Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Ali Kamwe awananga wanaoibeza Yanga ikitoa sare

Machapisho ya hivi karibuni

Kelvin Nashoni ahusishwa na Simba

Klabu ya Simba SC imezidi kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao baada ya kufanikiwa kunasa saini ya kiungo fundi wa Pamba Jiji, Kelvin Nashon (25), ambaye amesaini mkataba wa miaka mitatu kuitumikia klabu hiyo ya Msimbazi. Nashon anatarajiwa kujiunga rasmi na wekundu wa Msimbazi mara baada ya msimu huu kukamilika, usajili ambao umeanza kuzua gumzo kubwa miongoni mwa wachambuzi wa soka kutokana na uwezo mkubwa wa kumiliki dimba na kuanzisha mashambulizi alionao nyota huyo. Hatua hii ya Simba ni mwendelezo wa mkakati wao wa kusajili damu changa na zenye vipaji ili kurejesha utawala wao kwenye soka la ndani na kimataifa, huku mashabiki wakimsubiri kwa hamu "Balaa" huyo jipya atakapoanza kuwasha moto katikati ya uwanja akiwa na jezi nyekundu na nyeupe. Simba walianza kumuania Nashoni tangia anaichezea Singida Black Stars hivyo kumsajili sasa hivi ni kama kutimiza ahadi yao ya kumsajili.

ASILI YA BINADAMU

Inaandikwa na Fikiri Salum DOMENI+ Eukaryota, Himaya- Animalis (wanyama) Fails: chordata (wanyama) au (wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni) Ngeli; Mamalia (wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao) Oda: primatei (wanyama wanaofanana kiasi na binadamu). Familia ya Hominoidea au (wanyama kama binadamu) Fakilia: hominidea (wako na mnasaba na binadamu). Nusufamilia: hominidea (wanaofanana sana na binadamu) Jenasi; Homo, Linnaeus, 1758 Spishi! H Sapiens, Linnaeus 1758 Numspishi: H S, Sapiens. Binadamu (pia mwanadamu) ni neno linalomaanisha mwana wa Adamu anayeaminiwa na dini ya Uyahudi, Ukristo na Uislamu kuwa ndiye mtu wa kwanza. BINADAMU KADIRI YA SAYANSI Kisayansi jina hilo linaweza kutumika kwa maana ya Homo Sapiens Ili kumtofautisha na viumbe wengine wa Jenasi Homo ambao wote walitoweka walau miaka 12,000 hivi iliyopita. Watu wote walioko leo hii ni spishi Ile Ile na tofauti zinazoonekana kati ya maumbile yao katika sehemu mbalimbali za dunia ni kidogo tu. Utafiti juu ya DNA umet...

Youssouph Dabo awaita mezani Yanga

Kocha wa zamani wa Azam FC na ya Tanzania na AS Vita ya DR Congo,Youssouph Dabo raia wa Senegal ameweka wazi nia yake ya kurejea kufundisha soka nchini Tanzania ikiwa tu itatokea klabu ambayo watakubaliana kwenye misingi ya ufanyaji kazi. Dabo ni kocha mwenye mbinu za kisasa na mwenye kupenda heshima na adabu kwa timu yake.

Rais wa Senegal amtetea Motsepe

Kwa mujibu wa Mwandishi Micky, amesema; Rais wa Senegal leo amewasiliana na Dkt. Patrice Motsepe na kumhakikishia kuwa anaungwa mkono kikamilifu katika uongozi wake na kazi anayoifanya ndani ya CAF. Licha ya Senegal kupeleka kesi hiyo katika Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo CAS, wameweka wazi kuwa Motsepe hakuhusika kwa namna yoyote katika mchakato wa kufanya uamuzi huo, wakisisitiza kuwa hukumu hiyo ilitolewa na chombo huru. Pia wameeleza kuwa Motsepe hakuwa na mchango wowote katika matokeo ya mwisho ya uamuzi huo.

Mashujaa FC yaikazia Azam FC

TIMU ya Azam FC imetoa sare ya 0-0 na wenyeji Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma. Kwa matokeo hayo, Azam FC inafikisha pointi 29 ikisalia nafasi ya pili nyuma ya mabingwa watetezi, Yanga SC wenye pointi 37 baada ya timu zote kucheza mechi 15. Kwa upande wao Mashujaa baada ya sare ya leo wanafikisha pointi 19 katika mchezo wa 17 ilisalia pia nafasi ya 11.

Achraf Hakim wa Morocco aukataa wa dezo

Achraf Hakimi baada ya CAF kutoa uamuzi wa kuwapa Morocco ubingwa wa AFCON 2025 baada ya kuwanyima Senegal taji kwa sababu ya Sababu za Kugomea Mchezo. “Kwa kweli, haileti Picha Nzuri. Tulishindwa mechi uwanjani na kila mtu anajua hivyo. Sielewi kwanini CAF waliamua kuibadilisha baadaye.” “Kuambiwa kuwa wewe ni mabingwa miezi kadhaa baadaye haimaanishi ulishinda mechi kwa kweli.”