Machapisho

Dkt Mwigulu aagiza ujenzi wa viwanja vya mazoezi AFCON vijengwe

Picha
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza kuongezwa kasi ya ujenzi wa viwanja vya mazoezi vitakavyotumika katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, ili vikamilike kwa wakati na kukidhi viwango vinavyotakiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF). Amesema kazi hiyo inapaswa kufanyika kwa kasi, ikiwemo kuongeza muda wa kufanya kazi pale inapobidi, ili viwanja vikamilike kwa wakati na Tanzania iwe tayari kabla ya ukaguzi wa maandalizi unaotarajiwa kufanywa na CAF. Waziri Mkuu ametoa maelekezo hayo leo (Ijumaa, Agosti 21, 2026) baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa viwanja vya mazoezi vya Farasi na Leaders Club jijini Dar es Salaam, ambavyo ni miongoni mwa viwanja vitakavyotumika katika maandalizi ya mashindano ya AFCON 2027 yatakayofanyika kwa ushirikiano wa Tanzania, Kenya na Uganda. Amesema Tanzania haipaswi kusubiri hadi dakika za mwisho kukamilisha maandalizi yake kwa sababu CAF inahitaji kujiridhisha mapema kuwa miundombinu inayohitajika iko tayari. “Twen...

Sijamkatia tamaa Doumbia- Barker

Picha
Aliwafunga Singida pale Rwanda CECAFA Kagame cup . Nitampa nafasi mapema aweze kunionyesha kwamba anaweza kufanya hivyo tena. Sijawahi kuwa wa kwanza Wala wa mwisho kuhusu kuamini maendeleo ya mchezo always nachagua nyakati sahihi kuweza kutafakari,kung'amua na kufanya hitimisho kwa mchezaji kwa sababu mpira wa miguu ni process. Ibrahim Doumbia Ni mshambuliaji ambae alikotoka alikuwa daraja la juu sana Wala sio mchezaji mbovu na anaweza kuipa Simba SC Mabao 10+ kwa msimu. Kinachotokea sasa ni kujaribu kumuondoa kwenye zile process za kukaa sawa hasa kiakili na kuzoea mazingira mapya. Wanasimba ndio watu wa kwanza wanaotakiwa kumuamini na kumpa moyo. Kama ilivyo kauli NGUVU MOJA basi iende hadi kuwalinda Wachezaji weru hawa Nimeangalia washambuliaji wa wapinzani yule Shalulile na Hata wengine nao wanastruggle ila mashabiki wanawalinda kama Yai na husikii kelele za kuwakatisha tamaa. Nimemuangalia mshambuliaji mpya wa Azam FC pia ni yaleyale ila timu yake imechagua kumlinda na anaf...

Picco Kikongwe aeleza sababu za kutunga wimbo kikongwe

Picha
Msanii wa muziki, Picco ambaye alitamba na wimbo ‘Kikongwe’ amedai wimbo huo aliuandaa kwaajili ya kupinga mauaji ya vikongwe kwa kuwaonyesha upendo. Picco ambaye ni miongoni mwa wasanii ambao watafanya show kwenye miaka 30 ya BongoFleva Dodoma.

Seleman Mwalimu kila kitu safi

Picha
Young Africans SC tayari imeshamuingiza mshambuliaji wao Selemani Mwalimu kwenye mfumo wa FIFA Connect na kupata karatasi zote za leseni za kuitumikia klabu hiyo kuelekea msimu ujao kutoka Wydad AC! Simba SC hawakuhusika katika kugoma na kutomtoa kwenye mfumo wasababu uhamisho wake ulikuwa umekwisha na kurudi katika klabu yake ya Wydad AC ambao wanammiliki na taarifa za Simba SC kugoma kumtoa kwenye mfumo sio za ukweli. Selemani Mwalimu amepewa session ya peke yake na Mwalimu Manqoba Mngoithi ili kuwa vizuri na kuungana na wenzake kwasababu hakufanya mazoezi ya pre-season na wenzake na muda wowote kuanzia sasa atawatumikia Wananchi. Seleman Mwalimu

Kocha Singida Black Stars aigwaya Simba

Picha
Kocha Mkuu wa Singida Black Stars, Pappy Kimoto, amefunguka wazi kuhusu mchezo wao ujao dhidi ya Simba SC, akitambua ugumu wa wapinzani wao lakini akisisitiza malengo yao ya kusaka ushindi. Kimoto amekiri wazi kuwa Simba ni timu bora na yenye ushindani mkubwa uwanjani. Licha ya kutokuwa na muda wa kutosha wa kufanya maandalizi ya kina kuelekea mchezo huo, alieleza kuwa kikosi chake kipo tayari kwa mapambano. Amesisitiza kuwa wamejiandaa kwenda kupambana vikali ili kuhakikisha wanaondoka na ushindi na alama tatu kamili kesho Kocha wa Singida Black Stars Pappy Kimoto

Singida Black Stars yazindua jezi mpya

Picha
Klabu ya Singida Black Stars imezindua jezi zake mpya kuelekea msimu mpya wa mashindano.Klabu hiyo imewasilisha seti tatu za jezi, ambazo ni Home Kit, Away Kit na Third Kit, kwa ajili ya msimu mpya. Jezi hizo zimekuja ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Singida Black Stars kuelekea msimu wa 2026/27, ambapo timu hiyo itaendelea kushiriki mashindano ya ndani.Wewe umezipa alama ngapi kati ya 10?

Okello aanika mshahara wake, ni kufuru

Picha
Aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Yanga SC, Allan Okello, amevunja ukimya na kuaga rasmi klabu hiyo baada ya kuitumikia kwa muda mfupi lakini wenye mafanikio. Katika ujumbe wake wa kwaheri, nyota huyo raia wa Uganda ametoa shukrani za dhati kwa uongozi wa Yanga SC chini ya Rais wa klabu, wachezaji wenzake, pamoja na mashabiki wa Wananchi kwa kumfanya ajisikie yupo nyumbani Tanzania, huku akisisitiza kuwa imekuwa heshima kubwa kwake kuvaa jezi ya kijani na njano. ​Mara baada ya kuaga Wananchi, Okello amekamilisha usajili wa kujiunga na miamba ya soka nchini Morocco, klabu ya AS FAR (FAR Rabat), ambapo amesaini mkataba wa miaka mitatu kuanza changamoto mpya ya soka barani Afrika Kaskazini. Hatua hii inamfanya kiungo huyo wa kimataifa wa Uganda kuanza maisha mapya katika Ligi Kuu ya Morocco (Botola Pro) akiwa miongoni mwa wachezaji kutoka Afrika Mashariki waliopata fursa ya kujiunga na klabu hiyo kubwa. ​Usajili huu unakuja na maslahi makubwa ya kifedha ambapo Okello atakua akilipwa jumla ...