Machapisho

Gwalala aamua kusepa Coastal Union

Picha
Kiungo Greyson Gwalala ameachana na Coastal Union FC kuelekea msimu mpya na amesaini mkataba wa TRA United FC. Kila kitu kimekamilika na Greyson Gwalala ni mali ya TRA United FC. 32yrs

Yanga yapita na dogo wa Fountain Gate

Picha
Juma Abushiri (18) to Yanga Ni almost a Deal Done Yanga wame-hijack dili la kinda wa Fountan gate,Juma Abushiri (Chuga Boy) kwenda KAA Gent ya Belgium. Abushiri tayari amesaini mkataba wa miaka mitatu na Yanga Yanga wamempa kiungo huyo sign on fee tsh 90milion,kisha watalipa tsh 100 milion kwenda Fountain gate ili kuvunja mkataba wake wa miaka mitano. Mkataba wa Abushiri na Yanga umesainiwa kwenye hotel ya Gran Melia Arusha Kiungo huyo alikuwa na ofa ya kwenda Gent na alitakiwa kuondoka nchini tarehe 12/8/2026 ila Yanga wamepindua meza na kijana kasaini Jangwani.

Camara atimkia FC Annecy

Picha
Mlinda mlango wa zamani wa Simba Sports, Mousa PinPin Camara anajiunga na FC Annecy inayoshiriki Ligi daraja la pili Ufaransa akiwa mchezaji huru baada ya kumaliua kandarasi unyamani. Camara atacheza French Ligue 2 msimu ujao. FC Annecy walihusika pia na rehab yake kupona majeraha kipindi hiki alichokuwa nje na kusafiri mara kdhaa kuelekea Ufaransa kwa Matibab

Slavia Prague yabisha hodi Msimbazi

Picha
Klabu ya Slavia Prague,Czechia imetuma ofa kwenda Simba ili kumpata Hussein Ally Mbegu (16). Slavia wanataka kinda huyo akafanye majaribio kwa siku kadhaa ili wajiridhishe na baadhi ya vitu kabla ya kulipa pesa Simba na kukamilisha manunuzi hayo. Barua ya ofa iko Simba ila bado hawajajibu chochote.

Ligi Kuu bara kutimua vumbi Agosti 16

Picha
Ligi Kuu ya msimu ujao wa 2026/2027 inatarajiwa kuanza kutimua vumbi kuanzia Agost 16 2026 na kumalizika kabla ya June 1 2027! Mojawapo ya sababu kubwa ya Ligi kurejea mapema ni uwepo wa AFCON 2027 ambayo itafanyika Tanzania, Kenya na Uganda kuanzia June 19 2027 mpaka July 18 2027! Ratiba ya Ngao ya Jamii itatoka mapema ikifuatiwa na ratiba ya ligi kuu 2026/2027!

Naby Camara aachwa Simba

Picha
Klabu ya Simba SC imeingia kwenye mabadiliko makubwa ya kikosi chake kuelekea msimu mpya baada ya kukamilisha taratibu za kuachana na kiungo wao, Naby Camara.  Pande zote mbili zimefikia makubaliano ya kirafiki ya kuvunja mkataba uliokuwa unawaunganisha, hatua inayohitimisha rasmi safari ya mchezaji huyo ndani ya uwanja wa Mo Simba Arena baada ya kuitumikia timu hiyo kwa msimu mmoja pekee. ​Kuondoka kwa kiungo huyo hakujashtukiza uongozi kwani tayari alishafunganya virago na kuondoka nchini tangu Juni 25, 2026, huku akiiacha Simba ikiendelea na mikakati mingine ya kusuka safu yake ya kiungo. Camara kwa sasa anatajwa kuwa mchezaji huru (free agent), jambo linalompa fursa ya kukaa mezani na timu yoyote ndani au nje ya Afrika inayohitaji huduma yake kwa ajili ya changamoto mpya za kisoka. ​Hatua hii ya Simba SC ni mwendelezo wa mpango wao wa kupunguza wachezaji wa kigeni ambao hawakuwa na mchango mkubwa wa moja kwa moja kwenye kikosi cha kwanza msimu uliopita. Mashabiki wa Wekundu wa Msim...