yanga Selemani Mwalimu ameweka bayana ni kwa namna gani klabu ya Yanga imempa thamani tofauti na klabu amepita hapo mwanzo. Seleman amesema kwa heshima hii inaniongezea Nguvu za kupambana, hivyo nitapambana kwasababu timu yangu inaniheshimisha ,pia nitaweka Jitihada zangu zote katika mechi zangu endapo Mwalimu akinipa nafasi nitazitumia vizuri na mashabiki wa Yanga watapenda. Amesema Mwalimu

Mchezaji wa zamani Simba afariki dunia

Picha
Kiungo mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Simba SC Bakari Iddi amefariki dunia arasiri mitaa ya nyumbani kwake Kigogo jijini Dar es Salaam. Ndugu wa marehemu Andi Iddi Bakari na Gharib Bashiru wameujuza mtandao wa Mambo Uwanjani Blog kwamba mchezaji huyo wa zamani wa Simba miaka ya 1990 hatunaye. Ikumbukwe Iddi alikuwemo katika kikosi cha Simba kilichotwaa ubingwa wa Klabu Bingwa Afrika mashariki na kati, maarufu kombe la Kagame Cup mwaka 1991 kilichoifunga SC Villa ya Uganda mabao 3-0. Mwili wa marehemu umepelekwa hospitali na taratibu za mazishi zitafanyika mara baada ya kupangwa na familia. Innalillah wainnailayh raajiun

Manqoba ashangazwa na waandishi

Picha
Kocha Mkuu wa Yanga SC, Manqoba Mngqithi, amesema ameshangazwa na idadi kubwa ya waandishi wa habari waliofika uwanjani kwa wakati mmoja. Mngqithi amesema katika kipindi chote ambacho amekuwa akifanya kazi ya ukocha, hajawahi kuona waandishi wengi wa habari wakifika uwanjani kwa wakati mmoja kama ilivyokuwa leo. “Tangu nianze kazi ya ukocha, sijawahi kuona waandishi wengi wa habari wakifika uwanjani kwa wakati mmoja kama nilivyoona leo. Hata kwenye fainali za Klabu Bingwa Barani Afrika haijawahi kutokea waandishi wa habari wakifika uwanjani kutafuta habari kwa idadi kubwa kama leo.”

Diamond Platinum aenda kumfariji Rais Samia Kizimkazi

Picha
Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya Nasibu Abdul @DiamondPlatnumz akimfariji Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 09 Septemba, 2026, kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Septemba, 2026

Ngasa ampa makavu Chama Jr

Picha
Mkongwe wa Soka la Tanzania na Top Scorer of All Time wa Tanzania National team Mrisho Ngasa ametoa dukuduku lake kwenye sakata linalomhusisha mchezaji wa Simba ChamaJR. Ngassa ametoa ushauri kwa mchezaji huyo kuwa ni bora zaidi kwake kujikita viwanjani kuliko hizi vita za nje ya uwanja. Ngassa amesema kwamba hizi timu ukiwa kwenye nyakati sahihi kama hizi utapata likes, comments na kila hitaji la moyo wako lakini ukishatoka hvyo vyote vinapungua so lazima kusoma alama za nyakati.