Machapisho

Tchakei arejea mzigoni Singida BS

Picha
Kiungo wa Klabuya Singida Black Stars, Marouf Tchakei amejiunga na kikosi baada ya majeraha ya Muda Mrefu . Tchakei alikosekana kwa muda mrefu hasa baada ya kurejea kwenye kikosi hicho baada ya kuachwa na Yanga SC na baadaye kutumia. Kiungo huyo mahiri na fundi wa mpira atakuwepo katika mchezo wao dhidi ya KMC FC unaotazamiwa kuchezwa kesho

Singida Black Stars kutambulisha kocha mpya, Kanu kuongoza kwa muda

Picha
Muda wowote kutoka sasa Singida BS tutatangaza benchi ldtu jipya la ufundi. Kwa sasa timu itakuwa chini ya mtaalamu @muhibukanu mpaka pale tutakapomtambulisha Kocha Mpya na Wasaidizi wake. Kanu ni sehemu ya viongozi wa klabu mwenye taaluma ya Ukocha (CAF Diploma A) na uongozi ulimuamini kumuweka sehemu ya benchi lililopita ili kumjengea uwezo na uzoefu. Kesho ataiongoza timu yetu kutafuta ushindi dhidi ya KMC FC

Loemba aleta mgogoro- wa Jayruthy na Magori

Picha
Sakata la Inno Josepin Loemba linaendelea kuibua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki wa Simba SC baada ya kauli tofauti zinazotolewa kuhusu usajili wake. Ikumbukwe kuwa Jayrutty, ambaye ni mzabuni wa vifaa vya michezo ndani ya klabu hiyo, aliwahi kuwaahidi mashabiki kuwa angechangia kuleta mchezaji mmoja kama sehemu ya mchango wake kwa timu. Katika mahojiano yake na Crown TV, alieleza wazi kuwa tayari wamemleta Loemba, kauli iliyopokelewa kwa shangwe na mashabiki wengi. Hata hivyo, kauli za hivi karibuni kutoka kwa Magori zimeleta mkanganyiko baada ya kueleza kuwa Loemba ni usajili wa klabu yenyewe, jambo linaloonekana kupingana na ile ahadi na maelezo ya awali ya Jayrutty. Hali hii imeacha maswali mengi kwa wadau wa soka: Je, mchango wa mzabuni ulikuwa upi hasa? Na ni kwa nini kuna utofauti wa taarifa juu ya suala nyeti kama hili? Mashabiki wanahitaji uwazi na kauli moja kutoka kwa uongozi wa Simba SC ili kuondoa sintofahamu hii. Bila kufanya hivyo, maswali yataendelea kuongezeka na...

Ali Kamwe azua maswali kwa wanahabari

Picha
Afisa Habari wa klabu ya Yanga SC, Ali Shabani Kamwe, ni kama amezua maswali kwa wanahabari kutokana na andiko lake alilolitoa leo. Nilitegemea mpaka sasa hivi Waandishi wa habari/ Wachambuzi wangekuwa wameshafanya Yafuatayo.. 1: Kupiga Simu TFF kuthibitisha kama ni kweli TAASISI HII YA MPIRA NCHINI ndio ilikwenda Uhamiaji na kumuombea URAIA mchezaji Kibu Dennis 2: Kupiga Simu Idara ya Uhamiaji na kuuliza kama Taratibu za Nchi yetu zinaruhusu Taasisi kumuombea Mtu URAIA wa Tanzania kwa sababu ya mpira 3: Nilitegemea warudi tena TFF kuuliza ilikuwaje mchezaji KIBU DENNIS alicheza Ligi Kuu [Mbeya City/ Simba SC] akiwa Binadamu ambaye hana URAIA (FREE STATE). Kanuni Gani ilitumika kuruhusu hili? 4: Nilitegemea Waandishi/Wachambuzi waulize tena WIZARA husika ni kweli Tanzania anaweza kuishi Mtu na akafanya kazi kama mchezaji akiwa HANA URAIA WA TAIFA LOLOTE??

CAF yatoa tarehe rasmi ya kuanza AFCON 2027

Picha
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limethibitisha rasmi kuwa mashindano ya kihistoria ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) ya mwaka 2027, maarufu kama "Pamoja Bid", yatafanyika kuanzia Juni 19 hadi Julai 18, 2027.  Mashindano hayo yatakayozikutanisha nchi za Tanzania, Kenya, na Uganda kama wenyeji wa pamoja, yanatarajiwa kuandika ukurasa mpya katika soka la ukanda huu, huku maandalizi ya miundombinu yakishika kasi katika miji mbalimbali ili kuhakikisha viwango vya kimataifa vinafikiwa kabla ya muda uliopangwa. ​Hatua hii imepokelewa kwa shangwe kubwa na mashabiki wa soka Afrika Mashariki kwani ni mara ya kwanza kwa nchi hizi tatu kuandaa mashindano makubwa namna hii kwa pamoja.  Kwa mujibu wa Rais wa CAF, Patrice Motsepe, mashindano haya yatakuwa na msisimko wa kipekee na yanalenga kukuza vipaji na uchumi wa nchi wanachama, huku viwanja kama Benjamin Mkapa (Dar es Salaam), Mandela (Kampala), na Talanta (Nairobi) vikiwa miongoni mwa maeneo makuu yatakayoshuhudia buruda...

Magori asisitiza Mpanzu hajagoma ila anaumwa

Picha
“Elie Mpanzu mkataba wake wa sasa utaisha Septemba, kusema anagoma kwa mahitaji ya mkataba mpya ni jambo la ajabu sana. Kwanza katika wachezaji wana heshima ni Mpanzu na ameumia sana kuikosa mechi ya Azam. Hayo ni maneno ambayo hayana kichwa wala miguu. Anaumwa lakini anaendelea vizuri na amesafiri na timu kwenda Arusha. Sina uhakika na mechi ya tarehe 9 kama atacheza lakini labda kuanzia tarehe 12.” “Ilianzia tukapelekwa kuchezwa Zanzibar sababu ya mashindano ya Quran, huko nyuma mashindano yameshawahi kufanyika na baada ya mashindano mchezo ukachezwa. Tuliwauliza wasimamizi wa mashindano ya Quran wakasema wao wanamaliza mapema shughuli zingine zinaweza kuendelea lakini bado mchezo ukapelekwa Zanzibar.” “Kwanza Loemba hajaletwa na JayRutty, alitafutwa na Kamati ya Usajili kwa kushirikiana na kocha. Mkataba wa JayRutty ndio unasema atasajili mchezaji mmoja ndio tukamwambia alipie gharama zake za usajili. Kwani Mohammed [Dewji] anavyosajili wachezaji kwahiyo ni wachezaji ni wa Mohammed...

Simba bado wanazitaka pointi 3 za Damaro

Picha
Ni kama bado wanazitaka pointi 3 za chee kutoka kwa watani wao wa jadi Yanga SC kwa kitendo chao cha kumtumia mchezaji wao Mohamed Damaro ambaye uraia wake wa Tanzania haujakamilika. Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba SC Crescentius Magori ameendelea kukazia mpango wao wa kutaka wapewe pointi 3 licha kwamba madai yao yalitupiliwa mbali na TFF. "Mwaka jana na sisi tuliandika barua ya kubadili uraia wa wachezaji wetu lakini haijajibiwa hadi leo. Ligi Kuu ya Tanzania ikiwa haipo kwenye mizania sawa sio japo sawa. Hili japo sio tu tunakwenda CAS lakini pia tunaiandikia FIFA. Kama mtu anapewa uraia ili tu achezee klabu pekee bila timu ya taifa ni jambo ambalo halikubaliki. Damaro hata ipite miaka 100 hawezi kucheza timu ya Taifa. Jambo lingine ambalo TFF walitakiwa walifanye, kama kanuni zetu halizungumzii hilo basi wangetumia kanuni za juu kufanya maamuzi." "Hili jambo sio fair sababu kuna timu moja ina wachezaji 13 kwa kutumia mlango wa nyuma. Na aliyedanganya mamla...