Salah atambulishwa Trabzonsor
Mohhamed Salah sasa ni rasmi mchezaji wa Trabzonspor, akijiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili unaoripotiwa kuwa na thamani ya €17 milioni kwa mwaka, sawa na takribani TSh bilioni 51 kwa mwaka. Mkataba huo unatajwa kuwa na: €10 milioni mshahara — takribani TSh bilioni 30 kwa mwaka. €7 milioni bonasi ya kusaini — takribani TSh bilioni 21. 20% ya mapato yatokanayo na mauzo ya bidhaa zenye chapa ya Salah. Hivyo Kwa miaka miwili, thamani ya mshahara na bonasi pekee inaweza kufikia takribani TSh bilioni 102.