Machapisho

Elvis Rupia achafua hali ya hewa Simba Day

Picha
Klabu ya Simba usiku huu imepokea kichapo cha bao 1-9 toka kwa Police FC ya Kenya, mchezo wa kirafiki uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Goli pekee lilisubiri hadi dakika ya nyongeza 90+2 lililofungwa na nyota wa zamani wa Singida Black Stars, Elvis Rupia. Simba ilichezesha wachezaji wake wote wakiwemo wapya, mpira ulikuwa mzuri na timu zote zilionesha uwezo wake.

Rais Samia aipongeza Simba kuadhimisha Simba Day

Picha
Ninawapongeza Klabu ya Simba kwa tamasha lililofana la Simba Day 2026, lililoambatana na maadhimisho ya kutimiza miaka 90. Ninawatakia kila la kheri katika msimu ujao wa Ligi Kuu.

Okwi akumbushia goli 5-0 walizoifunga Yanga

Picha
Nyota wa zamani wa Simba SC, Mganda Emmanuel Okwi azikumbuka nyakati ambazo walipata ushindi wa magoli matano dhidi ya Yanga. Afunguka sababu za kutopiga penati siku hiyo ambayo ingemfanya aifikie rekodi ya mkongwe Abdallah Kibadeni ya kufunga hat trick.

Simba wamiminika Simba Day

Picha
Klabu ya Simba SC maarufu Wekundu wa Msimbazi leo hii eanaadhimisha siku ya Simba Day ambapo wapenzi na mashabiki wa timu hiyo wanajumuika pamoja kusherehekea. Pia mashabiki wa Simba wataadhimisha miaka 90 ya kuzaliwa klabu hiyo, baadaye saa mbili usiku wataingia uwanjani kucheza na timu ya Police FC ya Keny

Kocha mkuu Yanga amkataa Diarra

Picha
Kocha mpya wa Young Africans SC, Manqoba Mngqithi, ameripotiwa kuanza kazi ya kukifanyia tathmini kikosi cha Yanga kwa kuangalia wasifu na uwezo wa wachezaji aliowakuta klabuni hapo. Taarifa hizo zinaeleza kuwa licha ya Yanga kufanya maboresho makubwa kwenye usajili kuelekea msimu mpya, Mngqithi ameona bado kuna maeneo ambayo yanahitaji kuimarishwa ili kikosi kiweze kushindana kwa mafanikio katika mashindano ya ndani na kimataifa. Miongoni mwa masuala yanayodaiwa kuwa yameibua mjadala ni hali ya nidhamu ya baadhi ya wachezaji, huku Djigui Diarra akitajwa kutokana na madai ya makosa ya kinidhamu yanayodaiwa kujirudia.Kwa mujibu wa taarifa hizo, Mngqithi anaamini kuwa nidhamu ni msingi muhimu wa mafanikio katika soka, na anataka kujenga kikosi ambacho kinafuata falsafa yake ndani na nje ya uwanja. Aidha, kocha huyo anadaiwa kuweka msisitizo katika kuimarisha safu ya ulinzi pamoja na kiungo cha kati, akiamini maeneo hayo yana umuhimu mkubwa katika mfumo wake wa soka unaosisitiza kushambul...

Rayon Sports mabingwa kombe la Kagame Cup

Picha
Timu ya Rayon Sports ya Rwanda imefanikiwa kulibakiza kombe nyumbani baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo mkali uliochezwa dakika 120. Dakika 90 za kawaida timu hizo zilitoka sare ya 1-1 na kupelekea kuongezwa muda wa ziada, Rayon walianza kupata bao dakika ya 28 kupitia kwa Herman Kameni kabla ya Gor Mahia kusawazisha kupitia kwa Sharrif Mussa dakika ya 53. Muhoza Daniel aliiandikia bao la pili Rayon katika dakika ya 97, sasa ni rasmi Rayon inaivua ubingwa Singida Black Stars ya Tanzania iliyotolewa mwanzoni mwa mashindano hayo.

Chuga wa Yanga kukosa mechi 8

Picha
Mchezaji mpya wa Young Africans SC, anayefahamika kwa jina la Chuga Boy, ameripotiwa kupata jeraha la mguu katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Magereza, hali inayoweza kumfanya aanze msimu mpya akiwa nje ya uwanja. Taarifa hiyo imetolewa na mchambuzi wa michezo Ansibert Mwombeki, ambaye amesema vyanzo vyake vimemweleza kuwa Chuga Boy kwa sasa yupo hospitalini akiendelea kupata matibabu. Kwa mujibu wa taarifa hizo, jeraha hilo linaweza kumfanya nyota huyo akose kati ya mechi 5 hadi 8 za mwanzo za msimu, jambo ambalo linaweza kuwa pigo kwa Yanga katika maandalizi ya msimu mpya. Hata hivyo, kwa kuwa taarifa hii imetolewa kama taarifa ya awali, hali halisi ya jeraha na muda rasmi wa kurejea uwanjani utategemea vipimo na tathmini ya madaktari wa klabu.