Machapisho

Azam FC yalamba matapishi yake kwa Kipre Junior

Picha
WINGA Muivory Coast, Kipré Tiagori Emmanuel Junior Zunon ‘Kipre Junior’ amejiunga tena na Azam FC akitokea MC Algiers ya Algeria. “Tunayo furaha kuwataarifu kuwa tumemrejesha nyota wetu wa zamani, Zunon Kipre Emmanuel Junior, baada ya kumnunua kutoka klabu ya MCA | Mouloudia Club d'Alger. Welcome back home, Zunon Kipre Emmanuel Junior “ wameandika Azam FC kwenye page yao. Kipre Junior anarejea Azam FC ambako awali alicheza kuanzia msimu wa 2022-2023 akitokea SOL FC d’Abobo ya kwao, Ivory Coast hadi 2024-2025 alipohamia MC Algiers.

Uzinduzi wa Wiki ya Wananchi kufanyika Katoro

Picha
Klabu ya Young Africans SC imetangaza rasmi kuwa uzinduzi wa Wiki ya Mwananchi 2026 utafanyika Katoro, mkoani Geita, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya msimu mpya wa mashindano. Akizungumza, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe, amesema klabu hiyo pia itazindua rasmi jezi mpya za msimu wa 2026/2027 mwishoni mwa mwezi huu.Uzinduzi huo unatarajiwa kuwakutanisha maelfu ya mashabiki wa Yanga kutoka maeneo mbalimbali ya nchi, huku ukiwa mwanzo wa maandalizi rasmi ya timu kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu ya NBC na mashindano ya kimataifa.

Simba yamnasa Kouasi

Picha
Simba SC inaendelea na harakati za kuimarisha kikosi chake huku beki wa kulia Blè Kouasi akitajwa kuwa kwenye rada za Wekundu wa Msimbazi. Nyota huyo anasifiwa kwa uwezo wake wa kupanda na kushuka kwa kasi, pamoja na kupiga krosi zenye ubora mkubwa. Endapo usajili huu utakamilika, ushindani katika nafasi ya beki wa kulia utaongezeka, huku Shomari Kapombe na David Kameta "Duchu" wakilazimika kupambana zaidi kuwania nafasi ya kuanza kikosini msimu wa 2026/27.

Mrithi wa Dube amwaga wino Jangwani

Picha
Klabu ya Yanga imefikia hatua ya mwisho ya kuimarisha safu yake ya ushambuliaji baada ya kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Guinea, Mohamed Saliou Bangoura, aliyekuwa akiichezea MC Alger ya Algeria, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya msimu mpya wa mashindano. Bangoura anaingia Jangwani akiwa na sifa ya kuwa mmoja wa washambuliaji vijana wenye uwezo mkubwa barani Afrika. Kabla ya kujiunga na MC Alger mwaka 2025, aliitumikia Hafia FC ya Guinea ambako alijitengenezea jina kutokana na uwezo wake mkubwa wa kufunga mabao, kasi, nguvu za mwili na uwezo wa kucheza ndani ya eneo la hatari. Baada ya kuhamia MC Alger, mshambuliaji huyo aliendelea kuonyesha kiwango bora, akifanikiwa kufunga mabao muhimu na kuchangia mafanikio ya klabu hiyo katika Ligi Kuu ya Algeria. Aidha, amewahi kuitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Guinea, jambo linaloonyesha kiwango chake na imani aliyonayo kutoka kwa benchi la ufundi la taifa hilo. Usajili wa Bangoura unatajwa kuwa sehemu ya mkakati wa Yan...

Kigogo Yanga amfagilia Karia

Picha
Mjumbe wa kamati ya utendaji kwenye klabu ya Yanga,Alex Ngai anasema kuwa amefurahishwa na maamuzi ya Rais wa TFF, Wallace Karia ya kufuta kanuni ya timu ya ugenini kufanya mazoezi siku moja kabla ya mchezo husika (dhidi ya timu mwenyeji) "Kwani hii kanuni si kuna timu moja tu ndiyo imeharibu?,ila nimefurahi kufutwa kwa hii kanuni"- Alex Ngai

Azam FC yapigwa faini

Picha
KLABU ya Azam imetozwa Faini ya Sh. Milioni 50, huku viongozi na wachezaji wake nao wakichukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu kwa makosa tofauti kwenye mchezo wa Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB. Azam Football Club Tanzania Football Federation CRDB Bank Plc Azam Sports TBC Taifa Precision Air

Vilabu vyamgombea kocha wa Mtibwa

Picha
Licha ya klabu ya Mtibwa Sugar kutokuwa tayari kumuachia kocha wao raia wa Kenya Yusuf Chippo imefahamika vipo Vilabu kadhaa vya ligi kuu ya NBC vimeonesha uhitaji wa kuipata huduma yake, Uongozi wa klab ya Mtibwa Sugar haupo tayari kumpoteza kocha huyo na unaamini ni mwalimu sahihi kuendelea kuwepo hapo kwenye project yao wa kuwarejesha ligi kuu msimu wa 2027/28, Bado mpaka muda huu haijafahamika kama Kocha huyo atasalia na Mtibwa Sugar ama ataondoka,