Machapisho

Depu aanza na goli Petro de Luanda

Picha
Mshambuliaji wa zamani wa Young Africans, Laurindo Depu, leo ameanza kuonyesha makali yake baada ya kufunga bao moja katika ushindi wa 2-0 wa Petro de Luanda dhidi ya Académica do Lobito kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Angola. Hili ni bao lake la kwanza Depu tangu ajiunge na miamba hiyo ya Angola.

Maua Sama kuwa mama mtarajiwa

Picha
Msanii wa Bongo Flava Maua Sama ameamua kuwafahamisha mashabiki zake kuwa anatarajiwa kuwa mama hivi karibuni baada ya ku-share picha zake mpya ambazo zimemuonyesha akiwa mjamzito baada ya tetesi kusambaa mitandaoni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Maua ameweka picha hizo akisindikiza na ujumbe uliosomeka, “Am grateful Alhamdulillah, post ambazo imepata comments mbalimbali za wasanii na mashabiki zake wakimpa hongera na kumtakia kheri. Maua Sama

Nabi ajiuzuru

Picha
Kocha Nasreddine Mohammed Nabi, rasmi amejiuzulu nafasi yake ya kocha mkuu ndani ya Raja CA baada ya kinachosemwa kutofautiana na mkurugenzi wa michezo "sporting director" wa klabu hiyo. Moja ya makubaliano ambayo Nabi alitilia mkazo wakati anasaini mkataba ni pamoja na kuhusishwa kwenye usajil wa wachezaji wapya ikiwemo matakwa yake yeye na moja ya wachezaji aliowakosa na kupelekea mzozo ni Thapelo Maseko ambaye ametimkia Copenhagen Nabi alikua anamtaka huku Sporting Director anasema hafai kwenye mpango wa klabu Nabi amehudumu ndani ya Raja CA kwa muda wa miezi 2 na nusu sawa na siku 78 tu tangu alipoteuliwa June 12, 2026 Kwasasa Nabi yuko zake huko Brussels, Ubelgiji kupumzika lakini kusikilizia majibu ya uongozi wa Raja CA kuhusu barua yake

Steve Barker aihofia safu ya ushambuliaji Geita

Picha
Kocha Mkuu wa Simba SC, Steve Barker, ameweka wazi kuwa kikosi chake kinakabiliwa na changamoto ya kuwakosa wachezaji kadhaa katika mchezo unaofuata dhidi ya Geita Gold, huku akiahidi kuwa wamejipanga vizuri kwa ajili ya ushindani huo. Barker ameeleza kuwa kuna idadi kubwa ya wachezaji wanaoweza kukosa mchezo huo kuliko inavyofikiriwa, kutokana na adhabu na majeraha mbalimbali. Amesisitiza kuwa kukosekana kwa wachezaji hao ni sehemu ya mchezo na benchi la ufundi linaendelea kujiandaa vyema ili kuwa tayari kukabiliana na Geita Gold. Akizungumzia wapinzani wao, kocha huyo amekiri kuwa Geita Gold ni timu nzuri, iliyofundishwa vyema na inayojua kufunga mabao, hivyo anatarajia mchezo mgumu wenye ushindani wa hali ya juu.

Dube atakata Hardrock

Picha
Prince Dube na Hardrock FC wametinga hatua ya robo fainali baada ya kuwatwanga kama mihogo Jordan Sinoti kwenye kombe la Munhumatapa Challenge Cup Katika mchezo huo Dube aliianza lalini hakufamikiwa kufunga kwenye karamu ya mabao 5-1 FT: Hardrock 5-1 Jordan Sinoti

Kocha Geita Gold aizimia Simba

Picha
Kocha wa Geita Gold, Zubery Katwila, amesema kesho wanakutana na timu bora ambayo inaendelea kuimarika zaidi kiuchezaji dimbani. Katwila amesema kadri siku zinavyosonga, Simba inaendelea kuwa bora zaidi, hivyo wao kama Geita Gold wamejiandaa na mbinu zitakazowasaidia kufanya vizuri. Pia amesema watajaribu kutumia makosa ambayo Simba itafanya ili kuwapa adhabu uwanjani na kutafuta matokeo mazuri.

Magori atamba kuifunga Geita Gold kesho

Picha
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya klabu ya Simba SC, Crescentius Magori akielezea mchezo dhidi ya Geita Gold unaotarajiwa kupigwa tarehe 31.8.2026 pale Meja Gen. Isamuhyo. "Kila mchezo tunaocheza tukiwa nyumbani hakuna budi kushinda, kwa maana mechi zote tushinde tukiwa nyumbani kama tulivyoshinda za ugenini. "Pia timu kama Geita FC, kwetu sisi ni kama marafiki, kwa hiyo utakuwa mchezo ambao tunapambana na timu tunayoijua vizuri". Anaongeza kuwa "Nasema hivyo kulingana na timu yetu tuliyo nayo. kucheza mechi moja na kupoteza sio ndio kushindwa, ila ndio mwanzo mzuri wa kujua wapi tumekosea, wapi tuboreshe. *Tazama mchezo wetu dhidi ya Coastal Union, tulicheza vizuri bila kadi yoyote nyekundu kama mechi za ugenini. "Tunahitaji kuweka heshima, ndio kila kitu kwenye mpira, kwa hiyo na hilo tumelishughulikia vikali na sasa tunashinda kama kawaida", Anamaliza.