Ni kama anawapiga kijembe watani zao Simba SC ambao watakutana nao Machi 01, 2026 katika uwanja wa New Amaan Stadium, Zanzibar, Meneja Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe amewaambia watu wanaobeza kiwango cha timu yake waandae timu yao na walawafunge. “Wote wanaosema kwamba Yanga haichezi vizuri, basi andaeni timu mje mtufunge…… tukutane New Amaan Complex”. Bila shaka huu ni ujumbe kuelekea Kariakoo Derby, Yanga vs Simba, Machi 01, 2026.
MAMBO UWANJANI
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com