Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2017

Chuji Busungu, Seme nao kimeeleweka

Picha
Kiungo wa zamani wa Yanga na Simba Athuman Idd 'Chuji' amesaini mkataba wa mwaka mmoja kujiunga na timu ya Ligi Kuu ya Ndanda FC ya mjini Mtwara. Chuji aliwahi kutamba kwenye vilabu vya Simba na Yanga kwa nyakati tofauti zote akizichezea mara mbili mbili, lakini alijiunga na Mwadui ya Shinyanga ambayo nayo aliachana nayo kabla ya msimu uliopita kujiunga na timu ya daraja la kwanza ya KCM ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. Naye mshambuliaji wa zamani wa Mgambo JKT na Yanga, Malimi Busungu amesaini mkataba wa mwaka mmoja kujiunga na Lipuli ya mjini Iringa ambayo nayo itashiriki Ligi Kuu Bara. Wakati Busungu akisaini kujiunga na Lipuli, kiungo mwingine wa zamani wa Yanga na Ndanda, Omega Seme amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na Lipuli Omega Seme, mwenye jezi nyekundu, akitambulishwa kujiunga na Lipuli Malimi Busungu (Katikati) akitambulishwa kutua Lipuli Athuman Idd "Chuji" akisaini Ndanda

SIMBA YAMALIZANA NA MANULA, APAA

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam. Hatimaye klabu ya Simba imekamilisha usajili wa mlinda mlango namba moja hapa nchini Aishi Salum Manula ambaye pia ni mchezaji wa Azam FC na timu ya taifa, Taifa Stars, Manula amesaini Simba mkataba wa miaka miwili. Minong' ono ilikuwa mingi kwamba kipa huyo asingejiunga Simba lakini Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano wa Simba, Haji Manara akathibitisha kuwa kipa huyo sasa ni mali ya Simba na anakuwa mchezaji wa 13 kusajiliwa na kikosi hicho huku huenda Haruna Niyonzima naye akatambulishwa. Manula atapaa kesho kuelekea Afrika Kusini ambako wenzake wapo huko wakijifua kwa kambi maalum ya kujiandaa na msimu mpya, Manula atakuwa na kazi ngumu kukaa langoni kwakuwa atakuwa sambamba na kipa mwenzake wa Stars, Said Mohamed Nduda Aishi Manula amejiunga Simba

AVEVA, KABURU NAO KUSOTA HADI AGOSTI 7

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Mahakama ya Kisutu leo imeipiga tena kalenda kesi ya utakatishaji fedha inayowakabili viongozi wa klabu ya Simba, Rais Evans Aveva na makamu wake Geofrey Nyange Kaburu ambapo sasa wamerudishwa rumande hadi Agosti 7 mwaka huu wakati kesi yao itakaposikilizwa tena. Wawili hao wanakabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha ambapo kisheria wanakosa dhamana, Aveva na Kaburu leo wote wamefika mahakamani tofauti na  Julai 21 ambapo Kaburu hakufika mahakamani alikuwa akiugua ghafla. Kusogezwa mbele kwa kesi hiyo kunapisha kukamilika kwa upepelezi na kama ukikamilika basi kuna uwezekano wawili hao wakahukumiwa na kama usipokamilika kuna uwezekano wa kuendelea kusota mahabusu Evans Aveva (Kushoto) na Geofrey Nyange Kaburu (Kulia) wanaendelea kusota rumande

Akina Malinzi kuendelea kusota

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Kesi ya utakatishaji fedha inayomkabili Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini, (TFF) Jamal Malinzi na wenzake, katibu wa TFF, Celestine Mwesigwa na mkurugenzi wa fedha wa Shirikisho hilo, Isiande Isowafe imepigwa kalenda. Kesi hiyo imesogezwa hadi Agosti 11 mwaka huu, Malinzi na wenzake walifika mahakamani Kisutu leo na hakimu aliyekuwa akisikiliza shauri lao akaamua kuipiga kalenda kesi hiyo hivyo Malinzi na wenzake wamerudishwa tena rumande hadi Agosti 11. Kusogezwa mbele kwa kesi hiyo kunapisha upepelezi ambapo ukikamilika basi viongozi hao wanaweza kuhukumiwa, na kama ushahidi kamili utakosekana basi wanaweza kuachiwa, tayari Malinzi ameshaachia ngazi nafasi ya Urais na sasa Walace Karia anakaimu nafasi yake Malinzi na wenzake wakirudishwa rumande

Hatimaye mrithi wa Niyonzima asaini Yanga

Picha
Na Ikram Khamees. Morogoro Hatimaye klabu bingwa ya soka Tanzania Bara, Yanga SC imefanikiwa kukamilisha usajili wa kiungo fundi wa Mbeya City na timu ya taifa, Taifa Stars, Raphael Daudi ambaye amesaini mkataba wa miaka miwili. Mchezaji huyo anaungana na kikosi hicho kesho, Yanga imeweka kambi mjini hapa ikijiandaa na mchezo wake wa Ngao ya Jamii na mahasimu wao Simba mchezo ambao utapigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Daudi anakuwa mchezaji wa nane kusajiliwa na Yanga akiungana na Abdallah Shaibu "Ninja" kutoka Taifa Jang' ombe ya Zanzibar, Ibrahim Ajibu kutoka Simba, Pius Buswita kutoka Mbao FC. Wengine ni Youthe Rostand kutoka African Lyon, Ramadhan Kabwili (Huru) na Burhan Akilimali (Huru ), Daudi ni mrithi wa Niyonzima aliyekwenda Simba Raphael Daudi ajiunga na Yanga

Kilichomvua unahodha Mkude hiki hapa

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Siku moja baada ya kuvuliwa unahodha wa Simba Jonas Mkude na kukabidhiwa Mzimbabwe Method Mwanjale atakayesaidiana na John Bocco "Adebayor" na Mohamed Hussein "Tshabalala", siri imefichuka. Taarifa ambazo zina uhakika kabisa kutoka Msimbazi zinasema kuwa Mkude amevuliwa unahodha baada ya kuhangaishana na mabosi wa timu hiyo katika suala la kuongeza mkataba. Inasemekana mchezaji huyo alikuwa rafiki mkubwa wa mshambuliaji Ibrahim Ajibu aliyejiunga na Yanga na wote lao lilikuwa moja ambapo kila mmoja alitaka dau kubwa zaidi ili wasalie Msimbazi na Ajibu aliamua ajiunge na Yanga baada ya Simba kukataa kumpa dau hilo. Ilikuwa chupuchupu Mkude naye aende Yanga kama ilivyo kwa Ajibu, hapo ndipo alipoanza kuwachefua mabosi wa Simba na walipokamilisha kandarasi wakaamua kumpoka unahodha kwani siku zote nahodha huwa na nidhamu ndani na nje ya uwanja Jonas Mkude amevuliwa unahodha

Tizi la Yanga Morogoro kama Ulaya

Picha
Na Ikram Khamees. Morogoro Asikwambie mtu, Yanga SC wanapiga zoezi la hatari kama vile vilabu vya Ulaya, Kocha mkuu wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara, Mzambia George Lwandamina anaendelea kukiweka fiti kikosi cha Yanga ambacho Agosti 23 kitavaana na mahasimu wao Simba SC. Mzambia huyo amekuwa akiwapa mazoezi mbalimbali ambayo pia yamekuwa yakifanywa na vilabu vikubwa barani Ulaya kama FC Barcelona, Real Madrid, Chelsea, Manchester United, Manchester City, Liverpool, Arsenal, Ac Milan na nyinginezo. Baadhi ya mashabiki wanaojitokeza kushuhudia mazoezi hayo wanasema kama kikosi hicho kitafungwa katika mechi zake zijazo basi hakina bahati kwani zoezi wanaloliona ni hatari, shabiki mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Mau amedai Yanga itatetea ubingwa wake. Baadhi ya wachezaji ambao wamekuwa kivutio ni pamoja na Mzambia Obrey Chirwa, Ibrahim Ajibu, Juma Abdul na kiberenge Baruhan Akilimali, Yanga itacheza mchezo wa kirafiki na Singida United Wachezaji wa Yanga wanafanya mazo

YANGA NA RAPHAEL DAUDI WAFIKA PATAMU

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga SC, wamefikia pazuri na kiungo wa Mbeya City, Raphael Daudi ambapo sasa anaweza kumwaga wino kwa ajili ya kujiunga nao hiyo kesho. Yanga walianza kumwania Daudi tangu mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania bara, lakini mipango haikuweza kukamilika, mabingwa hao waliingia tena kutaka saini yake baada ya kuondokewa na kiungo wake wa kimataifa, Haruna Niyonzima raia wa Rwanda anayedaiwa kujiunga na Simba. Uongozi wa Mbeya City leo umethitisha kumruhusu kiungo huyo ambaye pia anaichezea timu ya taifa, Taifa Stars akakipigeJangwani, naye mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Yanga , Hussein Nyika amesema wao na Daudi watamalizana hivi karibuni lakini duru zinasema kesho mchana Raphael Daudi kutua Yanga

BABU MWANJALE NAHODHA MPYA SIMBA

Picha
Na Mwandishi Wetu. Afrika Kusini. Klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam leo imemvua rasmi unahodha Jonas Mkude na kumpachika Mzimbabwe Method Mwanjale "Babu" ambaye atasaidiwa na John Bocco "Adebayor" na Mohamed Hussein "Tshabalala". Kwa mujibu wa Mkuu wa kitengo cha Habari na mawasiliano wa klabu hiyo, Haji Sunday Manara imesema kuwa Mwanjale atakuwa nahodha mpya wa klabu hiyo badala ya Jonas Mkude ambaye sasa atakuwa mchezaji wa kawaida. Haijajulikana sababu gani iliyopelekea kumuondoa Mkude katika nafasi hiyo, ingawa Mambo Uwanjani inafahamu kila kitu kuondoshwa kwa Mkude katika nafasi hiyo, Mwanjale ni mchezaji mwenye nidhamu ya hali ya juu na pia ni mkongwe na ndiyo imepelekea akabidhiwe nafasi hiyo Method Mwanjale, awa nahodha mpya Simba

Rasmi,Msuva asaini El Jajida

Picha
Kiungo wa kimataifa wa Tanzania Simon Happygod Msuva amesaini mkataba wa kujiunga na timu ya Ligi Kuu ya Difaa El Jajida ya Morocco lakini klabu hiyo imefanya siri haijaweka wazi mkataba huo ni wa muda gani. Taarifa iliyotolewa na klabu hiyo mchana wa leo imesema kwamba, Difaa El Jajida imemalizana na mchezaji huyo na tayari imeshamtambulisha kwa mashabiki wake. Aliyekuwa katibu wa Yanga Sc, Dk Jonas Tiboroha anahusika katika usajili huo akianza kupatana na kumuuza pia, inasemekana Yanga itapatiwa Dola 150,000 ambazo ni sawa na shilingi Milioni 300 za Kitanzania. Msuva anaungana na winga mwingine wa Tanzania, Ramadhan Singano "Messi" ambaye alikuwa anaichezea Azam FC, Msuva alijiunga na Yanga mwaka 2012 akitokea Moro United ambayo nayo ilimchukua akitokea Akademia ya Azam FC Simon Msuva ameondoka Yanga Simon Msuva (wa pili kutoka kulia, akitambulishwa kujiunga na Difaa El Jajida, wa kwanza kulia ni meneja wake Jonas Tiboroha

Tshishimbi asaini miaka miwili Jangwani

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Klabu bingwa ya soka Tanzania Bara, Yanga SC, hatimaye imemalizana na kiungo mkabaji Papy Tshishimbi Kabamba raia wa DRC kwa kandarasi ya miaka miwili, kwa maana hiyo kiungo huyo atakipiga Jangwani hadi mwaka 2019. Papy Tshishimbi alianza kuingia kwenye rada za Yanga tangu alipokuja nchini na kikosi cha Mbabane Swallors cha Swaziland kilipocheza na Azam FC mchezo wa kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilikuwa ikihaha kutafuta kiungo mkabaji namba sita kwa muda mrefu baada ya kuondokewa na mafundi Athuman Iddi 'Chuji' na Frank Domayo ambao waliweza kumudu kucheza nafasi hiyo, Tshishimbi alifuzu vipimo vya afya na kuingia rasmi mkataba leo mchana Papy Tshishimbi Kabamba mwenye jezi nyekundu amesainj Yanga miaka miwili

Ajibu asema Simba wakawaida sana atawatungua tu

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Kiungo mshambuliaji mpya wa mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga SC, Ibrahim Ajibu Migomba maarufu Kadabla amesema klabu yake ya zamani Simba SC ni timu ya kawaida sana na wala hana wasiwasi nao atawatungua tu ifikapo Agosti 23. Simba na Yanga zitakutana Agosti 23 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam mchezo wa kuwania Ngao ya Jamii, Ajibu ambaye aliichezea Simba msimu uliopita amejiunga na Yanga na atakuwemo kwenye kikosi cha Wanajangwani hao. Akizungumza jana wakati timu hiyo ikimalizia mazoezi yake ya Gym jijini Dar es Salaam kabla ya leo kupaa zao kuelekea mjini Morogoro kwa ajili ya kambi ya kujiandaa na mchezo huo, amedai mashabiki wa Yanga wajiandae kwa kicheko tu Simba wa kawaida lazima awalaze mapema. Ajibu anasifika kwa kasi yake aliyonayo na uwezo mkubwa wa kupiga mipira ya kutenga huku pia akisifika kwa mashuti, mashabiki wa Yanga wanaamini Ajibu akicheza sambamba na Donald Ngoma, Amissi Tambwe na Obrey Chirwa kuna uwezek

Simba kuanza kucheza na Orlando, Bidvest

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Timu ya soka ya Simba SC, ya jijini Dar es Salaam ambayo kwa sasa imeweka kambi yake nchini Afrika Kusini ikiwa katika maandalizi ya msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara. Kwa mujibu wa Mkuu wa kitengo cha Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo Haji Manara amesema Wekundu hao wanatarajia kushuka viwanjani kucheza mechi za kujipima nguvu. Simba itacheza na Orlando Pirates kisha itacheza na Bidvest Wits ambazo zote zinashiriki Ligi Kuu ya Afrika Kusini, mechi hizo zitachezwa juma lijalo na Simba itamaliza ziara yake kisha itarejea Dar es Salaam kucheza mechi nyingine ya kirafiki kuadhimisha Simba Day Wachezaji wa Simba wakijifua

Azam FC yaibutua Lipuli ya Seleman Matola 'Veron'

Picha
Na Mwandishi Wetu. Iringa Timu ya Azam FC ya jijini Dar es Salaam imefufua matumaini baada ya kuilaza Lipuli ya Iringa mabao 4-0 mchezo wa kirafiki uliopigwa leo. Azam ilianza vibaya ziara yake ya nyanda za juu kusini baada ya  kupoteza mechi zake mbili moja ikitoka sare tasa na Mbeya City 0-0 na nyingine kufungwa na Mji Njombe 2-0. Kikosi cha Azam kinachonolewa na Mromania, Aristica Cioaba kilianza kuonyesha kandanda safi tofauti na ilivyocheza na Mji Njombe na kuweza kujipatia ushindi huo mkubwa siku ya leo, Lipuli iliyopanda daraja ikiwa chini ya kocha Seleman Matola 'Veron' ambaye amewahi kuichezea Simba SC na baadaye kuwa kocha msaidizi imeweza kuwasononesha mashabiki wake. Mabao ya Azam FC yalifungwa na Yakubu Mohamed, Waziri Junior, Yahya Zayid na Salum Abubakar "Sure Boy", Azam imeweka kambi nyanda za juu kusini ikijiandaa na Ligi Kuu Bara Azam FC imeifumua Lipuli ya Iringa mabao 4-0

HUMUD,TEGETE WAENDA MAJIMAJI

Picha
Na Mwandishi Wetu. Ruvuma Mshambuliaji wa zamani wa Yanga SC, Jerryson Tegete na kiungo wa zamani wa Mtibwa Sugar na Simba SC, Abdulhalim Humud wote kwa pamoja wamejiunga na Majimaji ya Songea kwa ajili ya msimu ujao. Majimaji inayonolewa na Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga na Kajumulo World Soccer  , Kalimangonga Mtoro Ongala wamesaini mkataba wa miaka miwili kila mmoja. Tegete ambaye alikuwa akiichezea Mwadui FC ya Shinyanga ameamua kubadili upepo na kujiunga na timu hiyo iliyowahi kutwaa ubingwa wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania mara mbili, Humud naye alikuwa akicheza soka la kulipwa nchini Oman Abdulhalim Humud amejiunga na Majimaji Jerry Tegete naye amejiunga na Majimaji

Ronaldo wa Ndondo Cup atua Mbeya City

Picha
Na Exipedito Mataruma. Mbeya Wagonga Nyundo wa Mbeya City ya jijini Mbeya imeendelea kujiimarisha baada ya kufanikiwa kuwasainisha wachezaji wawili kwa mkupuo. Wagonga nyundo hao jana wamekamilisha usajili wa Antony Mwingira na kiungo mshambuliaji wa zamani wa Ashanti FC na KCM zote za Dar es Salaam, Iddi Seleman maarufu kama Ronaldo. Ronaldo anasifika sana kwa uchezaji wake katika michuano ya Ndondo Cup inayochezwa jijini Dar es Salaam, kiungo huyo amekuwa akizivhezea timu mbalimbali ikiwemo Faru Jeuri, wachezaji wote hao wamesaini mkataba wa miaka miwili Iddi Seleman "Ronaldo" amejiunga na Mbeya City

Aishi Manula amgwaya Nduda Simba

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Kipa chaguo la kwanza wa timu ya taifa, Taifa Stars, Aishi Manula amesema hawezi kujiunga na Simba SC kwa sasa mpaka pale mkataba wake na Azam FC utakapomalizika. Manula amedai kwa sasa anajipanga kurejea Azam kwani anaheshimu mkataba wake ambao utamalizika katikati ya Agosti mwaka huu, ameongeza kuwa anataka kuwasiliana ma meneja wa Azam, Philipo Arando ili ampe maelekezo na aingia kambini. Azam imefanya ziara katika mikoa ya nyanda za juu Kusini hivyo na yeye atalazimika kuwafuata, hii ina maana kwamba hatojiunga na Simba kama inavyoelezwa kuwa amesaini mkataba wa miaka miwili. Lakini taarifa za chini kwa chini zinasema kipa huyo amemkacha kipa mwenzake Said Mohamed Nduda ambaye naye amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na Simba, Nduda naye ni kipa wa timu ya taifa, Taifa Stars na alipangwa mara moja katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu dhidi ya Lesotho ambapo alidaka vizuri na kuchaguliwa kipa bora wa mashindano ya Cosafa Castle Cup yaliyo

Kabwili asaini Yanga miaka mitano

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Kipa chipukizi wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Ramadhan Kabwili amesaini mkataba wa miaka mitano kwa ajili ya kujiunga na mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga SC. Kabwili atadumu na Yanga hadi mwaka 2022, kipa huyo chipukizi aliitwa kwenye timu ya taifa, Taifa Stars inayonolewa na Salum Mayanga kwa ajili ya michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani maarufu Chan. Kabwili aliibukia kwenye timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 maarufu Serengeti Boys ambayo ilishiriki fainali za mataifa ya Afrika kwa vijana wa umri huo zilizofanyika mapema mwaka huu nchini Gabon, kipa huyo aliweza kushiriki mechi zote katika kikosi cha kwanza na ndipo Yanga ilipomuona na kuamua kumnasa Kipa wa Serengeti Boys, Ramadhan Kabwili amesaini Yanga miaka mitano

NDEMLA NAYE KUTIMKIA SWEDEN

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Kiungo mwenye mashuti wa Simba SC, Said Khamis Ndemla naye anatarajiwa kuelekea nchini Sweden tayari kabisa kujiunga na timu ya Ligi Kuu, AFC Eskilistuna ambayo pia anaichezea Mtanzania Thomas Ulimwengu. Eskilistuna ilimuhitaji Ndemla tangia mwishoni mwa msimu uliopita lakini Simba SC ikakataa kumuachia akajiunge na timu hiyo kwa madai bado wanamuhitaji, lakini sasa endiketa ya kijani imewaka. Simba ambayo imemnasa Haruna Niyonzima kutoka Yanga ina kila sababu ya kumruhusu Ndemla akajaribu bahati yake, inasemekana kiungo huyo ataondoka baada ya mchezo wa Ngao ya Hisani kati ya Yanga na Simba, Agosti 23 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Said Ndemla (Kushoto) anaelekea Sweden kucheza soka la kulipwa

Msuva kimeeleweka Morocco, kesho anapaa

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Kiungo mshambuliaji wa mabingwa wa soka hapa nchini, Simon Msuva anatarajiwa kuondoka nchini kesho kuelekea nchini Morocco tayari kabisa kujiunga na timu yake mpya ya Difaa El Jajida. Msuva atapaa kesho jioni akiwa na uhakika kabisa wa kujiunga na timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya nchi hiyo, Msuva ambaye pia ni mchezaji wa timu ya taifa, Taifa Stars, amecheza kwa mafanikio makubwa akiwa na klabu yake ya Yanga. Difaa El Jajida imemchukua Mtanzania mwingine Ramadhan Singano "Messi" wa Azam FC, Msuva anaungana pia na nyota Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu, Elius Maguli na Farid Musa ambao wanacheza soka la kulipwa nje ya nchi Simon Msuva, anaondoka kesho kuelekea Morocco

Rage aichambua Zanzibar, asema haikustahili kupewa uanachama Caf

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Mwenyekiti wa zamani wa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage ameichambua Zanzibar na kudai haikustahili hata kidogo kupewa uanachama hata wa muda na Shirikisho la mpira wa miguu Barani Afrika, (CAF) na waliojaribu kuipa walikosea sana. Akizungumza jana, Rage amesema Zanzibar haina hadhi ya kupewa uanachama na CAF kwakuwa siyo nchi kamili inayotambuliwa na Umoja wa mataifa na Afrika pia. Amefafanua kuwa nchi inayotambulika na kupewa uanachama ni ile mwanachama wa Umoja wa Mataifa (UN), amezitaja nchi zilizopata uanachama ambazo si nchi kamili kama Zanzibar kuwa ni Ireland, Scotland, Trinidad and Tobacco na Wiles kuwa hizo zilipewa kwakuwa Uingereza ndiyo mwanzilishi wa FIFA. Rage amedai Zanzibar ni sehemu ya Tanzania hivyo nchi moja haiwezi kuwa na wanachama wawili na amewataka Wazanzibar kwa hili wawe wapole Alhaj Ismail Aden Rage, amesema Zanzibar haikustahili kupewa uanachama

Azam FC yabutwa na Mji Njombe

Picha
Na Mwandishi Wetu. Njombe Timu ya Mji Njombe jioni ya leo imefanikiwa kuwasambaratisha mabingwa wa Afrika mashariki na kati, Azam FC ya jijini Dar es Salaam mabao 2-0 mchezo wa kirafiki uliofanyika katika uwanja wa Mji Njombe. Ikicheza kwa kutumia karibu nyota wake wote wakiwemo wale wa kimataifa, vijana wa Mji Njombe ambao msimu ujao watacheza Ligi Kuu bara walifanikiwa kupata bao la kuongoza katika dakika ya 34 kipindi cha kwanza lililofungwa na Adam Baiko. Hadi mapumziko Mji Njombe walikuwa mbele kwa bao hilo, kipindi cha pili Azam walikuja na nguvu mpya baada ya kuwatoa wachezaji wake 11 na kuingiza wengine lakini hawakumzuia Raphael Siame ambaye alifunga bao la pili dakika ya 80. Huo ni mchezo wa pili kwa Azam tangu waanze ziara yao ya Nyanda za juu kusini, katika mchezo wa kwanza, Azam ilitoka suluhu na Mbeya City Azam FC leo wamepigwa na Mji Njombe

Wallace Karia aweka wazi uraia wake

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Kaimu Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini, (TFF) Wallace Karia leo ameweka wazi uraia wake baada ya kuwekewa pingamizi na Iman Madega. Karia ambaye pia ni makamu wa Rais wa Shirikisho hilo na mgombea nafasi ya Urais, aliwekewa pingamizi na mgombea mwenzake Iman Madega kuwa siyo raia wa Tanzania kama sheria inasema. Karia amedai yeye ni Mtanzania wa kuzaliwa lakini ana asili ya Somalia, akizungumzia hilo, Karia ameshangazwa na mgombea mwenzake aliyemwekea pingamizi akidai ni wivu tu kwake. Ameongeza kuwa wapo Watanzania kadhaa ambao wameshika nyadhifa mbalimbali za uongozi lakini ni Waarabu au Wahindi ingawa ni raia wa Tanzania kama ilivyo kwake yeye Wallace Karia, amedai yeye ni Mtanzania ila ana asili ya Kisomali

Mtibwa Sugar yalamba dume kwa Dilunga

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Timu ya Mtibwa Sugar yenye maskani yake katika mashamba ya miwa yaliyopo Turiani, mkoani Morogoro leo imefanikiwa kumsainisha mkataba wa miaka miwili kiungo fundi Hassan Dilunga. Dilunga mmoja kati ya viungo bora kabisa hapa nchini aliyewahi kuichezea Yanga SC kwa mafanikio lakini ameangukia kwa Wakata miwa hao. Dilunga anaungana na straika chipukizi wa Ndanda FC, Riffat Khamis ambaye naye amesaini kujiunga na timu hiyo, mbali na nyota hao, tayari Mtibwa Sugar imeshafanikiwa kumnasa Salum Kanoni ambaye aliwahi kucheza Simba Hassan Dilunga akisaini Mtibwa Sugar leo

STRAIKA LA MABAO LA GHANA HILI HAPA MSIMBAZI

Picha
Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam Simba SC sasa imepania kwenye suala la usajili kwani imeamua kusajili wachezaji wote nyota ndani ya nje ya Tanzania, Nicholaus Gyan raia wa Ghana ndiye straika mpya anayetarajia kutua katika klabu hiyo. Gyan ameonyesha uwezo mkubwa katika Ligi Kuu ya Ghana huku akifanikiwq kufunga mabao 12, straika huyo unaambiwa ni hatari kinoma  na Wekundu wa Msimbazi wamepanga kumshusha hivi karibuni. Hadi sasa Simba imeshasajili wachezaji 12 na inadaiwa kuna wengine wawili watasajiliwa, Gyan ameshawekwa katika orodha ya watakaosajiliwa na kitu kinachosubiriwa kwa sasa ni ujio wake tu, Gyan atasimama namba tisa na anasifika kwa mashuti Nicholaus Gyan, straika mpya Simba

Kambi ya Simba, South usipime

Picha
Na Exipedito Mataruma. Afrika Kusini Mabingwa wa kombe la FA, Simba SC wamepiga kambi hapa Afrika Kusini wakifanya mazoezi yao katika Uwanja wa Edenvale uliopo hapa Afrika Kusini, timu hiyo inayonolewa na Mcameroon Joseph Omog na msaidizi wake Jackson Mayanja inafanya mazoezi ya hatari. Simba iko hapa ikijiandaa na mchezo wake wa Ngao ya Jamii dhidi ya mahasimu wao Yanga SC mchezo utafanyika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Simba imekuja hapa na wachezaji 12 na nyota wake wengine waliokuwa na kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars nao watajiunga na wenzao hivi punde hasa baada ya jana kuondoshwa katika michuano ya Chan, Ingia Youtube tumewawekea video ya mazoezi ya Simba Wachezaji wa Simba wakiwa mazoezini Afrika Kusini

Tenga aula CAF

Picha
Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam Rais wa zamani wa Shirikisho la kandanda hapa nchini, (TFF), Leodegar Chila Tenga amechaguliwa kuwa makamu wa Rais  wa kamati ya ufundi na maendeleo wa Shirikisho la kandanda barani Afrika, (CAF). Tenga ambaye ni mjumbe wa heahima wa TFF amepata nafasi hiyo kupitia mkutano wa CAF uliofanyika Rabat, Morocco ambao pia ulipitisha maazimio mbalimbali. Naye Kaimu Rais wa TFF, Walace John Karia amemtumia salamu za pongezi Tenga na kusema hiyo ni nafasi adimu kwa Tanzania, Karia amesema kitendo na Tenga kuteuliwa kuwa makamu wa Rais wa kamati hiyo ya ufundi na maendeleo kunadhihiriaha Tanzania kulivyojaaliwa viongozi wa soka Leodegar Tenga

Singida United wafunga usajili kwa Kigi Makasi

Picha
Na Paskal Beatus. Mwanza Timu ya Singida United imefanikiwa kukamilisha usajili wake baada ya kumsajili kiungo mshambuliaji wa Ndanda FC, Kigi Makasi kwa mkataba wa miaka miwili. Kwa mujibu wa uongozi wa Singida United umesema kuwa Kigi anakuwa mchezaji wa mwisho kusajiliwa na timu hiyo baada ya kumaliza kwa wachezaji wa kimataifa. Timu hiyo kwa sasa itakuwa imeshawasajili wachezaji 15 huku wachezaji saba pekee wakiwa wa kimataifa kutoka nchi za Zimbabwe, Rwanda na Uganda, Hans Van der Pluijm ndiye kocha mkuu wa kikosi hicho kilichopanda Ligi Kuu Kigi Makasi (Kushoto) akitambulishwa kujiunga na Singida United, kulia ni kocha wa timu hiyo, Mholanzi Hans Pluijm

Rooney apiga bonge la bao, Samatta achomoa

Picha
Mshambuliaji Wayne Rooney jana alifunga bonge la goli katika mchezo wa kirafiki baina ya Everton ya Uingereza na KRC Genk ya Ubelgiji ulioisha kwa sare ya bao 1-1. Mtanzania Mbwana Samatta aliisawazishia Genk katika dakika ya 55 na kufanya matokeo yawe sare sare maua, Everton wapo katika maandalizi ya msimu ujao na juma lililopita ilikuwa katika ardhi ya Tanzania ambapo ilicheza na Gor Mahia ya Kenya na kushinda mabao 2-1. Wayne Rooney amekuwa katika mwanzo mzuri tangu ajiunge na timu hiyo akitokea kwa Mashetani Wekundu, Manchester United, staa huyo amekuwa akifunga karibu mechi zote ilizocheza Everton Mtanzania, Mbwana Samata leo amefunga goli la kusawazisha Wayne Rooney (Katikati) akishangilia goli lake

Peter Manyika atolewa kwa mkopo

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Mlinda mlango Peter Manyika Jr anatolewa kwa mkopo wakati kipa mwingine Dennis Richard ametemwa rasmi. Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu ya Simba, Zacharia Hanspoppe amesema leo kuwa wameamua kumtoa kwa mkopo Manyika Jr kwakuwa akarejeshe kiwango. Manyika ameonekana kushuka kiwango na ndio maana hakuwa akianza katika kikosi cha kwanza, pia Hanspoppe amesema Simba imewaacha Novat Lufunga, Hamad Juma, Pastory Athanas, Janviel Bokungu na Dennis Richard. Mwenyekiti huyo amesifu usajili walioufanya na kudai umezingatia mahitaji ya mwalimu Joseph Omog na msaudizi wake Jackson Mayanja Peter Manyika ametolewa kwa mkopo

Tanzania yatupwa nje CHAN

Picha
Na David Pasko. Rwanda Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars jioni ya leo imetupwa nje ya michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani (CHAN) baada ya kulazimishwa sare tasa 0-0 na wenyeji Rwanda (Amavubi) katika mchezo wa marudiano uliofanyika Uwanja wa Nyamirambo, mjini Kigali. Wenyeji Rwanda walikuwa wanahitaji sare tasa ama ushindi wa aina yoyote kwakuwa tayari wana bao moja la ugenini walilolipata jijini Mwanza baada ya kulazimisha sare ya mabao 1-1 na Taifa Stars. Kocha wa Tanzania Salum Mayanga leo amewaanzisha Simon Msuva, Muzamil Yasini, John Bocco 'Adebayor na Shiza Kichuya lakini hawakuweza kupenya ukuta wa Rwanda ambao sasa wanakwenda kukutana na Uganda katika mchezo ujao. Kwa maana hiyo Taifa Stars imeondoshwa kwenye michuano hiyo nanitaendelea kuwa mtazamaji, wachezaji wa kikosi hicho sasa watarejea kwenye vilabu vyao kwa ajili ya nashindano yajayo Kikosi cha Stars kimetolewa 

MAMBO UWANJANI WAANZISHA TV YAO

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Tovuti inayokuja juu kwa sasa hapa nchini hasa kwa utayarishaji na uandishi wao mzuri wa habari wa Mambo Uwanjani Blogspot wenye makazi yake jijini Dar es Salaam umefungua Tv yake ya Online. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mtendaji mkuu wa Mambo Uwanjani, Prince Hoza amesema, ni kweli Mambo Uwanjani wameanzisha tv yao inayopatikana kupitia chanel ya youtube. Hoza amesema tv yao inaitwa Mambo Spoti Tv ama kwakifu MSTV ambapo amewataka wapenzi wa Mambo Uwanjani kutembelea tv yao kupitia youtube na amedai wataanza pia kurusha mpira live. "MSTV ipo kwa ajili ya michezo, burudani na vichekesho, na wala hatutadili na siasa wala mambo mengine yasiyotuhusu", alisema Hoza ambaye pia ni mwandishi wa makala za uchambuzi katika gazeti la Msimbazi Moja kati ya logo za MSTV Mtendaji mkuu wa Mambo Uwanjani Blogspot, Prince Hoza, wameanzisha Tv yao

Kaseke naye atua Singida United

Picha
Na Paskal Beatus. Dar es Salaam Timu ya Singida United inayonolewa na kocha wa zamani wa Yanga SC, Mholanzi, Hans Van der Pluijm, jana imekamilisha kandarasi ya winga wa Yanga, Deus Kaseke kwa kipindi cha miaka miwili. Kaseke amekubali kutua kwenye timu hiyo iliyojaza nyota lukuki wa Afrika mashariki, Kaseke anakuwa mchezaji wa nne kuondoka katika kikosi cha Yanga ndani ya wiki moja baada ya Simon Msuva aliyetua Difaa Hassan El Jajida, Deo Munishi "Dida" aliyekwenda Afrika Kusini na Ally Mustapha 'Barthez' aliyejiunga na Singida United. Kuondoka kwa Kaseke ndani ya Yanga kunaleta wasiwasi mkubwa kwenye kikosi hicho kwani mchezaji huyo aliisaidia Yanga kutwaa ubingwa mara mbili mfululizo, akiwa kwenye ubora wake Kaseke aliiwezesha pia Mbeya City kutikisa soka la Tanzania Deus Kaseke (Kulia) akitambulishwa kujiunga na Singida United

Stars na Amavubi ni kusuka au kunyoa

Picha
Na David Pasko. Rwanda Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars jioni ya leo inatelemka katika dimba la Nyamirambo Stadium mjini Kigali, Rwanda kurudiana na wenyeji Timu ya taifa ya Rwanda, Amavubi. Mchezo huo wa marudiano kufuzu fainali za mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza Ligi za nyumbani, maarufu Chan, timu hizo zilikutana Jumamosi iliyopita katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na kutoka sare ya kufungana bao 1-1. Goli la ugenini linaonekana kuipa nguvu Rwanda, kupitia kwa kocha wake mkuu, Antoine Hey kwamba wanamaliza tu kwani ushindi walishaupata Mwanza, lakini kocha wa Taifa Stars, Salum Mayanga amesema vijana wake hawatamwangusha na wataipeperusha vema bendera ya Tanzania. Nahodha wa Tanzania, Himid Mao ambaye ndiye mfungaji wa goli la kusawazisha kwa mkwaju wa penalti ametamba kuwa Stars itavuka hatua inayofuatia, mchezo huo unaanza saa 9:30 kwa saa za Rwanda na mshindi wa hapo atacheza na Uganda au Sudan Kusini Taifa Stars

Kisa Malinzi, Zanzibar yaporwa uanachama Caf

Picha
Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam Shirikisho la kandanda Barani Afrika, (CAF) limeipoka uanachama Zanzibar na bado haijafahamika kipi kilichopelekea Shirikisho hilo kuipoka uanachama. Taarifa za Zanzibar kuporwa uanachama wake zimewashangaza wengi lakini chanzo kimoja cha habari kinasema Rais wa Shirikisho la kandanda nchini, (TFF) Jamal Malinzi amehusika. Inasemekana Caf imeipoka uanachama Caf ambayo majuzi tu ikiwapa uanachama kamili ambao ungeifanya timu ya taifa ya Zanzibar kuweza kushiriki michuano ya mataifa barani Afrika, lakini sasa haitaweza kushiriki tena. Inasemekana rais mpya wa Caf na kamati yake wameona ni bora kuipoka uanachama Zanzibar kwavile Jamal Malinzi alikuwa akimuunga mkono Issa Hayatou Zanzibar imepokwa uanachama

Milioni 300 zamng' oa Msuva Yanga

Picha
Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam Klabu ya Difaa El Hassan Jajida ya Morocco itailipa Yanga SC karibu Dola 150,000 ambazo ni sawa na shilingi Milioni 300 za Kitanzania ili kumnyakua kiungo mshambuliaji mwenye kasi ya ajabu, Simon Msuva. Mipango ya kumng'oa Msuva ilianza tangu kumalizika kwa msimu uliopita na jamaa walianza kumfukuzia hadi timu ya taifa ilipokuwa Afrika Kusini kushiriki michuano ya kombe la Cosafa Castle Cup. Msuva jana alishindwa kuondoka na wachezaji wenzake wa timu ya taifa ambapo ilielekea nchini Rwanda kwa ajili ya kurudiana na timu ya taifa ya nchi hiyo mchezo wa mataifa ya Afrika maarufu Chan na alikuwa akiangaikia taratibu za kusafiri. Kwa maana hiyo Msuva anaungana na Mtanzania mwenzake Ramadhan Singano "Messi" ambaye tayari ameshajiunga na timu hiyo ya Ligi Kuu, kwa sasa kinachongojewa kwa Msuva ni kipimo cha afya yake Simon Msuva, ameuzwa na Yanga

GOR MAHIA YAITAKA SIMBA,SIMBA DAY

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Kocha mkuu wa timu ya Gor Mahia ya Kenya, Dylan Kerr amesema angependa kama klabu yake ya zamani ya Simba SC itawaalika kuja kucheza nao katika tamasha la Simba Day hapo Agosti 8 mwaka huu. Kerr aliyasema hayo hivi karibuni wakati timu yake ya Gor Mahia ilipokuwa hapa nchini ambapo pia ilicheza mchezo wa kirafiki na timu ya Everton ya Uingereza. Kocha huyo amewahi kuifundisha Simba SC lakini baadaye akaondolewa kwenye kikosi hicho hasa baada ya timu kufanya vibaya, hata hivyo Kerr amedai angefurahi kama Simba itacheza na Gor Mahia ili awaonyeshe kitu na wajutie kumuacha Dylan Kerr, kocha wa Gor Mahia

Mdogo wake Yahaya Akilimali asaini Yanga

Picha
Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam Mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga SC, jana imemsainisha kiungo mshambuliaji Baruan Akilimali ambaye ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Yahaya Akilimali. Kiungo huyo ilikuwa atue Lipuli ya Iringa, lakini mabingwa hao wa Bara wamemua kumpa mkataba wa miaka miwili kuichezea timu hiyo ambayo tayari imeshaondokewa na winga wake Simon Msuva. Akilimali anatajwa mmoja kati ya mawinga wenye mbio ambapo mashabiki wa soka wamempachika jina la Kiberenge ambacho kinasemekana kinakimbia kuliko gari Baruani Akilimali akisaini mkataba wa kujiunga na Yanga

Mtibwa Sugar yamrejesha Kado

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam. Timu ya Mtibwa Sugar imefanikiwa kumrejesha mlinda mlango wake wa zamani, Shaaban Kado ambaye alikuwa anaichezea Mwadui FC ya Shinyanga. Kocha wa timu hiyo Zuberi Katwila amesema baada ya kuondokewa na kipa wao chaguo la kwanza, Said Mohamed Nduda ambaye amesaini mkataba wa miaka miwili, alimpendekeza Kado. Uongozi wa Mtibwa Sugar umeona ni bora umrejeshe Kado ambaye alikuwepo hapo kabla hajaenda kujiunga na Yanga SC, Kado ameamua kurejea kwani hadi sasa Mtibwa imemnyakua mlinzi wa Mwadui, Salum Kanoni, Kado amesaini mkataba wa miaka miwili Shaaban Kado anarejea Mtibwa Sugar Kado akisaini mkataba mbele ya mratibu wa timu hiyo, Jamal Bayser

Safari ya Msuva Morocco imeiva

Picha
Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam. Baada ya jana kuwaaga Wanayanga, kiungo Simon Msuva anatarajia kuondoka nchini kuelekea Morocco kujiunga na klabu ya Difaa El Jajida inayoshiriki Ligi Kuu. Awali Msuva ilikuwa akajiunge na klabu moja ya nchini Afrika Kusini, lakini Waarabu hao wa Morocco wamemfuata hadi Afrika Kusini alikokuwa na timu ya taifa iliyokuwa inashiriki michuano ya Cosafa Castle Cup. Hata hivyo Msuva anayekwenda kujiunga na timu hiyo ambayo tayari imemnasa Mtanzania mwingine, Ramadhan Singano "Messi" ambaye alikuwa anaichezea Azam FC, malengo yake ni kwenda kucheza Ureno au Hispania. Msuva jana ilikuwa aambatane na timu ya taifa, Taifa Stars iliyokwenda Rwanda kurudiana nao Jumamosi ijayo lakini safari yake ikaishia Uwanja wa ndege wa Mwl Nyerere jijini Dar es Salaam baada ya kutakiwa haraka na Waarabu hao hivyo sasa anashughurikia safari yake Simon Msuva, anaondoka Yanga

KABURU HOI MAHABUSU, AVEVA AJITOKEZA KISUTU

Picha
Na Prince Hoza. Dar es Salaam Makamu wa Rais wa klabu ya Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' yuko hoi mahututi na amelazwa katika hospitali ya Keko inayomilikiwa na gereza la Keko ambako yeye na mwenzake Evans Aveva wanashikiliwa. Kaburu leo hakutokea mahakamani ambako wamehitajika kwa ajili ya kusikiliza shauri lililo mbele yao likihusu utakatishaji fedha, Rais wa klabu hiyo Evans Aveva alijitokeza mahakamani hapo ila Kaburu hakutokea. Wawili hao sasa wataendelea kusota rumande hadi Julai 31 watakaudhuria tena katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambako ndiko inakosomwa kesi yao, wawili hao walikamatwa tangu Juni 29 mwaka huu wakituhumiwa kwa makosa matano Evans Aveva ametokea mahakamani Kisutu leo, lakini mwenzake Kaburu hakutokea

Msuva aitosa Yanga, atua Mbao FC

Picha
Na Ikram Khamees. Dar es Salaam Kiungo James Happygod Msuva amejiunga na Mbao FC ya Mwanza baada ya kuachana na Yanga SC aliyoitumikia kwa vipindi kadhaa. James ni mdogo wa winga wa Yanga na Taifa Stars, Simon Msuva ambaye kwa sasa yupo kwenye ubora wake. Kiungo huyo amejiunga na Mbao na msimu ujao ataitumikia timu hiyo, awali Msuva aliwahi kuzichezea Simba SC na Azam zote zikiwa timu za vijana James Msuva, ameihama Yanga James (Kushoto, akiwa na kaka yake, Simon, wote hao wameihama Yanga