Inaandikwa na Fikiri Salum BONDE la Oltupai (maarufu kwa Kiingereza kama Olduvai Gorge) ni eneo la Kiakiojia linalopatikana katika mkoa wa Arusha nchini Tanzania ambalo ni kati ya yale muhimu zaidi duniani. Bonde hilo lipo katika hifadhi ya Ngorongoro na karibu na Ile mbuga ya Serengeti, ni mahari ambapo Zamadamu, viumbe wa kale waliokaribiana na mwili wa binadamu, waliishi tangu miaka milioni 2 hivi iliyopita. Kwa kuwa watu wanadhaniwa kutokana nao, eneo hilo pengine limeitwa kwa Kiingereza Craile of manking, kitovu cha binadamu, ambako wameishi katika eneo hilo kwa walau miaka 17, 000 mfululizo. Katika eneo hili Mwanaakiolojia Mary Leakey ndipo alipogundua fuvu la kichwa la kiumbe wa kale wa jamii hiyo. Pamoja na mabaki ya mifupa ya Tembo, Kongoo wenye pembe kubwa na Mbuni, tarehe 17 Julia 1959 aligundua mabaki ya fuvu la kichwa la Pararthropus Boisei (pamoja na mumewe alimwita kwanza zinjanthropus) ambalo lipo katika makumbusho ya Dar es Salaam. Huyo anadhaniwa kuwa mtangulizi wa bi...