Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Adam Salamba aigomea Coastal Union kisa fedha zake

Machapisho ya hivi karibuni

Senegal wakaidi kurudisha kombe la AFCON, CAF

Senegal wamewasilisha kombe lao la AFCON mbele ya mashabiki 80,000 katika dimba la Stade de France nchini France, wakipuuza uamuzi wa CAF wa kuwanyang’anya ubingwa wa 2026!

Boubacar Keita kutua Simba

Klabu ya Simba imeanza mchakato wa kuwania saini ya kiungo wa kati Boubacar Keita (24) anaecheza katika klabu ya Djoliba AC ya nchini Mali. Simba wanataka kumuongeza nyota huyo mapema pale dirisha kubwa la usajili litakapofunguliwa .

Usajili wa matawi Simba SC sasa kijigitali

Klabu ya Simba SC inaendelea kupiga hatua kubwa katika mchakato wake wa mabadiliko ya kiutendaji baada ya kutangaza kuwa zoezi la usajili wa matawi kwa mfumo wa kidijitali sasa limefikia 81%. Hatua hii ni sehemu ya mkakati wa klabu hiyo ya Msimbazi kuhakikisha inapata kanzidata (database) sahihi ya wanachama na mashabiki wake nchi nzima, jambo litakalosaidia kurahisisha mawasiliano, ukusanyaji wa mapato, na utambuzi wa wanachama hai. ​Mchakato huu wa kidijitali unatazamwa kama mfano wa kuigwa kwa klabu za soka nchini Tanzania katika kuachana na mifumo ya kizamani ya makaratasi na kuelekea kwenye weledi wa kisasa. Kwa kufikia hatua hii kubwa, Simba inajiweka kwenye nafasi nzuri ya kukamilisha zoezi hilo hivi karibuni, jambo litakalowawezesha wanachama kupata huduma mbalimbali za klabu kwa urahisi zaidi kupitia mifumo ya kielektroniki, huku uongozi ukipata picha halisi ya nguvu ya mashabiki wake kulingana na maeneo walipo.

Muasisi wa Singida Black Stars afariki dunia

ALIYEKUWA Mwenyekiti na Mwasisi wa Singida Black Stars, Yusuph Mwandami amefariki dunia jana baada ya gari alilokuwa wakisafiria kusombwa na maji katika Mto Mang’onyi, Singida. Ajali hiyo imechukua pia na uhai wa mke wa Mwandami, Luluwa Suleimani na mtoto wao, Sabri Yusuph pamoja na dereva wao ambao wote walisombwa na maji katika Mto Mang’onyi. Taarifa zinasema hadi jana kufikia Machi 27, 2026, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Singida lilikuwa limefanikiwa kuopoa miili ya Yusuph Mwandami na mke wake, Luluwa Suleiman pekee. Ajali hiyo ilitokea wakati familia hiyo ikijaribu kuvuka mto huo uliokuwa na maji mengi na tukio hilo limeacha simanzi mkoani Singida kutokana na mchango wake katika uongozi na sekta ya madini. Pamoja na Uenyekiti wa Singida Black Stars, Mwandami pia alikuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida na mmiliki wa mgodi wa dhahabu wilayani Ikungi. Klabu ya Singida Black Stars imetoa pole kufuatia msiba huo mzito. “Tumepokea kwa m...

MTU MWEUSI NA OIDUVAI GORGE

Inaandikwa na Fikiri Salum BONDE la Oltupai (maarufu kwa Kiingereza kama Olduvai Gorge) ni eneo la Kiakiojia linalopatikana katika mkoa wa Arusha nchini Tanzania ambalo ni kati ya yale muhimu zaidi duniani. Bonde hilo lipo katika hifadhi ya Ngorongoro na karibu na Ile mbuga ya Serengeti, ni mahari ambapo Zamadamu, viumbe wa kale waliokaribiana na mwili wa binadamu, waliishi tangu miaka milioni 2 hivi iliyopita. Kwa kuwa watu wanadhaniwa kutokana nao, eneo hilo pengine limeitwa kwa Kiingereza Craile of manking, kitovu cha binadamu, ambako wameishi katika eneo hilo kwa walau miaka 17, 000 mfululizo. Katika eneo hili Mwanaakiolojia Mary Leakey ndipo alipogundua fuvu la kichwa la kiumbe wa kale wa jamii hiyo. Pamoja na mabaki ya mifupa ya Tembo, Kongoo wenye pembe kubwa na Mbuni, tarehe 17 Julia 1959 aligundua mabaki ya fuvu la kichwa la Pararthropus Boisei (pamoja na mumewe alimwita kwanza zinjanthropus) ambalo lipo katika makumbusho ya Dar es Salaam. Huyo anadhaniwa kuwa mtangulizi wa bi...

Gamondi aweka rekodi Taifa Stars

Tangu ateuliwe kuifundisha Tanzania (Taifa Stars), Kocha wa timu ya taifa ya Tanzania, Miguel Gamondi hajashinda mechi yoyote akiwa na timu hiyo. FIFA SERIES 2026 RWANDA FT: Tanzania 0-1 Liechtenstein AFCON 2025 MOROCCO FT: Morocco 1-0 Tanzania FT: Tunisia 1-1 Tanzania FT:Uganda 1-1 Tanzania FT: Nigeria 2-1 Tanzania MECHI YA KIMATAIFA YA KIRAFIKI Kuwait 4-3 Tanzania NEXT : FIFA SERIES 2026 Macau vs Tanzania Hata hivyo Gamondi amekuwa kocha wa kwanza nchini kuiwezesha Stars kufika hatua ya 16 bora ya kombe la mataifa Afrika, AFCON 2025 zilizofanyika Morocco huku timu ya Morocco ikitawazwa mabingwa.