Machapisho

Simba SC weka mbali na watoto

Picha
Wekundu wa Msimbazi, Simba SC unaweza kusema weka mbali na watoto, baada ya usiku huu kuifunga Coastal Union ya Yanga mabao 2-0 mchezo wa Ligi Kuu bara uwanja wa Meja Isamuyo Mbweni jijini Dar es Salaam. Mabao yote ya Simba SC yamepatikana kipindi cha kwanza yakiwekwa kimiani na kiungo mshambuliaji Seleman Mwalimu dakika ya 25 goli ambalo linaonekana kuwa bora wakati bao lingine limefungwa na beki wa kati Ismail Toure dakika ya 45. Kwa matokeo hayo Simba SC sasa imefikisha pointi 34 ikiwa imecheza mechi 15 ikiwashusha Azam FC kwenye nafasi ya pili huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi.

Magori, Mangungu awaongoza Simba SC kumzika mwanachama wao

Picha
Viongozi mbalimbali wa klabu wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi, Crescentius Magori wameshiriki mazishi ya mwanachama mkongwe, Emmanuel Macha Nderimo ‘Babu Macha’ yaliyofanyika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Damaro aibwaga Simba SC, TFF

Picha
TFF imeitupa kesi ya Simba SC dhidi ya Mohamedi Damaro na Yanga SC kama ilivyotarajiwa, baada ya kusikiliza kesi hiyo upande mmoja wa Simba SC pekee. Hapa chini nimekuwekea hoja za Simba katika kesi hiyo ambayo inategemewa kupelekwa CAS:- HOJA ZA SIMBA 1. Kanuni za Ligi kuu zinamtambua mchezaji wa Kigeni na Mzawa, hakuna lugha nyingine. Mgeni ni aliyetoka nje ya Tanzania na Mzawa ni Mchezaji wa Kuzaliwa. Damaro anatokea wapi hapo maana hajazaliwa Tanzania. 2. ⁠Kupewa uraia kwa naturalization hakumpi mtu haki zote kama Mzawa, mf. Raia kwa naturalization hawez kuchaguliwa kuwa Rais wa nchi. Je, kwenye mpira kuna kanuni iliyoruhusu mchezaji ambaye ni raia wa nje kuja kuhesabika ni Mtanzania kwenye Klabu. 3. ⁠Kama Damaro ni Mtanzania, je ana sifa za kucheza timu ya Tanzania au Guinea? Kama hajakidhi matakwa ya kuchezea timu ya Tanzania, maanake kwenye Club ni Mtanzania but National Team ni Guinea. Tanzania lini imeruhusu duo nationality? Hatuoni kwa kiruhusu hili tunavunja sheria za nchi n...

Moallin amrejesha Mkude Yanga, Sure Boy na Farid ndani

Picha
Kocha msaidizi wa Young Africans SC, Abdilamin Moallin amewaongeza wachezaji Faridi Musa, Abuubakar Salum "Sure boy" na Jonas Mkude kwenye mipango ya timu kuelekearoundya pili. Lakini story kubwa ni kiungo Jonas Mkude ambaye alishasahaurika kama yupo Young Africans na taarifa zilizopo mkude alikua anaumwa kwa muda mrefu, na alikuwa na matatizo binafsi na alipopona kocha Pedro hakua na mpngo na mchezaji huyo. Lakini hali imekuwa tofauti, kwani ujio wa Moalin ameenda kuwarejesha kwenye kikosi nyota hawa na tunaona kikosi kipana kwa eneo la nafasi kwenye timu. Hii imekuja baada ya kuonekana hawa ni wachezaji waandamizi ndani ya ligi kuu Tanzania bara na kuyafahamu vyema mazingira ya viwanja vya mikoani kama ambavyo taarifa ya kuongezeka kwa kocha katika benchi la ufundi ilisema.

MADUDU YA WAAMUZI WA TANZANIA, TFF ICHUKUE WA NJE

Picha
Na Prince Hoza Matua KWANZA namshukuru mwenyezi Mungu kwa kunipa uzima ambao unanifanya leo niandike makala maalum ya MIKASI ambayo kila siku ya Alhamisi inawajia, lakini pia namshukuru kwa kuniwezesha kuuona mwaka wangu mpya. Ikumbukwe Machi 31 majuzi ya wiki hii nimeadhimisha siku ya kuzaliwa (Happy Birthday) ambapo mimi na familia yangu tulikuwa na furaha ya kutimiza siku za kuzaliwa ya mpendwa wao (Prince Hoza). Naenda kwenye mada kama ilivyo kawaida yangu kuwaletea mjadala ambao unawahusu wasomaji wangu kutoka pande mbalimbali ulimwenguni. Mjadala wangu unahusu waamuzi, hasa wale wanaochezesha michuano ya Ligi Kuu bara, kombe la CRDB, Ngao ya Jamii, kombe la Mapinduzi na kombe la Muungano. Lakini pia waamuzi wetu ni mahususi kwa kuchezesha mechi za kirafiki za timu zetu kubwa zinazoshiriki mashindano makubwa ya nchi na pia ligi ya Championship. Nikielekea zaidi kwenye Ligi Kuu bara, ushindani wa ligi ni mkubwa na safari hii timu zote kubwa za Yanga SC, Simba SC, Azam FC na Singida...

CAF yabadili muundo wa michuano ya vilabu Afrika

Picha
Shirikisho la soka Afrika (CAF) kupitia kwa Rais Patrice Motsepe jana ilitangaza muundo mpya wa mashindano ya timu za taifa. CAF inatazamiwa kuchukua nafasi ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika kwa muundo mpya kabisa uitwao AFRICAN NATIONS LEAGUE. Hii ndio maana yake; 1. Ligi ya Mataifa ya Afrika - BARA Inachezwa kila mwaka Huanza katika kanda za kikanda Timu bora zaidi zinafuzu kwa mashindano ya mwisho katika nchi moja mwenyeji - Wachezaji WOTE wanaostahiki (pamoja na nyota wa Uropa) 2. Ligi ya Mataifa ya Afrika - PAN-AFRICAN Inachezwa kila baada ya miaka 2 Muundo sawa na Kombe la Mataifa ya Afrika (timu 24) 3. AFCON inabaki lakini inabadilika Sasa inachezwa kila baada ya miaka 4 Inakuwa shindano na bora barani Afrika

IJUE ULAYA NA HISTORIA YA KUZAA MADOLA MAKUBWA

Picha
Inaandikwa na Fikiri Salum ULAYA (asili ya jina ni neno la Kiarabu, Wilayaatuni, inaitwa pia Uropa kutoka Kigiriki European ama Ueram jina la Mungu jike Europa) ni bara lililoko katika kaskazini ya dunia likipakana na bahari ya Aktiki upande wa kaskazini, bahari ya Atlantiki upande wa magharibi na bahari ya Mediterranean upande wa kusini. Mpaka wake wa mashariki kwa kawaida hufafanuliwa kupitia milima ya Uraia, mto Uraia, bahari nyeusi, ingawa mipaka hii ni ya kijiografia na kihistoria zaidi kuliko ya kisiasa. Kwa eneo la takribani kilomita za mraba milioni 10, 18, Ulaya ni bara dogo la pili baada ya Australia lakini lina idadi kubwa ya watu, ikifikia zaidi ya milioni 750, na yenye msongamano mkubwa wa watu duniani. Ulaya ina historia ndefu na imechangia pakubwa katika maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kitamadumi duniani, bara hili lina mataifa 44 yanayotambulika kimataifa yakiwemo mataifa makubwa kama Ujerumani, Ufaransa na Uingereza. Lakini pia ni pamoja na mataifa madogo kama Vatika...