Machapisho

Duchu kazi anayo kwa Chilambo

Picha
Nathaniel Chilambo ni bonge la fullback wa kulia na kwa kiwango alichonacho, hivi karibuni anaweza kuanza kumpa presha kubwa David Kameta Duchu kwenye nafasi hiyo. Chilambo alionyesha uwezo mkubwa tangu akiwa Azam FC, tatizo lilikuwa ushindani wa namba. Sasa akiwa Simba, kwa kuangalia kiwango chake pamoja na umri wa Kapombe, naamini ushindani wa fullback wa kulia utakuwa mdogo sana kwake. Kwa kifupi, Chilambo namba ya David kameta duchu ameichukua mapema maana duchu amejichanganya sana kwenye kadi nyekundu.

BMT yatoa ufafanuzi Katiba ya Simba

Picha
Baraza la Michezo la Taifa, BMT, limetoa ufafanuzi kwa umma, wanachama na wadau wa Klabu ya Simba kuhusu utekelezaji wa Katiba iliyorekebishwa ya klabu hiyo iliyoidhinishwa tarehe 18 Februari, 2026, hatua inayokuja baada ya mashabiki na wanachama wa klabu ya hiyo kulalamima kuhusu utekelezaji wa katiba mpya. Taarifa iliyotolewa leo Agosti 19, 2026 na Katibu Mtendaji wa BMT, Neema Y. Msitha, imeeleza kuwa marekebisho ya Katiba ya Simba yalipitishwa na Mkutano Mkuu wa Wanachama wa Klabu ya Simba mnamo Novemba 30, 2025, na kuwasilishwa kwa Msajili wa Vyama na Vilabu vya Michezo kwa uchambuzi na kuidhinishwa kwa mujibu wa sheria na kanuni husika ambapo baada ya uchambuzi huo, BMT kupitia Msajili ilikabidhi rasmi Katiba hiyo kwa Simba ili ianze kutumika. Taarifa hiyo imeeleza kuwa Serikali imefafanua kuwa ilikamilisha wajibu wake wa kuidhinisha na kukabidhi Katiba hiyo na kuanzia hapo, wajibu wa kutekeleza Katiba na kukamilisha mabadiliko yaliyopitishwa na wanachama ni wa Klabu ya Simba yen...

Simba yaiziba mdomo Pamba Jiji

Picha
Timu ya Simba jioni ya leo imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Pamba Jiji katika muendelezo wa Ligi Kuu bara katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Mabao ya Simba yalifungwa kipindi cha kwanza na Clatous Chama na Anicet Oura wakati goli la kufuatia machozi la Pamba limefungwa kwa mkwaju wa penati iliyotibua ‘clean-sheet’ kwa Simba; Idrisa Diomande. Kwa matokeo hayo Simba insfikisha pointi 6 na kukaa kileleni baada ya kucheza mechi mbili.

Haruna Chanongo silaha ya Mashujaa FC

Picha
Mashujaa FC ya Kigoma Itanufaika sana kwa kuwa na huduma ya Kiungo Mshambuliaji, Haruna Chanongo mwenye umri wa miaka (32) kwa Mkataba wa mwaka mmoja akitokea Klabu ya Tanzania Prisons SC ya Jijini Mbeya. Haruna Chanongo Amejiunga na Mashujaa FC akiwa Mchezaji huru baada ya kumaliza Mkataba wake na Tz Prisons SC, Nyota huyo Amewahi Kuzitumikia Klabu za Simba SC, Mtibwa Sugar, Pamba Jiji FC kabla ya Kujiunga na Tanzania Prisons SC ya Jijini Mbeya.

Yanga yatoa tamko kuhusu Mwenda

Picha
Klabu ya Yanga imekanusha shutuma kwamba imewahi kumtuhumu mchezaji wake Israel Patrick Mwenda kwa “Kuuza” mechi na haijawahi hata kumuandikia barua ya kumsimamisha kazi. Yanga SC wanasema mchezaji ni MTORO kazini na hajulikani alipo na wamekuwa wakimuandikia barua za kutaka kujua alipo na kwanini hafiki kazini, lakini mchezaji hajawahi kujibu na wala hajataka kuripoti kazini. Hali hii imeifanya klabu kutomuingizia mshahara wake kwakuwa ni mtoro kazini na hajulikani alipo. Inasemekena mchezaji aliondoka kambini kwa kuandika barua ambayo Bin Kazumari imeiona ikiwa na tarehe 03/07/2026 na kichwa cha habari UAMUZI WANGU WA KUJIWEKA PEMBENI. Kwenye barua hiyo mchezaji alisema amejithamini na kuona kwamba “uamuzi huo ulihitaji ujasiri mkubwa, lakini niliuchukulia kama sehemu ya uwajibikaji wangu ishara ya kuheshimu malengo ya pamoja ya timu”. Yanga SC inamtambua Israel kama mchezaji wake mwenye mkataba lakini ametoweka bila taarifa “Absent Without Leave - AWOL” kwenye kituo cha kazi. Katika...

Simba leo kuwakosa wachezaji wake wawili

Picha
Klabu ya Simba SC, inayofundishwa na Kocha Steve Barker, ina kibarua kizito leo Agosti 19, 2026, itakapokutana na Pamba Jiji FC katika mchezo wa NBC Premier League huku ikiwa bila huduma ya nyota wake wawili muhimu. Mchezo huo, ambao utakuwa wa pili kwa timu zote mbili katika msimu huu, unatarajiwa kuchezwa katika Uwanja wa CCM Kirumba saa 10:15 jioni. Simba SC inatarajiwa kumkosa mlinda mlango wake namba moja, Mamadou Kasali, ambaye alipata maumivu katika mchezo uliopita dhidi ya Kagera Sugar. Hali hiyo inatarajiwa kumpa nafasi kipa namba mbili, Hussein Abel, kuanza katika dakika 90 za mchezo huo.Mbali na Kasali, Simba pia itamkosa beki David Kameta Duchu. Beki huyo wa upande wa kulia alionyeshwa kadi nyekundu dakika ya 53 katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar baada ya kumchezea faulo beki David Luhende. Uamuzi wa kumtoa Kameta Duchu ulifikiwa baada ya mfumo wa FVS (Football Video Support) kutumika na mwamuzi wa kati, Saad Mrope, kufanya maamuzi.