Bendera ya Marekani kupepea nusu mlingoni siku 7 kumlilia Dolly Parton
Rais Donald Trump ameagiza bendera ya Marekani kushushwa nusu mlingoti nchini humo kwa muda wa siku 7 kuanzia jana Jumanne jioni, kufuatia kifo cha nguli wa muziki wa country Dolly Parton kilichotokea mapema siku ya jana. "Hajawahi kutokea mtu kama yeye, na hatatokea tena," ameandika Trump. Mpwa wa Parton, Bryan Seaver, alitangaza kifo cha Dolly Parton kupitia video iliyorekodiwa mapema na kuchapishwa kwenye mitandao ya kijamii, amefariki akiwa na umri wa miaka 80, siku 4 baada ya kulazwa hospitali. Dolly alikuwa mmoja wa wanamuziki pendwa zaidi wa nyakati zote, akiwa na nyimbo kama “Jolene,” “9 to 5,” na “I Will Always Love You” zilizompa umaarufu zaidi enzi za uhai wake.