Machapisho

Rayon Sports mabingwa kombe la Kagame Cup

Picha
Timu ya Rayon Sports ya Rwanda imefanikiwa kulibakiza kombe nyumbani baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo mkali uliochezwa dakika 120. Dakika 90 za kawaida timu hizo zilitoka sare ya 1-1 na kupelekea kuongezwa muda wa ziada, Rayon walianza kupata bao dakika ya 28 kupitia kwa Herman Kameni kabla ya Gor Mahia kusawazisha kupitia kwa Sharrif Mussa dakika ya 53. Muhoza Daniel aliiandikia bao la pili Rayon katika dakika ya 97, sasa ni rasmi Rayon inaivua ubingwa Singida Black Stars ya Tanzania iliyotolewa mwanzoni mwa mashindano hayo.

Chuga wa Yanga kukosa mechi 8

Picha
Mchezaji mpya wa Young Africans SC, anayefahamika kwa jina la Chuga Boy, ameripotiwa kupata jeraha la mguu katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Magereza, hali inayoweza kumfanya aanze msimu mpya akiwa nje ya uwanja. Taarifa hiyo imetolewa na mchambuzi wa michezo Ansibert Mwombeki, ambaye amesema vyanzo vyake vimemweleza kuwa Chuga Boy kwa sasa yupo hospitalini akiendelea kupata matibabu. Kwa mujibu wa taarifa hizo, jeraha hilo linaweza kumfanya nyota huyo akose kati ya mechi 5 hadi 8 za mwanzo za msimu, jambo ambalo linaweza kuwa pigo kwa Yanga katika maandalizi ya msimu mpya. Hata hivyo, kwa kuwa taarifa hii imetolewa kama taarifa ya awali, hali halisi ya jeraha na muda rasmi wa kurejea uwanjani utategemea vipimo na tathmini ya madaktari wa klabu.

Ally Kamwe akanusha Yanga kufungiwa na FIFA kusajili

Picha
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Young Africans SC, Ally Kamwe, amekanusha madai yanayoelezwa kuwa klabu hiyo imefungiwa kufanya usajili kwa kipindi cha misimu mitatu mfululizo. Kamwe amesema Yanga SC bado inaendelea na shughuli zake za usajili, huku akisisitiza kuwa taarifa za usajili wa klabu hiyo zimewasilishwa na zinaonekana kwenye mfumo husika.Kauli hiyo imekuja wakati ambapo taarifa kuhusu hali ya usajili wa Yanga zimeendelea kusambaa na kuzua mjadala miongoni mwa mashabiki na wadau wa soka nchini. Hata hivyo, Kamwe amesema kwa maelezo zaidi kuhusu suala hilo, wadau wanapaswa kuwasiliana na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), akieleza kuwa TFF ndiyo yenye taarifa na majibu rasmi kuhusu hali ya usajili wa klabu hiyo.

Yanga yampa cheti cha shukrani Waziri Mkuu JMT

Picha
Rais wa Klabu ya YANGA, Eng. Hersi Said mchana leo amemkabidhi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, Cheti cha Shukrani kwa kutambua mchango wake mkubwa alioutoa wakati akihudumu nafasi ya Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Klabu yetu. Aidha, Eng. Hersi alimpongeza na kumtakia kila la kheri, Mhe. Mwigulu katika majukumu yake mapya ya kulitumikia Taifa. Sambamba na hilo, Rais wa Yanga alimkabidhi Mhe. Mwigulu jezi rasmi za Msimu mpya wa 2026/27 na kutumia fursa hiyo kumkaribisha rasmi kwenye YANGA DAY itakayofanyika siku ya Jumapili, uwanja wa Uhuru, Jijini Dar Es Salaam.

Mfungaji bora NBC Primier huyoo Algeria

Picha
KAMA ilivyoripotiwa na Mwanaspoti siku chache zilizopita, mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Mossi Nduwumwe, amekamilisha rasmi uhamisho wake kutoka Singida Black Stars kwenda kwa mabingwa wa Algeria, MC Alger. Awali, Mwanaspoti ilifichua kuwa Mossi alikuwa katika hatua za mwisho za kujiunga na MC Alger baada ya mazungumzo kati ya klabu hizo kufikia pazuri huku zikisalia taratibu chache za kukamilisha dili hilo. Sasa taarifa hizo zimethibitishwa rasmi baada ya MC Alger kumtambulisha nyota huyo kupitia kurasa zake rasmi za mitandao ya kijamii. Klabu hiyo ilimkaribisha mshambuliaji huyo kwa ujumbe wa "Welcome to Mouloudia", ikithibitisha kumalizika kwa moja ya usajili uliokuwa ukifuatiliwa kwa karibu baada ya kiwango bora alichoonyesha akiwa Singida Black Stars msimu uliopita.

Gor Mahia yalalamikia kupangwa na Pyramids

Picha
Droo ya CAF Champions League 2026/27 imezua mjadala mkubwa nchini Kenya baada ya Gor Mahia kupewa Pyramids FC ya Misri kama mpinzani wao katika raundi ya kwanza ya hatua ya awali.Mashabiki na baadhi ya wanahabari wa michezo nchini humo wameeleza kutoridhishwa na droo hiyo, wakidai kuwa kipimo walichopewa Gor Mahia ni kikubwa mno kwa hatua ya kwanza ya mashindano. Kwa mtazamo wao, kuipanga Gor Mahia na mabingwa wa Afrika wa mwaka 2025 katika raundi ya kwanza ni changamoto kubwa sana, hasa kwa klabu inayolenga kusonga mbele hadi hatua ya makundi.Baadhi ya sauti kutoka Kenya zimeenda mbali zaidi kwa kuuliza iwapo CAF kweli inataka Gor Mahia isonge mbele katika mashindano hayo. Hoja yao kubwa ni kwamba:"Kama CAF haikuwa na nia ya kutaka Gor Mahia ifuzu hatua inayofuata, ingesema mapema tu!"Hata hivyo, licha ya malalamiko hayo, droo tayari imepangwa na Gor Mahia sasa inakabiliwa na kazi kubwa dhidi ya Pyramids FC. Ni vita ya Gor Mahia dhidi ya bingwa wa Afrika na K’Ogalo sasa inah...

Youssouf Ibrahim straika la mabao Gaborone United, ajiweka sokoni

Picha
Youssouf Ibrahim (32) mshambualiaji wa zamani wa Gabrone United ya Botswana mwenye uwezo wa kucheza winga zote mbili na mshambualiaji wa kati na bado akatoa ufanisi kwenye kutengeneza nafasi na kuzitumia msimu uliopita akifunga mabao 11 na Assit 3 hivyo kuwa na mchango wa 14GA kwa sasa ni free agent baada ya kumaliza mkataba wake na Gabrone United , Youssouf ana quality na experince ya kutosha matuzi mazuri ya kichwa na shoot power ya viwango pia ni kiongozi uwanjani Youssouf ni national team player anakidhi vigezo vya TFF kutaka foreign player awe anacheza timu ya taifa ya taifa analotoka au timu za vijana sababu ana magoli 10 akiwa na jezi ya Comoro National team.