Machapisho

Minziro atambulishwa Fountain Gate

Picha
KLABU ya Fountain Gate imemtambulisha Fredy Felix Minziro kuwa kocha wake mpya Mkuu. Minziro alikuwa akiinoa timu ya Bigman inayoshiriki Championship na anasifika kwa kuzipandisha timu Ligi Kuu bara na pia kuzibakisha kwenye ligi hiyo.

Makonda asimamisha uchaguzi TOC

Picha
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amesimamisha uchaguzi na uongozi wa kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) kufuatia malalamiko ya wagombea kuenguliwa bila haki na kukosekana kwa uwazi. Waziri amesisitiza kuwa uamuzi huo umefanyika kwa mujibu wa Sheria ya Baraza la Michezo la Taifa Sura ya 49 ili kulinda utawala wa sheria na maslahi ya umma. Ili kuziba pengo la uongozi, ameteua Kamati ya Muda itakayoongozwa na Ismail Aden Rage (Mwenyekiti) na Dkt. Steven Mabagala (Makamu Mwenyekiti). Aidha, kutaundwa kamati ya uchunguzi itakayoshirikisha TAKUKURU na Polisi ili kuchunguza tuhuma za mchakato wa uchaguzi huo na kuchukua hatua stahiki. Waziri amewataka wadau kuwa watulivu wakati Serikali ikirejesha uadilifu ili kuhakikisha Tanzania inafanya vizuri katika michezo ya kimataifa.

Singida Black Stars nao kama Simba

Picha
Tayari Meneja Mkuu wa Singida Black Stars, Papy Kimoto na Msaidizi wake Kapiten Ngoyi wameanza majukumu yao baada ya kuwasili salama . Singida Black Stars kama Simba SC ambao nao waliwahi kuajiri kocha mkuu lakini wakamuita Meneja Mkuu.

Tshisekedi awapiga mkwara wachezaji DR Congo

Picha
Baada ya mgogoro uliotokea hivi karibuni kati ya wachezaji wa timu ya taifa ya DR Congo na vilabu vyao, kutokana na kuchelewa kurejea baada ya kusherehekea kufuzu Kombe la Dunia. Rais wa nchi hiyo, Félix Tshisekedi, ameingilia kati suala hilo na kutoa ujumbe mzito kwa wachezaji: "Faini zote… zipelekeni kwa shirikisho, sisi tutalipa. Hivyo basi, msibebe mzigo huo.” — maneno ya rais Felix Kiufupi rais amewahakikishia wachezaji kuwa faini au adhabu yoyote ya kifedha watakayotozwa na vilabu vyao, itagharamiwa na Shirikisho la Soka la Congo. Lakini pia amewataka wasiwe na wasiwasi na badala yake waweke nguvu zao zote katika kuiwakilisha nchi yao kwa kiwango bora zaidi. Huu ni uthibitisho wa thamani ya mafanikio yao na furaha waliyoileta kwa taifa zima.

JKT Tanzania, Mashujaa FC zatangulia robo fainali kombe la CRDB

Picha
TIMU za Ligi Kuu, JKT Tanzania na Mashujaa FC zimefanikiwa kwenda Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) baada ya kuzitoa timu za Ligi ya Championship leo. JKT Tanzania imeitupa nje Mbuni FC ya Arusha kwa kuichapa 3-0, mabao ya Edward Songo na Anuar Kilemile Uwanja wa Meja Jenerali Charles Isamuhyo, Mbweni, Dar es Salaam. Nayo Mashujaa FC imeitoa Geita Gold kwa penalti 4-2 kufuatia sare ya bila mabao Uwanja wa Sekondari ya Nyankumbu, Geita.

Singida Black Stars wamng' oa Chobwedo

Picha
Klabu ya Singida Black Stars,inapambana kumsaini Kiungo wa TRA,Ramadhan Chobwedo. Awali Singida walikubaliana kila kitu na Chobwedo na usiku wa Tarehe 22/3/2026 baada ya mechi ya TRA na Simba kumalizika Singida walimpa ofa ya mkataba wa miaka mitatu na Tsh 120m Kama (sign on fee) Ila hadi leo Chobwedo anachenga (hataki kusaini mkataba huo). Viongozi wa Singida wanapambana nyota huyo asabını ila kila siku anaingilia kulia anatokea kushoto.

Pedro Goncalves awakomalia wachezaji wa Yanga kushinda kila mechi

Picha
Kocha Mkuu wa Yanga, Pedro Gonçalves, amesema wachezaji wake wanapaswa kujituma kikamilifu bila kujali wanakutana na timu gani, iwe Al Ahly SC au TMA, katika kuelekea mchezo wa Kombe la Shirikisho la CRDB. Akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mchezo huo wa kesho, Gonçalves amesema Yanga inaelekea kwenye mashindano yenye hadhi kubwa, hivyo wanahitaji kushinda ili kufuzu hatua inayofuata. Amesema wachezaji wanapaswa kucheza kwa bidii na umakini, akibainisha kuwa kushindwa kuzingatia hilo kunaweza kuwaweka katika hali ngumu, kwani wapinzani wao hawana cha kupoteza. “Tunajua tukipoteza kesho tutakuwa tumepoteza nafasi ya ubingwa, lakini tukitekeleza kila jambo ipasavyo tuna nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa tena,” amesema Gonçalves. Aidha, amesema TMA wanafahamu kuwa mchezo huo ni jukwaa muhimu la kuonesha uwezo wao, hivyo Yanga haitawabeza wapinzani wao licha ya kwamba waliitoa timu ya Ligi Kuu. Kwa upande wake, mchezaji wa Yanga, Allan Okello, amesema wapinzani wao hawana cha kupotez...