Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Simba kuachana na Sowah

Machapisho ya hivi karibuni

Mbeya City ya Mexime hoi kwa Fountain Gate

TIMU ya Fountain Gate imepata ushindi wa ugenini wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji, Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Bao pekee la Fountain Gate lililoilaza Mbeya City nyumbani limefungwa na winga chipukizi wa umri wa miaka 19, Sadick Said Ramadhan dakika ya 79. Kwa ushindi huo, Fountain Gate inafikisha pointi 15 katika mchezo wa 15 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya 13, wakati Mbeya City inabaki na pointi zake 13 za mechi 15 pia nafasi ya 14 kwenye Ligi ya timu 16. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.

Kumwembe amkosoa kocha wa Yanga

Mchambuzi nguli wa soka nchini, Edo Kumwembe Edo Kumwembe ametoa tathmini yake juu ya mwenendo wa kocha mkuu wa Young Africans, Pedro Gonçalves, akibainisha kuwa kocha huyo amekuwa akipitia milima na mabonde tangu awasili klabuni hapo. Kumwembe ameeleza kuwa uteuzi wa viungo wanne wenye sifa zinazofanana uwanjani umekuwa ukirudisha nyuma makali ya timu hiyo katika kushambulia. ​Katika uchambuzi wake, Edo Kumwembe {@edokumwembe } amefafanua mbinu hizo kwa kusema: ​"Kocha Pedro Gonçalves amekuwa na milima na mabonde tangu awasili, kwa kucheza na viungo wanne wanaofanana, Duke Abuya, Mudathir, Damaro na Maxi Nzingeli aliyekuwa anashinda katikati ilikuwa kama vile anacheza na 'handbrake'. Wazungu huwa wanasema hivyo kwa kocha ambaye anaangalia zaidi namna ya kujihami kuliko kupeleka mashambuliaji mbele."

Mwbomu ya Iran yamkimbiza Ronaldo Saudi Arabia

Wakati mvutano kati ya Israel, Marekani na Iran ukiendelea huko Mashariki ya Kati, mshambuliaji wa zamani wa Manchester United na Real Madrid, Cristiano Ronaldo ameondoka kutoka Riyadh, Saudi Arabia na kuelekea, Hispania huku wafuasi wake na mashabiki duniani kote wakionesha wasiwasi kuhusu usalama wa nyota huyo na familia yake. Mshindi huyo mara tano wa tuzo ya Ballon d'Or aliruka kutoka Jijini Riyadh alipokuwa akiishi tangu alipojiunga na klabu ya Al-Nassr FC kwenda Madrid, Uhispania akitumia ndege yake binafsi usiku wa manane wakati Jiji hilo likikabiliwa na mashambulizi ya anga huku ndege zisizo na rubani zikiripotiwa kulenga ubalozi wa Marekani Nchini humo. Kwa mujibu wa taarifa za ufuatiliaji wa safari za ndege, ndege binafsi ya Ronaldo aina ya Bombardier Global Express 6500 iliondoka Riyadh majira ya saa 8:00 usiku na kuwasili Madrid majira ya saa 1:00 asubuhi, ikipitia anga la Misri na Bahari ya Mediterania kabla ya kutua Hispania.

HISTORIA YA MTUME MUHAMMAD NA UISLAMU-2

Inaandikwa na Fikiri Salum Ilipoishia jana. KITENDO chenyewe alichokiazimia kuifanya mara mbili zote hizo na mwenyezi Mungu akamfadhi nacho ni kutaka kukesha katika ngoma za Arusi mbili za marafiki zake waliooa katika mji wa Makkah. Endelea. Lakini Mungu alimpa usingizi mkubwa katika masiku yote hayo mawili hata hakuweza kufumbua jicho, wala kunyanyua miguu kwenda mahari, hajapata kuudhuria hata mara moja katika ibada za kuabudu sanamu wala kula chakula kilichochinjwa kwa ajili yao, moyo wake ulichukizwa na hayo na mambo mengine yaliyo mabaya. Tangu udogo wake mtume alipndokea na sifa nzuri ambazo hapana hata mtu mmoja katika hirimu zake aliyekuwa nazo zote, kila sifa zinazohesabiwa kuwa ni njema na ndizo alizokuwa nazo tangu utoto wake. Mkewe Aisha alipoombwa kutaja kidogo sifa za mtume, alisema hivi, "sifa zake ni zile sifa nzuri zinazosofiwa na kurani na katika kurani zimetajwa chungu ya sifa zilizo nzuri. Mtume mara nyingi alikuwa akisema sikupata kufanya hata siku moja yale m...

Azam FC yanusurika kichapo mbele ya Pamba Jiji

TIMU ya Azam FC imelazimisha sare ya kufungana mabao 2-2 na wenyeji, Pamba Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza. Ni Pamba Jiji waliouanza vyema mchezo huo na kupata mabao mawili ya uongozi kupitia kwa kiungo wa Azam FC, Himid Mao Mkami aliyejifunga dakika ya 45 na mshambuliaji wake, Mganda John Ben Nakibinge dakika ya 48 . Lakini Azam FC ikazinduka kipindi cha pili na kusawazisha mabao yote kupitia kwa mshambuliaji Mkongo, Jean-Jacques Ngita dakika ya 56 na kiungo Feisal Salum Abdallah kwa penalti dakika ya 59, kabla ya kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 62. Kwa matokeo hayo, Azam FC inafikisha pointi 23 katika mchezo wa 11, ingawa inabaki nafasi ya tano ikizidiwa pointi moja na Pamba Jiji FC ambayo pia imecheza mechi nne zaidi.

Uwanja wa Mkapa wafungwa tena

Serikali imetangaza rasmi kuufunga Uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia Machi 2026 kwa ajili ya awamu ya mwisho ya ukarabati mkubwa kuelekea AFCON 2027. Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amethibitisha kuwa ukarabati huo utachukua kati ya miezi 6 hadi mwaka mmoja, ukilenga zaidi kuboresha: Eneo la kuchezea (Pitch). Miundombinu muhimu ya uwanja. Nini kitatokea? Hakutakuwa na mechi yoyote itakayochezwa pindi kazi itakapoanza. Timu zote zitalazimika kutafuta viwanja mbadala kwa mechi za ndani na kimataifa. Huu ni uamuzi muhimu kuhakikisha Tanzania inatoa burudani ya kiwango cha dunia mwaka 2027