Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Mbuni yaitupa nje Mtibwa Sugar kombe la CRDB

Machapisho ya hivi karibuni

Yusuph Kagoma aongeza miwili tena

Klabu ya Simba imefanikiwa kumuongezea mkataba miaka miwili (2) mchezaji wao Yusuph Kagoma ambapo utatamatika 2028 mwezi June. Simba inajiimarisha vyema kuelekea msimu ujao kwaajili ya michuano ya kimataifa

Yanga yaipiga Polisi Tanzania 7-1, Depu aondoka na mpira wake

Timu ya Yanga SC usiku huu imepata ushindi mnono wa mabao 7-1 dhidi ya Polisi Tanzania uwanja wa KMC Complex jijini Dar es Salaam mchezo wa kombe la CRDB. Kwa matokeo hayo Yanga SC inaungana na Simba SC kutinga hatua ya 16 bora, mabao ya Yanga yamefungwa na Mudathir Yahya dakika ya 01, Laurindo Depu 22, ambaye pia alifunga mabao mengine mawili dakika ya 32 na 59, mabao mengine yamefungwa  na Joseph Majagi dakika ya 38, Bubah Jammeh dakika ya 76 na Abdulnassir Mohamed "Casemilo". Goli la Polisi Tanzania limefungwa na beki wa Yanga, Frank Assink dakika ya 81. Hata hivyo mshambuliaji wa Yanga, Laurindo Depu ameondoka na mpira wake baada ya kufunga mabao matatu.

Ahoua afunga bonge la goli CR Belouizdad

Kiungo Mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Jean Charles Ahoua hapo jana aliifungia bao Klabu yake ya CR Belouizdad kwenye ushindi wa bao 3-0 dhidi ya MB Rouisat kwenye mchezo wa Ligi Kuu Nchini Algeria. . Ahoua mwenye umri wa miaka 24 alisajiliwa na Klabu hiyo akitokea Simba SC ya Tanzania.

Simba yawapa magari wachezaji wanne

Wachezaji wanne wa Klabu ya Simba Gibril Kasali, Ismail Toure, Anicet Oura na Libasse Gueye,wamekabidhiwa gari zao na kampuni ya utengenezaji wa vifaa vyote vya michezo vya Simba SC Jayrutty. Ikumbwe kuwa gari hizi zitakuwa mali ya Simba SC endapo wachezaji hao wataamua kwenda kutafuta changamoto nyingine au kuvunjiwa mkataba.

MJUE NABII IBRAHIM- 2

Inaandikwa na Fikiri Salum Ilipoishia Mwa 22: 1-19 inatuletea habari ya kusisimua kuhusu sadaka ambayo Mungu alimdai Abraham yaani kumchinja Isaka, ni kimoja kati ya vielezo vya imani ya binadamu, imani inayooneshwa kwa matendo ya utiifu (Yak 2:21-22). Endelea Abraham hakusita kumrudishia Mungu kile alichopewa, akaondoka alfajiri akasafiri mpaka mahari alipoambiwa (Wayahudi) wanaamini mlima huo ndipo walipojenga hekalu la Yerusalem) kwa niaba ya waamini wote, Abraham alikuwa tayari kumchinjia Mungu mwanae pekee ampendaye. Lakini kadiri ya Injili atakayemtoa kweli mwana pekee ni Mungu baba (Yoh 8-16) Yesu ndiye mwanakondoo aliyeuliziwa na Isaka na ambaye Mungu akajipatia juu ya mlima Kalivari alioupanda huku amejitwika kuni, basi mti wa msalaba. Abraham aliamini uwezo wa Mungu juu ya mauti na hasa uaminifu wake kwa ahadi alizompa kwa hiyo akarudishiwa mwana hai kama mfano wa ufufuko, na katika yeye, yaani katika mzawa wake watu wote wakabarikiwa Maisha ya imani yanadai daima sadaka, has...

ATCL yarudisha safari za Dubai

Shirika la ndege la Air Tanzania (ATCL) limetangaza safari maalum za ndege kati ya Dar es salaam na Dubai Jumapili March 08,2026 safari ambazo zitawahusu Abiria walioathiwa na kusitishwa kwa safari za Dubai kutokana na vita inayoendelea kati ya Iran dhidi ya Marekani na Israel. ATCL kupitia taarifa yao ya leo March 06,2026 imesema safari hizo zitakuwa ni Dar es salaam - Dubai - Dar es aalaam na imesisitiza kuwa safari hizo sio zile za kawaida za kibiashara bali ni safari maalum zinazolenga kufidia safari ambazo zilisitishwa na Abiria wakashindwa kusafiri licha ya kuwa walilipia tiketi zao. Kipaumbele kitatolewa kwa Abiria ambao wana tiketi halali kwa safari iliyoathirika ya route ya Dar es salaam - Dubai, Abiria wanashauriwa kuwasiliana na ofisi za ATCL kwa maelezo zaidi na kupata uthibitisho wa safari na muda wa kuondoka”