Machapisho

Ronaldinho Gaucho arejea kwenye soka na mabao

Picha
Miaka 11 baada ya kuaga soka la ushindani, Ronaldinho Gaúcho amerudi tena kwenye soka la kulipwa akiwa na miaka 46 Nguli huyo wa Brazil amejiunga na Ravenna FC ya Italia, inayoshiriki Serie C, akiwa tayari kutoa mchango wake kwa timu hiyo. Cha kuvutia zaidi, Ronaldinho ameacha mlango wazi wa kucheza angalau mchezo mmoja rasmi, huku akitamani kufikisha bao lake la 300 katika soka la kulipwa. Mechi ya kwanza katokea Sub katupia chuma mbili kumbe miaka inaweza kupita, lakini uchawi wa Gaucho hauzeeki.

Allasane Kante atemwa Simba

Picha
Jioni ya leo Klabu ya Simba imemuaga kiungo wake Allasane Kante, katika mchakato wa maboresho na mabadiliko ndani ya kikosi cha Mnyama. Lakini binafsi, niliona bado Kante alikuwa na nafasi pale Msimbazi. Alikuwa na uwezo mkubwa wa kukaba, kushinda mipira na kuanzisha mashambulizi, hasa kupitia pasi zake zenye ubora. Wakati mwingine kwenye maboresho ya kikosi, si kila anayeondoka alikuwa hafai. Kante alikuwa na kitu chake ndani ya uwanja. Huenda Simba wameona kitu kingine mbele, lakini kwangu mimi, kumuacha Kante ni uamuzi ambao bado utahitaji kuthibitishwa na matokeo.

Oruma aiponda Yanga, aifagilia Simba

Picha
Mchambuzi wa michezo Wilson Oruma ametoa kauli nzito kuhusu ubora wa kikosi cha Yanga SC, akidai kuwa timu hiyo haina kikosi cha kutosha kwa ushindani wa msimu huu. Oruma ameenda mbali zaidi kwa kutoa utabiri kwamba Simba SC itatwaa ubingwa, akiamini itakuwa na tofauti ya pointi 10 mbele ya Yanga. Kauli hiyo imeibua mjadala miongoni mwa mashabiki wa soka, huku msimu ukiwa bado katika hatua za mwanzo na timu zikiendelea kupambania alama.  Wilson Oruma

Singida BS yaishushia lundo la magoli Polisi Tanzania

Picha
Timu ya Singida BS usiku huu imeibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Polisi Tanzania katika uwanja wa Airtel uliopo mjini Singida mchezo wa Ligi Kuu bara. Ilianza Polisi kupitia Baraka Michael na goli lao la pili lilifungwa na Ibrahim Ame. Wenyeji Singida BS wakafungua karamu ya magoli kupitia Jonathan Sowah, kisha James Mwashinga, Shekhan Ibrahim na baadae Jeancy Mboma akaweka goli la nne.

Said Mtanda aisifu Pamba Jiji kufungwa 2-0 na Yanga

Picha
Licha ya Pamba Jiji FC kupokea kwa kichapo cha mabao 2-0 dhidi ya Yanga SC katika mchezo wa jana, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mlezi wa klabu hiyo, Said Mtanda— ambaye pia ni shabiki wa damu wa klabu ya Yanga SC ameeleza kuridhishwa kwake na kiwango kilichoonyeshwa na timu hiyo. Mtanda ameeleza kuwa watu wengi walidhani Pamba Jiji ni timu dhaifu na ingekubali kipigo kizito cha magoli matano (5) au zaidi kutoka kwa Yanga SC, lakini wameonyesha ushindani mkubwa uwanjani. Kilichomfurahisha zaidi ni uamuzi wa kocha kuwatumia wachezaji sita (6) kutoka kikosi cha vijana cha U-20 kwenye mchezo huo dhidi ya Mabingwa watetezi Yanga. Mtanda ametoa kauli hizo baada ya kushuhudia mchezo wake wa mwisho kabla ya kuondoka Mwanza, na kuelekea Mkoa wa Simiyu kuendelea na majukumu yake.

Geita Gold yaifuata Simba na ndege

Picha
Kikosi cha Geita Gold FC kimewasili rasmi jijini Dar es Salaam kwa usafiri wa ndege ya Air Tanzania kwa ajili ya maandalizi ya michezo yao miwili mikubwa ya NBC Premier League dhidi ya miamba ya soka nchini, Simba SC na Yanga SC. Hii ni mara ya pili msimu huu kwa Geita Gold kutumia usafiri wa anga kusafiri kuelekea mechi zao ili kuwapa wachezaji mapumziko ya kutosha na kuepuka athari za safari ndefu za barabarani.

Maxi Nzengeli afichua siri za Simba

Picha
Kiungo mshambuliaji raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Maxi Mpia Nzengeli, amefichua kuwa Simba SC ndiyo iliyokuwa klabu ya kwanza kabisa kutoka Tanzania kuonyesha nia ya dhati na kutuma ofa rasmi ya kumhitaji kutoka AS Maniema Union. Akizungumza kupitia podcast ya The Physics inayozungumzwa na Denis Nkane, Maxi alieleza kuwa ingawa Simba ilitangulia, mazungumzo na taratibu zao hazikufikia mwafaka au kwenda kama ilivyotarajiwa, hali iliyotoa fursa kwa Yanga SC kuingia kwenye mbio hizo na kufanikisha saini yake. ​Akifafanua zaidi kwenye mahojiano hayo, Maxi alibainisha kuwa njia yake ya kuelekea Yanga SC ilirahisishwa zaidi na mahusiano mazuri na ya karibu ya kibiashara yaliyokuwepo kati ya bosi wa AS Maniema Union, Jenerali Amisi Kumba, na uongozi wa Yanga. Ushirikiano huo ulikuwa umeimarika kufuatia mafanikio ya usajili wa wachezaji waliotangulia kufanya vizuri kutoka DRC kama Fiston Mayele na Tuisila Kisinda. Kwa kuwa uongozi wa Maniema Union ulimchukulia Maxi kama mtoto wa fa...