Timu ya Simba SC ya Tanzania usiku huu imepata ushindi wake wa kwanza kwenye michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika hatua ya makundi, baada ya kuilaza Stade Malien ya Mali bao 1-0 uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam. Goli pekee la ushindi limefungwa na kiungo mshambuliaji Anicet Oura dakika ya pili ya mchezo, ushindi ambao unaifanya Simba kufikisha pointi 5 lakini ikisalia nafasi ya mwisho. Wakati huo huo timu ya Esperance inaungana na Stade Malien baada ya kushinda mabao 2-0 dhidi ya Petro de Luanda na kufikisha pointi 9 huku Malien licha ya kufungwa imefikisha pointi 11 na kukwea nafasi ya kwanza.
MAMBO UWANJANI
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com