Machapisho

Seleman Mwalimu kila kitu safi

Picha
Young Africans SC tayari imeshamuingiza mshambuliaji wao Selemani Mwalimu kwenye mfumo wa FIFA Connect na kupata karatasi zote za leseni za kuitumikia klabu hiyo kuelekea msimu ujao kutoka Wydad AC! Simba SC hawakuhusika katika kugoma na kutomtoa kwenye mfumo wasababu uhamisho wake ulikuwa umekwisha na kurudi katika klabu yake ya Wydad AC ambao wanammiliki na taarifa za Simba SC kugoma kumtoa kwenye mfumo sio za ukweli. Selemani Mwalimu amepewa session ya peke yake na Mwalimu Manqoba Mngoithi ili kuwa vizuri na kuungana na wenzake kwasababu hakufanya mazoezi ya pre-season na wenzake na muda wowote kuanzia sasa atawatumikia Wananchi. Seleman Mwalimu

Kocha Singida Black Stars aigwaya Simba

Picha
Kocha Mkuu wa Singida Black Stars, Pappy Kimoto, amefunguka wazi kuhusu mchezo wao ujao dhidi ya Simba SC, akitambua ugumu wa wapinzani wao lakini akisisitiza malengo yao ya kusaka ushindi. Kimoto amekiri wazi kuwa Simba ni timu bora na yenye ushindani mkubwa uwanjani. Licha ya kutokuwa na muda wa kutosha wa kufanya maandalizi ya kina kuelekea mchezo huo, alieleza kuwa kikosi chake kipo tayari kwa mapambano. Amesisitiza kuwa wamejiandaa kwenda kupambana vikali ili kuhakikisha wanaondoka na ushindi na alama tatu kamili kesho Kocha wa Singida Black Stars Pappy Kimoto

Singida Black Stars yazindua jezi mpya

Picha
Klabu ya Singida Black Stars imezindua jezi zake mpya kuelekea msimu mpya wa mashindano.Klabu hiyo imewasilisha seti tatu za jezi, ambazo ni Home Kit, Away Kit na Third Kit, kwa ajili ya msimu mpya. Jezi hizo zimekuja ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Singida Black Stars kuelekea msimu wa 2026/27, ambapo timu hiyo itaendelea kushiriki mashindano ya ndani.Wewe umezipa alama ngapi kati ya 10?

Okello aanika mshahara wake, ni kufuru

Picha
Aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Yanga SC, Allan Okello, amevunja ukimya na kuaga rasmi klabu hiyo baada ya kuitumikia kwa muda mfupi lakini wenye mafanikio. Katika ujumbe wake wa kwaheri, nyota huyo raia wa Uganda ametoa shukrani za dhati kwa uongozi wa Yanga SC chini ya Rais wa klabu, wachezaji wenzake, pamoja na mashabiki wa Wananchi kwa kumfanya ajisikie yupo nyumbani Tanzania, huku akisisitiza kuwa imekuwa heshima kubwa kwake kuvaa jezi ya kijani na njano. ​Mara baada ya kuaga Wananchi, Okello amekamilisha usajili wa kujiunga na miamba ya soka nchini Morocco, klabu ya AS FAR (FAR Rabat), ambapo amesaini mkataba wa miaka mitatu kuanza changamoto mpya ya soka barani Afrika Kaskazini. Hatua hii inamfanya kiungo huyo wa kimataifa wa Uganda kuanza maisha mapya katika Ligi Kuu ya Morocco (Botola Pro) akiwa miongoni mwa wachezaji kutoka Afrika Mashariki waliopata fursa ya kujiunga na klabu hiyo kubwa. ​Usajili huu unakuja na maslahi makubwa ya kifedha ambapo Okello atakua akilipwa jumla ...

Girumugisha awasifu viongozi wa Yanga

Picha
Baada ya Jean Claude Girumugisha kujiunga na klabu ya Al Ahli Tripoli ya nchini Libya ameweka wazi jinsi ambavyo dili lake la kujiunga na klabu ya Yanga liliikwama, huku akiwamwagia sifa mabosi wa Yanga. "Ni kweli Yanga walinitaka na nilikuwa tayari kwenda.Nilifurahishwa sana na namna viongozi wao walivyoniheshimu na walivyokutana na mimi,Tatizo lilikuja kwenye maslahi ya klabu kwa klabu. Kulikuwa na mambo ambayo yalihitaji makubaliano kati ya Al Hilal na Yanga, hivyo haikuwezekana kumaliza kila kitu," "Pengine baadaye nitakuja Tanzania, nilipenda mabosi wa Yanga walivyozungumza na mimi kwa heshima kubwa." -Jean Claude Girimugisha (Akielezea jinsi ambavyo dili lake kujiunga na Yanga lilivyokwama na kutua Al Ahli Tripoli)

Rashid Juma aibukia Mbeya City

Picha
Klabu ya Mbeya City ya mkoani Mbeya hii leo imemtambulisha kiungo mshambuliaji wa zamani wa Simba, Rashid Juma Mtabigwa kuwa mchezaji wake.

Ibrahim Jaabar avunja ukimya

Picha
Kiungo wa Simba SC, Ibrahim Jabaar, amevunja ukimya na kuonyesha ukomavu wa hali ya juu kufuatia kadi nyekundu aliyoonyeshwa katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Pamba Jiji FC jijini Mwanza. Kupitia ukurasa wake wa Instagram (Insta Story), nyota huyo ameonyesha uwajibikaji kwa kuandika ujumbe mfupi uliosomeka: "Hakuna visingizio, nawajibika kwa hili", akikubali kosa lililoiweka timu yake kwenye presha ya kucheza pungufu kipindi chote cha pili. ​Kauli hiyo ya Jabaar inakuja muda mfupi baada ya Msemaji wa Simba SC, Ahmed Ally, kuweka wazi kuwa benchi la ufundi na uongozi utakaa na wachezaji kukemea rafu zisizo na ulazima zinazopelekea kadi nyekundu. Mwitikio huu wa Jabaar umepokelewa kwa hisia chanya na mashabiki wengi wa Msimbazi, wakimsifu kwa kuonyesha nidhamu, ukweli na ujasiri wa kukubali kosa badala ya kutafuta visingizio. ​Unazungumziaje kitendo hiki cha Ibrahim Jabaar kukubali kosa na kuwajibika waziwazi kufuatia kadi hiyo nyekundu? Dondosha maoni yako!