Machapisho

Simba yamnasa nyota wa Taifa Stars

Picha
Klabu ya Simba Sports Club imekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji na winga wa kimataifa wa Tanzania, Tarryn Allarakhia, baada ya kumsajili kama mchezaji huru (Free Agent), hatua inayotajwa kuwa sehemu ya mkakati wa klabu hiyo kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu mpya wa mashindano ya ndani na kimataifa. Allarakhia, ambaye alizaliwa jijini London nchini England lakini anaitumikia Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, anajiunga na Simba akiwa na uzoefu mkubwa wa kucheza katika soka la Uingereza. Katika safari yake ya soka amewahi kuzichezea klabu mbalimbali zikiwemo Aveley, Maldon & Tiptree, Colchester United, Crawley Town, Woking, Wealdstone pamoja na Rochdale, ambapo alijijengea sifa kutokana na uwezo wake wa kucheza nafasi zaidi ya moja katika eneo la ushambuliaji. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 ana uwezo wa kucheza kama winga wa kushoto, winga wa kulia pamoja na kiungo mshambuliaji. Kasi yake, ubunifu wa kutengeneza nafasi, uwezo wa kupiga chenga na kutoa pasi za ...

Aman Josiah kocha mpya Mashujaa

Picha
Mashujaa FC,imemuajiri kocha wa zamani wa Dodoma Jiji,Amani Richard Josiah kuwa kocha wao mkuu. Julio amefukuzwa,Amani Josiah amepewa kazi

Inno Loemba atua Azam FC

Picha
Klabu ya Azam FC imekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji wa kimataifa kutoka Jamhuri ya Congo, Inno Jospin Loemba, akitokea Simba SC katika hatua inayotarajiwa kuongeza nguvu kubwa kwenye safu ya ushambuliaji ya timu hiyo kuelekea msimu mpya wa mashindano. Loemba, ambaye anacheza nafasi ya kiungo mshambuliaji, alijiunga na Simba SC mwanzoni mwa mwaka 2026 akitokea Colombe Sportive ya Congo-Brazzaville, akiwa ametambulishwa kama mmoja wa vijana wenye kipaji kikubwa katika ukanda wa Afrika ya Kati. Hata hivyo, kutokana na ushindani mkubwa wa nafasi ndani ya kikosi cha Simba, hakupata muda mwingi wa kucheza na kuonyesha kiwango chake ipasavyo. Sasa Azam FC imeamua kumpa nafasi mpya ya kuendeleza kipaji chake, huku ikiamini uwezo wake wa kutengeneza nafasi za mabao, kutoa pasi za mwisho na kuongeza ubunifu katika eneo la ushambuliaji. Usajili huo unaonekana kuwa sehemu ya mkakati wa Azam FC wa kuimarisha kikosi chake kwa ajili ya kupambana katika Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na mashin...

Azam FC yalamba matapishi yake kwa Kipre Junior

Picha
WINGA Muivory Coast, Kipré Tiagori Emmanuel Junior Zunon ‘Kipre Junior’ amejiunga tena na Azam FC akitokea MC Algiers ya Algeria. “Tunayo furaha kuwataarifu kuwa tumemrejesha nyota wetu wa zamani, Zunon Kipre Emmanuel Junior, baada ya kumnunua kutoka klabu ya MCA | Mouloudia Club d'Alger. Welcome back home, Zunon Kipre Emmanuel Junior “ wameandika Azam FC kwenye page yao. Kipre Junior anarejea Azam FC ambako awali alicheza kuanzia msimu wa 2022-2023 akitokea SOL FC d’Abobo ya kwao, Ivory Coast hadi 2024-2025 alipohamia MC Algiers.

Uzinduzi wa Wiki ya Wananchi kufanyika Katoro

Picha
Klabu ya Young Africans SC imetangaza rasmi kuwa uzinduzi wa Wiki ya Mwananchi 2026 utafanyika Katoro, mkoani Geita, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya msimu mpya wa mashindano. Akizungumza, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe, amesema klabu hiyo pia itazindua rasmi jezi mpya za msimu wa 2026/2027 mwishoni mwa mwezi huu.Uzinduzi huo unatarajiwa kuwakutanisha maelfu ya mashabiki wa Yanga kutoka maeneo mbalimbali ya nchi, huku ukiwa mwanzo wa maandalizi rasmi ya timu kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu ya NBC na mashindano ya kimataifa.

Simba yamnasa Kouasi

Picha
Simba SC inaendelea na harakati za kuimarisha kikosi chake huku beki wa kulia Blè Kouasi akitajwa kuwa kwenye rada za Wekundu wa Msimbazi. Nyota huyo anasifiwa kwa uwezo wake wa kupanda na kushuka kwa kasi, pamoja na kupiga krosi zenye ubora mkubwa. Endapo usajili huu utakamilika, ushindani katika nafasi ya beki wa kulia utaongezeka, huku Shomari Kapombe na David Kameta "Duchu" wakilazimika kupambana zaidi kuwania nafasi ya kuanza kikosini msimu wa 2026/27.

Mrithi wa Dube amwaga wino Jangwani

Picha
Klabu ya Yanga imefikia hatua ya mwisho ya kuimarisha safu yake ya ushambuliaji baada ya kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Guinea, Mohamed Saliou Bangoura, aliyekuwa akiichezea MC Alger ya Algeria, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya msimu mpya wa mashindano. Bangoura anaingia Jangwani akiwa na sifa ya kuwa mmoja wa washambuliaji vijana wenye uwezo mkubwa barani Afrika. Kabla ya kujiunga na MC Alger mwaka 2025, aliitumikia Hafia FC ya Guinea ambako alijitengenezea jina kutokana na uwezo wake mkubwa wa kufunga mabao, kasi, nguvu za mwili na uwezo wa kucheza ndani ya eneo la hatari. Baada ya kuhamia MC Alger, mshambuliaji huyo aliendelea kuonyesha kiwango bora, akifanikiwa kufunga mabao muhimu na kuchangia mafanikio ya klabu hiyo katika Ligi Kuu ya Algeria. Aidha, amewahi kuitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Guinea, jambo linaloonyesha kiwango chake na imani aliyonayo kutoka kwa benchi la ufundi la taifa hilo. Usajili wa Bangoura unatajwa kuwa sehemu ya mkakati wa Yan...