Machapisho

Samatta afunga bao lake la kwanza Ufaransa

Picha
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Sammata leo amefunga goli lake La kwanza tangu ajiunge na Le havre ya nchini ufaransa dhidi ya OG Nice Samatta ameweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kufunga Goli ligi kuu nchini Ufaransa.

Azam FC yaichakaza Fountain Gate 4-0

Picha
Klabu ya Azam imetinga robo fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB (FA Cup) kufuatia ushindi wa 4-0 dhidi ya Fountain Gate FC katika dimba la Azam Complex, Chamazi kwenye mchezo wa hatua ya 16 bora. Wanalambalamba hao wameungana na Simba, Yanga, Coastal Union, JKT Tanzania, TRA United, Singida BS na Mashujaa kwenye hatua hiyo. Mabao ya Azam FC yamefungwa na Japhte Kitambala dakika ya 15, Abah Abbel dakika ya 21, Ashrafu Kibeku dakika ya 81 na Alobigast Kyobya dakika ya 90.

Simba yakata ngebe za Dodoma Jiji

Picha
TIMU ya Simba SC imefanikiwa kwenda Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Dodoma Jiji FC jioni ya leo Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arisha. Mabao ya Simba SC yamefungwa na mshambuliaji Suleiman Abdallah Mwalimu mawili dakika ya 54 na 67 na winga wa kushoto Muivory Coast, Alain Anicet Oura dakika ya 60 baada ya kiungo Khleffin Salum Hamdoun kuanza kuifungia Dodoma Jiji FC dakika ya tisa.

Aziz Ki azidi kuwasha moto Libya

Picha
Stephanie Azizi Ki leo ameendelea kuonesha makali yake kwenye ligi kuu ya Libya akiwa na klabu yake ya Al-Ittihad SC. Aziz Ki leo amefanikiwa kufunga bao 1 kwenye ushindi wa mabao 4-1 walioupata Al-Ittihad dhidi ya klabu ya Shabab Al Ghal kwenye mchezo wa ligi kuu ya Libya. Hili sasa linakuwa ni goli lake la pili kwenye michezo 6 aliyocheza mpaka sasa ndani ya klabu hiyo kwenye ligi kuu msimu huu.

Singida Black Stars siyo ya mchezo mchezo, yaiua Mbeya City 5-1

Picha
TIMU ya Singida Black Stars imefanikiwa kwenda Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Mbeya City Uwanja wa Airtel Mwigulu mjini Singida. Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na Khalid Aucho, winga wa kulia Mgambia, Lamin Jarjou, beki wa kushoto Mghana Ibrahim Imoro mawili na mshambuliajii kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Malanga Horso Mwaku.

TRA yaiua Namungo pale pale kwa Majaliwa

Picha
TIMU ya TRA United imetinga Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji, Namungo FC jioni ya leo Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi. Mabao yote ya TRA United inayofundishwa na Kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania, Mrundi Etienne Ndayiragijje yamefungwa na wachezaji wazawa, winga Denis Nkane na kiungo Ally Ng'azi.

Maximo: KMC itashuka daraja

Picha
Kocha Mbrazili Marcio Maximo ameibuka na kutoa ukweli mchungu kuhusu hali ya KMC FC inayozidi kuporomoka kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara. Baada ya kuondoka kwa Abdallah Mohamed ‘Bares’ (aliyechukua nafasi ya Maximo), Maximo ameweka wazi kuwa tatizo la KMC ni kubwa kuliko mwalimu yeyote: Makosa ya Msingi: Maximo amekiri kuwa yalifanyika makosa wakati wa maandalizi ya mwanzo wa msimu (Pre-season) kipindi yeye akiwa kocha mkuu. Ubora wa Wachezaji: Amesema baadhi ya wachezaji kikosini hawana ubora wa kuhimili presha ya ushindani wa Ligi Kuu. Hali ya Hatari: KMC sasa inashika mkia (nafasi ya mwisho) ikiwa na pointi 8 pekee baada ya mechi 18, huku ikiruhusu mabao 33! "Ingekuwa inawezekana, msimu ungeanza upya ili kikosi kiandaliwe upya, lakini kwa sasa timu itaendelea kubeba matatizo yaleyale," amesema Maximo kupitia gazeti la Mwanaspoti