Machapisho

TP Mazembe hiyoo raundi ya kwanza

Picha
Klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imefuzu hatua ya pili ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) baada ya kuiondosha Medeama SC ya Ghana kwa matokeo ya jumla ya 4-1 kwenye hatua ya awali. TP Mazembe imechomoza na ushindi wa 3-1 kwenye mchezo wa marudiano uliopigwa Lubumbashi baada ya kuibuka na ushindi wa 1-0 kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa huko Ghana wiki iliyopita. FT: TP Mazembe πŸ‡¨πŸ‡© 3-1 πŸ‡¬πŸ‡­ Medeama SC ⚽ 03' Mwaungulu ⚽ 19' Kazema ⚽ 88' Mwaungulu ⚽ 90+2' Amponsah TIMU ZINGINE ZILIZOFUZU HATUA YA PILI: πŸ‡ΏπŸ‡¦ Orlando Pirates πŸ‡ΈπŸ‡© Al Merreikh SC πŸ‡ΈπŸ‡© Al Hilal Omdurman πŸ‡ΈπŸ‡Έ Al Merreikh Bentiu FC πŸ‡ΏπŸ‡Ό Scottland FC πŸ‡²πŸ‡¬ CFFA FC πŸ‡²πŸ‡¦ Maghreb Fez FC πŸ‡¦πŸ‡΄ Petro de Luanda πŸ‡³πŸ‡¦ African Stars

Yanga yatinga raundi ya kwanza Ligi ya mabingwa Afrika

Picha
Mchezo wa marudiano hatua ya swali Ligi ya Mabingwa barani Afrika (CAF Champions League) kati ya klabu ya Yanga dhidi ya Gaborone United umemalizi kunako dimba la Azam Complex jijini Dar Es Salaam huku Yanga wakifuzu kwenda hatua ya pili kwa mabao (2-1). Mabao ya Yanga wamefungwa na Peter Shalulile na Sheikh Ibrahim Toure wakati goli la Goborone United limefungwa na Lebongang. Hivi sasa uwiano wa mabao ya jumla "Aggregate" ni (3-2).

Singida BS kukutana na Tusker kombe la Shirikisho

Picha
Iwapo Singida Black Stars watafanikiwa kufuzu kesho dhidi ya Al Ghazala Wau, watakutana na Tusker FC katika raundi ya pili ya awali ya CAF Confederation Cup. Tusker FC tayari imefuzu rasmi hatua hiyo baada ya kuiondosha Al Ahli Madani kwa ushindi wa jumla ya mabao 3-2.

Clara Luvanga aandika historia soka la wanawake duniani

Picha
Mchezaji wa Kimataifa wa Tanzania, Clara Luvanga, ameandika historia ya kuwa Mchezaji aliye sajiliwa kwa pesa Nyingi zaidi katika Historia ya soka la Wanawake Duniani baada ya kukamilika kwa uhamisho wa kujiunga na Washington Spirit ya Marekani akitokea Al-Nassr, kwa kusaini mkataba wa miaka minne utakaodumu hadi mwaka 2029. πŽπ‘πŽπƒπ‡π€ π˜π€ π’π€π‰πˆπ‹πˆ (4) π†π‡π€π‹πˆ 𝐙𝐀 π–π€π‚π‡π„π™π€π‰πˆ 𝐖𝐀 πŠπˆπŠπ„ πƒπ”ππˆπ€ππˆ 1. Clara Luvanga kutoka: Al Nassr to Washington kwa ada ya €1.7m (tsh 5.2bilion). 2.Grace Geyoro kutoka PSG to London City €1.65m (tsh 5bilion). 3.Kerolin Nicoli kutoka Man City to Barcelona €1.5m (tsh 4.6 bilion). 4.Felicia SchrΓΆder HΓ€cken to Real Madrid €1.5m (tsh 4.6bilion). Kwa kifupi Mtanzania Luvanga ndo mchezaji ghali kuliko wote Duniani.

Opah Clement naye asajiliwa Saudi Arabia

Picha
Kapteni wa timu ya taifa ya Tanzania, Twiga Stars, Opah Clement, amejiunga na klabu ya AlUla FC Women inayoshiriki Ligi Kuu ya Wanawake Saudi Arabia. Opah amejiunga na AlUla akitokea SD Eibar ya Ligi Kuu nchini Hispania ambayo ameitumikia kwa msimu mmoja, huku klabu hiyo ya Alula ikiwa tayari imemtambulisha rasmi kama mchezaji wake mpya.

Harmonize aenda kumpa pole Samia Kizimkazi

Picha
Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya Rajab Abdul Kahali 'Harmonize' amefika kumpa pole na kumfariji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, leo Septemba 11, 2026, kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan. Maalim Hafidh amefariki dunia Septemba 7, 2026 katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar.

Eto'o atuhumiwa kulamba bilioni 1.7

Picha
Samuel Eto’o yuko kikaangoni baada ya kupewa tuhuma za matumizi ya pesa hovyo. kwa taarifa kutoka vyanzo vya habari, vinaeleza kuwa nyota wa Barcelona, ambaye pia ni Rais wa Shirikisho la Soka la Cameroon (FECAFOOT), Kuna kiasi cha pesa fulani hakionekani, na kiwango hicho si chini ya takribani dola 665,000 [TZS bilioni 1.7], zilizohusishwa na malipo ya mchezo wa kirafiki kati ya Cameroon na Urusi mwaka 2023. Kufuatia sakata hilo, Eto’o, ambaye amekuwa akiongoza FECAFOOT tangu mwaka 2021, wataanza zoezi la uchunguzi dhidi ya jambo hilo linalomkabili. Kwa upande wa mshitakiwa ambaye ni Eto’o, amesema kuwa upande wake uko wazi kwa uchunguzi zaidi ili kuona wapi amekosea. Pia, nyaraka zake zote zitaanza kuchunguzwa, na kuripotiwa kuonyesha kuwa fedha hizo ziliagizwa kutumwa kwenye akaunti yake binafsi katika benki nchini Qatar.