Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Massanza amsifia mkandarasi wao aliyejenga Airtel Stadium

Machapisho ya hivi karibuni

Mokwena afutwa kazi MC Alger

Mwalimu wa soka kutoka nchini Afrika Kusini, Rulani Mokwena, amehitimisha rasmi safari yake na klabu ya MC Alger ya nchini Algeria kwa makubaliano ya pande zote mbili.  Baada ya kuachana na klabu hiyo, ripoti za uhakika zinaeleza kuwa kocha huyo sasa anatarajiwa kuelekea nchini Libya kuchukua nafasi ya kocha mkuu wa klabu ya Al Ittihad. ​Hatua hiyo inamfanya Mokwena kwenda kuungana na wachezaji wake wa zamani, Thembinkosi Lorch na fundi wa mpira Stephane Aziz Ki, ambao tayari wapo nchini humo wakitumikia klabu hiyo. Muunganiko huu unatazamwa kama "reunion" ya kiufundi inayoweza kuifanya Al Ittihad kuwa tishio kubwa, kwani Mokwena anajua vyema jinsi ya kuwatumia nyota hao wawili waliowahi kung'ara chini ya mikono yake huko nyuma.

Mvua yavunja pambano la TRA na Simba Sheikh Amri Abeid

Mechi ya Ligi Kuu ya NBC kati ya TRA United vs Simba SC iliyopangwa kuchezwa leo saa 10:00 jioni, imeahirishwa kutokana hali ya uwanja iliyosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha jijini Arusha.  Mechi hiyo sasa itapangiwa siku nyingine, Simba ilitakiwa kucheza leo Ili kufikisha mechi 13 sawa na wenzake Yanga, Azam FC na Singida Black Stars ambao wana viporo.

Ibenge aigwaya Yanga

Kocha mkuu wa timu ya Azam FC ya Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, Florent Ibenge raia wa DR Congo, ameigwaya Yanga SC ambao atakutana nao kesho katika uwanja wa Mkapa. "Huu mchezo tulipaswa tucheze Chamazi, Tutacheza mechi zote mbili uwanja wa Benjamin Mkapa ambao ni uwanja wa nyumbani wa Yanga na Simba, Yanga Wana nafasi ya kushinda kwasababu wapo nyumbani ila hatulalamiki, tutacheza na kujaribu kushinda" Frolent Ibenge, Kocha Mkuu Azam FC.

KANISA KATOLIKI NA HISTORIA YAKE

Inaandikwa na Fikiri Salum Ilipoishia Katika juhudi hizo Monasteri za Wabenedikto na Wamisionari waliotumwa katika Ulaya nzima walitoa mchango mkubwa, pamoja na ule wa Karolo mkuu, mfalme wa Wafaranki kabila la Kijerumanik muhimu zaidi katika historia, ambalo lilikuwa la kwanza kuingia kanisa katoliki moja kwa moja bila kupitia Ukristo na Kiario. Endelea KATOLO alitawazwa na Papa Leo 111 kuwa Kaisari wa magharibi (800), ushirikiano kati ya mapapa na makaisari wa Dola takatifu la Kiroma (Ujerumani wa leo na nchi kando kando) ulikuwa na mafanikio kadhaa na matatizo mengi zaidi na zaidi. Baada ya Uislamu kuanza katika Karne ya 7 na kuteka maneno mengi ya Kikristo, kanisa katoliki liliona wajibu wake kuitikia maombi ya Wakristo waliohitaji msaada dhidi ya dhuluma iliyolenga kuwafanya wasilimu, ndiyo chanzo cha vita ya msalaba vilivyotawala karne zilizofuata. Wengi wanaoma karne ya 13 kuwa kilele cha matunda ya kanisa katoliki katika kulea upya Ulaya magharibi kwa kuzaa hasa mashirikia ya o...

Mashujaa FC yasawazishiwa goli dakika ya mwisho wa mchezo

TIMU ya Mashujaa FC imelazimishwa sare ya kudungana bao 1-1 na Fountain Gate katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni hii Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma. Beki Nyenyezi Shaaban alianza kuifungia Mashujaa FC dakika ya 55, kabla ya Sadick Ramadhani ‘Immobile’ kuisawazishia Fountain Gate dakika ya 90’+4. Kwa matokeo hayo, Mashujaa FC inafikisha pointi 18, ingawa inabaki nafasi ya 11 ikiizidi pointi mbili Fountain Gate baada ya timu zote kucheza mechi 16 hadi sasa.

Duke Abuye, Bajaber waitwa Harambee Stars

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, ametangaza kikosi rasmi kitakachoshiriki mashindano ya FIFA Series 2026, huku majina ya nyota wanaokipiga katika Ligi Kuu ya NBC nchini Tanzania yakivutia macho ya wengi.  Katika orodha hiyo, kiungo fundi wa Young Africans, Duke Abuya, na mshambuliaji chipukizi wa Simba SC, Mohammed Bajaber, wamejumuishwa kufuatia viwango bora walivyoonyesha kwenye klabu zao msimu huu. Kikosi hicho kimechanganya uzoefu na damu changa, kikiongozwa na nahodha na mshambuliaji tegemeo Michael Olunga (Al Arabi). Safu ya ulinzi itaimarishwa na nyota kama Zak Vyner anayecheza nchini Uingereza (Wrexham) na Rooney Onyango (Sogndal), wakati safu ya kiungo ikiwa na mafundi kama Richard Odada na Manzur Suleiman anayecheza nchini Ufaransa (Stade De Reims). Uteuzi wa Bajaber na Abuya unathibitisha kukua kwa ushindani katika ligi ya Tanzania na jinsi inavyotoa nafasi kwa wachezaji kuonekana katika anga za kimataifa. ​Kikosi kamili kilichotajwa ni kama ifuatavyo: ​...