Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2013

NWOFOR WA NIGERIA AJIUNGA NA SC HEERENVEEN

Picha
Timu ya taifa ya Nigeria Mshambulizi wa kimataifa wa Nigeria Uche Nwofor amejiunga na klabu ya Uholanzi ya SC Heerenveen, kwa mkpo kutoka kwa klabu ya VVV Venlo iliyoshushwa daraja.

SOLOMON KALOU KUTUA ARSENAL

Picha
KLABU ya Arsenal ipo katika mazungumzo na Lille ya Ufaransa juu ya kumsajili Salomon Kalou huku wakijiandaa kumtema Nicklas Bendtner aende Crystal Palace.

CHEKA AENDELEZA UMWAMBA WAKE, AMCHAKAZA MMAREKANI NA KUTWAA MKANDA WA DUNIA

Picha
BONDIA Mtanzania, Francis ‘SMG’ Cheka (Pichani akimdunda ngumu mpinzani wake) jana usiku ametawazwa kuwa bingwa mpya wa dunia wa WBF, katika uzito wa Super Middle baada ya kumshinda Mmarekani, Phil Williams kwa pointi katika pambano la Raundi 12, lililofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.

MAKALA: 'MATRAFIKI FEKI' TUNAO WENGI KWENYE MICHEZO

Picha
Kwa sasa kila kitu kinaendeshwa kiujanjaujanja, kama imetokea mtu kujipenyeza na kujipa ajira ya uaskari wa barabarani (traffic) kwa vitu vingine ni rahisi tu, tena  kichekesho eti alianza kazi hiyo mjini Singida.

BAADA YA KUTIMUA VIGOGO, IGP MWEMA YAMKUTA MAKUBWA

Picha
Jeshi la Polisi limeingia katika kashfa nzito baada ya mkuu wake, Inspekta Jenerali Said Mwema, kuibiwa upanga wa dhahabu ambao ni mali ya Shirikisho la Wakuu wa Majeshi ya Polisi wa nchi za Kusini mwa Afrika (SARPCCO).

BIG MECHI ULAYA, YAFUTA PAMBANO LA SIMBA MAFUNZO JUMAPILI

Picha
Mechi ya Simba na Mafunzo imesogezwa mbele mpaka Jumatatu ijayo ili kuwapa fursa mashabiki wa soka nchini kushuhudia mechi ya upinzani ya Ligi Kuu ya England kati ya mahasimu Liverpool na Manchester United itakayochezwa kesho alasiri.

YANGA YALIZWA TENA NA AZAM TV

Picha
Wakati Kampuni ya Azam Media na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) zikisaini rasmi mkataba wa kuonyesha Ligi Tanzania Bara, Klabu ya Yanga imeshangazwa na hatua hiyo ikisema imefanyika kinyume na mapendekezo yake.

KAGAME ATAADHALISHWA.................

Picha
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ametoa wito kwa rais wa Rwanda, kuwa mvumilivu huku uhasama kati yake na nchi jirani ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ukiendelea kutokota katika maeneo ya mipakani.

KUMEKUCHA ULAYA: ARSENAL, MAN CITY WATAWEZA?

Picha
Timu ya Arsenal (Pichani) huenda ikawa na kibarua kigumu katika mechi za kutafuta nafasi ya kujitosa katika duru ya muondoano ya kombe la klabu bingwa bara ulaya.

ETO'O SASA WA CHELSEA, AFURAHIA MAISHA YA LONDON

Picha
Chelsea imemsajili mshambuliaji wa Cameroon, Samuel Eto'o kutoka klabu ya Anzi Makhachkala ya Urussi.

TAJIRI WA CHELSEA AKATISHA UFADHILI WAKE KWENYE SOKA

Picha
Mfanyabiashara tajiri na mmiliki wa klabu ya Chelsea, Roman Abramovich (Pichani) amesema amesitisha ufadhili wake wa soka nchini Urussi.

MWAISABULA APINGA PENALTI YA COASTAL

Picha
Mkwaju wa penalti wa dakika za mwisho waliopewa Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Yanga na Mwamuzi Martin Saanya, umepokelewa kwa hisia tofauti na wadau wa soka nchini.

TAMBWE AANZA MCHECHETO LIGI KUU, ADAI NI NGUMU KULIKO KWAO BURUNDI

Picha
Baada ya kucheza kwa mara ya kwanza katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara, mshambuliaji Amisi Tambwe (Pichani) wa Simba amesema ligi hiyo ni ngumu ukilinganisha na Ligi Kuu ya Burundi aliyotokea.

NI CHEKA AU MMAREKANI KUIBUKA MBABE LEO!

Picha
Pambano la ngumi la kimataifa kati ya bondia Francis Cheka wa Morogoro na Phil 'The Drill' Williams (Pichani) wa jimbo la Minneapolis, Minnesota nchini Marekani la kuwania mkanda unaotambuliwa na Shirikisho la Ngumi Duniani (WBU) linatarajiwa kufanyika leo kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

AKINA BALOTELLI WAFUZU HATUA YA MAKUNDI ULAYA

Picha
Wachezaji wa AC Milan AC Milan ya Italia kwa mara ya kumi na moja katika muda wa miaka kumi na mbili iliyopita imefuzu kushiriki Kombe la Klabu Bingwa baranai Ulaya.

HENRY JOSEPH SHINDIKA KUTAMBULISHWA SIMBA JUMAPILI

Picha
KOCHA Mkuu nwa Simba SC, Alhaj Abdallah ‘King Kibaden’ amelainika kwa Mwenyekiti wa klabu yake, Alhaj mwenzake, Ismail Aden Rage na kukubali timu hiyo icheze mchezo wa kirafiki Jumapili Dar es Salaam na Mafunzo ya Zanzibar.

NEYMAR AANZA UFALME HISPANIA, MESSI AREJEA KWA 'GUNDU' AKOSA PENALTI

Picha
NYOTA wa Brazil, Neymar (Pichani) ameshinda taji lake la kwanza Barcelona kufuatia vigogo hao wa Katalunya kutwaa taji la nne la Super Cup ya Hispania ndani ya miaka mitano kwa faida ya bao la ugenini, baada ya sare bila kufungana 0-0 usiku wa jana Uwanja wa Nou Camp.

MGONGOLWA AIKATA MAINI YANGA KUHUSU NGASA

Picha
Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji, Alex Mgongolwa (Pichani) amesema kamati yake haikumhoji winga wa Yanga, Mrisho Ngassa ilijitosheleza na maelezo ya kimaandishi.

GAZETI LA NIPASHE KUDHAMINI MISS TANZANIA

Picha
Gazetila NIPASHE jana lilitangaza kuwa limedhamini shindano la urembo nchini la Miss Tanzania 2013.

DHAIRA AIBEBA SIMBA, MWAMUZI AINYONGA YANGA, JKT RUVU KUKAMATA USUKANI

Picha
Kipa Mganda Abel Dhaira ambaye alishutumiwa kwa makosa yaliyoifanya Simba ishikiliwe kwa sare katika mechi ya ufunguzi, jana alidaka penalti na kuisaidia Simba kuibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya JKT Oljoro mkoani Arusha, wakati jijini Dar es Salaam penalti ya Jerry Santo iliinyima Yanga pointi tatu katika sare ya 1-1 dhidi ya Coastal Union ya Tanga.

CHEKA NA MMAREKANI WAKE KUPIMA UZITO LEO

Picha
Mabondia Francis Cheka (Pichani) kutoka Morogoro na Phil William wa Marekani wanatarajia kupima uzito leo kujiandaa na pambano la kuwania ubingwa wa Shirikisho la Ngumi la Dunia (WBU) litakalofanyika kesho kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

WENGER AMTOLEA MACHO JUAN MATA

Picha
Arsenal manager Arsene Wenger has expressed admiration for Juan Mata, but he was reluctant to reveal the extent of the club's interest in the Chelsea midfielder.

STEPHEN KESHI HATARINI KUFUNGIWA NA FIFA

Picha
Shirikisho la mchezo wa soka duniani FIFA, limethibitisha kuwa limepokea malalamishi kutoka kwa shirikisho la mchezo wa soka nchini Malawi FAM, kuhusiana na matamshi yaliyotolewa na kocha wa Nigeria, Stephen Keshi (Pichani).

WALIOFELI 1,800 SASA KUJIUNGA CHUO KIKUU LIBERIA

Picha
Rais wa Liberia, Ellen Sirleaf Johnson (Pichani), amesema chuo kikuu kinachomilikiwa na serikali, kimekubali kuwasajili wanafunzi elfu moja mia nane ambao walifeli mtihani wa mwisho wa kitaifa wa shule ya upili.

SAMUEL ETO'O AKARIBIA KUTUA CHELSEA, KUMWAGA WINO NDANI YA MASAA 48

Picha
KLABU ya Chelsea iko katika hatua za mwishoni za kukamilisha usajili wa Samuel Eto'o kutoka Anzhi Makhachkala na dili hilo linaweza kukamilika ndani ya saa 48.

NSAJIGWA NAYE AJA NA KITABU CHAKE

Picha
Nahodha wa zamani wa Yanga anayeifundisha hivi sasa timu ya Lipuli ya Iringa, Shadrack Nsajigwa “Fuso” (Pichani) amepanga kutoa kitabu kinachozungumzia historia ya maisha yake.

SAKATA LA NGASA LATINGA FIFA

Picha
Uongozi wa klabu ya soka ya Yanga umesema unatarajia kujipanga kupeleka malalamiko yao katika Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) ili kupinga adhabu ya kufungiwa mechi sita na kuilipa Simba Sh. milioni 45 ambayo amepewa mshambuliaji wake mpya, Mrisho Ngasa (Pichani).

BRANDTS AANZA VISINGIZIO, SIMBA NAO YAUFYATA KWA WANAJESHI ARUSHA

Picha
Kocha wa Yanga, Ernie Brandts (Pichani) ameelezea ushindani mgumu anaoutarajia katika mechi yao ya leo ya Ligi Kuu ya Bara dhidi ya Coastal Union kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, huku Simba wakifanya mazoezi kwa kujificha mkoani Arusha kuelekea mechi yao ya leo dhidi ya JKT Oljoro.

WANAFUNZI WOTE WAFELI MTIHANI WA SEKONDARI LIBERIA

Picha
Siyo bongo peke yake: Wanafunzi wote walifeli mtihani wa kujiunga na chuo kikuu cha Liberia Kwa mara ya kwanza katika historia ya Liberia, wanafunzi wote wamefeli mtihani wao wa mwisho wa sekondari na hivyo kumaanisha kuwa hakuna hata mmoja ambaye atafuzu kuingia chuo kikuu. Waziri wa elimu wa Liberia amesema ameshinda kufahamu ni kwa nini hakuna wanafunzi hao wamefeli kiasi hicho.

MAN UNITED, CHELSEA HAKUNA MBABE

Picha
Jinsi mambo yalivyokuwa uwanjani Old Trafford Klabu za Chelsea na Manchester United zimeminyana uwanjani Old Trafford. Pande zote mbili zimekosa kufunga bao, na hivyo kutoka sare ya bila kwa bila.

ROONEY KUNG'OKA MAN UNITED MASAA 48 AMA SIVYO.........

Picha
KOCHA Jose Mourinho amempa Wayne Rooney (Pichani0 saa 48 kutangaza hadharani nia ya kuondoka Manchester United kuhamia Chelsea.

ABEL DHAIRA AKALIA KUTI KAVU SIMBA, REKODI YAKE YA KUFUNGWA HII HAPA

Picha
KIPA Mganda wa Simba SC, Abbel Dhaira (Pichani) amekwishafungwa mabao 18 katika mechi 11 alizoidakia klabu hiyo tangu Januari mwaka huu alipojiunga nayo, akitokea IBV ya Ligi Kuu ya Iceland, huo ukiwa ni wastani wa karibu mabao mawili kila mechi.

SIMBA KAMILI GADO KUIVAA JKT OLJORO, TAMBWE, KAZE YAWAPA JEURI

Picha
Baada ya uongozi wa Simba kufanikiwa kupata Hati za Uhamisho wa Kimataifa (ITC) za nyota wao wa kigeni Warundi, Amisi Tambwe na Gilbert Kaze, meneja wa timu hiyo, Mosses Basena (Pichani) amesema kikosi chao sasa ni ‘moto wa kuotea mbali’.

MPINZANI WA CHEKA KUTUA DAR, MASHALI KUOGOPA MZIKI WA MAUGO

Picha
Wakati bondia Phil Williams kutoka Marekani pamoja na kocha na daktari wake wanatarajia kutua nchini usiku wa leo ili kumkabili Francis Cheka, bondia Thomas Mashali ameendelea kusisitiza kuwa hatapigana na Mada Maugo siku ya Ijumaa.

COASTAL UNION WAAPA KUIVURUGIA YANGA KESHO

Picha
Huku timu zao zikiwa zimeshinda mechi za kwanza za Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, kocha wa Yanga, Ernie Brandts amesema kuwa kikosi chake kina uwezo wa kushinda mechi ya kesho huku kocha Hemed Morocco wa Coastal Union (Pichani) ya jijini Tanga akitamba 'kuwavurugia' mabingwa hao watetezi.

AZAM FC YAINGIA MCHECHETO KWA RHINO

Picha
KIKOSI cha Azam FC (Pichani)  kimewasili usiku wa jana mjini Tabora, kikitokea Morogoro tayari kwa mchezo wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Jumatano dhidi ya wenyeji, Rhino Rangers Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini hapa.

MAN CITY KIBONDE KWA CARDIFF

Picha
Cardiff yachapa Manchester City Hiki ni kichapo cha kwanza kwa Man City kumkaribisha meneja mpya wa Manuel Pellegrini katika ligi ya England.

MOURINHO AMVURUGA MOYES

Picha
KOCHA Jose Mourinho amemuambia David Moyes: Sikumvurugia Wayne Rooney, umefanya wewe.

DIAMOND AANIKA SIRI YA UTAJIRI WAKE

Picha
MKALI wa muziki wa bongo fleva nchini, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinum’ (Pichani), amefunguka mengi juu ya historia ya maisha yake na changamoto alizozipitia katika safari yake ya muziki mpaka kufikia hapa, katika semina ya Fursa, iliyoandaliwa na Clouds Fm katika kila mkoa tamasha la Fiesta linapopita.

LIGI KUU BARA YAANZA KWA KISHINDO, MABAO 19 YAFUNGWA

Picha
Mabao 19, yametumbukizwa wavuni wakati wa mechi za ufunguzi wa msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliohusisha timu 14  mwishoni mwa wiki.

ROMA MKATOLIKI AFANYA MAKAMUZI YA HATARI DAR

Picha
Msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya, Roma Mkatoliki na bendi ya muziki wa dansi ya African Stars 'Twnaga Pepeta' walikonga nyoyo za mashabiki tele waliojitokeza katika bonanza maalum lililoandaliwa kwa udhamini wa kinywaji cha Vita Malt kwenye viwanja vya Posta, Kijitonayama jijini Dar es Salaam juzi.

TAMBWE, KAZE SASA KUKIPIGA SIMBA, MOTO WAO UTAWAKA DHIDI YA OLJORO

Picha
Hatimaye wachezaji wapya wa Simba kutoka Burundi mshambuliaji Amisi Tambwe na beki Gilbert Kaze (Pihani) kutoka Burundi, jana walipata uhamisho wa kimataifa kwa ajili ya kuanza kuichezea klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, ilielezwa jijini Dar es Salaam jana.

IRAN YACHIMBA MKWARA DHIDI YA SYRIA

Picha
Jenerali wa daraja ya juu wa Iran ameionya Marekani kwamba matokeo yanaweza kuwa mabaya iwapo Marekani itapindukia ule aliosema "mstari mwekundu" nchini Syria.

WENGER AMPIGIA SALUTI PODOLSKI

Picha
Arsene Wenger  Arsenal manager Arsene Wenger saluted Lukas Podolski after his brace helped the Gunners pick up their first Premier League points of the season in a 3-1 win at Fulham.

CHELSEA YAIFANYIA KITU MBAYA SPURS

Picha
Willian Chelsea imekubali kulipa pauni millioni 30 kumsajiliwa kiungo mchezaji Willian kutoka klabu ya Urussi Anzhi Makhachkala.

AZAM TV KUANZA SEPTEMBA

Picha
  Mashabiki wa soka wa Tanzania Bara wataanza kuishuhudia Ligi Kuumoja kwa moja kupitia kituo cha televisheni cha Azam TV katikamzunguko wa nne sambamba na tiketi za elektroniki.

SIMBA YAUMBULIWA NA RHINO, PENGO LA KASEJA LAONEKANA

Picha
Simba jana ilianza kwa lawama na majanga msimu mpya wa ligi kuu ya Bara baada ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na timu ya Rhino Rangers iliyopanda daraja kwa mara ya kwanza na ambayo Wekundu wa Msimbazi walikuwa wakipewa nafasi kubwa ya kuifunga.

YANGA MATAWI YA JUU, YAI[A KIPIGO CHA MBWA MWIZI ASHANTI

Picha
Mabingwa watetezi Yanga jana walitumia vizuri ugeni kwenye ligi kuu ya Bara wa Ashanti United iliyokuwa na wachezaji 10 uwanjani kufunga mabao matatu ya mapema katika kila kipindi, yaliyoisaidia kuichabanga 5-1 na kuipa pointi tatu baada ya mchezo mmoja.

BALE KIMEELEWEKA REAL MADRID, ATUA KUKAMILISHA DILI

Picha
NYOTA Gareth Bale amewasili Hispania kujiandaa kusaini Real Madrid, lakini Tottenham na vigogo hao wa Hispania bado wanavutana kwenye bei.