Machapisho

Kassali kuivaa Coastal Union

Picha
Golikipa wa klabu ya Simba, Djibrilla Kassali ataukosa mchezo wa Ligi Kuu bara dhidi ya Pamba Jiji FC, baada ya golikipa huyo kuumia kwenye mchezo uliopita dhidi ya Kagera Sugar. Taarifa ya Ahmed Ally, meneja habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba amesema baada ya kufanyiwa vipimo vya awali, imethibitika kassali ameumia goti (msuli wa pembeni ) na ripoti ya madaktari imeeleza jeraha lake sio kubwa na halihitaji upasuaji wa aina yoyote. Kassali atarudi uwanjani kwenye mchezo unaofuata baada ya mchezo wa Pamba Jiji FC utakaochezwa jijini mwanza.

Jayrutty atakiwa kuilipa Simba bilioni 5 za mkataba wake

Picha
Mzabuni CPA Joseph Rwegasira (@joerwegasira ) mkataba wake na Simba SC, Unamtaka kutoa kiasi cha Tsh. Shilingi Bilioni 5.7 (B.5.7) kwenye mwaka wake wa kwanza kiasi ambacho kitakuwa kinaongezeka kila mwaka kwa asilimia 10% ndani ya miaka mitano ambapo jumla itakuwa Bilioni 38. JAYRUTTY mwaka wake ndani ya Simba SC hadaiwi kiasi chochote cha fedha ambacho kinamtaka kimkataba, JAYRUTTY mwaka wake wa kwanza amenunua Bus (Irizar) ambalo aliahidi kutokana na mkataba wake na Simba SC. Lakini pia JAYRUTTY kwenye mwaka wake wa kwanza amesajili mchezaji (Inno Loemba) kitu ambacho hakipo Kimkataba ni Utashi wake tu mwenyewe. Wachezaji kama Kassali, Anicet Oura, Libasse Gueye, Ismael Toure na Inno Loemba kila mmoja alinunuliwa gari na JAYRUTTY jambo ambalo halipo Kimkataba amefanya tu kwa mapenzi na utashi wake. Sijajua wanaosema Mzabuni wa jezi JAYRUTTY hatoshi wanatumia nini kufikiri? Lakini pia sijui kwanini upande wa Tajiri MO DEWJI unamuona CPA Joseph Rwegasira kama tatizo wakati anaisaidi...

George Mpole atambulishwa Mashujaa FC

Picha
Kiungo mshambuliaji mpya wa Yanga, Stephane Aziz KI akiwa katika mazoezi ya kikosi hicho katika viwanja vya Avic Town Kigamboni Yanga wanapiga tizi kujiandaa na mchezo unaofuata wa ligi kuu Tanzania Bara dhidi ya Coastal Union utakaopigwa Alhamisi agosti 20,2026 Seleman Mwalimu naye alikuwepo katika viwanja hivyo vya mazoezi Avic Town ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu asajiliwe na Yanga

Stephanie Aziz Ki mzigoni Avic Town

Picha
Kiungo mshambuliaji mpya wa Yanga, Stephane Aziz KI akiwa katika mazoezi ya kikosi hicho katika viwanja vya Avic Town Kigamboni Yanga wanapiga tizi kujiandaa na mchezo unaofuata wa ligi kuu Tanzania Bara dhidi ya Coastal Union utakaopigwa Alhamisi agosti 20,2026 Seleman Mwalimu naye alikuwepo katika viwanja hivyo vya mazoezi Avic Town ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu asajiliwe na Yanga

Injinia Hersi awatoa wasiwasi Wanayanga

Picha
Rais wa Yanga SC, Injinia Hersi Said, alitangaza rasmi uamuzi wa klabu hiyo kumuuza Allan Okello kuelekea msimu wa 2026/27. Akizungumza wakati wa utambulisho wa Stephane Aziz Ki, Hersi amesema mashabiki hawapaswi kuwa na wasiwasi kuhusu kuondoka kwa Okello, akisisitiza kuwa milango ya Yanga itabaki wazi endapo mchezaji huyo atahitaji kurejea Jangwani. Hersi Said: “Licha ya kwamba tumemuuza Okello, lakini hapa kwake ni nyumbani. Atarudi wakati wowote tukitaka kumrudisha au akitaka kurudi.”Okello alijiunga na Yanga Januari 2026 akitokea Vipers ya Uganda na ndani ya miezi saba aliweka alama kubwa, akimaliza msimu akiwa mfungaji bora wa Yanga kwenye Ligi Kuu kwa mabao 14. Kwa mujibu wa taarifa zilizopo, Okello ameuzwa kwenda ASFAR Rabat ya Morocco, klabu inayofundishwa na kocha wa zamani wa Yanga, Pedro Gonçalves.

JKT Tanzania yafunga usajili na mchezaji wa Yanga

Picha
Klabu ya JKT Tanzania imetangaza kukamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji Offen Chikola kutoka Yanga SC, huku ikimtaja kama ‘X-Factor’ wa kikosi hicho kwa msimu wa NBC Premier League 2026/27. JKT Tanzania imesema usajili huo umekamilika baada ya kukamilisha taratibu za kumpata Chikola, ikiwa ni sehemu ya maboresho ya kikosi kwa msimu ujao. “Kilio cha mashabiki wa JKT Tanzania kuwa wanataka X-Factor kimewafikia viongozi wetu wasikivu, nao wakasema mali hii itacheza JKT Tanzania FC msimu huu,” imeeleza taarifa ya klabu hiyo. Chikola amewahi kuzitumikia Singida Black Stars na Tabora United kabla ya kujiunga na Yanga SC.

Ismail Mgunda mseme nyie.....

Picha
Ismail Mgunda ameanza kazi rasmi katika kikosi cha Simba SC, mchezaji huyo anayecheza nafasi ya mshambuliaji wa kati amesajiliwa kwenye dirisha kubwa akipewa matumaini makubwa. Mgunda amejiunga na kikosi hicho akitokea timu ya Mashujaa FC ya Kigoma, anakamilisha safi ya ushambuliaji yenye nyota watatu wakiwemo Elie Mpanzu raia wa DR Congo na Ibrahim Doumbia raia wa Mali.