Machapisho

Tumepanga kuwashambulia Yanga- Ndayiragije

Picha
Kocha Mkuu wa TRA United SC, Etienne Ndayiragije, ameweka wazi kuwa mchezo wao ujao dhidi ya mabingwa watetezi, Young Africans SC, utakuwa ni fursa adhimu ya kuendelea kuitangaza na kuitambulisha timu yao kwa Watanzania. Ndayiragije amebainisha kuwa tofauti na mechi ya mzunguko wa kwanza iliyopigwa kwenye uwanja wao wa nyumbani jijini Arusha na kumalizika kwa sare ya 0-0, mchezo wa kesho utakuwa wa aina yake kwani unachezwa katika Uwanja wa KMC huku kikosi chake kikiwa kimeshapata mdundo mzuri wa ushindani. Katika upande wa mbinu, kocha huyo mwenye uzoefu mkubwa amefunguka mpango madhubuti wa kukabiliana na safu kali ya ushambuliaji ya Yanga SC, akisisitiza kuwa hawatenda kuzuia badala yake wataingia kwa kushambulia zaidi ili kuwalazimisha wapinzani wao kurudi nyuma kulinda lango lao. Aidha, Etienne Ndayiragije amepiga chini dhana kuwa timu hiyo ni tishio wakiwa tu kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, akitolea mfano matokeo yao makubwa ya ugenini ikiwemo ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Si...

Nasri Kombo mali ya Yanga msimu ujao

Picha
Yanga SC wapo hatua za mwisho kukamilisha dili hili beki wa kati bwana mdogo Nasri Kombo ambaye amekuwa na kiwango bora msimu huu ndani ya TRA United. Yanga SC inataka beki mzawa wa kwenda kuongeza nguvu kwenye ukuta wao pamoja na kutoa Challange kwa Job,Bacca na Mwamnyeto.

Kitambala awaniwa na Singida Black Stars

Picha
Singida Black Stars,wako kwenye mazungumzo ya kina na mshambuliaji wa Azam FC,Jephte Kitambala (27). Mazungumzo yako kwenye hatua nzuri na Kitambala ameonyesha nia ya kujiunga na Singida mwishoni mwa msimu huu.

Barker aeleza mambo matano kuelekea mechi ya kesho

Picha
Mambo 5 Aliyoyasema Kocha Steve Barker Kuelekea Mechi ya Kesho Dhidi ya Singida Black Stars: (LIGI KUU). Tahadhari kwa Mossi Ndumumwe: Barker amekiri kuwa safu ya ushambuliaji ya SBS ni hatari, na Kinarabwa mabao Mossi Ndumumwe amekuwa na moto mkali tangu Januari. Ni mtu wa kuchungwa kwa ukaribu sana. Matumaini ya Ubingwa: Simba bado hawajakata tamaa. Hesabu ni kushinda mechi zao zote huku wakivizia wapinzani wao kuteleza na kudondosha pointi. Vita ya Mbinu: Kocha anaamini wachezaji wake wamekomaa zaidi kimbinu kuliko wapinzani wao, hivyo ushindi kesho ni amri! Ripoti ya Kikosi: Kibabage bado yuko mashakani kuanza hali yake (itaendelea kuangaliwa leo), Anicet Oura kuna uwezekano mkubwa akaanza, na habari njema ni kurejea kwa Morice Abraham kutoka majeraha. Nguvu ya Mashabiki: Barker amewapongeza Wanasimba kwa support ya maana tangu ameanza kazi Msimbazi, na anaomba mzigo uendelee kesho.

Kiboko ya Yanga, atua Caps United Zimbabwe

Picha
Uchizi Vunga amejiunga na klabu ya CAPS United inayoshiriki Ligi Kuu ya Zimbabwe akitokea Silver Strikers FC. - Vunga anakuwa mchezaji wa pili kuondoka katika wiki za hivi karibuni, kufuatia kuondoka kwa beki wa kulia McDonald Lameck ambaye amejiunga na Hard Rock FC. - Vunga alijiunga na Silver Strikers mwaka 2021 akitokea Mzuzu City Hammers, iliyokuwa ikijulikana awali kama Ekwendeni Hammers

Tuzo ya MVP yamponyoka Feitoto

Picha
Inawezekana ubora wa Feisal Salum Feitoto' usitoshe pekee kumbeba kwenye mbio za tuzo ya mchezaji bora wa msimu (MVP) ikiwa hana ubingwa wa Ligi Kuu mkononi. Mambo yamebadilika kwenye takwimu: Asisti: Elie Mpanzu sasa ndiye kinara akiwa nazo 9, akimwacha Fei Toto mwenye 8. Ufungaji: Yupo sawa na Mossi Ndumumwe, wote wakiwa na mabao 14, Allan Okello hayupo mbali (11). Bila kombe la Ligi Kuu, njia pekee ya Fei kutwaa tuzo ya MVP inakuwa ni kutawala takwimu zote mbili. Mchezo wa jana dhidi ya Yanga SC unaweza ukawa umehamisha mjadala mzima kwenda kwa wachezaji wa Simba au Yanga (iwapo mmoja wapo akibeba ubingwa), labda tu kama Feisal atarejesha ufalme wake kileleni kwenye takwimu. Haina ubishi, Fei Toto ni kiungo mfungaji bora zaidi nchini tangu atue Chamazi, lakini mechi dhidi ya Coastal Union na Dodoma Jiji ndizo zitakazoamua hatma yake.

Aucho akaribia kutua Gor Mahia

Picha
Nahodha wa Uganda Cranes, Khalid Aucho, anatajwa kuwaniwa na klabu za Gor Mahia na Tusker FC kwa ajili ya usajili wake, kwa mujibu wa taarifa zinazoripotiwa nchini Uganda. Kiungo huyo mwenye uzoefu mkubwa kwa sasa anakipiga katika kikosi cha Singida Black Stars, huku klabu hizo mbili za Kenya zikifuatilia kwa karibu uwezekano wa kumpata katika dirisha hili la usajili