Rais wa Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), Patrice Motsepe, ametangaza rasmi kuanzishwa kwa mashindano mapya ya kimataifa yatakayojulikana kama African Nations League, yenye lengo la kuongeza ushindani na mapato katika soka la Afrika. Mashindano hayo mapya yanachukua nafasi ya michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN), huku yakibuniwa kwa mfumo mpya utakaoleta ushindani mkubwa zaidi na kushirikisha wachezaji wa viwango vya juu wanaocheza ndani na nje ya bara la Afrika. Kwa mujibu wa Motsepe, mashindano hayo yatakuwa na mifumo miwili tofauti ambapo wa kwanza African Nations League Continental, utaendeshwa kwa mfumo wa kanda ambapo timu bora kutoka kila ukanda zitashindana na hatimaye kupata washindi watakaoingia hatua ya fainali itakayofanyika katika nchi mwenyeji. Pili, African Nations League Pan-African, utakuwa na muundo unaofanana na AFCON, ukizikutanisha timu bora zaidi barani Afrika pamoja na wachezaji nyota wanaocheza katika ligi kubwa duniani. Mots...
MAMBO UWANJANI
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com