Machapisho

Kigogo Yanga amfagilia Karia

Picha
Mjumbe wa kamati ya utendaji kwenye klabu ya Yanga,Alex Ngai anasema kuwa amefurahishwa na maamuzi ya Rais wa TFF, Wallace Karia ya kufuta kanuni ya timu ya ugenini kufanya mazoezi siku moja kabla ya mchezo husika (dhidi ya timu mwenyeji) "Kwani hii kanuni si kuna timu moja tu ndiyo imeharibu?,ila nimefurahi kufutwa kwa hii kanuni"- Alex Ngai

Azam FC yapigwa faini

Picha
KLABU ya Azam imetozwa Faini ya Sh. Milioni 50, huku viongozi na wachezaji wake nao wakichukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu kwa makosa tofauti kwenye mchezo wa Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB. Azam Football Club Tanzania Football Federation CRDB Bank Plc Azam Sports TBC Taifa Precision Air

Vilabu vyamgombea kocha wa Mtibwa

Picha
Licha ya klabu ya Mtibwa Sugar kutokuwa tayari kumuachia kocha wao raia wa Kenya Yusuf Chippo imefahamika vipo Vilabu kadhaa vya ligi kuu ya NBC vimeonesha uhitaji wa kuipata huduma yake, Uongozi wa klab ya Mtibwa Sugar haupo tayari kumpoteza kocha huyo na unaamini ni mwalimu sahihi kuendelea kuwepo hapo kwenye project yao wa kuwarejesha ligi kuu msimu wa 2027/28, Bado mpaka muda huu haijafahamika kama Kocha huyo atasalia na Mtibwa Sugar ama ataondoka,

Kitambala kuondoka Azam kisa mshahara

Picha
Klabu ya Azam imeshindwa kulipa dola 150k ili kuendelea kumtumia mshambuliaji wao Japhet Kitambala ambaye alijiunga na Azam fc kwa mkopo akitokea Maniema. Klabu ya Maniema imeiambia uongozi wa Azam ili mshambuliaji huyo aendelee kusalia Chamazi wanatakiwa kulipa dola 150k kitu ambacho Azam wamekataa. Hivyo kufanya dili hilo kushindikana, lakini Singida Black Stars wamejaribu kuwasiliana na kambi ya Kitambala kuona namna ya kumpata mshambuliaji huyo lakini bado kambi ya mchezaji na klabu ya Maniema haijatoa majibu yenye muelekeo. Ikumbukwe kuwa Kitambala haukuwa usajili wa moja kwa moja ulikuwa ni wa mkopo ili kama klabu itaridhika na huduma ya mshambuliaji huyo wafanye biashara ya moja kwa moja. Lakini mpaka sasa matajiri wa Azam hawajaridhishwa na huduma ya mchezaji huyo ambae alijiunga na Azam dirisha kubwa la msimu uliopita.

Mrithi wa Pedro Yanga huyu hapa

Picha
KLABU ya Yanga imemtambulisha Manqoba Brilliant Ferrimant Mngqithi (55) kutoka Golden Arrows ya kwao, Afrika Kusini kuwa kocha wake mpya Mkuu akichukua nafas ya Mreno, Pedro Valdemar Soares Gonçalves aliyeondolewa Mei mwaka huu

Kagame Cup kulamba milioni 79

Picha
Klabu ya Al Hilal ya nchini Sudan imechukua hatua kubwa na ya kihistoria baada ya kujitolea kudhamini michuano ya Kombe la CECAFA Kagame Cup 2026 kwa kutoa kiasi cha dola za Kimarekani laki moja ($100,000), ambazo ni zaidi ya Shilingi Milioni 263 za Kitanzania. Kwa mujibu wa taarifa za ndani, miamba hiyo ya soka ya Sudan imekubali kutoa mkono huo wa heri ili kufanikisha uendeshaji wa mashindano hayo yanayotarajiwa kurindima hivi karibuni nchini Rwanda. ​Lengo kuu la Al Hilal kuingia kama mdhamini mkuu ni kuyatumia mashindano hayo adhimu ya ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kama sehemu ya maandalizi yao ya msimu mpya (Pre-Season). Klabu hiyo inataka kupima makali ya kikosi chake dhidi ya timu pinzani ili kujiweka sawa kuelekea mashindano ya ndani na yale ya kimataifa, huku ikiongeza chachu na mvuto wa kiushindani katika michuano hiyo. ​Kufuatia udhamini huo mnono, mchanganuo wa zawadi zitakazotolewa kwa timu zitakazofanya vizuri umebadilika na kuwa wa kuvutia zaidi. Bingwa mpya wa mich...

Anicet Oura hatihati kubaki Simba

Picha
Kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Anicet Oura, ameingia kwenye rada za klabu tatu za Ulaya kufuatia kiwango bora alichoonyesha tangu ajiunge na Wekundu wa Msimbazi mwezi Januari mwaka huu. Taarifa zinaeleza kuwa Bursaspor (Uturuki), Víkingur Reykjavík (Iceland) na DAC 1904 Dunajská Streda (Slovakia) zinafuatilia kwa karibu hali ya nyota huyo wa Ivory Coast. Bursaspor inaongoza mbio za kumsajili Oura na inatajwa kuwa tayari kuwasilisha ofa ya Euro 250,000. Hata hivyo, Kocha Steve Barker amesisitiza kuwa anahitaji kubaki na kiungo huyo kwa ajili ya msimu ujao. Kwa tafsiri ndogo ni ngumu Simba Sc kumuuza Anicet Oura.