Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2026

MWANZO WA AFRIKA -3

Picha
Inaandikwa na Fikiri Salum Ilipoishia  WAJERUMANI nao wakachukuwa Togoland, Cameroon na baadhi ya nchi katika Afrika ya magharibi na Afrika ya mashariki, lakini baada ya vita vya kwanza vya dunia wakanyang' anywa. Endelea Waitalia wakachukuwa Libya, Eritrea na sehemu kubwa ya Somalia. UHURU WA AFRIKA Nchi ya kwanza kujitawala upya katika Afrika ni nchi ya Afrika Kusini zilizojiunga na kujiendesha wao wenyewe katika mwaka 1910, Misri, katika mwaka 1922 walikuwa wanajiendesha wenyewe, na Tongier katika mwaka wa 1925. Madola mengi ya Afrika yalianza kupigania uhuru katika miaka ya baina ya 1950 na 1960, na Wazungu wakasalimu amri na kuanza kutoa uhuru. Libya wakajinyakulia uhuru katika mwaka wa 1951, Eritrea katika mwaka 1952 ikiwa imejiunga na Ethiopia, Morocco katika mwaka 1956 na wakarudishiwa Tongier. Katika mwaka wa 1960:Ufaransa ukatoa uhuru kwa Cameroon, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Chad, Kongo Brazzaville, Cote D Ivoire, Dahomey (Benin), Gabon, Madagascar, Mali, Mauritania, Nige...

Dar City yapigwa huko Sauzi

Picha
Timu ya mpira wa kikapu ya Dar City kutoka Tanzania imepoteza kwa mara ya kwanza kufuatia kipigo cha vikapu 118 kwa 97 dhidi ya Al Ahly Benghazi ya Libya kwenye Michuano ya BAL 2026, (Basketball African League) Dar City ambayo ilishinda michezo miwili mfulululizo kabla ya kipigo cha leo imesaliwa na michezo miwili dhidi ya Petro de Luanda ya Angola Aprili 3, 2026 kabla ya kuvaana na RSSB Tigers ya Rwanda Aprili 4, 2026. Michezo hiyo miwili inatarajiwa kuamua hatma Wawakilishi hao pekee wa Tanzania kwenye michuano hiyo inayoendelea Nchini Afrika Kusini.

Mkude aishitaki Yanga, TFF

Picha
Kiungo mkabaji wa zamani wa timu za Simba, Yanga na Taifa Stars, Jonas Gerard Mkude bado hajaonekana uwanjani kwa muda mrefu kutokana na sakata lake la madai dhidi ya timu yake ya zamani ya Yanga SC. Inaelezwa kuwa Mkude amefungua kesi katika Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) akidai alipwe fedha anazodai kabla hajafanya maamuzi ya kujiunga na klabu nyingine yoyote. Kutokana na hilo, Mkude pia alikataa wazo la kutolewa kwa mkopo kwenda Singida Black Stars FC, akisisitiza kwanza amalize suala la madai yake ili haki yake ipatikane. Mashabiki wengi wa soka Tanzania wanaendelea kufuatilia kwa karibu sakata hili wakisubiri kuona Mkude atarejea lini tena dimbani. Jonas Mkude

Timu 10 za Afrika kombe la Dunia 2026

Picha
RASMI: Afrika itaenda kuwakilishwa na mataifa 10 kwenye fainali za kombe la dunia mwezi June pale Marekani, Mexico na Canada mara baada ya hii leo DR Congo kupata ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamaica katika mchezo wa mchujo (Play-off). Na hiyo inatokana na timu ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DR Congo) imefanikiwa kukata tiketi ya kushiriki michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2026 baada ya kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Jamaica. Katika mchezo huo wa hatua ya mchujo uliokuwa na ushindani mkali, bao la ushindi lilipatikana katika dakika ya 100 ya muda wa nyongeza kupitia kwa beki Axel Tuanzebe, aliyewahakikishia "The Leopards" nafasi hiyo adhimu. ​Hatua hii ni mafanikio makubwa kwa majirani zetu DR Congo, kwani inawafanya kuwa miongoni mwa wawakilishi wa bara la Afrika watakaopeperusha bendera katika fainali hizo zitakazofanyika Marekani, Canada, na Mexico.  Ushindi huo umepokelewa kwa shangwe kubwa na mashabiki wa soka kote ukanda wa Afrika Mashariki na...

Depu aanza mazoezi Yanga, sasa mabeki watamkoma

Picha
MSHAMBULIAJI wa Yanga, raia wa Angola, Laurindo Dilson Maria Aurélio ‘Depu’ aliyekuwa anasumbuliwa na maumivu ya nyama za paja leo ameanza mazoezi mepesi ya peke yake. Depu alikuwa akijifua peke yake leo Yanga ikijiandaa na mchezo ujao wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara dhidi ya Tanzania Prisons Aprili 4 Uwanja wa KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam

Samson Adamu kukaimu ukatibu mkuu CAF

Picha
CAF: Shirikisho la Soka Afrika (CAF), limemteua Samson Adamu raia wa Nigeria, kuwa Katibu Mkuu wa muda, kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa awali, Veron Mosengo-Omba. Veron Mosengo-Omba ametangaza rasmi kujiuzulu na kustaafu baada ya kudumu katika nafasi hiyo kwa miaka mitano tangu mwaka 2021. Uteuzi huo uliothibitishwa leo unaashiria kuongezeka kwa ushawishi wa taifa la Nigeria katika maamuzi ya juu ya soka la Afrika, huku Adamu akitarajiwa kuchukua majukumu muhimu ya kiutawala katika taasisi hiyo. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Adamu anakuwa Mnigeria wa kwanza kushika nafasi hiyo tangu kuanzishwa kwa CAF zaidi ya miaka 70 iliyopita.

Shabiki mwenye vituko wa DRC anyimwa viza

Picha
Shabiki wa soka wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Michel Kuka Mboladinga, anayejulikana sana kama Lumumba Vea, amewaambia wafuasi wake kuwa hataweza kusafiri kwenda Mexico kuiunga mkono timu ya taifa, baada ya kunyimwa viza. Shabiki huyo mwenye umri wa miaka 53 alijitokeza hadharani kwa kushangilia kama sanamu wakati wa Mashindano ya mwisho ya AFCON nchini Morocco. Katika ujumbe mzito kwenye mitandao ya kijamii, Mboladinga alielezea kwa kina juhudi kubwa za nchi nyingi kufikia mashindano hayo. Lumumba Vea alifahamika kwa kufanana kwake na Patrice Lumumba, Waziri Mkuu wa kwanza wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na mtu mkuu katika vita vya kupigania uhuru wa nchi hiyo. DR Congo itaingia dimbani leo kucheza mchezo wa mwisho wa kuwania kufuzu kombe la Dunia, mashindano yatakayofanyikia Marekani, Mexico na Canada.

Duke Abuye ang' ara Harambee Stars, FIFA Series

Picha
Duke Abuya leo ameiongoza timu yake ya taifa ya Kenya kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Grenada katika mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu wa mashindano ya FIFA series. Duke alianza kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo kabla ya baadae kuja kufanyiwa mabadiliko kwenye dakika ya 78. Mohamed Bajaber nae alikuwepo kwenye mchezo huo, yeye aliingia mwanzoni mwa kipindi cha pili na akacheza dakika zote 45+5 za kipindi cha pili.

FIFA Series yamng' arisha Ahmed Arajiga

Picha
Mwamuzi wa kimataifa, Ahmed Arajiga, ameendelea kuonyesha kiwango bora kwa kuamua mchezo wa FIFA Series 2026 kati ya Kenya national football team na Grenada national football team uliopigwa Amahoro, Rwanda Arajiga anaendelea kuthibitisha ubora wake kwenye majukwaa ya kimataifa, akiipeperusha vyema bendera ya Tanzania. Wengi wanaamini ni miongoni mwa waamuzi bora nchini, licha ya changamoto za ndani zinazoweza kuathiri maendeleo yake

Allan Okello akwama Uganda

Picha
Siku kadhaa zilizopita niliwataarifu hapa kuwa Allan Okello ataichezea timu yake ya mkoa wa Lango kwenye mchezo wa robo fainali ya mashindano ya FUFA Drum dhidi ya mkoa wa Teso. Mchezo wenyewe ulichezwa jana na Allan Okello alishindwa kucheza kwenye mchezo huo ambao ulimalizika kwa timu ya mkoa wake kupata ushindi wa bao 1-0. Sababu za kutocheza kwake ni zuio kutoka kwa viongozi wa klabu yake, Young Africans. Okello alifanya mazoezi na wachezaji wenzake wa timu yake ya mkoa hadi dakika za mwisho, lakini klabu yake ya Yanga SC haikumruhusu kucheza mchezo huo. Yanga kwa sasa inakabiliwa na wimbi kubwa la majeruhi kwa wachezaji wake, hivyo hawakutaka kuchukua hatari yoyote ile. Walihofia kwamba anaweza kuumia, hivyo wakamtaka arejee Dar Es Salaam Jumapili asubuhi. Hata hivyo, Allan aliweza kuwashawishi wamruhusu kubaki na kuangalia mechi kama shabiki, lakini hawakumpa ruhusa ya kucheza. Kwa hiyo Allan Okello hakucheza mchezo huo kutokana klabu ilitaka kumlinda ili abaki fiti kwa ajili ya ...

Fukwe ya Coco Beach yafungwa

Picha
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule amesema Coco Beach haijauzwa, bali serikali inaboresha ili kulipa hadhi eneo hilo na kudhibiti shughuli zisizokubalika kisheria. "Vijana wengi waliopo pale Coco Beach hawana kazi hawana biashara wanazurura tu na wengine ni walevi wengine wanatumia bangi na wengine wanajiuza sasa tunaishukuru jeshi la polisi kwa kufanya upembuzi yakinifu na kutusanua juu ya hili jambo hivyo sisi kama manispaa ya kinondoni tumeamua kuifanya hili eneo liwe la kistaarabu kwa kuleta wawekezaji wapya ili kuwe na usalama zaidi"

Damaro kuigharimu Yanga, kukatwa pointi tatu za Simba

Picha
Klabu ya Simba SC imeweka wazi mpango wake wa kukata rufaa dhidi ya mchezaji wa Yanga SC, Mohamed Damaro ikitaka ipewe alama tatu huku pia iliitaka TFF kuipoka Yanga alama zaidi kutokana na mchezaji huyo kushiriki katika mechi nyingine. Simba SC wameorodhesha hatua 6 ambazo zinafuatwa katika mchakato wa kuhama Shirikisho kwa mchezaji kwa mujibu wa FIFA, ambazo hazikufuatwa. Kwa mujibu wa Regulations Governing the Application of the Statutes (RGAS), maombi ya kubadilisha Shirikisho lazima yapelekwe kwa Players’ Status Committee (PSC) Kuna aina 4, lakini nimechukua hii ambayo Damaro inamhusu tu. b) Kwa wachezaji wanaotaka kubadili chama cha soka (association) baada ya tayari kushiriki katika mashindano rasmi, katika ngazi yoyote au aina yoyote ya mpira wa miguu, kwa niaba ya chama kingine (Kifungu cha 9 aya ya 2 ya RGAS) Mohamedi Damaro Camara ana angukia kipengele (b), kwani akiwa Guinea alishacheza vilabu vya HAFIA FC na MILO FC, lakini mwaka 2019 alikuwemo kwenye kikosi cha Guinea ch...

Dkt Kikwete aipongeza Dar City

Picha
Rais mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jopo la Wazee la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, amekutana na timu ya mpira wa kikapu ya Dar City inayoshiriki Michuano ya Ligi ya Mpira wa Kikapu Afrika 2026, inayoendelea jijini Pretoria, Afrika Kusini. Katika mazungumzo hayo, yaliyoihusisha pia timu hiyo pamoja na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF), Hasheem Thabit, na viongozi wengine wa Serikali, Dkt. Kikwete ameipongeza Dar City kwa kufikia hatua hiyo muhimu, akieleza kuwa mafanikio hayo yanaashiria kukua kwa kiwango cha mpira wa kikapu nchini Tanzania. Aidha, amewatia moyo wachezaji wa Dar City kupambana katika mchezo wao unaofuata Machi 31, 2026, akisisitiza umuhimu wa nidhamu, kujituma na kujiamini wanapoingia uwanjani. “Kwa hatua mliyofikia, nina imani kabisa mnaweza kutinga fainali na hatimaye kubeba kombe hili,” amesema Dkt. Kikwete. Dkt. Kikwete yupo nchini Afrika Kusini kwa ziara ya kikazi, ambapo pia amekutana na Rais Cyril Ramaphosa, ...

Makonda aja na ligi yake ya wazawa

Picha
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema Wizara hiyo ina mpango wa kuanzisha ligi ya wachezaji wa ndani ili kukuza uwezo wa wachezaji hao. Waziri Makonda ameyasema hayo Mkoani Arusha wakati akifungua kikao kazi cha 16 cha Maafisa Utamaduni na Maafisa Maendeleo ya michezo kinachoendelea mkoani humo. . Mfano kwa sasa ikianzishwa Ligi ya wazawa,klabu ipi itachukua ubingwa asubuhi na mapema?

Taifa Stars walipovishwa medali zao FIFA Series

Picha
Timu ya taifa ya Tanzania , Taifa Stars jana wakivalishwa medali za mshindi wa tatu Kundi B FIFA Series 2026, Kigali, Rwanda. Stars ilifanikiwa kushika nafasi ya tatu baada ya kuichabanga bila huruma timu ya taifa ya Macau mabao 6-0

MWANZO WA AFRIKA -2

Picha
Inaandikwa na Fikiri Salum Ilipoishia  UKOLONI WAZUNGU walianza kugundua bara la Afrika katika karne ya 15, wakati Wareno walipokuja kwenye fukwe za bara la Afrika kutafuta njia nyepesi na ya amani ya kufikia India, na kuweza kupata nafasi ya kushikilia biashara ya dhahabu na pembe na watumwa ambayo ilikuwa ikiendelea wakati huo katika bara la Afrika. Endelea Katika mwaka 1488 Bartolomeo Dio alizunguka rasi ya Tumaini Jema (kwa Kiingereza Cape of Good Hope) na katika mwaka 1498;Vasco da Gama alifika ufukwe wa Afrika mashariki na kuendelea mpaka India. Baada ya hapo, Ureno ulianzisha vituo vya biashara Afrika, ukifuatiwa na Waholanzi, Waingereza, Wafaransa na Wazungu wengineo, na biashara ya watumwa iliyosimamiwa na Waarabu na baadhi ya Waafrika wenyewe ikashika kasi kwa nguvu. Wakati huo huo Waturuki walishikilia sehemu za kaskazini ya Afrika na Waomani wakashikikia ufukwe wa Afrika mashariki. Kati ya miaka ya 1880 na 1972 Wazungu waligawana bara la Afrika, na nchi zote zikawa chini ya...

Uwanja wa Gombani Pemba wageuka kivutio

Picha
Uwanja wa Gombani umeendelea kuvutia hisia za wadau wa michezo baada ya kuonekana katika mwonekano mpya unaoashiria kasi ya maboresho ya miundombinu ya soka nchini. Maboresho hayo yanaendelea kuibua matumaini kwamba Tanzania inaweza kufikia viwango vya juu vya kuandaa mashindano makubwa ya kimataifa siku zijazo. Kwa mujibu wa wadau wa michezo waliotembelea eneo hilo, maendeleo ya uwanja huo yanaonyesha dhamira ya kuendeleza soka na kuimarisha viwanja vya kisasa, hasa katika maeneo ya visiwani. Mwonekano wa nyasi, taa za uwanja, pamoja na miundombinu ya jukwaa umeonyesha hatua kubwa ya maendeleo. Baadhi ya mashabiki na wachambuzi wa michezo wameeleza kuwa kama kasi hii ya maboresho itaendelea, Tanzania inaweza kuwa na uwezo wa kuandaa mashindano makubwa kama AFCON kwa kiwango cha juu zaidi siku za usoni. Hata hivyo, kwa sasa maandalizi ya AFCON 2027 yanaendelea kufanyika kwa ushirikiano wa nchi za Afrika Mashariki, ambazo ni Tanzania, Kenya na Uganda. Ushirikiano huo unalenga kuhakikish...

CAF yaanzisha mashindano mapya

Picha
Rais wa Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), Patrice Motsepe, ametangaza rasmi kuanzishwa kwa mashindano mapya ya kimataifa yatakayojulikana kama African Nations League, yenye lengo la kuongeza ushindani na mapato katika soka la Afrika. Mashindano hayo mapya yanachukua nafasi ya michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN), huku yakibuniwa kwa mfumo mpya utakaoleta ushindani mkubwa zaidi na kushirikisha wachezaji wa viwango vya juu wanaocheza ndani na nje ya bara la Afrika. Kwa mujibu wa Motsepe, mashindano hayo yatakuwa na mifumo miwili tofauti ambapo wa kwanza African Nations League Continental, utaendeshwa kwa mfumo wa kanda ambapo timu bora kutoka kila ukanda zitashindana na hatimaye kupata washindi watakaoingia hatua ya fainali itakayofanyika katika nchi mwenyeji. Pili, African Nations League Pan-African, utakuwa na muundo unaofanana na AFCON, ukizikutanisha timu bora zaidi barani Afrika pamoja na wachezaji nyota wanaocheza katika ligi kubwa duniani. Mots...

Taifa Stars yaipiga Macau 6-0 FIFA Series

Picha
TIMU ya Tanzania imeibuka na ushindi wa mabao 6-0 dhidi ya Macau katika mchezo wa Kundi B kuwania nafasi tatu michuano ya FIFA Series jioni ya leo Uwanja wa Pele Jijini Kigali, Rwanda. Mabao ya Taifa Stars yamefungwa na mshambuliaji wa Floriana ya Malta, Kokola Charles William M’Mombwa dakika ya 16, nyota wa Yanga SC, beki Bakari Nondo Mwamnyeto dakika ya 26 na kiungo Mudathir Yahya Abbas dakika ya 45. Mengine yamefungwa na mshambuliaji wa JKT Tanzania, Paul Peter Kasunda dakika ya 56, kiungo wa Gotzepe ya Uturuki, Novatus Dismas Miroshi dakika ya 74 na winga wa Rochdale ya England, Tarryn Allarakhia dakika ya 87. Taifa Stars imeangukia kwenye mchezo wa kuwania nafasi ya tatu michuano ya FIFA ya Series mwaka huu baada kufungwa 1-0 na Liechtenstein katika mchezo wa kwanza Alhamisi hapo hapo Uwanja wa Pele.

CAF yaanza kumeguka, Veron aachia ngazi

Picha
Veron Mosengo-Omba amestaafu rasmi kama Katibu Mkuu wa Shirikisho la soka barani Afrika CAF. Sura muhimu inafungwa katika katika shirikisho la soka Afrika CAF ambapo Mosengo-Omba alikuwa na jukumu muhimu katika usimamizi na mageuzi ya kandanda ya Afrika. Kwasasa nguvu anazielekeza katika majukumu mengine ya kisoka akiwa miongoni mwa wagombea wa Rais wa shirikisho la soka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Uchaguzi ambao ungefanyika mwezi huu ulisogezwa mbele baada ya FIFA kubaini uwepo wa uhaba wa fedha za kuandaa uchaguzi huo.

Azam FC waifuata Singida Black Stars kibabe

Picha
Kikosi cha Azam FC kimeondoka leo jijini Dar es Salaam kuelekea Singida kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Singida Black Stars. Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Aprili Mosi, mwaka huu ambapo Azam FC itakuwa ikisaka alama muhimu katika mbio za ligi hiyo, huku Singida Black Stars nao wakilenga kutumia faida ya uwanja wa nyumbani.