Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2016

Wachezaji Yanga wapewa likizo

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Yanga imewapa likizo fupi wachezaji wake hasa baada ya kuhairishwa kwa mchezo wao wa Ligi kuu bara dhidi ya JKT Ruvu uliokuwa uchezwe Jumatano ijayo. Wachezaji wa Yanga wameruhusiwa kurejea majumbani kwao huku wengine tisa wakijiunga kwenye timu za taifa zinazojiandaa na mechi zao za kufuzu fainali za mataifa Afrika mwishoni mwa wiki. Yanga Jumapili ikiyopita iliifunga African Lyon mabao 3-0 katika uwvja wa Taifa Dar es Salaam na kuanza ligi vizuri wakijikusanyia pointi tatu muhimu, shukrani kwa Deus Kaseke, Saimon Msuva na Juma Mahadhi waliokwamisha mipira nyavuni. Pia wachezaji wake wawili walipata pigo kwa kufiwa, kipa Deo Munishi 'Dida' alifiwa na baba yake mzazi aliyefariki katika hospitali ya Mwananyamala na kiungo Deus Kaseke akafiwa na babu yake

Yanga kusaka heshima leo Taifa

Picha
Na Mrisho Hassan, Dar es Salaam Mabingwa wa soka wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara, Yanga SC, jioni ya leo inajitupa katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam kuwavaa African Lyon. Huu unakuwa mchezo wa kwanza wa Yanga ambao wanakumbukumbu mbaya baada ya kufumuliwa mabao 3-1 na Tp Mazembe mchezo wa kombe la Shirikisho barani Afrika. Mabingwa hao watetezi waliondolewa kwenye michuano hiyo baada ya kumaliza kwenye kundi A wakiwa na pointi nne huku Tp Mazembe ikimaliza ya kwanza na Mo Bejaia ikishika ya pili na kusonga mbele. Hivyo Yanga wataingia uwanjani leo wakiwa na hasira ya kutolewa na kuhitaji matokeo mazuri ili waweze kuwafurahisha madhabiki wao, endapo itapata ushindi itafikisha pointi tatu, Lyon wao wameshacheza mechi moja dhidi ya Azam FC ambayo walitoka sare ya kufungana 1-1

Simba yashikwa na JKT Ruvu

Picha
Na Ikram Khamees, Dar es Salaam SIMBA SC jioni ya leo imebanwa mbavu na JKT Ruvu katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam kwa kutoka suluhu 0-0 mchezo wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara. Kwa matokeo hayo Simba imefikisha pointi nne ikiwa imecheza mechi mbili wakati JKT Ruvu imecheza mechi moja na siku ya Jumatatu inaumana na Yanga katika uwanja huo huo wa Taifa. Simba wakiwa na washambuliajj wake Fredrick Blagnon na Laudit Mavugo walionekana kulishambulia lango la JKT Ruvu lakini ngome ya JKT ilikuwa imara na kuzuia hatari hizo, hata hivyo Blagnon na Mavugo hawakuwa katika maelewano mazuri kwani walikosa mabao kadhaa. Kipindi cha pili Simba walimtoa Blagnon na kumwingiza Ibrahim Ajibu 'Kadabla' lakini naye hakuweza kubadilisha mchezo, kipa wa JKT Ruvu Said Kipao anastahili pongezi kwa kuiokoa timu yake isifungwe katika mchezo huo

Manji amaliza mzozo Yanga

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam MWENYEKITI wa Yanga Yusuff Manji juzi usiku alikutana na wachezaji wa Yanga na kuwalipa malimbikizo ya posho zao zote za msimu uliopita kutokana na kutwaa mataji yote matatu nchini, Ngao ya Jamii, Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Kombe la Azam Sports Federation Cup (ASFC). Pia Manji alitumia zaidi ya masaa 4 kujadiliana na wachezaji pamoja na benchi la ufundi, majadiliano hayo yalihusu tathmini ya ushiriki wa Yanga katika michuano mbalimbali msimu uliopita kisha waliweka makubaliano na malengo kwa msimu huu, Manji aliwapa hamasa zaidi kwa kuwaambia wana-Yanga wanahitaji vikombe zaidi msimu huu na wanapaswa kufika mbali katika michuano ya kimataifa.Benchi la ufundi pamoja na wachezaji kwa kauli moja wameahidi kuwapa raha zaidi wanajangwani msimu huu.

Manji amrudisha Bin Kleb Jangwani

Picha
Na Prince Hoza, Dar es Salaam Mwenyekiti wa Klabu ya Young Africans, ndugu Yusufu Manji ameiunda upya kamati ya mashindano na kumteua Injinia Paul Malume kama mwenyekiti wa kamati hiyo ambayo awali ilikuwa chini ya ndugu Chanji.    Kamati hiyo inaundwa na wajumbe 17 kama ifuatavyo; 1. Mustafa Ulungo 2. Eng Mahende Mugaya 3. Abdallah Bin Kleb 4. Jackson Maagi 5. Samwel Lucumay 6. Hussein Nyika 7. Athuman Kihamia ( Arusha ) 8. Felix Felician Minde ( Mwanza ) 9. Leonard Chinganga Bugomola ( Geita ) 10. Omary Chuma 11. Hussein Ndama 12. Hamad Ali Islam ( Morogoro ) 13. Yusuphed Mhandeni 14. Beda Tindwa 15. Mosses Katabalo 16. Roger Lamlembe 17. John Mogha ( Mbeya ) Imetolewa na Kurugenzi ya habari ; Young Africans Sports Club

Yanga kurejea kwenye anga zake VPL

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam YANGA SC sasa imetangaza kiama kwa wapinzani wake baada ya kuondoshwa kwenye michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika, mabingwa hao watetezi wameichimba mkwara African Lyon ambayo watakutana nayo Jumapili ijayo uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Kaimu katibu mkuu wa Yanga, Baraka Deusidetit ameiambia Mambo Uwanjani kuwa Yanga inewasili nchini ikitokea Lubumbashi ambako ilitolewa rasmi katika michuano ya Shirikisho kwa kufungwa mabao 3-1 na wenyeji wao Tp Mazembe ya DR Coongo. Deusdetit amedai Yanga inarejea kwenye anga zake za Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara (VPL) hivyo timu yoyote itakayokatiza mbele yao wataipa kisago, Yanga Jumapili ijayo itakutana na African Lyon hivyo wanaanzia katika mchezo huo na kuendeleza kwa JKT Ruvu ambao watakutana nao Jumatano ijayo

Samatta aipeleka Genk mdomoni mwa Man United

Picha
Mshambulizi nyota raia wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ameendelea kung' ara katika timu yake ya KRC Genk ya Ubelgiji baada ya kuifungia bao muhimu wakati timu yake ikiifunga Locomotive mabao 2-0 na kutinga kwenye hatua ya makundi kombe la Ulaya. Samatta alitangulia kufunga bao la kwanza katika dakika ya pili ya mchezo kipindi cha kwanza kabla ya Leon Beila kuongeza la pili, kwa maana hiyo Genk imefuzu kwenye makundi na inaweza kujikuta inapangwa pamoja na Man United inayonolewa na kocha mbwatukaji Jose Mourinho. Tangu ajiunge na Genk, Samatta amekuwa na mwanzo mzuri akifanikiwa kufunga kila mechi, mshambuliaji huyo wa zamani wa Tp Mazembe anaongoza kwa ufungaji katika ligi kuu ya nchi hiyo

Staa Wetu: Mshamu Hassan "Mfuga Njiwa" Mtangazaji chipukizi wa mpira wa miguu, mwenye ndoto za kumfikia Juma Nkamia

Picha
Na Prince Hoza, Dar es Salaam Anaitwa Mshamu Hassan lakini anajulikana zajdi kwa jina la Baba Nuraty Mfuga Njiwa, Ni mtangazaji wa redio Sibuka 94.5 FM inayosikika nchi nzima ikiwemo Dar es Salaam. Mtangazaji huyo ameanza kujipatia umaarufu mkubwa kutokana na utangazaji wake kuvutia wengi na wale waliopata bahati ya kumsikia wamefurahishwa naye. Alianza kazi hiyo akiwa kama mwanasalamu wa kawaida katika redio mbalimbali kiasi kwamba akajipatia umaarufu, Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu, Mfuga Njiwa alisema utangazaji ni kazi aliyoipenda ingawa hakupata kujua ataianzia wapi. Salamu zilimwezesha kupata nafasi ya kujulikana na wengj na ndipo alipoweza kufanya interview katika vituo vya redio 13 na kimoja cha televisheni, Lakini anasema ni redio Sibuka pekee ndiyo iliyotambua kipaji chake. Akaanza kazi katika redio hiyo na kipindi cha michezo cha kila siku cha Sportaiment na kile cha wiki kinachofanyika kila siku ya Jumamosi kiitwacho MBS ambavyo vyote anashiriki. Pia Mfuga Nj

Tambwe, Ngoma waitisha African Lyon

Picha
Na Saida Salum Washambuliajj wawili wa kimataifa wa mabingwa wa soka nchini Yanga SC, Amissi Tambwe raia wa Burundi na Donald Ngoma raia wa Zimbabwe  wameanza kuipasua kichwa timu ya African Lyon ambayo imepanda Ligi kuu msimu huu. African Lyon itakutana  na Yanga siku ya Jumapili katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam mchezo wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara, lakini hofu yao ipo kwa washambuliaji hao hatari wa Yanga. Kocha wa African Lyon, Myugoslavia Dragan Popadic ambaye pia aliwahi kuinoa Simba mwaka 1993 na kuifikisha fainali ya kombe la CAF, amesema Yanga ina washambuliajj wawili ambao ni hatari na mabeki wake watakuwa na kazi kubwa kuwakabili. Lakini kocha huyo amesema atawawekea mabeki watulivu na wataweza kuwazuia na hawataweza kuleta madhara langoni kwao, African Lyon iliwalazimisha sare ya 1-1 Azam FC katika uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi nje kidogo ya jijj la Dar es Salaam

Stand United kujitoa Ligi kuu bara

Picha
Na Paskal Beatus, Shinyanga Uongozi wa timu ya Stand United umesema wako mbioni kujitoa Ligi kuu bara baada ya kuchoshwa na mgogoro uliochochewa na Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) na kuzaa makundi mawili Stand Kampuni na Stand Wananchi. Stand ambayo tayari imeshacheza mchezo mmoja na Mbao FC ya Mwanza na kuambulia pointi moja, imeweka bayana mpango wake wa kujitoa ili pande zote zinazolumbana zione madhara ya mgogoro na hatimaye timu ishuke daraja. Uongozi huo ulithibitisha jana ambapo umeonekana kuibebesha lawama TFF kwa kushindwa kuwapatisha na badala yake kuchochea mgogoro uliopelekea kuigawa timu hiyo, endapo Stand itajitoa Ligi kuu bara, itasababisha Ligi hiyo kusimama ili kupisha mabadiliko ya ratiba, na pia huenda timu hiyo ikashushwa daraja hadi ngazi ya wilaya kutokana na kosa la kujitoa

Yanga yabutuliwa 3-1 na TP Mazembe

Picha
Na Ikram Khamees, Lubumbashi Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya kimataifa, Yanga SC, imemaliza ushiriki wake wa kombe la Shirikisho barani Afrika, baada ya kupokea kichapo cha mshangao cha mabao 3-1 toka kwa mabingwa wa Afrika, TP Mazembe ya Lubumbashi. TP Mazembe ambao tayari wamefuzu Nusu fainali, lakini wakataka kuweka heshima kwa kuwafunga mabingwa wa Tanzania bara Yanga, magoli ya TP Mazembe iliyofikisha pointi 13 yaliwekwa kimiani na Rayfred Kalaba aliyetupia mawili na Bolingi aliyefunga moja. Yanga walipata bao lao la kufutia machozi lililofungwa na straika wake hatari Amissi Tambwe ambaye pia ni mfungaji bora wa Ligi kuu bara, Yanga sasa wanarejea Tanzania ambapo Jumapili wataanza kampeni yao ya kutetea ubingwa wa bara watakaposhuka Uwanja wa Taifa Dar es Salaam kucheza mechi yao ya kwanza

Samatta aongoza kwa ufungaji Ubelgiji

Picha
Na Mwandishi Wetu Mshambuliajj wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga KRC Genk inayoshiriki Ligi kuu nchini Ubelgiji Mbwana Ali Samatta anaongoza kwa upachikaji magolj kwenye ligi ya nchi hiyo. Samatta amefunga magoli manne wakati anayemfuatia amefunga magoli matatu, kung' ara kwa mshambuliajj huyo wa zamani wa African Lyon, Simba SC na TP Mazembe kunatokana na juhudi zake binafsi ambako kutamfanya apate soko haraka. Samatta alijiunga na Genk mwanzoni mwa mwaka huu akitokea TP Mazembe ya DR Congo aliyoipa ubingwa wa Afrika, Samatta ndiye mwanasoka bora wa bara la Afrika kwa mwaka huu

Simba balaa sana yaiua Ndanda 3-1

Picha
Na Salum Fikiri Jr, Dar es Salaam SIMBA SC jioni ya leo imeichapa Ndanda FC mabao 3-1 na kujikusanyia pointi tatu muhimu katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam mchezo wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara. Vijana wa Simba wakiwa na hamasa kubwa kutoka kwa mfanyabiashara Mohamed Gulam Dewji "Mo Dewji", walianza kuliandama lango la Ndanda na kujipatia bao la kwanza lililofungwa na mshambuliaji wake mpya raia wa Burundi, Laudit Mavugo. Bao hilo la Mavugo limeingia kwenye rwkodi ya kuwa bao la kwanza msimu huu kwenye uwanja huo, Ndanda wakasawazisha kupitia kwa Omari Mponda na kufanya timu hizo ziende kupumzika zikiwa sare. Kipindi cha pili Simba walimtoa mshambuliaji wake Ibrahim Ajibu na kuingia Fredrick Blagnon raia wa Ivory Coast, mabadiliko hayo yakazaa matunda kwani Simba ilipata bao la pili lililofungwa na Blagnon. Shiza Ramadhan Kichuya akafunga bao la tatu na la ushindi, kwa matokeo hayo Simba imefikisha pointi tatu na huenda ikawa kileleni mwa msimamo wa ligi, mbali na rw

Kessy ruksa Yanga- TFF

Picha
Na Ikram Khamees, Dar es Salaam Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) kupitia kamati yake ya Sheria na Hadhi za wachezaji leo imepitisha usajili wa vilabu vinavyoshiriki Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara (VPL) na Ligi Daraja la kwanza (FDL) huku ikipitisha jina la beki Hassan Ramadhan Kessy kuichezea Yanga msimu huu wa 2016/17. Mwenyekiti wa kamati hiyo Richard Sinamtwa amempitisha Kessy akidai alisajiliwa kihalali na hata madai ya klabu yake ya zamani ya Simba hayaendani na usajili wake, Kessy alisota benchi kwa muda mrefu baada ya klabu yake ya zamani ya Simba kumuwekea ngumu asicheze. Hata hivyo mchezaji huyo akaanza kucheza kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii ambapo Yanga ilikutana na Azam FC Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, na katika mchezo huo Yanga ililala kwa mikwaju ya penalti 4-1 baada ya kumaliza dakika 90 kufungana mabao 2-2, Kessy alikosa penalti katika mchezo huo

Michano: Mkola Man, Mwanahip hop anayesota, ni sawa na mkulima wa pamba wakati wa njaa hawezi kuzila

Picha
Na Ikram Khamees, Dar es Salaam Yap....yap...yap...Michano yangu ya leo inamchana msanii wa miondoko ya Hip hop mkazi wa Hale mkoani Tanga, huyu jamaa ameanza muziki kitambo ila naye bado hajapata bahati ya kutoka. Alijaribu kutoka miaka minne iliyopita alipoachia ngoma yake ya kwanza 'Utajiri hewa' lakini haikufanya vizuri, akaachia nyingine 'Mr Mapesa' ambayo ilisumbua kidogo TBC FM hadi kuingia kumi bora. Mkola Man akaachia nyimbo nyingine kama 'Kilevi changu', 'Malovedavi time', 'Jana na leo' na 'Kitabu cha historia' aliyoiachia sasa, mwanamuziki huyo anajitahidi kutoa nyimbo ila tatizo promo. Amekuwa akifanya promo ya kitoto kwani zinatamba muda mfupi na kuzimika, Yaani namfananisha Mkola Man na mkulima wa pamba ambaye anajitahidi kutayalisha shamba na kulima lakini soko kamili la biashara hiyo halijui. Kinapofika kipindi cha njaa anashindwa kula pamba, basi tukutane wiki ijayo Ikram Khamees ndani ya michano

Simba na Ndanda kesho Taifa

Picha
Na Prince Hoza Simba SC kesho jioni itajitupa katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam kuwakaribisha "Wana kuchele" Ndanda FC mchezo wa ufunguzi Ligi kuu ya Vodacom Tanzanis bara. Simba inaingia kwenye mchezo huo ikiwa na matumaini kibao hasa baada ya kutoka kucheza mechi mbili za kirafiki za kimataifa ambapo moja iliwafunga AFC Leopards ya Kenya mabao 4-0 na nyingine ikatoka sare ya 1-1 na URA ya Uganda. Wekundu hao pia wanaingia uwanjani wakiwa na furaha na kikosi chao kilichosheheni nyota kama Laudit Mavugo, Method Mwanjali na Fredrick Blagnon, Lakini Ndanda hawatishiki na majina kwani wao nao wanaye Salum Telela 'Abo Master' aliyetokea Yanga SC hivyo wametamba kutoa upinzani mkali katika mchezo huo, Mwamuzi wa yote ni dakika tisini

Badala ya akina Joti, Elia Daniel naye shakani

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Jeshi la polisi nchini linawasaka wasanii wa kundi la Orijino Komedi linalowahusisha wasanii Emmanuel Mgaya (Masanja Mkandamizaji), Joti na Mac Regan kwa kosa la kuvaa sare za polisi kinyume cha sheria. Wasanii hao walitinga sare hizo wakati wa sherehe ya harusi ya msa ii mwenzao Masanja, inasemekana wasanii hao wakivaa sare hizo za polisi, hata hivyo wasanii hao walikamatwa na polisi na kuhojiwa kwa masaa kadhaa isipokuwa Masanja bado anaendelea kutafutwa. Wimbi la wasanii kuvaa sare za polisi linazidi kukithiri, si mara ya kwanza kwa wasanii hao kuvaa sare za polisi kwani mwaka juzi msanii Diamond Platinum alidakwa na polisi kwa kuvaa sare za JWTZ, ukiachana na hao, wapo wasanii wengine wanaoshiriki katika sanaa zao wakiwa wanatumia silaha kama hapo (Pichani)

Azam FC yainyuka Yanga 4-1 kwa penalti na kubeba Ngao ya Jamii

Picha
Na Mrisho Hassan, Dar es Salaam AZAM FC kwa mara ya kwanza leo imetwaa Ngao ya Jamii baada ya kuitandika Yanga SC mabao 4-1 kwa mikwaju ya penalti baada ya kumaliza dakika 90 zikiwa zimefungana mabao 2-2. Yanga watabidi wajilaumu wenyewr hasa baada ya kuongoza kwa mabao mawili hadi mapumziko, magoli ya Yanga yote mawili yaliwekwa kimiani na mshambuliaji wake raia wa Zimbabwe Donald Dombo Ngoma huku moja akifunga kwa mkwaju wa penalti baada ya yeye mwenyewe kuangushwa. Kipindi cha pili Azam walifanya mabadiliko mazuri na kufanikiwa kukomboa mabao yote mawili, Shomari Kapombe alianza kuifungia Azam bao la kwanza, kabla ya nahodha John Bocco "Adebayor" kusawazisha kwa mkwaju wa penalti. - Hadi mwisho matokeo ni sare ya 2-2 ndipo timu hizo zilipokwenda kwenye mikwaju ya penalti ambapo Azam ikawa mabingwa kwa kufunga penalti nne na Yanga wakapata moja huku wakipoteza mbili zilizopigwa na Hassan Kessy na Haruna Niyonzima, Hii ni ndoo ya kwanza kwa Azam na inaashiria msimu huu

Hatimaye Simba na MO kimeeleweka

Picha
Na Mrisho Hassan, Dar es Salaam Kikao cha kamati ya utendaji cha klabu ya Simba kilichoketi Jumatatu kilichomkutanisha na mfanyabiashara mashuhuri barani Afrika Mohamed Gulam Dewji 'MO Dewji' kimeeleweka na sasa mambo yote shwari. Taarifa za ndani kutoka kwenye kikao hicho ambapo Mambo Uwanjani imepata data, kwamba Kamati ya utendaji imeridhia kumkabidhi timu MO kwa sasa lakini ni kwa ajili ya kuisaidia tu huku mchakato rasmi wa kumuuzia ukiandaliwa. Taarifa hizo zinasema kwa sasa MO Dewji ruksa kutoa chochote ndani ya Simba na anaweza kusafiri nayo ama kugharamia safari za Simba, Wakati mambo yakiwa shwari ndani ya Simba, Yanga wanazozana na bosi wao Yusuph Manji

MANJI AHOFIWA KUJIUZURU YANGA

Picha
Na Salum Fikiri Jr, Dar es Salaam Taarifa zilizosambaa jijini Dar es Salaam ni kujiuzuru kwa mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Yusuph Mehbood Manji (Pichani), Manji amefikia uamuzi hasa baada ya kutoungwa mkono na Wanayanga wenzake katika mpango wake wa kutaka kuikodisha klabu hiyo. Manji alitaka kuikodisha Yanga kwa muda wa miaka kumi lakini akakumbana na maneno ya kejeli na vitisho kutoka kwa Wanayanga, akizungumza jioni hii mara baada ya kuenea kwa taarifa za kujiuzuru, Manji amesema bado hajawa tayari kuzungumzia taarifa hizo lakini kwa sasa anaomba aachwe kwanza. Kwa maana hiyo Manji amejiweka kando Yanga hivyo sasa watakuwa katika wakati mgumu, Manji amejikuta akiandamwa na viongozi wa serikali juu ya mpango wake huo, hivi karibuni Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Poul Makonda alipost maneno katika ukurasa wake wa Facebook ambao ulionekana kumkashifu bosi huyo wa Yanga ambaye ni mmiliki wa Quality Group

Mkude ainusuru Simba

Picha
Na Prince Hoza, Dar es Salaam Goli la kusawazisha lililofungwa na Jonas Gerrald Mkude jioni ya leo limeiokoa klabu yake ya Simba baada ya kutoka sare ya kufungana 1-1 na URA ya Uganda mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika uwanja wa Taifa Dar es Salaam. URA ambao juzi waliilazimisha Azam FC kwenye uwanja wao wa Azam Complex Chamazi kwa kufungana 1-1, walikuwa wa kwanza kuandika bao la kwanza kipindi cha kwanza kabla ya Mkude ambaye leo hii ameanza majukumu mapya ya kuwa nahodha wa Simba. Mkude amechukua nafasi ya Mussa Hassan Mgosi ambaye amestaafu rasmi kucheza soka la ushindani na leo ameaga rasmi, Mgosi sasa anakuwa meneja wa Simba akisaidiana na Abbas Ally. Vijana wa Simba walicheza kandanda safi na la kupendeza huku mshambuliaji wake mpya Laudit Mavugo akicheza vizuri ingawa hakuwa kwenye kiwango chake kama alichokionyesha katika mchezo uliopita na AFC Leopards

Yanga yaona mwezi, yailaza MO Bejaia 1-0

Picha
Na Ikram Khamees, Dar es Salaam Wawakilishi pekee wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Yanga SC, jioni ya leo imepata ushindi wa kwanza tangia kuingia hatua ya makundi, baada ya kuilaza MO Bejaia ya Algeria bao 1-0 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Ushindi wa leo umeifanya Yanga kufikisha pointi 4 na sasa itasubiriwa miujiza katika mchezo wake wa mwisho ili iweze kutinga Nusu fainali, Licha ya kupata ushindi huo mwembamba, Yanga ilikosa magoli mengi kupitia kwa Obrey Cholla Chirwa ambaye alipoteza nafasi tatu za wazi. Yanga iliandikisha bao la kwanza na la ushindi lililofungwa na mshambuliaji wake mahiri Amissi Tambwe ambaye aliunganisha mpira wa adhabu iliyopigwa na Juma Abdul, kipa wa Yanga Deogratus Munishi 'Dida' alionyesha uwezo mkubwa licha ya kuumizwa mara kwa mara na wachezaji wa MO Bejaia

Yanga na MO Bejaia hatumwi mtoto dukani

Picha
Na Prince Hoza, Dar es Salaam Mabingwa wa soka wa Tanzania bara Dar Young Africans (Yanga), jioni ya leo inashuka uwanja wa Taifa Dar es Salaam kuwavaa wageni wao Moulodia Olympic Bejaia ya Algeria mchezo wa kombe la Shirikisho barani Afrika hatua ya makundi. Yanga inataka kulipiza kisasi baada ya kuchapwa bao 1-0 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Algeria, lakini pia inataka kupata ushindi wake wa kwanza ili ijinasue kutoka mkiani mwa kundi A, Yanga imevuna pointi moja pekee ambapo ijishinda inaweza kupanda kidogo. MO Bejaia wenyewe nao wanataka ushindi kwani hadi sasa wamefikisha pointi tano na kama wakishinda watafikisha pointi nane na kujihakikishia nafasi ya kutinga Nusu fainali

Mzee Yusuph aachana na taarabu

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Gwiji la muziki wa taarabu nchini ambaye pia ni mkurugenzi wa bendi yake ya Jahazi, Mzee Yusuph ametangaza kuachana na muziki huo na kuamua kumrejea mungu. Taarifa zilizotufikia ambazo zimethibitishwa na yeye mwenyewe zinasema kuwa ameamua kuachana na muziki na kuamua kumrejea mwenyezi mungu. Yusuph amedai binadamu tuna deni kubwa kwa mwenyezi mungu hivyo umefika wakati wa kumrejea na kuachana na mambo ya duniani, mwanamuziki huyo ameongeza kuwa ataendelea kuwasapoti wanamuziki chipukizi

Michano: Suma G alivyopotea kwenye muziki, ni sawa na mvuvi aliyesinzia

Picha
Na Mkola Man, Tanga yap yap yap leo michano inamchana SUMA G mkali wa uswahilini kuna vituko na pombe ukizidisha ina kuwa noma kama kuna wana hip hop ama wanaharakati wa mfano yeye ni mmoja wapo alikubalika sana hasa kwa staili yake tamu ya kurap na mbwembwe na vinogesho vyenye ladha ya uswahilini ila ameshindwa kuilinda aina ya mziki anaofanya na matokeo yake amekuwa kama ndio anaaza mziki michana mnafananisha na mvuvi wa samaki anaye tumia ndoano wakati wezake wanatumia nyavu kisha yeye analala apati samaki wengi bila kujua mziki wa sasa sio wajana tukutane wiki ijayo kwenye michano ya mkola man

Kessy ruksa kucheza Yanga- CAF, lakini.....

Picha
Na Ikram Khamees, Dar es Salaam Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika (CAF) usiku wa leo limeidhinisha jina la mlinzi wa kulia wa Yanga, Hassan Khamis Ramadhan Kessy kuitumikia timu yake hiyo lakini limeitaka Yanga kuzungumza na Simba. Kessy alishindwa kuitumikia timu yake hiyo mpya aliyojiunga nayo mwanzoni mwa mwezi uliopita, lakini imeshindwa kumtumia katika mechi zake za makundi kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga imecheza mechi nne na Jumamosi itacheza mchezo wa watano na Mo Bejaia ya Algeria huku ikiendelea kumkosa Kessy, Yanga ilionyesha jeuri na ilikataa kukaa mezani na Simba hivyo imepelea klabu ya Simba kudai mchezaji huyo hatocheza msimu mzima mpaka Yanga iwalipe shilingi milioni 62

Yanga waapa kufia Taifa Jumamosi

Picha
Na Salum Fikiri Jr, Dar es Salaam Mabingwa wa soka Tanzania bara, Yanga SC, wameapa kufia uwanjani Jumamosi watakapoikaribisha MO Bejaia ya Algeria katika michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika kundi A. Kocha msaidizi wa Yanga, Juma Mwambusi ameiambia Mambo Uwanjani kuwa ni lazima waibuke na ushindi katika mchezo huo kwani wanahitaji pointi tatu. Endapo Yanga itapata ushindi itafufua matumaini ya kusonga mbele kwani itafikisha pointi nne ingawa itaendelea kushikilia mkia, Yanga ndio timu pekee kwenye kundi hilo ambayo haijaonya ushindi ikiwa imepoteza mechi tatu kati ya nne ilizocheza

Vital'0 yamng' ang' ania Mavugo, yadai bado mali yao

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Pamoja na klabu ya Simba kusisitiza mshambuliaji wake mpya, Laudit Mavugo ni mali yake, Vital'0 ya Burundi imeendelea kusisitiza bado inammiliki. Vital'0 imetuma jina lake kwenye Shirikisho la soka la Burundi (BF) ikiwa ni sehemu ya wachezaji itakaowatumia msimu ujao. Hali hiyo inaashiria mgogoro wa usajili kwa Mavugo ambaye amejiunga na Simba msimu huy akielelezwa kumaliza mkataba na timu yake hiyo ya zamani. Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano wa Simba, Haji Manara amesema Mavugo hana tatizo lolote la usajili, "Ni mchezaji wa Simba na hakuna maelekezo mengine zaidi", alisema. Lakini Rais wa Vital'0, Benjamin Bikorimana amesema Mavugo hajamaliza mkataba na timu yake kama inavyoelezwa. "Ni kitu cha kushangaza sana, Simba wanapoteza muda, ITC yake ipo kwetu, huyu ni mchezaji wetu na tuna mkataba naye Simba wanajisumbua", alisema Bikorimana

Mgosi ala shavu Simba, Mkude awa nahodha

Picha
Na Mrisho Hassan, Dar es Salaam Mshambuliajj na nahodha wa Simba, Mussa Hassan Mgosi ameteuliwa kuwa meneja wa Simba kuanzia leo kuchukua nafasi ya Abbas Seleman aliyepewa cheo kingine cha uratibu. Kwa maana hiyo Mgosi anastaafu rasmi kucheza soka la ushindani na sasa atakuwa bize katika kazi yake mpya ya umeneja, wakati Simba ikimpa ulaji Mgosi, kiungo mkabaji Jonas Mkude amechaguliwa kuwa nahodha mpya akirithi mikoba ya Mgosi. Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano wa Simba, Hajji Manara amethibitisha taarifa hizo, pia Manara amesema, Mchezaji Peter Mwalyanzi amepelekwa kwa mkopo African Lyon inayoshiriki Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara

Simba kuivaa URA J,pili

Picha
Na Prince Hoza Baada ya Jumatatu iliyopita kuipa kipigo kitakatifu AFC Leopards ya Kenya cha mabao 4-0, Kikosi cha Simba SC kinatelemka tena uwanja wa Taifa Dar es Salaam kuwavaa URA ya Uganda mchezo wa kirafiki wa kimataifa. Vijana wa Simba walicheza kandanda safi siku ya Jumatatu waliyosheherekea Simba Day ikiadhimisha siku yake ya kuzaliwa iliibuka na ushindi mnono wa mabao 4-0, magoli ya Simba yalifungwa na Ibrahim Ajibu (Mawili), Shiza Kichuya na Laudit Mavugo. Mashabiki wa Yanga wamekibeza kikosi cha Leopards wakidai ni dhaifu na ndio maana Simba kashinda mabao mengi hivyo URA inakuja kutoa ushindani kwa mianba hiyo, Leopards wanashika nafasi ya 12 ikiwa mkiani, lakini URA imekuwa ikiisumbuaga sana Simba hivyo Jumapili na mwisho wa ubishi

Azam yatangaza kikosi chake kamili, Farid nje, anakwenda Hispania

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam USAJILI KAMILI AZAM FC UONGOZI wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, unayofuraha kubwa kuwatangazia kuwa imemaliza kikamilifu hatua ya kwanza ya usajili wa wachezaji kwa ajili ya msimu ujao. Katika hatua hiyo ya kwanza iliyofungwa Jumamosi iliyopita saa 6.00 usiku, Azam FC tumewasajili jumla ya wachezaji 21 na kuwatoa wengine sita kwa mkopo. Wachezaji wapya walioingia katika orodha hiyo ni mabeki Bruce Kangwa anayetokea Highlanders ya Zimbabwe, Daniel Amoah kutoka Medeama ya Ghana pamoja na winga Enock Atta Agyei (Medeama). Mbali na nyota hao watatu wa kigeni, wachezaji wa msimu uliopita waliofanikiwa kupenya kwenye orodha hiyo ni makipa Aishi Manula, Mwadini Ally, mabeki Gadiel Michael, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, Aggrey Morris, Pascal Wawa, David Mwantika na kinda Ismail Gambo ‘Kusi’. Viungo ni Nahodha Msaidizi, Himid Mao ‘Ninja’, Jean Mugiraneza ‘Migi’, Michael Bolou, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Mudathir Yahya, Frank Domayo ‘Ch

Tulishatuma usajili wetu TFF- Yanga

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Uongozi wa Yanga umethibitisha kwamba ulishawasilisha usajili wake ndani ya Shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF na wanashangaa wanapoambiwa kwamba wamekaidi. Yanga ilishatuma usajili wake mapema kwenye mfumo wa TMS, Ila kwa siku za karibuni kulikuwa na matatizo ya mtandao ambapo kuna muda taarifa zilionesha usajili huo kuonekana na kutoonekana!ndipo Yanga SC walipowasiliana na wahusika waliambiwa ni matatizo ya mtandao. . Jumamosi ilikuwa siku ya mwisho na ndio siku tulikuwa na mkutano mkuu wa dharula, makamu mwenyekiti Clement Sanga aliwasiliana na katibu mkuu Baraka Deusdedit ambaye alithibitisha kuwa yametumwa! Leo sekretarieti ya Yanga itakaa na TFF kutolea ufafanuzi wa jambo hilo. . Tuwe na subira wala tusilaumiane tusubiri mrejesho wa maafikiano ya kikao hicho.

He kumbe Simba ilicheza na kibonde!

Picha
Na Saida Salum, Dar es Salaam Simba SC jana iliibamiza bila huruma AFC Leopards ya Kenya katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam mabao 4-0 mchezo wa kirafiki wa kimataifa wa kuadhimisha Simba Day. Magoli ya Simba yalifungwa na Ibrahim Ajibu (Mawili),  Shiza Kichuya na Laudit Mavugo, mashabiki wa Simba wakaanza kuchonga na kuwaambia wenzao wa Yanga kazi wanayo na wakikutana nao Oktoba 1 mwaka huu watawapiga 5-0. Lakini mashabiki wa Yanga bao wakawajibu wa Simba na kuwaambia wamecheza na timu dhaifu ambayo inakamata nafasi ya sita kutoka mkiani, kwa maana hiyo Leopards iko katika janga la kushuka daraja. Simba kama ingecheza na Gor Mahia au Interclube ya Angola huenda wasingeshangilia kama wanavyoshangilia sasa, walisema mashabiki wa Yanga waliokuwa uwanja wa Taifa kushuhudia mchezo huo

He kumbe Simba ilicheza na kibonde jana!

Picha
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM Mashabiki wa Simba wanatembea vifua mbele hasa baada ya timu yao jana kuichapa bila huruma AFC Leopards ya Kenya mabao 4-0 katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam, mchezo wa kuadhimisha tamasha la Simba Day. Katika mchezo huo wa kirafiki Simba ilipata mabao yake kupitia kwa Ibrahim Ajibu 'Kadabla' aliyefunga mawili, Shiza Kichuya na Laudit Mavugo waliofunga moja moja, mara baada ya kumalizika mchezo huo tambo zilianza kutolewa na mashabiki wa Simba. Wasikie watani zao Yanga wanachosema tena wakiwa na ushahidi mkononi, Kumbe Simba SC Ilicheza na timu dhaifu ambayo ilishindwa hata kulifikia lango la Simba, AFC Leopards inashikilia nafasi ya sita kutoka mkiani, kwa maana hiyo wanaweza kutelemka daraja

Simba yatakata Taifa, yaifumua AFC Leopards 4-0

Picha
Na Prince Hoza, DAR ES SALAAM SIMBA SC jioni ya leo katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam imeifanyia kitu mbaya AFC Leopards baada ya kuifumua mabao 4-0 mchezo wa kirafiki wa kimataifa kuadhimisha Simba Day. Simba inayonolewa na Mcameroon Joseph Marius Omog iliingia uwanjani kwa kasi ikiliandama lango la Leopards, Ibrahim Ajibu Migomba alitangulia kuipatia bao la kwanza timu yake lilikifungwa kipindi cha kwanza. Hadi mapumziko Simba walikuwa mbele kwa bao la kwanza, kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo vijana wa Simba waliweza kuongeza mabao mengine matatu, Ajibu aliongeza bao lingine la pili kabla ya Shiza Kichuya kuongeza bao la tatu. Wakicheza mbele ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe Poul Makonda, vijana wa Simba waliongeza bao la nne lililofungwa na Laudit Mavugo raia wa Burundi, hadi mpira unamalizika Simba 4 AFC Leopards 0

KIUNGO WA YANGA AKWAMA UMANGANI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar Kiungo wa zamani wa mabingwa wa soka Tanzania bara, Yanga SC, Abdi Kassim 'Babbi' amekwama kuendelea kuitumikia timu yake ya Ligi kuu nchini Malysia na sasa yupo yupo Zanzibar akihaha kusaka timu ya kujiunga nayo. Babbi mwenye rekodi ya kufunga bao la kwanza Uwanja wa Taifa Dar es Salaam akiwa na timu ya taifa, Taifa Stars, alijiunga na timu ya Malysia ambapo mkataba wake umenalizika. Baada ya kumalizika mkataba wake, Babbi ameshindwa kuendeleza mkataba mwingine hasa baada ya timu hiyo kushindwa kufikia maelewano naye, kiungo huyo amerejea Zanzibar akisaka timu

AVEVA ALIHAMISHIA DOLA 62,000 HONG KONG CHINA, YASEMA TAKUKURU

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya kupambana na rushwa nchini (Takukuru) imesema, rais w klabu ya Simba, Evans Aveva alihusika kuhamishia fedha za klabu zipatazo milioni 600 katika akaunti yake binafsi kutoka akaunti ya klabu. Pia rais huyo alituma Hong Kong China Dola 62'000 ambapo sasa Takukuru inawasiliana na wenzao wa Hong Kong ili kujua fedha hizo zimetumikaje. Aveva alishikiliwa katika kituo cha polisi cha Mabatini, Kijitonyama kwa siku mbili akidaiwa kukwapua fedha za usajilj wa mshambuliaji Emmanuel Okwi, fedha hizo zilitumwa na Etoile du Sahel ya Tunisia ambayo ilikuwa ikidaiwa baada ya kumsajili bila kuilipa Simba mpaka pale iliposhitaki FIFA ambayo nayo iliiagiza Etoile kuilipa Simba ama sivyo watawashusha daraja

Manji akodishwa Yanga miaka 10

Picha
Na Ikram Khamees, Dar es Salaam Wanachama wa klabu ya Yanga mchana wa leo kwa hiari yao wamekubaliana kumkodisha mwenyekiti wao ambaye pia ni Mkurugenzi wa Quality Group, Yusuph Mehbood Manji kwa kipindi cha miaka 10. Wakikubaliana kwa hiari wanachama hao wameridhia Manji apewe timu hiyo na sasa itakuwa mali yao binafsi, Manji ataiendesha klabu hiyo ambapo amesema atachukua asilimia 75 za mapato ya klabu na asilimia 25 ataziacha kw wanachama. Pia atabaki na timu pamoja na nembo ya klabu wakati jengo na mali nyinginezo zitasalia kwa wanachama, Manji amedai ataiendesha klabu hiyo na hata kama akipata hasara au faida hawezi kuachana nayo mpaka miaka kumi itimie. Wakati huo huo Manji amewafuta uanachama Salum Mkemi, Hashim Abdallah na Ayoub Nyenzi, Manji amesema hawezi kufanya nao kazi wanachama hao ambao pia ni wajumbe wa kamati ya utendaji, Manji aliungwa mkono na wanachama wote walioudhuria kwenye mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee

Aveva aachiwa huru na Takukuru

Picha
Na Salum Fikiri Jr, Dar es Salaam Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini (Takukuru) imemwachia kwa dhamana rais wa klabu ya soka ya Simba, Evans Elieza Aveva baada ya kumshikilia kwa muda wa siku mbili. Aveva alikamatwa juzi na maafisa wa Takukuru na alifikishwa katika kituo cha polisi cha Urafiki kilichopo Ubungo, bosi huyo wa Simba alihojiwa na taasisi hiyo kwa makosa ya kuhamisha fedha za klabu yake kwenye akaunti yake binafsi. Kamati ya utendaji na viongozi wengine wa klabu hiyo nao walihojiwa na Takukuru na baada ya kujiridhisha ikawaachia na rais Aveva naye akapewa dhamana  awali Takukuru ilikataa kumwachia kwa dhamana mpaka pale itakapokamilisha uchunguzi

Rage kumburuza mahakamani Hanspoppe

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Mwenyekiti wa zamani wa klabu ya Simba, Alhaj Ismail Aden Rage amemtaka mwenyekiti wa kamati ya usajili wa klabu hiyo Zacharia Hanspoppe kumuomba radhi ndani ya siku aaba ama sivyo atamfikisha mahakamani kutokana na kauli yake aliyoitoa jana ikisema Rage aliwahi kuhamishia fedha za usajili wa Mbwana Samatta kwenye akaunti ya mkewe. Akizungumza leo na kipindi cha michezo cha redio Efm, Rage amemtaka Zacharia Hanspoppe kumuomba radhi haraka kabla hajachukua maamuzi ya kwenda kumfungulia mashitaka mahakamani, 'Tayari nimeshaongea na mwnaasheria wangu na sasa nampa siku saba Hanspoppe kuniomba radhi ama sivyo nampandisha kizimbani', alisema Rage. Jana Hanspoppe akiongea kupitia redio hiyo alisema anawashangaa Takukuru kumkamata Evans Aveva kwa kosa la kuhamisha fedha za klabu ya Simba za usajili wa mshambuliaji Emmanuel Okwi wakati Ismail Aden Rage akiwa mwenyekiti wa Simba aliwahi kuhamisha fedha za usajili wa Mbwana Samatta kwenye akaunti ya mk

UZI WA SIMBA NA YANGA 2016/17 HUU HAPA

Picha
Na Prince Hoza, Dar es Salaam Vilabu vya Simba na Yanga na vinginevyo vinavyoshiriki Ligi kuu bara jana vimetambulisha jezi zao itakazotumia katika msimu unaotarajia kuanza Agosti 20 mwaka huu, wanamitindo jana walizitambulisha jezi hizo. Jezi za Simba zimeonekana kutulia zaidi kuliko za timu zote ingawa za Yanga zimeonekana kuvutia zaidi, uzinduzi huo wa jezi umefanyika jana

Fedha za Okwi zamtokea puani Aveva, ashikiliwa na Takukuru

Picha
Na Salum Fikiri Jr, Dar es Salaam TAASISI ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini (Takukuru) inamshikilia rais wa klabu ya Simba, Evans Elieza Aveva na amesekwa rumande katika kituo cha polisi Urafiki na muda wowote anaweza kufikishwa mahakamani. Takukuru haijaweka wazi kama imemkamata Aveva kwa kosa lipi, lakini Mambo Uwanjani inafahamu kwamba Aveva amekamatwa na Takukuru kwa kosa la kuhamisha fedha za usajili wa mshambuliaji Emmanuel Okwi katika akaunti yake binafsi. Fedha za Okwi kutoka Etoile de Sportive Sahel ya Tunisia zilitumwa kwenye akaunti ya Simba lakini rais huyo alihamishia kwenye akaunti yake binafsi, kukamatwa kwa bosi huyo ni siku chache mara baada ya kukutana na mfanyabiashara Mohamed Gulam Dewji 'Mo' ambaye anataka kuinunua klabu hiyo, Mo alitoa shilingi milioni 100 za kusaidia usajiki

Kipre Tchetche azitosa Simba, Yanga na Azam, asaini Al Na

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Mshambuliaji Kipre Herman Tchetche raia wa Ivory Coast ametambulishwa na timu ya Al Nahdha ya Oman inayoshiriki Ligi kuu na amezitosa kabisa Yanga na Simba ambazo zilivumisha kutaka kumsajili. Kipre aliyekuwa anakipiga Azam FC kwa mafanikio makubwa, ameamua kuachana nayo na jana akatambulishwa na uongozi wa timu ya Al Nahdha ya Oman, kwa maana hiyo Mshambuliaji huyo ameondoka rasmi kwenye soka la bongo

Azam yalazimishwa sare na JKT Ruvu

Picha
Na Mrisho Hassan, Dar es Salaam Mshambuliaji Atupele Green aliisawazishia timu yake ya JKT Ruvu, ikiwabana mbavu nyumbani Azam FC ya kufungana mabao 1-1 mchezo wa kirafiki. Atupele ambaye alikuwa akiwaniwa pia na Simba SC, aliisawazishia timu yake katika kipindi cha pili, Azam walikuwa wa kwanza kujipatia bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza likifungwa na beki wake Agrey Morris kwa mkwaju wa penalti. Katika mchezo huo beki Shomari Kapombe alicheza kwa mara yake ya kwanza tangu baada ya kufanyiwa upasuaji nchini Afrika Kusini

Simba yamleta Mavugo

Picha
Na Prince Hoza, Dar es Salaam BAADA ya bilionea Mohamed Gulam Dewji 'Mo' kuimwagia mamilioni, Klabu ya Simba imefanikiwa kumleta nchini mshambuliaji wa Vital'0 ya Burundi, Laudit Mavugo tayari kabisa kwa kujiunga nao. Mavugo alipokelewa na mashabiki wa Simba kwenye uwanja wa ndege wa Mwl Nyerere na alikabidhiwa jezi ya Simba yenye namba 45, kutua kwa mshambuliaji huyo aliyekuwa gumzo kwa muda mrefu kunafufua matumaini ya Wekundu hao katika kurejea kwenye makali yake. Mavugo anatarajia kusaini mkataba wa miaka miwili hivi karibuni na atatambulishwa kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifa wa kuadhimisha Simba Day dhidi ya Interclube Agosti 8 mwaka huu