Machapisho

Rais wa soka Kongo Brazzaville atoroka na kapu la hela

Picha
Rais wa Shirikisho la Soka la Congo-Brazzaville (FECOFOOT), Jean-Guy Blaise Mayolas, anatafutwa pamoja na mkewe na mtoto wake baada ya kutoweka, Mamlaka za Congo-Brazzaville zimewasilisha ombi kwa Interpol ili kutoa hati za kimataifa za kuwakamata, Mayolas na familia yake walipatikana na hatia ya ubadhirifu wa dola milioni 1.1 za Marekani kutoka FIFA, fedha zilizotolewa kama msaada wa COVID-19 mwezi Februari 2021, Sehemu ya fedha hizo, dola 500,000, zilikuwa zimetengwa kwa ajili ya timu ya taifa ya wanawake ya Congo, Inadaiwa kuwa walikimbia nchi wiki chache kabla ya kusikilizwa kwa kesi yao na wachunguzi wanahisi huenda wanajificha nchini Cameroon au Democratic Republic of the Congo.

MwanaFA uso kwa uso na Mkazuzu wa Clouds FM

Picha
Naibu Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Hamis Mwijuma "MwaFA" amekutana na Mkuu wa Idara ya Michezo Clouds Media Yahaya Mohamedy "Mkazuzu" pamoja na David Mponda Afisa Biashara (Citadel Tanzania Limited) na mbunifu mvumbuzi wa uthaminishwaji wa ligi kuu Tanzania bara na visiwani Zanzibar ofisini kwake Mtumba Jijini Dodoma. Kikao hicho kilihusisha mazungumzo ya uthaminishwaji wa ligi Kuu na kuingia kwa soka la Tanzania soko la hisa ambapo TFF na DSE wanatarajia kuingia makubaliano siku za karibuni. Mazungumzo hayo yaligusia pia uanzishwaji wa mfumo wa wachezaji wote Tanzania kuwa na mfuko wao wa uwekezaji kuchangia maendeleo ya wachezaji wa mpira wa miguu nchini Tanzania. Bwana Mponda pia, ndiye mvumbuzi wa chanzo kipya cha mapato kwa TFF kupitia michezo ya kubashiri (betting) ambapo amefanya kazi kubwa ya kuhakikisha wachezaji na timu za ligi za kuu pamoja na TFF wanaenda kunufaika na sekta hiyo.

Dodoma Jiji yaichakaza Fountain Gate 3-0

Picha
TIMU ya Dodoma Jiji FC imeibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Fountain Gate FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara mchana wa leo Uwanja wa Airtel Mwigulu mjini Singida. Mabao ya Dodoma Jiji FC yamefungwa na beki Augustino Nsata dakika ya 38, winga Iddi Kipagwile dakika ya 69 na mshambuliaji Yassin Mgaza dakika ya 90’+1. Kwa ushindi huo, Dodoma Jiji FC inafikisha pointi 24 katika mchezo wa 18 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya saba, wakati Fountain Gate inabaki na pointi zake 16 za mechi 17 sasa nafasi ya 12 kwenye ligi ya timu 16. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.

KMC yapokea kichapo kwa Mbeya City

Picha
TIMU ya Mbeya City imetoka nyuma na kushinda mabao 3-2 dhidi ya KMC FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati mkoani Manyara . Mabao ya Mbeya City yamefungwa na Riphat Msuya dakika ya 64, Adili Buha kwa penalti dakika ya 76 na Said Naushad dakika ya 86, wakati ya KMC yamefungwa na Oscar Paulo dakika ya 44 na Juma Shemvuni dakika ya 78. Kwa ushindi huo, Mbeya City inafikisha pointi 16 katika mchezo wa 17 na kusogea nafasi ya 12 kutoka ya 14, wakati KMC inaendelea kushika mkia ikibaki na pointi zake nane za mechi 17 sasa. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.

Nyota wa Bomu FC na Ashanti za Ilala, afariki dunia

Picha
Mchezaji wa zamani wa Bomu FC, Ashanti FC zote za Ilala, Kumbukumbu FC ya Kinondoni, Agatoni FC ya Mbagala - Mangaya, AFC ya Arusha na MOGO FC ya Majumba 6, Steven Antony Mwaigaga amefariki Dunia jioni ya leo katika hospital ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam, baada ya kuugua kwa muda ambapo alikuwa amelazwa katika wodi ya Mwaisela namba 6. Msiba upo nyumbani kwa Baba yake Mzazi eneo la Machimbo Kitunda, taarifa zaidi za mazishi tutawaletea, Mwaigaga ameacha mjane na watoto 2. Bwana ametoa, Bwana ametwaa, Jina lake Lihimidiwe.!

Sakata la Damaro, lamuibua Samuel Eto' o

Picha
Samuel Eto'o alipata uraia wa Hispania mnamo Oktoba 17, 2006, wakati akiwa mchezaji wa Barcelona. Hii ilimruhusu kucheza kama mchezaji wa Ulaya, na kumfaa katika mashindano ya klabu za Ulaya. Na kwa mujibu wa katiba ya Cameroon nchi hiyo hairuhusu uraia pacha. Lakini Eto'o alipata uraia wa Hispania na kuendelea kuitumikia Cameroon na leo hii ni rais wa Shirikisho la nchi hiyo Fédération Camerounaise de Football (FECAFOOT) Najaribu kujiuliza kwa nini FIFA walishindwa kumzuia mchezaji aliyebadilisha uraia wake kutoka kwenye nchi isiyoruhusu uraia pacha?Na Eto'o siyo mchezaji wa kwanza duniani.Lakini naambiwa na wajuzi wa mambo ya uraia Na hivi karibuni kuliibuka sakata la uhalali wa wachezaji Wacongo Wachezaji wa DR Congo waliohusika katika kesi hiyo, kama vile Aaron Wan-Bissaka na Axel Tuanzebe, wamekuwa na uraia wa Ulaya au Ufaransa, lakini sheria za Kongo haziruhusu uraia wa pacha. Nigeria inadai kuwa wachezaji hao hawakuwa na sifa za kucheza kwa DR Congo kutokana na ...

UKRISTO NI CHIMBUKO LA UYAHUDI

Picha
Inaandikwa na Fikiri Salum UKRISTO (kutoka neno la Kigiriki, Khistos, ambalo linatafsiri lile la Kiebrania Masia, linalomaanisha "mpakwa mafuta" ni dini inayomwamini Mungu pekee kama alilivyofunuliwa kwa Waisrael katika historia ya wokovu ya Agano la kale la hasa Yesu Kristo katika Agano jipya ambaye ni mwanzilishi wake katika karne ya 1. Dini hiyo iliyotokana na Ile ya Uyahudi, inalenga kuenea kwa binadamu wote, na Kwa sasa ni kubwa kuliko zote duniani ikiwa na wafuasi 2, 400, 000, 000 sawa na asilimia 33 kati ya watu 7, 274 bilioni ambao nusu ya pili wamegawanyika kati ya Waorthodoksi (asilimia 11, 9) na Waprotestant (asilimia 38,) wa madhehebu mengi sana. Karibu wote wanakubali utatu mtakatifu yaani kwamba milele yote Mungu ni nafsi tatu zenye umoja kamili, baba, mwana na roho mtakatifu, ni kwa jina lao, kwamba mataifa yote wanahimizwa kubatizwa kwa maji Ili kuzaliwa upya, kadri ya agizo la Yesu ni kuingizwa katika fumbo la Mungu pekee kupitia fumbo la kifo na ufufuko wake...