Machapisho

Watoto wa wanamuziki, wageuka lulu mwenye soka

Picha
Dr Remmy Ongalla wa Ochestra Matimila na Bwammy Walomuna wa Ochestra Mangelepa Viongozi wa bendi za Muziki huku watoto wao wakiwa miamba ya Soka. Kali Ongala (jina kamili Kalimangonga Sam Daniel Ongallah Rampling) ni mwanasoka wa zamani na kocha wa mpira wa miguu kutoka Tanzania. Ni mtoto wa mwanamuziki mashuhuri wa Tanzania, marehemu Remmy Ongala, alizaliwa tarehe 31 Agosti 1979 jijini London, Uingereza. Licha ya kuzaliwa Uingereza, alikulia na kupata malezi yake jijini Dar es Salaam, Tanzania, ambapo alianza kupata hamu ya michezo na soka tangu utotoni. Safari yake ya soka ilianza rasmi mwaka 1999 alipojijiunga na Young Africans SC (Yanga) kutoka Bajaro FC, akijitengenezea sifa kama kiungo mshambuliaji mwenye ufundi mkubwa. Baada ya mafanikio yake nchini Tanzania, alifanya majaribio ya kucheza soka nchini Uingereza na Marekani kabla ya kupata mikataba ya kucheza nchini Uswidi, akichezea klabu za FC Väsby United na GIF Sundsvall kati ya mwaka 2007 na 2011. Baada ya kustaafu kutoka sok...

TRA yaisimamisha Simba SC

Picha
TIMU ya Simba SC imetoa sare ya bila mabao na wenyeji, TRA United katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha. Kwa matokeo hayo, TRA inayofundishwa na Kocha Mrundi, Ettienne Ndayiragijje inafikisha pointi 24 na kupanda kwa nafasi moja hadi ya saba ikiizidi tu wastani wa mabao Dodoma Jiji FC baada ya wote kucheza mechi 18. Kwa upande wao Simba SC wanafikisha pointi 36 katika mchezo wa 17, ingawa wanabaki nafasi ya pili wakizidiwa pointi nane na mabingwa watetezi, Yanga ambao hata hivyo wamecheza mechi moja zaidi.

Kocha mwenye jina kubwa DR Congo, apewa Singida Black Stars

Picha
Singida Black Stars imepata mrithi wa mikoba ya David Ouma baada ya kukamilisha makubaliano na kocha mwenye jina kubwa kutoka DR Congo, Papi Kimoto. Nini unapaswa kujua kuhusu usajili huu wa benchi la ufundi? Taarifa kutoka nchini DR Congo zinathibitisha kuwa pande zote mbili zimeingia "ndoa" mpya baada ya Kimoto kusaini mkataba rasmi jana asubuhi. Kimoto anatua akitokea klabu ya Union Maniema, ambayo msimu huu imeonyesha makali kwa kufika hatua ya 16 bora katika Kombe la Shirikisho Afrika (CAF CC). Msaidizi na Watu Wake: Kocha huyu haji peke yake; anatarajiwa kutua nchini wiki hii akiwa na wasaidizi wake wawili kuanza kazi mara moja. Inaelezwa kuwa Singida BS walihamishia nguvu kwa Kimoto baada ya dili la kocha Guy Bukasa kugonga mwamba kutokana na majukumu yake ya timu ya taifa ya vijana ya DR Congo. Sasa ni rasmi, upepo mpya umeanza kuvuma kule Singida! Je, unaona Papi Kimoto ndiye mtu sahihi wa kurudisha makali ya Singida Black Stars kwenye Ligi Kuu?

Mbeya City sare sare na Azam FC

Picha
TIMU ya Azam FC imelazimishwa sare ya bila kufungana na wenyeji, Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati mkoani Manyara. Kwa matokeo hayo, Azam FC inafikisha pointi 34 katika mchezo wa 18, ikibaki nafasi ya tatu, wakati Mbeya City inafikisha pointi 17 katika mchezo wa 18 pia, nayo ikibaki nafasi ya 12 kwenye Ligi Kuu inayoshirikisha timu 16. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.

Simba imevunja mkataba wa Sowah

Picha
Klabu ya Simba SC imevunja mkataba na aliyekuwa Mshambuliaji wake, Jonathan Sowah kutokana na kutoridhishwa na tabia yake.

UKRISTO NI CHIMBUKO LA UYAHUDI- 7

Picha
Inaandikwa na Fikiri Salum Ilipoishia  BAADAYE akawa katika mji mkubwa wa Antiokia, katika taarifa ya Luka tumemwona tena Yerusalemu alipokutana na Paulo na kushauriana juu ya kupokea wapagani katika Ukristo. Endelea Agano jipya ina nyaraka mbili zilizoandaliwa kwa jina lake, kumbukumbu ya kale inasema alifika mpaka Roma, hapo aliuawa pamoja na Paulo katika mateso ya kwanza ya Wakristo chini ya serikali. Petro ni mfano mzuri wa nguvu na udhaifu katika maisha ya Kikristo, alikuwa na moyo mkuu kumtetea Yesu kwa upanga asikamatwe- lakini mpaka siku Ile hakuelewa kwamba njia ya Yesu si njia ya silaha. Alitaka kuwa karibu na Yesu lakini kwa hofu akamkana, alimwingiza katika kanisa jemedari mpagani lakini baadaye akawaogopa waliosema kwamba mpagani asiingie katika ushirika mpaka awe ametahiriwa na kuwa Myahudi kwanza. Mwishoni mwa maisha yake, Petro akawa shahidi wa damu kwa bwana wake kule Roma akafa msalabani kama Yesu. Kanisa la Roma linamkumbuka kama Askofu' wake wa kwanza, kila Papa...