Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Mashujaa FC yasawazishiwa goli dakika ya mwisho wa mchezo

Machapisho ya hivi karibuni

Duke Abuye, Bajaber waitwa Harambee Stars

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, ametangaza kikosi rasmi kitakachoshiriki mashindano ya FIFA Series 2026, huku majina ya nyota wanaokipiga katika Ligi Kuu ya NBC nchini Tanzania yakivutia macho ya wengi.  Katika orodha hiyo, kiungo fundi wa Young Africans, Duke Abuya, na mshambuliaji chipukizi wa Simba SC, Mohammed Bajaber, wamejumuishwa kufuatia viwango bora walivyoonyesha kwenye klabu zao msimu huu. Kikosi hicho kimechanganya uzoefu na damu changa, kikiongozwa na nahodha na mshambuliaji tegemeo Michael Olunga (Al Arabi). Safu ya ulinzi itaimarishwa na nyota kama Zak Vyner anayecheza nchini Uingereza (Wrexham) na Rooney Onyango (Sogndal), wakati safu ya kiungo ikiwa na mafundi kama Richard Odada na Manzur Suleiman anayecheza nchini Ufaransa (Stade De Reims). Uteuzi wa Bajaber na Abuya unathibitisha kukua kwa ushindani katika ligi ya Tanzania na jinsi inavyotoa nafasi kwa wachezaji kuonekana katika anga za kimataifa. ​Kikosi kamili kilichotajwa ni kama ifuatavyo: ​...

FIFA yapitisha sheria mpya za soka

FIFA imeidhinisha mabadiliko kadhaa ya Sheria ambayo yataanza kutumika kwenye Kombe la Dunia 2026: Wachezaji watakaobadilishwa wana sekunde 10 kuondoka uwanjani. Wakichelewa, mchezaji anayeingia atalazimika kusubiri dakika moja kabla ya kuingia. Mipira iliyokwenda nje itakuwa inafanywa ndani ya sekunde 5, la sivyo mpira utapelekwa upande wa pili. Wachezaji wanaopata matibabu watalazimika kuondoka uwanjani na kusubiri dakika moja kabla ya kurudi Uwanjani. VAR sasa itaruhusiwa kuingilia kati kwenye kadi za njano za pili (Kadi nyekundu) na kwenye mipira ya kona kama kuna kosa la wazi la kiamuzi.

MO Dewji aporomoka kwa utajiri Afrika

Rais wa Heshima wa Simba SC na mfanyabiashara, Mohammed Dewji ameshuka kwa nafasi mbili katika chati ya mabilionea Afrika kwa mujibu wa ripoti ya jarida na mtandao wa Forbes ambayo imetoka Jumatatu, Machi 9, 2026. Kwa sasa Dewji anashika nafasi ya 14 akiwa na utajiri ambao unatajwa kufikia kiasi cha Dola 2.1 bilioni (Sh5.4 trilioni) ukichangiwa na uwekezaji katika viwanda vya nguo, unga wa ngano na sembe, mafuta ya kupikia, sabuni, sukari, vinywaji na biashara ya katani. Kabla ya orodha hiyo ya mabilionea ya kwanza kutolewa kwa mwaka 2026, Dewji alikuwa nafasi ya 12 katika orodha ya mwisho kwa mwaka 2025 iliyotoka Desemba 8, 2025 akiwa na utajiri uliokadiriwa kufikia Dola 2.2 bilioni (Sh5.7 trilioni). Wakati Dewji akishuka kwa nafasi mbili, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Patrice Motsepe amependa kwa nafasi moja kutoka ile ya tisa aliyokuwepo Desemba mwaka jana hadi ya nane. Utajiri wa Motsepe umepanda hadi kufikia kiasi cha Dola 4.3 bilioni (Sh11 trilioni) kutoka u...

Yanga yampa dili Seleman Kitunda

Baada ya kufanikiwa timu yake ya Cosmopolitan kufungwa mabao machache dhidi ya Yanga SC katika mchezo wa hatua ya 32 kombe la CRDB, hatimaye klabu ya Hausing FC ya Njombe inayoshiriki Championship imeamua kumchukua kocha huyo na kuwa kocha wake mkuu. Seleman Kitunda Simota au maarufu Guardiola, amejiunga rasmi na timu hiyo iliyoweka kambi mkoani Manyara, akizungumza na Mambo Uwanjani Blog, Kitunda amefurahishwa na kujiunga kwake na timu hiyo inayopambania kupanda daraja msimu ujao. Hausing imeamua kumchukua Kitunda kutokana na uwezo wake aliouonesha dhidi ya Yanga na kuifanya timu hiyo inayoongoza ligi kupata idadi ndogo ya mabao tofauti ikicheza na timu nyingine kubwa ikizitandika idadi kubwa ya mabao. Katika mchezo huo Yanga dhidi ya Cosmopolitan, Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 huku pia Kitunda anasifika kwa kuwaagiza vijana wake kuoheshimu Yanga na kushambulia kwa mipira ya kushtukiza. Kocha mpya wa Hausing FC ya Njombe

Wilson Nangu atembelewa na viongozi wa Simba nyumbani kwake

Beki wa Klabu ya Simba Wilson Nangu ametembelewa na Uongozi wa timu hiyo ili kumjuli hali maendeleo yake nyumbani kwao Kilimanjaro Mchezaji huyo ni miongoni mwa wachezaji wa klabu ya Simba SC ambao walipatwa na majeraha siku za karibuni na kupelekea kukosekana katika michezo kadhaa.

KANISA KATOLIKI NA HISTORIA YAKE

Inaandikwa na Fikiri Salum KANISA katoliki likiwa la zamani (Waorthodoksi) na Waorthodoksi wa mashariki wanashiriki sifa hiyo) na kubwa kuliko madhehebu yote ya Ukristo, historia yake inashika sehemu muhimu ya historia ya kanisa lote duniani tangu lilipoanza mwaka 30 hivi BK hadi leo. Baada ya Yesu Kristo kuhubiri na kukusanya wafuasi kati ya Wayahudi wa Karne ya 1 hao walitumwa naye duniani kote, hasa wanaume 12 aliowaita mitume "yaani walitumwa".  Waandamizi wao katika uongozi wa kanisa walianza kuitwa maaskofu, na kati ya yule wa Roma alizidi kushika nafasi ya pekee kwa sababu mtume Petro alifia dini katika mji huo kutokana na dhuluma dhidi ya Ukristo ambayo ilianzishwa na Kaisari Nero (mwaka 64) na kuendelea kwa kwikwi hadi ilipokomeshwa na Kaisari Konstantino mkuu aliyetangaza huko Milano Uhuru wa dini kwa wananchi wote (313). Dhuluma haikufaulu kuzuia uenezi wa dini hiyo mpya katika Dola la Roma, mwishoni mwa  karne ya 2, maaskafu walianza kukusanyika katika sinadi Ili ...