Bao 6 za Simba zaondoka na kigogo wa Mighty Wonderers-
Kipigo kizito walichokipata miamba ya Malawi, Mighty Wanderers, kwenye michuano ya CAF Champions League mikononi mwa Simba SC kimeleta mtafaruku mkubwa uliomfanya Rais na Mdhamini Mkuu wa klabu hiyo, Dr Thomson Mpinganjira, kutangaza kujiuzulu rasmi. Matokeo hayo mabaya uwanjani yameonekana kuwa chanzo kikuu cha maamuzi hayo ya ghafla, yakionyesha jinsi dozi ya Mnyama Simba ilivyoingia hadi kwenye korido za uongozi wa Wanderers. Kuondoka kwa Dr Mpinganjira, ambaye pia ndiye alikuwa mwekezaji na mdhamini mkuu, kunaiweka klabu hiyo ya Malawi kwenye utata mkubwa wa kifedha kuelekea michezo inayofuata.