Machapisho

Mtoto wa kaka wa Diamond Platinum apewa jina la Aaliyah

Picha
Ricardo Momo ambaye ni kaka wa Diamond Platnumz amethibithisha kuwa mtoto wake aliyozaliwa amepewa jina la Aaliyaah. Riacardo Momo ameeleza kuwa jina hilo alikuwa nalo tangu kipindi cha nyuma kwasababu huwaga anaplan za majina kabla hajapata watoto. Aidha Ricardo Momo amesema kuwa haoni ubaya kwenye jina la Aaliyaah licha ya jina hilo kufanana na Aaliyaah wa Wasafi. ''Mimi huwaga na plan za majina kabla ya kupata watoto''Amesema -Ricardo

Feitoto' kurudi Yanga

Picha
Klabu ya Young Africans SC (Yanga SC) imeendelea kuibua mijadala mikubwa katika anga za soka la Tanzania baada ya kuhusishwa na mpango wa kumrejesha kiungo mshambuliaji wao wa zamani, Feisal Salum maarufu kama Feitoto, ambaye kwa sasa anakipiga katika klabu ya Azam FC. Hatua hii imeibua hisia tofauti miongoni mwa mashabiki wa Wananchi, kwani Feisal ni mchezaji mwenye historia kubwa na mchango wa kipekee katika mafanikio ya Yanga SC kabla ya kuondoka. Feisal anatambulika kama kiungo mwenye ubunifu, kasi na uwezo wa kutengeneza nafasi za mabao. Ni mchezaji ambaye mara nyingi huleta uwiano wa kiufundi na kuongeza chaguo la ushambuliaji kwa benchi la Yanga SC. Uwezo wake wa kupenya safu za ulinzi za wapinzani na kutoa pasi sahihi unamfanya kuwa mchezaji wa thamani kubwa kwa kikosi chochote. Hii ndiyo sababu mashabiki wengi wa Yanga SC wanatamani kumuona akirejea Jangwani ili kuimarisha safu ya kiungo na kuongeza nguvu katika mashindano ya ndani na kimataifa.

Girumugisha aikwepa Yanga na kutimkia Libya

Picha
Winga Jean Claude Girumugisha amewasili nchini Libya kwaajili ya kukamilisha mchakato wake wa usajili wa kujiunga na Al Ahli Tripoli akitokeaAl Hilal Omdurman kwa msimu mpya! Jean Claude Girumugisha hatajiunga na Young Africans SC kuelekea msimu ujao wa 2026-27 ambao waliulizia thamani ya winga huyo na hawakurudi tena mezani kupambania saini na huduma ya mchezaji huyo ambaye amekuwa na misimu bora sana

Bajaber na Simba kwishinei

Picha
Klabu ya Simba SC imefikia makubaliano rasmi ya kuvunja mkataba na kiungo mshambuliaji raia wa Kenya, Mohamed Bajaber (23). ​Uamuzi huo umekuja baada ya mchezaji huyo kuonekana kutokuwa kwenye mipango ya kocha mkuu wa Msimbazi, Steve Barker, jambo lililopelekea pande zote mbili kuridhia kutengana kwa amani. Bajaber tayari ameanza mchakato wa kutafuta changamoto mpya katika klabu nyingine.

Al Ahly yaangukia Shirikisho

Picha
Maamuzi ya Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) kukataa ombi la Shirikisho la Soka la Misri (EFA) la kuongeza idadi ya timu kwenye Ligi ya Mabingwa, yamekuja kufuatia klabu kongwe ya Al Ahly kumaliza katika nafasi inayowatupa nje ya kufuzu CAF Champions League kwa msimu wa 2026/27. ​Kulingana na msimamo wa Ligi Kuu ya Misri, Al Ahly imeshindwa kukamata nafasi mbili za juu zinazotoa tiketi ya Ligi ya Mabingwa, na badala yake itabidi washiriki Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CAF Confederation Cup). ​Jaribio la EFA kutaka kuokoa jahazi la miamba hiyo ya Cairo kwa kuomba nafasi zaidi kutoka CAF limegonga mwamba, ikimaanisha mabingwa hao mara nyingi zaidi wa Afrika watapaswa kupambana kwenye Kombe la Shirikisho msimu ujao.

Makamu wa Rais Yanga awatoa hofu kuhusu uwanja Jangwani

Picha
Makamu wa Rais wa klabu ya Young Africans (Yanga SC), Arafat Haji, amewatoa hofu mashabiki na wanachama wa klabu hiyo kuhusu mradi wa ujenzi wa uwanja wao wa kisasa eneo la Jangwani, kwa kueleza kuwa tayari wameshasaini mkataba rasmi na mwekezaji GSM tangu tarehe 12 na mchakato wa maandalizi unaendelea vizuri. Ametoa ufafanuzi kuwa sababu ya kutooana ujenzi wa moja kwa moja ukiendelea eneo la tukio ni kutokana na kuwepo kwa miradi mingine inayotegemeana kama mradi wa Mto Msimbazi na daraja jipya, huku vifaa vya uwanja huo vikiwa vinaandaliwa na kuunganishwa huko vinakotoka. Arafat aliongeza kuwa uwanja huo utatumia teknolojia ya kisasa na hautakuwa wa zege tupu, bali vifaa vingi vitaletwa kutoka nje ya nchi na kuunganishwa mahali hapo baada ya kukamilisha kujaza eneo hilo ili kufikia kiwango na urefu ulioshauriwa na wataalamu wa Bonde la Jangwani. Hatua hiyo inachukuliwa kwa umakini mkubwa ili kuepuka changamoto za mafuriko na athari za maji ya mvua, huku wakihakikisha ujenzi unafuata ...

Omari Omari rasmi Singida Black Stars

Picha
Singida Black Stars FC imekamilisha usajili wa kiungo Omary Omary kutoka Mashujaa FC ambayo anaitumikia kwa mkopo akitokea Simba SC. Omary Jr alikuwa na mkataba wa miaka mitatu na Simba SC na mpaka sasa Singida Black Stars ilishamalizana na Simba SC kwa uhamisho huo kwa kila kitu!