Machapisho

DABI IMEHARIBU MATAMASHA

Picha
Na Prince Hoza Matua WIKI iliyopita ilikuwa siku muhimu kwa timu zote mbili hasimu kuweza kusherehekea matamasha yake na kutambulisha vikosi vyao, ilianza Simba SC tarehe 8, Agosti ambapo iliadhimisha Simba Day. Na kufuatiwa na Yanga SC tarehe 9 Agosti waliadhimisha Wiki ya Wananchi, kwa kifupi matamasha yote yalifana sana hasa kwenye matukio mengine mambo yalienda safi ila katika suala la mchezo kwa upande wa timu kubwa ya wanaume mambo hayakuwa mazuri. Kwa upande wa Simba timu yao tegemezi haikufanya vizuri ingawa ilitambulisha wachezaji wake wapya, Simba ilicheza na timu ya Police FC ya Kenya na ilikubali kichapo cha bao 1-0. Mashabiki wa timu hiyo hawakuwa na furaha baada ya kushindwa kuwaona nyota wake wapya wakionesha viwango vyao, ndivyo hivyo kwa Yanga nako walikutana na kipigo. Yanga ilicheza na Les Aigle De Congo ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC  ambapo mwisho wa mchezo ilichalazwa mabao 2-1, kipigo cha Yanga nacho kimewauma mashabiki wake ambapo hawakuona viwango vya...

Rais Samia azitakia kila kheri Simba na Yanga

Picha
Tumeshuhudia burudani katika Dabi nyingine ya Kariakoo kupitia mchezo wa Ngao ya Jamii. Pongezi kwa Klabu ya Yanga kwa ubingwa wa 10 wa Ngao ya Jamii. Ninazitakia kila la heri timu zote katika msimu mpya wa Ligi Kuu, pamoja na mashindano mengine ya kitaifa na kimataifa.

Yanga yatwaa tena Ngao ya Jamii

Picha
Yanga SC imeanza vema msimu mpya wa 2026/2027 baada ya kushinda Ngao ya Jamii kufuatia ushindi wa bao 1-0 dhidi ya mtani wake wa jadi Simba SC katika uwanja wa New Amaan Stadium Zanzibar. Bao pekee lilifungwa na Mzambia Albert Kingwanda aliyeunganisha krosi ya Mkongoman Chadrack Boka dakika ya 32 kipindi cha kwanza. Yanga sasa imekabidhiwa Ngao ya Jamii na kuashiria msimu mzuri kwao

Aziz Ki arejea rasmi Yanga SC

Picha
Young Africans SC imemsajili kiungo Stephane Aziz Ki kutoka Al Ittihad SC kuelekea msimu ujao. Young Africans SC wanamalizia vitu kadhaa kwenye papers na masharti ya Al Ittihad SC ili waweze kumtangaza rasmi. KI Aziz hataki kuitumikia tena na tayari alishawapa taarifa mapema sana Al Ittihad SC na klabu hiyo ya Libya ilikuwa tayari kumuachia na iliheshimu mahitaji ya mchezaji huyo.

Wababe wa Yanga wakiona chamoto kwa JKT Tanzania

Picha
Wababe wa Young Africans SC, Les Aigles Du Congo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wanapokea kichapo cha kizalendo huko Meja Janerali Isamuhyo dhidi ya Maafande wa JKT Tanzania. Ni katika mchezo wa kirafiki ikiwa ni muendelezo wa maandalizi kuelekea msimu mpya wa NBC Primier League 2026/2027. Mabao ya JKT Tanzania yamefungwa na Said Mkopi na Paul Peter Kasunda.

Fei atoweka Simba SC

Picha
Kiungo Feisal Salum atawasili Arusha, Tanzania kwaajili ya kufanyiwa summalization ya jeraha lake dogo la nyama za paja akiwa na kikosi cha Azam FC na ataukosa mchezo wa kwanza wa Azam FC dhidi ya Polisi Tanzania. Feisal Salum hatojiunga na Simba SC katika dirisha hili na ataendelea kuitumikia Azam FC kwa mkataba wa mwaka mmoja uliobaki hadi June 30, 2027 ambapo atakuwa mchezaji huru (Free agent).

AS Vita yanasa kinda Singida Black Stars

Picha
Klabu ya AS Vita Club ya DR Congo imekamilisha usajili wa kinda hatari Candidat Mapendo (20) kutoka Singida Black Stars kwa mkopo wa msimu mmoja. Mapendo amepelekwa kwa mkopo baada ya kukosa nafasi kwenye mipango ya kocha wa Singida Black Stars, Papy Kimoto. Kuna madai kwamba sababu ya kutokubalika kwake inahusishwa na ukabila, ingawa madai hayo hayajathibitishwa rasmi. Msimu uliopita, Mapendo alifunga mabao 21 na kuibuka mfungaji bora wa Ligi Kuu ya DR Congo, jambo lililoifanya Singida Black Stars kutumia kiasi kikubwa cha fedha kumsajili. Kesho Alhamisi, Mapendo anatarajiwa kuanza safari kutoka Kinshasa kuelekea Burundi, kisha ataelekea Baraka, ambako atapata nafasi ya kuiaga familia yake kabla ya kurejea kazini.