Machapisho

Juma Mgunda amwadhibu Minziro

Picha
Wauaji wa Kusini, Namungo FC usiku huu imeibuka na ushindi wa bao 1-0 katika uwanja wa Majaliwa Ruangwa mkoani Lindi mchezo wa Ligi Kuu bara dhidi ya Fountain Gate. Bao pekee la Namungo limefungwa na Herbert Lukindo dakika ya 10, kwa matokeo hayo Namungo FC imefikisha alama 6 na ikiishusha Singida Black Stars inayokwenda nafasi ya saba. Namungo inanolewa na Juma Mgunda wakati Fountain inanolewa na Fred Minziro.

Tanzania na Kenya zapangwa AFCONU23

Picha
Tanzania imepangwa kuanza na Kenya kwenye mchezo wa awali kufuzu AFCON U23

Edo Kumwembe amfananisha kocha wa Yanga na Mourinho

Picha
Mchambuzi wa soka nchini, Edo Kumwembe, kupitia ukurasa wake wa Instagram amemnukuu na kumpa ujumbe mzito mchezaji 'Chuga Boy' pamoja na mtindo wa ukocha wa Yanga SC: ​"Huyu wa Yanga kama sio tabia zake binafsi basi atakuwa amewachagua akina Mourinho wawe mfano wake. Wanakuchana hapo hapo. Uwe mchezaji wake au Mwandishi wa habari." ​"Alichofanywa Chuga boy ndio ajifunze kucheza chini ya makocha tofauti. Lakini jambo la msingi katika hili ni kwamba aliambiwa ukweli. Alijaribu kucheza na Jukwaa wakati kule mbele Yanga wanacheza mpira rahisi ndio maana wanatengeneza nafasi nyingi." ​"Kijana ana kipaji kikubwa asiwe na haraka ya kuthibitisha. Siku hizi tunahesabu zaidi pasi, Assists na mabao. Chenga nyingi tuliacha."

TFF, Bodi ya Ligi yapokea ugeni kutoka Mali

Picha
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), leo Agosti 25, 2026, imepokea ujumbe kutoka Chama cha Mpira wa Miguu cha Mali. Wawakilishi Abidane Issa Sangare na Niama Loua Berete wapo nchini kwa ajili ya kubadilishana uzoefu na kujifunza mifumo mbalimbali ya uendeshaji wa soka, hususan katika maeneo ya ligi na maendeleo ya mchezo Ujio wao unatoa fursa muhimu ya kushirikishana maarifa, uzoefu na mbinu bora katika kuendeleza mpira wa miguu kati ya Tanzania na Mali.

Rais Samia awatakia kheri ya Maulid

Picha
Ninawatakia Waislamu na Watanzania wote kheri na baraka za Sikukuu ya Maulid. Kumbukizi ya siku hii njema ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) itukumbushe kuendelea kuishi kwa upendo, huruma, uvumilivu na kuwajali wengine. Tusherehekee kwa amani na furaha, huku tukidumisha umoja na mshikamano wetu. Mwenyezi Mungu Mtukufu aendelee kuibariki nchi yetu, kuitunza katika amani na utulivu, na kutuwezesha kuijenga kwa maendeleo na ustawi wa wote. Mawlid Al Nabi Mubarak.

Anaandika Nasri Khalfan mchambuzi wa Wasafi FM

Picha
Magoli mawili katika michezo mi3 ya mwanzo wa Ligi sio mbaya... yeye na Jonathan Sowah ndio Washambuliaji wakati wenye takwimu nzuri katika hii michezo mi3 ya mwanzo. Mazingira mapya na amezungukwa na Wachezaji wapya. Lazima ilihitajika time kuonekana muunganiko wa moja kwa moja kati yake na viungo wake. Akiongezeka na Aziz Ki bila ya shaka huduma itakua ya uhakika zaidi kwake.

Anaandika Nasri Khalfan mchambuzi wa Wasafi FM

Picha
Magoli mawili katika michezo mi3 ya mwanzo wa Ligi sio mbaya... yeye na Jonathan Sowah ndio Washambuliaji wakati wenye takwimu nzuri katika hii michezo mi3 ya mwanzo. Mazingira mapya na amezungukwa na Wachezaji wapya. Lazima ilihitajika time kuonekana muunganiko wa moja kwa moja kati yake na viungo wake. Akiongezeka na Aziz Ki bila ya shaka huduma itakua ya uhakika zaidi kwake.