Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Yanga wamkataa refa wa JS Kabylie

Machapisho ya hivi karibuni

Dodoma Jiji yaishusha Simba

Timu ya Dodoma Jiji imeendelea kutakata kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania bara inayodhaminiwa na benki ya NBC, baada ya usiku huu kuilaza TRA United mabao 3-0. Kwa matokeo hayo Dodoma Jiji iliyokuwa nyumbani, imeishusha Simba kwenye nafasi ya sita ikifikisha pointi 20 huku Simba ikiangulia nafasi ya saba na pointi 19. Mabao ya Dodoma Jiji yamefungwa na Faraji Kayanda dakika ya 15, Gadiel Michael dakika ya 40 na William Edgar dakika ya 55. Edgar amekuwa na mwendelezo mzuri wa kufunga mabao tangu alipoanza kufanya hivyo dhidi ya Yanga na kupelekea kupewa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Januari wa Ligi Kuu bara.

Kiungo mshambuliaji mpya Yanga alivyoanza mazoezi

Kiungo Mshambuliaji mpya wa Klabu ya Yanga, Buba Jammeh ameanza rasmi mazoezi na wenzake tayari kwa kuwatumikia Wananchi.

Samuel Eto' o awasili Dar

Rais wa Shirikisho la Soka nchini Cameroon, Samuel Eto’o, amewasili Dar es Salaam leo, tayari kwa mkutano wa kamati ya utendaji ya CAF, utakaofanyika kesho, Februari 13, 2026. Eto’o ni miongoni mwa wajumbe wa kamati hiyo ambao tayari wamekwishashawasili nchini kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika, kwa ajili ya mkutano huo unaolenga kujadili na kuimarisha maendeleo ya mpira wa miguu barani Afrika.

Afrika mashariki kupokwa uenyeji wa AFCON 2027 The Guardian Uingereza

Nimeona taarifa ya The Guardian ya England kuwa AFCON 2027 inaweza isifanyike sababu ya utayari wa nchi tatu za Afrika Mashariki. Lakini mara ya mwisho Rais wa CAF Dr Patrice Motsepe aliulizwa kuhusu swali hilo na majibu yake yalikuwa ni kuwa mashindano yatakuwepo na hakuna mpango wa kuondoa mashindano Afrika Mashariki, mkutano wa kesho wa CAF hapa utakuwa kwa ajili ya kuzungumza kuhusu maandalizi ya michuano hiyo. Dr. Motsepe yuko mstari wa mbele kuhakikisha kila kitu kitakuwa sawa sababu kazi yake ni kukuza mpira wa Afrika.

Yao Kouassi Attohoula mbioni kutua Azam FC msimu ujao

Uongozi wa Azam FC umeanza mazungumzo rasmi na Yanga SC ili kuchunguza uwezekano wa kumsajili Yao Kouassi Attohoula. Attohoula ni beki wa pembeni anayejulikana kwa uwezo wake wa kukaba na kushambulia kwa kiwango cha juu. Azam FC inakusudia kumchukua mwishoni mwa msimu huu, ama kwa mkopo wa muda mfupi au kwa usajili wa kudumu. Vyanzo vya ndani vinaarifu kuwa Azam FC inathamini sana uwezo wake. Uwepo wake kwenye mstari wa ulinzi unaweza kuleta tofauti kubwa kwa kikosi chao. Timu ya Azam FC inajiandaa kushindana na Yanga SC, Simba SC na Coastal Union msimu ujao. Kwa upande wa Yanga SC, Attohoula anachukuliwa kuwa mchezaji muhimu. Anachangia ulinzi thabiti na pia husaidia katika mashambulizi. Mazungumzo ya mwisho yanalenga kufanikisha masharti ya kifedha na mikataba. Hatimaye, Attohoula anaweza kuhamia Azam FC mwishoni mwa msimu.

SIMBA WAANZE UPYA MCHAKATO WA MABADILIKO

Na Prince Hoza Matua KWENYE hali ya kushangaza, Mwekezaji wa Klabu ya Simba, Mohamed Dewji kupitia ukurasa wake wa Instagram amehoji kwenye ukurasa wa Klabu ya Simba kuwa suala la Mabadiliko ndani ya Simba limefikia wapi? . Jambo ambalo limewashangaza wengi ni namna ambavyo Mwekezaji huyo amekuja kuuhoji uongozi wa Simba kuhusu suala la Mabadiliko ikiwa naye ni sehemu ya watu wanaohusika na kufanya Mabadiliko ndani ya Simba na huku ikiwa ni siku chache tangu zitoke tetesi za kwamba Bilionea huyo amejiondoa ndani ya Simba. . Mo Dewji anaahidi kuwaacha njiapanda mashabiki wa Klabu hiyo juu ya yeye kuwepo Simba na mbaya zaidi anahoji mitandaoni badala ya kuwafuata viongozi wenzake kwenye ofisi zao. Kwa vyovyote mchakato wa mabadiliko ya klabu ya Simba SC inaonekana kama ya kiini macho na badala yake klabu ya Simba wanatakiwa kuanza upya mchakato, Wekundu hao wa Msimbazi, wameshindwa kukamilisha mchakato wa uwekezaji na kilichobaki ni sinema tu. Kitendo cha MO Dewji kuhoji mchakato wa maba...