Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Wilson Nangu afanyiwa upasuaji

Machapisho ya hivi karibuni

Yanga yaiondosha Cosmopolitan kombe la CRDB

Timu ya Yanga SC usiku huu imepata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya mabingwa wa zamani wa Ligi Kuu Tanzania bara, Cosmopolitan zote za Dar es Salaam katika uwanja wa KMC Complex jijini Dar es Salaam mchezo wa kombe la CRDB Cup. Mchezo ulikuwa wa kuvutia kwani Cosmopolitan ilicheza vizuri na kujaribu kulifikia lango la Yanga mara kadhaa na kuna nyakati kidogo ilikuwa wafunge bao lakini mpira ulienda kugonga mwamba. Mabao yote ya Yanga walifungwa na winga wao mpya Bubah Jameh dakika ya 13 na 23, kwa ushindi huo Yanga imetinga raundi ya tatu ya michuano hiyo ikiwa ni bingwa mtetezi.

Tanzania Prisons yahamis Jamhuri Dodoma

BAADA ya kufungiwa kwa Uwanja wa Sokoine, Tanzania Prisons imehamishia mechi zake za Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma — wakati mechi ya Kombe la CRDB watachezea Uwanja wa Halmashauri ya Chunya.

Serikali yaidhinisha marekebisho ya katiba Simba

Serikali kupitia Baraza la Michezo la Taifa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Michezo imeridhia rasmi marekebisho ya Katiba ya Simba Sports Club, hatua inayotarajiwa kuimarisha mfumo wa uendeshaji wa klabu hiyo, kuongeza uwazi wa umiliki na kufungua milango zaidi ya uwekezaji. Akizungumza katika taarifa kwa vyombo vya habari, Msajili wa Vyama vya Michezo Nchini, Abel Mathias Nilangwa, alisema mchakato wa marekebisho hayo umehitimishwa kikamilifu baada ya kukamilika kwa hatua zote za kisheria na kiutawala, ikiwemo kukabidhi rasmi Katiba iliyoidhinishwa kwa uongozi wa klabu. Nilangwa alisema hatua hiyo imefikiwa kufuatia maelekezo ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, aliyetoa msisitizo mapema Februari kuhakikisha mchakato huo unakamilika kabla ya mwezi kuisha kwa maslahi ya klabu, wanachama wake na maendeleo ya michezo kwa ujumla. Kwa mujibu wa Msajili, Simba ilianza mchakato wa mageuzi ya mfumo wake wa uendeshaji mwaka 2018 kwa lengo la kuruhusu uwekezaji. Hata...

KMC timu ya Ligi Kuu bara yawa ya kwanza kutolewa na timu ya mchangani

Licha ya Simba SC inayoshiriki Ligi Kuu bara kushinda mabao 3-0 na kuendelea na mashindano ya kombe la CRDB, lakini timu nyingine ya Ligi Kuu bara kuondoshwa katika michuano hiyo na timu ya daraja la chini ni KMC baada ya kufungwa mabao 3-2 kwa mikwaju ya penalti. KMC waliondoshwa na timu ya first League, Bandari Tanzania kufuatia sare ya mabao 3-3 kwenye uwanja wa Filbert Bayi uliopo Kibaha mkoani Pwani. Matokeo ya michezo ya hatua ya 64 Bora CRDB Bank Federation Cup 2025/2026.

Simba yaendeleza umwamba wake kombe la CRDB

Timu ya Simba SC usiku huu imeichapa bila huruma timu ya Greenland mabao 3-0 mchezo wa kombe la CRDB katika uwanja wa Meja Isamuyo Mbweni jijini Dar es Salaam. Greenland inayotoka mkoani Kagera, imecheza vizuri kwani ingeweza kuchakazwa mabao mengi zaidi, lakini iliwachukua Simba kupata bao la kuongoza dakika ya 13 na mshambuliaji Baraka Mwangosi kabla ya beki wa kushoto Anthony Mligo dakika ya 45 kufunga la pili. Hadi mapumziko Simba walikuwa kileleni kwa mabao hayo mawili, kipindi cha pili Simba walipata bao la tatu kupitia kwa Neo Maema dakika ya 90, kesho watani zao Yanga wataumana na mabingwa wa zamani wa Ligi Kuu bara wakati huo Ligi daraja la kwanza Tanzania bara, Cosmopolitan uwanja wa KMC Complex jijini Dar es Salaam

Kibu Denis atambulishwa Al Nassr

Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania Kibu Dennis ametambulishwa rasmi kwenye Klabu yake mpya ya Al Nassr inayoshiriki Ligi Kuu nchini Libya. Kibu alikuwa mchezaji wa klabu ya Simba SC ya Tanzania inayoshiriki Ligi Kuu bara lakini akiwa hajawahi kubeba ubingwa wa Ligi Kuu bara akiwa na timu hiyo.