Mashujaa FC inayonolewa na Kocha Salum Mayanga haijashinda mchezo wowote kwenye michezo 5 ya karibuni ya Ligi Kuu bara. Kwa mwenendo huo wa kocha Mayanga, kwa vyovyote anaataharisha nafasi yake kwani muda wowote uongozi wa Mashujaa FC unaweza kusitisha mkataba wake. Mayanga anaheshimika sana kwakuwa amewahi kufundisha timu ya taifa, Taifa Stars, lakini pia amewahi kuzifundisha Mtibwa Sugar na Tanzania Prisons. Rekodi zake za hivi karibuni katika mechi 5 zilizopita ni kama ifuatavyo. 0-0 V Dodoma Jiji sare 0-0 V Coastal Union sare 6-0 V Yanga SC kufungwa 2-0 V Simba SC kufungwa 1-0 V KMC kufungwa, ni dalili mbaya sana kwa upande wake. Pia hawajafunga goli lolote kwenye michezo hiyo 5
MAMBO UWANJANI
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com