TIMU ya Azam FC imetoa sare ya bila kufungana na wenyeji, Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Kwa matokeo hayo, Azam FC wanafikisha pointi 24 katika mchezo wa 12 na kupanda kwa nafasi moja hadi ya nne, wakati Tanzania Prisons inafikisha pointi 13 katika mchezo wa 15, ingawa inabaki nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.
MAMBO UWANJANI
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com