Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2018

Zidane abwaga manyanga Real Madrid

Picha
Baada ya kuiwezesha kutwaa tena taji la Ligi ya Mabingwa barani Ulaya, kocha wa Real Madrid, Zinedine Zidane "Zizzou" ameachia ngazi kuinoa timu hiyo. Taarifa zilizotangazwa na vyombo mbalimbali vya habari barani Ulaya vinasema Zidane ameachia ngazi baada ya kuiwezesha timu hiyo kutwaa taji la tatu Ulaya na moja la La Liga, huku akiwa na rekodi ya kushinda mechi 104 na kutoka sare mara 29 jumla akibeba mataji tisa kwa wakati wote akiwa na Real Madrid. Zidane amesema bado anaipenda Real Madrid na ataendelea kuishabikia katika kipindi chake chote cha maisha ya soka, Zidane amewahi pia kuichezsa klabu hiyo pamoja na timu ya taifa lake ya Ufaransa na kujipatia umaarufu mkubwa enzi zake Zinedine Zidane ameachia ngazi Real Madrid

Wachezaji Singida United wapewa mifuko 50 ya Cement kila mmoja

Picha
Na Mrisho Hassan. Arusha Akizungumza na vyombo vya habari hiii leo,Mkurugenzi wa Singida United Ndg. Festo Sanga amesema, Uongozi wa klabu kuanzia chini ya Rais na mwenyekiti wa timu hiyo wameamua kutoa mifuko ya Cement kwa kila mchezaji na mtumishi wa klabu hiyo kama shukrani na pongezi kwa namna walivyopambana kufanikisha sehemu ya malengo ya klabu kwa msimu wa 2017/2018. Tukio hilo ambalo kama sila kwanza hapa nchini, basi ni tukio la heshima na upendo wa hali ya juu katika kuimarisha mahusiano ya klabu na wachezaji, Singida United imetoa mifuko hiyo kama alama katika maisha ya wachezaji na watumishi kwamba katika maisha ya soka kuna maisha mengine ya kuanza kujitegemea mapema. Uongozi wa Singida United umetoa mifuko 50 ya Cement kwa kila mchezaji mmoja na mwalimu wao

Tshishimbu, Ajibu na Kamuoko wapaana Yanga Kenya

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Kikosi cha wachezaji 20 cha Yanga Sc kinatarajia kusafiri kuelekea Nakuru nchini Kenya jioni ya leo kwa ajili ya kushiriki michuano ya Sportpesa Super Cup. Yanga imewaacha nyumbani mshambuliaji wake Mzambia Obrey Chirwa, mabeki Juma Abdul na Kelvin Yondani lakini katika kikosi chake kinachoanza safari muda huu wamo Mzimbabwe Thabani Kamusoko, Ibrahim Ajibu na Mkongoman, Papy Kabamba Tshishimbi. Kikosi kamili kinachoelekea Kenya ni pamoja na makipa Youthe Rostand, Ramadhan Kabwili, mabeki Hassan Kessy, Mwinyi Haji, Abdallah Shaibu, Pato Ngonyani, Viungo Baruani Akilimali, Pius Buswita, Ibrahim Ajibu, Maka Edward, Thabani Kamusoko, Juma Mahadhi, Said Makapu, Said Musa, Papy Tshishimbi, Yusuf Mhilu na Raphael Daudi, washambuliaji ni Yohana Nkomola, Matheo Antony na Amissi Tambwe, Yanga itashuka dimbani Jumatatu ijayo kucheza na Kakamega Homeboys katika uwanja wa Afraha mjini Nakuru Yanga wanaelekea Kenya kushiriki Sportpesa Super Cup

Simba yawatema Okwi na Bocco safari ya Kenya

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Simba Sc imeondoka asubuhi ya leo kuelekea nchini Kenya kushiriki michuano ya Sportpesa Super Cup lakini katika kikosi chake imeachana na nyota wake karibu wote waliofanikisha ubingwa wa Bara wakiwemo vinara wa mabao, Nahodha John Raphael Bocco na Mganda, Emmanuel Okwi. Pia mabingwa hao imewaacha Waghana wake wote beki Asante Kwasi, kiungo James Kotei na mshambuliaji Nicolaus Gyan, beki Mganda Juuko Murushid na Mrundi, mshambuliaji Laudit Mavugo. Waliosafiri leo ni makipa Aishi Manula, Said Mohamed, mabeki Ally Salim, Ally Shomari, Paul Bukaba, Erasto Nyoni, Yusuf Mlipili, Mohamed Tshabalala, viungo Jonas Mkude, Shomari Kapombe, Mzamiru Yassin, Said Ndemla, Haruna Niyonzima, Shiza Kichuya, washambuliaji ni Rashid Juma, Moses Kitandu, pia imemjumuhisha mshambuliaji wake mpya kutoka Majimaji Songea, Marcel Kaheza lakini kama ameenda kuralii tu kwani kanuni za mashundano hayo haziruhusu wachezaji wapya Simba imeondoka leo

Ngasa kurejea Yanga kwa mara ya tatu

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Klabu ya Yanga iko mbioni kumalizana na kiungo mshambuliaji Mrisho Khalfan Ngasa wa Ndanda Fc ya Mtwara kwa mkataba wa mwaka mmoja imebainika, taarifa zilizosambaa jana zinasema tayari mchezaji huyo ameshazungumza na viongozi wa klabu hiyo na muda wowote kuanzia sasa anaweza kumwaga wino. Ngasa amecheza vizuri akiwa na Ndanda Fc na kuipigania timu hiyo kusalia Ligi Kuu Bara mpaka mabosi wa Yanga kuvutiwa naye na kuamua kumrejesha tena mitaa ya Jangwani kwa mara ya tatu, Ngasa alijiunga Yanga kwa mara ya kwanza mwaka 2006 akitokea Kagera Sugar ya Bukoba kabla hajanunuliwa na Azam Fc kwa usajili uliovunja rekodi mwaka 2010, nyota huyo akidumu Azam Fc na baadaye akajiunga na Simba kabla hajarejea Yanga kwa mara pili. Ngasa hakudumu sana Jangwani kwani akajiunga na Free State Stars ya Afrika Kusini ambako nako hakudumu akavunja mkataba na kujiunga na Fanja ya Oman, pia hakudumu akarejea nyumbani Tanzania na kujiunga na Mbeya City aliyodumu nayo kwa nusu msi

Mkwasa awatoa wasiwasi Yanga, adai hata Simba nao ni choka mbaya

Picha
Na Albert Babu. Dar es Salaam Katibu mkuu wa klabu ya soka ya Yanga, Charles Boniface Mkwasa amewatoa wasiwasi wapenzi na mashabiki wa Yanga kuwa timu yao itafanya usajili wa kishindo lakini haitaruhusu mchezaji wake mwingine kuhamia timu nyingine mpaka pale yenyewe itakaporidhia ama kumuuza. Akizungumza na Mambo Uwanjani, Mkwasa amesema hata watani zao Simba nao wana njaa ila wanachofanya sasa ni propaganda tu, kuhusu kumkosa Adamu Salamba na kutua Simba,Mkwasa amedai Lipuli na Simba ni damu moja hivyo isingewezekana wao kumpata Salamba. "Yanga tunashikiriki michezo ya kimataifa ingemsaidia Salamba kuonekana nje ya nchi, amekwenda kujimaliza Msimbazi", amesema Mkwasa, kuhusu tetesi za kuondoka nyota wao kuanzia Juma Abdul, Papy Kabamba Tshishimbi, AndrewVicent 'Dante' na Kelvin Yondan wanaodaiwa kujiunga na Simba pamoja na Azam, Mkwasa amedai hakuna mpango kama huo. Mkwasa ambaye aliwahi kuichezea na kuinoa Yanga miaka iliyopita, amesema Yanga haitakubali kumwach

Samatta aenda Makka kumshukuru Mwenyezi Mungu

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga katika timu ya KRC Genk ya Ubelgiji ameenda kufanya ibada ndogo ya Hijja katika mji wa Makka na Madina kama sehemu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kufuatia kumaliza vema msimu kwa kuiwezesha timu yake ya Genk kupata tiketi ya kushiriki European League msimu ujao. Katika mtandao wake, Mbwana Samatta ambaye pia ni nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars ameonekana akiwa na rafiki yake ambaye naye ni mchezaji wa Genk, Omar Colley wakiwa katika msikiti wa Haram wakiadhimisha ibada ya Ihram ambapo waumini wa Kiislamu wanaouruhusiwa kufika hapo ni wale wasiofanya maovu. Eneo hilo linaloaminika kuwa ni la Mwenyezi Mungu, Samatta alienda kushukuru hasa baada ya kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Zulte Weregem katika uwanja wa Luminus Arena mjini Genk, Samatta anatazamiwa kuwasili nchini hivi karibuni akijiandaa kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya rafiki yake Ali Kiba Mb

WACHEZAJI WAPYA WAZUIWA KUCHEZA SPORTPESA SUPER CUP

Picha
Na Mwandishi Wetu. Kenya Waandaaji wa michuano wa soka ya Sportpesa Super Cup 2018 wamepiga marufuku vilabu vitakavyowatumia wachezaji wapya na kutaka kila klabu itakayoshiriki michuano hiyo kutumia wachezaji wake walewale waliocheza ligi. Michuano ya mwaka huu inatarajia kuanza Juni 3 kwa mchezo kati ya mabingwa wa soka wa Tanzania Bara, Simba Sc na Kariobangi Sharks ya Kenya na kufuatiwa na watani wao Yanga siku inayofuata Juni 4 ikicheza na Kakamega Homeboys pia ya Kenya. Michuano hiyo ambapo bingwa hujipatia dola 30,000 na kupata tiketi ya kwenda nchini Uingereza kucheza na Everton, itaendelea tena Juni 4 Singida United ikiumana na AFC Leopards na Gor Mahia itacheza na JKUya Zanzibar, tayari Simba na Yanga zimeshaanza kusajili wachezaji wapya na zikitaka kuwajaribu katika michuano hiyo hivyo sasa hawaturuhusiwa kuwatumia

KIROHO SAFI MEXIME AENDA KUMRITHI NSAJIGWA YANGA

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Kocha mkuu wa timu ya Kagera Sugar, Mecky Mexime amrkubali kuachia ngazi katika klabu yake hiyo na kwenda kuwa kocha msaidizi wa mabingwa wa zamani wa Ligi Kuu Bara, Yanga Sc akichukua nafasi ya Shadrack Nsajigwa anayetarajia kufutwa kazi. Tayari Mexime ameshaaga Kagera Sugar ambao wako mbioni kumalizana na kocha wa Mwadui Fc ili akachukue nafasi yake, Mexime alikuwa akitakiwa na Yanga tangu msimu uliopita lakini ikashindikana na sasa mambo yametimia kutua kwa kocha huyo mwenye rekodi nzuri ya kuifunga Simba, hivi karibuni Kagera Sugar iliifunga Simba bao 1-0 katika mchezo wa kukabidhiwa kombe la ubingwa wa bara Simba mbele ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dr John Pombe Magufuli. Mexime aliwahi kuichezea timu ya Mtibwa Sugar na Taifa Stars akihudumu kama nahodha na baadaye akawa kocha wa timu hiyo kabla ya kuhamia Kagera Sugar na msimu uliopita alitangazwa kuwa kocha bora Mecky Mexime anaenda Yanga

KUTINYU AMFUATA DONALD NGOMA AZAM FC

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Kiungo Mzimbabwe Tafadwa Raphael Kutinyu amejiunga na klabu ya Azam Fc kwa mkataba wa mwaka mmoja akitokea Singida United ya mkoani Singida, huo unakuwa usajili wa pili wa Azam Fc ambayo tayari imemsajili Mzimbabwe mwingine kutoka Yanga, Donald Ngoma. Usajili wa Kutinyu ni mapendekezo ya kocha mpya wa Azam Fc,Mholanzi Hans Van der Pluijm ambaye naye alikuwa akiinoa Singida United na analizia kibarua chake keshokutwa Jumamosi akiiongoza timu hiyo itakapoumana na Mtibwa Sugar katika fainali ya kombe la Azam Sports Federation Cup. Azam Fc pia inatajwa kumwania mlinzi wa kulia wa Yanga, Juma Abdul Mnyamani ambapo taarifa za awali zinasema beki huyo amemaliza mkataba na huenda akasaini mkataba wa kuitumikia Azam msimu ujao Tafadzwa Kutinyu anajiunga na Azam Fc

SPORTPESA SUPER CUP KUZIKUTANISHA TENA SIMBA NA YANGA

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Kwa vyovyote mahasimu wa soka la bongo Simba na Yanga wakakutana tena nchini Kenya katika michuano ya Sportpesa Super Cup inayotarajia kuanza Juni 3 mwaka huu kwa mabingwa wa soka nchini, Simba kuumana na Kariobangi Sharks ya Kenya katika uwanja wa Afraha. Juni 4 washindi wa tatu wa Ligi Kuu Bara, Yanga Sc wataumana na Kakamega Homeboys pia ya Kenya na kama timu hizo zitashinda kwenye mechi zao hizo basi zitakutana katika nusu fainali na kufanya timu hizo zikutane kwa mara ya tatu ndani ya mwaka huu. Tayari Simba imeshatangaza kuyapania mashindano hayo na itasafirisha kikosi chake cha kwanza kilichotwaa ubingwa wa Tanzania Bara na dhamira yao mwaka huu ni kushinda taji la michuano hiyo ili wapate tiketi ya kwenda nchini Uingereza kucheza na Everton kama wadhamini wa michuano hiyo wanavyotaka, Yanga nao wameahidi kutoa ushindani katika michuano hiyo baada yakushindwa kwenye ligi yanyumbani Simba na Yanga zitakutana Kenya 

KAHEZA ATOBOA SIRI KILICHOMPELEKA SIMBA

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Mshambuliaji wa Majimaji ya Songea ambayo jana imetelemka daraja, Marcel Boniventure Kaheza ametoboa siri iliyopelekea kujiunga na mabingwa wa soka nchini Simba Sc. Akizungumza na Mambo Uwanjani,Kaheza aliyeifungua Majimaji mabao 14 amedai ameamua kuachana na timu hiyo kwakuwa hajalipwa fedha zake za usajili huku akicheleweshewa mshahara wake, Kaheza ambaye tayari amesaini mkataba wa miaka miwili Simba Sc amedai viongozi wa Majimaji wamechangiakuishusha daraja. Mchezaji bora huyo wa mwezi Aprili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara amedai kushangazwa na uongo wa viongozi wa Majimaji ambao wamechangia timu hiyo kupotea, Kaheza amesema yeye bado alikuwa na mapenzi na timu hiyo lakini kwakuwa hakuna fedha ameamua kujiunga na Simba ambao wamemuahidi maisha bora Marcel Kaheza

ALBUM YA NGWEA YAJA

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Kundi la muziki wa kizazi kipya la Chemba Squad lenye maskani yake jijini Dodoma linatarajia kuachia album ya aliyekuwa nsanii wao marehemu Albert Mangwea 'Ngwea' itakayojumlisha baadhi ya nyimbo zake mpya na za zamani inatoka hivi karibuni. Akizungumza jana wakati wa kuandhimisha kumbukumbu ya miaka mitano ya kifo chake, M To the P amesema ujio wa album ya Ngwea ndio mipango yao kwa sasa na amewataka wapenzi na mashabiki wa msanii huyo kujiandaa kupokea album hiyo. M To the P ambaye alikuwa sambamba na Ngwea nchini Afrika Kusini kabla ya kufikwa na mauti huku naye akiwa hoi hospitalini, amedai wameamua kuitoa album ya Ngwea ili kurejesha enzi za kutamba kwa kundi lao na msanii huyo, aidha msanii huyo amewataka wasanii wanaotumia sauti ya Ngwea kuacha kufanya hivyo kwani sheria ya Hakimiliki itachukua mkondo wake Marehemu Albert Mangwea 

SALAMBA ASAINI SIMBA MIAKA MITATU

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Klabu ya Simba imeanza kufanyia kazi mapendekezo ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dr John Pombe Magufuli aliyewataka kubadilika na leo wamemsainisha straika wa Lipuli ya Iringa, Adam Salamba kwa mkataba wa miaka mitatu. Salamba ilikuwa atue Azam Fc hasa baada ya uongozi wa Lipuli kukataa maombi ya Yanga Sc ambao walituma maombi ya kumuhitaji nyota huyo ili akawasaidie kwa mkopo katika michuano ya kombe la Shirikisho hatua ya makundi. Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah "Try Again" amethibitisha usajili wa mshambuliaji huyo chipukizi alifikishwa mbele ya bilionea Mohamed Dewji 'MO: Adam Salamba (Wa kwanza kushoto) amesaini mkataba wa miaka mitatu Simba Sc

Yanga yatobolewa matatu na Azam Fc

Picha
Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam Klabu bingwa Afrika mashariki na kati, Azam Fc usiku huu imeilaza Yanga Sc mabao 3-1 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ukiwa ni mchezo wa kufunga pazia. Azam Fc walianza kuandikisha kalamu ya mabao kupitia kwa Yahya Zayd dakika ya 4 kipindi cha kwanza ambalo lilidumu hadi mapumziko, kipindi cha pili Yanga walirudi na kasi na kufanikiwa kusawazisha kupitia kwa Mateo Antony dakika ya 49 kabla ya dakika ya 51 Azam kuongeza bao la pili lililofungwa na Shaaban Iddi Chilunda na dakika 67 Salum Abubakar akaiandikia Azam bao la tatu. Kwa matokeo hayo Azam imemaliza katika nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Simba ikifikisha pointi 58 huku Yanga ikiwa ya tatu na pointi zake 52 Azam imetoboa matundu matatu kwa Yanga leo

Simba yamaliza kwa sare, Majimaji na Njombe zaipa kisogo Ligi Kuu Bara

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Timu ya soka ya Simba Sc ya jijini Dar es Salaam jioni ya leo imemaliza Ligi Kuu Bara kwa heshima ya aina yake baada ya kuilazimisha sare ya kufungana bao 1-1 Majimaji Fc katika uwanja wa Majimaji mjini Songea. Kwa matokeo hayo Simba imefikisha pointi 69 na ikiwa mabingwa wa Tanzania Bara msimu huu huku timu ya Majimaji ikiwa imetelemka daraja ikiungana na Njombe Mji, Majimaji walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia Marcel Kaheza kabla ya Simba kusawazisha kwa penalti kupitia Haruna Niyonzima ambaye pia alikosa penalti iliyotaka kuzaa bao la pili iliyppanguliwa na kipa wa Majimaji, Hashim Mussa. Matokeo mengine Mbao Fc 1 Ruvu Shooting 1 uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Mtibwa Sugar 0 Mbeya City 0 Uwanja wa Manungu Complex mjini Morogoro. Kagera Sugar 2 Lipuli 0 uwanja wa Kaitaba mjini Kagera. Ndanda Fc 3 Stand United 0, Nangwanda Sijaona mjini Mtwara. Mwadui Fc 2 Njombe Mji 0 Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe. Tanzania Prisons 1 Lipuli 0 Uwanja wa

Kipa wa Liverpool atishiwa kifo

Picha
Mlinda mlango wa Liverpool Loris Karius raia wa Ujeruman ametishiwa maisha yake baada ya kusababisha klabu yake ya Liverpool kufungwa mabao 3-1 na Real Madrid Jumamosi iliyopita katika mchezo wa fainali ya Ligi ya mabingwa barani Ulaya Uwanja wa Olimpiki mjini Kiev,Ukraine. Karius aliruhusu mabao mawili ya kirahisi mno moja akimzawadia Mfaransa, Karim Benzema na lingine akimpa mtokea benchi Gareth Bale, Karim Benzema alifunga bao la kwanza dakika ya 51 baada ya kipa huyo kuupiga mpira bila uangalifu na kumgonga Benzema na kuuweka nyavuni. Kipa huyo aliyejiunga na timu hiyo mwaka 2016 akitokea Mainz, alifungwa goli la kirahisi na Gareth Bale dakika ya 83 akifumua shuti la mbali ambapo kipa huyo aliufuata bila mafanikio na kuingia nyavuni, polisi mjini Merseyside wameimarisha ulinzi kwa kipa huyo pamoja na familia yake kufuatia vitisho hivyo toka kwa mashabiki wa Liverpool kupitia mitandaoni Kipa Loris Karius wa Liverpool ametishiwa kifo na mashabiki kwa kufungisha

Pazia la Ligi Kuu Bara kufungwa leo

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Pazia la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2017/18 linafungwa leo kwa mechi nane kupigwa katika viwanja mbalimbali hapa nchini, ligi hiyo inafikia tamati ikiwa bingwa ameshapatikana ambaye ni Simba SC. Vita pekee iliyosalia ni ya kumsaka mshindi wa pili ambayo inawaniwa vikali na timu za Azam Fc na Yanga Sc ambao leo wanaumana usiku katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambapo Azam wana pointi 55 na Yanga ina pointi 52 hivyo nafasi iko wazi kwa Yanga endapo itashinda ila Azam inahitaji sare. Pia vita ipo kwa timu mbili za Ndanda Fc ya Mtwara na Majimaji Songea ambapo moja leo itaungana na Njombe Mji kushuka daraja. Ratiba kamili hii hapa Yanga Sc vs Azam Fc Uwanja wa Taifa Dar es Salaam kuanzia saa 2;00 usiku. Majimaji Fc vs Simba SC uwanja wa Majimaji Stadium mjini Songea. Kagera Sugar vs Lipuli Uwanja wa Kaitaba, Bukoba. Tanzania Prisons vs Singida United Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya. Ndanda Fc vs Stand United Uwanja wa Nangwanda

Kispoti

Picha
DR RAHMAN ALIWATABIRIA UBINGWA REAL MADRID KABLA YA MECHI Na Prince Hoza TIMU ya Real Madrid ya Hispania imefanikiwa kutwaa taji la Ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Liverpool ya England usiku wa Jumamosi katika Uwanja wa Olimpiki mjini Kiev, Ukraine. Hilo linakuwa taji la 13 la rekodi ya michuano hiyo kwa Real Madrid, baada ya awali kushinda miaka ya 1956, 1957, 1958, 1959, 1960, 1966, 1998, 2000, 2002, 2014, 2016 na 2017 na kufungwa katika fainali za 1962, 1964 na 1981. Liverpool wamecheza fainali nane na ya kwanza tangu mwaka 2007 ambayo walishindwa dhidi ya AS Roma ya Italia wakiwa na rekodi ya kushinda taji hilo mara tano katika miaka ya 1977, 1978, 1981, 1984 na 2005 na Jumamosi usiku wamefungwa kwa mara ya tatu kwenye fainali baada ya mwaka 1985 na 2007. Katika mchezo huo wa fainali mjini Kiev, Liverpool ilipata pigo mapema tu katika mchezo huo baada ya mshambuliaji wake nyota, Mmisri, Mohamed Salah kutolewa nje dakika ya 30 kipindi cha kw

Ni Real Madrid mabingwa tena Ulaya

Picha
Timu ya Real Madrid ya Hispania usiku wa jana imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya kuilaza Liverpool mabao 3-1 mchezo wa fainali iliyopigwa katika uwanja wa Olimpiki mjini Kiev, Ukraine. Liverpool ilipata pigo mapema dakika ya 30 baada ya mshambuliaji wake tegemeo, Mmisri, Mohamed Salah kutolewa nje kufuatia kuumia, dakika ya 51 Real Madrid walipata bao baada ya kipa wa Liverpool, Karius kupiga mpira uliomgonga Karim Benzema na kuujaza nyavuni. Lakini Msenegar Sadio Mane akaikomboa Liverpool dakika ya 59 baada ya kufunga bao zuri, vijana wa Real Madrid walisherehekea taji lao la 13 kufuatia mtokea benchi Gareth Bale kufunga mabao mawili dakika ya 64 na 83 Real Madrid mabingwa tena Ulaya

Okwi humwambii kitu kwa Kamusoko, Aslay

Picha
Na Asher Maliyaga. Dar es Salaam Unaambiwa hakuna kitu kinachotawala hisia za mtu yeyote kama mapenzi, Mapenzi kila kiumbe kilichoumbwa na mwenyezi mungu anayo, basi kinara wa mabao Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Emmamuel Okwi raia wa Uganda anayekipiga katika klabu ya Simba ya Dar es Salaam humwambii kitu kwa wanadamu watano ambao mwenyewe amikiri anawapenda. Akizungumza hivi karibuni na kituo kimoja cha redio, Okwi mwenye mabao 20 na aliyeisaidia klabu yake ya Simba kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara amekiri kukoshwa na kiwango cha Mzimbabwe, Thabani Scara Kamusoko anayekipiga Yanga. Okwi amedai katika wanasoka wote wanaosakata soka hapa nchini anampenda mno Kamusoko na huwa anafurahi mno anapomuona nyota huyo akicheza, lakini pia Okwi amedai anakoshwa mno na mwanamuziki anayetamba sasa Dogo Aslay na kinachomvutia ni sauti yake. Ila anayemzimia zaidi ni mkewe ambapo ameweka wazi kuwa anampenda mno mzazi mwenzake huyo, hata hivyo Okwi amesema pia anawapenda pia Ommy Dimpoz na Nan

NI REAL MADRID AU LIVERPOOL KUBEBA NDOO YA ULAYA LEO

Picha
Fainali ya kusisimua kabisa inatarajia kupigwa usiku wa leo huko mjini Kiev,Ukraine kati ya wababe wa Ulaya, Real Madrid ya Hispania na Liverpool ya England kuwania ubingwa wa Champions League. Hiyo inatajwa kuwa fainali kali na ya kusisimua kutokana na ushindani wa timu zote na mashabiki wa timu hizo walibyopaniana, fainali itakuwa ya kusisimua zaidi hasa pale washambuliaji wawili hatari wanapokutana. Mo Salah raia wa Misri aliyekatika kiwango bora kabisa ataiongoza Liverpool ambapo huenda akaisaidia timu yake kubeba taji la sita tangia walipoanza kulinyakua miaka kadhaa iliyopita, Cristiano Ronaldo raia wa Ureno ataiongoza Real Madrid kutwaa taji la 13 na mara tatu mfululizo Real Madrid na Liverpool zinaumana leo

NGOMA AMWAGA WINO AZAM

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Mshambuluaji wa Yanga Sc, Mzimbabwe Donald Ndombo Ngoma amesaini mkataba wa mwaka mmoja kujiunga na Klabu bingwa Afrika mashariki na kati, Azam Fc imefahamika leo. Taarifa zilizothibitishwa na viongozi wa Azam Fc zinasema kuwa Ngoma amesaini mkataba wa mwaka mmoja akitokea Yanga Sc ambao wamekubaliana kuvunja mkataba uliosalia mwaka mmoja, Ngoma alijiunga na Yanga mwaka 2015 akitokea FC Platinum ya kwao Zimbabwe lakini hawakuwa na maelewano mazuri na kusababisha kukaa nje kwa muda mrefu akisingizia majeraha. Kwa mujibu wa daktari wa Yanga, Edward Bavu amesema Ngoma hakuwa na majeraha makubwa isipokuwa hakuwa na maelewano na uongozi, hata hivyo Azam imekubali kugharamia matibabu ya mchezaji huyo atakayepelekwa nchini Afrika Kusini kutazamwa vizuri na ataitumikia timu hiyo msimu ujao na mashindano ya kombe la Kagame yanayotarajia kuanza hivi karibuni Donald Ngoma amejiunga na Azam.FC

AZAM YAJIPANGA KUMREJESHA VIALI

Picha
Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam Klabu bingwa ya soka Afrika mashariki na kati, Azam FC imejipanga kumrejesha mshambuliaji wake wa zamani Khamis Mcha "Viali" anayekipiga Ruvu Shooting ya Mlandizi mkoani Pwani, mabosi wa timu hiyo kwa sasa wanahaha kutaka kumchomoa kwenye timu hiyo. Mcha ameonyesha kiwango kikubwa akiwa na Ruvu Shooting akiisaidia timu hiyo kupata matokeo mazuri kiasi kwamba msemaji wa timu hiyo akianzisha msemo wake binafsi unaokua kwa kasi "Kupapasa" akizitambia timu pinzani. Mcha aliachwa kimakosa sambamba na nyota wengine akina Mudathir Yahya aliyeenda Singida United, Gardiel Michael akaenda Yanga, Erasto Nyoni, Shomari Kapombe, Aishi Manula na John Bocco waliojiunga na Simba, uongozi wa Azam umeweka wazi mpango wake wa kutaka kumrejesha kiungo huyo mshambuliaji ambaye jana aliifungia bao timu yake dhidi ya Yanga katika Uwanja wa Uhuru Khamis Mcha "Viali" anarejea Azam

YANGA NA RUVU SHOOTING ZAGAWANA POINTI

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Mabingwa wa zamani wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga Sc jioni ya leo imeshindwa kuondoka na pointi tatu muhimu baada ya kulazimishwa sare ya kufungana mabao 2-2 na masarange wa Ruvu Shooting ya Mlandizi Pwani katika Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam. Yanga ilicheza vizuri kipindi cha kwanza na kulisakama lango la Ruvu Shooting lakini washambuliaji wake hawakuwa makini na kujipatia magoli, Yanga waliandika bao la kuongoza kunako dakika ya 18 lililofungwa na Matheo Antony aliyepasiwa na Thabani Kamusoko, Goli hilo halikudumu kwani beki wa Yanga Abdallah Shaibu "Ninja" alounawa mpira na mwamuzi aliamuru ipigwe penalti iliyowekwa kimiani na Khamis Mcha "Vialii". Yanga waliongez bao la pili katika dakika ya 36 lililofungwa na chipukizi Maka Edward aliyepasiwa na Pius Buswita, hadi mapumziko Yanga walikuwa mbele kwa mabao hayo, kipindi cha pili kilianza kwa kasi lakini Ruvu Shooting walikuja na kasi na kufanikiwa kusawazish

SIMBA WHATSAAP WAMZAWADIA LAKI TANO KAPOMBE

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Wanachama na wapenzi wa klabu ya Simba kupitia katika mtandao wa Whatsaap, wanaojulikana kama Simba Whatsaap wamemzawadia mchezaji wa klabu hiyo Shomari Salum Kapombe kutokana na mchango wake mkubwa alioutoa katika kipindi kifupi alichoitumikia Simba. Kapombe alikuwa majeruhi wa muda mrefu na alikosa kucheza mechi nyingi za mzunguko wa kwanza mpaka wa pili hadi kupelekea kushutumiwa na mwenyekiti wa kamati ya usajili wa klabu hiyo Zakaria Hanspoppe, wanachama hao wanaounda group la Simba Whatsaap wamekoshwa na uchezaji wa Kapombe na wakaamua kumtunza shilingi 500, 000 za Kitanzania. Wanachama hao wamemzawadia fedha hizo jana baada ya kumualika na kupiga naye picha, Kapombe alirejea mzunguko wa pili na sasa amekuwa katika kikosi cha kwanza cha Simha na kuchangia kuleta ubingwa wa Ligi Kuu Bara kwa mara ya kwanza baada ya miaka mitano Shomari Kapombe (Wa pili kutoka kushoto akiwa na zawadi yake aliyopewa na Simba Whatsaap "Spora" waliopic

ULIMWENGU ASAINI MIAKA MIWILI EL HILAL

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Thomas Ulimwengu amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na timu ya Al Hilal ya Sudan baada ya kuachana na AFC Eskilistuna ya Sweden. Ulimwengu aliachana na Eskilistuna baada ya kupata majeraha ya muda mrefu akitibiwa nchini Afrika Kusini, Al Hilal inayoshiriki Ligi Kuu ya Sudan ikiwa kileleni mwa msimamo wa ligi imeamua kumnasa straika huyo baada ya kuridhika naye. Ulimwengu aliibukia TP Mazembe ya DRC ambapo aliitumikia vizuri sambamba na mwenzake Mbwana Samatta ambaye akauzwa Ubelgiji katika klabu ya Genk huku yeye akitua Eskilistuna ya Sweden ambayo nayo ikaachana nayo baada ya majeraha, hata hivyo dau alilonunuliwa Ulimwengu limebaki kuwa siri kwakuwa mchezaji huyo ni huru Thomas Ulimwengu (Kulia) amejiunga na El Hilal ya Sudan

Yanga kuipapasa Ruvu Shooting leo?

Picha
Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inaendelea tena leo kwa mechi moja kupigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ikiwakutanisha mabingwa wa zamani Yanga Sc na Ruvu Shooting ya Mlandizi Pwani mchezo ambao unatajwa kuwa mkali na wa kusisimua. Yanga ambao wameonja ushindi wa kwanza tangu alipoondoka kocha wake mkuu, Mzambia George Lwandamina inashuka dimbani jioni ya leo ikitaka kuendeleza wimbi lake la ushindi ili kuifukuzia Azam FC iliyo katika nafasi ya pili. Lakini vijana wa Ruvu Shooting yenye msemaji wake mwenye maneno mengi, Masau Bwire hawatakubali kupapaswa na vijana hao wa Jangwanj kwani nao wanataka kujenga heshima na kuibuka na ushindi ili kuwapa furaha mashabiki wake, kinachosubiriwa ni dakika 90 Yanga inaumana na Ruvu Shooting leo

Kipa wa Simba awa kipa bora Ethiopia

Picha
Mlinda wa mlango wa zamani wa mabingwa wa soka nchini, Simba SC, Daniel Agyei amechaguliwa kuwa kipa bora katika Ligi Kuu nchini Ethiopia akiwa anaichezea timu ya Jimma Ketema FC. Agyei alisajiliwa na Simba sambamba na mwenzake James Kotei lakini akaachwa kwa mizengwe na kusajiliwa makipa wengine watatu ambao ni Aishi Manula, Said Mohamed na Emmanuel Mseja huku yeye akitimkia nchini Ethiopia ambapo msimu huu ameonekana bora na kutunukiwa tuzo Daniel Agyei amekuwa kipa bora Ethiopia

Sportpesa yawajaza manoti Simba

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Kampuni ya michezo ya kubahatisha ya Sportpesa Tanzania leo imewapatia shilingi Milioni 100 klabu ya Simba ya Dar es Salaam ikiwa kama shukrani yao kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu wa 2017/18. Akizungumza leo katika ofisi za Sportpesa Osterbay Dar es Salaam, Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Abas Tarimba amesema kampuni yao imewapa Simba kiasi hicho kama sehemu ya masharti waliyokubaliana katika mkataba ambapo walikubaliana kwamba timu kama ikichukua ubingwa wa Ligi Kuu wataipa kiasi hicho nje ya kile walichoandikiana. Tarimba ameongeza kuwa Simba itaongezewa zaidi fedha kama itachukua na ubingwa wa Afrika, Sportpesa pia inaidhamini Yanga ambao ni mahasimu wakuu wa Simba, nahodha wa Simba John Bocco alikabidhi kikombe kwa wakurugenzi wa kampuni hiyo yenye makao yake makuu nchini Uingereza ikopitia Kenya na kutua Tanzania Simba wamejazwa manoti leo na Sportpesa

Minziro aonyeshwa mlango wa kutokea KMC

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Baada ya kufanikiwa kuipandisha Ligi Kuu, klabu ya KMC ya Kinondoni imepanga kuachana na kocha wake Fred Felix Minziro imefahamika. Akizungumza jana, kiongozi wa timu hiyo Suzan Massawe amesema wamepanga kuachana na Minziro na tayari wameshaanza mazungumzo na makocha wengine ambao watafaa kuinoa timu hiyo, kiongozi huyo ambaye ni mwanamama amedai Minziro alipewa kibarua cha kuipandisha Ligi Kuu na ameweza hivyo sasa wakati wa kusaka kocha wa kushindana na Simba na Yanga umefika. Aidha kigogo huyo ambaye pia ni mtumishi wa Halmashauri ya Kinondoni amedai hawana mpango wa kumchukua kocha wa zamani wa Mbao FC, Mrundi, Etienne Ndayiragije ambaye pia anatajwa kujiunga na Singida United, amedai kocha huyo hatoshi kukinoa kikosi chao kwa vile ameshindwa kuiongoza Mbao Fc na imenusurika kutelemka daraja msimu huu Fred Felix Minziro amekalia kuti kavu KMC

Ali Kiba na Samatta kukinukisha Taifa Juni 9

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Mkali wa kusakata kandanda Mbwana Samatta ambaye pia ni nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars na mkali wa kuimba Bongofleva, Ali Kiba ambaye pia ni balozi wa Tembo Tanzania wanatarajiwa kukutana katika mchezo wa soka Juni 9 mwaka huu. Akizungumza na vyombo vya habari, mratibu wa pambano hilo la soka, Daniel Cleverest amesema wakali hao wataunda vikosi viwili na kuchuana katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa lengo la kupata fedha ambazo zitasaidia vifaa na miundombinu mashuleni. Ali Kiba ataunda kikosi chake cha wanasoka anaowafahamu yeye wakati Mbwana Samatta naye ataunda kikosi chake anachokifahamu na kutengeneza timu mbili zitazochuana siku hiyo, wawili hao ni marafiki na wamekubaliana kufanya hivyo likiwa ni jambo zuri kuigwa Ali Kiba na Mbwana Samatta wataunda vikosi vyao na kuchuana Juni 9 mwaka huu

Majina ya wachezaji 30 watakaowania tuzo za VPL hawa hapa

Picha
Na Asher Maliyaga. Dar es Salaam Shirikisho la mpira wa miguu nchini, TFF limetangaza jumla ya wachezaji 30 wanaocheza Ligi Kuu Bara hapa nchini watawania tuzo mbalimbali za wachezaji bora kwa mwaka huu inayotarajiwa kutolewa Juni 23 mwaka huu katika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam. Taarifa iliyotolewa na Afisa Habari wa Shirikisho hilo, Clifford Ndimbo imesema kwamba kufanyika kwa tuzo ni utaratibu ambao Shirikisho la mpira wa miguu hapa nchini, TFF limejiwekea kila mwaka baada ya kumalizika Ligi Kuu. Tuzo hizo zitatolewa chini ya wadhamini wa ligi hiyo kampuni ya simu za mkononi, Vodacom na Azam Tv huku wakiongezeka wadhamini wengine ambao ni benki ya KCB na Primier Bet, alisema Ndimbo. Aidha Ndimbo amedai TFF imefuta tuzo ya mchezaji bora wa kigeni. Licha ya kufutwa tuzo hiyo, Ndimbo amesema kutakuwa na tuzo mbalimbali za wachezaji bora, tuzo zirakazotolewa ni Timu yenye nidhamu, Mchezaji bora chini ya umri wa miaka 20, (Ismail Khalfan), Mchezaji bora chipukizi, Mwamuzi bo

Akina Ngasa wainusuru Ndanda, ikiwaadabisha Mwadui FC

Picha
Na Mwandishi Wetu. Mtwara Kikosi cha timu ya ndanda FC "Wana Kuchele" jioni ya leo kimeibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Mwadui FC ya Shinyanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliofanyika uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara. Ushindi huo umeifanya Ndanda kusalia Ligi Kuu Bara na kusababisha timu ya Njombe Mji ya Njombe kutelemka daraja, Ndanda imefikisha pointi 26 na sasa inashikilia nafasi ya 14 ikiiacha nyuma Majimaji yenye pointi 24 atija nafasi ya 15 na Njombe yenye pointi 22 nafasi ya mwisho. Magoli yaliyoibakisha Ligi Kuu Ndanda yamefungwa na Jacob Massawe kunako dakika ya 3, Mrisho Ngasa dakika ya 5 na Tibar John dakika ya 40, Ligi hiyo itaendelea tena Ijumaa ijayo kwa Yanga Sc kuikaribisha Ruvu Shooting uwanja wa Taifa Dar es Salaam Ndanda imenusurika kushuka ligi

Ngasa kuinusuru Ndanda kushuka daraja leo!

Picha
Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam Winga wa zamani wa kimataifa wa Tanzania aliyepata pia kung' ara katika vilabu vya Toto Africans ya Mwanza, Kagera Sugar ya Bukoba, Yanga, Azam na Simba za Dar es Salaam pamoja na Free State ya Aftika Kusini, Fanja ya Oman na Mbeya City ya Mbeya, Mrisho Khalfan Ngasa leo atakuwa na majukumu mazito ya kuinusuru timu yake ya sasa ya Ndanda FC ya mjini Mtwara itakaposhuka uwanjani kuwaalika Mwadui FC ya Shinyanga mchezo wa Ligi Kuu Bara. Mchezo huo unataraji kuanza saa 10:00 jioni kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara macho yote yataelekezwa kwa mkali huyo aliyewahi pia kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika klabu ya West Ham ya Uingereza huku pia akiwa na rekodi ya kucheza na Manchester United alipojiunga kwa muda na timu ya Seatle Sounders ya Marekani. Mbali ya Ngasa, Ndanda pia inamtegemea mshambuliaji wake Omari Mponda ambaye atawasuuza wakazi wa Mtwara, hivi karibuni Mwadui iliifunga Yanga bao 1-0 hivyo leo itakuwa kazi ny

RAIS AAGIZA KUKAMATWA HARAKA KIONGOZI WA JUU WA SHIRIKISHO LA KANDANDA

Picha
Rais wa Ghana Akufo Addo ameamrisha kukamatwa mwenyekiti wa Shirikisho la kandanda la Ghana Kwesi Nyantekyi, ambaye pia ni makamu wa Rais wa kwanza wa Shirikisho la kandanda barani Afrika, CAF. Hatua hiyo inafuatia makala moja ya uchunguzi ambayo inamuhusisha Kwesi Nyantekyi na vitendo vya ulaghai, inadaiwa kuwa Kwesi alitumia jina la Rais wakati wa kutekelez ulaghai huo. Uchunguzi huo uliofanywa na mwandishi wa habari maarufu Anas Aremeyaw Anas uliwasilishwa kwa Rais wa nchi, uchunguzi huo pia unadaiwa kufichua vitendo vya ufisadi miongoni mwa maofisa wengine wa Shirikisho la kandanda nchini Ghana. Video inayoonyesha ulaghai huo imepangwa kuonyeshwa kwa umma mnamo tarehe 6 mwezi ujao, Kwesi Nyantekyi amekuwa mwenyekiti wa Shirikisho la kandanda nchini Ghana tangu mwaka 2005 hajatamka lolote Kiongozi wa chama soka nchini Ghana, Kwesi anatakiwa kukamatwa haraka

MSEMAJI WA YANGA NDANI YA KASHFA NZITO YA UPIGAJI PESA

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano wa klabu ya Yanga, Dissmas Ten ameingizwa kwenye kashfa nzito na kudaiwa ameihujumu klabu hiyo katika mradi mkubwa wa kalenda na majarida ya klabu hiyo. Yanga ilijiingiza katika biashara ya kutengeneza kalenda na majarida ambapo msemaji huyo inasemekana alikuwa mhusika mkuu kwenye biashara hizo lakini hadi sasa fedha zilizopatikana hazijulikani zilipo na akiulizwa mtendaji huyo anasema hajui. Taarifa ambazo Mambo Uwanjani inazo, zinasema kuwa mpango huo umeratibiwa na uongozi wa Yanga kwa njia ya majaribio na wanakiri kweli baadhi ya makampuni yamejitokeza kutangaza biashara zao katika jarida lililotolewa na klabu hiyo. Katibu mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa amesema ni kweli fedha za majarida na kalenda hazionekani lakini walitoa kwa majaribio tu na hakuna mdhamini aliyelipia fedha za matangazo isipokuwa walifanya kama kujaribu, naye Dissmas Ten alipohojiwa kuhusu hilo amesema kama Mkwasa na hakuna upi

MBEYA CITY SASA NAYO YAWA KAMPUNI, YAIPIKU SIMBA KWA MKWANJA

Picha
Na Exipedito Mataluma. Mbeya Timu ya Mbeya City Council Footbal Club ya jijini Mbeya imeingia katika rada za Simba baada ya wamiliki wake kuiingiza katika mfumo wa kampuni na ikisajiliwa kwa msajili wa makampuni (Brela) na sasa inajulikana kwa jina la Mbeya City Football Club Public Limited Company. Akizungumza jana, mtendaji mkuu wa Mbeya City, Emmanuel Kimbe amesema mpango wa kuifanya Mbeya City kuingia katika mfumo wa kuuza Hisa ulianza tangu  mwanzoni mwa mwaka huu na amedai kwa sasa ni kampuni. Mbeya City inakuwa klabu ya pili kuwa kampuni baada ya Yanga SC iliyoingia katika mfumo wa kampuni mwaka 2001, lakini wanachama wake wakaenda mahakamani kupinga Yanga kampuni, Simba imeingia katika mfumo wa kampuni na wanachama wake wamebariki hivyo sasa inakuwa klabu ya kwanza nchini kuingia kwenye utaratibu huo ikifuatiwa na Mbeya City inayomilikiwa na halmashauri ya jiji la Mbeya. Simba kupitia kwa mwekezaji wake mfanyabuashara, Mohamed "Mo" Dewji ameweka mezani shilingi Bi

KAMUSOKO AITOLEA GUNDU YANGA, IKIICHAPA MBAO FC

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Kiungo Mzimbabwe, Thabani Scara Kamusoko jioni ya leo ameifutia aibu klabu yake ya Yanga baada ya kuichapa Mbao FC bao 1-0 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Bao hilo lilipatikana kunako dakika ya 26 kipindi cha kwanza kwa mkwaju wa adhabu ndogo uliompita kipa wa timu hiyo ambaye alishindwa kuwapanga mabeki wake vizuri, kwa ushindi huo Yanga inafikisha pointi 51 na ikiwa imecheza mechi 28 lakini bado wanaendelea kukaa nafasi ya tatu. Tayari Yanga imeshavuliwa ubingwa wa Bara na mahasimu wao Simba SC waliofikisha pointi 68 wakiwa na mechi moja mkononi, Yanga itashuka tena uwanjani siku ya Ijumaa ikicheza na Ruvu Shooting kisha Jumatatu ijayo itaumana na Azam FC mechi ya mwisho ya kufunga msimu. Katika mchezo wa leo Yanga ilionekana kulishambulia zaidi lango la Mbao na kama si washambuliaji wake kutokuwa makini huenda wangeibuka na ushindi mnono Thabani Kamusoko (Mwenye jezi ya kijanj) ameifungia

NDAYIRAGIJE RASMI SINGIDA UNITED

Picha
Na Mwandishi Wetu. Singida Klabu ya Singida United ya mkoani Singida leo imethibitisha kumalizana na kocha wa zamani wa Mbao FC, Mrundi, Etienne Ndayiragije kuwa kocha wake mkuu hasa baada ya Mholanzi Hans Van der Pluijm kujiunga na Azam FC ya Dar es Salaam. Ndayiragije amesaini mkataba wa miaka miwili na atakuwa na jukumu kubwa kuhakikisha anaiweka matawi ya juu klabu hiyo kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wake Pluijm ambaye ameiweka katika nafasi za juu katika msimamo wa Ligi Kuu ya Bara na vilevile kuiwezesha kuingia fainali ya kombe la Azam Sports Federation Cup ambapo bingwa wake huliwakilisha taifa katika michuano ya kombe la Shirikisho. Ikumbukwe Ndayiragije alikuwa akiinoa Mbao FC naye akisifika kwa kuifanya timu hiyo kuwa ya ushindani akiiongoza kuzitisha Simba na Yanga na kuingia fainali ya Azam Sports Federation Cup mwaka jana, kocha huyo aliachana na Mbao FC mapema mwaka huu na kumuachia msaidizi wake Fulgence Novatus kuiongoza hadi sasa Etiene Ndayiragije akimwaga wino

KIPA WA DRC ALIYETUNGULIWA NA KICHUYA ATUA YANGA

Picha
Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam Kocha mpya wa Yanga SC, Mkongoman, Mwinyi Zahera anatarajia kumshusha katika kikosi hicho kipa wa kimataifa wa DRC, Vumi Ley Matampi ambaye ni kipa wa kwanza wa kikosi cha timu ya taifa ya DRC, The Leopords ambayo ilifungwa mabao 2-0 na timu ya taifa, Taifa Stars Machi 27 mwaka huu. Katika mchezo huo wa kirafiki uliotambuliwa na FIFA, kipa huyo alikubali kutunguliwa mabao mawili na winga, Shiza Kichuya ambaye pia ni mchezaji wa Simba SC ya Tanzania Bara ambao ni mahasimu wa Simba. Tayari wachezaji wawili nao kutoka DRC wameshawasili na wanatazamiwa kuanza mazoezi Alhamisi na wachezaji hao watakuwepo katika kikosi kitakachoenda nchini Kenya kushiriki kombe la Sportpesa, wachezaji waliotua ni Alain Mulumba ambaye ni winga wa kulia anayekipiga DC Motema Pembe na Cedrick Kabale kiungo mchezeshaji anayekipiga timu ya Don Bosco zote za huko huko DRC. Nyota hao watajaribiwa kupitia michuano hiyo na kama watafanya vizuri watasajiliwa moja kwa moja na kushiri

PLUIJM AWAAGA SINGIDA UNITED, WACHEZAJI WAMWAGA MACHOZI

Picha
Na Mwandishi Wetu. Singida Kocha mkuu wa timu ya Singida United ya mkoani Singida, Mholanzi Hans Van der Pluijm amewaaga wachezaji, viongozi na mashabiki wa timu hiyo akiwa safarini kujiunga na mabingwa wa kombe la Mapinduzi, Azam FC ya Chamazi Dar es Salaam. Kocha huyo wa zamani wa Yanga SC aliyewapa ubingwa wa Bara mara mbili mfululizo pamoja na kombe la Azam Sports Federation Cup maarufu FA Cup alitumia muda mfupi kuwaaga Singida United. Pluijm tayari amefanikiwa kuiingiza fainali timu hiyo ya Azam Sports Federation Cup ambapo itaumana na Mtibwa Sugar itakayopigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta mjini Arusha, baadhi ya wachezaji wa Singida United wamekiri kuwa watamkumbuka kocha huyo kwani alifanikiwa kuisuka timu hiyo na kuifanya iwe miongoni mwa timu tishio msimu huu Kocha Hans Van der Pluijm amewaaga rasmi Singida United

Yanga kusaka ushindi wa kwanza leo

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Mabingwa wa zamani wa Tanzania Bara, Yanga SC leo inawakaribisha timu ya Mbao FC ya jijini Mwanza katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam,mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara. Yanga inaweza kupata ushindi wake wa kwanza baada ya mechi tisa bila kupata ushindi ikiwa chini ya makocha wake wa muda, Mzambia Noel Mwandila na msaidizi wake Shadrack Nsajigwa. Pia mabingwa hao wa zamani wanaipigania nafasi ya pili ambayo inakaliwa na Azam FC yenye pointi 55 wakati Yanga yenyewe iko nafasi ya tatu ikiwa na pointi 48 na bado ina mechi tatu mkononi hivyo inaweza kumaliza kwenye nafasi hiyo ya pili,hata hivyo Yanga inayotumia kikosi mchanganyiko na cha pili inaweza isipate mtelemko kwa vijana hao wa Mbao FC ambao nao wanataka kubaki Ligi Kuu na kuendeleza ubabe wao kwa Yanga. Yanga inaumana na Mbao FC leo

Baada ya kupitisha katiba, Simba kumjadili Mfaransa wao

Picha
Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam Baada ya jana wanachama wa klabu ya Simba kuipitisha katiba yao kwa kishindo na sasa kuingia rasmi katika mtindo wa kampuni ya kuuz Hisa, Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo inatarajia kukutana hivi karibuni kumjadili kocha wao mkuu Mfaransa, Pierre Lechantre. Kikao hicho kinatarajiwa kufanyika siku za hivi karibuni ikiwa ni siku chache tangu Simba ikabidhwe ubingwa wake wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dr John Pombe Magufuli Jumamosi iliyopita katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Taarifa ambazo Mambo Uwanjani imezipata zinasema kuwa kamati ya utendaji inakutana ili kumjadili kocha huyo ambaye ameiwezesha klabu hiyo kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara baada ya miaka mitano ikisota bila mafanikio, Lechantre alisaini mkataba wa miezi sita ambao unamalizika mwishoni mwa msimu hivyo uongozi unaazimia kumuongeza mkataba mpya. Licha ya Simba kufungwa bao 1-0 mbele ya Rais Magufuli, lakini kocha huyo ameonesh

Nyota watano waliokatia umeme Simba mbele ya Rais Magufuli

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Mabingwa wa soka nchini Simba SC walipokea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Kagera Sugar mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliopigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Simba ilipokea kichapo hicho mbele ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dr John Pombe Magufuli siku ya Jumamosi ya Mei 19 mwaka huu, Simba ilikabidhiwa ubingwa wake ilioutwaa Mei 10 mwaka huu na hasa baada ya mahasimu wao Yanga kulala mabao 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika uwanja wa Sokoine mjini Mbeya. Katika mchezo kati ya Simba na Kagera ulioudhuriwa na Rais Magufuli, Simba ilijikuta ikibanwa na kuchapwa bao hilo moja lililofungwa na Christopher Edward ambaye alilelewa na Simba. Wafuatao ni nyota wanne ambao waliikatia umeme Simba SC mbele ya Rais Magufuli 1. Juma Kaseja Kipa mkongwe aliyepata kuzichezea Simba na Yanga kwa nyakati tofauti, kipa huyo alikuwa kikwazo kwa washambuliaji wa Simba ambao walishindwa kumfunga, sifa yake kubwa kwenye mchezo huo ni p

Kispoti

Picha
Alphonce Modest anahitaji msaada wa wadau wa soka na serikali Na Prince Hoza RAIS wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dr John Pombe Magufuli aliudhuria kwa mara ya kwanza katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kushuhudia mchezo wa soka kati ya Simba SC Kagera Sugar wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara. Magufuli alikuwa mgeni wa heshima na aliweza kuikabadhi kikombe cha ubingwa wa Ligi Kuu Simba SC na vilevile aliikabidhi kikombe timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys ambayo ilifanikiwa kubeba kombe la mataifa Afrika mashariki na kati yaliyofanyika nchini Kenya. Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini, TFF, Wallace Karia alimuomba Rais Magufuli awe mgeni wa heshima katika mchezo huo ili kukabidhi ubingwa kwa Simba SC na Serengeti Boys ambao ni mabingwa wa CECAFA. Hata hivyo kaimu katibu mkuu wa TFF, Wilfred Kidao alitoa ufafanuzi kuhusu TFF kumuomba Magufuli awe mgeni wa heshima katika mchezo huo. Kidao alisema kuhudhuria kwa mheshimiwa Rais Magu

Azam FC yaichapa Tanzania Prisons 4-1

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Klabu bingwa Afrika mashariki na kati, Azam FC jana usiku imeifunga Tanzania Prisons mabao 4-1 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uwanja wa Azam Complex, Chamazi. Ushindi huo unaifanya Azam Fc kuendelea kukalia nafasi ya pili ikifikisha pointi 55 lakini imesaliwa na mchezo mmoja pekee ambao wataucheza dhidi ya Yanga SC ambao wanasuasua. Magoli ya Azam katika mchezo huo yamefungwa na Shaaban Iddi Chilunda (Hat trick) na kiungo Frank Domayo wakati lile la Prisons lilifungwa na Mohamed Rashid kwa mkwaju wa penalti, jana pia timu ya Mtibwa Sugar imeizamisha Njombe Mji mabao 2-0 mechi ikipigwa nyumbani Njombe katika uwanja wa Sabasaba na kuishusha rasmi daraja timu hiyo Azam FC imeifunga Prisons 4-1

Mtibwa Sugar yairudisha Njombe Mji ilikotokea

Picha
Na Exipedito Mataluma. Njombe Timu ya soka ya Mtibwa Sugar ya Turiani, mkoani Morogoro jioni ya leo imepeleka simanzi katika mji wa Njomhe baada ya kuichapa timu ya Njombe Mji bao 1-0 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na kusababisha timu hiyo kurejea ilipotoka. Kipigo hicho kimefanya Njomhe Mji kushuka daraja na sasa itashiriki Ligi Daraja la kwanza Tanzania Bara msimu ujao, bao ambalo limepeleka simanzi na vilio limefungwa na kiungo mshambuliaji Hassan Dilunga ambaye katika siku za karibuni amekuwa mwiba mkali kwa timu pinzani. Mtibwa Sugar sasa wanafikisha pointi 40 wakiwa katika nafasi ile ile ya saba, Ligi hiyo inaendelea tena usiku huu ambapo Azam FC wanaikaribisha Tanzania Prisons katika uwanja wake wa nyumbani wa Azam Complex, Chamazi, tayari Simba SC imetawazwa kuwa nabingwa wa msimu huu wa 2017/18 Mtibwa Sugar imeishusha daraja Njombe Mji leo

Wanachama Simba sasa wakataa 'Mbumbumbu' kuwania Urais, Ujumbe

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Mkutano mkuu wa wanachama uliofanyika hii leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere, Ocean Road ulioudhuriwa na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dr Harrison Mwakyembe umepitisha katiba mpya ya kuelekea kwenye kampuni ambapo sasa Simba itaendeshwa kwa Hisa. Katika mkutano huo ulioitishwa na kaimu Rais wa klabu hiyo, Salim Abdallah "Try Again", na kuudhuriwa na zaidi ya wanachama 1000 ulipitisha mpango wa kuuza Hisa asilimia 49 kwa mwekezaji na asilimia 51 kubaki kwa wanachama kama ambavyo serikali imezitaka klabu za wanachama kufanya hivyo. Tayari mfanyabiashara, Mohamed 'Mo' Dewji ambaye alikuwa mwanachama pekee wa klabu hiyo kujitokeza na kutaka kununua Hisa asilimia 51 kwa kumwaga Bilioni 20 alisharidhia kununua Hisa asilimia 49 hivyo leo ilikuwa kazi ndogo tu kurekebisha baadhi ya vifungu. Wanachama haowalikubaliana Simba ijiendeshe kisasa na huenda msimu ujao ikatumia uwanja wake wenyewe kuchezea mechi zake za Ligi Kuu Ba

DIAMOND PLATINUM AMJIBU ALI KIBA

Picha
Na Asher Maliyaga Mwanamuziki nguli wa miondoko ya kizazi kipya, maarufu bongofleva, Nasibu Abdul "Diamond Platinum" ni kama amemjibu hasimu wake kimuziki, King Ally Kiba baada naye jana kuzindua kinywaji chake cha Bilauri chenye picha yenye sura yake. Hayo ni mapinduzi mengine kwa msanii huyo ambaye tayari anamiliki mradi wa kuuza Karanga zinazojulikana kwa jina la Diamond Karanga huku pia akianzisha kituo chake cha televisheni pamoja na redio, pia Diamond anamiliki studio yake mwenyewe inayojulikana Wasafi Record akiwa na utitiri wa wasanii ambao wako chini yake na wakiendelea kuachia ngoma kila kukicha. Uzinduzi huo wa kinywaji cha Diamond unaenda sambamba na mwenzake Ali Kiba "King Kiba" kuanzisha kinywaji chake cha Mofaya ambacho kimekuwa kikikubalika, hivyo Diamond anaingia katika ushindani mwingine na Kiba badala ya muziki Diamond Platinum akiwa na kinywaji chake alichokizindua