Machapisho

Top scorer wa Simba Queens atimka

Picha
Mshambuliaji wa Simba Queens, Jetrix Shikangwa, ameondoka rasmi klabuni hapo na kujiunga na FC Masar ya Misri. Jetrix anaondoka baada ya msimu bora, akifunga mabao 16 na kuwa mmoja wa nyota walioisaidia Simba Queens kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania. Anatarajiwa kuungana na Mtanzania, Hasnath Ubamba, anayekipiga FC Masar.

Seleman Mwalimu atabaki Simba

Picha
Kocha Steve Barker amemtaja Selemani Mwalimu kuwa mmoja wa washambuliaji anaotaka kubaki nao Simba SC kuelekea msimu wa 2026/27 Mkataba wa sasa wa mkopo wa Selemani Mwalimu na Simba SC hauna kipengele chochote cha kuongeza muda wa mkopo au kumnunua moja kwa moja Hii ina maana kuwa Mwalimu anatakiwa kurejea Wydad AC mara baada ya mkopo wake kumalizika, then Simba SC na Wydad AC wafungue mazungumzo mapya(kama wanahitaji kubaki naye) Taarifa zinaeleza kuwa Wydad AC wako tayari kumruhusu Mwalimu aondoke kwa uhamisho wa moja kwa moja(kuuzwa), na si kwa mkopo mwingine Hata hivyo, ada inayotarajiwa kuhitajika inaweza kuwa changamoto kwa Simba SC Licha ya kuvutiwa na vilabu kadhaa, Selemani Mwalimu ameipa Simba SC kipaumbele na yuko tayari kusubiri uamuzi wa Simba sc kabla ya kusikiliza ofa nyingine Kwa sasa, mchezaji anaitaka Simba kwanza... lakini uamuzi wa mwisho utategemea kama Simba SC na Wydad AC watafikiana

Barker amng' ang' ania Ibraheem Jabaar

Picha
Kocha mkuu wa Simba Steve Barker,ana-push sana Simba wakamilishe usajili wa kiungo wa Stellenbosch raia wa Nigeria, Ibraheem Jabaar (23). Personal terms Siyo ishu kwani mchezaji huyo yuko huru. Kocha anamtaka Jaabar kwani anamfahamu vizuri ila viongozi wa Simba wanamtaka namba 10 wa Chile,Diego Mauricio ambae nae ni mchezaji huru. Simba wanamuona Diego ni Top Top Number 10 ambae atakuju kumpa changamoto Chota Chama….na Simba wako tayari kumlipa mshahara wa $20,000 (52,646,460) kila mwezi. Wiki ijayo itakuwa muhimu sana kufanya maamuzi ya nani aje kati ya Diego Mauricio au Jabaar.

Azam FC yamkomalia Iddi Nado kwenda Yanga

Picha
Azam FC imeanza mazungumzo na kiungo wake Nado kwa lengo la kuongeza mkataba wake, kufuatia kiwango bora alichoonyesha tangu aliporejea kikosini mwezi Julai 2025. Nado, ambaye alijiunga na Azam FC mwaka 2019 akitokea Mbeya City, ameendelea kuwa mmoja wa wachezaji muhimu ndani ya kikosi hicho kutokana na mchango wake mkubwa katika safu ya kiungo. Taarifa zinaeleza kuwa hatua ya Azam FC kumuita mezani inalenga kuhakikisha inamdumisha nyota huyo, hasa baada ya kuvutia macho ya watani wa jadi, Yanga SC na Simba SC, ambao wanatajwa kuwa na nia ya kupata saini yake. Hatma ya Nado sasa inategemewa kuamuliwa na mazungumzo kati yake na Azam FC huku dirisha la usajili likiendelea kushika kasi. 

Rasmi, Yanga wanamleta Fadlu

Picha
Inaripotiwa nchini Afrika Kusini mchana huu kwamba, Yanga Afrika wameweka ofa mezani na wako kwenye mazungumzo kumsaini Kocha Fadlu Davids kama kocha wake mpya mkuu kuelekea msimu ujao. Fadlu Davids aliitumikia Simba Sports msimu huu, hapa Tanzania kabla ya kutimkia Raja Club huko Morocco ambako baada ya matokeo mabovu dhdi ya vilabu vikubwa na kuukosa Ubingwa wa Botola Pro alifutwa kazi jijjni Casablanca wiki chache zilizopita.

Diarra kinara wa clean sheets

Picha
Kipa wa Yanga SC na Timu ya Taifa ya Mali, Djigui Diarra, ameendelea kuonyesha kiwango cha juu baada ya kufikisha clean sheets 17 kufuatia mchezo dhidi ya TRA. Rekodi hiyo inamfanya kuwa kipa mwenye clean sheets nyingi zaidi msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara, huku kukiwa bado kumesalia mchezo mmoja kabla ya msimu kumalizika. Hii ni mara ya tatu kwa Djigui Diarra kumaliza akiwa kinara wa clean sheets tangu ajiunge na Yanga SC, jambo linaloonyesha uthabiti wake langoni kwa misimu kadhaa mfululizo. Rekodi zake za Clean Sheets: 2021/22 – 15 2022/23 – 17 2023/24 – Ley Matampi (15) 2024/25 – Moussa Camara (19) 2025/26 – 17 (bado mchezo mmoja umebaki) Djigui sasa ana nafasi ya kuongeza idadi hiyo katika mchezo wa mwisho wa msimu na kuendelea kuimarisha rekodi yake kama mmoja wa makipa bora kuwahi kucheza Ligi Kuu Tanzania Bara.

TZ Prisons, Mbeya City na Mtibwa Sugar hatarini kushuka daraja

Picha
TIMU za Mbeya City na Tanzania Prisons zote za Mbeya – kwa pamoja na Mtibwa Sugar ya Morogoro zote zipo hatarini kushuka Daraja baada ya mechi za mzunguko wa 29 leo. Wakiwa nyumbani, Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya, Tanzania Prisons wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mtibwa Sugar ya Morogoro, huku Mbeya City ikitoa sare ya kufungana bao 1-1 na wenyeji, Dodoma Jiji FC Uwanja wa Jamhuri, Dodoma Baada ya matokeo hayo, Mtibwa Sugar inashukia nafasi ya 15 ikibaki na pointi zake 27, nyuma ya Tanzania Prisons nafasi ya 14 na Mbeya City nafasi ya 13 baada ya timu hizo zote kucheza mechi 29 zikiwa hatarini kuungana na KMC FC ambayo tayari imeshuka daraja. Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, mabingwa watetezi, Yanga SC wamelikaribia taji la tano mfululizo la Ligi Kuu baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya TRA United Uwanja wa KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam. Nao Simba SC wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Singida Black Stars Uwanja wa Meja Jenerali Charles Isamuhyo, Mbweni, Dar es ...