Klabu ya Simba SC imezidi kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao baada ya kufanikiwa kunasa saini ya kiungo fundi wa Pamba Jiji, Kelvin Nashon (25), ambaye amesaini mkataba wa miaka mitatu kuitumikia klabu hiyo ya Msimbazi. Nashon anatarajiwa kujiunga rasmi na wekundu wa Msimbazi mara baada ya msimu huu kukamilika, usajili ambao umeanza kuzua gumzo kubwa miongoni mwa wachambuzi wa soka kutokana na uwezo mkubwa wa kumiliki dimba na kuanzisha mashambulizi alionao nyota huyo. Hatua hii ya Simba ni mwendelezo wa mkakati wao wa kusajili damu changa na zenye vipaji ili kurejesha utawala wao kwenye soka la ndani na kimataifa, huku mashabiki wakimsubiri kwa hamu "Balaa" huyo jipya atakapoanza kuwasha moto katikati ya uwanja akiwa na jezi nyekundu na nyeupe. Simba walianza kumuania Nashoni tangia anaichezea Singida Black Stars hivyo kumsajili sasa hivi ni kama kutimiza ahadi yao ya kumsajili.
MAMBO UWANJANI
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com