Machapisho

Girumugisha awasifu viongozi wa Yanga

Picha
Baada ya Jean Claude Girumugisha kujiunga na klabu ya Al Ahli Tripoli ya nchini Libya ameweka wazi jinsi ambavyo dili lake la kujiunga na klabu ya Yanga liliikwama, huku akiwamwagia sifa mabosi wa Yanga. "Ni kweli Yanga walinitaka na nilikuwa tayari kwenda.Nilifurahishwa sana na namna viongozi wao walivyoniheshimu na walivyokutana na mimi,Tatizo lilikuja kwenye maslahi ya klabu kwa klabu. Kulikuwa na mambo ambayo yalihitaji makubaliano kati ya Al Hilal na Yanga, hivyo haikuwezekana kumaliza kila kitu," "Pengine baadaye nitakuja Tanzania, nilipenda mabosi wa Yanga walivyozungumza na mimi kwa heshima kubwa." -Jean Claude Girimugisha (Akielezea jinsi ambavyo dili lake kujiunga na Yanga lilivyokwama na kutua Al Ahli Tripoli)

Rashid Juma aibukia Mbeya City

Picha
Klabu ya Mbeya City ya mkoani Mbeya hii leo imemtambulisha kiungo mshambuliaji wa zamani wa Simba, Rashid Juma Mtabigwa kuwa mchezaji wake.

Ibrahim Jaabar avunja ukimya

Picha
Kiungo wa Simba SC, Ibrahim Jabaar, amevunja ukimya na kuonyesha ukomavu wa hali ya juu kufuatia kadi nyekundu aliyoonyeshwa katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Pamba Jiji FC jijini Mwanza. Kupitia ukurasa wake wa Instagram (Insta Story), nyota huyo ameonyesha uwajibikaji kwa kuandika ujumbe mfupi uliosomeka: "Hakuna visingizio, nawajibika kwa hili", akikubali kosa lililoiweka timu yake kwenye presha ya kucheza pungufu kipindi chote cha pili. ​Kauli hiyo ya Jabaar inakuja muda mfupi baada ya Msemaji wa Simba SC, Ahmed Ally, kuweka wazi kuwa benchi la ufundi na uongozi utakaa na wachezaji kukemea rafu zisizo na ulazima zinazopelekea kadi nyekundu. Mwitikio huu wa Jabaar umepokelewa kwa hisia chanya na mashabiki wengi wa Msimbazi, wakimsifu kwa kuonyesha nidhamu, ukweli na ujasiri wa kukubali kosa badala ya kutafuta visingizio. ​Unazungumziaje kitendo hiki cha Ibrahim Jabaar kukubali kosa na kuwajibika waziwazi kufuatia kadi hiyo nyekundu? Dondosha maoni yako!

Yanga wametoa burudani ya mabao

Picha
Na Hans Raphael Yanga leo wametoa burudani ya mabao ya aina yake, Bao Yakideo na ufundi binafsi. Maxi Nzengeli: Bao la pili lilikuwa Golazo la kiwango cha juu kabisa! Mudathir Yahya ameendelea kuonyesha ukomavu kwenye umaliziaji, na kwanini ni mchezaji muhimu akiwa uwanjani. Albert Kangwanda: Kwenye kipindi cha kwanza, alionyesha ukali kwa kubadili half-chance kuwa bao kamili akiwa ndani ya kisanduku. Mohamed Hussein, Goli la leo karudia alichofanya kipindi alivyokuwa Simba SC, kwenye mechi ya kimataifa. Takwimu za Kipindi cha Kwanza: Mchezo ulikuwa upande mmoja zaidi (flat performance kutoka kwa Coastal Union). Yanga walitawala kila idara: Mpira wa Miguu (Possession): Yanga 73% vs Coastal Union 27% Mashuti: Yanga walipiga 15 (7 zikiwa on target) na kupata mabao 2. Coastal Union: Takwimu zote muhimu za mashambulizi zilisoma 0. Bila umaridadi na uokoaji wa kipa Chuma Ramadhan Mgeni, coastal wangeweza kupata msiba mkubwa zaidi. Mbinu za Low Block Hazisaidii: Kwa timu za daraja la chini a...

Polisi Tanzania yawabutua JKT Tanzania

Picha
Polisi Tanzania FC iliyopanda Ligi Kuu mwaka huu, imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya maafande wenzao wa JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliochezwa leo. Mabao ya Polisi Tanzania yamefungwa na Jamal Mtegeta kunaki dakika ya 45+1 ya kipindi cha kwanza na Habib Kyombi dakika ya 65 ya kipindi cha pili. Ushindi huo unaifanya Polisi Tanzania kuboresha matokeo yake baada ya mchezo wa awali dhidi ya Azam FC kutoka sare ya bao 1-1, hali ambayo inaonesha Polisi Tanzania wako vizuri. Kwa upande wa JKT Tanzania, sasa inapaswa kujikwamua katika hali hiyo katika mchezo wake ujao dhidi ya Yanga SC, utakaochezwa Agosti 24. Polisi Tanzania ilirejea Ligi Kuu Bara mwaka huu baada ya kukaa nje kwa misimu mitatu tangu iliposhuka daraja mwishoni mwa msimu wa 2022/23.

Yanga haikamatiki, yailalua Coastal 4-1

Picha
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu bara Yanga SC usiku huu imepata ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Coastal Union ya Tanga katika uwanja wa KMC Complex jijini Dar es Salaam. Kwa ushindi huo Yanga insongoza ligi hiyo baada ya kufikisha pointi 6, Yanga ilitangulia kupata bao kupitia kwa Albert Kangwanda na kufuatia na Maxi Nzengeli. Kikosi hicho cha Yanga kinachonolewa na Manqoba raia wa Afrika Kusini, kiliandika bao tatu lilifungwa na Mudathir Yahya, Coastal Union walipata bao la kufutia machozi likifungwa na Gradi Kiala. Yanga waliendeleza kulishambulia goli la Coastal na kupata bao la nne likiwekwa wavuni na Mohamed Hussein Zimbwe Jr .

Injinia Hersi aikabidhi jezi ya Yanga familia ya Kifukwe

Picha
Rais wa Yanga, Hersi Said amekabidhi Jezi za Young Africans Sports kwa familia ya Rais wa zamani wa Yanga Francis Kifukwe, ikiwa ni ishara ya heshima na kutambua mchango mkubwa wa Baba yao kwenye klabu ya Yanga kipindi cha uongozi wake. - Mwili wa Kifukwe aliyefariki Jumamosi akiwa matibabu nchini India unaagwa mchana huu kwenye Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam na utazikwa Jumamosi wiki hii yumbani kwao Kyela, Mbeya. (Picha kwa hisani ya Yanga SC).