Machapisho

TRA United na Mexime kimeeleweka

Picha
TRA United imefanya mabadiliko kwenye benchi la ufundi baada ya kuachana na Kocha Mkuu Etienne Ndayiragije, huku Mecky Maxime akitarajiwa kuchukua nafasi hiyo. Ndayiragije ameondoka katika klabu hiyo baada ya uongozi wa TRA United kutangaza kusitisha ushirikiano wake na kocha huyo. Kwa mujibu wa taarifa zilizopo, Maxime tayari yupo njiani kujiunga na kikosi cha TRA United, ambako anatarajiwa kuanza majukumu yake mapya baada ya kukamilika kwa taratibu za mwisho. Maxime anarejea kwenye benchi la ufundi baada ya kuwa nje ya kazi ya ukocha kwa kipindi fulani, huku akitarajiwa kuiongoza TRA United katika hatua inayofuata ya msimu. Mabadiliko hayo yanakuja wakati TRA United ikihitaji kurekebisha mwenendo wake na kuongeza ushindani katika mashindano ya msimu huu.

Mzize, Job safi Yanga

Picha
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe, amesema nyota wa timu hiyo Clement Francis Mzize na Dickson Job wako katika hali nzuri na hivi karibuni wataanza tena mazoezi na timu. Wachezaji hao walifanyiwa check-up nchini Afrika Kusini na baada ya kuruhusiwa, sasa wanatarajiwa kurejea kwenye mazoezi rasmi. Kurejea kwa Mzize na Job ni nyongeza kubwa kwa Yanga, kwani timu hiyo inapata nguvu mpya kwenye safu ya ushambuliaji kupitia Mzize na kwenye ulinzi kupitia Job. Kwa mashabiki wa Yanga, kurejea kwa nyota hao wawili ni kama usajili mpya katikati ya msimu.

Makipa Afrika watemwa tuzo za Ballon d'Or

Picha
Baadhi ya majina makubwa ya makipa wa Afrika wameachwa nje ya orodha fupi ya Tuzo ya Yashin ya Ballon d’Or: Ronwen Williams πŸ‡²πŸ‡± Djigui Diarra πŸ‡¬πŸ‡­ Benjamin Asare πŸ‡ΏπŸ‡¦ Sipho Chaine πŸ‡ΏπŸ‡¦ Brandon Petersen πŸ‡³πŸ‡ͺ Djibrilla Kassali πŸ‡ͺπŸ‡¬ Mostafa Shobeir πŸ‡¨πŸ‡² AndrΓ© Onana πŸ‡³πŸ‡¬ Stanley Nwabali πŸ‡ΉπŸ‡Ώ Aishi Manula πŸ‡ΉπŸ‡³ Memmiche Amanallah

Mecky Mexime njiani kutua TRA

Picha
Kocha wa zamani wa Mbeya City, Mecky Mexime, yupo njiani kujiunga rasmi na klabu ya TRA United ili kuchukua mikoba ya kocha Etienne Ndayiragije. Kocha Mecky Mexime anaenda kuifundisha timu hiyo ya wakusanya mapato ya TRA United na kuchukua nafasi ya Kocha Etienne Ndayiragije. Hatua hii ya Mexime inakuja baada ya kuachana na klabu ya Mbeya City

Viongozi Yanga waenda kumfariji Pacome

Picha
Sehemu ya Idara ya Habari ya Yanga SC ikiongozwa na Meneja Habari na Mawasiliano wake Ally Kamwe, imemtembelea nyota wao Pacome Zouzoua nyumbani kwake na kumkabidhi mahitaji mbali mbali. Kwa mujibu wa Kamwe, nyota huyo huenda akawepo katika dimba la Azam Complex, Chamazi kuushuhudia mchezo wa mkondo wa pili wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) dhidi ya Gaborone United. Mechi itapigwa Jumamosi ya Septemba 12, 2026 saa 1:00 usiku.

Simba yamkaribisha Gamondi

Picha
Tumepata ugeni wa Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Miguel Gamondi akiongozana na maafisa wengine wa benchi la ufundi na Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini kwa lengo la kujenga ushirikiano kati ya klabu na TFF katika eneo linalohusisha timu za taifa.

Chama awapiga mkwara Yanga

Picha
Mchezaji wa Simba SC, Clatous Chama, amevunja ukimya na kutoa onyo kwa watu anaodai wameanza kuvuka mipaka kupitia mijadala inayoendelea kwenye mitandao ya kijamii. Chama amesema amekuwa kimya kwa muda wa kutosha, lakini sasa baadhi ya watu wameanza kwenda mbali zaidi, akisisitiza kuwa mitandao ya kijamii ina ukweli na pia kuna watu wanaozungumza kwa lengo la kutafuta umaarufu, ‘likes’ na maoni. Mchezaji huyo amesema kusimama na kusema ukweli hakupaswi kutafsiriwa vibaya au kutumiwa dhidi yake, akidai kuwa ana ukweli pamoja na ushahidi wa kile anachokizungumza. Ameongeza kuwa endapo ataona chapisho lingine likitolewa dhidi yake, yuko tayari kuweka hadharani mazungumzo yote aliyofanya na wahusika.