Machapisho

GUEDE AENDELEA KUCHEKA NA NYAVU

Picha
Yanga SC imeendelea kuchanja mbuga baada ya jioni ya leo kuilaza Mashujaa FC bao 1-0 katika uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma mchezo wa Ligi Kuu bara. Kwa ushindi huo Yanga inazidi kuongoza ligi ikiwa na alama 65 ikisaliwa mechi. 4 kukamilisha Ligi hiyo huku Mashujaa ikiwa kwenye hali mbaya. Bao pekee la Yanga limefungwa na Joseph Guede dakika ya 41 huku akiwa na mwendelezo mzuri wa kucheka na nyavu

KUELEKEA FAINALI LIGI YA MABINGWA, AHLY YAOMBA UFAFANUZI

Picha
Kuelekea Mchezo wa Fainali ya kwanza CAF Champions league kati ya Esperance na Aly Ahaly Uongozi Wa Aly Ahaly umeomba ufafanuzi CAF juu ya mambo muhimu Kwao kabla ya Mchezo huo. Aly Ahaly wamesema awatoitaji mwamuzi yeyote kutokea kaskazini mwa Africa kusimamaia mchezo huo. Lakini pia wameuliza juu ya utendaji kazi Wa VAR wanataka VAR dabithi. Lakini pia Wameomba kutafutiwa ulinzi imara Kwa ajili ya kulinda Timu Yao, viongozi na mashabiki wao ambao watasafiri Kutoka Misri Mpaka Tunisia. Lakini pia wanataka kujua kuhusu mgawanyo Wa Ticket amabzo zitauzwa ili kupata idadi sawa ya mashabiki. Mchezo utachezwa may 18 /5/2024 Tunisia na Fainali ya pili itachezwa May 25/5/2024 Misri

RULANI MOKWENA AKATAA OFA LUKUKI KUBAKI SUNDOWNS

Picha
Kocha mkuu wa Mamelodi Sundowns Rulani Mokwena anasema alikataa ofa nyingi za kuwania mikoba ya Wabrazil, kufuatia kukatishwa tamaa kwao katika Ligi ya Mabingwa wa CAF. "Nataka kuwa katika klabu hii. Ndio maana nilisaini mawasiliano ya miaka minne. Ingawa nilikuwa na klabu kubwa katika hadhi hiyo zinazotoa ofa na nilichagua kuwa nataka kubaki Sundowns. Sikuchagua hilo kwa sababu nilikuwa nilichagua ile ya kura, (kwa sababu) ya mazungumzo na familia yangu, na klabu, na familia ya Motsepe na pia na wachezaji," Mokwena aliwaambia waandishi wa habari. "Na hivyo nia yangu ni kuwa hapa na kujaribu kufanya niwezavyo kila siku ili kutoa kombe la Ligi ya Mabingwa." "Lakini kiukweli soka ni mchezo wa biashara na unaozingatia matokeo na sifanyi maamuzi hayo kuhusu kocha yupi abaki au aende kocha yupi lakini nikiwa hapa klabu itajua nitatoa. 150% na kama 150% haitoshi, kama leo, nitatoa 200% wakati ujao," Mokwena alisema.

ZUCHU ADAI HARMONIZE AMEBAKIA KUCHAMBANA TU

Picha
Mwimbaji wa Bongofleva, Zuchu amemtolewa uvivu Harmonize na kusema alichobakiza ni vichambo tu!. Kauli ya Zuchu inakuja baada ya Harmonize kuonekana kukejeli malalamiko ya mrembo huyo dhidi ya Diamond Platnumz. "Harmonize huna hit mjini, una kazi ya kuchambana tu...." ameandika Zuchu katika Insta Story na kuongeza. "Baba mzima kazi kudandia visivyokuhusu, mwanamke wako yupo busy kuomba nafasi kwa huyo anayejifanya nusu yako shenzi" - Zuchu.

YANGA NA MASHUJAA KESHO MTOTO HATUMWI DUKANI

Picha
Na Ikram Khamees. Kigoma Kesho ndio kesho katika uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma mabingwa watetezi wa Ligi Kuu bara inayodhamimiwa na benki ya NBC, Yanga SC watakapokuwa uwanjani dhidi ya wenyeji wao Mashujaa FC. Mchezo huo unatazamwa kuwa mkali na wa upinzani hasa kwakuwa kila timu inamahitaji yake, Yanga inayoongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 62 na inahitaji kushinda ili itangaze ubingwa mapema jambo ambalo litakuwa gumu kwa Mashujaa kuiona Yanga ikitwaa ubingwa mikononi kwao. Mashujaa nao wapo nafasi mbaya kwani sasa wanashika nafasi ya 14 wakiwa na pointi 23 hivyo wanataka kushinda ili wafikishe pointi 26 ambazo zitawashusha Geita Gold na Ihefu. Jioni ya leo Yanga wamefanya mazoezi kabambe kujiandaa na mchezo huo wa kesho

WAWILI TWIGA STARS KESHO KUKIWASHA UTURUKI

Picha
Mastaa wawili wa timu ya Taifa ya wanawake, Twiga Stars, Opah Clement pamoja na Diana Lucas kesho watashuka dimbani kwenye Ligi Kuu ya wanawake nchini Uturuki katika michezo ya raundi ya 30 ya ligi ambayo itatamatisha msimu wa 2023/2024 nchini humo. Timu za wachezaji hao wote wawili, Besiktas W ya Opah Clement na Amed SK W anayoichezea Diana Lucas zipo kwenye eneo salama ambalo linazihakikishia timu hizo kuwepo kwenye ligi kuu msimu ujao.

AZAM FC YAIFANYIA KITU MBAYA SIMBA

Picha
Taarifa zilizonifikia mezani ni kwamba Azam FC wanakaribia kukamilisha dili la kumsajili mlinzi wa Coastal Union, Lameck Lawi nyota wa timu ya taifa ya Tanzania. Inaelezwa kuwa Azam FC watalipa dau lisilopungua Tsh million 150 kuvunja mkataba wa nyota huyo huko Coastal Union. Nyota huyo alikuwa akiwindwa pia na Simba SC kwaajili ya kwenda kuboresha safu yao ya ulinzi pale Msimbazi