Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Al Nassr yakamilisha usajili wa Kibu Denis

Machapisho ya hivi karibuni

Kibu atimkia Al Nassr

Muda wowote kuanzia sasa, Simba itakamilisha makubaliano ya kumuuza mshambuliaji Kibu Denis kwenda Al Nasr ya Libya. Chanzo kutoka ndani ya klabu hiyo kimeithibitishia Mwananchi Digital kuwa mshambuliaji huyo anajiandaa kukamilisha mchakato wa kujiunga na miamba hiyo ya Libya. “Kibu anaenda Libya. Klabu imeshafikia makubaliano ya kumuuza na kuna mambo machache tu yamesalia ili uhamisho huo ukamilike,” kimefichua chanzo hicho. Hii ni mara ya pili kwa Al Nasr kumhitaji Kibu kwani mara ya kwanza ilikuwa katika dirisha kubwa la usajili kabla ya kuanza kwa msimu huu ambapo nia yao haikufanikiwa. Lakini awamu hii Al Nasr wameonekana kuja na nguvu mpya ambayo imewafanya wafanikiwe kumuachia Kibu ili kukwepa nyota huyo kuondoka bure baada ya msimu kumalizika. Ifahamike kwamba mkataba wa Simba na Kibu Denis utafikia tamati mwishoni mwa msimu huu hivyo klabu hiyo imeonekana haiko tayari kuziachia noti za Walibya hao kwa sasa. {Via @mwananchi

Msuva na timu yake wabanwa Ligi Kuu Iraq

Nyota wa Tanzania Simon Msuva na timu yake ya Al Talaba wametoka sare ya 1-1 dhidi ya timu ya Al Karma kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Iraq. Msuva alikuwa kwenye kiwango kizuri alipokuwa katika timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars iliyoshiriki fainali za AFCON zilizofanyika nchini Morocco ambapo Stars ilifika hatua ya 16 bora.

Depu ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa Yanga mwezi Januari

MSHAMBULIAJI mpya, Laurindo Dilson Maria AurĂ©lio ‘Depu’ ameshinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa Yanga mwezi Januari 2026.

Mukwala awa Mganda wa kwanza kulipwa mshahara mkubwa

SMshambuliaji wa Uganda Cranes, Steven Desse Mukwala ameandika historia mpya baada ya kuwa mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa zaidi kutoka Uganda kwa sasa. Mukwala analipwa dola 55,000 kwa mwezi (takribani shilingi milioni 220 za Uganda na zaidi ya milioni 140 za kitanzania)akiwa na klabu ya Al-Nassr Benghazi ya Libya ambayo amejiunga nayo akitokea Simba Sc ya Tanzania.

Mtanzania mwingine amfuata Asha Masaka Uingereza

Kiungo Malaika Meena amejiunga na klabu ya Ipswich Town FC Women inyoshiriki ligi daraja la kwanza nchini Uingereza kwa mkopo akitokea klabu ya Bristol City inayoshiriki ligi daraja la kwanza nchini Uingereza. Malaika alijiunga na Bristol City Februari 2025 baada ya kumaliza masomo yake na kucheza soka la chuo nchini Marekani. Alisaini mkataba wa miaka miwili na nusu (2.5 years) wenye chaguo la kuongeza mwaka mmoja zaidi. Timu / akademi alizopita Malaika Meena 1. Arsenal Academy – alianza kukuza kipaji chake hapo. 2. Chelsea Academy – akaendelea na maendeleo ya soka la vijana. 3. Wake Forest University (USA) – alicheza kwa takribani miaka mitatu na nusu kabla ya kurejea England. 4. Bristol City Women FC – amedumu kwa mwaka mmoja Malaika Meena anahesabiwa kama mchezaji wa wa kimataifa wa Tanzania (Twiga Stars) ingawa hajawahi vaa jezi ya Tanzania na badala yake aliwahi kuiwakilisha England katika ngazi za vijana ikiwemo mwaka jana timu ya taifa ya Uingereza chini ya miaka 23.

Yanga Princess yamtambulisha straika mpya balaa

Rasmi klabu ya Yanga Princess imemtambulisha mshambuliaji wake mpya Oluwa Samwel Yemis. Oluwa ambaye amewai itumikia klabu ya Edo Queens na TP Mazembe pia amewai itumikia timu ya taifa ya Nigeria chini ya miaka 20 ana mudu kucheza nafasi zote za ushambuliaji. Kama atakuwa katika ubora wake pasi na shaka hapa Yanga Princess wameongeza idadi ya magoli, wameongeza mtu anaeweza kukupa magoli 5+ au kutengeneza nafasi zaidi ya 5+ katika mechi kuanzia 10.