Machapisho

Ben Lee atua Tanzania

Picha
Tanzania imepiga hatua nyingine katika juhudi za kuendeleza mchezo wa uogeleaji kufuatia kuwasili kwa kocha wa kimataifa, Ben Lee, ambaye atatoa mafunzo ya kiwango cha kimataifa kwa waogeleaji, makocha na wazazi. Mafunzo hayo yatafanyika kupitia programu maalumu iliyoandaliwa na Monti International School. Ujio wa Ben Lee unaelezwa kuwa ni hatua muhimu katika safari ya kuinua viwango vya uogeleaji nchini kwa kuwaletea Watanzania utaalamu wa kimataifa bila kulazimika kusafiri nje ya nchi. Kocha huyo ana uzoefu mkubwa wa kuwafundisha waogeleaji walioshiriki mashindano ya NCAA na Olimpiki. Akizungumza na waandishi wa habari katika mapokezi ya kocha huyo jijini Dar es Salaam, Afisa Michezo wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Petro Gallos mbali na kupongeza ujio wake, amesema wakufunzi wa ndani wa mchezo huo wanapaswa kutumia mwanya huo adhimu kwa kuchota ujuzi wenye manufaa.

Neo Maema arejea Mamelodi

Picha
Kiungo mshambuliaji mwenye uraia wa Afrika Kusini, Neo Maema ambaye mkataba wake na Simba umemalizika rasmi, hatimaye amerejea Mamelodi Sundowns. Taarifa zenye uhakika ambazo Mambo Uwanjani Blog imeyhibitisha kwamba mchezaji huyo amerejea timu yake ya nyumbani. Kipengere cha mkataba wake na Mamelodi dhidi ya Simba kimemfanya arejee tena, Maema amekuwa na kiwango kizuri msimu uliopita na kupelekea Mamelodi kumuhitahi tena.

Simba yanogewa na sare

Picha
Timu ya Simba ya Tanzania imeendelea kulazimishwa sare 0-0 tasa katika michuano ya kombe la Kagame Cup nchini Rwanda dhidi ya Jamus ya Sudan Kusini na kufanya nafasi yake ya kusonga kuwa ngumu. Sasa italazimika kushinda dhidi ya Singida Black Stars watakaocheza mchezo wa mwisho ama sivyo itatolewa, jioni hii Singida Black Stars imeichapa Mogadishu City Club mabao 4-1 na kuweka hai nafasi yake ya kutetea kombe hilo. Simba sasa ina pointi mbili baada ya sare mbili wakati Singida Black Stars wana pointi tatu na wanashika nafasi ya pili wakati Jamus vinara wa kundi.

Sio kweli Injinia Hersi kamsajili Shalulile ashinde uchaguzi

Picha
Kwamba Eng Hersi Said @caamil_88 alihitaji kumsajili Peter Shalulile ili ashinde uchaguzi? Sio kweli... Hakuna mwana Yanga ambaye ana mashaka na Hersi na GSM, wamebeba ubingwa mara 5, wamemfunga Simba mara nyingi kwenye kipindi chao, wamefika fainali ya CAFCC. N arudia, Hersi hana wasiwasi wa kushinda uchaguzi wa Yanga na hahitaji nguvu kubwa kurejea madarakani. Turudi kwa Shasha Man (Peter Shalulile) Nimesikia kwamba Simba walimtaka Shalulile lakini wakajiondoa baada ya kushauriwa na Steve Barker kwa hoja hizi 3:- 1) Umri wa mchezaji 2) Kiwango cha mchezaji 3) Fedha anayotaka Kwamba Kocha Steve Barker alishauri kuwa umri wa miaka 32 na kiwango chake cha hivi karibuni (current form) haviendani na fedha anayoitaka mchezaji na wakala wake (Usd 750k kwa mwaka) Kwamba Shalulile msimu uliopita kafunga mabao matatu katika mechi 13 (moja la penati) hivyo uwezo wake umepungua... Kwa mtazamo wangu, Nafikiri tunaposema kuhusu umri wa Peter tusisahau kwamba Meddie Kagere akiwa na miaka 32 alifung...

Ally Kamwe aanika viingilio Wiki ya Wananchi

Picha
Klabu ya Yanga SC imetangaza rasmi viingilio vya Wiki ya Wananchi Agosti 9 mwaka huu katika uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Akizungumza na vyombo vya habari, Afisa Habari wa klabu hiyo Ally Kamwe amesema kuwa ili kushuhudia uzinduzi wa kikosi chao nyota wapya na burudani ya kipekee itaoneshwa kwa shilingi 300, 000. Jezi mpya ya msimu iliyosainiwa na mchezaji unayemchagua. usafiri wa kwenda na kurudi uwanjani kutoka Serena Hotel. chakula wakati wa mapumziko uwanjani 𝐕𝐈𝐏 𝐓𝐢𝐜𝐤𝐞𝐭 – 𝐓𝐒𝐡 𝟏𝟎𝟎,𝟎𝟎𝟎 M𝐳𝐮𝐧𝐠𝐮𝐤𝐨 – 𝐓𝐒𝐡 𝟐𝟎,𝟎𝟎𝟎 Nafasi ni chache sana Uwanja wa Uhuru, wahi mapema kukata tiketi yako.

Rais Samia aipongeza Twiga Stars

Picha
Ninaipongeza Timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania (Twiga Stars), kwa kuanza vyema michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) 2026 nchini Morocco kwa ushindi dhidi ya Timu ya Taifa ya Wanawake ya Afrika Kusini, (Banyana Banyana). Ninaungana na Watanzania wote kuitakia kila la kheri Twiga Stars inapoendelea kupeperusha bendera ya Taifa letu katika michezo inayofuata. Endeleeni kupambana kwa moyo huo huo, mkionesha uzalendo, nidhamu na ari ya ushindani inayolitangaza vyema Taifa letu.

Peter Shalulile asajiliwa na Yanga

Picha
Klabu ya Young Africans imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Namibia, Peter Shalulile, aliyekuwa akiitumikia Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini. Shalulile anatarajiwa kujiunga na kikosi cha Yanga kama sehemu ya maboresho makubwa ya kuelekea msimu mpya, huku akitajwa kuziba pengo lililoachwa na mshambuliaji Prince Dube, ambaye ameondoka ndani ya klabu hiyo.