Machapisho

Hussein Abel kuwa kipa chaguo la kwanza Simba?

Picha
Golikipa namba mbili wa Simba, Hussein Abel ambaye leo katika uwanja wa Kaitaba Bukoba mkoani Kagera amechukua nafasi ya Mamadou Djibrila Kassali Tanja aliyeumia wakati timu yake ikiumana na Kagera Sugar. Abel anaweza kuchukua nafasi na kuwa golikipa chaguo la kwanza endapo ataweza kuwajibika golini na kumshawishi kocha Steve Barker kusajili kipa mwingine endapo majibu ya daktari yatakuwa magumu kwa Kassali. Kassali, amepata jeraha katika mchezo wa leo na hali yake imezua hofu baada ya kuonekana akilia uwanjani, jambo linaloashiria kuwa huenda majeraha hayo yakawa makubwa. Kwa misimu kadhaa mfululizo, Simba imekuwa ikikumbwa na changamoto ya majeraha kwa makipa wake. Aishi Manula, Ayoub Lekred, Moussa Pinpin Camara na Yacoub Selemani ni miongoni mwa makipa waliowahi kukumbwa na majeraha yaliyowafanya kukaa nje kwa vipindi mbalimbali. Hata hivyo, kuhusu hali ya Tanja Kassali, bado ni mapema kutoa hitimisho kuhusu ukubwa wa jeraha hilo. Tunasubiri ripoti rasmi ya madaktari ili kufahamu h...

Ronaldo aweka wazi ataacha soka mwaka huu

Picha
Cristiano Ronaldo ametoa kauli inayoweza kuwa ishara kubwa ya mwisho wa safari yake ya soka, akisema mwaka 2026 huenda ukawa mwaka wake wa mwisho kucheza soka la kulipwa. Akizungumza katika mahojiano na jarida la Vogue, nyota huyo mwenye umri wa miaka 41 amesema: “Huenda huu ukawa mwaka wangu wa mwisho katika soka. Nataka kuacha urithi wa ajabu. Tayari nina mipango yote ya maisha yangu ya baadaye.” Ronaldo amesema tayari ana picha kamili ya maisha yake baada ya soka, akitarajia kutumia muda zaidi kusafiri, kuwa na familia yake na kufurahia michezo mingine kama padel. Kauli hiyo imezua gumzo kubwa duniani, huku Ronaldo akiwa bado anaendelea kuichezea Al-Nassr na akiwa katika harakati za kufikia rekodi ya mabao 1,000 katika maisha yake ya soka.

Al Hilal yafanya balaa kubwa Rwanda

Picha
Miamba ya Sudan, Al Hilal Omdurman, imeendelea kuthibitisha umahiri wake mkubwa kwenye sekta ya usajili baada ya kuikanda Kiyovu Sports mabao 5-0 nchini Rwanda, huku nyota wao mpya Ansumana Samura akiwa mwiba mchungu dimbani! Kijana huyo mwenye umri wa miaka 18 pekee, aliyekabidhiwa jezi ya aliyekuwa nyota wa timu hiyo Jean Girumugisha, ametia kambani mabao matatu na kuonyesha mwanzo wa kishindo. Mabao mengine ya Al Hilal yaliwekwa kambani na Qamardine pamoja na Ahmed Salem kusaidia kukamilisha ushindi huo mnono wa mabao 5-0.

Simba yaendeleza ilipoishia

Picha
Wekundu wa Msimbazi au Simba SC jioni ya leo imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Kagera Sugar katika uwanja wa Kaitaba Bukoba mkoani Kagera. Mabao ya Simba yamewekwa kimiani na beki wa kati Ismail Toure raia wa Ivory Coast na baadaye mshambuliaji Elie Mpanzu raia wa DR Congo. Ushindi huo ni mwanzo mzuri wa Ligi Kuu bara ikipata ushindi ugenini na kufikisha alama 3 ikishika nafasi ya tatu ikiwa nyuma ya Singida Black Stars inayongoza na Yanga.

Starboy kuagwa kwa heshima

Picha
Kuna uwezekano mkubwa Yanga wakamuaga kwa heshima Starboy Allan Okello,kwenye mechi ijayo dhidi ya Coastal Union. Rabat wanamtaka Okello aripoti kambini haraka sana ila Yanga wanaomba wavumiliwe hadi tarehe 20 dhidi ya Coastal ili wamuage Okello ataingia leo Dar es salaam na kikosi kizima cha Yanga wakitokea Lindi na baada ya hapo watajadiliana.

Housseine Zakouani kiungo mshambuliaji mwenye kasi Yanga

Picha
Housseine Zakouani ndiye mchezaji wa Yanga kwenye eneo la kushambulia ambaye anaweza kuwa yupo haraka sana kwenye kuamua. Hatari zaidi anagonga miguu yote,alitoa pasi ya bao na mguu wa kulia kwa njia ya krosi kutokea pembeni,alafu kuna nyingine alipiga na kushoto ikala chuma ilibaki kidogo sana nyavu zitikisike. Amekuja kuwaongezea Yanga haraka kipindi cha pili kwenye kujenga mashambulizi na impact yake imeonekana kwenye mabao yote mawili. Housseine Zakouani ni moja ya wachezaji ambao nimewabetia kufanya vizuri na jezi ya Yanga,na imani yangu naendelea kuiongeza kwake.

FAR Rabat yamtambulisha Okello

Picha
Klabu ya FAR Rabat ya Morocco imefanikiwa kukamilisha usajili wa Allan Okello kwa ada ya dola za Marekani milioni 1.2 (takribani shilingi bilioni 3.1 za Kitanzania). Uhamisho huo unatajwa kuwa miongoni mwa mauzo makubwa ya wachezaji yaliyofanywa na Yanga katika siku za hivi karibuni, huku ukionyesha jinsi kiwango cha Allan Okello kilivyovutia klabu mbalimbali kutoka nje ya Tanzania. Kiungo huyo amekuwa mmoja wa wachezaji muhimu wa Yanga kutokana na uwezo wake wa kutengeneza nafasi, kufunga mabao na kuiongoza timu katika mechi mbalimbali za mashindano ya ndani na kimataifa. FAR Rabat, ambayo ni moja ya klabu kubwa na zenye mafanikio nchini Morocco, imeamua kuwekeza kiasi hicho kikubwa cha fedha ili kuipata saini ya Okello, jambo linaloonyesha imani kubwa waliyonayo juu ya uwezo wake.