Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Mamelodi Sundown's kwishnei, yachapwa 2-1 na Lupopo

Machapisho ya hivi karibuni

Dodoma Jiji yaizima KMC

TIMU ya Dodoma Jiji imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya KMC FC katika mchezo Wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Mabao ya Dodoma Jiji yamefungwa na mshambuliaji Faraj Kayanda dakika ya 43 na winga Iddi Bahati Kipagwile dakika ya 77, wakati la KMC limefungwa na mshambuliaji Rashid Mohamed Chambo dakika ya 76. Kwa ushindi huo, Dodoma Jiji FC inatimiza pointi 17 katika mchezo Wa 14 na kuruka kutoka nafasi ya nane hadi ya sita, wakati KMC inaendelea kushika mkia kwenye ligi ya timu 16 ikibaki na pointi nane za mechi 14 sasa.

Singida Black Stars hoi kwa CR Belouizdad

Timu ya Singida Black Stars ya Tanzania imekubali kichapo cha bao 1-0 dhidi ya CR Belouizdad ya Algeria mchezo wa kombe la Shirikisho Afrika uwanja wa New Amaan Stadium, Zanzibar usiku huu. Goli ambalo limewalaza Singida Black Stars limefungwa na Abdenoour Belhocin, nafasi ya Singida Black Stars kusonga mbele ni ndogo sana hivyo kimahesabu imetolewa kama ilivyo Simba SC pia ya Tanzania.

Ligi ya mabingwa ingeanza sasa basi Simba ingeshinda mechi sita mfululizo - Ahmed Ally

Meneja wa Habari wa Simba SC, Ahmed Ally ametamba kama Ligi ya mabingwa Afrika ingeanza sasa basi Simba SC ingepata ushindi wa mechi sita mfululizo. “Tulikuja hapa kwa ajili ya kupigania heshima ya Mnyama” Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally anasema kama hatua ya makundi ingeanza sasa, basi timu hiyo ingeshinda mechi zote sita. Ahmed amezungumza hayo baada ya Simba kutoka sare na Petro Atletico kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Kocha Al Ahly aahidi kuibeba Yanga

Kocha mkuu wa Al Ahly ya Misri, Jess Thorup ameahidi kuibeba Yanga na kufuzu robo fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika kwani anapambana kupata ushindi dhidi ya AS FAR Rabat ya Morocco katika mchezo wa mwisho ambapo Yanga inatakiwa kushinda dhidi ya JS Kabylie ya Algeria. “Sijaridhishwa na tulivyocheza leo, (jana). Ni vile tumetuzu robo ambacho ndio ilikuwa muhimu...! Jumapili tunacheza vs AS FAR na tutatakiwa kuonesha tupo serious na mashindano.. Tunatakiwa kuamua tuongoze kundi na si vinginevyo..! Tutalazimisha kushinda na itatakiwa iwe hivyo...! Ni lazima tushinde”, amesema Jess Thorup kocha wa Al Ahly

Tresor Mputu; Mchezaji bora wa muda wote TP Mazembe

Mwamba huyu hapa Tresor Mputu mabi anatajwa kuwa ndiye mchezaji bora wa muda wote wa TP Mazembe yaani sio Rainford Kalaba au Mbwana Samatta anayeheshimiwa zaidi pale Mazembe.  Imagine kuna kipindi mzee arsène wenger aliwahi kumuhita kucheza arsenal lakini mwamba alikataa akisema hali ya hewa ya England ni changamoto kwake. Mputu alijiunga na TP Mazembe mwaka 2002 ambapo alicheza mechi 292 na kufunga magoli 144. Ameshinda mataji yafuatayo akiwa na TP Mazembe; 1:Caf Champions mara 1 mwaka 2009 2:Caf Super Cup mara 1 mwaka 2010 3:Ligi Kuu ya Congo DRC mara 5 2006,2007,2009,2011 na 2012. Tuzo binafsi alizoshinda Mputu ni 1:Mchezaji Bora kwa wachezaji wanaocheza ndani ya Afrika mwaka 2009. Mchezaji Bora Ligi Kuu ya DR  Congo mara 3; 2007,2009 na 2011. Tuzo ya mfungaji Bora IFFHS 2007. Mputu amecheza vilabu viwili tu kwenye career yake ya mpira mwaka 2014 alijiunga na Kabuscorp ya Angola ambapo alicheza mechi 49 na kufunga goli ...

Yanga yalala kwa FAR Rabat 1-0

Wawakilishi wengine wa Tanzania katika michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika, Yanga SC usiku huu wamekubali kichapo cha bao 1-0 dhidi ya wenyeji wao AS FAR Rabat uwanja wa Stade Olympique mjini Rabat. Yanga ikicheza vizuri ikitaka kuzuia muda wote Ili wasifungwe, lakini ikakubali kuruhusu goli dakika ya 85 na kufanya mchezo wake wa mwisho dhidi ya JS Kabylie lazima ishinde zaidi ya goli moja huku FAR Rabat ipoteze dhidi ya Al Ahly. Bao la ushindi la FAR Rabat limefungwa na Anas Bach dakika ya 85, wakati huo JS Kabylie ya Algeria imeshindwa kupata ushindi mbele ya Al Ahly ya Misri kwa kutoka sare ya 0-0. .