Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Mokwena amfuata Aziz Ki Al Ittihad

Machapisho ya hivi karibuni

Pamba Jiji yaingia mchecheto mechi na Simba

Taarifa za ndani kutoka jijini Mwanza ilipo kambi ya timu ya Pamba Jiji FC inayoshiriki Ligi Kuu bara, inasema kwamba uongozi wa timu hiyo umeingia mchecheto kuelekea mchezo wake dhidi ya Simba SC keshokutwa. Mchezo huo utakaopigwa uwanja wa CCM Kirumba, uongozi wa timu hiyo umedai tangu timu yao ipande Ligi Kuu bara hawajawahi kuifunga Simba hivyo itakuwa ngumu kupata matokeo keshokutwa. Hofu hiyo imekuja sasa kutokana na Simba kubadilika na kucheza soka la kuvutia kiasi kwamba hata wapinzani wao wakuu Yanga kurudi nyuma walipokutana nao hivi karibuni. Lakini hata hivyo uongozi huo umewaambka mashabiki wa timu hiyo kutokana tamaa kwani lolote linaweza kutokea na wanaweza kuibuka na ushindi.

Majeruhi yaiandama Yanga, Depu naye ndani

Klabu ya Young Africans imetoa ripoti rasmi ya kitabibu inayowahusu wachezaji wake wanne ambao wameingia kwenye mkumbo wa majeraha, jambo linalozidi kutoa mtihani kwa benchi la ufundi la kocha Pedro Gonçalves. ​Orodha ya Majeruhi na Muda wa Kukaa Nje: ​Ibrahim Abdullah (Bacca): Beki huyu kisiki amepata jeraha la nyonga. Taarifa za kitabibu zinaeleza kuwa atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa wiki tatu. ​Laurindo Dilson (Depu): Mshambuliaji huyu amepata majeraha ya nyama za paja na atalazimika kukaa nje kwa kipindi cha wiki mbili. ​Chadrack Boka: Beki wa kushoto amepata jeraha la enka (foot ankle) ya mguu wa kushoto, jambo litakalomuweka nje kwa wiki mbili. ​Edmund John: Amepata jeraha la bega na atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa wiki mbili. ​Hali hii inaongeza presha kwenye kikosi cha Yanga ambacho tayari kinapambana na mapengo ya Dickson Job na Clement Mzize, huku ikilazimisha mabadiliko makubwa katika safu ya ulinzi na ushambuliaji kuelekea mechi zijazo za Ligi Kuu ya NBC.

Sowah ang' ara mchangani

Mshambuliaji wa Klabu ya Simba SC, Jonathan Sowah ameonekana akicheza ndondo mtaani nchini kwao Ghana wiki hii ikiwa ni siku chache tangu zilipotoka taarifa za kutaka kuichukulia hatua za kisheria Klabu yake ya Simba kwa kutojali kuhusu kipaji chake. . Kwa mjibu wa taarifa za ndani zinaeleza Mshambuliaji huyo pamoja na Wakala wake wameuambia Klabu hiyo wamvunjie mkataba Mshambuliaji huyo kwa kumlipa pesa zake za kuvunjia mkataba ili apate timu ya kwenda kucheza ili alinde kipaji chake.

HISTORIA YA WAARABU -2

Inaandikwa na Fikiri Salum Ilipoishia Nabii Ismail hakuwa Mwarabu lakini baada ya kukaa hapo Makkah na kutifuka chemchem ya Zamzam, walikuja Waarabu wa Kiyemeni wa kabila la Qurhum na walipoona maji hapo waliomba kubakia hapo na ndipo Nabii Ismail akakulia kwenye kabila hilo na kujifunza Kiarabu na kuoa katika kabila hilo. Endelea MASKANI YA MWARABU YA ASILI Waarabu kama tulivyoeleza hapo nyuma mwanzo walikuwa wakiishi Yemen lakini baadaye wakaanza kutawanyika kwenye sehemu nyinginezo za Bara Arabu, na Kwa kuwa wengi wao walikuwa wakiishi maisha ya kibedui ya kusafiri kutoka mahali pamoja kwenda kwingine kutafuta chakula na maji kwa nafsi zao na wanyama wao. Waliweza kuenea sehemu zote za Bara Arabu na kufika Shamu na Iraq na Misri na Afrika mashariki na Afrika Kaskazini, kutawanyika huku kulizidi kwa kasi baada ya kuvunjika bwawa lao kubwa lililokuwa Maarib huko Yemen lililokuwa likilimbika maji mengi kwa ajili ya ukulima na mabustani yao na malisho ya wanyama wao. Na mtawanyo mkubwa ...

Yanga yawasili Arusha kuivaa TRA

Vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara wamewasili Arusha kwaajili ya kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya TRA United. Yanga na TRA zinatazamiwa kukutana Jumatano ya keshokutwa katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid ambao juzi ulishindwa kutumika wakati TRA ikitaka kucheza na Simba.

Depu mchezaji bora Ligi Kuu bara mwezi Februari

MSHAMBULIAJI wa Kimataifa wa Angola, Laurindo Dilson Maria Aurélio ‘Depu’ wa Yanga SC amechaguliwa Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara kwa mwezi Februari 2026, wakati Steven Robert Barker raia wa Afrika Kusini amechaguliwa Kocha Bora wa mwezi huo.