Machapisho

Simba kutumia uwanja wa Uhuru mechi za kimataifa

Picha
Uhuru Stadium inaendelea kujiandaa kikamilifu kwa ajili ya usiku wa soka la kimataifa, huku uwanja huo ukitarajiwa kuwa mwenyeji wa mchezo wa nyumbani wa Simba SC katika hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF Champions League) mwishoni mwa wiki ijayo. Jukwaa linaandaliwa, Simba inajiandaa ni muda wa Wanasimba kuonyesha nguvu zao kwenye anga za CAF

Yanga yazindua jezi za kimataifa

Picha
Klabu ya Young Africans (Yanga SC) imefanya uzinduzi wa kipekee wa jezi zao mpya zitakazotumika katika michuano ya kimataifa ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika (CAF Champions League) kwa kumtumia mwandishi nguli wa habari za usajili duniani, Fabrizio Romano.  Uzinduzi huo wa aina yake umefanyika kupitia video iliyochapishwa kwenye ukurasa wa Instagram wa @liveherewego unaomilikiwa na mwandishi huyo. ​Katika video hiyo, Fabrizio Romano anaonekana akifungua kisanduku maalum chenye jezi tatu mpya za Yanga zilizotengenezwa kwa ajili ya ushindani wa barani Afrika.  Mwandishi huyo maarufu alitumia fursa hiyo kuitambua na kuipongeza klabu hiyo, huku akiitaja rasmi Yanga kama klabu kubwa zaidi nchini Tanzania. ​Pamoja na kuzionyesha jezi hizo kwa mashabiki wa soka ulimwenguni, Romano alihitimisha ujumbe wake kwa kutumia msemo maarufu unaotumiwa na Wana-Yanga pamoja na mdhamini wao GSM wa "Yanga Bingwa".  Hatua hii ya masoko imepokelewa kwa hisia kubwa na mashabiki wa soka nchini, ikio...

Simba yaja na Marathon

Picha
“Wote mnafahamu mwaka huu Simba tumefikisha miaka 90 tangu kuanzishwa kwa klabu yetu kwa kuzingatia hilo tumeandaa matukio mengi ya kufikisha miaka 90. Kufikisha miaka sio jambo jepesi, kufanikiwa kufikia hatua hiyo haiwezi kupita kimya kimya. Lazima ipite kwa matukio mbalimbali ya kuazimisha miaka 90. Ndani ya miaka 90 sio tu imekuwa klabu kongwe lakini klabu kongwe yenye mafanikio.” “Tulifungua sherehe za miaka 90 kwa kwenda hifadhi ya Ngorongoro na linabaki kuwa tukio bora ambalo limewahi kutokea kwenye hifadhi ya Ngorongoro. Kwa mujibu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ilivunja rekodi ya msafara mkubwa wa watu kuingia hifadhini kwa wakati mmoja. Simba tumefanikiwa kwa kufanya jambo hilo, na hilo lilifanyika kuadhimisha miaka 90. Baada ya hapo tulienda kwenye Simba Day ambayo tunaijua na sherehe za miaka 90 ya Simba. Tukasema tuendelee na maadhimisho haya hadi tamati ya mwaka 2026.” “Vilabu vingi vimeshafanya jogging na hata sisi tulifanya jogging mwaka jana lakini hii ni maratho...

Yanga SC yarudi uwanja wa Azam Complex

Picha
YANGA SC itautumia Azam Complex kama uwanja wao wa nyumbani katika mchezo wa marudiano dhidi ya Gaborone United kwenye michuano ya CAF Champions League.Azam Complex,12 Septemba 2026,19:00 . Mchezo huo unatarajiwa kuwa muhimu kwa Yanga katika harakati za kusonga mbele kwenye hatua inayofuata ya mashindano hayo ya kimataifa. Wananchi, maandalizi yanaanza! Azam Complex ndiyo itakuwa sehemu ya Yanga katika usiku wa kusaka tiketi ya hatua inayofuata ya CAF Champions League.

Yanga yawasili salama

Picha
Kikosi cha Yanga SC kimewasili jijini Johannesburg Afrika Kusini kabla ya kuelekea Gaborone nchini Botswana. Yanga itakabiliana na Gaborone United siku ya terehe 5, mwezi huu, wachezaji wake wamekuwa na hali nzuri kabla ya kushuka uwanjani.

Kante apata timu Algeria

Picha
Aliyekuwa kiungo wa Simba SC, Alassane Kanté ametangazwa rasmi kama mchezaji mpya wa klabu ya JS EI Biar inayoshiriki Ligi Kuu ya Algeria (Ligue 1) kama mchezaji huru baada ya kuvunja mkataba na Simba SC kwa maslahi ya pande zote mbili. Kante (25) raia wa Senegal amesaini mkataba wa miaka miwili utakaombakisha kwenye klabu hiyo iliyopanda daraja msimu huu kwenda Ligue 1 ikitokea Ligue 2 mpaka Juni 2028.

Fofana wa Yanga atambulishwa Ufaransa

Picha
Kungo mshambuliaji Souleymane Fofana (20) amekamilisha uhamisho wake wa kujiunga na klabu ya FC Annecy ya Ufaransa kutoka ASEC Mimosas akiwa MVP wa Ligi Kuu ya Ivory Coast kwa msimu wa 2025-26. Souleymane Fofana amesaini mkataba wa miaka minne hadi 2030 kwa FC Annecy ya Ligi daraja la pili nchini Ufaransa