Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inno Loemba aingia kwenye vita kali na mashabiki wa Yanga

Machapisho ya hivi karibuni

Tanzania Prisons ya Nsajigwa yaibana Azam FC

TIMU ya Azam FC imetoa sare ya bila kufungana na wenyeji, Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Kwa matokeo hayo, Azam FC wanafikisha pointi 24 katika mchezo wa 12 na kupanda kwa nafasi moja hadi ya nne, wakati Tanzania Prisons inafikisha pointi 13 katika mchezo wa 15, ingawa inabaki nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.

Yanga yaifumua Singida Black Stars

MABINGWA watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya wenyeji, Singida Black Stars katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Mwigulu Airtel Complex, Singida. Mabao ya Yanga SC leo yamefungwa na mshambuliaji Mzimbabwe, Prince Mpumelelo Dube dakika ya 39, winga Mganda, Allan Okello kwa penalti dakika ya 45’+2 na kiungo Mudathir Yahya Abbas dakika ya 56. Kwa ushindi huo, Yanga SC wanafikisha pointi 32 katika mchezo wa 12 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi nne zaidi ya JKT Tanzania ambayo pia imecheza mechi tano zaidi. Kwa upande wao Singida Black Stars wanabaki na pointi zao 19 za mechi 12 pia nafasi ya tisa.

TUKUBALI TU SIMBA IPO BORA SASA KULIKO YANGA, PEDRO ASILAUMIWE

Na Prince Hoza Matua NAMSHANGAA sana aliyekuwa Rais wa klabu ya Yanga SC, Tarimba Abbas Tarimba ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Kinondonj kupitia Chama Cha Mapinduzi, CCM. Tarimba amezungumza mengi kuhusu klabu yake ya Yanga SC ambapo pia yeye ni mfadhili kupitia kampuni yake ya Sportpesa, kigogo huyo wa Yanga na Tanzania kwa ujumla alikosoa sajili zinazofanywa na klabu hiyo kwa siku za karibuni akidai kwamba si nzuri. Kwa kifupi Tarimba amechukizwa na matokeo ya timu hiyo iliyoyapata Jumapili iliyopita ilipocheza na hasimu wake Simba SC katika uwanja wa New Amaan Stadium, mjini Zanzibar. Katika mchezo huo Yanga ililazimishwa sare tasa na Simba ya 0-0, sio siri matokeo hayo ya sare yaliwahudhi mashabiki wengi wa timu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani, Kariakoo jijini Dar es Salaam. Tarimba amepeleka malalamiko yake moja kwa moja kwa Rais wa sasa wa klabu hiyo Injinia Hersi Ally Said ambaye pia amekuwa akihusika moja kwa moja kufanya sajili za wachezaji wapya. Wanayang...

Jayruthy yamzawadia gari aina ya Crown Inno Loemba

Kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Inno Loemba, ameanza kuonja matunda ya kazi yake baada ya kukabidhiwa gari jipya aina ya Toyota Crown. Zawadi hiyo imetolewa na kampuni ya JAYRUTTY Investment, ambao ndio wazabuni rasmi wa jezi na vifaa vyote vya michezo vya klabu ya Simba SC. ​Hili ni mwanzo tu wa neema kwa wachezaji wa Simba, kwani JAYRUTTY imepanga kutoa magari mengine kwa nyota ​Libasse Gueye, ​Anicet Oura na ​Djibrilla Kassali.

Kisa Yanga, Singida Black Stars yafyata kwa Khalid Aucho, yamrejesha

Klabu ya Singida Black Stars imemfuta adhabu ya kusimamishwa kwa miezi mitatu mchezaji wake, Khalid Aucho, baada ya kupitia utetezi wake na kuomba radhi kwa makosa. Uamuzi huu umefanywa na Kamati ya Nidhamu ya timu hiyo, kufuatia barua ya kukiri na kuomba radhi iliyotolewa na mchezaji huyo. Aucho sasa anaruhusiwa kurejea kikosini na kuendelea kuitumikia timu hiyo. Singida Black Stars inaendelea kusisitiza nidhamu, uwajibikaji na weledi kwa watumishi wake wote .

HISTORIA YA MTUME MUHAMMAD NA UISLAMU- 4

Inaandikwa na Fikiri Salum ILIPOISHIA MTUME akamjibu "mimi sijui kusoma kwani sijapata kujifunza", akaja akamkamata, akambana akamwambia tena "soma", mtume akamjibu jawabu lile lile, hata mara ya tatu akamwambia "soma" iqra a bismi ra bbik. Endelea. Akamsomea sura ya 96 mpaka kati yake kisha mtume akaisoma kama alivyosomewa, hii ndiyo sura ya kwanza kushika katika kurani, ingawa haijawekwa mwanzo. Mara yule mtu (malaika) akaondoka mwchoni pake asimwone, kaenda wapi, naye akarejea kwake hofu imemshika. Alipofika nyumbani Khadija alidhani ana homa, akamfunika nguo gubigubi akakaa mbele yake akimsikiliza anavyoweweseka, homa ilipomwachia alimweleza Khadija yote yaliyomtokea, naye akamtuliza moyo wake, akamyakinishia ya kuwa hapana lolote baya litakalomzukia. Mara bibi huyu akaondoka, akaenda kwa jamaa yake Waraga bin Naufat akampa habari yote iliyompata mumewe, naye akamwamrisha amwite na mtume akaenda akamweleza habari yake yote. Bwana Waraga akamwambia ...