Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Kiungo Ghana, ahukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kufanya ngono bila ridhaa

Machapisho ya hivi karibuni

Saed Ramovic afikisha mechi 50 CR Belouizdad, amshukuru Rais wa klabu hiyo

Kocha mkuu wa CR Belouizdad amefikisha mechi 50 tangu aanze kuifundisha klabu hiyo, akieleza fahari yake kuwa sehemu ya moja ya vilabu vikubwa barani Afrika. Katika maelezo yake, kocha huyo amesema kuwa ni heshima kubwa kufanya kazi katika klabu hiyo yenye historia kubwa na kuvaa rangi zake kila siku. Ameeleza pia shukrani zake kwa Rais wa klabu kwa kumuamini, pamoja na kujivunia wachezaji, benchi la ufundi na mashabiki wanaopigania nembo ya klabu hiyo kila siku. Kocha huyo alisisitiza kuwa mafanikio yote wanayoyapata yanawahusu zaidi mashabiki wa klabu hiyo, ambao wamekuwa wakiendelea kutoa sapoti kubwa kwa timu yao. Ameongeza kuwa sasa amebakiza mechi tano tu kufikia rekodi ya kuwa kocha aliyeiongoza CR Belouizdad katika michezo mingi zaidi mfululizo katika historia ya klabu hiyo ndani ya kipindi kimoja cha kazi. Hii ni hatua muhimu na ya kujivunia kwake binafsi. 📊 Hata hivyo, kocha huyo amesisitiza kuwa kuvunja rekodi pekee hakutoshi, kwani lengo kuu la klabu hiyo kubwa ni kushinda...

Pyramids FC yaifuata FAR Rabat kwa ndege binafsi

Huu ni msafara wa wachezaji wa klabu ya Pyramids FC wakiwa safarini hapo jana wakielekea Morocco kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya AS FAR katika CAF Champions League. Kama kawaida yao, klabu imeandaa ndege maalum (private jet) yenye viti vya Business Class kwa ajili ya timu nzima, ili kuhakikisha wanapata faraja na maandalizi bora kabisa kabla ya mchezo wao wa robo fainali. Mchezo utapigwa siku ya March 13 kwenye uwanja wa Prince Moulaye Abdellah jijini Rabat na itakuwa ni kwenye majira ya saa 4 usiku kwa saa za Morocco ambapo ni sawa na saa 7 usiku kwa saa za Tanzania.

TRA haitaki utani Ligi Kuu bara, yailaza Namungo 2-0

TIMU ya TRA United imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara mchana wa leo Uwanja wa Black Rhino, Karatu Jijini Arusha. Mabao ya TRA United, zamani Tabora United yamefungwa na beki Muivory Coast, Chamou Karaboue dakika ya 62 na mshambuliaji Mganda, Joseph Akandwanaho dakika ya 90’+2. Kwa ushindi huo, TRA United inafikisha pointi 19 katika mchezo wa 14 na kusogea nafasi ya tisa, wakati Namungo FC inabaki na pointi zake 21 za mechi 17 sasa na kushuka kwa nafasi moja hadi ya saba. Beki wa zamani wa Simba SC na Cote RC Abidjan ya kwao, Iivory Coast, Chamou Karaboue ndiye aliyechaguliwa Mchezaji Bora wa Mechi baada ya mchezo huo.

Simba yaiduwaza Singida Black Stars

Licha ya kucheza ugenini, Simba SC jioni ya leo wamepata ushindi mbele ya wenyeji wao Singida Black Stars katika uwanja wa Airtel uliopo Singida mchezo wa Ligi Kuu bara inayodhaminiwa na NBC. Mabao ya Simba SC yamefungwa na Anicet Oura dakika ya 06 na Elie Mpanzu dakika ya 86, goli pekee ya Singida Black Stars limefungwa na Mossi Nduwumwe dakika ya 37. Kwa matokeo hayo Simba inaendelea kushikilia nafasi ya tatu ikiwa na pointi 27 na mechi 12, kesho watani zake Yanga SC watacheza na Tanzania Prisons katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma. Hata hivyo pambamo hilo lilikuwa na ushindani mkali kwani Singida Black Stars waliikamia Simba na wakitaka kupata ushindi lakini vijana wa Simba nao walikuwa makini na kuibuka na ushindi.

Job afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Beki wa klabu ya Young Africans Sports Club, Dickson Job, leo asubuhi amefanyiwa upasuaji uliofanikiwa nchini South Africa kufuatia majeraha aliyoyapata kwenye mchezo dhidi ya Simba Sports Club. Job alipata majeraha wakati wa mchezo huo na kushindwa kuendelea kuumaliza uwanjani. Kupitia taarifa iliyotolewa na Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe, amesema nahodha huyo amefanyiwa operesheni asubuhi ya leo na kwa mujibu wa madaktari hali yake inaendelea vizuri. “Nahodha wetu Dickson Job amefanyiwa operesheni asubuhi ya leo nchini Afrika Kusini na Alhamdulillah jambo limekwenda vizuri kabisa,” amesema Kamwe. Mashabiki na wanachama wa Yanga pamoja na Watanzania kwa ujumla wamemtakia nafuu ya haraka beki huyo muhimu wa timu hiyo anayefahamika kwa umahiri wake mkubwa uwanjani. Dickson Job amefanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Uwanja wa Yanga sasa wafikia pazuri

Uongozi wa klabu ya Young Africans SC, chini ya Rais Eng. Hersi Said, umezidisha kasi ya kutekeleza ahadi ya ujenzi wa uwanja wa klabu hiyo baada ya kufanya kikao cha pili cha kimkakati na ofisi za TARURA pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo. Kikao hicho kilichofanyika leo kimelenga kupokea na kujadili uwasilishwaji wa ramani ya awali pamoja na maelezo ya kina ya kitaalamu kuhusu mradi huo, hatua inayozidi kuwapa matumaini mashabiki wa "Wananchi" kuona klabu yao inamiliki miundombinu ya kisasa. ​Katika kikao hicho, wadau na wataalamu wamejadili mambo muhimu yanayohusu utekelezaji wa mradi, ikiwa ni pamoja na ukaguzi wa eneo na taratibu za kisheria na kiufundi ili kuweka msingi imara kabla ya ujenzi kuanza rasmi. Eng. Hersi amesisitiza kuwa dhumuni la klabu ni kuhakikisha mradi huu unatekelezwa kwa kiwango cha juu cha weledi, jambo ambalo litaifanya Yanga SC kuwa miongoni mwa klabu chache barani Afrika zinazomiliki viwanja vyenye sifa za kimataifa, hivyo kuimarisha zaidi ch...