TP Mazembe hiyoo raundi ya kwanza
Klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imefuzu hatua ya pili ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) baada ya kuiondosha Medeama SC ya Ghana kwa matokeo ya jumla ya 4-1 kwenye hatua ya awali. TP Mazembe imechomoza na ushindi wa 3-1 kwenye mchezo wa marudiano uliopigwa Lubumbashi baada ya kuibuka na ushindi wa 1-0 kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa huko Ghana wiki iliyopita. FT: TP Mazembe π¨π© 3-1 π¬π Medeama SC ⚽ 03' Mwaungulu ⚽ 19' Kazema ⚽ 88' Mwaungulu ⚽ 90+2' Amponsah TIMU ZINGINE ZILIZOFUZU HATUA YA PILI: πΏπ¦ Orlando Pirates πΈπ© Al Merreikh SC πΈπ© Al Hilal Omdurman πΈπΈ Al Merreikh Bentiu FC πΏπΌ Scottland FC π²π¬ CFFA FC π²π¦ Maghreb Fez FC π¦π΄ Petro de Luanda π³π¦ African Stars