Dr Remmy Ongalla wa Ochestra Matimila na Bwammy Walomuna wa Ochestra Mangelepa Viongozi wa bendi za Muziki huku watoto wao wakiwa miamba ya Soka. Kali Ongala (jina kamili Kalimangonga Sam Daniel Ongallah Rampling) ni mwanasoka wa zamani na kocha wa mpira wa miguu kutoka Tanzania. Ni mtoto wa mwanamuziki mashuhuri wa Tanzania, marehemu Remmy Ongala, alizaliwa tarehe 31 Agosti 1979 jijini London, Uingereza. Licha ya kuzaliwa Uingereza, alikulia na kupata malezi yake jijini Dar es Salaam, Tanzania, ambapo alianza kupata hamu ya michezo na soka tangu utotoni. Safari yake ya soka ilianza rasmi mwaka 1999 alipojijiunga na Young Africans SC (Yanga) kutoka Bajaro FC, akijitengenezea sifa kama kiungo mshambuliaji mwenye ufundi mkubwa. Baada ya mafanikio yake nchini Tanzania, alifanya majaribio ya kucheza soka nchini Uingereza na Marekani kabla ya kupata mikataba ya kucheza nchini Uswidi, akichezea klabu za FC Väsby United na GIF Sundsvall kati ya mwaka 2007 na 2011. Baada ya kustaafu kutoka sok...