Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2014

HATUTAKUWA DARAJA LA UBINGWA- MBEYA CITY

Picha
MBEYA City timu iliyopanda daraja msimu huu imetangaza vita kali na Azam FC na kudai hawatakubali kugeuzwa daraja la ubingwa kwa vinara wa ligi hiyo Azam wakati watakapokutana katika mchezo wao muhimu wa ligi kuu. Uongozi na wachezaji wa Mbeya City wamejipanga vilivyo kuhakikisha wanachukua moja ya nafasi mbili za juu ili angalau wapate kushiriki michuano ya kimataifa mwakani, lakini kama watazikosa nafasi hizo basi nguvu zao watazielekeza katika nafasi ya tatu na sivingevyo. Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mazoezi ya timu hiyo jijini Mbeya, wachezaji na viongozi hao bila kutaja majina yao wamedai wanataka kuonyesha kuwa msimu huu ni mwanzo tu ila msimu ujao mambo makubwa yanakuja kutoka kwao.

SCHOLES ATAKA MOYES APEWE MUDA MAN UNITED

Picha
David Moyes Kiungo wa kati wa zamani wa Manchester United Paul Scholes ametoa wito kwa mabingwa wa Uingereza ambao wamekuwa wakihangaika wasimteme meneja David Moyes licha ya kichapo kingine cha aibu. Wiki moja tu baada ya kushindwa 3-0 nyumbani na mahasimu wao wa jadi Liverpool, United walilazwa kwa maabo sawa debi ya Manchester nyumbani kwao Old Trafford Jumanne. Edin Dzeko alifungia Manchester City la kwanza sekunde ya 43 na straika huyo wa Bosnian akaongeza jingine mapema kipindi cha pili kabla ya Yaya Toure kukamilisha kichapo hicho kwa bao la tatu dakika ya 90. Kichapo hicho kiliacha United wakiwa nambari saba ligini na alama 12 nyuma ya Arsenal walio nambari nne. Hayo yameacha mashabiki wakiwa na mshangao, kwamba kikosi kile kile kilichoshinda ligi msimu uliopita na meneja wa zamani Alex Ferguson kabla ya kustaafu, kimekuwa hakijiwezi hivyo dhidi ya timu za Uingereza kikiwa mikononi mwa raia

MESSI KULIPWA ZAIDI DUNIANI

Picha
KLABU ya Barcelona itamfanya Lionel Messi kuwa mchezaji anayelipwa zaidi duniani, kwa kumpa mshindi huyo wa Ballon d'Or nne mshahara wa zaidi ya Pauni 335,000 kwa wiki. Hiyo ni ahadi ya rais wa klabu hiyo, Josep Maria Bartomeu inayokuja siku mbili tu baada ya nyota huyo wa Argentina kupiga hat-trick Barca ikiifunga Real Madrid na kurejea kwenye mbio za ubingwa. "Wote tunataka Messi awe mchezaji anayelipwa zaidi duniani na hilo ndilo tunalolifanyia kazi kwa sasa,"alisema Bartomeu. "Hadi sasa tunaelekeza fikra zetu kwenye mashindano tunayoshiriki, lakini itatokea karibuni,"

LOGARUSIC MGUU NDANI MGUU NJE SIMBA

Picha
Wakati  kikosi cha Simba kikiendelea kupata matokeo yasiyoridhisha katika mechi za Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara inayoendelea, Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, amesema yuko njia panda kutokana na kutojua hatma yake ndani ya klabu hiyo. Mcroatia huyo aliyejiunga na Simba  Desemba mwaka jana baada ya kuitumikia Gor Mahia ya Kenya, anamaliza mkataba wake wa awali wa miezi sita Mei 31, mwaka huu. Awali Kamati ya Utendaji ya Simba ilitaka kumuongeza mkataba kocha huyo lakini baadaye ikaamua kusitisha kufuatia muda wao wa kukaa madarakani kubakia mchache.

YANGA YAFANYA KUFURU KWA PRISONS, YAITANDIKA 5-0

Picha
Mabingwa Yanga walirejea katika kasi yao ya kutoa vipigo vikali zaidi vya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu wakati walipobamiza Tanzania Prisons ya Mbeya kwa magoli 5-0, lakini ushindi huo haukutosha kuitingisha kileleni Azam ambayo nayo ilishinda 2-0 dhidi ya Mgambo mjini Tanga.  Mabao ya Emmanuel Okwi, Mrisho Ngassa, Nadir Haroub 'Cannavaro' na mawili kutoka kwa mtokeabenchini, Hamis Kiiza yaliwapa Yanga ushindi mnono kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kujiimarisha katika nafasi ya pili ya msimamo wakiwa  na  pointi  46,  nne  nyuma  ya Azam. Vinara Azam, ambao wamefikisha pointi 50 wakiwa wamecheza mechi moja zaidi ya Yanga, walipata ushindi huo kwenye Uwanja wa Mkwakwani kupitia magoli ya John Bocco 'Adebayor' (dk.59), na Brian Umony (dk.82) na kujiweka katika mazingira mazuri kutwaa ubingwa wao wa kwanza katika historia zikiwa zimebaki mechi nne.

OBAMA KUKUTANA NA PAPA FRANCIS

Picha
Obama Kukutana na Papa Francis Rais Barrack Obama wa Marekani anatarajiwa kukutana na kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis, katika makao yake makuu huko Vatican. Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Obama kukutana na papa Francis. Wawili hao wanatarajiwa kujadili namna ya kupunguza tofauti iliyopo kati yao katika maswala mengi mbali na kujaribu kuinua maisha ya watu maskini duniani baada ya takwimu kuonyesha kuwa tofauti ya mapato kati ya matajiri na Masiki inaendelea kupanuka .

BAADA YA KUSOTA, BATAROKOTA AULA TUZO ZA KILL MUSIC AWARD

Picha
HATIMAYE mwanamuziki  Batarokota amefanikiwa kuingia kwenye tuzo za muziki za Kilimanjaro Music Award mwaka 2014, kwa mujibu wa waandaaji wa tuzo hizo, Batarokota ameingia na wimbo wake Kwejaga nyangisha. Tayari makundi ya washiriki wa tuzo hizo yameshapangwa hukua akichuana na wanamuziki wengine wenye majina makubwa hapa nchini, makundi hayo yanahusisha wanamuziki maarufu kama Diamond lakini kundi la Batarokota lipo kama ifuatavyo. Wimbo bora wenye vionjo vya asili ya Kitanzania 1 Kwejaga nyangisha-Batarokota 2 Nalonji-Kumpeneka 3 Bora Mchawi-Dar Bongo massive 4 Tumbo lamsokota-Ashimba 5 Aliponji -Wanakijiji 6 Agwemwana-Cocodo African music band Batarokota amekuwa katikamafanikio mazuri baada ya kutengenezxa wimbo huo kupitia njia ya video, hivi karibuni alifanya ziara yake ya kimuziki katika nchi za Swaziland na Afrika Kusini.

RAMADHANI SINGANO KUADHIBIWA NA SIMBA

Picha
SIMBA SC imesema haitamuacha hivi hivi kiungo wake mshambuliaji, Ramadhani Yahya Singano ‘Messi’ anayedaiwa kuvunja kioo cha mlango wa chumba cha kubadilishia nguo cha timu yake jana, ikiahidi kumchukulia hatua za kinidhamu. Mchezaji huyo anayeishi Keko Machungwa, Dar es Salaam anadaiwa kuvunja kioo hicho Uwanja wa Taifa, Jijini hapa baada ya mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Coastal Union ya Tanga, timu yake ikifungwa 1-0. “Viongozi walikutana jana, walilijadili hilo suala, kwa sasa siwezi kusema lolote, ila ni wazi lazima Messi atachukuliwa hatua, hataachwa hivi hivi,”alisema Ofisa Habari wa klabu hiyo, Asha Muhaji leo alipozungumza.

MABEKI WANANIKAMIA SANA- OKWI

Picha
Ukame  wa kucheka na nyavu unamtesa mshambuliaji wa Kimataifa wa Yanga kutoka Uganda, Emmanuel Okwi, lakini amejitetea kuwa bado kiwango chake cha kucheza soka kiko juu licha ya kutofunga mabao kwenye mechi za Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara inayoendelea. Yanga ilimsajili Okwi kwa gharama ya zaidi ya milioni 100 akitokea SC Villa ya Uganda ambayo ilipewa kibali cha kumtumia kufuatia kutofautiana na klabu yale ya Etoile Sportive du Sahel ya Tunisia. Okwi alifunga bao moja wakati mabingwa hao watetezi wakipata ushindi wa 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting na akafunga tena kwa penalti walipokuwa Alexandria wakirudiana na Al Ahly kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika mapema mwezi huu. Akizungumza Okwi, alisema kuwa anapokuwa uwanjani kila mchezaji wa timu pinzani anajipanga kumzuia yeye ili asiweze kuutawala mchezo. Okwi ambaye pia ni mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Uganda (The Cranes) alisema licha ya kutofunga, mchango wake kwenye timu unaonekana na anafurahia kuona Yanga bado ina uwezo w

SIMBA KUTIBUA NDOTO ZA AZAM KUTWAA UBINGWA WA BARA JUMAMOSI

Picha
Majaliwa ya Yanga na Azam FC kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara yapo mikononi mwa Simba ambayo imebakiza mechi na vigogo hivyo vinavyofukuzana kwa karibu katika msimamo wa ligi hiyo inayotarajiwa kumalizika Aprili 19, mwaka huu. Azam ambayo ipo kileleni ikiwa na pointi 47, nne zaidi ya Yanga inayoshika nafasi ya pili, imebakiza mechi nne huku wapinzani wao wakibakiza tano, lakini zote zitalazimika kukutana na Simba, hivyo kupoteza dhidi ya Kikosi hicho cha Zdravko Logarusic kwa timu hizo kunaweza kupeperusha ndoto za kutwaa ubingwa. Hata hivyo, Azam italazimika kuanza kushinda Jumamosi dhidi ya Simba kabla ya kujipanga kuibuka na ushindi itakapokutana na Ruvu Shooting ugenini na baadaye kuikabili Mbeya City kabla ya kumaliza na JKT Ruvu.

DANTE AONGEZA MKATABA MWINGINE BAYERN MUNICH

Picha
Dante Difenda wa kati wa Bayern Munich Dante ameongeza mkataba wake katika klabu hiyo iliyoshinda mataji matatu msimu uliopita, na sasa atakaa huko hadi 2017, klabu hiyo ilisema Jumatatu. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil, aliyejiunga nao kutoka Borussia Moenchengladbach mwaka 2012, alijivunia ufanisi mkubwa msimu wake wa kwanza kwa kushinda Bundesliga na German Cup na pia Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya. "Dante amekuwa bila shaka mmoja wa wachezaji wazuri zaidi tulionunua miaka ya hivi majuzi,” alisema afisa mkuu mtendaji Karl-Heinz Rummenigge kupitia taarifa. "Amkekua na kuwa mmoja wa wachezaji wetu muhimu zaidi uwanjani nan je ya uwanja.” Mchezaji huyo wa miaka 30 aliitwa mara ya kwanza kuchezea Brazil mwaka jana na anatumai kwamba atapata fursa ya kucheza Kombe la Dunia litakalochezewa kwao Juni.

ANDRE MARRINER ALIKOSEA KUTOA KADI NYEKUNDU: FA

Picha
Wachezaji wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain na Kieran Gibbs wameondolewa adhabu ya kadi nyekundu baada ya Gibbs kuondolewa uwanjani kimakosa wakati wa mchuano wa siku ya Jumamosi ambapo Arsenal ilishindwa vibaya na Chelsea kwa kipigo cha magoli 6-0 uwanjani Stamford Bridge. Jopo la chama cha soka England, FA, limesema kuwa refa Andre Marriner alikosea kwa kumtimua uwanjani Kieran Gibbs na kwamba tukio la Oxlade-Chamberlain kuunawa mpira katika eneo la hatari haikustahili kadi nyekundu.

KIJANA LONDON AKAMATWA KWA MAUAJI

Picha
Shereka Fab-Ann Marsh msichana mwenye umri wa miaka 15 aliyeuawa Kijana mwenye umri wa miaka 15, amefikishwa mahakamani kwa kosa la mauaji mjini London Uingereza. Kijana huyo alimuua msichana Shereka Fab-Ann Marsh mwenye umri wa miaka 15 katika mtaa wa Hackney siku ya Jumamosi. Polisi wamesema kuwa msichana huyo alifariki katika nyumba moja mtaani humo saa kumi Jioni. Kadhalika Kijana huyo ambaye ambaye jina lake halikutajwa kwa sababu ya umri wake mdogo, anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.

AZAM YAZIDI KUPAA KILELENI

Picha
AZAM FC imepiga hatua kuikimbia Yanga SC katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kufuatia kuifunga JKT Oljoro bao 1-0 jana Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Matokeo hayo yanaifanya Azam FC itimize pointi 47 baada ya kucheza mechi 21, ikiwazidi mabingwa watetezi, Yanga SC kwa pointi nne ambao hata hivyo wana mechi moja mkononi. Shujaa wa Azam FC hiyo jana alikuwa ni John Bocco ‘Adebayor’ aliyefunga bao hilo peke dakika ya 71 kwa shuti kali baada ya kupokea pasi ya kinda Kevin Friday. Azam FC ilipoteza nafasi nyingi za wazi kupitia kwa Brian Umony dakika ya tisa, Khamis Mcha ‘Vialli’ dakika ya 11, Kipre Tchetche dakika ya 13, John Bocco ‘Adebayor’ dakika ya 39.

BAO LA LALA SALAMA LAIBEBA SPURS

Picha
Christian Eriksen Gylfi Sigurdsson alifunga bao la ushindi dakika ya mwisho baada ya Christian Eriksen kufunga mawili na kusaidia Tottenham Hotspur kujikwamua kutoka 2-0 chini na kulaza Southampton 3-2 katika Ligi ya Premia Jumapili. Sigurdsson alifunga bao kutoka kwa kiki ya raia wa Denmark Eriksen na kuweka hai matumaini ya Spurs ya kumaliza katika nne bora. Wamo nambari tano na alama 56, sita nyuma ya Arsenal walio wa nne wakiwa wamecheza mechi moja zaidi. “Lazima utafute njia ya kushinda, haukuwa mteremko, haukuwa uchezaji wa kupendeza lakini mwishowe lazima utafute njia ya kushinda,” meneja wa Spurs Tim Sherwood aliambia wanahabari. “Tumejikwamua na baada ya mechi mbili au tatu za vichapo, tumeonyesha ustadi wetu na hilo ndilo natafuta.” Southampton walitawala mechi mwanzoni wakiwa na soka safi ya nipe nikupe na makosa mawili kutoka kwa beki wa kulia wa Spurs Kyle Naughton yaliwezesha

MOYES AAHIDI USHINDI DHIDI YA MAN CITY

Picha
David Moyes Meneja wa Manchester United, David Moyes, amepigia klabu chake upatu kitatamba Jumanne watakapo wakaribisha majirani wao na watana shari Manchester City katika uga wao wa Old Trafford katika kivumbi cha ligi ya Premier. Moyes alinogeshwa na ushindi wao wa 2-0 ugenini West Ham United Jumamosi na ametangaza kuwa ni ishara kuwa vijana wake wanaimarika katika wakati unaofaa. City wanazuru Old Trafford wakiwa alama 12 mbele ya mabingwa hao waliodorora msimu huu na waliweza kuadhibu United 4-1 katika mechi ya mkondo wa kwanza katika uga wa Etihad Septemba iliyopita. Waliendeleza harakati zao za kuridhi waasimu wao kama mabingwa pale walipocharaza Fulham 5-0 kabla ya United kujibwaga uwanjani na kuchakaza West Ham 2-0 huku kiungo Michael Carrick akicheza kama beki wa kati wa dharura kutokana na majeraha yaliokumba timu hiyo ya Moyes.

MATOLA AWALILIA OKWI, YONDANI, KASEJA SIMBA, ADAI PENGO LAO BADO LINAWATESA

Picha
Kocha  msaidizi wa timu ya Simba, Selemani Matola, amesema kuwa mabadiliko yaliyofanywa katika benchi la ufundi la timu hiyo ndiyo yalisababisha kikosi hicho kupotea kwenye mbio za kusaka ubingwa wa msimu huu wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara ambayo inatarajiwa kumalizika Aprili 19 mwaka huu. Msimu uliopita Simba ilimaliza ligi ikiwa na Mfaransa Patrick Liewig, ambaye alitimuliwa na nafasi yake kuchukuliwa na mshambuliaji wa zamani wa timu hiyo, Abdallah Kibaden 'King' ambaye naye aliondolewa na mikoba yake ikarithiwa na Mcroatia Zdravko Logarusic. Akizungumza jana, Matola, alisema kuwa mabadiliko hayo yaliifanya timu ianze mchakato wa kusaka kikosi cha kwanza wakati ligi ikiwa tayari imeanza.

SIMBA KIMENUKA, YAFUMULIWA TENA NA COASTAL UNION

Picha
Kikosi cha Coastal Union kilichofanyiwa mabadiliko kikiwaacha nje nyota wa zamani wa Simba akiwamo beki Juma Nyosso na kiungo Haruna Moshi 'Boban', jana kiliwashangaza Wekundu wa Msimbazi kwa kipigo kingine kisichotarajiwa cha 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, huku Azam FC ikibaki kileleni kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya JKT Oljoro. Kilikuwa ni kipigo cha nne kwa Simba msimu huu kilichowaacha Wekundu hao katika nafasi ya nne ya msimamo wakiwa na pointi 36, wakati Azam walijiimarisha kileleni kwa kufikisha pointi 47, nne juu ya Yanga iliyo katika nafasi ya pili. Yanga imecheza mechi moja pungufu. Azam walipata goli lao la pekee kupitia kwa John Bocco 'Adebayor' katika dakika ya 71 kwenye Uwanja wa Azam Complex, ambako timu hiyo ambayo haijapoteza mchezo hata mmoja ilionekana kama ingedondosha pointi mbili baada ya kipindi cha kwanza kumalizika matokeo yakiwa 0-0.

REAL MADRID YAKALISHWA NA BARCELONA 4-3, MESSI ADHIHIRISHA UCHAWI WAKE

Picha
MSHAMBULIAJI Lionel Messi amepiga hat-trick usiku wa jana Barcelona ikishinda 4-3 dhidi ya Real Madrid katika mchezo wa La Liga uliofanyika Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid. Andres Iniesta alianza kuifungia Barcelona dakika ya saba, Karim Benzema akaisawazishia Real dakika ya 20 na kufunga la pili dakika ya 24. Barcelona ikazinduka na kupata bao la kusawazisha dakika ya 42 kupitia kwa Messi, lakini Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo akaifungia Real bao la tatu dakika ya 55 kwa penalti. Messi akafunga mara mbili mfululizo kwa penalti dakika za 65 na 84 kukamilisha hat trick yake Barcelona ikifufua matumaini ya kutetea ubingwa wake msimu huu.

KOCHA WA GHANA ATUA LIVERPOOL

Picha
Kocha Kwessi Appiah Kocha wa timu ya taifa ya Ghana, Kwesi Appiah yuko ziarani nchini Uingereza kupata uzoefu kutoka kwa klabu ya soka ya Liverpool. Appiah pamoja na kocha wa golkipa Nassam Yakubu, watajionea Liverpool inavyofanya maandalizi kabla ya michuano yoyote. Zaidi ya hayo kocha huyo wa Black stars, atakutana na maafisa wa shirikisho la mameneja katika uwanja wa St. George, kituo cha mazoezi ya timu ya taifa ya soka ya England.

TAMBWE AAHIDI KUFIKISHA MAGOLI 22 LEO

Picha
MSHAMBULIAJI wa kutegemewa wa klabu ya Simba Amissi Tambwe leo ameahidi kufikisha magoli 22 wakati klabu yake ya Simba itakapomenyana na Coastal Union ya Tanga katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kauli hiyo ameitoa mapema leo wakati wa maandalizi ya mchezo huo ambapo amedai anataka kutoka na magoli matatu mguuni kwake ili afikishe magtoli 22, lakini endapo itashindikana anataka kufunga goli moja, aidha amesisitiza ndoto yake msimu huu ni kufikisha magoli 25. Akizungumza kwa upole zaidi Tambwe amedai kiola mechi kwake ni fainali na anataka kufunga, Simba iliyo katika nafasi ya nne ikipigania nafasi ya pili au ubingwa inakabiliana vikali na Coastal Union ya Tanga ambayo hivi karibuni ilipokea kipigo cha mabao 4-0 toka kwa Azam FC. Mchezo wa leo hautakuwa rahisi kwa Simjba kuchomoza na ushindi kwani vijana wa Coastal wanaonekana kuupania mchezo wa leo ili watoke na pointi tatu muhimu, beki wa kutumainiwa aliyemo kwenye kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars Abdi Banda ames

YANGA YAFUFUA MATUMAINI YA UBINGWA

Picha
MABINGWA watetezi, Yanga SC jana wamezinduka baada ya kuwachapa mabao mawili 3-0 wenyeji Rhino Rangers katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabira. Shujaa wa Yanga SC, jana alikuwa ni mshambuliaji Jerry Tegete aliyefunga mabao mawili moja kila kipindi, wakati lingine lilifungwa na Hussein Javu kipindi cha pili. Yanga SC sasa inatimiza pointi 43 baada ya mechi 20 na kuendelea kubaki nafasi ya pili, nyuma ya Azam FC yenye pointi 44 baada ya kucheza mechi 20 pia. Kocha Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm alifanya mabadiliko katika safu yake ya ushambuliaji jana akiwaanzisha pamoja Mrisho Ngassa na Tegete badala ya Didier Kavumbangu na Hamisi Kiiza, wakati Emmanuel Okwi na Simon Msuva walikuwa wakishambulia kutokea pembezoni mwa Uwanja.   Tegete aliifungia Yanga SC bao la kwanza dakika ya 30 kwa shuti kali akiwa ndani ya eneo la hatari baada ya kuuwahi mpira uliotemwa na kipa Charles Mpinuki kufuatia mchomo mkali wa kiungo

ARSENAL NDEMBENDEMBE, YALALA 6-0 KWA VIDUME CHELSEA

Picha
GHARIKA. Jose Mourinho amempa mechi ya 1,000 chungu Arsene Wenger baada ya Chelsea kuigaragaza Arsenal mabao 6-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Uwanja wa Stamford Bridge, London. Siku moja baada ya Wenger kukabidhiwa tuzo ya dhahabu kwa kuiongoza Arsenal katika mechi 1,000 tangu aanze kazi, jana alitoka Uwanja wa Stamford Bridge akiwa kichwa chini na asiye na hamu kwa kipigo kikali kutoka kwa wapinzani wao hao kwenye mbio za ubingwa. Mcameroon Samuel Eto’o alitangulia kuifungia The Blues dakika ya tano kwa pasi ya Andre Schurrle, ambaye yeye mwenyewe akafunga la pili dakika ya saba kwa pasi ya Nemanja Matic kabla ya Edin Hazard kufunga kwa penalti dakika ya 17.

MAN CITY HAISHIKIKI ENGLAND

Picha
MANCHESTER City imerudi kwa hasira katika Ligi Kuu ya England ikitoka kutolewa Ligi ya Mabingwa Ulaya- baada ya jana jioni kuifumua mabao 5-0 Fulham katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Etihad mjini Manchester. Mwanasoka Bora wa Afrika, Yaya Toure jana amepiga hat trick yake ya kwanza, mabao mawili akifunga kwa penalti dakika ya 26 na 54 na lingine dakika ya 65 akimalizia pasi ya Samir Nasri. Mabao mengine ya Man City yamefungwa na Fernandinho dakika ya 84, akimalizia pasi ya Milner na Demichelis dakika ya 88. Ushindi huo, unaifanya City ifikishe pointi 63 baada ya kucheza mechi 28 na kupanda nafasi ya tatu mbele ya Arsenal yenye pointi 62 za mechi 30.

RAIS KIKWETE KUWEKA HISTORIA KESHO DODOMA, APANGA KUHUTUBIA MBELE YA WATANGULIZI WAKE

Picha
Rais Jakaya Kikwete kesho ataambatana na ujumbe mzito wa marais wastaafu wa pande zote za Muungano, wake wa waasisi wa taifa na mawaziri wakuu wastaafu atakapokwenda kuzindua Bunge Maalumu la Katiba. Hatua ya Rais kuambatana na ujumbe huo imepongezwa na viongozi wa vyama vikuu vya upinzani nchini, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na mwenzake wa Chadema, Freeman Mbowe. Mbali na viongozi hao, Rais Kikwete pia ataambatana na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein na Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad.

MAAJABU: MAN UNITED YATINGA ROBO FAINALI ULAYA

Picha
MAAJABU yamewezekana. Manchester United imekuwa timu ya pili ya England kutinga Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, ikiungana na Chelsea baada ya Arsenal na Manchester City kutolewa. Hiyo inafuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Olympiacos ya Ugiriki jana usiku Uwanja wa Old Trafford, ambao unawafanya wasonge mbele kwa ushindi wa jumla wa 3-2, baada ya awali kufungwa 2-0 ugenini.

JINAMIZI LA WAARABU LAZIDI KUITESA YANGA.

Picha
BAO la dakika ya 83 la kinda Kevin Friday limeinusuru Azam FC kulala mbele ya Yanga SC baada ya kulazimisha sare ya kufungana 1-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara. Azam ilicheza kwa zaidi ya dakika 20 za mwisho ikiwa pungufu baada ya beki wake wa kulia, Erasto Nyoni kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kutoa lugha chafu kwa refa. Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa askari wa jeshi la Polisi Tanzania, Hashim Abdallah wa Dar es Salaam aliyesaidiwa na Anold Bugado wa Singida na Florentina Zablon wa Dodoma, hadi mapumziko tayari Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0. Bao hilo lilifungwa na mshambuliaji kutoka Burundi, Didier Kavumbangu dakika ya 14 aliyekutana na mpira uliorudi baada ya kupanguliwa na kipa Aishi Salum Manula kufuatia kutokea piga nikupige langoni mwa Azam.

MOTO WAITEKETEZA BAA YA HIGHLAND TABATA BARACUDA

Picha
MOTO mkubwa uliotokea asubuhi ya leo umeweza kuiteketeza kabisa bar maarufu ya Highland Night Park iliyopo Tabata Baracuda iliyo pembezoni mwa barabara iendayo Vingunguti na kusababbisha uahiribu mkubwa wa mali. Mwandishi wetu alikuwepo kwenye tukio ambapo inasemekana chanzo cha kutokea moto huo ni shoti ya umeme, jitihada za majirani zilishindakana kuokoa mali zilizokuwemo ndani ya bar hiyo licha ya kufanikiwa kuwaokoa watu na hakuna majeruhi hata mmoja.

ANGALIA PICHA KUMI ZA BIRTHDAY YA BALOTELLI WA TANZANIA

Picha
Picha ya kwanza, Balotelli wa Tz akimlisha keki mama yake mzazi Beatrice wa Kariakoo. -------------------------

SIMBA YAITAKA TFF IMWEKEE ULINZI TAMBWE

Picha
SIMBA SC imeliomba Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) liwe macho na mchezo mchafu unaotaka kufanywa na wapinzani wao katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Yanga SC na Azam kwa mshambuliaji wao Mrundi, Amisi Tambwe. Mchezo gani huo? Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Pope amesema jana kwamba magazeti yamekuwa yakiandika Yanga na Azam wanamtaka Tambwe, lakini ajabu hawajawahi kufuatwa na kiongozi yoyote wa klabu hizo. Pope amesema kwamba kwa mujibu wa sheria za usajili, klabu yoyote inayomtaka mchezaji ambaye bado ana Mkataba na klabu yake, inatakiwa kwanza kuwasiliana na klabu yake na Tambwe amebakiza mwaka mmoja  na ushei katika Mkataba wa miaka miwili aliosaini Agosti mwaka jana. “Ingekuwa mkataba wake umebakiza miezi sita na hajaongezewa mwingine, basi klabu nyingine zingeruhusiwa kuzungumza naye, ila huyu mchezaji atamaliza mwaka wa kwanza wa Mkataba wake Agosti mwaka huu.

HANSPOPE AZIFANYIA UMAFIA AZAM, YANGA, AMREJESHA KAPOMBE MSIMBAZI

Picha
KIUNGO anayeweza kucheza nafasi za ulinzi pia, Shomary Kapombe atarejea kwenye kikosi cha Simba SC msimu ujao baada ya makubaliano yaliyofikiwa baina ya klabu hiyo na AS Cannes ya Ufaransa. Habari za ndani kutoka Simba SC ambazo tumezipata, zinasema kwamba Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amefikia makubaliano mazuri na AS Cannes juu ya Kapombe. “Pope amezungumza na Cannes na wamekubaliana kulipana fedha ili Kapombe arejee Simba SC,” kimesema chanzo kutoka Simba SC na alipotafutwa Poppe mwenyewe alisema; “Nipo safarini, lakini kwa kifupi Kapombe anarudi Simba SC kwa Mkataba wa miaka mitatu kuanzia msimu ujao,”alisema.    Pope amesema kwamba Simba SC imekubali kuilipa Cannes Euro 33,000 ambazo sawa na Sh. Milioni 66 ili kurejeshewa mchezaji wake huyo.

MRISHO NGASA FITI KUIVAA AZAM KESHO, KASEJA AAHIDI MAKUBWA GOLINI

Picha
MRISHO Ngassa amefanya mazoezi vizuri na kumaliza kuashiria yuko tayari kwa mchezo wa Jumatano dhidi ya Azam FC Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara. Ngassa aliyewasili kwenye kambi ya timu yake, Yanga SC katika hoteli ya Kiromo, Bagamoyo mkoani Pwani alikosekana katika mchezo uliopita wa ligi hiyo dhidi ya Mtibwa Sugar mjini Morogoro kwa sababu ya majeruhi. Ngassa alitoka uwanjani kipindi cha pili Jumapili ya wiki iliyopita baada ya kuumia Yanga SC ikimenyana na Al Ahly ya Misri mjini Alexandria katika mchezo wa marudiano Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika na kutolewa kwa penalti 4-3 kufuatia sare ya jumla ya 1-1. Na baada ya kutua Dar es Salaam Jumatano, alikwenda Mwanza mapumzikoni, huku wenzake wakiingia kambini kujiandaa na mechi dhidi ya Mtibwa Sugar mjini Morogoro Jumamosi iliyoisha kwa sare ya bila kufungana. Ngassa anatarajiwa kucheza dhidi ya timu yake ya zamani, Azam FC kwa mara ya kwanza msimu huu baada ya kukosa mechi mbili, ya Ngao ya Jamii Yanga ikishinda bao 1-0 na

KANYE WEST AHUKUMIWA KIFUNGO CHA NJE

Picha
Kanye West Jukwaani anasesemekana kuwa na tatizo la kudhibiti hasira Mwanamuziki wa muziki wa kufoka au Rap nchini Marekani Kanye West, hajakana wala kukubali mashitaka ya kumshambulia mpiga picha katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Los Angeles. Adhabu yake ni kifungo cha nje cha miaka miwili na ameshurutishwa na mahakama kupata ushauri nasaha kuhusu anavyoweza kudhibiti hasira. Pia ametakuwa kuhudumia jamii kwa masaa 250 kwa kosa hilo alilofanya Julai mwaka jana.

VIPAJI 36 VYATAJWA MABORESHO TAIFA STARS

Picha
Jopo wa wang’amuzi vipaji limetangaza majina ya wachezaji 36 waliopatikana katika mchakato wa maboresho ya Taifa Stars ulioshirikisha mechi za mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar. Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Salum Madadi amesema jopo hilo liling’amua vipaji 143 katika mchakato, lakini waliochukuliwa kwa sasa ni hao 36 tu. Amewataja wachezaji waliochaguliwa katika mchakato huo kwa upande wa makipa ni Abdulaziz Khatib Haji (Mjini Magharibi), Abubakar Abbas Ibrahim (Tanga), Benedicto Tinoko Mlekwa (Mara) na Mtindi Kheri Ali (Kaskazini Unguja). Kwa upande wa mabeki wa pembeni waliochaguliwa katika mchakato huo ambao upo chini ya udhamini wa Kilimanjaro Premium Lager ni Edward Peter Mayunga (Kaskazini Pemba), Hussein Moshi (Tabora), Omari Kindamba (Temeke) na Shiraz Abdallah (Ilala).

YANGA WAPONEA TUNDU LA SINDANO KUFA, BASI LAO LATUMBUKIA MTARONI MIKESE

Picha
Wachezaji na viongozi wa Yanga SC wamenusurika kifo baada ya basi lao kuacha njia na kutumbukia mtaroni eneo la Mikese majira ya saa 3:30 asubuhi wakati wakitoka Morogoro kuelekea Dar es Salaam. Akizungumza ajali hiyo katika eneo la tukio Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizunguti alisema basi lao liliacha njia baada ya dereva wao kukwepa kugongana uso kwa uso na basi lingine lililokuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea mikoa ya bara. “Hii ajali kama siyo akili ya haraka haraka ya dereva wetu kuacha njia na kuseleleka, basi hapa leo kungetokea ajali mbaya tena ingehusisha majeruhi na vifo, lakini tunamshukuru Mwenyezi Mungu hakuna aliyeumia zaidi ya basi kupata mikwaruzo kidogo.”

RAGE AWAITA SIMBA MAMBUMBUMBU, ATANGAZA KUTOGOMBEA RASMI UENYEKITI

Picha
Wakati wanachama wa Simba wakipitisha mapendekezo ya marekebisho ya katiba yao, Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage ametangaza kutogombea tena nafasi hiyo jana asubuhi kwenye ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay. Akizungumza kwenye mkutano huo wa marekebisho ya Katiba ya Simba, Rage alisema: “Simba oyee...Wanasimba msifanye makosa Mei 4 hakikisheni mnachagua kiongozi ambaye atakaa madarakani miaka minne, msifanye makosa baada ya mwaka mmoja mkataka aondoke, Katiba ya Simba inakataza mapinduzi. “Mimi sitagombea, mimi siyo maskini, sina njaa, hata mkizomea nasemaje mimi sina njaa, na wanachama wengi mliopo hapa ni mambumbumbu.” Kauli hiyo iliamsha hasira kwa baadhi ya wanachama ambao walitaka kumvamia na kumtwanga makonde, lakini Polisi waliingilia kati na kusababisha wanachama kupambana na wale wanaomuunga mkono Rage, tafrani hiyo ilidumu kwa zaidi ya nusu saa hadi pale Rage alipoomba radhi kwa kutangaza kuifuta kauli yake hali ikatulia na mkutano ukaanza.

ROONEY ADAI JINAMIZI LAZIDI KUWAANDAMA

Picha
Wayne Rooney Mshambulizi wa Manchester United Wayne Rooney amesema kuwa kipigo cha mabao 3-0 walichokipata kutoka kwa Liverpool ni kama janga kwake na hiki ndio kipindi kigumu kwake kuwahi kukishuhudia tangu kuanza kucheza soka ya kulipwa. Steven Gerrard aliingiza mabao mawili kutokana na mikwaju miwili ya Penalti na kukosa la tatu kabla ya Luis Suarez kuongeza bao la tatu. Mchezaji Nemanja Vidic alifurushwa uwanjani kwa kufanya masihara. Rooney mzaliwa wa Liverpool mwenye umri wa miaka 28, amesema kuwa hiki ni kipindi kigumu sana kwake na wembe ambao hautoshi hata kumezwa.

MESSI NOOMA APIGA HAT TRICK BARCA IKIUA 7-0 LA LIGA

Picha
MSHAMBULIAJI Lionel Messi amefunga mabao matatu katika ushindi wa 7-0 wa Barcelona dhidi ya Osasuna Uwanja wa Camp Nou kwenye mchezo wa La Liga jana. Messi sasa anaweka rekodi nyingine kwa hat-trick hiyo, akiwa mfungaji bora wa kihistoria Barcelona kwenye mashindano yote, baada ya kufikisha mabao 371 akimpiku Paulino Alcantara. Messi pia sasa amebakiza bao moja kumfikia gwiji wa zamani wa Real Madrid, Hugo Sanchez kwa ufungaji bora kwenye historia ya La Liga. Anaweza kumpiku Sanchez wiki ijayo katika dhidi ya mahasimu, Real Madrid Uwanja wa Santiago Bernabeu. Muargentina huyo alifungua biashara leo dakika ya 18 akimalizia pasi ya Alexis Sanchez ambaye alifunga la pili dakika ya 22 kwa pasi ya Jordi Alba kabla ya Andres Iniesta kufunga la tatu dakika ya 34 kwa pasi ya Sergio Busquets.

MAN UNITED YAZIDI KUMUUMIZA KICHWA MOYES, YAPIGWA 3-0 NA VIJOGOO

Picha
KLABU ya Manchester United imeizawadia ushindi wa kwanza Liverpool Uwanja wa Old Trafford baada ya miaka mitano, kufuatia kuchapwa mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England. Kiungo Steven Gerrard amefunga mabao mawili kwa penalti dakika za 34 na 46 wakati Luis Suarez amefunga bao lake la 25 msimu huu dakika ya 84 kukamilisha ushindi mnono wa 3-0.Gerrard alifunga penalti ya kwanza baada ya beki wa United, Rafael kuunawa mpira kwenye eneo la hatari na Nahodha huyo wa Wekundu wa Anfield akafunga tena kwa tuta lingine kufuatia Phil Jones kumchezea rafu Joe Allen kipindi cha pili. Nahodha huyo wa England angeweza kuifungia Liverpool hat-trick ya kwanza Old Trafford tangu mwaka 1936 kama mkwaju wake wa tatu wa penalti usingegonga mwamba baada ya Nemanja Vidic kumchezea rafu Daniel Sturridge.

MTIBWA SUGAR WAAPA KUITIBULIA YANGA YA MISRI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Morogoro WAKATA miwa wa Mtibwa Sugar wenye maskani yao Tuliani Manungu wilayani Mvomelo mkoani Morogoro ambao kesho Jumamosi wataikaribisha Yanga ya 'Misri' katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro wameapa kuitibulia rekodi timu hiyo kwa kuifunga. Akizungumza na Mambo Uwanjani, msemaji wa timu hiyo Tobias Kifaru amesema kuwa kikosi chake kina rekodi nzuri ya kuifunga Yanga hivyo kesho kitalinda heshima yake, ameongeza kuwa Yanga hii ya sasa yenye uwezo wa kushinda magoli 7-0 na kuivimbia timu kubwa na mabingwa wa Afrika Al Ahly ya Misri lakini jeuri yao imekwisha. Kifaru analingia ushindi wa mabao 3-0 ilioupata mwaka juzi katika mzunguko wa kwanza, naye kocha wa Mtibwa Sugar Meck Mexime ametamba kuibuka na ushindi katika mchezo huo, 'Yanga ni timu ya kawaida kama nyingine hivyo sioni sababu ya kuiogopa' alisema Mexime.

MO FARAH ATETEA MAAMUZI YAKE

Picha
Mo Farah akiwa na Gebreselasie Mwanariadha wa Uingereza, mzaliwa wa Somalia Mo Farah, amekariri kuwa alifanya uamuzi bora kushiriki katika mashindano kadhaa ya barabarani kabla ya kushiriki katika mbio za London Marathon mwezi ujao. Farah atakuwa miongoni mwa wanariadha watakaoshiriki katika mbio za kilomita ishirini na moja mjini New York Jumapili hii. Mwanariadha mashuhuri wa Ethiopa, Haile Gebrselassie alikuwa amesema ni mapema sana kwa Farah mwenye umri wa miaka 30 kushiriki katika mbio hizo za marathon, na badala yake kutoa ushauri kwake kuipa mashindano ya uwanjani nafasi ya kwanza.

MWAKA WA TAABU KWA WAINGEREZA, SPURS YABUTULIWA NYUMBANI 3-1

Picha
KLABU ya Tottenham Hotspur imeanza vibaya hatua ya 16 Bora ya Europa League baada ya usiku wa jana kuchapwa mabao 3-1 nyumbani Uwanja wa White Hart Lane, London na Benfica ya Ureno. Ni pigo lingine kwa Waingereza wa England baada ya Manchester City na Arsenal kutolewa katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, Spurs wanachungulia mlango wa kutokea kwenye michuano hiyo ya Ulaya. Spurs sasa inatakiwa kufanya maajabu ambayo yamewashinda City na Arsenal kwenda kushinda ugenini mabao 3-0 ili kusonga mbele. Mabao ya Wareno yalifungwa na Rodrigo dakika ya 30, Luisao dakika ya 58 na 84 wote pasi za Ruben Amorim, wakati bao la Spurs lilifungwa na Eriksen dakika ya 64.

WANACHAMA SIMBA WAMSHIKA RAGE, WAPINGA AJENDA MOJA.

Picha
VIONGOZI wa matawi ya Simba, wamepinga maamuzi ya Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo kuitisha mkutano mkuu wa dharura Jumapili ukiwa na ajenda moja tu badala yake wametaka kuwe na ajenda tano. Kamati ya Utendaji ya Simba chini ya Mwenyekiti Ismail Aden Rage imeitisha mkutano huo wenye ajenda moja tu ya kufanya marejkebisho ya katiba kuingiza kipengele cha kuwa na Kamati ya Maadili ya klabu kama ilivyoagizwa na Shirikisho la Soka nchini (TFF) kwa wanachama wake Desemba mwaka jana. Wakizungumza na Waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa Idara ya Habari (MAELEZO) mchana wa leo, baadhi ya viongozi wa matawi na wanachama wa Simba walimtaka Rage na kamati yake ya utendaji waongeze ajenda nyingine ili mkutano huo uwe na ajenda tano.

SITTA AIGEUKA CCM, ATANGAZA KURA YA SIRI

Picha
Mwenyekiti Mteule wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta amezungumzia uwezekano wa kutumia kura ya siri katika kuamua ibara nyeti katika Rasimu ya Katiba. Sitta aliyechaguliwa juzi kushika wadhifa huo, alisema atashirikiana na kamati ya uongozi itakayoundwa ya wenyeviti wa Kamati 15 za Bunge hilo na kamati ya ushauriano kupata jawabu la suala hilo. Akizungumza katika mahojiano maalumu nyumbani kwake mjini Dodoma juzi, Sitta alisema: “Unajua kuna baadhi ya vifungu na ibara za Rasimu ya Katiba ni vizuri vipigiwe kura ya wazi na vingine ambavyo ni nyeti zaidi vipigiwe kura ya siri.” Alisema si vizuri vifungu vyote vipigiwe kura sawa, yaani si lazima zote ziwe za siri au ziwe za wazi. Alitoa mfano wa ibara inayosema kutakuwa na Mahakama Kuu ya Tanzania na kusema: “Hatuwezi kushindana katika suala la kuwapo kwa Mahakama na ni wazi kuwa jambo hilo mnaweza kupiga kura ya wazi. Nasema hivyo kwa sababu Katiba yoyote lazima ionyeshe mihimili yote ambayo ni Bunge, Serikali na Mahakama.”

LOGA AITABIRIA UBINGWA YANGA.

Picha
Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic ‘Loga’ amesema tiketi ya timu yake kufuzu kucheza michuano ya kimataifa ipo mikononi mwa Azam FC, Yanga na Mbeya City. Awali, Loga ambaye alijiunga na kikosi cha Wekundu hao wa Msimbazi Desemba mwaka jana, aliweka wazi kwamba kikosi chake hakina nafasi ya kutwaa ubingwa msimu huu. Kwa sasa Simba inakamata nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 36, baada ya kucheza mechi 21, kati ya hizo kushinda tisa, kutoka sare tisa na kupigwa mara tatu,  kama Simba watashinda mechi zake zote tano itafikisha pointi 51. Azam FC inakamata uongozi wa ligi hiyo ikiwa na pointi 40 wakiwa na mechi nne mkono, Mbeya City ni ya pili ikiwa na pointi 39 na Yanga ni ya tatu ikiwa na pointi 38. Hata hivyo, Yanga inapewa nafasi zaidi ya kunyakua taji hilo kutoka kutokana na kusaliwa na michezo mitano  mkononi.

LOGARUSIC AULA SIMBA, AONGEZEWA MWAKA MMOJA ZAIDI

Picha
Licha ya timu ya Simba kusuasua kwenye mechi za Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, uongozi wa klabu hiyo ya jijini Dar es Salaam unatarajia kumpa mkataba mpya wa mwaka mmoja kocha mkuu wa timu hiyo, Mcroatia Zdravko Logarusic, imefahamika. Logarusic aliyetua nchini Desemba mwaka jana, alipewa mkataba wa miezi sita kuifundisha Simba huku akilipwa mshahara wa Dola za Marekani 3,000. Kwa mujibu wa habari zilizopatikana jijini Dar es Salaam kutoka chanzo chetu kilichopo ndani ya klabu hiyo, zinaeleza kuwa uongozi wa klabu hiyo umeridhishwa na kiwango kilichoonyeshwa na kocha huyo wa zamani wa Gor Mahia ya Kenya.

SAMUEL SITTA AIBUKA KIDEDEA, AJA NA STAILI MPYA

Picha
Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amechaguliwa kwa kishindo kuliongoza Bunge Maalumu la Katiba, huku akisema kuchaguliwa kwake ni sawa na kumrudisha chura kwenye dimbwi la maji. Jana, Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Urambo Mashariki kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), alipata kura 487 na kumbwaga mpinzani wake, Hashimu Rungwe wa Chama cha Ukombozi wa Umma aliyepata kura 69. Wajumbe wengine, Dk. Terezya Huvisa pia wa CCM na John Chipaka wa Tadea, walijitoa katika kinyang’anyiro hicho ambacho tangu awali Sitta alionyesha kujiandaa kwa kutengeneza vipeperushi alivyovisambaza kwa wajumbe kama sehemu ya kujinadi.

UMEISIKIA HII? BAYERN MUNICH WAWAITA ARSENAL 'MASHOGA'

Picha
MABINGWA wa Ulaya, Bayern Munich wanaweza kuadhibiwa na UEFA baada ya kikundi cha mashabiki wake kupeperusha bango la udhalilishaji kwa wapinzani wao, Arsenal wakati wa mchezo wa marudiano Hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya jana Uwanja wa Allianza Arena, timu hizo zikitoka sare ya 1-1. Kwa matokeo hayo,Bayern wamesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-1 baada ya awali kushinda 2-0 Uwanja wa Emirates mjini London. Bango hilo lilikuwa linasomeka 'Gay Gunners' yaani Mashoga Gunners na lilionekana kumlenga kiungo Mesut Ozil likipeperushwa kabla ya mechi kuanza Uwanja wa Allianz Arena.

BARCELONA YAITOA MASHINDANONI MAN CITY

Picha
Manchester City baada ya mechi yao na Barcelona Dani Alves alifunga bao dakika za mwisho ya mechi yao na kuipa Barcelona ushindi dhidi ya Manchester City na kufuzu kwa robo fainali ya kuwania kombe la klabu bingwa barani Ulaya. Manchester ambayo ilinyukwa magoli mawili kwa bila katika mechi ya raundi ya kwanza, ilipoteza nafasi nyingi wakati wa mechi hiyo nzuri zaidi ikiwa ni mkwaju wa Samir Nasri uliookolewa na kipa wa Barcelona Victor Valdes. Lionel Messi alikamilisha pasi ya Cesc Fabregas kati kati mwa kipindi cha pili kabla ya Pablo Zabaleta kuonyeshwa kadi nyekundu.

OBAMA AICHIMBA MKWARA URUSI

Picha
Rais Obama akiwa wa Waziri Mkuu wa Ukraine Rais wa Marekani Barrack Obama, ameonya Urussi kusitisha mpango wake wa kutaka kutwaa eneo la Crimea nchini Ukraine lasivyo iwekewe vikwazo. Akiongea katika Ikulu ya White House baada ya kufanya mashauriano na kaimu Waziri Mkuu wa Ukraine, Arseniy Yatsenyuk, rais Obama amesema nchi moja haiwezi kulazimisha taifa lingine kwa mtutu wa bunduki. Bwana Yatsenyuk amesema taifa lake sasa ni sehemu ya mataifa ya Magharibi na kamwe haliwezi kurudi nyuma.