Machapisho

Aucho akaribia kutua Gor Mahia

Picha
Nahodha wa Uganda Cranes, Khalid Aucho, anatajwa kuwaniwa na klabu za Gor Mahia na Tusker FC kwa ajili ya usajili wake, kwa mujibu wa taarifa zinazoripotiwa nchini Uganda. Kiungo huyo mwenye uzoefu mkubwa kwa sasa anakipiga katika kikosi cha Singida Black Stars, huku klabu hizo mbili za Kenya zikifuatilia kwa karibu uwezekano wa kumpata katika dirisha hili la usajili

Simba yaibomoa Stellenbosch

Picha
Klabu ya Simba SC wapo kwenye mazungumzo ya kumchukua Ibraheem Jabaar Na Tayari wameweka Ofa Nono Mezani kwa ajili ya Midfielder hii hatari kutoka Stellenbosch FC Ya Afrika Kusini Ibraheem anaweza kucheza maeneo matatu ya mbele, number 8, number 10 na winga zote mbili kushoto au kulia. Kwa taarifa nilizonazo ni kwamba Ibraheem Jabaar ni pendekezo la kocha Steve Baker ambae Alimsajili akiwa kama kocha wa Stellenbosch FC...

Simba hawalazi damu

Picha
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, ameweka wazi kuwa kikosi chao hakina muda wa kupoteza ambapo mara baada ya ushindi mnono dhidi ya Mtibwa Sugar, timu hiyo ilisafiri usiku huohuo kutoka Morogoro kurejea Dar es Salaam kwa ajili ya kuingia kambini moja kwa moja. Simba sasa inaelekeza nguvu zote kwenye mchezo wa raundi ya 29 wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Singida Black Stars, mtanange utakaopigwa Jijini Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo kuanzia saa 10:00 jioni. ​Ahmed amefunguka kuwa kwa sasa klabu hiyo imeweka pembeni mpango wa kucheza soka la kuvutia au kuonyesha mbwembwe uwanjani, bali nguvu zote zimeelekezwa kwenye kusaka alama tatu muhimu pekee Aliongeza kuwa mbinu hiyo ya kucheza soka la moja kwa moja (direct football) ilianza kutumika tangu raundi ya 25 kutokana na mazingira magumu ya viwanja vya mikoani kama Jamhuri, pamoja na ukweli kwamba wanakutana na timu zinazopambana kufa na kupona kujinasua kutoka janga la kushuka daraja. ​Kuelekea mc...

Yanga yaikandika Azam FC 3-0

Picha
MABINGWA watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara nuliofanyika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar jioni ya leo. Mabao ya Yanga yamefunwa na beki Ibrahim Hamad Abdullah ‘Bacca’ dakika ya 41, mshambuliaji Laurindo Dilson Maria AurĂ©lio ‘Depu’ kutoka Angola dakika ya 73 na kiungo Muivory Coast, Peodoh Pacome Zouzoua dakika ya 81. Kwa ushindi huo, Yanga SC wanafikisha pointi 69 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi mbili ya watani wao, Simba baada ya timu hizo zote kucheza mechi 28 kuelekea mechi mbili za kukamilisha Kwa upande wao Azam FC baada ya kupoteza mchezo huo wanabaki na pointi zao 58 wakibaki pia katika nafasi ya tatu mbele ya Singida Black Stars yenye pointi 50 kufuatia timu hizo nazo kucheza mechi 28.

Simba yailowesha Mtibwa Sugar

Picha
TIMU ya Simba SC imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji, Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro. Mabao ya Simba SC yamefungwa na beki Rushine De Reuck kutoka Afrika Kusini kwa penalti dakika ya tisa, mshambuliaji mzawa, Suleiman Abdallah Mwalimu dakika ya 77 na winga Muivory Coast, Alain Anicet Oura dakika ya 90 Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 67, ingawa inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi mbili na mabingwa watetezi, Yanga SC – wakati Mtibwa Sugar inabaki na pointi zake 27 na kushukia nafasi ya 14 kwenye ligi ya timu 16 kufuatia timu zote kucheza mechi 28. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja moja kwa moja na nyingine mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani n...

Yanga wanamrudisha tena Aziz Ki

Picha
Klabu ya Young Africans SC imetuma ofa rasmi ya USD 350K (Tshs Milioni 920) kwenda Al Ittihad SC ya Libya ili kupata saini na huduma ya kiungo mshambuliaji Stephane Aziz Ki (30). KI Aziz amekubali kuitumikia Young Africans SC kwa mara nyingine tena baada ya kuondoka klabuni hapo na kujiunga na Wydad AC na baadae kusajiliwa na Al Ittihad SC ya Libya na klabu ya Young Africans inapambania hili ili kupata saini yake kwa wakati.

Makonda amteua Leodgal Tenga kamati ya AFCON

Picha
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Christian Makonda amemteua Nahodha wa zamani wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Leodegar Chilla Tenga kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ndani ya Maandalizi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 ambazo Tanzania inaandaa kwa ushirikianona majirani, Kenya na Uganda.