DABI IMEHARIBU MATAMASHA
Na Prince Hoza Matua WIKI iliyopita ilikuwa siku muhimu kwa timu zote mbili hasimu kuweza kusherehekea matamasha yake na kutambulisha vikosi vyao, ilianza Simba SC tarehe 8, Agosti ambapo iliadhimisha Simba Day. Na kufuatiwa na Yanga SC tarehe 9 Agosti waliadhimisha Wiki ya Wananchi, kwa kifupi matamasha yote yalifana sana hasa kwenye matukio mengine mambo yalienda safi ila katika suala la mchezo kwa upande wa timu kubwa ya wanaume mambo hayakuwa mazuri. Kwa upande wa Simba timu yao tegemezi haikufanya vizuri ingawa ilitambulisha wachezaji wake wapya, Simba ilicheza na timu ya Police FC ya Kenya na ilikubali kichapo cha bao 1-0. Mashabiki wa timu hiyo hawakuwa na furaha baada ya kushindwa kuwaona nyota wake wapya wakionesha viwango vyao, ndivyo hivyo kwa Yanga nako walikutana na kipigo. Yanga ilicheza na Les Aigle De Congo ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC ambapo mwisho wa mchezo ilichalazwa mabao 2-1, kipigo cha Yanga nacho kimewauma mashabiki wake ambapo hawakuona viwango vya...