Machapisho

Anaandika Nasri Khalfan mchambuzi wa Wasafi FM

Picha
Magoli mawili katika michezo mi3 ya mwanzo wa Ligi sio mbaya... yeye na Jonathan Sowah ndio Washambuliaji wakati wenye takwimu nzuri katika hii michezo mi3 ya mwanzo. Mazingira mapya na amezungukwa na Wachezaji wapya. Lazima ilihitajika time kuonekana muunganiko wa moja kwa moja kati yake na viungo wake. Akiongezeka na Aziz Ki bila ya shaka huduma itakua ya uhakika zaidi kwake.

Anaandika Nasri Khalfan mchambuzi wa Wasafi FM

Picha
Magoli mawili katika michezo mi3 ya mwanzo wa Ligi sio mbaya... yeye na Jonathan Sowah ndio Washambuliaji wakati wenye takwimu nzuri katika hii michezo mi3 ya mwanzo. Mazingira mapya na amezungukwa na Wachezaji wapya. Lazima ilihitajika time kuonekana muunganiko wa moja kwa moja kati yake na viungo wake. Akiongezeka na Aziz Ki bila ya shaka huduma itakua ya uhakika zaidi kwake.

Bodi ya Ligi yapiga mkwara matumizi ya FVS

Picha
Kamati ya Bodi ya Ligi imezikumbusha timu zote kuzingatia kikamilifu Kanuni ya 20 inayohusu matumizi ya Teknolojia ya Football Video Support System (FVS). Kwa mujibu wa Kanuni ya 20(4), Kocha Mkuu au kiongozi mwingine wa juu kwenye benchi la ufundi ndiye mwenye mamlaka ya kuwasilisha ombi la marejeo ya tukio kupitia Mwamuzi wa Akiba. Mchezaji akiona tukio linahitaji marejeo ya FVS, anatakiwa kumjulisha Kocha Mkuu au kiongozi wa benchi kwa ishara, ili kiongozi huyo awasilishe ombi hilo.Bodi ya Ligi imeonya kuwa mchezaji haruhusiwi kumlalamikia au kumshinikiza mwamuzi moja kwa moja ili kuomba marejeo ya FVS.Mchezaji atakayekiuka utaratibu huo ataadhibiwa kwa mujibu wa Kanuni ya 17:62.

Yanga yatamba kwa mabao, Shasha Man atupia

Picha
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu bara Yanga SC usiku huu imepata ushindi mnono wa mabao 4-0 katika uwanja wake wa KMC Complex. Mchezo wa leo umekuwa na clean sheets kwa kipa wa Yanga Djigui Diarra baada ya kuruhusu mabao kwenye mechi mbili mfululizo, mabao ya Yanga yamefungwa na Albert Kangwanda dakika ya 28, Ibrahim Bacca dakika ya 34 na Chadrack Boka dakika ya 38. Bao lingine la mabingwa hao wa bara limefungwa na Peter Shalulile 'Shasha Man" dakika ya 68, kwa matokeo hayo Yanga inarudi kileleni ikiwa na pointi 9 sawa na Simba ila Ina wastani mzuri wa kufunga.

Clara Luvanga atupia tena huko...

Picha
Mshambuliaji wa Timu ya Taifa Tanzania "Twiga Stars" Clara Luvanga amefunga Magoli Saba pekee yake kwenye ushindi wa Magoli 12 ya timu yake ya Al Nassr Women Nyota huyo ameendelea kuonesha ubora mkubwa wa Ufungaji wa Magoli akiwa na timu ya Al Nassr Women baada ya kuwafunga magoli Saba timu ya CSKA Dushanbe kwenye mchezo wa Uefa Asian Women

TFF yataka Yanga iilipe Simba kisa usajili wa Sele

Picha
Selemani Mwalimu ukiingia kwenye mfumo wa Usajili wa FIFA Connect anasoma kuwa ni mchezaji wa Yanga SC na si kweli Simba SC haijamuachia kwenye mfumo japo iliweka pingamizi TFF Kutaka ilipwe gharama ilizotumia wakati wanapambana kumsajili tena kwa mkopo. Kwa mujibu wa taarifa nilizonazo ni kuwa pingamizi la Simba Sports Club ilikuwa ni kutaka kuzuia Usajili wa Sele Gomez wakitaka kulipwa kwanza pesa zao walizotumia wakati wanapambana kumsajili. Issue ilikuwa siku ya mwisho wa Usajili Simba SC walikuwa wanakataa ombi la kumuachia Selemani Mwalimu ila Yanga SC baada ya kuonesha ushahidi na makubaliano kati ya Yanga SC na Wydad Casablanca kimkataba ndipo TFF wakaruhusu usajili wa Selemani Mwalimu kwenye mfumo wa usajili wa FIFA Connect. Kesi ipo kati ya Simba SC na Selemani Mwalimu, Kwa mujibu wa taarifa nilizonazo Selemani Mwalimu hakuwa amelipwa fedha za usajili na Simba SC na fedha ambazo zinaweza kuwa anadaiwa ni tiketi ya ndege ya kutoka Morocco Kuja Tanzania. Selemani Mwalimu ni mch...

Simba SC chapa bora Tanzania

Picha
Klabu ya Simba SC imeendelea kudhihirisha ukubwa na uthabiti wa chapa yake baada ya kutunikiwa rasmi cheti cha Superbrand kama taasisi namba moja inayojihusisha na michezo nchini Tanzania kwa mwaka wa pili mfululizo. ​Tuzo hii inadhihirisha ukuaji mkubwa wa thamani ya chapa (brand) ya Msimbazi, ubora wa utendaji wa kitaasisi, pamoja na ushawishi wake mkubwa katika sekta ya michezo nchini na barani Afrika.