Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Uwanja wa Gombani Pemba wageuka kivutio

Machapisho ya hivi karibuni

CAF yaanzisha mashindano mapya

Rais wa Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), Patrice Motsepe, ametangaza rasmi kuanzishwa kwa mashindano mapya ya kimataifa yatakayojulikana kama African Nations League, yenye lengo la kuongeza ushindani na mapato katika soka la Afrika. Mashindano hayo mapya yanachukua nafasi ya michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN), huku yakibuniwa kwa mfumo mpya utakaoleta ushindani mkubwa zaidi na kushirikisha wachezaji wa viwango vya juu wanaocheza ndani na nje ya bara la Afrika. Kwa mujibu wa Motsepe, mashindano hayo yatakuwa na mifumo miwili tofauti ambapo wa kwanza African Nations League Continental, utaendeshwa kwa mfumo wa kanda ambapo timu bora kutoka kila ukanda zitashindana na hatimaye kupata washindi watakaoingia hatua ya fainali itakayofanyika katika nchi mwenyeji. Pili, African Nations League Pan-African, utakuwa na muundo unaofanana na AFCON, ukizikutanisha timu bora zaidi barani Afrika pamoja na wachezaji nyota wanaocheza katika ligi kubwa duniani. Mots...

Taifa Stars yaipiga Macau 6-0 FIFA Series

TIMU ya Tanzania imeibuka na ushindi wa mabao 6-0 dhidi ya Macau katika mchezo wa Kundi B kuwania nafasi tatu michuano ya FIFA Series jioni ya leo Uwanja wa Pele Jijini Kigali, Rwanda. Mabao ya Taifa Stars yamefungwa na mshambuliaji wa Floriana ya Malta, Kokola Charles William M’Mombwa dakika ya 16, nyota wa Yanga SC, beki Bakari Nondo Mwamnyeto dakika ya 26 na kiungo Mudathir Yahya Abbas dakika ya 45. Mengine yamefungwa na mshambuliaji wa JKT Tanzania, Paul Peter Kasunda dakika ya 56, kiungo wa Gotzepe ya Uturuki, Novatus Dismas Miroshi dakika ya 74 na winga wa Rochdale ya England, Tarryn Allarakhia dakika ya 87. Taifa Stars imeangukia kwenye mchezo wa kuwania nafasi ya tatu michuano ya FIFA ya Series mwaka huu baada kufungwa 1-0 na Liechtenstein katika mchezo wa kwanza Alhamisi hapo hapo Uwanja wa Pele.

CAF yaanza kumeguka, Veron aachia ngazi

Veron Mosengo-Omba amestaafu rasmi kama Katibu Mkuu wa Shirikisho la soka barani Afrika CAF. Sura muhimu inafungwa katika katika shirikisho la soka Afrika CAF ambapo Mosengo-Omba alikuwa na jukumu muhimu katika usimamizi na mageuzi ya kandanda ya Afrika. Kwasasa nguvu anazielekeza katika majukumu mengine ya kisoka akiwa miongoni mwa wagombea wa Rais wa shirikisho la soka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Uchaguzi ambao ungefanyika mwezi huu ulisogezwa mbele baada ya FIFA kubaini uwepo wa uhaba wa fedha za kuandaa uchaguzi huo.

Azam FC waifuata Singida Black Stars kibabe

Kikosi cha Azam FC kimeondoka leo jijini Dar es Salaam kuelekea Singida kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Singida Black Stars. Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Aprili Mosi, mwaka huu ambapo Azam FC itakuwa ikisaka alama muhimu katika mbio za ligi hiyo, huku Singida Black Stars nao wakilenga kutumia faida ya uwanja wa nyumbani.

MWANZO WA AFRIKA

Inaandikwa na Fikiri Salum HISTORIA ya Afrika ni historia ya bara hilo lililo asili ya binadamu wote, kwa ujumla, historia ni kumbukumbu ya maisha ya mwanadamu duniani hasa Ile tarehe iliyosajiliwa na kuhifadhiwa katika vitabu, maandishi mbalimbali, na simulizi au hekaya za mapokeo. Ingawa historia iliyobebwa katika simulizi za hekaya huchukuliwa na baadhi kuwa haina nguvu kwa kukosa ithibati ya maandishi, bado hivi ni vyanzo muhimu vya historia. Mara nyingi historia iliyoko katika maandishi huwa imehifadhiwa katika simulizi na hekaya kwa muda mrefu kabla ya kuandikwa. HISTORIA YA AFRIKA Hapo kale, bara la Afrika lilishuhudia matukio mengi ya harakati za mwanadamu kuliko mabara mengine ya ulimwenguni. Wataalamu wa athali wamegundua athali za Zamadamu zinarudi nyuma kufikia hadi miaka ya milioni nne, na athali za ustaarabu wa Wamisri wa kale huko Misri na Wafoinike huko Tunis na sehemu nyinginezo za Afrika kaskazini katika karne ya 9 KK. Harakati za madola makubwa ya Wazungu na Waarabu ...

Adam Salamba aigomea Coastal Union kisa fedha zake

Mshambuliaji wa Coastal Union, Adam Salamba, ameripotiwa kujiweka kando na kikosi cha ‘Wagosi wa Kaya’ kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni kutokamilishiwa kiasi cha fedha zake za usajili. Inaelezwa kuwa Salamba, aliyejiunga na timu hiyo Agosti 1, 2025, ameshaondoka kambini na hatakuwa sehemu ya kikosi kitakachochuana na Simba Aprili 2, 2026, hadi hapo stahiki zake zitakapolipwa. Hata hivyo uongozi wa Coastal Union umekiri kuwepo kwa deni hilo na kusema mchakato wa kumlipa unaendelea, huku wakitamani mchezaji huyo angeendelea na mazoezi wakati taratibu zikikamilishwa. Salamba amewahi kuzitumikia klabu kadhaa ikiwemo Simba, Namungo, na Stand United, pamoja na kucheza soka la kulipwa nchini Libya, Misri, na Kuwait.