Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2015

YANGA YAIFUATA SIMBA ZENJI

Picha
Wakati Simba imechagua Zanzibar kuwa kambi yake, kikosi cha cha mabingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, Yanga, nacho kinatarajiwa kwenda kujichimbia mjini humo kwa ajili ya kuweka kambi kujiandaa na msimu mpya wa ligi hiyo itakayoanzia Septemba 12, mwaka huu. Katibu Mkuu wa Yanga, Jonas Tiboroha, alisema jana kuwa wameamua kwenda visiwani humo ili kujiimarisha kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa ligi. Tiboroha alisema kwamba kambi hiyo itakuwa ya siku saba na lengo ni kuwafanya wachezaji waliobakia nchini kujijenga na kuwa imara tayari kukabiliana na ushindani wa mechi za ligi hiyo. "Tunataka wachezaji wenzao ambao wako na timu za taifa wakirudi wote wawe fiti kwa ajili ya kushindana ligi itakapoanza," alisema Tiboroha.

STARS KUKIPIGA NA LIBYA

Picha
Taifa Stars inatarajiwa kushuka dimbani leo Ijumaa kucheza mechi ya mazoezi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Libya ambayo pia imeweka kambi katika mji huu wa Kartepe, Uturuki. Taarifa zilizotoka jana usiku, mechi hiyo itapigwa saa 5 asubuhi kwa saa hapa pia nyumbani Tanzania Libya inanolewa na kocha maarufu na mkongwe duniani, Javier Clemente, raia wa Hispania, ambaye amewahi kuzifundisha klabu maarufu na timu mbalimbali za taifa. Clemente ,65, raia wa Hispania, aliyewahi kuzinoa klabu za Athletic Bilbao, Atletico Madrid, Real Betis, Real Sociedad, Espanyol na Tenerife, amesema ana imani Stars itampa ushindani. Clemente amesema amefurahishwa kuona Stars ina wachezaji wengi vijana.

ARSENAL WAWEKWA KUNDI MOJA NA BAYERN

Picha
Olivier Giroud  Arsenal watakutana na Bayern Munich Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya tatu katika misimu minne baada ya kuwekwa pamoja na klabu hiyo ya Ujerumani hatua ya makundi. Manchester United watakabiliana na PSV Eindhoven wanaporejea tena dimba hilo kuu la Ulaya, mshambuliaji wao mpya Memphis Depay akilazimika kukabili klabu aliyotoka kabla ya kuhamia Old Trafford. Chelsea nao watakabiliana na Porto, ambao kocha wao Jose Mourinho aliongoza kushinda dimba hilo 2004. Manchester City wamepangwa kundi moja na Juventus kutoka Serie A, mabingwa wa Europa League Sevilla na Borussia Monchengladbach ya Ujerumani. Vijana wa Arsene Wenger pia watakutana na Olympiakos ya Ugiriki na Dinamo Zagreb ya Croatia.

MAKALA: WAKUBWA WANAPOAMUA KWA MECHI MOJA, WAKUSAJILI AMA WAKUTIMUE

Picha
Na Prince Hoza SOKA ni mchezo wa bahati, unaweza kumuona mchezaji fulani aa kiwango kizuri kwa kucheza vizuri kwenye mechi moja na ukamuamini mpaka kufikia hatua ya kumpa mkataba, lakini anapocheza mechi nyingine ya pili anachemsha na baadaye mnaanza kulaumiana wenyewe kwa wenyewe kwanini mmepitisha usajili wake. Ndivyo ulivyo mchezo wa soka, bahati huchukua nafasi yake, lakini pia kuna bahati nzuri na bahati mbaya, katika mcheZo wa soka mchezaji anaweza akawa na sifa nyingi huko alikotoka na akasajiliwa timu nyingine ili aonyeshe makali yake ila kwa bahati mbaya akashindwa kuonesha kile alichokuwa akikionyesha mwanzo. Mchezaji huyo yapaswa umpe muda mwingine ili ujiridhishe naye, lakini ukimkatia tamaa kwa mechi moja tu, unaweza kuchuma dhambi za bure na kumrudisha kwao. Simba SC imeshawarudisha makwao wachezaji zaidi ya wawili, ilianza na Daniel Akufor baadaye Gervais Kago na sasa Papa Niang, na tayari imewaleta nchini washambuliaji wengine wawili ambao ni Pape Abdoulaye N&

HALL AIKUBALI MUZIKI WA YANGA SC

Picha
Baada ya kuikosa Ngao Jamii kwa mara ya pili mfululizo mbele ya Yanga, Kocha Mkuu wa Azam FC, Muingereza Stewart Hall, amekiri kuwa vijana hao wa Mholanzi Hans van der Pluijm waliwazidi uwezo katika mechi hiyo iliyopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam juzi. Hall pia alifafanua kuwa timu yake haikuwa vizuri katika dakika 20 za mwisho na walionekana wako tayari kusubiri kufika hatua ya matuta jambo ambalo halikuwa sahihi. Kocha huyo alisema mechi hiyo ilikuwa ngumu na yenye ushindani kwa timu zote mbili hali iliyosababisha kumalizika dakika 90 za kawaida bila ya kufungana. "Katika soka lazima uwe fiti kila upande, kama hauko fiti labda ukacheze mpira wa kikapu," alisema Hall. Aliongeza kuwa mashabiki wa Yanga walisaidia pia kuipa ushindi timu yao, jambo lililowafanya wachezaji wao kujiona kama wako 12 kitu ambacho timu yake inakikosa. "Nataka kusema jambo moja, mashabiki wa Yanga walifanya vizuri sana kuisaidia timu yao kwa kuishangilia, kitu ambacho sisi hatuna, k

Kolarov, Nasri wasaidia Man City kutua kileleni

Picha
Aleksandar Kolarov Aleksandar Kolarov na Samir Nasri waliwezesha Manchester City kupata ushindi nadra wa 2-0 ugenini Everton Jumapili wakifikia rekodi ya klabu hiyo na kuwafikisha kileleni mwa Ligi ya Premia. City walikuwa awali wameshinda mechi moja pekee kati ya sita walizochezea Goodison Park – ushindi huo wa pekee ukiwa kwenye safari yao ya kushinda taji 2014. Kutwaa tena taji hilo ndilo lengo lao msimu huu baada yao kutumia pesa nyingi tena kujengwa upwa kikosi, hesabu ambayo huenda ikaongezeka wakifanikiwa kushawishi Wolfsburg kuwauzia kiungo muhimu Kevin De Bruyne. Vijana hao wa Manuel Pellegrini wamepata mwanzo bora zaidi kwenye kampeni yao baada ya kuandikisha ushindi mara tisa mfululizo ligini kwa mara ya kwanza tangu 1912 na kufikisha kikomo mwanzo wa kutoshindwa wa Everton msimu huu.

MAKALA: YANGA SC NDIYO MABINGWA WA KIHISTORIA WA NGAO YA HISANI

Picha
MLINDA mlango Ally Mustapha 'Barthez' amepangua penalti mbili na kuiwezesha Yanga SC kutwaa Ngao ya Hisani baada ya kuifunga Azam FC kwa penalti 8-7 kufuatia sare ya 0-0 ndani ya dakika 90 jioni ya Jumamosi ya Agosti 22 uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Barthez alipangua penalti za beki raia wa Ivory Coast Serge Wawa Pascal na mshambuliaji Ame Ali 'Zungu', wakati kipa wa Azam FC Aishi Manula naye alicheza penalti ya nahodha wa Yanga Nadir Haroub 'Cannavaro'. Penalti za Yanga SC zilifungwa na Haruna Niyonzima 'Fabregas', Deus Kaseke, Amissi Tambwe, Andrey Coutinho, Godfrey Mwashiuya, Thabani Kamusoko, Mbuyu Twite na Kelvin Yondani aliyefunga ya mwisho. Penalti za Azam FC zilikwamishwa wavuni na Kipre Thetche, nahodha John Raphael Bocco, Himid Mao, Aggrey Morris, Erasto Nyoni, Shomari Kapombe na Jean Bapstita Mugiraneza 'Migi', ushindi huo wa Yanga SC ni sawa na kulipiza kisasi baada ya kufungwa kwa penalti 5-4 katika robo fainali ya klabu bingw

WANACHAMA CUF WAKINUKISHA OFISINI KWAO LEO ASUBUHI, HOFU YA LIPUMBA KUJIUZURU YATANDA

Picha
WANACHAMA wa Chama cha Wananchi (CUF) wamevamia makao makuu ya chama hicho leo asubuhi na kusababisha kikao cha mwenyekiti Profesa Ibrahim Lipumba na wanahabari kuhairishwa. Mkutano wa mwenyekiti huyo ulikuwa ufanyike leo saa nne asubuhi makao makuu ya Cuf yaliyopo Buguruni, Dar es Salaam lakini hadi saa tano, mwenyekiti alikuwa kwenye kikao cha ndani na “wazee wa chama” waliokuwa wanataka ufafanuzi kwa baadhi ya mambo. “Wazee wanataka ufafanuzi kwa baadhi ya mambo ikiwa ni pamoja na taarifa zilizoenea kuwa amejiuzulu,” amesema Magdalene Sakaya, Naibu Katibu Mkuu Bara amewaamabia wanahabari.

DI MARIA AFURAHIA KUJIUNGA NA PSG

Picha
Winga wa timu ya taifa ya Argentina Angel Di maria amefurahishwa na uhamisho wake toka Manchester United na kujiunga na matajiri wa Psg. Nyota huyu mwenye umri wa miaka 27 alifanyiwa vipimo vya afya huko Qatar na kukamilisha uhamisho wake uliogharimu kiasi cha pauni milioni 44.3. Baada ya uhamisho huo kukamilika Di Maria alisema ana furaha kujiunga na Paris St –German .Lakini vilabu vya Manchester United na Psg havijatangaza rasmi kukamilika kwa uhamisho huo .

YANGA YAMTEMA RASMI ZUTTAH

Picha
Mabingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, timu ya Yanga ya jijini Dar es Salaam, imemuondoa rasmi katika orodha ya usajili beki wake wa kimataifa, Mghana Joseph Zutah. Kwa mujibu wa habari zilizopatikana jijini jana kutoka ndani ya uongozi wa klabu hiyo, zinaeleza kuwa Zutah anatarajiwa kuondoka nchini leo na kurejea kwao Ghana. Taarifa zaidi kutoka Yanga zinaeleza kuwa licha ya kuwa mchezaji huyo alishalipwa fedha za awali za usajili ambazo ni Dola za Marekani 10,000, kiwango chake hakijawaridhisha viongozi wa klabu hiyo. "Tayari wameshakubaliana aondoke na kesho (leo), ndiyo anaondoka nchini kurudi kwao," kilieleza chanzo chetu. Habari zaidi zinaeleza kuwa, Yanga imeamua kuachana na nyota huyo kutokana na kutoridhishwa na kiwango chake alichoonyesha kwenye michuano ya Kombe la Kagame baada ya kuona hana tofauti na wazawa wengi ambao si wa gharama kama yeye.

MAAJABU YA CHIFU PANDUKA YAZIDI KUWAVUTIA WENGI

Picha
Yule mganga maarufu Chifu Panduka aliyerejea hivi karibuni kutokea falme za Kiarabu na kufikia katika kituo chake kilichopo Tabata jijini amezidi kuwavutia wengi kutokana na miujiza yake ya kutumia utabiri. Mganga huyo ambaye aliwahi kutabiri kuwa CCM kitapata mchituko mkubwa wa kuondokewa na mwanasiasa wake maarufu na kweli ikatokea hivyo baada ya aliyekuwa waziri mkuu wa kwanza wa serikali ya awamu ya nne ya Jakaya Kikwete, Edward Lowassa kukihama chama hicho na kujiunga na wapinzani. Lowassa amehamia Chadema ambacho nacho kimemtangaza kuwa mgombea wake katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 25 mwaka huu, mganga huyo anayetumia nyoka wake wa maajabu anazidi kuwashangaza wengi kufuatia juzi kutangaza mshindi wa kiti cha urais wa jamhuri ya muungano.

CHAMBERLAIN AIWEZESHA ARSENAL KUICHAPA CHELSEA 1-0

Picha
Mabingwa Kombe la FA Arsenal waliwalaza mabingwa wa ligi Chelsea 1-0 katika mechi ya Community Shield, ambayo hutumiwa kufungua msimu mpya wa ligi Uingereza, iliyochezewa Wembley Jumapili. Bao safi la Alex Oxlade-Chamberlain dakika ya 24 lilitosha kuamua mshindi wa mechi hiyo iliyochezewa katika anga yenye jua kiasi. Mchezaji huyo wa miaka 21 alipokea pasi kutoka kwa Theo Walcott, akambwaga difenda wa Chelsea Cesar Azpilicueta before na kisha kutuma kombora kona ya juu ya goli, kombora ambalo Thibaut Courtois hakuweza kulizuia. Ilikuwa mara ya kwanza katika majaribio 14 kwa meneja wa Arsenal Arsene Wenger kumpiku mkufunzi wa Chelsea Jose Mourinho na matokeo hayo yaliwapa matumaini kwa wapinzani wa Chelsea kwamba huenda wasiwe na mteremko kama waliokuwa nao msimu uliopita.

SHERMAN APIGWA BEI 'SOUTH', MILIONI 300 ZATUA YANGA

Picha
MSHAMBULIAJI wa Yanga SC, Mliberia Kpah Sean Sherman amesaini Mkataba wa miaka mitatu na klabu ya Mpumalanga Black Aces ‘AmaZayoni’ ya Afrika Kusini. Habari za ndani zinasema Yanga SC italipwa dola za Kimarekani 150,000 (Sh. Milioni 300) kama ada ya uhamisho ya mchezaji huyo aliyesaini Jangwani kwa dola 60,000 (Sh. Milioni 120,000) Desemba mwaka jana. Na Sherman aliyekuwa analipwa doka 3,000 (Sh. Milioni 6) kwa mwezi Yanga SC, sasa atakuwa analipwa dola 5,000 (Sh, Milioni 10) Black Aces kabla ya kukatwa kodi. Mwenyekiti wa Aces, Mario Morfou amesema kwa simu leo kwamba wanatarajia Sherman atakuwa pacha mzuri wa Mzambia, Collins Mbesuma katika safu ya ushambuliaji ya timu yake msimu huu. “Ni mchezaji mzuri na mmoja wa wachezaji bora sana tuliowahi kusaini na sasa tunajivunia kuwa naye AmaZayoni,” amesema Morfou. Sherman alijiunga na Yanga SCS Desemba mwaka jana akitokea klabu ya Cetinkaya ya Ligi Kuu ya Cyprus Kaskazini na katika kipindi hicho ameichezea timu ya Jangwani mechi 27 na k

UBINGWA WA AZAM NI HISTORIA NYINGINE CECAFA

Picha
Azam imeandika historia mpya kwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Kagame bila ya kufungwa bao lolote, baada ya kuichapa Gor Mahia ya Kenya kwa mabao 2-0 jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mabao ya John Bocco na Kipre Tchetche yalitosha kuifanya Azam kutawazwa kuwa ufalme wapya na kufanikiwa kulibakiza kombe hilo katika ardhi ya Tanzania kwa rekodi ya aina yake ya kutoruhusu bao lolote katika michezo yake sita ya mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika Mashariki na Kati. Azam ilianza kwa kushinda 1-0 dhidi ya KCCA, ikaichapa Al Malakia 2-0, ikimaliza hatua ya makundi kwa kuisambaratisha Adama City 5-0, katika robo fainali ikitoa Yanga kwa penalti 5-3, na nusu fainali ikaishinda KCCA 1-0 na fainali 2-0 dhidi ya Gor Mahia.

MANJI WA YANGA, FELLA WA MKUBWA NA WANAYE WAIBUKA KIDEDEA UDIWANI

Picha
Wadau wawili wa michezo na burudani nchini; Yusuf Manji na Said Fella wameibuka kidedea katika kinyang’anyiro cha udiwani katika jimbo jipya la Mbagala jijini hapa. Manji ambaye ni Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Quality Group, alishinda katika udiwani katika Kata ya Mbagala Kuu wakati Fella ambaye ni msimamizi wa kazi za wasanii na muasisi wa Kundi la Mkubwa na Wanawe, alishinda katika Kata ya Kilungure. Fella ni Meneja wa mwanamuziki maarufu nchini, Diamond Platnumz, TMK Family na Yamoto Band. Kaimu Katibu CCM Wilaya ya Temeke, Rutami Masunu alisema uchaguzi huo ulikwenda vizuri katika maeneo mengi isipokuwa changamoto kidogo katika kata moja ambayo itafanya uchaguzi huo leo. Alisema tayari matokeo ya kata 28 kati ya 32 za wilaya yake yamewasilishwa ofisini kwake na baada ya kuyapitia na kukusanya taarifa zinazowahusu madiwani na wabunge na muda wowote leo atatoa taarifa kamili.

MTOTO WA SOKOINE AMRITHI LOWASSA MONDULI

Picha
Binti wa Waziri mkuu wa zamani, Edward Sokoine, Namelock Sokoine ameshinda kura za maoni kugombea ubunge Jimbo la Monduli kupitia CCM huku mkwe wa Lowassa, Siyoi Sumari akishindwa Jimbo la Arumeru Mashariki. Namelock ambaye ni mbunge wa Viti Maalumu (CCM) alipata kura 29,582 akifuatiliwa na Loota Sanare aliyepata kura 8,809 na nafasi ya tatu, ilichukuliwa na Lolinyu Mkoosu aliyepata kura 235 na Payani Leyani akipata kura 226. Arumeru Mashariki: Sumari aliyewania jimbo hilo kwa mara ya kwanza baada kifo cha baba yake Jeremia Sumari na kushindwa na Joshua Nassari wa Chadema alipata kura kura 3,664 dhidi ya 12,071 za John Pallangyo. Mshindi wa tatu alikuwa ni William Sarakikya ambaye alipata kura 3,552 na wagombea hao waliwaacha mbali wapinzani wao wengine wanne. Arusha Mjini: Katika Jimbo la Arusha Mjini, mfanyabiashara Philemon Mollel ameshinda kwa kura 5,320, akifuatiliwa na mfanyabiashara mwingine Justine Nyari aliyepata kura 1,894 na nafasi ya tatu, ilichukuliwa na Moses Mwiz