Machapisho

Manqoba amuhofia Mgunda

Picha
Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga Manqoba Mngqithi ameweka wazi kuwa anaamini kuwa Namungo watacheza kwa kujihami zaidi na kujiamini na amekiri kuwa Namungo wana Kocha mzuri sana Juma Mgunda. "Ninaamini Namungo watakuja kwa kujiamini na kujihami kwa wakati huo huo, najua wana kocha mzuri sana na namjua tangu akifundisha timu ya Taifa, Hivyo nasisi tutatumia Ubora wetu na tutatengeneza nafasi zetu ili kushinda mechi" Aidha kocha huyo ameongeza kuwa hawajapata muda mzuri wa kujiandaa na Mechi dhidi ya Namungo. "Kwakweli hatujapata muda mrefu wa kujiandaa dhidi ya Namungo lakini kwa namna tulivyojipanga tangu mchezo wa Derby naamini tutakuwa kwenye mfumo wetu ule ule na Nina amini tutapata Matokeo mazuri" -Manqoba Mngqithi (Kocha wa klabu ya Yanga kupelekea mchezo wa Ligi kuu ya NBC hapo kesho dhidi ya Namungo FC).

Kiungo wa boli atimkia Libya

Picha
Kiungo James Akaminko (30) raia wa Ghana ametambulishwa rasmi kama mchezaji mpya wa klabu ya Al-Akhdar SC ya nchini Libya kwa uhamisho huru akitokea klabu ya Azam FC ya Tanzania. Akaminko amesaini mkataba wa mwaka mmoja utakaombakisha klabuni hapo mpaka Juni 2027 akihitimisha utumishi wake kwa Wanalambalamba tangu ajiunge nayo mwaka 2022 akitokea Great Olympics ya Nchini kwao Ghana.

Mdogo wake Ngassa aweka aweka rekodi Ligi Kuu bara

Picha
Mshambuliaji wa Dodoma Jiji FC, Beno Ngassa ndiye mfungaji wa bao la kwanza kwenye NBC Premier League msimu wa 2026/27 akifunga bao hilo dhidi ya Pamba Jiji FC katika uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza wakati timu hizo zikitoshana baada ya nusu saa ya mchezo. Bao la Pamba Jiji limefungwa dakika ya 23 na Deogratus Mafie wakati timu zilifungana bao 1-1 hadi mapumziko

Okello auzwa AS FAR Rabat

Picha
Klabu ya Young Africans imefikia maamuzi ya kumuuza kiungo mshambuliaji wake raia wa Uganda, Allan Okello, kwenda klabu ya AS FAR Rabat ya nchini Morocco. ​Maamuzi hayo yanakuja mara baada ya Wananchi kufanikiwa kukamilisha dili la kurejea kwa Stéphane Aziz Ki kikosini hapo, jambo lililowafanya viongozi wa Yanga kuwa tayari kuachia saini ya Okello. ​Kwa Taarifa AS FAR wamefanikiwa kumpata mchezaji huyo baada ya kuweka mezani dau kubwa zaidi lililowapiku wapinzani wao wa ligi kuu ya Morocco, Wydad Casablanca, waliokuwa wakiwania pia saini ya Okello.

Beki aliyetambulishwa Yanga kutemwa

Picha
Yanga wana mpango wa kumkata beki wao wa kati Oumar Farouk Comara,ili kupata nafasi ya kumuingiza kwenye mfumo namba 10 wao mpya ajaye. Comara alisaini mkataba wa miaka miwili wenye kipengele cha kutazamwa ndani ya miezi sita ila hadi sasa bado hajawashawishi. Awali Yanga walitaka kumuuza Okello ili wapate nafasi ya namba 10 wao mpya ila hadi sasa hakuna timu iliyofika bei $1.5m hivyo Comara yuko kwenye hatari ya kukatwa.

Kigwangala aliamsha tena Simba

Picha
Aliyekuwa Waziri na Mwanachama wa Simba SC, Dr. Hamisi Kigwangalla, ameibua mtafaruku mpya Msimbazi baada ya kuweka wazi nia yake ya kuvunja kile alichokiita "utawala wa mtu mmoja". Huku akitangaza kuwa yuko tayari kuweka fedha taslimu (cash) mezani kununua hisa za mwekezaji mkuu wa sasa, Mohammed 'Mo' Dewji. Kigwangalla ameyasema hayo huku akijibu shinikizo la baadhi ya wanasimba wanaomtaka agombee nafasi ya Uwenyekiti wa Simba SC kwenye uchaguzi ujao. Sina Hamu na Siasa za Mpira, Tatizo ni Mfumo" Akieleza sababu za kukataa kuingia kwenye kinyang'anyiro cha Uwenyekiti kwa sasa, Dr. Kigwangalla amebainisha kuwa tatizo la Simba silo uongozi wa mtu mmoja, bali ni muundo mbovu wa uendeshaji (governance) na umiliki wa klabu (ownership). "Kwanza, sijioni nikijikita kwenye siasa za mpira wa miguu wa klabu kubwa kama Simba. Pili, naamini tatizo la Simba si mtu mmoja. Tatizo kubwa ni mfumo wa uongozi na umiliki," alisema Kigwangalla. Mpango wa Kuondoa '...

Allan Okello ahitajika FAR Rabat

Picha
Jioni hii Klabu ya FAR Rabat ya Morocco imetuka ofa ya pili yenye thamani ya $1,000,000 (tsh 2.6b) kwenda Yanga ili kumpata Allan Okello. Hii ni ofa ya pili kutoka Rabat baada ya jana Yanga kukataa ofa ya $700,000. Yanga wanataka $1.5m (tsh 3.9b) ili kumuachia Okello.