Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Dudubaya, Wastara kimeeleweka

Machapisho ya hivi karibuni

Ally Kamwe awapiga kijembe Simba SC

Ni kama anawapiga kijembe watani zao Simba SC ambao watakutana nao Machi 01, 2026 katika uwanja wa New Amaan Stadium, Zanzibar, Meneja Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe amewaambia watu wanaobeza kiwango cha timu yake waandae timu yao na walawafunge. “Wote wanaosema kwamba Yanga haichezi vizuri, basi andaeni timu mje mtufunge…… tukutane New Amaan Complex”. Bila shaka huu ni ujumbe kuelekea Kariakoo Derby, Yanga vs Simba, Machi 01, 2026.

Droo ya hatua ya 32 kombe la CRDB kufanyika kesho

Droo hatua ya 32 bora Kombe la Shirikisho la CRDB, kufanyika Jumanne hii Februari 24. Droo hii itafanyika kuanzia saa 6:30 mchana na kuruka mbashara kupitia AzamSports1HD.

Wengi wampongeza Gabriel Geay kwa kutwaa medali ya dhahabu Korea Kusini

Mwanariadha wa kimataifa wa Tanzania, Gabriel Geay, amepongezwa kwa kuibuka mshindi na kutwaa medali ya dhahabu katika Mbio za Daegu zilizofanyika Korea Kusini. Geay alimaliza mbio hizo kwa muda wa saa 2:08:04, akiandika ushindi wake wa pili mfululizo katika mashindano hayo, baada ya mwaka 2025 pia kutwaa taji hilo kwa muda wa 2:05:22. Miongoni mwa waliompongeza ni Jasmin Kikwete, Balozi wa Utalii na Uwekezaji wa Jumuiya ya Madola na Mkurugenzi wa Blue Visit Tanzania & Zanzibar, ambaye kwa kushirikiana na wadau wengine amekuwa akiunga mkono riadha kupitia dhana ya utalii wa michezo. Ushindi huo unaendelea kuiweka Tanzania kwenye ramani ya riadha kimataifa. Gabriel Geay

Kiwango cha kocha wa Yanga chatia shaka

Nimefuatilia kiwango Cha Yanga michezo minne iliyopita Kwa Ufundi na mbinu za Kocha Pedro kwakweli anatoa funzo kubwa yeye ni tactian based coach siyo technician Kwa maana ni Kocha anayebadirika mno haonekani Kwenye mtindo mmoja kitu ambacho Kwa wapenzi Wa Soka la Ufundi mwingi zaidi anaonekana haleti mvuto. Lakini Kwa mahitaji na Mpira wakisasa na muda aliyokuwa nao yeye na wachezaji maingizo mapya tafsiri yake anaugua huku anatakiwa kupona kujenga timu Kwa mfumo na wachezaji wapya Kwa ubora Kwenye mashindano inahitaji kocha mkomavu mithili yake. Kwani Pedro anatumia Tactical periodization yaani Kila mechi anahesabu yake kuficha mbinu zake na kusomeka kwa wapinzani haswa kuelekea mchezo Wa derby sababu muonekano Wa kikosi cha YANGA mechi ya mwisho dhidi ya JS klabu bingwa ni tofauti na michezo hii anajaribu na kuonesha kuficha nguvu na Mipango ya wazi ya timu kuepuka kusomeka kiwepesi . Mpira wa kisasa ni Sayansi siyo muda wote kuwa kama fanani kuburudisha hadhira Soka ni ushindi! Kut...

Kibu katika majukumu yake mapya Libya

Mchezaji wa zamani wa klabu ya Simba, Kibu Dennis jana alifanikiwa rasmi kucheza mchezo wake wa kwanza akiwa na klabu yake mpya ya Al Nasry ya Libya. Kibu Dennis aliingia kwenye dakika ya 71 ndani ya mchezo huo ambao Al Nasry iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Al Murooj kwenye mchezo wa group 4 ligi kuu ya Libya. Kwa upande mwengine pia wachezaji wengine wa zamani wa Simba, Steven Mukwala pamoja na Fabrice Ngoma nao pia walikuwa sehemu ya mchezo huo. Fabrice Ngoma alianza kwenye kikosi cha kwanza cha mchezo huo na kucheza dakika zote 90 huku Steven Mukwala akiingia kwenye dakika ya 71 ndani ya mchezo huo.

Moallin kurejea tena nchini

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Yanga, Abdihamid Moallin ‘Master Lecturer’, huenda akarejea Tanzania hivi karibuni ikiwa atafikia makubaliano na timu tatu zinazoshiriki Ligi Kuu Bara, baada ya kuonyesha uhitaji mkubwa kwa kocha huyo. Kocha huyo mwenye uraia wa Marekani akiwa na asili ya Somalia, kwa sasa yupo mapumziko Marekani tangu alipoachana na Yanga Julai 27, 2025, akiwa ni Mkurugenzi wa Ufundi, ingawa huenda muda wowote akarejea nchini ikiwa mazungumzo na timu hizo yatafikiwa ipasavyo. Hata hivyo, Mwanaspoti limepenyezewa taarifa zikieleza miongoni mwa timu zinazofanya mazungumzo na Moallin, kimya kimya ni TRA United inayonolewa na Mrundi Etienne Ndayiragije, ambaye hadi sasa kumekuwa na sintofahamu juu ya kibarua chake. Ndayiragije aliyejiunga na timu hiyo baada ya kuachana na Kenya Police FC ya Kenya, Oktoba 29, 2025, baada ya kuipa pia ubingwa wa Ligi ya Kenya, inadaiwa hana uhusiano mzuri na mabosi wa TRA, jambo linalofungua mazungumzo hayo na Moallin. Kocha huyo aliipa Ken...