Machapisho

Dkt Mwinyi atembelea mradi wa AFCON mkoa Mjini Magharibi

Picha
Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameutembelea mradi wa Mji wa AFCON Fumba uliopo Mkoa wa Mjini Magharibi. Ziara hiyo imefanyika leo Aprili 14, 2026, akiambatana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Riziki Pembe Juma, pamoja na wadau wa mradi wa AFCON Fumba Zanzibar. Katika ziara hiyo, Rais Dkt. Mwinyi amekagua maeneo mbalimbali ya uwanja huo wa kisasa wa AFCON unaojengwa na kampuni ya ORKUN GROUP ya Uturuki, ambao unaotarajiwa kutumika kwa michuano ya #AFCON2027 itakayofanyika kwa ushirikiano wa nchi tatu za Afrika Mashariki za Kenya, Uganda na Tanzania. Aidha Dkt. Mwinyi ametembelea na kukagua miundombinu inayotarajiwa kujengwa kuzunguka uwanja huo, ikiwemo hospitali, barabara, migahawa, maduka makubwa (mall) pamoja na huduma nyingine muhimu zitakazouzunguka mji huo wa kisasa. Uwanja huo unakadiriwa kuchukua watazamaji elfu 35, ukiwa na viwango vya ubora vinavyokubalika na Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF).

Magori aungana na Simba kula nyama choma Arusha

Picha
Mwenyekiti wa Bodi, Crescentius Magori na Mjumbe wa Bodi, Dr. Seif Muba wamefika hapa katika Simba Nyama Choma Festival hapa Arusha.

Simba yamrejesha kikosini Jonathan Sowah

Picha
Simba SC wamemrejesha rasmi mchezaji wao Sowah kwenye kikosi cha klabu hiyo baada ya kipindi cha kutokuwa sehemu ya timu ya kwanza. Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana, uongozi wa Simba umeamua kumpa nafasi nyingine mchezaji huyo huku ukimwelekeza kuanza mazoezi na kikosi cha vijana chini ya umri wa miaka 20 (U-20). Hatua hiyo inaonekana kuwa sehemu ya mpango wa kumjengea upya utimamu wa mwili, nidhamu na kurejesha kiwango chake kabla ya kujiunga tena na kikosi cha wakubwa. Sowah anatarajiwa kuonyesha uwezo wake katika mazoezi hayo ili kushawishi benchi la ufundi kumpa nafasi ya kurejea kwenye timu ya kwanza katika mechi zijazo.

Klabu ya Ligi Kuu Burkina Faso yaja kujifunza Young Africans

Picha
Timu ya soka ya Usfaburkina kutoka Ouagadougou inayishiriki Ligi Kuu nchini Burkina Faso imewasili makao makuu ya klabu ya Yanga SC kwaajili ya Semina ya Mafunzo ya mfumo wa uendeshaji wa klabu ya mpira wa miguu. Mafunzo hayo yameanza leo chini ya idara ya Wanachama na Masoko kisha kuendekea kesho kupitia idara nyingine kabla ya kuhitimisha semina hii na kukutana na Rais wa Yanga Eng Hersi Said.

UKRISTO NI CHIMBUKO LA UYAHUDI - 12

Picha
Inaandikwa na Fikiri Salum Ilipoishia  KWA kweli karne za kati zilikuwa na mchanganyiko wa mambo yaliyopingana ibada za nje tu na za shati kabisa teolojia iliyoelekeza kutenda kwa msingi wa nipe nikupe na hakika ya kwamba binadamu anategemea kabisa neema ya Mungu. Endelea Kutojali wajibu hata upande wa viongozi wa kanisa na marekebisho safi ya mashirika ya kitawa. Karne ya 15 ilikuwa kipindi cha umo motomoto wa pekee katika kanisa, ambapo walei wengi zaidi na zaidi walipata aimu nzuri, hivyo walitamani hotuba bora na mafundisho ya kuwasaidia kuishi Kikristo zaidi. Luther aliitikia haja hizo zilizomgusa sana kama mtu wa wakati wake Luther alitumia kwa nadra neno urekebisho, lakini ukaja kuwa jina la kawaida la matukio yale mengi ya miaka 1517- 1555. Yaani kuanzia uenezi wa hoja 95 za Martin Luther hadi amani ya Augsburg , kati yake chanzo, yaani mabishano ya kikamisa yaliyosababishwa na teolojia ya Luther, yalichanganyika mapema na sasa. Uchumi na utamaduni, kutokana na hali halisi ya w...

Fikiri Elias awa kocha mkuu Coastal Union

Picha
Fikiri Elias Mahiza amejiunga na klabu ya Coastal Union akiwa ndiye kocha mkuu wa klabu hiyo akichukua mikoba ya Mohamed Muya. Hii sio mara ya Kwanza Kwa Fikiri kuwa kocha mkuu kwenye kikosi hicho kwani mwaka 2023 alikuwa ndiye kocha mkuu huku pia akiwahi kuwa kocha msaidizi wa klabu hiyo chini ya kocha Mwinyi Zahera. Fikiri Elias amewahi kufundisha timu za JKT Oljoro na Kengold ikumbukwe kuwa Kwa sasa Fikiri ni miongoni mwa makocha waliopo kwenye idara ya Ufundi ya TFF lakini ni Mkufunzi wa makocha Kwa ngazi ya CAF na FIFA

Kocha JKT Queens amlilia straika wake

Picha
Kocha wa JKT Queens, Kessy Abdallah amesema kukosekana kwa mshambuliaji wake tegemeo, Winifrida Gerald kumewaathiri kwa kiasi kikubwa kutokana na umuhimu wake katika safu ya ushambuliaji. Winifrida anayeongoza kwa ufungaji wa mabao ndani ya JKT Queens akiwa na Mabao 8, alifungiwa mechi tatu na faini ya Sh500,000 kwa kumshambulia beki wa Geita Queens. "Ni mchezaji muhimu tena sana, kimetuathiri kwa sababu hata wenzake wanamtegemea, kwa hiyo ilikuwa kazi kubwa sana kuwaelewesha kuwa tunaweza kufanya kitu bila yeye,” alisema Kessy. Aliongeza changamoto kubwa haikuwa tu kiufundi bali pia kisaikolojia kwa wachezaji wengine, ambao walipaswa kujijenga upya kujiamini na kucheza kwa mshikamano zaidi. "Baadae walinielewa na kweli tumeweza kufanya vizuri michezo miwili bila yeye na nashukuru Mungu na tunaamini tutafanya vizuri,” aliongeza. Pamoja na mafanikio hayo, Kessy alikiri ushindani katika mechi zao umekuwa mkubwa, huku kila timu ikipambana kwa nguvu kutafuta ushindi. “Vijana wana...