Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2014

PODOLSKI KUIKOSA ALGERIA LEO

Picha
Mshambulizi wa Ujerumani na Arsenal ya Uingereza Lukas Podolski hatoweza kushiriki mechi ya mkondo wa pili kati ya Ujerumani na Algeria iliyoratibiwa kuwa Porto Alegre.

WADAU WAMTEMBELEA KIMWAGA WA AZAM FC

Picha
WADAU wa soka na mashabiki wa Azam FC wamejitokeza kwa wingi kwenda kumpa hali mchezaji huyo aliye majeruhi kwa muda mrefu sasa.

ROBBEN AKIRI KUJIANGUSHA KUMDANGANYA REFA AWAPE PENALTI UHOLANZI

Picha
WINGA Arjen Robben alijaribu kumdanganya refa katika mchezo wa 16 Bora jana Kombe la Dunia, Uholanzi ikiifunga mabao 2-1 Mexico na kwenda Robo Fainali. Mholanzi huyo alisema kwamba alijirusha kutafuta penalti, lakini lie iliyotolewa dakika ya tatau ya muda wa nyongeza baada ya kutimia dakika 90 za kawaida, ambayo Uholanzi waliitumia kusonga mbele katika mbio za kukimbilia Kombe la Dunia.

MAPOPO FC YAZIDI KUCHANJA MBUGA CHALINZE

Picha
TIMU ya soka ya Mapopo FC ya Mdaula Chalinze mkoani Pwani (Pichani nikikosi cha Mapopo FC) imezidi kuchanja mbuga katika michuano ya kuwania mbuzi mnyama baada ya kuilaza timu ngumu ya Majengo FC mabao 2-0 katika uwanja wa shule ya Mdaula.

HAMOSNOTA KUIBUKIA IDD NA ZAWADI YA MAMA

Picha
Na Prince Hoza MSANII chipukizi anayekuja kasi kwa sasa ambaye anatamba na wimbo wake wa 'Bye bye' Hashimu Momba 'Hamosnota' ameamua kumletea zawadi ya Idd mama yake mzazi lakini mashabiki wake ndio watakaoipokea siku ya sikukuu ya Idd el fitr. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi hivi karibuni, Hamosnota amesema anatarajia kuitambulisha nyimbo yake mpya iitwayo 'Safari kwa mama' ambapo ataiachia siku ya sikukuu ya Idd El Fitr.'Ifikapo Idd El Fitr nitaachia wimbo mpya unaokwenda kwa jina la 'Safari kwa mama' nimeamua kutunga wimbo huu kwa ajili ya wale wanawake wanaokwenda mara kwa mara kwa mama zao wakati wakiwa ndani ya ndoa', alisema na kuongeza.

THOMAS MULLER WA UJERUMANI AITOA KAMASI URENO NA RONADLO WAO, AANDIKISHA REKODI MPYA YA HAT TRIK

Picha
Furaha tupu wagumu hao: MJERUMANI Thomas Muller awa mchezaji wa kwanza  kufunga mabao matatu katika mechi moja `hat-trick`  kwenye fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil baada ya kuiongoza nchi yake kuilaza Ureno mabao 4-0 usiku huu mjini Salvador. Nyota huyo wa Bayern Munich alifunga bao la kuongoza dakika za mapema kwa mkwaju wa penati na kuwapa mwanzo mzuri katika uwanja wa Arena Fonte Nova wana nusu fainali hao wa mwaka 2010 nchini Afrika kusini.

GHANA NDEMBENDEMBE KWA MAREKANI YA OBAMA, YADUNGULIWA 2-1

Picha
MAREKANI imeendeleza kilo kwa timu za Afrika, baada ya usiku wa kuamkia leo kuifunga Ghana mabao 2-1 katika mchezo wa Kundi G Kombe la Dunia nchini Brazil. Shukrani kwao, Clint Dempsey aliyefunga bao la kwanza sekunde ya 31 baada ya kuwachambua mabeki wa Ghana na John Brooks aliyefunga la pili kwa kichwa dakika ya 86. Nyie waafrika nasikia mdebwedo tu Mshambuliaji huyo wa zamani wa Fulham, aliifungia timu ya Jurgen Klinsmann bao kla ushindi dkika nne tu tangu Andre Ayew aisawazishie Ghana.

WEMA AKANA UJAUZITO WA DIAMOND

Picha
Sina ujauzito wa Diamond nyie nani kawaambia Baada ya stori nyingi kuzagaa kuwa mwigizaji na mpenzi halali wa mwanamuziki wa bongo fleva Diamond Platinumz – Wema sepetu kuwa yu mjamztio wa wiki 7 na mimba ya msanii huyo, hatimaye jana mwanadada huyo ameamua kufunguka “exclusively” kwenye mtandao mmoja wa kijamii na kujibu habari hizo akisema haya yafuatayo kuwa hajabahatika kuwa na ujauzito.

KANISA LAWATAKA WAUMINI WAKE KUFANYA MAZOEZI YA VIUNGO

Picha
Na Mariamu Libibo UTAIPENDA tu: Kanisa la wasabato lililopo Tabata Mbuyuni jirani na maghorofa ya NSSF Aroma jijini Dar es Salaam limewataka waumini wake kufanya mazoezi mara kwa mara ili kuondokana na ugonjwa wa saratani ya matiti na kupunguza uzito wa mwili. Mazoezi ya viungo yanasaidia kupunguza uzito pamoja na maradhi ya saratani ya matiti kwa akina mama, amesema Mtoa mada hayupo pichani Wito huo umetolewa jana wakati mtoa mada akiwaelimisha waumini wa dhehebu hilo wakiwemo wamama na wababa waliofurika kumsikiliza mtoa mada huyo, aliwataka waumini hao kufanya mazoezi ya viungo kila siku ili kuondokana na maradhi ya saratani ya matiti inayoenea kwa kasi hapa nchini.

WAMBURA AMSHANGAA NDUMBARO KUMFUTA SIMBA

Picha
Na Prince Hoza ALIYEKUWA mgombea wa nafasi ya urais katika klabu ya Simba Michael Richard Wambura ambaye alirejeshwa hivi karibuni na kamati ya rufaa ya TFF, amemshangaa mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi wa klabu ya Simba wakili Damas Daniel Ndumbaro kwa kumfuta kabisa katika nafasi huyo wakati yeye akiwa ajarejeshwa rasmi. Wambura anasema, Ndumbari vipi tena: mimi nilishaenguliwa na kamati yako nashangaa kunifuta kabisa, wapi? Wambura amecheka kwanza kisha akasema, Ndumbaro si mwadilifu katika taaluma yake na ndio maana aliwahi kumwambia aende tena darasani, 'mimi sijarejeshwa rasmi katika kinyang'anyiro hicho nashangaa anatangaza mbele ya waandihsi amenifuta', alisema Wambura.

AZAM FC YAZIVUTIA KASI YANGA, TP MAZEMBE

Picha
Mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara Azam Fc leo wameanza Rasmi mazoezi ya kujiandaa na ligi kuu Tz Bara pamoja na Mashindano ya ligi ya mabingwa Afrika, hizo ni salamu kwa Yanga ambao ni washindi wa pili wa ligi kuu Tanzania bara na wawakilishi wa michuano ya kombe la shirikisho mwakani. Pia Yanga watakutana nayo Agosti katika mechi ya ngao ya hisani, mwaka jana timu hizo zilikuatana katika mechi kama hiyo na Azam ilikubali kichapo cha bao 1-0 hivyo mwaka huu haitakubali kufungwa na ndio maana wameingia kambini upesi.

UFARANSA YAFAIDI TEKNOLOJIA YA GOLI

Picha
Ufaransa yafaidi Teknolojia ya kuwasaidia marefarii Brazil 2014 Ufaransa ndiyo timu ya kwanza kuwahi kufaidi matumizi ya teknolojia ya kisasa kuzuia ubishi katika mechi ya kombe la dunia linaloendelea huko Brazil.

IVORY COAST ILIVYOITAKATISHA AFRIKA

Picha
Miamba ya soka barani Afrika Ivory Coast imeimarisha matumaini ya bara hili baada ya kutoka nyuma na kuishinda Japan kwa mabao mawili kwa moja.

SIMBA KWAZIDI KUWAKA MOTO, KAMATI YA NDUMBARO YAMFYEKA KABISA WAMBURA, YAMGOMEA MALINZI

Picha
Dk Ndumbaro kulia akizungumza leo KAMATI ya Uchaguzi ya Simba SC imesema kwamba, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) halina mamlaka kikatiba kusimamisha uchaguzi wa klabu hiyo, na maana yake uchaguzi huo upo kama ulivyopangwa kufanyika Juni 29, mwaka huu. Pamoja na hayo, Kamati hiyo imesema imemuondoa moja kwa moja mgombea Michael Richard Wambura kwenye kinyang’anyiro hicho kwa sababu amerudia kosa ambalo aliwahi kupewa onyo.

MESSI AIONGOZA ARGENTINA KUSHINDA 2-1 KWA MBINDE KOMBE LA DUNIA

Picha
ARGENTINA imeanza vyema Kombe la Dunia baada ya usiku wa jana kuilaza Bosnia-Herzegovina mabao 2-1 katika mchezo wa Kundi Kombe la Dunia Uwanja wa Maracana mjini  Rio de Janeiro, Brazil.

UKICHEZA SIMBA AU YANGA NDIO UNACHAGULIWA TAIFA STARS- CASILAS

Picha
Na Prince Hoza MLINDA lango wa kutumainiwa wa timu ya Mtibwa Sugar ya Manungu Turiani mkoani Morogoro Hussein Sharrif 'Cassilas' ambaye pia ndiye kipa bora wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara (2013/14) ameponda kauli zinazotolewa na wadau wa soka hasa baada ya yeye kutangazwa kipa bora. 'Mimi ndio kipa bora lakini siwezi kuitwa Stars labda niwe Simba, Yanga au Azam', anasema Casilas.

WAWAKILISHI WA AFRIKA KOMBE LA DUNIA KUTUPA KARATA YAO LEO

Picha
Cameroon kukabiliana na Mexico baadaye leo Baada ya kushuhudia mechi ya kwanza ya fainali ya kombe la dunia la mwaka huu huko Brazil,mamilioni ya mashabiki kutoka bara Afrika hii leo watafungua macho na kupaza sauti zao wawakilishi wa kwanza wa Afrika The Indomitable lions wa Cameroon ikitoana kijasho na Mexico katika mechi ya pili ya kundi A. Timu hizi zimewahi kukutana mara moja pekee kabla ya hii leo.Mexico ilishinda mechi hiyo ya kujipima nguvu kwa bao moja kwa nunge.

JENNIFER LOPEZ ALIVYOPAGAWISHA UFUNGUZI KOMBE LA DUNIA

Picha
+23 Mwanamuziki J-Lo akipagawisha mashabiki wakati wa sherehe za ufunguzi wa Fainali za Kombe la Dunia 2014 kabla ya mchezo wa kwanza wa Kundi A baina ya Brazil na Croatia usikuwa jana Uwanja wa Corintias mjini Sao Paulo.

UWANJA WA SIMBA BUNJU KINAELEWEKA

Picha
MATENGENEZO ya uwanja mpya na wa kisasa wa klabu ya Simba kama ilivyoahidiwa na uongozi unaomaliza muda wake chini yake Alhaj Ismail Aden Rage umeanza kutengenezwa na muda si mrefu utakuwa tayari kwa wana hao wa Msimbazi ambao kwa sasa macho yao yapo kwenye uchaguzi ujao. Tayari shughuri za ujenzi zinaendelea ambapo maroli yamekuwa yakimwaga vifusi katika eneo hilo la uwanja wa klabu ya Simba huku watani zao Yanga wakimuongezea mwaka mmoja mwenyekiti wao Yusuf Manji ili afanye usajili.

NEYMAR AANZA KUUTAFUTA UFALME BRAZIL AIONGOZA KUIA CROATIA 3-1

Picha
MWANZO mzuri kwa Neymar akifunga mabao mawili usiku wa jana, wenyeji Brazil wakianza vyema Fainali za Kombe la Dunia kwa ushindi wa 3-1 dhidi ya Croatia Uwanja wa Corinthias, mjini Sao Paulo.

MAKALA: ACHENI PROPAGANDA, WAMBURA SIYO YANGA

Picha
Na Prince Hoza (Mbabe: Wambura akiwapungia wafuasi wake mara baada ya kutangazwa mshindi wa rufaa yake aliyopinga kuenguliwa Simba. MARA baada ya kamati ya rufaa ya shirikisho la soka nchini TFF kutengua maamuzi ya kamati ya uchaguzi ya klabu ya Simba inayoongozwa na mwanasheria Damas Daniel Ndumbaro na kumrudisha tena katika kinyang'anyiro cha uchaguzi wa klabu hiyo Michael Richard Wambura.

MAMBO UWANJANI TV: MAJIBIZANO TOKA VIJIWENI

HIVI karibuni mtandao huu unakuja na kipindi chake kipya kijulikanacho kama Mambo uwanjani TV ambapo kutakuwa na makala mbalimbali za michezo zitaonyeshwa ama mtangazaji kuchambua habari huku majibizano kutoka katiika vijiwe mbalimbali jijini Dar es Salaam.

MALINZI AIKATAKATA YANGA, APINGA MANJI KUONGEZEWA MWAKA MMOJA

Picha
Wakati Shirikisho la Soka nchini (TFF) likiwa halijapokea rasmi maamuzi ya kusogeza mbele Uchaguzi Mkuu wa Klabu ya Yanga, Rais wa shirikisho hilo, Jamal Malinzi, amesema katika uongozi wake hataruhusu kuona wanachama wanafanya maamuzi yaliyo kinyume na katiba za vyama na klabu zao. Wanachama wa Yanga waliokutana Juni Mosi, mwaka huu katika mkutano wa marekebisho ya katiba, pia walikubaliana kusogeza mbele uchaguzi mkuu wa klabu hiyo hadi Juni 15, mwakani.

NANDO ATANGAZA NDOA KWA LULU

Picha
Na Robert Michael Habari mpya ni kuhusu mshiriki wa Big Brother Africa 2013 Nando kuzimika kwenye penzi la staa wa filamu Swahiliwood Elizabeth Michael " lulu". Akizungumza na mtandao huu Nando amesema kuwa anampenda sana Lulu (Pichani ) na yupo tayari kumuoa kwa sababu ni wife material ingawa bado hajamwambia mwenyewe hilo. Nando pia alisema kuwa anapenda sana kazi za filamu za Lulu na angependa kufanya nae filamu ziku za usoni "Lulu ni mkali, niko tayari kumuoa lakini sijamwambia, akikubali freshi nitamuoa. Kwa sasa ni mshikaji wangu tu na napenda kazi zake. Huwa ni mtu ambaye napenda kufuatilia ishu zake"

WAGENI WASITISHA MGOMO BRAZIL

Picha
Maafisa wa polisi wakimzuia mwandamanaji nchini Brazil Vuguvugu la watu wasio na makaazi nchini Brazil ambalo limekuwa likiunga mkono maandamano ya kupinga kombe la dunia sasa wametangaza kuwa wamesitisha maandamano hayo muda wote wa dimba hilo.

HAPANA CHEZEA CRISTIANO RONALDO, AIONGOZA URENO KUUA MTU YANGA

Picha
ILIMCHUKUA sekunde 52 Cristiano Ronaldo kuithibitishia dunia kwamba amepona na yuko fiti kwa Fainali za Kombe la Dunia wakati Ureno ikiitandika Jamhuri ya Irelando mabao 5-1 jana katika mchezo wa kirafiki Uwanja wa MetLife.

ULAYA WAMTAKA BLATTER AJIUZULU

Picha
Jiuzuru baba:  Maafisa wa kandanda wa Europa sasa wamemtaka rais wa shirikisho la kimataifa la kandanda FIFA, Sepp Blatter, ajuzulu kutokana na madai ya rushwa yanayoindama Fifa. Wametilia shaka uongozi wake.

JK AIFARIJI FAMILIA YA MZEE SMALL

Picha
Na Mariamu Libibo RAIS wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete jana aliwaongoza mamia ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam kumzika aliyekuwa msanii maarufu wa maigizo nchini Said Ngamba kwa jina maarufu Mzee Small Wangamba yaliyofanyika katika makaburi ya Tabata Segerea. Rais Kikwete alienda msibani nyumbani kwa marehemu Tabata Kisiwani na kuwafariji wafiwa ambapo pia alizungumza na familia ya marehemu, haijawahi kutokea kwa Tanzania kutembelewa na rais hasa kwenye misiba ya wasanii na wanamichezo. Lakini Rais Kikwete akiongozwa na walinzi wake alishiriki katika mazishi ya msanii huyo mkongwe ambaye alikuwa akisumbuliwa kwa muda mrefu, mbali ya Kikwete kuudhuria msiba huo wasanii mbalimbali nchini nao walishiriki katika mzishi hayo ya msanii huyo mkongwe ambaye anatajwa kama muasisi wa sanaa ya maigizo nchini.

TIMU NYINGI ZINANITAMANI: FERDINAND

Picha
Beki mashuhuri aliyefungia muda wake Manchester United msimu uliopita, Rio Ferdinand (Pichani) , ametangaza kuwa vilabu vingi vinatamani huduma zake. Ferdinand, 35, alichezea magwiji wa ligi ya Premier United miaka 12 baada ya kuwaunga kutoka Leeds United 2002. Alichezea Uingereza mara 81 lakini alikosa Kombe la Dunia la 2010 kufuatia jeraha la goti licha ya kutajwa kama kapteni.

KANALI MWANAKATWE KUZIKWA LEO MANYARA

Picha
Na Boniface Wambura, DAR ES SALAAM MAZISHI ya aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wakati huo likiitwa FAT, Kanali mstaafu Ali Hassan Mwanakatwe yanafanyika leo (Juni 10 mwaka huu) Magugu, Babati mkoani Manyara. Kanali Mwanakatwe alifariki dunia Juni 7 mwaka huu katika Hospitali Kuu ya Jeshi (GMH) Lugalo jijini Dar es Salaam wakati akipatiwa matibabu baada ya kuanguka bafuni nyumbani kwake Mbezi Beach.

FILIPPO INZAGHI KOCHA MPYA AC MILAN

Picha
Enzi zake Inzaghi akisakata soka, sasa ni kocha mpya AC Milan AC Milan imemfuta kazi mkufunzi wake Clarence Seedof baada ya kuhudumu kwa chini ya miezi 5 na kumtangaza Filipo Inzaghi kama kocha mpya.

NEYMAR AUMIA MAZOEZINI, LAKINI........

Picha
MASHABIKI na wapenzi wa soka Brazil jana waliingiwa hofu kufuatia mshambuliaji wao nyota, Neymar kukaa chini mazoezini akiugulia maumivu ya kifundo cha mguu na kuzua hofu juu ya uimara wake keuelekea Kombe la Dunia. Nyota huyo wa Barcelona aliumia enka wakati wa mazoezi Selecao nje ya Rio de Janeiro na kumlazimisha kupata huduma ya kwanza uwanjani.

KWAHERI LAMPARD, ANAONDOKA CHELSEA

Picha
KIUNGO Frank Lampard anaondoka Chelsea baada ya kuitumikia kwa miaka 13 na klabu hiyo sasa inaisaka saini ya Cesc Fabregas arithi mikoba.

STAR WARS YAMNYAKUA LUPITA NYONG'O

Picha
Msanii muigizaji kutoka Kenya Lupita Nyong'o ameteuliwa kuijiunga na mabingwa wengine wa kimataifa katika filamu maarufu zaidi duniani STAR WARS.

HAPANA CHEZEA HII! BALOTELLI, ROONEY WALIVYOFANANA NA MASHABIKI WAO

Picha
Mtoto Balotelli (Pichani) NI maajabu ya mungu tu yameweza kutofautisha sura za watu na kufananisha pia, jamii ya watu wa China ndio pekee iliyofanana sura, lakini kwa uwezo mkubwa wa Mungu wanasoka mahiri duniani Mario Balotelli 'Super Mario' na Wayne Rooney wamefanana mno na mashabiki wao hasa watoto.

WAMBURA AZIDI KUKINUKISHA MSIMBAZI, SASA KUMBURUZA NDUMBARO TFF

Picha
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa shirikisho la soka nchini, Michael Wambura, ambaye anapinga kuenguliwa katika uchaguzi mkuu wa Klabu ya Simba, amesema atamburuza Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Simba, Damas Ndumbaro, kwenye Kamati ya Maadili ya TFF kufuatia 'kumpakazia' kashfa ya kughushi nyaraka na pia kumtukana. Wambura alisema katika taarifa yake aliyoitoa kwa waandishi wa habari jana kuwa anawasilisha malalamiko yake katika Kamati ya Maadili ya TFF ili ukweli wa mambo ufahamike. "Kwa kuwa nimeshakata rufaa TFF kupinga maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya Simba, busara inanielekeza kutolumbana na na kujibizana na Ndumbaro ili kuipisha Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi ya TFF ifanye maamuzi yake," alisema katika taarifa yake hiyo. Aliongeza: "Kwa mambo ambayo hayana uhusiano na uchaguzi kama kughushi nyakara, matusi na kashfa mbalimbali mambo hayo nitayawasilisha kwa Kamati ya Madili ya TFF ili ukweli ufahamike na hatua zichukuliwe na baada ya hapo vyombo vya dola vinavyo

PRESIDENT JAKAYA KIKWETE AKUTANA USO KWA USO NA DIAMOND NEW YORK

Picha
Rais Jakaya Mrisho Kikwete yupo kwenye safari zake za kikazi na Diamond yupo kwenye safari za show zake huko Marekani.

SIMBA SASA HAKUKALIKI, NDUMBARO AMSHIKA PABAYA WAMBURA

Picha
Wakati Kamati ya Uchaguzi ya Klabu ya Simba jana imetangaza rasmi kuwatema wanachama saba waliokuwa wanawania nafasi ya Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo, wengine watano wameandika barua za kujiondoa kwenye kinyang'anyro hicho, imeelezwa.

UJUMBE WA FIFA KUTUA QATAR

Picha
Waandalizi wa kombe la dunia mwaka 2022 nchini Qatar wanatarajiwa kukutana na mchunguzi wa shirikisho la soka duniani FIFA, Michael Garcia hii leo huku kukiwepo wito kwa taifa hilo kunyimwa haki ya kuandaa mashindano hayo.

TAIFA STARS HAIKAMATIKI........

Picha
Timu ya soka ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) ilitinga hatua ya pili ya mchujo ya kuwania kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika 2015 kufuatia sare ya 2-2 ugenini iliyowapa ushindi wa jumla wa 3-2 dhidi ya Zimbabwe kwenye Uwanja wa Taifa jijini Harare jana. Matokeo hayo yanamaanisha kwamba Stars sasa itaikabili Msumbiji ambayo iliing'oa Sudan Kusini kwa jumla ya mabao 5-0 katika mechi ya hatua ya pili ya mchujo itakayofanyika nyumbani wikiendi ya Julai 18-20 na ya marudiano ugenini Maputo wikiendi ya Agosti 1-3. Mshindi baina ya Stars na Msumbuji ataingia katika hatua ya makundi.

ETO'O AENDELEZA VITA YAKE NA MOURNHO

Picha
MSHAMBULIAJI Samuel Eto'o jana amerudia kushangilia kama kikongwe baada ya kuifungia Cameroon bao la kuongoza ikitoka sare ya 2-2 na Ujerumani katika mchezo wa kirafiki kujiandaa na Kombe la Dunia.

MIRROR ATOBOA FAIDA ANAZOPATA KWA MENEJA WAKE.

Picha
Na Robart Michael Msanii anaetamba na single yake inayoitwa "Baby leo" hivi karibuni ameitambulisha single yake mpya inayoitwa "korokoro" aliyomshirikisha Jose Chamilion aliyofanyia nchini "Uganda". Vile vile Mirror alihojiwa kwenye chombo kimoja cha habari amesema kuwa enzi anaanza mziki alikutana na msanii Ay studio,Ay aliposikia kwa mara ya kwanza nyimbo ya Mirror alipenda sana uimbaji wake na akaamua kufanya nae korabo.