Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2016

Siri zavuja, Kessy aibwaga Simba

Picha
Na Mwandishi Wetu Dalili za beki Hassan Ramadhan Kessy kukipiga Yanga bila vikwazo huenda ikafanikiwa baada ya kamati iliyoketi hivi karibuni iliyoongozwa na wakili Richard Sinamtwa kuitaka Klabu ya Simba kuwasilisha vielelezo kama imewahi kumlipa beki huyo mshahara wake wa miezi mitatu kupitia akaunti yake ya benki. Endapo Simba itashindwa kuwasilisha vielelezo hivyo basi beki huyo atakuwa ameibwaga Klabu yake hiyo ya zamani kwani kesi hiyo itatupiliwa mbali. Mwanasheria wa Yanga, Alex Mgongolwa ndiye aliyeiomba kamati hiyo kuhoji kama ni kweli Simba walikuwa na uhalali wa kummiliki mchezaji huyo, hata hivyo kesi hiyo bado inapigwa danadana

Wakala wa Jesse Were awaita mezani Yanga

Picha
Na Saida Salum, Dar es Salaam Wakala wa mshambuliaji wa timu ya Zesco United ya Zambia Jesse Were raia wa Kenya, George Bwana amesema mchezaji wake yuko sokoni na anamuuza kwa kiasi kisichopungua Dola 150,000 sawa na shilingi Milioni 320 za Kitanzania. Bwana amewaambia Yanga kuweka mezani kitita hicho ili straika huyo atue Jangwani, Were ni chaguo la kocha mpya wa Yanga, Mzambia George Lwandamina. Tayari Yanga imeshamshusha kiungo mkata umeme wa Zesco United ya Zambia, Justin Zullu ambaye muda wowote atamwaga wino kuitumikia Klabu hiyo

Rage ampiga kijembe Malinzi

Picha
Na Mrisho Hassan, Dar es Salaam Aliyekuwa mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Alhaj Ismail Aden Rage amempiga kijembe Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) Jamal Malinzi kwambs si mtu wa mpira na ndio maana katika utawala wake tunashuhudia Tanzania ikiporomoka katika viwango vya ubora huku hali ikizidi kuwa mbaya. Rage amesema viongozi wa sasa wengine walikuwa wanaongoza masumbwi na anashangaa kuwaona wakiliongozs soka. Malinzi ndiye aliyekuwa akiongoza masumbwi, enzi zake akimpromoti bondia Rashid Matumla kupitia kampuni yake ya DJB Promotion. Kwa sasa Malinzi ameshindwa kuivusha Tanzania kwani timu zake zote za Taifa zimetolewa kwenye mashindano iliyoshiriki, pia tumeshuhudia Tanzania ikianguka kwenye viwango vya ubora vinavyotolewa na Shirikisho la mpira wa miguu Duniani (FIFA), Tanzania kwa sasa inashika nafasi ya 160 ikiwa ni nafasi mbaya kabisa kuwahi kushjka

Bokungu kuongezwa miezi sita Simba

Picha
Na Salum Fikiri Jr  Dar es Salaam Klabu ya Simba imesema itamuongezea mkataba wa mwingine wa miezi sita, beki wake wa kulia Janviel Besala Bokungu raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Bokungu atapewa mkataba huo mara baada ya kumalizika kwa huu mwingine wa miezi sita, Tayari Simba imeshamuongezea beki wake wa kushoto Mohamed Hussein 'Tshabalala' wa miaka miwili. Bokungu aliyesajiliwa sambamba na Mkongo mwenzake Musa Ndusha, ameonyesha kiwango kikubwa katoka michezo kadhaa ambayo klabu yake ya Simba imecheza, endapo atapewa miezi sita, atalazimika kucheza hadi mwakani

Lwandamina ambakiza Mwambusi Yanga, Akana kuwaleta nyota wa Zesco Jangwani

Picha
Na Enika Samson, Dar es Salaam Kocha mpya wa Yanga SC  Mzambia George Lwandamina ambaye leo ametambulishwa na uongozi wa Klabu hiyo amesema atafanya kazi na benchi la ufundi alilolikuta. Ina maana kocha huyo wa zamani wa Zesco United ataendelea kufanya kazi na Juma Mwambusi ambaye ni kocha msaidizi wa Yanga aliyefanya kazi na aliyekuwa kocha mkuu wa Yanga, Hans Pluijm ambaye leo hii ametambulishwa kama Mkurugenzi wa Ufundi wa timu hiyo. Lwandamina pia amekanusha uvumi ulioenezwa na mitandao ya kijamii pamoja na vyombo vya habari kwamba aliwapendekeza nyota wawili wa Zesco United, Jesse Were raia wa Kenya na Meshark Chaila

Genge la RNE lapata mkataba mnono wa kutangaza Condom

Picha
Na Ismail Mhina, Tanga Kundi la muziki wa kizazi kipya lililopo Hale jijini Tanga, liko mbioni kuingia mkataba na moja kati ya makampuni makubwa ya kusambaza Condom hapa nchini. Mmoja wa mamemba wa kundi hilo linalotamba kwa sasa katika miondoko ya Hip Hop jijini Tanga, amesema wako mbioni kusaini mkataba huo mnono nankampuni hiyo ya kusambaza Condom. Kundi hilo linaloindwa na wasanii sita, wakiwemo Jusa, Amour JJ, Dizonga, Jimmy Msauzi, Boss Rapa, Agga Swing na Mkola Man Miongoni mwa wasanii wa kundi la RNE lenye maskani yake Hale Tanga, wako mbioni kuingia mkataba wa kutangaza Condom

Tshabalala aongeza miaka miwili Simba

Picha
Na Ikram Khamees, Dar es Salaam Vinara wa Ligi Kuu Bara, Simba SC, leo wamemuongezea mkataba wa miaka miwili beki wao wa kushoto Mohamed Hussein 'Tshabala' (21) na kumfanya asalie mpaka mwaka 2018. Tshabalala ameongeza mkataba huo wa miaka miwili hii leo katika ofisi za Rais wa Klabu hiyo Evans Elieza Aveva, kwa maana hiyo zile tetezi zilizokuwa zikivumishwa kwamba beki huyo ataelekea mitaa ya Jangwani sasa zimezimwa. Simba inaendelea kumalizana na nyota wake ambao mikataba yao inaelekea ukingoni, Nahodha wa timu hiyo Jonas Mkude naye anaweza kumalizana na uongozi wa Simba kama ilivyokuwa kwa Tshabalala

Smart Sport yaikalia kooni TFF, sasa yataka kuipoka basi kufidia deni lake

Picha
Na Prince Hoza, Dar es Salaam Kampuni ya kuuza na kusambaza vya michezo ya Smart Sport imetishia kwenda mahakamani ili ikamate mali za Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) ambao eanawadai mamilioni ya shilingi. Akizungumza kwa njia ya simu, Mkurugenzi wa kampuni hiyo George Wakuganda amesema watalifikisha mahakamani Shirikisho hilo ili waweze kuwapoka basi lao kama hawatalipwa fedha zao. Smart Sport ndiyo iliyokuwa ikisambaxa vifaa vya michezo kwenye Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) ambapo timu zote za taifa zilikuwa zikitumia vifaa hivyo George Wakuganda

Simba sasa kuibomoa Zesco United, yamnasa mpachika mabao wao

Picha
Na Ikram Khamees, Dar es Salaam Baada ya kugonga mwamba kwa mshambulizi wake wa zamani Emmanuel Okwi, Simba imemgeukia mpachika mabao wa Zesco United ya Zambia, John Chingandu. Taarifa zenye uhakika kutoka ndani ya Klabu hiyo zinasema Chingandu ni chaguo la kocha wao Mkameruni, Joseph Omog kwa maana hiyo nyota huyo anaweza kutua Msimbazi kuimarisha safu ya ushambuliaji ambayo kwa sasa haifanyi vizuri. Haji Manara msemaji wa Klabu hiyo alikataa kuzungumzia hilo na kudai Simba inafanya usajili wake kimyakimya na wala mitandao ya kijamii haitaambiwa lolote, lakini Blogu hii imegundua janja ya timu hiyo kumnasa Chingandu ambaye ni mpachika mabao wa timu hiyo

Msaka vipaji wa Man U, Ubelgiji huyu hapa

Picha
Na Salama Ngale Klabu ya Manchester united imemteua mchunguza vipaji Raia wa ubelgiji Roland Jansen kuwa jicho katika soka la ubelgiji ambalo limefanikiwa kutoa nyota kadhaa wanao sakata kabumbu nchini uingereza. Janssen  alikua msaka vipaji wa klabu ya Genk ndio aliye wapeleka Kevin De bruyne na Thibaut courtois ambao waliuzwa katika klabu yaChelsea  kwa faida kubwa. Pia anahusisha wa kumpeleka Genk kiungo mkabaji Wilfried Ndidi (19) ambae kwasasa anakarbia kutua king power studium kwa dau lisilo pungua paun million 15.

Samatta atupwa nje tuzo ya mwanasoka bora Afrika

Picha
Na Salama Ngale Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania mbwana Ally Samatta (sama goal) ametupwa nje kwenye kinyang'anyiro cha kumpata mchezaji bora Afrika kwa mwaka 2016 Samatta ambaye alishinda tuzo ya mchezaji bora wa afrika kwa wchezaji wanaochezaligi za ndani ya afrika Mara hii alikua anagombea ya mchezaji bora Afrika anaye cheza soka la kulipwa. Samatta alikua ana chana na wachezaji wengine kutokabaran Afrika kama vile Yaya Toure,Mohammed. salaah na Riyadh Mahrez.

Samatta atupwa nje tuzo za mwanasoka bora Afrika

Picha
Na Salama Ngale Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania mbwana Ally Samatta (sama goal) ametupwa nje kwenye kinyang'anyiro cha kumpata mchezaji bora Afrika kwa mwaka 2016 Samatta ambaye alishinda tuzo ya mchezaji bora wa afrika kwa wchezaji wanaochezaligi za ndani ya afrika Mara hii alikua anagombea ya mchezaji bora Afrika anaye cheza soka la kulipwa. Samatta alikua ana chana na wachezaji wengine kutokabaran Afrika kama vile Yaya Toure,Mohammed. salaah na Riyadh Mahrez.

Clinton wa Yanga afariki dunia

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Aliyekuwa makamu mwenyekiti wa Klabu ya Yanga yenye maskani yake jijini Dar es Salaam, Isaack Shekiondo maarufu kama Clinton amefariki dunia usiku wa kuamkia leo. Taarifa iliyotolewa na familia inasema kwamba msiba upo nyumbani kwake Ilala Mchikichini jijini Dar es Salaam, marehemu alikuwa akiugua kwa muda. Enzi zake katika miaka ya 2000, Clinton aliyebatizwa jina hilo baada ya kuonekana mwenye misimamo kama aliyokuwa nayo Rais wa wakati huo wa Marekani Bill Clinton, marehemu Clinton alikuwa makamu wa mwenyekiti wa Yanga anayekumbukwa vema kwa kuanzisha mchakato wa kampuni. Marehemu enzi zake alifanya kazi pamoja na Tarimba Abbas Tarimba na kuifanya Yanga iwe kwenye maendeleo makubwa

Man United ilipoikosakosa Arsenal jana

Picha
Mpambano mkali na wa kusisimua kati ya Manchester United na Arsenal uliopigwa katika dimba la Old Trafford jijini Manchester. Timu hizo zilifungana 1-1 Man U wanaonolewa na Jose Mourinho wakitangulia kupata bao la kuongoza lililofungwa na Huan Matta kabla ya Arsenal  kuchomoa kupitia kwa Okivier Giroud

Okwi aota mbawa Msimbazi

Picha
Na Mrisho Hassan, Dar es Salaam Dili ya kumrejesha tena kwa mara ya pili mshambuliaji Emmanuel Okwi raia wa Uganda imekufa rasmi ama kwa lugha nyingine unaweza kusema imeota mbawa. Okwi anayecheza soka la kulipwa nchini Denmark katika Klabu ya Sonderjsky inayoshiriki Ligi Kuu na michuano ya Ulaya, kiungo huyo mshambuliaji ilikuwa atue Simba kufuatia makubaliano mazuri waliyofikiana. Lakini uongozi wa timu hiyo ukagoma kumwachia Okwi na sasa ataendelea kukipiga timu hiyo licha kwamba amekuwa akianzia benchi, taarifa za uhakika zinasema, Sondwrjsky walikuwa wakitaka walipwe kwanza Dola Laki mbili, na Simba ilikubali kufanya hivyo. Ila mkurugenzi wa timu hiyo amesema timu yoyote inayomuhitaji Okwi lazima imnunue kwa fedha wanazohitaji wao ambazo ni zaidi ya Dola laki mbili, kwa maana hiyo Simba imeshindwa kumrejesha tena Okwi na sasa wanaangaza Zambia ambapo wamevamia katika timu ya Zesco United wakitaka kumchukua mshambuliaji wao John Chigandu

Ivo Mapunda aanzisha kituo chake cha michezo, lengo kuondoa Panya Road

Picha
Na Prince Hoza, Dar es Salaam Kipa wa zamani wa Yanga, Simba na Taifa Stars, Ivo Philip Mapunda, ameamua kuanzisha kituo chake cha michezo kitakachojumlisha vijana kuanzia umri wa miaka 8- 18. Akizungumza jana, Mapunda amesema amefikia maamuzi hayo hasa baada ya kuona vijana wengi wakijihusisha na vitendo vya kihuni kama 'Panya Road' na makundi mengineyo. Kipa huyo aliyewahi pia kuzichezea Tukuyu Stars, Prisons, Moro United, African Lyon, Bandari Mombasa, Gor Mahia, St George na pia Azam FC, kipa huyo amedai bado hajaamua kustaafu soka na amevitaka vilabu vinavyomuhitaji yupo tayari kujiunga nazo

Okwi anarejea Msimbazi, Yanga matumbo joto

Picha
Na Nasri Alfan, Dar es Salaam Kiungo mshambuliaji Emmanuel Anord Okwi raia wa Uganda, anatarajia kutua Msimbazi kujiunga na vinara wa Ligi Kuu Bara, Simba SC kwa mkataba wa mwaka mmoja. Okwi tayari alishajiunga na Sobderjsky ya Denmark inayoshiriki Ligi Kuu lakini wamekubaliana na Simba kwamba watauvunja mkatana wao, Klabu hiyo imewataka Simba kuwarudishia fedha zao Dola laki mbili walizomnunulia awali. Uongozi wa Simba nao umeridhia kulipa fedha hizo na sasa kiungo huyo mshambuliaji atarejea kunako Klabu yake ya zamani, Okwi anakumbukwa vema na mahasimu zao Yanga kwani amewahi kuwafunga mara kadhaa

Azam FC awalembi, yabeba Waghana wawili

Picha
Na Mrisho Hassan, Dar es Salaam AZAM FC jana imewasajili wachezaji wawili wa kimataifa kutoka nchini Ghana, nshambuliaji Samuel Afful na kiungo Yahaya Mohamed wametia saini kuitumikia Azam katika mzunguko wa pili. Mabingwa hao wa Afrika mashariki na kati  tayari wameshawasaini Waghana watatu wakianza na Enock Atta Agyei ambaye alikuwa akiichezea Medeama. Azam imeachana na maproo wake watatu ambao ni Kipre Michael Balou, Kipre Herman Tchetche na Paschal Wawa ambao wote ni raia wa Ivory Coast

Wimbo wa Kilevi changu, wampa dili Mkola Man

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Muda wowote msanii wa muziki wa kizazi kipya anayeishi Hale mkoani Tanga, Christopher Mhenga ama Mkola Man anaweza kuwa milionea kufuatia wimbo wake wa 'Kilevi changu' unaohamasisha matumizi ya sigara kununuliwa na kampuni ya Sigara (TCC). Dili hilo limetokana na wimbo huo kusikika katika vituo kadhaa vya redio hivi karibuni na kuwavutia maofisa wa kampuni hiyo kubwa hapa nchini. Msanii huyo aliyetoa nyimbo mbalimbali ambazo nyingine bado hazijasikika popote huenda akanufaika kwani inasemekana TCC inataka kuununua wimbo huo ili iweze kuuingiza kwenye matangazo yake

Mzamiru Yassin awa mchezaji bora Simba

Picha
Na  Shabani Hussein, Dar es Salaam Kiungo mshambuliaji Mzamiru Yassin amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Klabu ya Simba baada ya kuonyesha ufanisi mkubwa mwezi Oktoba. Mzamiru ameshinda tuzo hiyo na atakabidhiwa zawadi yake ya uchezaji bora ambapo Wekundu hao wa Msimbazo watamkabidhi shilingi Lako tano.

Dula Mbabe kumbe dereva bodaboda!

Picha
Na Prince Hoza, Dar es Salaam Mwanamasumbwi anayekuja juu kwa sasa hapa nchini Abdallah Pazi maarufu Dula Mbabe amefichua siri kwamba kabla hajajikita kwenye ndondi alikuwa dereva bodaboda. Akizungumza katika kipindi cha michezo cha Sportaiment kinachorushwa na Sibuka FM, amesema aliingia kwenye ndondi kwakuwa alikuwa na kipaji cha kupigana tangu zamani. Ila mchezo huo umempa nafasi kubwa ikiwemo kufahamika ndani na nje ya nchi, lakini kazi yake inayomuingizia kipato ni kuendesha bodaboda, bondia huyo hivi karibuni alimdunda Mchina kwa TKO

Orlando Pirates wamfuata Pluijm Yanga

Picha
Na Mrisho Hassan, Dar es Salaam Klabu ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini imeweka bayana kwamba wanamchukua kocha anayetajwa kutemwa na mabingwa wa soka nchini Yanga SC, Mholanzi Hans Van der Pluijm. Maofisa wa Pirates wamekiri kumuhitaji Pluijm kwakuwa ni mmoja kati ua makocha bora wanaofaa kuinoa Klabu hiyo kubwa barani Afrika. Licha kwamba Pluijm bado ni kocha wa Yanga, lakini ujio wa George Lwandamina wa Zesco United unapelekea Mdachi huyo kutimka Yanga kwakuwa amekataa kazi ya Ukurugenzi wa ufundi

Kiungo mzuiaji wa Zesco United laja kumrithi Domayo Yanga

Picha
Na Prince Hoza, Dar es Salaam Hatimaye mabingwa wa soka nchini Yanga SC wako mbioni kumleta kiungo wa Zesco ya Zambia ili kumrithi kiungo Frank Domayo 'Chumvi' ambaye pengo lake mpaka sasa bado halijazibwa. KIUNGO mkabaji na mchezaji wa kutegemewa wa Zesco United, Meshack Chaila yupo katika hatua za mwisho kukamilisha usajili wake kutua Young African SC! Chaila raia wa Zambia anasifika kwa kucheza soka kazi, mzuri katika ulinzi na kuharibu mipango ya timu pinzani. Yanga SC imepigana vikumbo na vilabu vya Misri kuwania saini ya nyota huyo, Chaila amewekewa mezani mkataba wa miaka 2 na huenda Yanga wakakamilisha usajili wake mapema wiki hii.

Simba ya mwendokasi kufumuliwa

Picha
Na Ikram Khamees, Dar es Salaam Wekundu wa Msimbazi Simba SC maarufu kama 'mwendokasi' huenda wakakikosa kikosi chao hicho kufuatia fununu kwamba uongozi unataka kukifumua na kusajili wachezaji wengine huku taarifa zikienea kwamba Emmanuel Okwi anarejea. Licha ya Okwi, inasemekana beki wa Azam FC, Shomary Kapombe naye anatajwa kurejea Msimbazi, Kapombe aliwahi kuichezea Simba misimu kadhaa iliyopita. Mbali na wachezaji hao wa zamani, wakongwe wanaotajwa kurejea Simba ni Juma Kaseja na Haruna Moshi 'Boban' ambaye hata hivyo hakuna uhakika wa kusajiliwa tena, kipa wa JKT Ruvu Said Kipao anapewa nafasi ya kusajiliwa katika Dirisha dogo. Aidha timu hiyo ambayo ndiyo vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, ina npango wa kuwatema nyota wake watatu wa kigeni ambao ni Laudit Mavugo, Janviel Bokungu na Musa Ndusha

Azam FC waanza kujiimarisha,yamsainisha miaka mitatu Mghana

Picha
Na Mrisho Hassan, Dar es Salaam Klabu bingwa Afrika mashariki na kati, Azam FC, imemsainisha mkataba wa miaka mitatu kiungo wa zamani wa Medeama ya Ghana, Enock Atta Agyei. Kiungo huyo aliyetimiza miaka 18, ameruhusiwa kujiunga na Azam baada ya awali kukataliwa kwa sababu hakuwa na miaka 18 kwani sheria za Ghana haziruhusu mchezaji kucheza nje ya Ghana. Klabu hiyo inayokamata nafasi ya tatu ikiwa na pwenti 25 ikizidiwa pointi kumi na kinara wa ligi hiyo Simba ambao wana pointi 35, timu hiyo msimu huu imeonekana si tishio kama ilivyokuwa misimu iliyopita

Yanga yamsogelea mnyama kileleni

Picha
Na Ikram Khamees, Dar es Salaam Yanga SC imeifunga Ruvu Shooting mabao 2-1 katika uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam, mchezo wa Ligi Kuu Bara. Ruvu Shooting walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Abdulraman Juma dakika ya saba kipindi cha kwanza, Lakini Yanga wakachomoa kwa bao la Simon Msuva. Hadi mapumziko timu hizo zilikuwa sare, kipindi cha pili Yanga wakaongeza bao la pili likifungwa na Haruna Niyonzima ambaye aling' ara, Kwa ushindi huo Yanga imefikisha pointi 33 ikiwa nyuma ya pointi mbili na vinara Simba wenye pointi 35 huku zote zikicheza mechi 15, mzunguko wa kwanza ukimalizika rasmi

Simba kweli baiskeli la miti, yakalishwa 2-1 Sokoine

Picha
Na Exipedito Mataruma, Mbeya Vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba SC leo jioni imeendelea kudhihirisha kuwa ni baiskeli ya miti baada ya kulazwa 2-1 na Tanzania Prisons  katika uwanja wa Sokoine mjini Mbeya mchezo wa Ligi kuu bara, mabao mawili ya Koplo Victor Hangaya yalitosha kabisa kuisinamisha Simba kuzidi kuikimbia Yanga kileleni, kwa maana hiyo Yanga inahitaji kushinda kesho dhidi ya Ruvu Shooting ili kuisogelea Simba, hii ni mechi ya pili Simba inalala baada ya Jumapili kufungwa na African Lyon 1-0 uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Simba walikuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza lililofungwa dakika ya 43 kipindi cha kwanza likifungwa na Jamal Mnyate, kipigo hicho ni cha pili na kufanya iendelee kusimama na pointi zake 35 kwa mechi 15. Kesho Yanga watakutana na Ruvu Shooting uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, lakini hata kama watashinda hawataweza kuishusha Simba, Azam FC nayo imeamka kule mjini Shinyanga katika uwanja wa Mwadui baada ya kuichabanga Mwadui mabao 4-1 na ku

MAKALA: YANGA TAMBUENI LWANDAMINA SIYO MALAIKA

Picha
Na Prince Hoza. YANGA SC wanataka kufanya mabadiliko makubwa ya benchi lake la ufundi ili mradi waweze kurejesha makali yao mapya yaliyopotea katika siku za hivi karibuni, tayari jina la kocha mpya limeshajulikana na awali aliwahi kutua hapa nchini kuzungumza na mabosi wa timu hiyo. Mzambia George Lwandamina ndiye jina la kocha mpya wa Yanga anayetajwa kwenye vyombo vya habari pamoja na Mitandao ya kijamii, Mzambia huyo alianza kuzungumziwa miezi kadhaa iliyopita hadi kocha mkuu wa timu hiyo Mholanzi Hans Van der Pluijm akaamua kujiuzuru. Magazeti ya Tanzania hayakuficha yaliandika kila kitu, Mholanzi huyo alikasirishwa na kitendo hicho cha mabosi wa Yanga kuamua kumletea kocha mwingine wakati yeye anafanya vizuri, yaliyokuwa yakisemwa yote Babu Hans aliyaona hivyo akajipanga kuwasubiri viongozi wa Yanga wamfuate. Viongozi wa Yanga walipendekeza Lwandamina awe kocha mkuu na Babu Hans awe mkurugenzi wa ufundi, na walipomfuata kumpa taarifa hizo Babu akawatolea nje akaamua kubwaga ma

Kweli Julio ameachana rasmi na soka

Picha
Piçhani: Kocha wa zamani wa Mwadui FC ya Shinyanga, Jamhuri Kihwelu 'Julio' anaonekana katika picha akiwa kulia amesimama sambamba na gari la kifahari, lakini kimuonekano Julio yuko viwanja vya majuu akila maisha

Tusker mabingwa wapya Kenya

Picha
Na Mwandishi Wetu, Kenya Ligi Kuu ya Kenya (KPL) nayo iliendelea katika viwanja tofauti mwishoni mwa juma lililopita katika uwanja wa Mumias Complex KK Homeboyz ilishindwa kuutumia vema uwanja wake wa nyumbani pale ilipolazimishwa sare tasa 0-0 na Ulinzi Stars. Lakini Sony Sugar ilikubali kichapo nyumbani cha mabao 2-1 na Posta Rangers, Mathare United ikitumia uwanja wa Nyayo Stadium ililazimishwa sare ya 2-2 na Sofapaka, wakati Thika United ikicheza kwenye uwanja wake wa Thika Stadium ilishinda 1-0 dhidi ya Chemell Sugar. Kule mjini Mombasa, Bandari ikicheza kwenye uwanja wake wa Mbaraki Stadium ilishinda 1-0 dhidi ya Western Stima, Tusker FC nao wakatawazwa kuwa mabingwa wapya wa Kenya baada ya kuilaza AFC Leopards bao 1-0, wakati Gor Mahia wakiwa ugenini waliibutua Muhoroni Youth kwa mabao 2-0 mechi ikipigwa Moi Stadium

Bosi Azam afariki dunia

Picha
Na Ikram Khamees, Dar es Salaam Mwenyekiti wa Azam FC 'Wanalambalamba' Said Mohamed Abeid amefariki dunia katika hospitali ya Aga Khan iliyopo Dar es Salaam. Mohamed ambaye ni makamu mwenyekiti wa Bodi ya Ligi, amefariki baada ya kuugua kwa muda mfupi na alilazwa katika hospitali hiyo. Taratibu za mazishi zinafanywa na familia pamoja na Klabu yake na huenda akazikwa kesho, Mungu ailaze roho yake peponi, Amina

Mamelodi Sundowns washikwa, Orlando yaua

Picha
Na Mwandishi Wetu, Afrika Kusini Mechi za mwishoni mwa wiki iliyopita hapa Afrika Kusini, Michuano ya Telkom Knockout iliendelea kwa mechi nne kupigwa karika viwanja tofauti. Pale katika dimba la Orlando Stadium, wenyeji Orlando Pirates waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 yaliyowekwa kimiani na mshambuliaji wake hatari Ndoro, dhidi ya Highlanders Park ambao mfungaji wao ni Mvala aliyefunga dakika ya 66. Mechi nyingine ilipigwa pale Lucas Moripe Stadium mabingwa wa Afrika, Mamelodi Subdowns wakishikwa shati na Supersport United baada ya kutoka sare tasa ya 0-0. Lakini mechi ya kusisimua ilifanyika Peter Mokaba Stadium, Cape Town City Stars ikishinda mabao 4-3 dhidi ya wenyeji wao Baroka FC, Cape Town walianza kuandika magoli kupitia Majoro dakika ya 7, Jayiya dakika 20 na Mashikinya dakika ya 90, Baroka FC wakapata magoli yao matatu kupitia Mothuna dakika ya 45, Motshegwa dakika ya 59 na Mahashe dakika ya 90. Cape Town City walipata bao la ushindi likifungwa na Masina dakika ya 114. Mec

Matokeo na uchambuzi mechi zote za EPL

Picha
Na Nasri Alfan ARSENAL 1 TOTTENHAM 1 ARSENAL wali hitaji ushindi ili kuweza kukaa kileleni mwa ligii jambo ambalo lili washindaa Aresenal wali kuwa wakwanza kupata goli bada ya beki wa  Tottenham ( Kevin Wimmer ) kuji funga dk 42 ku tokana na mpira wa adhabu ulio pigwa na Mesut Ozil Kipindi Cha pili Spurs waliweza kusawa zisha kupitia kwa msha mbuliaji wao Harry kane dk 51 ambae alionekana kutokuwa na makali sana hii ina tokana na kuwa majeruhi kwa mdaa mrefu kido Liverpool 6 Watford 1 Liverpool waendeleza wimbi la ushindi  na sasa ndio vinara wa EPL  hii ni baada ya kutimiza pwenti 26 huku nyuma yao akiwa Chelsea anae shika nafasi ya 2 akiwa na pwenti 25 Safu bora ya ushambuliaji ndio silaha kubwa ya Liverpool huku ikiwa ndio timu ilio funga magoli mingi Epl mpaka sasa washa funga magoli 30 Tatizo la Liverpool ni eneo la beki yao kwenye mechi 11 zilizopita wame weza kuma liza dakika 90 bila kufungwa mechi moja tyu mechi ambayo walikutana na Manchester United Swansea 1 Man Utd

TP Mazembe yabeba ndoo ya Shirikisho Afrika

Picha
Na Prince Hoza, Lubumbashi TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidenokrasia ya watu wa Kongo, jioni ya leo imeibuka na ushindi wa mabao 4-1 na kutwaa ubingwa wa kombe la Shirikisho barani Afrika. Fainali ya leo ilikuwa ya pili kwani miamba hiyo iliwahi kukutana katika mchezo wa kwanza uliochezwa katika uwanja wa Stade Mustapha Tchaker Algeria. TP Mazembe hadi wanakwenda mapumziko walikuwa mbele kwa mabao mawili yaliyofungwa na Bokadi dakika ya 7 na Kalaba dakika ya 43. Mabao mengine yalifungwa kipindi cha pili yakifungwa tena na Kalaba dakika 62 na Bolingi dakika ya 77, lile la Bejaia lilifungwa na Khadir dakika ya 75

Kipute cha haja kupigwa Ulaya leo

Picha
Ligii kuu England ku endelea leo hii kwa michezo 5 kupigwaa Mechi ya mapema zaidii ita pigwaa saa 9.00 kwa saa za Africa mashariki Aresenal vs Tottenham Hindio mechi ya mapema kwa leo pia ni Darby ina yo kutanisha timu za jiji moja (LONDON) kwa record zina onesha mechi 5 zilizo pita timu hizi 2 zilipo kutana Aresenal walipata ushindi mechi moja na Tottenham walipata ushindi mechi 1 huku 3 ziki malizika kwa sare Mechi za karibuni zina onesha Aresenal wapo bora zaidi ya Spurs ambayo kwenye mechi 5 wame pata sare 2 na kupoteza michezo 3 huku Aresenal wakishinda michezo 4 na wakipata sare mchezo 1 Kurudi kwa Herry kane kuta I boost Tottenham hini kutokana kukosa mechi kadhaa nyuma huku Vecent Jenssen akishindwa kuziba na fasi hio ilio achwa na mpachika mabao bora wa Epl msimuu ulio pitaa Viwango bora vya mchezaji mmoja mmoja Ina weza kuwa athiri kwa Tottenham na safu hatari ya Aresenal leo ina weza kuwa faidaa kwa mzee  Wenger safu ambayo ita ongozwa na Alex Sanchez Mest Ozil na hat

Matokeo ya mechi za EPL

Picha
Na Nasri Alfan Mechi ya kwanza ili kuwa niya BOURNEMOUTH dhidi ya SUNDRELEND mechi ambayo Sunderland aliweza kubuka na ushindi ugenini wa goli 1 kwa 2 ushindi ambao ume msaidi David Moyess kuku sanya pwenti 5 pekee kwenye michezo 11 iliyo pita pia Sunderland ndio timu inayo shika mkia kwa sasa BURNLEY wali endeleza wimbi la matokeo mazuri bada ya jana kupata ushindi w Goli 3 kwa 2 nyumbani dhidi ya C.PALACE hii nibada wa wiki iliyo pita kupata Suluhu ugenini dhidi ya Manchester United Manchester City wali lazimishwa sare ya goli 1 kwa 1 dhiya Middlesbrough Middlesbrough ambayo pia waliweza kupata Suluhu mechi dhiya Aresenal jana wame fanikiwa kuwazia tena miamba ya EPL kwa goli la dakika za lala salama la de roon huku goli la Man City liki fungwa kipindi cha kwanza na Kun Aguero Sare ambayo ina ishusha City kile leni na sasa Chelsea ana ongoza ligi hiyo ita tegemea mechi ya leo kama Aresenal ataweza kupata matokeo mazuri dhiya TOTTENHAM Aresenal ata kuwa ana ongoza ligii Chelsea

Kivumbi Ligi Kuu Bara leo, Yanga kukinukisha na Prisons, Simba na Lyon

Picha
Na Saida Salum Kinyang' anyiro cha Ligi Kuu Tanzania bara kinaendelea leo kwa mechi nane kupigwa katika viwanja tofauti hapa nchini. Kule Manungu mjini Morogoro, wenyeji Mtibwa Sugar watawaalika Mbeya City kiboko wa Yanga, wakati katika uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, African Lyon watawakaribisha Wekundu wa Msimbazi, Simba SC. Mwadui wakitumia uwanja wao wa Mwadui kule Shinyanga watawaalika Majimaji ya Songea, Mbao FC ya Mwanza itautumia uwanja wa CCM Kirumba kuwakaribisha Azam FC ya Chamazi Dar es Salaam, na Ndanda ya Mtwara itawakaribisha Stand United 'Chama la wana' kule Nangwanda Sijaona. Kipute kitakuwa jijini Mbeya masarange wa Prisons wakiwakaribisha mabingwa watetezi ambao wanasuasua msimu huu Yanga SC ambao leo wameapa kukinukisha kwani Jumatano iliyopita walifungwa mabao 2-1 na Mbeya City. Kagera Sugar wakitumia uwanja wao wa Nyasi bandia wa Kaitaba watakuwa wenyeji wa Ruvu Shooting ya Masau Bwire na JKT Ruvu watacheza uwanja wao wa Mabatini kuwakaribisha Toto

Leo ndio leo fainali ya kombe la Shirikisho Afrika

Picha
Na Prince Hoza, Lubumbashi Leo nyasi za uwanja wa Stade TP Mazembe mjini Lubumbashi hapa Jamhuri ya Kidemokrasia ya watu wa Congo zitawaka moto kwa miamba TP Mazembe watakapoialika Mo Bejaia ya Algeria katika mchezo wa fainali. Timu hizo zilikutana Oktoba 29 mwaka huu katika dimba la Stade Mustapha Tchaker kule mjini Bejaia Algeria ambapo timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1. Kwa maana hiyo mchezo wa leo utakaopigwa saa 9:30 jioni TP Mazembe watahitaji sare isiyo na mabao ili waweze kutwaa ubingwa wa kombe la Shirikisho, msimu uliopita Mazembe ilitwaa ubingwa wa Ligi ya mabingwa ambapo msimu huu waliondoshwa mapema

USHAHIDI WA PICHA: MASHALI KUMBE ALISILIMISHWA NA SHEIKH SHARIFU

Picha
Picha/Habari na Salum Fikiri Jr Bondia Thomas Mashali ambaye jana alizikwa katika makaburi ya Kinondoni kwa dini ya Kikristo dhehebu la Katoliki kumbe siku za hivi karibuni alibadili dini na kuingia Uislamu. Mbaruku Heri ambaye naye ni bondia na kocha wa mchezo huo, amethibitisha kuwa Thomas Mashali ni muislamu lakini anashangaa kuzikwa kikristo, bondia huyo aliamua kusilimu yeye mwenyewe na Sheikh aliyehusika kumbadili ni Sharifu. Heri anadai kuwa bondia huyo aliamua aitwe Mohamed Mashali, lakini anasikitika kuona akizikwa kwa dini ya Kikristo aliyoikataa marehemu mwenyewe, Heri anasema iko wapi haki ya Waislamu mbona wapo Waislamu walioamua kuingia Ukristo na wakifa wanazikwa Kikristo, Heri anasema kuna kaubaguzi kidogo hapa nchini

Simba sasa hii sifa!

Picha
Na Prince Hoza, Shinyanga Simba SC wameendelea kulifukuzia kwa mwendokasi taji la ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kufuatia ushindi wa bao 1-0 dhidi ya timu ngumu msimu huu Stand United ya Shinyanga. Ushindi huo unaifanya Simba SC ifikishe pointi 35 baada ya kucheza mechi 13, wakati Stand inabaki na pointi zake 22 za mechi 14. Bao lililoipa ushindi Simba lilifungwa na winga machachari wa Wekundu hao wa Msimbazi Shiza Ramadhan Kichuya kwa mkwaju wa oenalti  katika dakika ya 33 baada ya Mrundi Laudit Mavugo kuangushwa na beki Adeyuni  Ahmed kwenye boksi

Yanga yakalishwa 2-1 na Mbeya City

Picha
Na Ikram Khamees, Mbeya Mbeya City FC imeutumia vema uwanja wake wa Sokoine mjini Mbeya baada ya kuwafunga mabingwa watetezi Yanga mabao 2-1. Ushindi huo wa kwanza kwa Mbeya dhidi ya Yanga tangu wapande Ligi Kuu, unaifanya Mbeya City ifikishe pointi 19 baada ya kucheza mechi 14 wakati Yanga inabaki na pointi zake 27 za mechi 13. Mabao ya Mbeya City yalifungwa kipindi cha kwanza na Hassan Mwasapili na nahodha Kenny Ally, na goli moja la Yanga nalo lilifungwa kipindi cha kwanza na mshambuliaji wake Mzimbabwe Donald Ngoma, Yanga wanaendelea kukaa nafasi ya pili

Nini kilichowaponza FC Barcelona?

Picha
Na Nasri Alfan Champions league jana iliendelea kwa michezo kadhaa kupigwa Takriban Timu kubwa zote ziliweza kupata matokeo mazuri Kasoro Fc barcelona walio poteza mbele ya Manchester City kwa goli 3  kwa 1 Magoli ya man city yali fungwa na Gundogan aliye funga 2 Na lile moja liki fungwa na D. Bruyner Huku goli barcelona liki fungwa na  Leonal Messi Kuwa kosa badhi ya wachezaji kuliwa athir barcelona walimkosa beki wao G.pique na kiunga Ander Iniesta huku nafasi ya Pique ikizibwana Umtiti na ile ya Iniesta ikizibwa na Ander Gomez Kuwa kosa wachezaji wa wili hawa kuna namna ambavyo ime wa Athiri moja kwa moja fc barcelona Pia huwezi kuacha kuwa pongeza Manchester City ambao waliweza kucheza kandanda safii hasa kipindi Cha pili Ubora wa mchezaji mjomoja pia uli chagiza City kupata matokeo K.D Bruyner nimoja ya wachezaji walio weza kuonesha uwezo mkubwa kipindi cha 2 na kuwa mwiba mkali kwa upande wa fc barcelona Namna alivo weza kutumia vyema mpira wa adhabu na kuweza kufung