Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Singida Black Stars wajivunia kucheza nyumbani, Simba wajiandae kulia

Machapisho ya hivi karibuni

Kocha Simba ataka pointi tatu za Singida Black Stars

Kocha mkuu wa klabu ya Simba SC Steve Barker raia wa Afrika Kusini, amesema leo kuelekea mchezo wao dhidi ya Singida Black Stars kwamba wanataka kushinda mchezo huo Ili waondoke na alama Amesema wachezaji wako imara kuhakikisha wanacheza kwa viwango vizuri ili kushinda mchezo huku wakiwa na uelewa kuwa Singida ni timu ambayo ina wachezaji pia wenye uwezo mkubwa. Kwa upande wake mchezaji wa Simba Daudi Semfuko amesema wamejianda kuipambania timu hiyo katika kuhakikisha ushindi unapatikana. Mchezo huu utachezwa kuanzia saa 10:15 jioni Steve Barker

Tanzania Prisons na Yanga sasa kupigwa Jamhuri Dodoma

BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) inatangaza mabadiliko ya uwanja kwa ajili ya mchezo namba 30 wa Ligi Kuu ya NBC, Tanzania Prisons FC dhidi ya Young Africans SC, ambao hapo awali ulipangwa kufanyika kwenye uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya Machi 12, 2026 kuanzia saa 10:00 alasiri. Mchezo huo sasa utafanyika katika tarehe hiyo kwenye uwanja wa Jamhuri uliopo jijini Dodoma kuanzia saa 2:00 usiku. Sababu ya mabadiliko hayo ya uwanja ni uwanja wa Sokoine kufungiwa na Kamati ya Leseni za Klabu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania Bodi inawatakia maandalizi memo ya mchezo huo wadau wote zikiwemo klabu shiriki.

Rais wa Kongo ahukumiwa kifungo cha maisha jela

Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini Congo, Federation Congolaise de Football (FECOFOOT), amehukumiwa kifungo cha maisha jela. Jean-Guy Blaise Mayolas amepatikana na hatia na mahakama na kuhukumiwa kifungo cha maisha kwa makosa kadhaa yakiwemo utakatishaji wa fedha, kughushi nyaraka, mgongano wa kimaslahi kinyume cha sheria, na ubadhirifu wa fedha za FIFA wakati wa kipindi cha janga la COVID-19. Fedha hizo zilikuwa zimetengwa kwa ajili ya maendeleo ya mpira wa wanawake na ujenzi wa kituo cha mafunzo (training center), lakini inadaiwa zilitumika vibaya. Mke wake na mwanawe pia wamepatikana na hatia katika kesi hiyo. Viongozi wawili wa shirikisho wamehukumiwa kifungo cha miaka mitano jela.

Kaze na mwenzake wagoma kuiachia Kaizer Chief

Makocha wawili wasaidizi wa Kaizer Chiefs, Cedric Kaze pamoja na Khalil Bin Youssef kwa pamoja wamegoma kuachia ngazi kwa matakwa yao ili kuinusuru timu kwenye mfululizo wa matokeo Mabaya ambayo wanayapitia kwa sasa Makocha hao wawili wanaamini kuwa bado wana kitu cha kufanya huku sababu ya malipo (wadhfa) kama kwa hiari yao watakubali kuondoka basi watakosa sehemu kubwa ya Malipo ya Vipengele Vya Mikataba Yao Kaze na mwezake kwa msimu ujao lengo kubwa ambalo wamewekewa na Uongozi wa Kaizer ni kuipeleka tena timu kwenye Michuano ya Kimataifa ya CAF !.

NABII MUSA KIONGOZI WA WANAISRAEL UTUMWANI MISRI- 2

Inaandikwa na Fikiri Salum Ilipoishia SAFARI YA KWENDA NCHI YA AHADI KUT 12:29-42 inasimulia Waisrael wote walivyokimbia Misri pamoja na mifugo yao waliposikia mayowe kutoka nyumba za majirani wao wote. Endelea. Katika safari yao wakaongozwa na Mungu kwa sura ya wingu mchana na ya moto usiku (KUT 13;17-22; Yoh 8;12): hivyo Mungu alionesha wazi kuwa hawaachi hata kidogo bali anawashughulikia kwa namna tofauti kadiri ya mahitaji. KUT 14;5-31 inasimulia jinsi Wamisri, kisha kuwalilia wafu wao, walianza kuwatafuta Waisrael kwa Farao na magari wakawakuta karibu na bahari ya Shamu. Lakini Waisrael walivuka bahari kama kwamba ni nchi kavu, kwa kuwa maji yamegawanyika, kumbe Wamisri wakazama kwa kuwa maji yamerudi mahari pake (EB 11;29) asubuhi Waisrael wakaona maiti za Wamisri wote zikielea, wakamshangilia Mungu aliyewaokoa. (KUT 15:1-21 inatuletea wimbo ambao maneno yake ni kati ya yale ya kale zaidi katika biblia) , hivyo Mungu aliwaokoa tena watu wake katika maji na huu pia ni mfano wa uba...

Mtoto wa Didier Drogba kufuata nyayo zake

Mtoto wa gwiji wa soka na mchezaji wa zamani wa Chelsea na Galatasaray, Didier Drogba, ambaye anacheza eneo la mshambuliaji mwenye umri wa miaka 25 Isaac Drogba, amehamia huko Hayk.. Isaac ni mhitimu wa academy ya Chelsea. Baadaye alihamia katika klabu ya Ufaransa, Guingamp, na klabu yake ya hivi karibuni ilikuwa La Louvière ya huko Ubelgiji.