Machapisho

Ndayiragije atupiwa virago TRA

Picha
Klabu ya TRA United SC imethibitisha kufikia makubaliano ya kusitisha mkataba na kocha mkuu Etienne Ndayiragije kwa makubaliano ya pande zote mbili kuanzia Septemba 7, 2026. Taarifa hiyo iliyotolewa na uongozi wa klabu hiyo huku ukimshukuru kwa dhati Kocha Ndayiragije kwa mchango wake mkubwa, weledi, na huduma ya kipekee aliyoitoa kwa timu katika kipindi chote alichokuwa sehemu ya klabu hiyo na kumtakia kila la kheri na mafanikio mema katika hatua inayofuata ya maisha na taaluma yake ya ukocha. Kwa mujibu wa taarifa hiyo TRA United itaendelea kuwasiliana na wanachama, mashabiki, na wadau wake kuhusu hatua zaidi zinazohusiana na uongozi wa benchi la ufundi la timu hiyo. Kocha huyo ameondolewa kwenye nafasi hiyo kufuatia mwenendo usioridhisha wa klabu hiyo ambayo imekusanya alama tatu kwenye michezo mitano huku ikishindwa kupata ushindi, vipigo viwili na sare tatu.

Gamondi azitembelea klabu za Ligi Kuu

Picha
Kocha wa Timu ya Taifa Taifa Stars_ Miguel Gamondi ameanza ziara ya kutembelea Klabu za Ligi Kuu ya NBC kwa lengo la kubadilishana mawazo na kufanya kazi kwa karibu ili kuimarisha mahusiano ya klabu na timu za Taifa. Gamondi ameanza ziara hiyo kwa ku tembelea klabu ya Azam FC

Nywele za Donald Trump zazua tafrani

Picha
Nywele za dhahabu za Rais wa Marekani Donald Trump zilionekana kuwa nyeusi zaidi—karibu na rangi ya udongo (brunette)—katika picha zilizopigwa alipokuwa akishuka kwenye ndege ya Air Force One huko Morristown, New Jersey, siku ya Ijumaa. Hali hiyo imezua uvumi mkubwa na utani mtandaoni kuhusu uwezekano wa kubadili rangi au mtindo wa nywele zake.

Arobaini ya mtoto wa Zuchu yatajwa

Picha
Mrembo Esma Platnumz ambaye ni dada wa Diamond Platnumz ameutumia ukurasa wake wa instagram kuitaja tarehe ya arobaini ya mtoto wa Zuchu na Diamond kuwa ni tarehe 12 mwezi huu . Esma Platnumz ameeleza kuwa hii itakuwa ni season 2 ya mwana kakua baada ya ile ya kwanza kule hospitalini. ''Season 2 ya mwana kakua Madale tarehe 12 mwezi huu''Ameandika -Esma Platnumz

Mbunifu wa jezi za Yanga, aibukia Chelsea

Picha
Aliyekuwa mbunifu rasmi wa jezi za Yanga SC na Zanzibar Heroes, Sheria Ngowi, amezua gumzo mtandaoni baada ya kuonyesha jinsi jezi alizobuni nyuma zilivyotangulia mitindo kabla ya makampuni makubwa duniani kama Nike, Adidas, na Macron kuitumia hivi karibuni. Chelsea FC vs Yanga SC: Mtindo wa mawingu/madoa ya bluu aliotengeneza kwenye jezi ya Yanga SC (2023/24) unafanana na ule uliotumiwa na Nike kwa Chelsea FC (2026/27). PSG vs Yanga SC: Muundo wa mistari inayopishana aliozindua Yanga SC (Julai 2022) uliitangulia jezi ya PSG x Jordan (Januari 2023). Crystal Palace vs Yanga SC: Jezi ya dhahabu yenye ukola aliyoibuni kwa Yanga SC (Novemba 2024) ilitoka kabla ya Macron kuitumia kwa Crystal Palace (Agosti 2025). Argentina vs Zanzibar Heroes: Nakshi za urembo kwenye jezi ya Zanzibar Heroes (2024) zinafanana na muundo mpya wa Adidas kwa Argentina 🇦🇷 (2026). NOTE: Ngowi anadhihirisha kuwa kazi za wabunifu wa nyumbani zina kiwango cha kimataifa na zimekuwa zikiongoza mitindo duniani (setting...

Mtanzania aanza kwa ushindi Algeria

Picha
KIUNGO wa Mtanzania, Alphonce Mabula ameanza na mguu mzuri kwenye Ligi Kuu ya Algeria baada ya chama lake kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya MB Rouissat katika mchezo wao wa kwanza. Mabula, ambaye kwenye mchezo huo alianzia benchi alieleza kuwa mchezo ulikuwa na ushindani mkubwa na timu yake ilifanikiwa kupata pointi tatu muhimu. Akizungumza na Mwanaspoti Mabula amesema amesema amevutiwa na kiwango cha ushindani huku akidai Ligi ya Algeria ina ushindani unaoweza kufananishwa na baadhi ya ligi za Ulaya, jambo ambalo limeifanya safari yake mpya kuwa yenye changamoto na kuvutia. Mabula amesema hali hiyo inaonyesha wazi ukubwa wa ushindani wa ligi hiyo, akisisitiza kuwa si mashindano yanayotawaliwa na klabu mbili au tatu pekee, bali timu nyingi zina uwezo wa kufanya vizuri na kupambana kwa ajili ya mataji. Mabula ambaye alitambulishwa hivi karibuni kwenye kikosi cha JS Kabylie ya Algeria akitokea Shamakhi FC ya Ligi Kuu Azerbaijan alipokuwa na msimu bora.

Mume wa Rais Samia afariki dunia

Picha
Mume wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, Hafidh Ameir, amefariki dunia. Taarifa za kifo cha Hafidh Ameir, zimetangazwa na Makamu wa Rais, Deogratius Ndejembi kupitia vyombo vya habari.