Inaandikwa na Fikiri Salum Ilipoishia Mwa 22: 1-19 inatuletea habari ya kusisimua kuhusu sadaka ambayo Mungu alimdai Abraham yaani kumchinja Isaka, ni kimoja kati ya vielezo vya imani ya binadamu, imani inayooneshwa kwa matendo ya utiifu (Yak 2:21-22). Endelea Abraham hakusita kumrudishia Mungu kile alichopewa, akaondoka alfajiri akasafiri mpaka mahari alipoambiwa (Wayahudi) wanaamini mlima huo ndipo walipojenga hekalu la Yerusalem) kwa niaba ya waamini wote, Abraham alikuwa tayari kumchinjia Mungu mwanae pekee ampendaye. Lakini kadiri ya Injili atakayemtoa kweli mwana pekee ni Mungu baba (Yoh 8-16) Yesu ndiye mwanakondoo aliyeuliziwa na Isaka na ambaye Mungu akajipatia juu ya mlima Kalivari alioupanda huku amejitwika kuni, basi mti wa msalaba. Abraham aliamini uwezo wa Mungu juu ya mauti na hasa uaminifu wake kwa ahadi alizompa kwa hiyo akarudishiwa mwana hai kama mfano wa ufufuko, na katika yeye, yaani katika mzawa wake watu wote wakabarikiwa Maisha ya imani yanadai daima sadaka, has...