Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Mtoto wa Didier Drogba kufuata nyayo zake

Machapisho ya hivi karibuni

Diarra ashinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Februari

KIPA wa Yanga, Djigui Diarra raia wa Mali ameshinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi February wa klab huyo, ambayo inadhaminiwa na Shirika la Bima la Taifa (NIC).

Azam FC na Yanga sasa kupigwa kwa Mkapa

Mchezo wa dabi ya kukata na shoka wa Ligi Kuu ya NBC kati ya Azam FC dhidi ya Young Africans sasa umerejeshwa rasmi katika dimba la Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam. Hatua hiyo inakuja kufuatia mabadiliko ya hivi punde yaliyothibitisha kuwa pambano hilo litapigwa Jumapili hii, Machi 15, 2026, jambo ambalo limeleta msisimko mkubwa kwa mashabiki wa soka nchini wanaosubiri kwa hamu kuona miamba hiyo ikiumana kwenye uwanja huo wa taifa wenye hadhi ya juu. ​Kurejeshwa kwa mechi hiyo Benjamin Mkapa kunatoa fursa kwa klabu zote mbili kuonyesha ufundi wao katika uwanja wenye nafasi kubwa na mazingira bora ya soka la ushindani, huku Azam FC wakitafuta kulinda heshima yao dhidi ya mabingwa watetezi Yanga. Maandalizi yamepamba moto kwa pande zote mbili, huku wadau wa soka wakitabiri mchezo wenye kasi na mbinu nyingi kutokana na ubora wa vikosi vya timu hizo msimu huu, hali inayofanya mechi hiyo kuwa moja ya dabi muhimu zaidi katika mbio za ubingwa.

Marekani kimenuka, milio ya risasi yasikika

Milio ya risasi ilisikika nyumbani kwa Rihanna huko Beverly Hills, California, Polisi wakisema kuwa hakuna aliyejeruhiwa katika tukio hilo. Polisi wanasema mshukiwa, Mwanamke mwenye umri wa miaka 30, alisimama mbele ya Nyumba kutoka kwenye gari na kufyatua risasi saba kabla ya kukimbia. Kwa mujibu wa Polisi Mwanamke huyo ambaye bado hajatajwa utambulisho wake alikamatwa na Maafisa usalama Kilomita 12 kutoka kwenye makazi ya mwimbaji huyo. Mnamo Septemba (9), Rihanna alijifungua mtoto wake wa tatu, binti, na mpenzi wake A$AP Rocky. Wanandoa hao tayari wana watoto wengine wawili wa kiume, Riot na RZA. Mzaliwa wa Barbados, Rihanna, ambaye jina lake halisi ni Robyn Fenty, alipata umaarufu miaka ya 2000 kwa vibao kama vile Pon de Replay na Umbrella.

NABII MUSA KIONGOZI WA WANAISRAEL

Inaandikwa na Fikiri Salum MUSA aliishi miaka ya 1250 hivi KK akawa kiongozi wa wana Israel walipoondoka nchini Misri kukimbilia nchi ya Kanaani iliyoitwa Palestina na Israel baadaye. Hasa Torati na vitabu vingine vya biblia vinasimulia habari zake, pia Kurani inamtaja Musa katika Aya 502, Waisrael waliishi Misri kama wageni tu zaidi ya miaka mia nne (Mdo 7-6-16 wakiongezeka kiasi cha kuwatisha wenyeji wao ambao walianza kuwafanya watumwa mwaka 1,300 hivi KK, kwa mujibu wa biblia, katika kuwakomboa utumwani, Mungu alijionesha mtetezi wa haki za masikini. Pamoja na kushurutishwa kufanya kazi walizozipenda, ilitolewa amri ya kuua watoto wote wa kiume, ingawa mpango huo haukutekelezwa sawa sawa (KUT 1:7-22). Mmoja kati ya watoto waliookolewa katika mpango wa kuua watoto wa kiume ni Musa wa kabila la Lawi (KUT 2:1-10; EB 11:23: Mdo 7:17-22), mama wa Musa alimficha mtoto halafu akamweka ndani ya kikapu mtoni. Hatimaye mtoto akaokotwa na binti Farao na kulelewa kama mtoto wa Kifalme, lakini ...

Simba yambakiza nahodha wake Kwa kumpa mkataba

Nahodha wa Klabu ya Simba SC, Rushine De Reuck ameongeza mkataba wa mwaka mmoja wa kuendelea kuitumikia Klabu ya Simba SC mpaka June 2027. . Rushine mwenye umri wa miaka 29 amesinya mkataba huo jana .

Yanga yatishia kujitoa Ligi Kuu bara

Klabu ya Yanga SC imeripotiwa kuwa tayari kususia Ligi Kuu Tanzania Bara iwapo hatua kali hazitachukuliwa dhidi ya Simba SC, huku wakidai kuwepo kwa upendeleo katika maamuzi mbalimbali ya ligi. Taarifa zinaeleza kuwa viongozi wa Yanga hawaridhishwi na namna baadhi ya matukio yanavyoshughulikiwa na mamlaka za soka nchini, wakisisitiza kuwa wanahitaji usawa na haki kwa klabu zote zinazoshiriki ligi. Inadaiwa kuwa endapo Simba haitachukuliwa hatua stahiki kulingana na kanuni za ligi, Yanga wanaweza kuchukua uamuzi wa kususia baadhi ya mechi kama njia ya kuonesha kutoridhishwa kwao. Hata hivyo, hadi sasa mamlaka zinazosimamia ligi bado hazijatoa tamko rasmi kuhusu suala hilo.