Machapisho

Bi Kauye aomba radhi kwa video iliyosambaa

Picha
Baada ya Video hiyo pembeni iliyosambaa ya mwigizaji maarufu, Bi Kauye, amejitokeza hadharani kuomba msamaha kwa Watanzania wote kufuatia kusambaa kwa video inayomuonesha akiwa pamoja na kijana mmoja katika mazingira yaliyozua mjadala mkubwa na hisia tofauti kwenye mitandao ya kijamii. Akizungumzia tukio hilo, Bi Kauye amefafanua kuwa kilichotokea hakikuwa na maana kama inavyotafsiriwa na baadhi ya watu, bali kilikuwa ni sehemu ya utani tu wakiwa 'location' wakati wa uandaaji wa kazi ya video. ​"Naombeni mnisamehe Watanzania wote. Hayo siyo mambo yangu, ilikuwa ni utani tu tukiwa location. Naombeni mfute hiyo video, mimi nina watoto wakubwa. BASATA pamoja na Bodi ya Filamu naombeni mnisamehe. Hayo siyo mambo yangu kabisa, napitia kipindi kigumu mno," alisema Bi Kauye kwa majuto. ​Bi Kauye amewataka Watanzania kutomuhukumu kwa kile kinachoonekana kwenye video hiyo, huku akisisitiza kuwa mazingira yaliyokuwa yanaendelea yalihusisha utani wa kikazi wakati wa utengenezaji...

Ibenge amtaja Chama

Picha
Kocha Mkuu wa Azam FC Florent Ibenge ametoa tathmini nzito kuhusu ushindani kileleni mwa soka la bongo, akibainisha kuwa kikosi chake bado kipo nyuma kidogo kulinganisha na Simba SC kutokana na mabadiliko makubwa ya wachezaji waliyoyafanya klabuni hapo. ​Akimulika mbinu za Simba SC athari ya kiungo mshambuliaji Clatous Chama Ibenge alisifu mtindo wa uchezaji wa watani wao: "Hatutabadilika na Simba hawatabadilika, wanapenda kucheza mpira na ukiwa na mchezaji kama Chama huwezi kubutua. Kwa upande wetu tuko nyuma kidogo kuliko Simba maana walibaki na timu yao hawajabadilika, sisi tumebadili wachezaji wengi sana." ​Kauli hiyo ya Ibenge {abainisha changamoto ya kiufundi inayokabili Azam FC katika kutengeneza muunganiko mpya kikosini, huku akiitazama Simba SC kama timu iliyostawi kufuatia kuwekeza kwenye muundo endelevu na uzoefu

Yanga bado hawatufikii- Katwila

Picha
Kocha mkuu wa klabu ya Geita FC, Zuberi Katwila, baada ya mchezo kumalizika kwa bao 1-0 dhidi ya yanga SC.amekiri kuwa klabu ya Yanga SC bado ina safari ndefu kwenye mpira. Amesema hayo baada ya mchezo alioutumia mbinu kubwa ili kupata matokeo, “Klabu ya Yanga bado hawana uwezo wa kutufikia sisi, yani hata kidogo. Hata wakipata bao, basi ni kwa bahati sana. Nimependa tulivyolinda nafasi pamoja na uwezo wa wachezaji wangu. Mfumo wao niliweza kuudhibiti. Hata kupata kadi ni sehemu ya mchezo, sio kwamba wamefanya vibaya, hapana, hii ni moja ya changamoto.” “Kwa upande wangu, niwapongeze wapinzani wangu. Safu yao ya ulinzi ilikuwa imara zaidi kuliko sisi, ila kwa uwezo wetu tumefanya makubwa. Walijua wakija watafanya makubwa au kupata mabao zaidi, lakini wamekuta matokeo yamekuwa kama haya.”.

Yanga tia maji tia maji yashinda 1-0

Picha
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu bara Young Africans au maarufu Yanga imepata ushindi kiduchu katika uwanja wake wa nyumbani KMC Complex usiku huu dhidi ya Geita Gold Kwa bao 1-0. Bao pekee la Yanga limefungwa na beki wake Farouk Komara dakika ya 60 ambalo limeifanya timu hiyo kuendelea kukaa kileleni na pointi 18, kesho Simba inacheza na Azam FC. Hata hivyo Yanga ilicheza pungufu baada ya kiungo mshambuliaji wake Stephanie Aziz Ki kuoneshwa kadi nyekundu, baada ya mpira kumslizika mashabiki wa Yanga walionekana kumlaumu kocha wao.

Bao 6 za Simba zaondoka na kigogo wa Mighty Wonderers-

Picha
Kipigo kizito walichokipata miamba ya Malawi, Mighty Wanderers, kwenye michuano ya CAF Champions League mikononi mwa Simba SC kimeleta mtafaruku mkubwa uliomfanya Rais na Mdhamini Mkuu wa klabu hiyo, Dr Thomson Mpinganjira, kutangaza kujiuzulu rasmi. Matokeo hayo mabaya uwanjani yameonekana kuwa chanzo kikuu cha maamuzi hayo ya ghafla, yakionyesha jinsi dozi ya Mnyama Simba ilivyoingia hadi kwenye korido za uongozi wa Wanderers. Kuondoka kwa Dr Mpinganjira, ambaye pia ndiye alikuwa mwekezaji na mdhamini mkuu, kunaiweka klabu hiyo ya Malawi kwenye utata mkubwa wa kifedha kuelekea michezo inayofuata.

Niffer atangaza kudata kwa Libasse Gueye

Picha
Mfanyabiashara na mrembo maarufu nchini, Niffer, ameshangaza watu kwa maranyingine baada ya kuanza kuonyesha hadharani mahaba na ukaribu wake kwa winga hatari wa Simba SC raia wa Senegal , Libasse Gueye. Licha ya Niffer kufahamika kama shabiki lialia wa Yanga SC, mrembo huyo amezua mshtuko kwa mashabiki baada ya ku-repost post mbili za Gueye siku ya leo pekee. Huku akiweka comments zilizozua maswali mengi ikiwemo kumwita "Top Simba SC treasure" akimaanisha "Hazina kuu ya Simba SC" na kuandika kuwa anamkubali popote alipo huku akimuombea afike mbali zaidi. Gueye anaendelea kuthibitisha kuwa yeye ni X-Factor wa Simba SC msimu huu, baada ya kutangazwa Mchezaji Bora wa Agosti kwa kuhusika kwenye mabao 6 ya Ligi Kuu, leo amefunga mabao mawili dhidi ya Mighty Wanderers kwenye ushindi wa 6-1.

Kutoitwa timu ya taifa, Chama alitangaza kustaafu kitambo

Picha
Nyota wa klabu ya Simba raia wa Zambia Clatous Chota Chama "Triple C" ametangaza rasmi kustaafu kuitumikia timu ya taifa ya Zambia "Chipopolo". Na hiki ndicho alichokisema Chama JR,kwa nini amefanya Maamuzi ya kustaafu kipindi hiki:- "Muda wangu umeisha,sasa hivi Zambia kuna wachezaji wengine wengi wana nguvu.Kwahiyo hao wanaweza kuipambania bendera ya Chipopolo" -Clatous Chama, Aliyekuwa Mchezaji wa timu ya taifa ya Zambia.