Machapisho

Les Aigle De Congo yatibua sherehe za Yanga

Picha
Timu ya Les Aigle De Congo ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, (DRC) imeharibu sherehr za Yanga SC baada ya kuifunga mabao 2-1 uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Licha ya mashabiki wa Yanga kujitokeza kwa wingi kusherehekea tamasha lao la Wiki ya Wananchi, lakini vijana hao Aigle wameweza kukomaa na kupata ushindi.

Zitoeni hela benki Yanga wana kikosi hatari

Picha
Na Hans Raphael Yanga wana timu bora sana acheni utani,kama mnasema hela zipo benk zitoeni zilete wachezaji kwasababu Yanga wana kikosi hatari sana ,umeona moto wa Mwijage, umeona moto wa Shalulile, umeona Moto Yao Kouass Umeona moto wa fullback wa kushoto,yule bwana mdogo ni fundi wa mpira,staki kusema sana lakini hapo bado hajaingia Albert Kagwanda bado hajaingia Toure,bado hajaingia Zakouan...aisee Yanga ni hatari toeni hela benk mlete wachezaji

Rashford kuvaa jezi namba 14 Man United hadi mwaka 2027

Picha
Mshambuliaji wa Manchester United, Marcus Rashford atavaa jezi namba 14 akiwa klabuni hapo kuanzia msimu ujao wa 2026/27 baada ya kurejea akitokea Barcelona alihudumu kwa mkopo wa msimu mmoja. Rashford ambaye kabla ya kuondoka klabuni hapo alikuwa akivaa jezi namba 10 amerejeshwa kikosini tayari kwa msimu mpya lakini kwa sasa jezi hiyo inavaliwa na Matheus Cunha hivyo amelazimika kuvaa jezi namba 14, jezi aliyokuwa akivaa huko Barcelona.

Shalulile mzigoni leo

Picha
Mshambuliaji mpya wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu bara Yanga SC Peter Shalulile akifanya mazoezi yake tayari kwa kutambulishwa usiku wa leo watakaocheza na Les Aigle ya DR Congo.

Wananchi wajitokeza siku ya Wiki ya Wananchi

Picha
Baada ya Simba SC kusherehekea tamasha lake Simba Day jana, leo ni siku nyingine ambapo klabu ya Yanga SC wanaadhinisha tamasha lao la Wiki ya Wananchi katika uwanja huo huo wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Mashabiki wa Yanga walijitokeza mapema kuadhimisha Wiki ya Wananchi ambapo watashiriki kucheza na baadaye timu yao ya wanaume ya wakubwa itaingia uwanjani kucheza na Les Aigle ya DR Congo.

Said Ndemla aibukia Kagera Sugar

Picha
Wana Super Nkurukumbi, Kagera Sugar FC wamemtambulisha kiungo wa zamani wa Simba SC, Saidi Hamisi Ndemla kama mchezaji mpya klabuni hapo kwa uhamisho huru baada mkataba wake na JKT Tanzania kufikia ukomo. Kiungo huyo wa kati mwenye umri wa miaka 30, raia wa Tanzania anatua kwenye klabu hiyo iliyopanda daraja l kwenda Ligi Kuu Bara kwa msimu wa 2026-2027 ikiwa ni muendelezo wa maboresho ya kikosi hicho.

Elvis Rupia achafua hali ya hewa Simba Day

Picha
Klabu ya Simba usiku huu imepokea kichapo cha bao 1-9 toka kwa Police FC ya Kenya, mchezo wa kirafiki uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Goli pekee lilisubiri hadi dakika ya nyongeza 90+2 lililofungwa na nyota wa zamani wa Singida Black Stars, Elvis Rupia. Simba ilichezesha wachezaji wake wote wakiwemo wapya, mpira ulikuwa mzuri na timu zote zilionesha uwezo wake.