Makamu wa Rais wa klabu ya Young Africans (Yanga SC), Arafat Haji, amewatoa hofu mashabiki na wanachama wa klabu hiyo kuhusu mradi wa ujenzi wa uwanja wao wa kisasa eneo la Jangwani, kwa kueleza kuwa tayari wameshasaini mkataba rasmi na mwekezaji GSM tangu tarehe 12 na mchakato wa maandalizi unaendelea vizuri. Ametoa ufafanuzi kuwa sababu ya kutooana ujenzi wa moja kwa moja ukiendelea eneo la tukio ni kutokana na kuwepo kwa miradi mingine inayotegemeana kama mradi wa Mto Msimbazi na daraja jipya, huku vifaa vya uwanja huo vikiwa vinaandaliwa na kuunganishwa huko vinakotoka. Arafat aliongeza kuwa uwanja huo utatumia teknolojia ya kisasa na hautakuwa wa zege tupu, bali vifaa vingi vitaletwa kutoka nje ya nchi na kuunganishwa mahali hapo baada ya kukamilisha kujaza eneo hilo ili kufikia kiwango na urefu ulioshauriwa na wataalamu wa Bonde la Jangwani. Hatua hiyo inachukuliwa kwa umakini mkubwa ili kuepuka changamoto za mafuriko na athari za maji ya mvua, huku wakihakikisha ujenzi unafuata ...