Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Abdulrazack Hamza ndio basi tena Simba

Machapisho ya hivi karibuni

Nane zilizofuzu robo fainali kombe la Shirikisho Afrika hizi hapa

Hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika imekamilika Jumapili 12 Februari 2026 na timu nane zikitinga hatua ya robo fainali. USM Alger, OC Safi, Wydad Casablanca, AS Maniema Union, CR Belouizdad, AS OtohΓ΄, Zamalek SC, na Al Masry SC zote zimefuzu hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika. Timu hizo zinasubiri droo, iliyopangwa kufanyika Jumanne, Februari 17, huko Cairo, ili kujua wapinzani wao katika hatua hiyo.

Makonda amwagiza msajili wa vyama vya michezo kuwapa majibu ya mchakato wa mabadiliko Simba SC haraka

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amemtaka Msajili wa Vyama vya Michezo nchini, Abel Ngilangwa kuipa Simba majibu ya kinachoendelea kuhusu mchakato wa mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji. Makonda amesema kuwa msajili anatakiwa kabla ya mwezi huu kumalizika, awe ametoa majibu kwa Wanasimba. "Msajili wa michezo nilitaka mkamilishe taratibu za Simba. Na nilitaka niwahakikishie kwamba katika kipindi ambacho sheria na kanuni zitafuatwa sana ni hiki cha uongozi wangu. "Kamilisha na ikiwezekana kabla ya mwezi huu uwape majibu Wanasimba. Tunachotaka sisi tuone timu hizi zikifanya vizuri. Kabla ya mwezi huu, jambo hili liwe limekamilika," amesema Makonda.

Kashfa ya kupanga matokeo Al Ahly na AS FAR Rabat, CAF yaanza uchunguzi

Shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) linalaani vikali matukio yasiyokubalika yaliyotokea wakati wa mechi ya Ligi ya Mabingwa kati ya Al Ahly ya Misri na ASFAR ya Morocco mjini Cairo Jumapili, Februari 15, 2026. CAF imelipeleka suala hilo kwenye Bodi ya Nidhamu kwa uchunguzi na imetaka hatua stahiki zichukuliwe kwa watakaobainika kuhusika baada ya Mashabiki kutupa chupa ndani ya Uwanja na kuzua vurugu. Katika mchezo huo timu zote zilitoka sare ya 0-0 na kutinga hatua ya robo fainali ya klabu Bingwa Afrika.

Al Hilal Omduman yaitelemsha Simba nafasi ya sita CAF

Klabu ya Al Hilal Omduman ya Sudan imefanikiwa kuishusha Simba SC ya Tanzania katika orodha ya viwango vya ubora vimavyotolewa na Shirikisho la soka barani Afrika, CAF. Al Hilal ambao jana wamefanikiwa kutinga robo fainali ya michuano hiyo na Simba SC kushindwa kuingia robo fainali ikiambulia nafasi ya mwisho kwenye kundi D. Kwa mujibu wa viwango vya ubora vya CAF, Al Hilal imeishusha Simba kwenye nafasi ya sita na Simba kuangukia nafasi ya name. 1. πŸ‡ͺπŸ‡¬ Al Ahly - 66 pts 2. πŸ‡ΏπŸ‡¦ Sundowns - 58 pts 3. πŸ‡ΉπŸ‡³ Esperance Tunis - 53 pts 4. πŸ‡²πŸ‡¦ RS Berkane - 52 pts 5. πŸ‡ͺπŸ‡¬ Pyramids - 48 pts 6. πŸ‡ΈπŸ‡© Al Hilal - 39 pts 7. πŸ‡ͺπŸ‡¬ Zamalek - 39 pts πŸ–. πŸ‡ΉπŸ‡Ώ π’π’π¦π›πš - πŸ‘πŸ– 𝐩𝐭𝐬 9. πŸ‡©πŸ‡Ώ USMA - 37 pts 𝟏𝟎. πŸ‡ΉπŸ‡Ώ 𝐘𝐚𝐧𝐠𝐚 - πŸ‘πŸ“ 𝐩𝐭𝐬 Al Hilal Omduman ya Sudan

Yanga yapaa nafasi mbili viwango CAF

Klabu ya Yanga imepanda kwa nafasi 2 kwenye rink za CAF kutoka nafasi ya 12 msimu uliopita mpaka nafasi ya 10 baada ya hatua ya makundi. Yanga wamefikisha alama 35 kwenye msimamo, kwa upande wa Simba wao wameshuka kwa nafasi 3 kutoka nafasi ya 5 mpaka nafasi ya 8 baada ya michuano ya msimu huu huku wakifikisha alama 38. Ikumbukwe, misimu mitatu nyuma Yanga walikuwa kwenye nafasi ya 80, hii inaashiria improvement kubwa mno sana.

Gamondi asaini mkataba kuwa kocha mkuu Taifa Stars

Rasmi kaimu kocha mkuu wa timu ya taifa, Taifa Stars, Miguel Gamondi amesaini mkataba wa kuitumikia Taifa Stars kama kocha mkuu Kila kitu kimekamilika na mkataba umesainiwa Gamondi ni balaa jipya Taifa Stars