Machapisho

JKT Tanzania yamng' oa Sure Boy Yanga

Picha
Mazungumzo baina ya pande zote mbili kwa maana upande wa Salum Abubakar Sure boy na JKT Tanzania yamekamilika na kilichosalia kwasasa ni kusaini kandarasi tu. Licha ya vilabu kama Dodoma Jiji na Mashujaa kuonesha nia ya kuipata huduma yake ila Maafande, Jkt Tanzania ndio wapo karibu zaidi kukamilisha usajili wake Sure (36) anaondoka Young Africans baada ya iandarasi yake kuisha

Akaminko njia nyeupe kwenda Yanga

Picha
Yanga SC wameanza mazungumzo rasmi na kambi ya James Akaminko wakipania kuimarisha safu yao ya kiungo kabla ya msimu mpya. Mkataba wa sasa wa kiungo huyo wa kimataifa wa Ghana unatarajiwa kumalizika Julai 5, na Kwa sasa akamiko anaweza kuzungumza na timu yeyote Yanga SC sasa wanatathimini uwezekano wa kumleta klabuni hapo,lakini mazungumzo bado yanaendelea na hakuna makubaliano ya mwisho ambayo yamefikiwa katika hatua hii

Chris Mugalu huyoo Caps United

Picha
Mshambuliaji Chris Mugalu (35) amejiunga na klabu ya CAPS United kwaajili ya msimu ujao wa 2026-27 kutoka Forest Rangers Chris Mugalu aliwahi kucheza Simba SC kabla ya kujiunga na CAPS United ambayo mkataba wake na klabu hiyo kumalizika.

Yanga yapanda dau kwa Girumugisha

Picha
Kama kuna mchezaji anawaumiza vichwa viongozi wa Yanga ni Jean Claude Girumugisha. Chanzo changu kimeniambia Yanga wanajua ofa ya Pyramid imekataliwa,Yanga wanajua kuna klabu ya Ittihad kutoka Libya ila Yanga wamegoma kukata tamaa. Yanga bado wanapambana kushinda vita ya Jean Claude Girumugisha. Chanzo changu kimenisiaitiza nisiwatoe Yanga kwenye vita ya Jean Claude Girumugisha.

Tshabalala kuongoza parade la ubingwa Jumamosi

Picha
Afisa Habari wa Young Africans SC, Ally Kamwe, ameendelea kuchanja mbuga na utani wa jadi mara baada ya timu yake kutwaa ubingwa, safari hii akimfanyia dhihaka nahodha wa Simba SC, Mohamed Hussein 'Zimbwe Jr'. Kamwe amedai kwa utani kuwa Zimbwe Jr ndiye atakayeongoza gwaride lao la ubingwa Jumamosi akiwa juu ya basi la wazi la Yanga, akijumuisha kijembe kuwa mara ya mwisho kwa beki huyo kufanya gwaride la ubingwa alipanda gari la mizigo aina ya kenta. ​Ujumbe wa Ally Kamwe ulisikika hivi: ​"Mohamed Hussein ndiye atakayeongoza parade letu Jumamosi, atakaa juu pale kwenye lile bus la ubingwa. Mara yake ya mwisho kufanya parade alipanda kenta. ​Jana alinionyesha kivideo cha miaka sijui elfu moja mia nane na ngapi huko, yupo kwenye kikenta anachungulia".

Al Ittihad Iko tayari kumuuza Aziz Ki

Picha
Klabu ya Al Ittihad SC ya Libya ipo tayari kumuuza kiungo wao mshambuliaji Stephane Aziz Ki ikiwa ofa itafika mezani kwao itakayowaridhisha kuelekea msimu ujao wa 2026-27. Al Ittihad SC imeshamlipa ada ya usajili na mishahara yote kwa Aziz Ki na imekanusha taarifa zilizovuma kuwa hawajalipa pesa hizo baada ya Young Africans SC umuhitaji kiungo Aziz Ki arudi klabuni kwao, Al Ittihad SC wanaheshimu mkataba wao na Aziz Ki na washalipa kila mchezaji ada yake ya usajili na mishahara.

Simba yaiomba Bodi ya Ligi ilete waamuzi wa nje ya nchi

Picha
Uongozi wa klabu ya Simba SC umeandika barua kwenda Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) na TFF kuwataka wachague Waamuzi ambao hawana maamuzi mabaya ya kujirudia. Simba SC ipo tayari kughalimikia Bodi ya Ligi na TFF kuleta Marefa kutoka nje ya nchi ikiwa humu ndani itashindikana