Machapisho

Seleman Mwalimu aisawazishia Yanga

Picha
Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika Dar Young Africans maarufu Yanga, usiku huu wamenusurika kulala baada ya kutoka sare ya 1-1 na Gaborone United uwanja wa Taifa nchini Botswana. Gaborone United walikuwa wa kwanza kupata bao kipindi cha kwanza lililofungwa na Obry Amseb dakika ya 33 kwa mpira wa kutenga, iliwachukua Yanga dakika ya 90 kusawazisha goli hilo likifungwa na Seleman Mwalimu Gomez. Yanga wanapata sare muhimu ya 1-1 ugenini baada ya bao la dakika za mwisho

Seleman Mwalimu amjibu Chama

Picha
Baada ya Clatous Chama kudai kuwa Seleman Mwalimu huenda akawa anajutia kujiunga na Yanga SC baada ya kuikataa Simba, mshambuliaji huyo ameibuka na kutoa majibu. Mwalimu amesema yupo na furaha kubwa Yanga na haoni sababu ya kulalamika, akisisitiza kuwa anafurahia maisha yake ndani ya klabu hiyo. “Kaka nipo na furaha sanaaaaaaa na enjoy kuwa hapa Yanga ya moto mzee. Wanasema nilalamike kwa kipi mzee? Huku maisha safi, Hamdullilah na enjoy kuwa hapa.” — Seleman Mwalimu kupitia Instagram

Seif Karihe atambulishwa Mtibwa Sugar

Picha
Klabu yenye historia kubwa kwenye soka la Tanzania, Mtibwa Sugar, imetangaza rasmi usajili wa mshambuliaji hatari Seif Karihe, ambaye ametua klabuni hapo akitokea Mashujaa FC ili kuongeza makali kwenye safu yao ya ushambuliaji. Uongozi wa Mtibwa Sugar umeridhishwa na uwezo wa mshambuliaji huyo, wakiamini uzoefu wake utasaidia kwa kiasi kikubwa kwenye mashindano ya ligi. Kupitia kauli mbiu yao ya “United WeStand”, wakazi wa Turiani na familia nzima ya Wana-Manungu wamemkaribisha mchezaji huyo kwenye "nyumba ya vipaji."

Simba nao kama Yanga, yatoa msaada kwa watoto Malawi

Picha
Klabu ya Simba imetembelea na kutoa msaada kwenye kituo cha kutunza watoto cha Ministry of Hope Crisis kilichopo hapa Lilongwe, Malawi kama sehemu ya kurudisha kwa jamii kuelekea mchezo wa kesho wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Al Ahli Tripoli yaisurubu bila huruma KMKM

Picha
Fiston Kalala Mayele na wenzake wameonyesha ubora mkubwa baada ya kuichapa KMKM 3-0 kwenye Uwanja wa New Aman Complex. Al Ahli Tripoli wameanza kwa kishindo safari yao ya CAF Confederation Cup, huku Mayele akiendelea kuonyesha makali yake! Mabao mengine ya Tripoli yamefungwa na Mahdou El Houni dakika ya 20 na Hocine Dehiri dakika ya 27, Mayele akifunga dakika ya 22 KMKM sasa wana kazi kubwa ya kwenda kupindua meza ugenini kwenye mchezo wa marudiano

Pacome awatakia kila kheri Yanga

Picha
Kiungo mshambuliaji aliyekwenye maumivu Pacome Zouzoua amewatumia salamu Watanzanis hasa klabu yake ya Yanga. "Kila la kheri familia nzima ya Yanga kwenye safari ya Ligi ya Mabingwa. Isivyo bahati kutokuwepo kwangu kunanizuia mimi kuwa nanyi dimbani, lakini moyo wangu na fikra zipo pamoja nanyi” Ni sehemu ya andiko la nyota wa Yanga SC, Pacome Zouzoua akiitakia heri timu yake ambayo leo itaanza mikikimikiki ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Gaborone United ya nchini Botswana. Pacome amewataka wachezaji wenzake kujitoa kwa kila hali ili kuipambania jezi yao na kuongeza kuwa atakuwa pamoja nao hata kama yeye yupo mbali.

Yanga na GSM Foundation zatoa msaada kwa watoto Botswana

Picha
Uongozi wa Klabu ya kwa kushirikiana na GSM Foundation leo umetembelea kituo cha Ramotswa Centre for Deaf Education na kuwapatia mahitaji mbalimbali kwa ajili ya kituo hicho. Kituo hiki kinatoa huduma za makazi (boarding) na malezi ya awali kwa watoto wenye changamoto za kusikia, kwa lengo la kuwasaidia kupata elimu, malezi na mazingira bora ya kukua na kujiendeleza.