Machapisho

Hii ndio Simba

Picha
Bao pekee lililofungwa na Anicet Oura limeiwezesha Simba kuibuka na ushindi wa bao 1-0 ugenini dhidi ya Might Wonderers katika uwanja wa Bingu, Lilongwe nchini Malawi jioni ya leo. Mchezo huo wa Ligi ya mabingwa Afrika mkondo wa kwanza, unaifanya Simba kusubiri mchezo wa marudiano utakaofanyika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kutoka sare yoyote Ili isonge mbele raundi ya kwanza. Shukrani wachezaji wa Simba Kwa kujituma ugenini na kuweza kupata ushindi.

Singida BS yaua kombe la Shirikisho

Picha
Singida Black Stars ya Tanzania imeanza msimu wa mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa kishindo baada ya kushusha kichapo kizito cha 7-1 ugenini dhidi ya A-Ghazala FC ya Sudan Kusini. FT: Al Ghazala 1-7 Singida Black Stars ⚽ 20' Tegisi ⚽ 23' Tegisi ⚽ 32' Tegisi ⚽ 41' Sheikhan ⚽ 63' Sowah ⚽ 86' Henry ⚽ 90' Sowah

Ismail Mgunda mshambuliaji mzawa ataanza leo?

Picha
Kocha Mkuu wa Simba SC, Steven Robert Barker leo akimuamini na kumpa dakika kiwanjani Ismail Mgunda aongoze mstari wa juu wa Msimbazi mbele ya Mighty Wanderes kuna tatizo lolote? Ikumbukwe Mgunda ndio Mshambuliaji mzawa pekee ambaye yupo ndani ya Simba kwa sasa pamoja na Ibrahim Doumbia kutoka Mali!

Mimi ni Simba lialia- Manara

Picha
Mimi kama mwanahabari na msemaji wa timu ya taifa pamoja na vilabu vyote Tanzania, nitajiunga na Simba SC kwenda kupambana ili tupate ubingwa na turejee nao tukiwa kidedea. Nasema hivyo sio kwa ubaya, hapana, nasema hivyo kulingana na kazi yangu ninayoifanya. Siwezi kwenda Yanga nimevaa uzi wa Yanga endapo mimi ni mwana Yanga SC, ila nitazuru mechi zote za timu zote nikiwa na jezi ya timu ya taifa. Basi, furaha sitokosa. Nafanya hivyo kwa sababu nyie waandishi wa habari mna tabia moja. Unaweza kukuta nashangilia Simba SC kupata ubingwa, mnakamua kukata kipande kimoja cha video kikinionyesha nimeshangilia Simba na mkasema nimehama timu yangu, nimerudi Simba SC. Mechi zote nitashiriki, mpaka ya Singida BS nitakuwa pamoja na nyie. Siwezi kuwaangusha mashabiki wote wa Tanzania. Nataka niweke hii kwa maana kuna kitu wengi wana-noti kuwa nitavaa jezi ya Singida. Hapana, yaani jezi ni ile ile ya Tanzania, timu ya taifa.

Mayele azikwepa timu za Tanzania bara

Picha
Nyota wa Al Ahly Tripoli na mshambuliaji wa zamani wa mabingwa wa Tanzania, Young Africans (Yanga SC), Fiston Mayele, amesema hatamani kukutana na timu kutoka Ligi Kuu ya Tanzania Bara katika hatua zinazofuata za mashindano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika. Mayele amesema sababu ni kwamba timu za Tanzania zina kelele nyingi tofauti na timu kutoka Zanzibar. Pia ameeleza kuwa kipindi alipokuwa akiichezea Pyramids, hakuwahi kukutana na timu za Tanzania na alifurahia hali hiyo. “Sitaki kukutana na timu za Tanzania kwa sababu timu za Tanzania zinakelele sana tofauti na Zanzibar. Kipindi nilipokuwa Pyramids, sikuwahi kukutana na timu za Tanzania na nilifurahi sana. Pia kuna watu nilikuwa na mawasiliano nao pale Yanga, marafiki zangu, nilikuwa nawaambia sitaki kukutana na timu za Tanzania.”

Seleman Mwalimu aisawazishia Yanga

Picha
Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika Dar Young Africans maarufu Yanga, usiku huu wamenusurika kulala baada ya kutoka sare ya 1-1 na Gaborone United uwanja wa Taifa nchini Botswana. Gaborone United walikuwa wa kwanza kupata bao kipindi cha kwanza lililofungwa na Obry Amseb dakika ya 33 kwa mpira wa kutenga, iliwachukua Yanga dakika ya 90 kusawazisha goli hilo likifungwa na Seleman Mwalimu Gomez. Yanga wanapata sare muhimu ya 1-1 ugenini baada ya bao la dakika za mwisho

Seleman Mwalimu amjibu Chama

Picha
Baada ya Clatous Chama kudai kuwa Seleman Mwalimu huenda akawa anajutia kujiunga na Yanga SC baada ya kuikataa Simba, mshambuliaji huyo ameibuka na kutoa majibu. Mwalimu amesema yupo na furaha kubwa Yanga na haoni sababu ya kulalamika, akisisitiza kuwa anafurahia maisha yake ndani ya klabu hiyo. “Kaka nipo na furaha sanaaaaaaa na enjoy kuwa hapa Yanga ya moto mzee. Wanasema nilalamike kwa kipi mzee? Huku maisha safi, Hamdullilah na enjoy kuwa hapa.” — Seleman Mwalimu kupitia Instagram