Machapisho

Mrithi wa Pedro Yanga huyu hapa

Picha
KLABU ya Yanga imemtambulisha Manqoba Brilliant Ferrimant Mngqithi (55) kutoka Golden Arrows ya kwao, Afrika Kusini kuwa kocha wake mpya Mkuu akichukua nafas ya Mreno, Pedro Valdemar Soares Gonçalves aliyeondolewa Mei mwaka huu

Kagame Cup kulamba milioni 79

Picha
Klabu ya Al Hilal ya nchini Sudan imechukua hatua kubwa na ya kihistoria baada ya kujitolea kudhamini michuano ya Kombe la CECAFA Kagame Cup 2026 kwa kutoa kiasi cha dola za Kimarekani laki moja ($100,000), ambazo ni zaidi ya Shilingi Milioni 263 za Kitanzania. Kwa mujibu wa taarifa za ndani, miamba hiyo ya soka ya Sudan imekubali kutoa mkono huo wa heri ili kufanikisha uendeshaji wa mashindano hayo yanayotarajiwa kurindima hivi karibuni nchini Rwanda. ​Lengo kuu la Al Hilal kuingia kama mdhamini mkuu ni kuyatumia mashindano hayo adhimu ya ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kama sehemu ya maandalizi yao ya msimu mpya (Pre-Season). Klabu hiyo inataka kupima makali ya kikosi chake dhidi ya timu pinzani ili kujiweka sawa kuelekea mashindano ya ndani na yale ya kimataifa, huku ikiongeza chachu na mvuto wa kiushindani katika michuano hiyo. ​Kufuatia udhamini huo mnono, mchanganuo wa zawadi zitakazotolewa kwa timu zitakazofanya vizuri umebadilika na kuwa wa kuvutia zaidi. Bingwa mpya wa mich...

Anicet Oura hatihati kubaki Simba

Picha
Kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Anicet Oura, ameingia kwenye rada za klabu tatu za Ulaya kufuatia kiwango bora alichoonyesha tangu ajiunge na Wekundu wa Msimbazi mwezi Januari mwaka huu. Taarifa zinaeleza kuwa Bursaspor (Uturuki), Víkingur Reykjavík (Iceland) na DAC 1904 Dunajská Streda (Slovakia) zinafuatilia kwa karibu hali ya nyota huyo wa Ivory Coast. Bursaspor inaongoza mbio za kumsajili Oura na inatajwa kuwa tayari kuwasilisha ofa ya Euro 250,000. Hata hivyo, Kocha Steve Barker amesisitiza kuwa anahitaji kubaki na kiungo huyo kwa ajili ya msimu ujao. Kwa tafsiri ndogo ni ngumu Simba Sc kumuuza Anicet Oura.

Akaminko ruksa kwenda Yanga

Picha
Klabu ya Azam FC imeachana na Kiungo wake James Akaminko Raia wa Ghana Baada ya Mkataba wake kumalizika. Kocha Mkuu wa Klabu ya Azam FC Florent Ibenge Raia wa Congo Anasema James Akaminko hayuko kwenye Mipango Yake Msimu Ujao. Lakini inaelezwa kwamba huo ni mpango wa Yanga ambayo ilionesha nia ya kumuhitahi sasa kitendo Cha kumuacha ni kuiruhusu Yanga iweze kumsajili kirahisi

MC Alger yavutiwa na Nduwumwe

Picha
MC Alger inavutiwa na kiwango cha mshambuliaji Mossi Nduwumwe (22) kutoka Singida Black Stars FC na tayari wameanza mazungumzo na Singida Black Stars FC ili kupata huduma yake! Ofa nono ilishawekwa mezani kwa Singida Black Stars kilichobaki ni makubaliano baina ya pande zote mbili na hakuna ofa yoyote kutoka Young Africans SC iliyofika mezani kwa Singida Black Stars FC.

16 wapitishwa kugombea Yanga

Picha
WANACHAMA 16 wamepitishwa kugombea nafasi za Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu ya Yanga kafika uchaguzi utakaofanyika Agosti 2, mwaka huu akiwemo Issa Ally Mangungu ambaye ni mdogo wa Mwenyekiti wa Simba, Murtaza Ally Mangungu. Wengine waliopitishwa ni Hersi Ally Said anayetetea nafasi yake ya Urais na Arafat Haji anayetetea pia nafasi ya Makamu wa Rais na ambao wote hawana wapinzani.

Leo Ufaransa vs Morocco kombe la Dunia

Picha
DIRISHA la usajili wa Ligi zote za Tanzania Bara limefunguliwa rasmi juzi, Julai 6 na litakuwa wazi hadi Agosti 15 Saa 5:59 usiku litakapofungwa.