Machapisho

Sele Gomez aja na muonekano mpya

Picha
Straika mpya wa Yanga SC, Selemani Mwalimu ‘Gomez’, akiwa mazoezini na mwonekano mpya. Kwa mujibu wa taarifa ya Yanga, kesho mshambuliaji huyu atakuwa uwanjani wakati Yanga wakikipiga dhidi ya Pamba Jiji FC. “Chuma kipo tayari kwa ajili ya kuwapa furaha Wananchi Kesho,” taarifa ya Yanga SC.

Simba yapata ushindi kiduchu

Picha
Timu ya Simba SC usiku huu imepata ushindi kiduchu baada ya kuifunga Coastal Union ya Tanga bao 1-0 katika uwanja wa Meja Isamuhyo Mbweni jijini Dar es Salaam. Mchezo huo wa Ligi Kuu bara ulikuwa wa upande mmoja kwa Simba kufanya mara kwa mara, bao pekee la Simba limefungwa na Ismail Toure baada ya kutokea nyuma.

Bodi ya Ligi Tanzania na Mali waenda kujifunza Yanga

Picha
Uongozi wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania ukiambatana na wageni wao kutoka Bodi ya Ligi ya Mali, umefika katika Klabu ya Yanga kwa ziara yenye lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu namna klabu inavyojiendesha. Katika ziara hiyo, wageni hao wamepata fursa ya kufahamu mifumo ya uendeshaji wa klabu, usimamizi wa shughuli za kila siku, maendeleo ya biashara na masoko, matumizi ya teknolojia, pamoja na namna Yanga inavyosimamia chapa yake na kuwahudumia mashabiki Wageni hao wamepokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Yanga SC, Andre Mtine

Wachambuzi na mashabiki acheni kumtoa kwenye reli Doumbia

Picha
Na Prince Hoza Matua  NI usajili muhimu uliofanywa na klabu ya Simba SC kwa ajili ya msimu huu wa 2026/2027, kamati ya usajili ya Simba ilifanya tathimini ikishirikisha benchi la ufundi. Viongozi wa kamati ya usajili ilishirikisha makundi mengine wakiwemo viongozi wa juu wa klabu na wadhamini, miongoni mwa majina yaliyopendekezwa kusajiliwa ni mshambuliaji Ibrahim Doumbia raia wa Mali. Wasifu wake tosha kumsajili kwani katika ligi ya nchi hiyo aliibuka kuwa mfungaji bora alifanikiwa kufunga mabao 17, ligi ya Mali ndio iliyomtoa kipa nambari moja wa Yanga Djigui Diarra ambaye pia ni miongoni mwa makipa bora kwenye ligi yeti. Nashangaa hata ajacheza mzunguko wa kwanza tayari ameanza kuoneshewa kidole wakiashiria awamtaki, mihemko ya kishamba wanayafanya mashabiki wa Tanzania hasa wa Simba. Kelele zinazopigwa na mashabiki wa Simba zinasapotiwa na baadhi ya wachambuzi ambao kazi yao si kulalia sehemu moja, wachambuzi wa soka hasa wa Tanzania na wao wamegeuka mashabiki. Inanisikitisha sana ...

Huyu hapa Deogratus Ndejembi kutoka ukuu wa wilaya hadi makamu wa Rais

Picha
Deo Ndejembi ni miongoni mwa wanasiasa ambao wamepanda hatua kwa hatua katika uongozi wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Ndejembi alianza kujijenga kisiasa kupitia UVCCM, kabla ya kuingia kwenye nafasi za uongozi wa Serikali. Mwaka 2016, aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma na Rais DktJohn Magufuli, nafasi ambayo aliitumikia kwa miaka kadhaa kabla ya kuingia kwenye siasa za uchaguzi. Baadaye alichaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Chamwino, Dodoma, kupitia CCM mwaka 2020. Safari yake ya uongozi iliendelea baada ya kuteuliwa kuwa Naibu Waziri, akihudumu katika maeneo mbalimbali ya Serikali, kabla ya baadaye kupandishwa kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Kutoka hapo, Ndejembi aliendelea kupanda kisiasa hadi kufikia nafasi ya Waziri wa Nishati. Sasa, jina lake limeibuka tena katika hatua kubwa zaidi baada ya CCM kumpendekeza Deo Ndejembi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa hiyo, safari yake inaweza kufupishwa kwa namna hii:...

Bendera ya Marekani kupepea nusu mlingoni siku 7 kumlilia Dolly Parton

Picha
Rais Donald Trump ameagiza bendera ya Marekani kushushwa nusu mlingoti nchini humo kwa muda wa siku 7 kuanzia jana Jumanne jioni, kufuatia kifo cha nguli wa muziki wa country Dolly Parton kilichotokea mapema siku ya jana. "Hajawahi kutokea mtu kama yeye, na hatatokea tena," ameandika Trump. Mpwa wa Parton, Bryan Seaver, alitangaza kifo cha Dolly Parton kupitia video iliyorekodiwa mapema na kuchapishwa kwenye mitandao ya kijamii, amefariki akiwa na umri wa miaka 80, siku 4 baada ya kulazwa hospitali. Dolly alikuwa mmoja wa wanamuziki pendwa zaidi wa nyakati zote, akiwa na nyimbo kama “Jolene,” “9 to 5,” na “I Will Always Love You” zilizompa umaarufu zaidi enzi za uhai wake.

Simba Queens yatupwa nje CECAFA

Picha
Simba Queens imeondolewa katika mashindano ya CECAFA yanayoendelea Kigali, Rwanda, baada ya kushika nafasi ya pili Kundi C ikiwa na pointi tatu. Timu hiyo ilishinda mchezo mmoja na kupoteza mmoja, hivyo kushindwa kufuzu hatua ya nusu fainali. Kenya Police Bullets ya Kenya imeongoza kundi hilo kwa pointi sita baada ya kuichapa Top Girls Academy ya Burundi mabao 3-1 na kutinga nusu fainali. Kwa Simba Queens, matokeo hayo ni pigo katika harakati za kurejesha taji linaloshikiliwa na JKT Queens ya Tanzania. Timu hiyo imeendelea kukosa mafanikio makubwa katika miaka ya hivi karibuni. Baada ya kufika nusu fainali mwaka 2022, ilishiriki tena mwaka 2024 na kumaliza nafasi ya nne. Matokeo ya mwaka huu yanaongeza changamoto kwa Simba Queens katika kurejesha ubabe wake kwenye soka la wanawake Afrika Mashariki na ‎kati.