Kampuni ya Sandaland Fashion Wear Limited imetangaza kuchukua hatua za kisheria dhidi ya kauli iliyotolewa hadharani na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, kuhusu jezi za Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars. Hatua hiyo imetangazwa kupitia tamko rasmi la kampuni hiyo, iliyosema kauli ya Makonda iliyotolewa Septemba 16, 2026 kupitia akaunti yake ya Instagram imeathiri jina, chapa, hadhi na uhalali wa bidhaa za Sandaland katika soko. Katika ujumbe huo, Makonda alinukuliwa akisema: “Hii sio jezi ya Taifa Stars, Taifa Stars kwa ubora wake hatuwezi kuwa na jezi za kiwango chini hivi. Acheni kutumia picha za Naibu wangu huku ofisi yangu haina taarifa.” Ujumbe huo uliambatana na picha ya Naibu Waziri Hamis Mwinjuma, maarufu Mwana FA, akiwa amevalia jezi yenye mchanganyiko wa rangi ya njano, bluu, nyeusi iliyochanganyika na kijani. Sandaland imesema kauli hiyo imezua taharuki na sintofahamu, huku ikidai kuwa tayari imesababisha madhara ya kiuchumi na kwa hadhi ya kam...