Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Hans Raphael aamua kuwa shabiki wa Inno Loemba

Machapisho ya hivi karibuni

Simba yakataa uteja wa Yanga

WATANI wa Jadi, Simba na Yanga wametoshana nguvu kwa sare ya bila mabao katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara dhidi ya watani, Simba usiku huu Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Kwa matokeo hayo, Yanga SC inafikisha pointi 29 katika mchezo wa 11 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi moja zaidi ya JKT Tanzania ambayo pia imecheza mechi sita zaidi. Kwa upande wao, Simba SC wanafikisha pointi 24 katika mchezo wa 11 pia, ingawa wanabaki nafasi ya tatu. Simba SC wameondoka uwanjani wakimlalamikia refa Msaidizi namba moja, Kassim Mpanga kukataa bao lililofungwa na mshambuliaji Suleiman Abdallah Mwalimu kipindi cha pili kwa kumhukumu alikuwa ameotea.

ATCL yasitisha safari za Dubai

Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) limeufahamisha umma kwamba, kutokana na kufungwa kwa anga katika eneo la Mashariki ya Kati na kwa kuzingatia usalama wa abiria na wahudumu, safari zote za ndege kwenda na kutoka Dubai zimesitishwa hadi itakapotangazwa tena. Shirika hilo limesema linaendelea kufuatilia hali hiyo kwa karibu na kwamba safari zitarejeshwa mara tu hali itakapothibitishwa kuwa salama na tulivu. ATCL imewataarifu wateja wenye tiketi za kusafiri kwenda au kutoka Dubai katika kipindi hiki kuwa wanaweza kubadilisha safari zao bila gharama ya ziada, kulingana na upatikanaji wa nafasi. ATCL inaomba radhi kwa usumbufu wowote unaoweza kusababishwa na hali hiyo na inathamini uvumilivu na uelewa wa abiria wake katika kipindi hiki.

Yanga na Simba kutachimbika Zanzibar

Leo ndio leo katika uwanja wa New Amaan Stadium, Zanzibar pale watani wa jadi wa soka la Tanzania, Yanga na Simba watakaposhuka uwanjani kuwania pointi tatu muhimu mchezo wa Ligi Kuu bara. Yanga itakuwa mwenyeji ikiongozwa na kocha wake Pedro Goncalves raia wa Ureno wakati Simba inaongozwa na kocha wake Steve Barker raia wa Afrika Kusini. Tutegemee mchezo utakuwa mzuri na wa kuvutia, Yanga inataka kuendeleza rekodi yake ya kushinda mbele ya Simba wakati Simba nao wanataka kuhakikisha wanaondoa wimbi la kufungwa na Yanga na ikiwezekana wanapata ushindi ama sare.

Hasheem Thabit achaguliwa kuwa Rais wa TBF

Nyota wa basketball Tanzania, Hasheem Thabeet amechaguliwa kuwa rais wa chama cha mpira wa kikapu Tanzania (TBF) baada ya kushinda kinyanganyiro hicho katika uchaguzi uliofanyika leo jijini Dodoma. Katika uchaguzi huo Hasheem ameibuka mshindi baada ya kupata kura 34 kati ya 60 zilizopigwa na wajumbe wote. Hashem kwa sasa anachezea timu ya kikapu ya Dar City ambayo inatarajiwa kucheza fainali za ‘BAL’ kwenye michezo itakayochezwa kuanzia Machi 27 nchini Afrika Kusini. Wengine walioshinda katika uchaguzi huo Mohamed Kisui (Makamu wa Rais), Mwenze Fiston Kabinda (Katibu Mkuu) na Simon Milondo (Naibu Katibu Mkuu).

Yanga wapiga tizi la mwisho la kuivaa Simba kesho

Kikosi cha Yanga SC leo kimefanya mazoezi ya mwisho kabla ya kuwavaa watani zao Simba SC kesho mchezo wa Ligi Kuu bara katika uwanja wa New Amaan Stadium, Zanzibar.

Sebastian Nkoma: Ni kocha wa soka la wanawake aliyeinua vipaji hapa Tanzania

Na Abdul Makambo KOCHA Sebastian Nkoma ni mmoja wa makocha wazawa waliotoa mchango mkubwa katika maendeleo ya soka hapa nchini Tanzania .Pamoja na nchi yetu wamepita makocha wengi wazawa wenye uwezo na majina makubwa kama Mansour Magram, Joel Bendera, Ray Gama, Ayoub Mohamed, Zacharia Kinanda na Elijah Kategile. Wengine ni Iddi Machupa, Pius Nyamko, Edmund Thomas, Mohamed Msomali, Salum Madadi, Abdalah Kibaden, Omary Mahadhi, Abdurahman Juma, Athuman Juma Kalomba, Silylelsaid Mziray, Kenny Mwaisabula, Hamim Mawazo na hao ni baadhi. Nkoma alipokuwa Yanga Princess (kulia) Nkoma ni mmoja wa makocha wetu wazawa mwenye moyo  Nkoma amezifundisha timu nyingi hapa Tanzania na baadhi ni kama Rhino ya Tabora. Soka la wanawake ndio lililomtoa kocha huyo, lakini kwa wanaume pia alianza kufanya mabalaa kwani aliifundisha timu ya taifa ya vijana ya Tanzania yeye na Bakari Shime aliipeleka katika AFCON ndogo kule nchini Gabon, akiwa na wanasoka vijana kama Ramadhan Kabwili, Kibwana Shomari, Dickson J...