Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Hasheem Thabit achaguliwa kuwa Rais wa TBF

Machapisho ya hivi karibuni

Yanga wapiga tizi la mwisho la kuivaa Simba kesho

Kikosi cha Yanga SC leo kimefanya mazoezi ya mwisho kabla ya kuwavaa watani zao Simba SC kesho mchezo wa Ligi Kuu bara katika uwanja wa New Amaan Stadium, Zanzibar.

Sebastian Nkoma: Ni kocha wa soka la wanawake aliyeinua vipaji hapa Tanzania

Na Abdul Makambo KOCHA Sebastian Nkoma ni mmoja wa makocha wazawa waliotoa mchango mkubwa katika maendeleo ya soka hapa nchini Tanzania .Pamoja na nchi yetu wamepita makocha wengi wazawa wenye uwezo na majina makubwa kama Mansour Magram, Joel Bendera, Ray Gama, Ayoub Mohamed, Zacharia Kinanda na Elijah Kategile. Wengine ni Iddi Machupa, Pius Nyamko, Edmund Thomas, Mohamed Msomali, Salum Madadi, Abdalah Kibaden, Omary Mahadhi, Abdurahman Juma, Athuman Juma Kalomba, Silylelsaid Mziray, Kenny Mwaisabula, Hamim Mawazo na hao ni baadhi. Nkoma alipokuwa Yanga Princess (kulia) Nkoma ni mmoja wa makocha wetu wazawa mwenye moyo  Nkoma amezifundisha timu nyingi hapa Tanzania na baadhi ni kama Rhino ya Tabora. Soka la wanawake ndio lililomtoa kocha huyo, lakini kwa wanaume pia alianza kufanya mabalaa kwani aliifundisha timu ya taifa ya vijana ya Tanzania yeye na Bakari Shime aliipeleka katika AFCON ndogo kule nchini Gabon, akiwa na wanasoka vijana kama Ramadhan Kabwili, Kibwana Shomari, Dickson J...

Barker aahidi ushindi dhidi ya Yanga kesho

Kocha wa Simba SC Steve Barker anasema wanayo fursa ya kubadili taswira yao kesho mbele ya watani wao Yanga. Ni mkutano wa makocha na manahodha wa Yanga na Simba

Pedro akiri Simba ni timu kubwa

Kocha wa Yanga SC, Pedro Goncalves anasema tangu ametua Jangwani wamecheza mechi kadhaa kubwa, lakini kesho wanakwenda kukutana na mpinzani wao mkuu. Ni mkutano wa makocha na manahodha wa Yanga na Simba 

Karia ampiga mkwara mwamuzi wa dabi

Rais wa TFF Wallace Karia amesema kuwa Mwamuzi atakaeharibu mchezo wa Dabi ya Kariakoo kati ya Yanga SC dhidi ya Simba SC atafunguliwa mashitaka mahakamani na kuondolewa kwenye Mpira kabisa "Atakaejaribu kuharibu huo mchezo, sio tu kwamba ataondoka kwenye Mpira maisha yake yote pia tutamfungulia mashitaka kumshitaki, tumfunge wala hatutakuwa na masihara na hilo nalizungumza wazi" Rais Karia ameyasema hayo leo wakati akizungumza kwenye mkutano wa 20 wa Mwaka wa TFF unaofanyika Leo Kahama.

Motsepe kuwania Urais Afrika Kusini

Bilionea wa Afrika Kusini, Patrice Motsepe, ameibuka katikati ya tetesi za uwezekano wa kugombea urais wa chama tawala cha African National Congress (ANC), licha ya yeye mwenyewe kukanusha mipango hiyo. Tetesi hizo zimeongezeka baada ya Motsepe kutangaza kustaafu nafasi yake ya mwenyekiti mtendaji wa kampuni ya madini ya African Rainbow Minerals, hatua iliyotafsiriwa na baadhi ya wachambuzi kama dalili ya mwelekeo mpya wa kisiasa. Baadhi ya wanachama wa ANC wanaamini uzoefu wake wa kibiashara unaweza kusaidia kukuza sekta ya viwanda na kupunguza ukosefu wa ajira nchini South Africa. Hata hivyo, iwapo angechaguliwa, Motsepe angekuwa kiongozi wa kwanza wa ANC katika enzi ya demokrasia asiye na historia ya mapambano ya moja kwa moja dhidi ya ubaguzi wa rangi au kifungo cha kisiasa