Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Pyramids kuibomoa Al Ahly

Machapisho ya hivi karibuni

Khalid Aucho akana kujihusisha na utovu wa nidhamu

KIUNGO wa Kimataifa wa Uganda, Khalid Aucho amesema kwenye maisha yake ya soka hajawahi kuhusishwa na utovu wa nidhamu kwa namna yoyote. Aucho ameandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kufuatia taarifa ya klabu ya klabu yake, Singida Bkack Stars kumsimamisha yeye na kipa Mnigeria, Amas Daniel Obasogie kwa tuhuma za utovu wa nidhamu. “Nimekuwa nikizingatia taaluma yangu kila wakati katika taaluma yangu, nikiiwakilisha kila klabu kwa heshima na nidhamu. Katika miaka yangu yote katika soka, sijawahi kuhusika katika kesi yoyote ya utovu wa nidhamu kwa sababu ninaelewa jukumu linalokuja na kuwa mchezaji mwadilifu. Kwa mashabiki wangu wapendwa ambao wamekuwa wakiniunga mkono kila wakati, hali litapita. Asante kwa msaada wako unaoendelea,” amesema mchezaji huyo wa zamani wa Yanga.

Ally Kamwe aihofia Simba

Afisa Habari wa Young Africans, Ally Kamwe, ametoa kauli ya kushtua na ya kiungwana kuelekea mahasimu wao, Simba SC, akieleza kuwa amekuwa akifuatilia michezo yao kwa ukaribu ili kujifunza vitu mbalimbali. Kamwe amekiri kuwa Simba wamefanya usajili mzuri katika dirisha dogo la usajili, akilinganisha na daraja ambalo klabu hiyo ipo kwa sasa katika ramani ya soka. ​Katika kile kinachoonekana kama kutuliza presha ya mashabiki, Ally Kamwe amesisitiza kuwa mchezo wa hivi karibuni wa Simba haukuwa mbaya kama ambavyo watu wengi wanautafsiri. "Jana nilisema, watu wanaona kama utani ila kimsingi mechi yao ya juzi walicheza vizuri, walikosa bahati tu," alisema Kamwe, akionyesha utofauti na kauli za kashfa zinazoweza kutolewa na upande mwingine katika kipindi hiki cha ushindani mkali wa ligi.

Dudubaya awashukuru mashabiki wake baada ya upasuaji India

Mwanamuziki mkomgwe wa muziki wa kizazi kipya, Bongofleva, Godfrey Tumaini "Dudubaya" ametoka salama katika chumba cha upasuaji huko Delhi, India amesema kwasasa anaendelea vizuri. Dudubaya amefanyiwa upasuaji wa kuweka sawa pingili za mgongo, mwanamuziki huyo mkongwe amemshukuru Mungu, madaktari, mashabiki wake na wote wanaomtakia mema. Dudubaya amepelekwa India kufanyiwa upasuaji wa pingili na mpenzi wake Wastara Ili amuoe.

Sowah awajia juu wanaomchafua

Mshambuliaji wa Simba SC Jonathan Sowah amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu sakata linaloendelea kati ya yeye na timu hiyo lililopelekea kuondolewa kwake kambini kuelekea mchezo muhimu dhidi ya Yanga SC. "Sijajua kwanini nimeambiwa natakiwa kurudi Dar. Alinifuata meneja wa timu akanip ujumbe huo. Kwa kuwa ni kiongozi wangu sikutakiwa kumhoji sana zaidi ya kutekeleza." "Kuhusu madai ya utovu wa nidhamu, nasikia kutoka kwako lakini pia nimeona watu wanaandika tu kwenye mitandao ya kijamii. Nimesoma, ila nasubiri kwanza hicho kikao cha uongozi kujua sababu." "Nikimalizana na uongozi ndio nitawarudia hao ambao wameandika vitu bila kujua ukweli kutoka kwangu. Mimi sio mtu wa kukubali jina langu kuchafuliwa kirahisi."

Taasisi ya MO Dewji na Simba zatoa misaada kituo cha watoto yatima Zanzibar

Kwa kushirikiana na Taasisi ya Mo Dewji, tumetoa msaada kwenye kituo cha Kutunza Watoto Yatima cha Mazizini kilichopo hapa Zanzibar, lakini pia tutapata futari pamoja leo jioni.

Bingwa wa Ligi ya mabingwa Afrika kupewa Dola milioni 6

Shirikisho la soka Afrika (CAF), limetangaza ongezeko la fedha za zawadi zinazotolewa kwa mshindi na mshindi wa pili katika Mashindano yake ya Vilabu, kuanzia msimu wa sasa wa 2025/2026. Chini ya muundo huo mpya wa zawadi, Mshindi wa Ligi ya Mabingwa wa CAF watapata Dola Milioni 6 ( Shilingi Bilioni 15.6 za Tanzania) huku Mshindi wa pili akijinyakulia Fola Milioni 2 (Shilingi Bilioni 5.2 za Tanzania). Timu zilizofika nusu fainali zitapata Dola Milioni 1.2 kila mmoja, na dola 900,000 kwa timu zilizotolewa katika robo fainali, na Dola 700,000 kwa vilabu vinavyomaliza nafasi ya tatu na nne katika hatua ya makundi. Kamati ya utendaji pia iliidhinisha pesa za juu zaidi kwenye Kombe la Shirikisho la CAF ambapo bingwa atatunukiwa Dola Milioni 4 (Shilingi Bilioni 10.4 za Tanzania) wakati Mshindi wa pili akitapata Dola Milioni 1 (Shilingi Bilioni 2.6 za Tanzania).