Machapisho

Chobwedo akwama Simba

Picha
Uhamisho wa Winga Ramadhani Chobwedo kujiunga na Simba SC kutoka TRA United FC umeshindikana katika hatua za mwisho baada ya Winga huyo kushindwa kufuzu vipimo vya afya! . Ramadhani Chobwedo alikuwa amesaini mkataba wa awali wa Simba SC na kilichokuwa kimebaki ni kusaini mkataba rasmi lakini Simba SC ilimfanyia vipimo vya afya kabla ya kumsainisha mkataba na kumkuta na majeraha ya muda mrefu na Simba SC imesitisha mchakato wa kupata huduma yake kwaajili ya msimu ujao wa 2026-27 na Chobwedo ataendelea kubaki TRA United FC

Hassan Mubiru atambulishwa Azam FC

Picha
KLABU ya Azam FC imemtambulisha winga wa kulia wa Kimataifa wa Uganda, Hassan Mubiru (21) kutoka SC Villa ya kwao, Kampala akiwa mchezaji mpya wa tano kuelekea msimu ujao. Wengine ni mabeki wa kati, Lupini Mawuku Dieumerci (20) kutoka AS Maniema Union ya kwao, DRC na Henri Braham Stanic Mbelgiji mwenye asili ya DRC pia kutoka Stellenbosch FC ya Afrika Kusini. Azam FC pia imesajili mawinga wengine wawili,, Henoc Molia (22) kutoka St. Eloi Lupopo ya kwao, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Muivory Coast, Kipré Tiagori Emmanuel Junior Zunon ‘Kipre Junior’ aliyejiunga tena na Azam FC akitokea MC Algiers ya Algeria. Kipre Junior amerejea Azam FC ambako awali alicheza kuanzia msimu wa 2022-2023 akitokea SOL FC d’Abobo ya kwao, Ivory Coast hadi 2024-2025 alipohamia MC Algiers. Hassan Mubiru Azam Football Club

Yanga yaanza na kinda

Picha
KLABU ya Yanga imemtambulisha mshambuliaji chipukizi, Hussein Juma Mihambo (19) kutoka Mashujaa FC kuwa mchezaji wake mpya kuelekea msimu ujao. Anakuwa mchezaji wa pili tu mpya baada ya chipukizi mwingine, winga Juma Issa Abushiri ‘Chuga Boy’ (18) kutoka Fountain Gate FC. Hussein Juma Mihambo  Young Africans Sports Club

Yanga na Simba kuanzia ugenini Ligi Kuu bara

Picha
VIGOGO wote, Simba na Yanga wataanzia ugenini msimu mpya wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara dhidi ya timu za Namungo FC na Kagera Sugar katikati ya mwezi ujao. Wakati mabingwa watetezi, Yanga SC watakuwa Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi dhidi ya wenyeji, Namungo FC Agosti 15, watani wao na washindi wa pili wa msimu uliopita, Simba SC watakuwa Uwanja wa Kaitaba, Bukoba dhidi ya wenyeji, Kagera Sugar siku itakayofuata Agosti 16.

Chilambo kumrithi Kapombe Simba

Picha
KLABU ya Simba imemtambulisha beki wa kulia, Nathaniel Raphael Chilambo (22) kuwa mchezaji wake mpya kuelekea msimu ujao akijiunga na Wekundu hao wa Msimbazi kutoka Azam FC. Anakuwa mchezaji mpya wa pili baada ya kiungo wa ulinzi, Kelvin Nashon Naftali (25) aliyetambulishwa jana kutoka Pamba Jiji FC ya Mwanza. Nathan Chilambo Nashon Kelvin Simba Sports Club

Simba yaanza na Kelvin Nashon

Picha
KLABU ya Simba SC imemtambulisha kiungo Kelvin Nashon Naftali kuwa mchezaji wake mpya kwanza kuelekea msimu ujao akijiunga na Wekundu hao wa Msimbazi kutoka Pamba Jiji FC ya Mwanza.

Hispania mabingwa kombe la Dunia

Picha
TIMU ya Hispania imefanikiwa kutwaa Kombe la Dunia baada ya kuwafunga waliokuwa mabingwa watetezi, Argentina bao 1-0 usiku huu katika mchezo uliodumu kwa dakika 120 na ushei Uwanja wa MetLife mjini East Rutherford, Bergen County, New Jersey nchini Marekani. Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, mshambuliaji wa Barcelona, Ferran Torres García dakika ya 106 akimalizia pasi ya winga wa Athletic Bilbao, Nicholas Williams Arthuer mwenye asili ya Ghana. Hispania ilicheza pungufu dakika zote 30 za nyongeza baada ya kiungo wake, Enzo Jeremías Fernández anayechezea klabu ya Chelsea ya England kutolewa kwa kadi nyekundu kufuatia kuonyeshwa kadi ya pili ya njano kwa kumchezea rafu beki wa Barcelona na Hispania, Pau Cubarsí Paredes dakika ya 90’+3 . Gwiji wa Argentina alikuwa mnyonge wa kutia huruma baada ya kipyenga cha mwisho akimshuhudia mchezaji aliyempakata akiwa mtoto, Lamine Yamal Nasraoui Ebana wa Barcelona mwenye asili ya Morocco kupitia kwa baba yake na Equatorial Guinea kupitia kwa m...