Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2016

AZAM YAZIFUATA SIMBA NA YANGA ROBO FAINALI FA CUP

Picha
Na Mrisho Hassan, Moshi Mabingwa wa Afrika mashariki na kati Azam Fc jioni ya leo imefanikiwa kutinga robo fainali ya michuano ya Azam Federation Cup ama kombe la FA baada ya kuilaza FC Panone ya Kilimanjaro mabao 2-1 uwanja wa Ushirika Moshi. Vijana wa Panone wanaonolewa na kocha wa zamani wa Yanga na JLT Ruvu walikuwa wa kwanza kujipatia bao la kuongoza lililofungwa na Geofrey Mbuda aliyetumia vema makosa ya beki wa Azam Paschal Wawa. Azam nao walisawazisha bao hilo kupitia kwa beki wake Paschal Wawa aliyerekebisha makosa yake, Azam walingeza bao la pili na la ushindi lililofungwa na mshambuliaji Alan Wanga. Kwa matokeo hayo Azam imeingia robo fainali ya michuano hiyo hivyo inaingana na Simba, Yanga, Mwadui, Coastal Union, Geita Gold, Ndanda na Prisons

A,ZAM FC YAZIFUATA SIMBA, YANGA ROBO FAINALI YA FA

Picha
Na Mrisho Hassan, Moshi Mabingwa wa Afrika mashariki na kati Azam Fc jioni ya leo imefanikiwa kutinga robo fainali ya kombe la FA baada ya kuichapa Panone Fc ya Kilimanjaro katika uwanja wa Ushirika Moshi. Wenyeji Panone wanaonolewa na Fred Felix Mjnziro ndio walikuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza lililofungwa na Geofrey Mbuda. Goli hilo lilitokana na makosa ya mabeki wa Azam ambao walishindwa kuuokoa mpira ulioelekezwa langoni mwao. Beki Paschal Wawa ambaye alihusika katika makosa ya kuruhusu bao, alisawazisha makosa yake na kuipatia Azam bao la kusawazisha kabla ya mshambuliaji Mkenya Alan Wakende Wanga kuongeza bao la pili. Kwa matokeo hayo Azam imetinga robo fainali ya michuano hiyo inayofahamika kama Azam Federation Cup, kwa maana hiyo Azam inaungana na miamba ya soka nchini Simba na Yanga kucheza hatua hiyo. Timu nyingine zilizofuzu ni Coastal Union ya Tanga, Ndanda ya Mtwata, Mwadui ya Shinyanga, Geita Gold ya Geita na Prisons ya Mbeya

YANGA YAIENDEA AZAM FC PEMBA

Picha
Na Ikram Khamees, Pemba Vinara wa ligi kuu bara Yanga Sc inatarajia kuwasili visiwani Pemba tayari kabisa kujiandaa na mchezo wake wa ligi jumamosi ijayo uwanja wa Taifa Dar es Salaam dhidi ya waoka mikate wa Azam Fc. Yanga imeamua kuijia Azam Pemba ni kutokana na ushndani wake unapokuwa mkubwa hivyo imeamua kuijia Pemba kama ilivyofanya hivyo dhidi ya Simba Sc. Yanga iliijia Simba Pemba na ikafanikiwa kuichapa mabao 2-0 uwanja wa Taifa Dar es Salaam mchezo wa ligi kuu bara. Vinara hao wa ligi kuu ndio mabingwa watetezi wa ligi hiyo na safari hii inataka kuhakikisha inachukua tena ubingwa, Akizungumza jana na blogu hii msemaji wavYanga Jerry Muro amesema Yanga itaweka kambi yake Pemba ili kujiandaa na Azam. Muro amedai Pemba ni sehemu tulivu hivyo panafaa kwa kambi, ameongeza Azam inawakamia sana hasa wanapokutana nao lakini safari ya Pemba itakuwa mwisho wao. Amedai kikosi chao lazima kiibuke na ushindi katika mchezo huo ili iendelee kuongoza ligi kwa uwiano wa pointi, kwa sasa

MAONI: KUNA SIKU BONDIA ATAKAYETANGAZWA MSHINDI ATAPELEKWA NA AMBULANCE MUHIMBILI

Picha
Na Prince Hoza Kwanza nianze kwa kutoa salamu zangu za pongezi kwa bondia Fransis Cheka hasa baada ya kutwaa ubingwa wa WBF juzi usiku katika ukumbi wa Leaders Club. Ushindi wa Cheka ni furaha kwa Watanzania kwani alikuwa akipeperusha bendera ya nchi, lakini ushindi wake umetawaliwa na hujuma za hapa na pale kwani sikuona ngumi za ufundi. Cheka ni Mtanzania mwenzangu lakini sioni umuhimu wowote kusifu pale ninapoona kuna makosa ya kiufundi. Bondia aliyepambana na Cheka alionekana kuimarika zaidi huku akirusha makonde yenye nguvu yaliyokuwa yakimtetemesha Cheka na kuna wakati alikuwa akianguka. Licha kwamba alionyesha ushujaa mkubwa kwa kutokubali kupigwa kwa Nock Out lakini alielemewa muda wote na kumfanya mpinzani wake aendelee kumkalia karibu. Cheka alikuwa akipokea masumbwi ya usoni lakini Cheka alishindwa kundunda mpinzani wake usoni na ngumi zake nyingi ziliishia mikononi kwa mzungu huyo raia wa Serbia. Mwamuzi wa mchezo huo alimtangaza Fransis Cheka mshindi wa pambano hilo

SAMATTA ATUPIA BAO LAKE LA KWANZA UBELGIJI

Picha
Na Mwandishi Wetu Mtanzania Mbwana Samatta leo amefungua akaunti yake ya mabao baada ya kuifungia bao la ushindi timu yake mpya ya KRC Genk inayoshiriki ligi kuu Ubelgiji. Mbwana Samatta aliyejiunga na timu hiyo hivi karibuni akitokea TP Mazembe ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo, alifunga bao hilo kunako dakika ya 81 zikiwa ni dakika mbili tu tangia aingie akitokea benchi. Samatta ameiwezesha timu yake hiyo kushinda 3-2 na kuondoka na pointi tatu muhimu katika ligi kuu ya Ubelgiji Hilo ndiyo goli lake la kwanza tangu alipojiunga na timu hiyo, Samatta alikuwa mfungaji bora na pia mchezaji bora wa Afrika, tuzo aliyoshinda mwishoni mwa mwaka jana

KAPOMBE AWA MCHEZAJI BORA JANUARI

Picha
Beki wa pembeni wa Azam Fc Shomari Kapombe ametangazwa mchezaji bora wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara kwa mwezi Januari. Kapombe ameshinda tuzo hiyo baada ya kuwashinda nyota wawili Jeremiah Juma Mgunda wa Prisons ya Mbeya na Miraji Adam Seleman wa Coastal Union. Kwa maana hiyo Kapombe mchezaji wa zamani wa Polisi Morogoro na Simba Sc atajinyakulia kitita xha shilingi milioni moja. Kapombe ambaye anacheza nafasi ya ulinzi wa pembeni, pia anamudu kucheza kiungo, kilichopelekea kuibuka mchezaji bora wa mwezi Januari kwamba aliitumikia ipasavyo Azam na kucheza karibu mechi zote tatu na kufunga magoli mawili

SIMBA YAINYANYASA SINGIDA UNITED

Picha
Na Ikram Khamees Simba Sc jioni ya leo imevuka hatua ya robo fainali michuano ya kombe la TFF baada ya kuilaza Singida United mabao 5-1 uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Wekundu hao wa Msimbazi walipata mabao kupitia kwa Awadh Juma "Maniche" na Hamisi Kiiza "Diego" ambao wote wamefunga mawili kila mmoja na lingine limefungwa na Danny Lyanga. Kwa matokeo hayo Simba imetinga robo fainali ikiungana na mtani wake Yanga Sc ambayo jumamosi iliyopita iliwalaza mabao 2-0. GeitavGold Fc nayo imetinga robo fainali ya michuano hiyo baada ya kuilaza Toto Africans ya Mwanza bao 1-0 uwanja wa CCM Kirumba Mwanza. Baada ya ushindi wa mechi ya leo, Simba inajiandaa na mchezo wake wa ligi kuu bara dhidi ya Mbeya City jumamosi

PRISONS YAISHIKISHA ADABU MBEYA CITY

Picha
Na Alex Jonas, Mbeya Tanzania Prisons jioni ya leo katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya imewaadhibu mahasimu wao Mbeya City mabao 2-0 na kutinga hatua ya robo fainali ya kombe la FA. Mabao ya Mohamed Mkopi na kipa Benno Kakolanya yalitosha kabisa kuwapa uahindi maafande hao, goli la kwanza la Prisons lilifungwa kipindi cha kwanza na la pilj lilifungwa kipindi cha pili. Licha ya Mbeya City kujitutumua angalau kusawazisha lakini ilishindikana kwani vijana wa Prisons walikuwa imara, goli la kufutia machozi la Mbeya City lilifungwa na Joseph Mahundi. Hata hivyo goli lililofungwa na kipa wa Prisons Benno Kakolanya limeingia katika rekodi ya aina yake, Kakolanya anakuwa kipa wa tatu kufunga. Iddi Pazzi 'Father' na Juma Kaseja ndio makipa pekee waliofanikiwa kufunga, Pazzi alifunga mwaka 1984 alipokuwa anaidakia Simba na Kaseja alifunga mwaka 2013 alipokuwa Yanga Sc

YANGA YATINGA RAUNDI YA KWANZA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

Picha
Na Prince Hoza Wawakilishi wa Tanzania Yanga Sc jioni ya leo imefuzu raundi ya kwanza ya ligi ya mabingwa barani Afrika baada ya kuilaza Cercle de Joachim ya Mauritius mabao 2-0 uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Licha ya mchezo huo kutokuwa wa ushindani mkubwa, lakini vijana wa Yanga walicheza kandanda safi na la kuvutia. Mabao yaliyopatikana dakika ya tatu kipindi cha kwanza na dakika 12 kipindi cha pili yaliyofungwa na Amissi Joselyin Tambwe raia wa Burundi na Thabani Scara Kamusoko raia wa Zimbabwe yalitosha kabisa kuwapeleka Yanga raundi ya kwanza. Kwa maana hiyo Yanga itakutana na APR ya Rwanda au Mbabane Swallors ya Swaziland, ushindi ilioupata leo unaifanya Yanga iwaondoe mashindanoni Cercle de Joachim kwa jumla ya mabao 3-0 baada ya ushindi wa ugenini wa bao 1-0. Yanga sasa itarejea kwenye ligi kuu bara jumatano itakaoikaribisha Mtibwa Sugar uwanja wa Taifa Dar es Salaam na jumamosi ijayo itavaana na Azam Fc

STAA WETU: THABANI SCARA KAMUSOKO: KIUNGO MSHAMBULIAJI MWENYE VITU ADIMU

Picha
Na Salum Fikiri Jr YANGA SC imebahatika kupata mchezaji wa kulipwa mwenye hadhi ya kuitwa 'Proffesional', si mwingine ni Thabani Scara Kamusoko. Jamaa huyu tayari ana tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Desemba 2015 ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara, TFF iliamua kumpa tuzo hiyo baada ya kuonyesha kiwango kikubwa na kuisaidia timu yake kukamata usukani wa ligi. Yanga ndiyo vinara wa ligi kuu bara na leo jioni inacheza mchezo wa marudiano ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Cercle de Joachim ya Mauritius. Kamusoko ametishia kiwango cha kiungo mwenzake Haruna Niyonzima raia wa Rwanda, katika kikosi cha kwanza cha Yanga chini ya kocha wake Mholanzi Hans Van der Pluijm, Kamusoko amekuwa akianzia katikati huku Niyonzima akitupwa pembeni ama benchi. Licha ya kukosekana katika mchezo wa kwanza dhidi ya Cercle de Joachim na Yanga kushinda 1-0 ugenini, leo ataonekana uwanjani na kuwaonyesha maujuzi yake. Kamusoko anasifika kwa uchezaji wake na pia amekuwa mfungaji mzuri, mpaka sa

YANGA LEO NI MWENDO WA KUJIPIGIA TU

Picha
Na Saida Salum Mabingwa wa soka nchini Yanga Sc jioni ya leo inajitupa uwanja wa Taifa Dar es salaam kukabiliana vikali na Cercle de Joachim ya Mauritius mchezo wa marudiano ligi ya mabingwa barani Afrika. Yanga inaingia uwanjani ikiwa na faida ya goli moja ililolipata mjini Curepipe ilipocheza mchezo wa kwanza. Donald Ngoma mfungaji wa goli hilo pekee atakosekana katika mchezo huo baada ya majuzi kusafiri kuelekea Zimbabwe ambapo mdogo wake alifariki uwanjani. Ngoma mchezaji tegemeo wa Yanga kwani ndiye aliyeipa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya mtani wao Simba Sc uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Yanga itajivunia mgambuliaji wake Amissi Tambwe na Malimi Busungu wakisaidiwa na viungo Simon Msuva, Geofrey Mwashiuya na Deus Kaseke. Lakini pia inapaswa kuwachunga sana Cercle de Joachim kwani si timu ya kubeza, endapo Yanga itasonga mbele itaingia raundi ya kwanza na huenda ikakutana na APR ya Rwanda au Mbabane Swallons ya Swaziland

GIANNY INFONTINO RAIS MPYA FIFA

Picha
Na Mwandishi Wetu Shirikisho la kandanda duniani FIFA leo limempata rais wake mpya atakayerithi nafasi ya Seppt Blatter ambaye ameenguliwa baada ya kuhusishwa na ufisadi mkubwa uliozingira taasisi hiyo kubwa ya soka duniani. Gianny Infontino ndiye aliyetawazwa kuwa bosi mpya wa shirikisho hilo baada ya kumshinda Al Salman, Infontino alipata kura 115 akimzidi kura 27 mpinzani wake huyo aliyekuwa akiungwa mkono na bara la Afrika. Infontino alikuwa katibu mkuu wa shirikisho la soka barani ulaya (UEFA) na anakuwa rais wa tisa wa FIFA baada ya Blatter aliyedumu kwa miaka 18

KASSIM MAPILI KUZIKWA IJUMAA, KUMBE ALIKUFA KWA PRESHA, BARCELONA YAHUSISHWA

Picha
Na Mwandishi Wetu Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi nchini Kassim Mapili amwfariki dunia jumanne iliyopita kwa maradhi ya shinikizo la damu. Kwa mujibu wa mkwe wa marehemu, Wema Mustafa Mgombelwa 'Baba wawili' amesema shughuri za mazishi ya marehemu mzee Kassim Mapili zinafanyika Magomeni Mapipa mtaa wa Magomeni namba 21. Wema alisema wanaweza kumzika katika makaburi ya Mwinyimkuu au Kisutu jijini Dar es Salaam (leo Ijumaa). Mkwe huyi ambaye ni seneta wa bendi ya Msondo Ngoma alisema mkwe wake alifariki jumanne usiku baada ya kutoka kuangalia mchezo wa mpira wa miguu kati ya Arsenal na Barcelona. "Kikubwa alikuwa akisumbuliwa na presha kwa muda mrefu, alifariki usiku na maiti tuliipeleka Muhimbili baada ya kupata taarifa za msiba huo, tunawaomba ndugu jamaa na marafiki kujumuika pamoja katika mazishi ya mzee wetu", alisema Wema. Marehemu Kassim Mapili alijipatia umaarufu mkubwa enzi zake akikung' uta gitaa la solo, pia alikuwa mwimbaji mahiri, Mungu ailaze

MICHANO: RITTA PAULSEN WA (BSS) NAYE NI JIPU

Picha
Na Mkola Man, Mwanatanga Yap yap yap leo michano yangu inaichana Bongo Star Search (BSS) hasa mkurugenzi wa kampuni ya Benchmark Production inayoandaa shindano hilo la BSS, Ritta Paulsen  au Madame Ritta. Mimi hapa (Mkola Man) namfananisha Madame Ritta na mkulima ambaye anapanda michungwa isiyozaa machungwa, kutokana na kutoipalilia toka mwaka 2007 Jumanne Idd, 2008 Misoji Nkwabi, 2009 Paschal Cassian, 2010 Mariam Mohamed,, 2011 Hajji Ramadhan, 2012 Waltel Chilambo, 2013 Emmanuel Msuya na mwaka 2014 hayakufanyika. Shindano hilo likarudi tena mwaka jana 2015 na akashinda Kayumba Juma, mchungwa huu unaanza kutoa maua hasa baada ya kufyekewa na kukutwa na mvua. Hii yote imetokana na uwepo wa Mkubwa Fella na Babu Tale, je mashindano ya huko nyuma yalikuwa na dhamila ya kweli ya kuinua vipaji au dhamila ya upigaji?. Ritta Paulsen kwa BSS yako umeshatuweka njia panda, hujawasaidia kidhati washindi, zipo BSS nyingi duniani ikiwemo ile ya American Star Search ambayo ilimtoa kimuziki mshindi

CHIFU PANDUKA NA TEGO LA NYOKA

Picha
Na Juma Mwema Watu wengi wanaamini mbwa ndiye mlinzi tosha wa mali zao nyumbani, lakini Chifu Panduka anatumia tego lake la nyoka. Kwa wale wanaochimba madini Merelani, kwa wale wanaowachunga wake zao na kwa wale wanaotaka kuweka mazindiko kwenye nyumba zao, basi fika kwa Chifu Panduka. Chifu Panduka alijipatia umaarufu mkubwa katika nchi za Uajemi na Uhindi kwa tego hilo la nyoka. Mali nyingi zinapotea katika mazingira ya kutatanisha, lakini tego la nyoka linaweza kunusuru mali zako na maisha yako. Fika ofisini kwake Tabata Relini jirani kabisa na Hai Bar ama waweza kumpigia simu nambari 0715281162

NGOMA ATIMKA YANGA, KUIKOSA CERCLE DE JOACHIM JUMAMOSI

Picha
Na Ikram Khamees Mshambuliaji wa kutumainiwa wa mabingwa wa soka nchini Yanga, Donald Dombo Ngoma ataikosa mechi ya kimataifa dhidi ya Cercle de Joachim ya Mauritius uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Yanga zinasema kuwa mchezaji huyo ataikosa mechi hiyo ya marudiano ligi ya mabingwa barani Afrika baada ya kufiwa na mdogo wake. Ngoma amefiwa na mdogo wake jana nchini Zimbabwe akiwa uwanjani aligongana na mchezaji mwenzake na kufariki dunia, Ngoma anayekipiga Yanga ndiye baba wa familia hivyo amelazimika kusafiri kuudhuria mazishi ya mdogo wake. Ngoma mfungaji pekee wa bao la kwanza Yanga ikiifunga Cercle de Joachim 1-0 katika uwanja wa Curepipe huko Mauritius, kukosekana kwa Ngoma ni pigo kubwa kwani mshambuliaji huyo yuko katika kiwango cha juu mno ambapo jumamosi iliyopita aliitungua Simba uwanja wa Taifa, Yanga ikishinda 2-0. Tayari mchezaji huyo ameshasafiri kuelekea Zimbabwe, Wakati huo huo wapinzani wa Yanga katika michuano ya ligi ya mabing

RACHEL BITHULO NDANI YA TUZO ZA NYAMBAGO

Picha
Na Prince Hoza Mwigizaji chipukizi wa filamu nchini Bongo Muvi, Rachel Bithulo "Recho" kesho atakuwa ndani ya tuzo za Nyambago zinazotarajia kufanyika mjini Dodoma. Akizungumza na blogu hii, Recho amesema amefanikiwa kuingia kwenye tuzo hizo kama mwigizaji bora wa kanda ya kati. Amewataka wapenzi wake na mashabiki kuendelea kumpigia kura ili aibuke kidedea, msanii huyo ambaye pia ni Video Queen wa muziki wa bongofleva, alifanya vizuri kwenye wimbo wa "Yuleyule' wa msanii PNC. Recho ameigiza vizuri katika filamu ya Craritta ambayo imemfanya aingie kwenye tuzo hizo, "Malengo yangu ni kuchukua tuzo, naomba sapoti zenu wadau kwani ushindi wangu ni wetu sote" alisema msanii huyo mwenye asili ya Usukumani

"KIKWETE ALINIPA MILIONI 18 YA KUNUNULIA KIWANJA"- MPOTO

Picha
Na Prince Hoza Msanii wa nyimbo za asili Mrisho Mpoto "Mpoto" amefichua uswahiba wake na aliyekuwa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk Jakaya Kikwete kuwa aliwahi kuzawadiwa shilingi milioni 18 ili anunue kiwanja. Akizu gumza hivi karibuni, Mpoto amesema, Kikwete alikuwa mpenzi mkubwa wa kazi zake hasa baada ya kurekodi wimbo wake wa "Mjomba" ambao baadaye ulimkutanisha na rais Kikwete, akisema. "Kikwete kupitia msaidizi wake Januari Makamba wakiniita na kudai wimbo wa Mjomba ulimlenga moja kwa mjomba JK, hata hivyo Makamba alisifu mashairi yangu na kuniambia kitu kuwa mheshimiwa rais wakati huo alifurahishwa nao", aliongeza. "Nilipokutana naye nchini Ufaransa, Kikwete aliahidi kunipatia shilingi milioni 18 huku akidai ni shabiki wa muziki wangu, niluporudi Tanzania, nilienda Ikulu ambapo walinipa fedha hizo", alifichua mwanamuziki huyo anayemsifu Kikwete kwa kusaidia maendeleo ya sanaa nchini

KAMUSOKO AWATUMBUA JIPU JKT MLALE, SASA WATINGA ROBO FAINALI

Picha
Na Mrisho Hassan Mabingwa wa soka nchini na vinara wa ligi kuu bara Yanga Sc jioni ya leo imewatumbua jipu wanajeshi wa JKT Mlale ya Ruvuma baada ya kuwachapa mabao 2-1 uwanja wa Taifa Dar es Salaam mchezo wa kombe la FA. Yanga moja kwa moja imesonga hadi robo fainali ya michuano hiyo na imekuwa timu ya kwanza kufanya hivyo. Huu ni ushindi wa pili mfululizo hasa baada ya wikiendi iliyopita kuichapa Simba Sc mabao 2-0 mchezo wa ligi kuu bara katika uwanja huo huo wa Taifa. Yanga ambayo jumamosi ijayo itashuka uwanja wa Taifa kuvaana na Cercle de Joachim ya Mauritius mchezo wa marudiano wa ligi ya mabingwa barani Afrika, iliutumia mchezo wa leo kama maandalizi. Vijana wa JKT Mlale walikuwa wa kwanza kupata bao lakini Geofrey Mwashiuya kama alivyofanya kwenye mchezo dhidi ya Simba ambapo alipiga krosi murua ikiyotua kwenye mguu wa Amissi Tambwe, leo alifanya hivyo na kumkuta Paul Nonga na kuisawazisbia Yanga. Thabani Kamusoko raia wa Zimbabwe alitumia vema krosi ya Mwashiuya na kuip

PRISONS YAISHIKA MBAYA AZAM FC

Picha
Na Saida Salum  Mbeya Wajelajela Prisons jioni ya leo katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya imeilazimisha sare ya 0-0 Azam Fc mchezo wa ligi kuu bara. Azam Fc ikiwa na washambuliaji wake mahiri John Raphael Bocco, Kipre Herman Tchetche na kiungo wake Abubakar Salum lakini walishindwa kupenya ukuta wa vijana hao walioongozwa na beki Nurdin Chona. Prisons ambao wako katika kiwango cha juu msimu huu mara kwa mara walijaribu kulifikia lango la Azam kutaka kufunga lakini ngome ya waoka mikate hao iliyokuwa ikiongozwa na Paskal Wawa. Kwa matokeo hayo Azam imefikisha pointi 46 na imeshindwa kuitoa Yanga kileleni hivyo itasalia katika nafasi yake ileile ya pili

MALINZI ATAKIWA KUJIUZURU

Picha
Na Prince Hoza Wadau wa michezo nchini wamemtaka rais wa shirikisho la kandanda nchini TFF Jamal Malinzi ajiuzuru nafasi hiyo kutokana na kashfa ya upangaji matokeo ligi Daraja la kwanza Tanzania bara (FDL). Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wadau hao wamesema, Malinzi amekuwa mstari wa mbele kutetea maovu yanayofanywa na watendaji wake ikiwemo suala la kuiruhusu Azam Fc kwenda Zambia kushiriki bonanza. Rais huyo wa TFF aliomba radhi kwa kitendo hicho kwani wakati Azam inaondoka nchini, ilitakiwa kucheza mechi zake mbili za ligi, Malinzi anatakiwa kujiuzuru ili kulinda heshima yake. Bosi huyo wa TFF anatajwa kuhusika na upangaji wa matokeo uliozikuta timu za Geita Gold Fc na Polisi Tabora, timu hizo kila moja ilipata ushindi wa kushangaza. Geita Gold Fc iliifunga JKT Kanembwa ya Kigoma mabao 8-0, wakati Polisi Tabora nayo ikaichapa JKT Oljoro mabao 7-0

BOSSOU- BADO TCHETCHE

Picha
Na Alex Jonas Mlinzi wa kati wa Yanga Vincent Bossou raia wa Togo ambaye jumamosi iliyopita alimdhibiti vilivyo mshambuliaji wa Simba Hamisi Kiiza katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam wakati miamba Simba na Yanga ilipokutana. Beki huyo wa kati aliyecheza kistadi na kumzuia kabisa kinara huyo wa mabao ligi kuu bara wakati timu yake ikiibuka na ushindi wa mabao 2-0 yaliyofungwa na Donald Ngoma raia wa Zimbabwe na Amissi Tambwe wa Burundi. Bossou ambaye aliwahi kufanya mazungumzo na blogu hii kule Pemba ambapo alidai ni kazi ndogo sana kumdhibiti mshambuliaji wa Simba Hamisi Kiiza kwani aliweza kumkaba Didier Drogba wa Ivory Coast. Hata hivyo Bossou aliweza kumkaba Kiiza mpaka alipotolewa na kumpisha mchezaji mwingine baada ya kuchemsha, sikia anachosema Bossou. Beki huyo mrefu mwenye nguvu ametamka maneno mengine ambayo kama yatasikilizwa na Kipre Tchetche basi anaweza akachukia, Bossou amedai anamtamani sana Tchetche na amesisitiza watakapokutana hivi punde atamjua yeye ni nani

NEY WA MITEGO AMPA SHAVU LA NGUVU RAY

Picha
Na Shafii Hoza Msanii maarufu wa filamu Bongo Movie Vincent Kigosi "Ray" anatarajia kuanzisha kampeni itakayomwezesha kupiga mkwanja wa nguvu. Akizungumza hivi karibuni, Ray amesema anatarajia kuanzisha kampeni ya nguvu ya kuwahamasisha watu kunywa maji kwa wingi ili kuimarisha afya zao ikiwemo kuimarisha ngozi zao. Ray ametajwa kwenye wimbo wa msanii Ney wa Mitego kuwa anatumia fedha nyingi kwa ajili ya kujiremba na kununua mkorogo ili awe mweupe. Pia msanii huyo ambaye wimbo wake uitwao "Shika adabu yako" unefungiwa na BASATA, Ray ametajwa tena kwenye wimbo huo ikiwa bado anaishi kwa wazazi licha kwamba ni mkubwa. Hata hivyo baada ya kuhit kwa wimbo huo, msanii Ray aliibuka na kukanusha vikali kuwa yeye hatumii mkorogo isiokuwa anakunywa sana maji na kufanya mazoezi. Pia akadai anaendelea kuishi kwa wazazi kwa sababu mama yake hataki ahame, tangia Ray alipotoa majibu hayo, tayari watu wengi wameokana kufurahia majibu yake na wengi wakionekana wanakunywa maji kwa

AZAM FC NA PRISONS, NGOMA INOGILE

Picha
Na Saida Salum, Mbeya Kesho ndiyo kesho katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya wakati wenyeji Tanzania Prisons watakapoikaribisha Azam Fc mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara. Azam Fc wataingia uwanjani kwa lengo la kutwaa pointi zote tatu ili ikamate usukani wa ligi kuu bara, kikosi cha Azam kina kumbukumbu nzuri kwani jumamosi iliyopita iliifunga Mbeya City mabao 3-0 katika uwanja huo huo wa Sokoine. Akizungumza na blogu hii jana, msemaji wa Azam Jaffari Idd amesema timu yake lazima ipate ushindi kwakuwa vijana wake wako vizuri. Azam itamkosa kiungo wake mahiri Himid Mao mwenye kadi tatu za manjano, nao vijana wa Prisons wamejinasibu kuondoka na ushindi katika mchezo huo. Vijana hao wa jeshi la Magereza, wamesema Azam ni timu ya kawaida kama nyingine walizowahi kukutana nazo hivyo wategemee kipigo kutoka kwao, Prisons wana kumbukumbu ya kuizuia Yanga baada ya kuilazimisha sare ya mabao 2-2 katika uwanja huo huo wa Sokoine

MAONI: SIMBA IACHE VISINGIZIO, IKUBALI ILIZIDIWA MBINU NA YANGA

Picha
Na Prince Hoza Simba Sc juzi jumamosi ilikubali kichapo cha mabao 2-0 toka kwa mahasimu wao Yanga Sc katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam mchezo wa ligi kuu bara. Jumla Simba imefungwa na Yanga mara mbili ndani ya msimu huu, kuelekea katika mchezo huo, timu zote zilijiandaa vema. Simba ndiyo iliyokuwa katika morali ya hali ya juu kwani ilikuwa ikifanya vizuri katika mechi, ushindi mfululizo ilioupata dhidi ya Kagera Sugar 1-0 na Stand United 2-1 zote ikishinda ugenini uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga ziliwapa hamasa kubwa wapenzi na mashabiki wake. Ushindi huo uliipeleka kileleni Simba na kuwafanya watambe, tofauti na mahasimu zao Yanga ambao waliambulia pointi moja katika mechi zake mbili za ugenini. Yanga ilifungwa mabao 2-0 na Coastal Union uwanja wa Mkwakwani Tanga, kisha kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na Prisons uwanja wa Sokoine Mbeya, matokeo hayo yaliwasononesha sana mashabiki wa timu hiyo na walianzabkuikatia tamaa timu yao. Licha kwamba Yanga ilichomoza na ushindi wa bao

MAYANJA ASEMA, YANGA WANA BAHATI SANA

Picha
Na Alex Jonas Kocha wa Simba Sc Jackson Mayanja raia wa Uganda amefunguka na kusema Yanga wana bahati sana hasa baada ya jana kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 uwanja wa Taifa Dar es Salaam mchezo wa ligi kuu bara. Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Mayanja amesema Yanga ilipata ushindi huo baada ya mchezaji wake Abdi Banda kuonyeshwa kadi nyekundu mwanzoni mwa mchezo. "Yanga wana bahati sana kwani mwamuzi (Jonnesia Rukyaa) alitutoa mchezoni kwa kitendo chake cha kumpa kadi nyekundu Banda bila makosa yoyote", alisema na kuongeza. "Mwamuzi aliganya vile ili kututoa mchezoni mapema na kweli tumefungwa, vijana wangu niliwaandaa vizuri nikiamini tutaibuka na ushindi", alisema kocha huyo wa zamani wa vilabu vya Kagera Sugar na Coastal Union. Simba jana ilichezewa sharubu na vijana wa Jangwani baada ya kuchapwa mabao 2-0 yaliyowekwa kimiani na Donald Ngoma raia wa Zimbabwe na Amissi Tambwe raia wa Burundi

NILITABIRI YANGA ITASHINDA 3-0 LAKINI NIYONZIMA KANITIBUA- MUUMINI MWINJUMA

Picha
Na Saida Salum Mkurugenzi wa bendi ya muziki wa dansi ya Double M, Muumin Mwinjuma akiwa na familia yake baada ya furaha kubwa aliyonayo kufiatia timu yake ya Yanga kuibuka na ushindi dhidi ya hasimu wake mkuu Simba uwanja wa Taifa Dar es Salaam jana. Awali Muumin alijua wazi kama Yanga itaibuka na ushindi wa mabao 3-0 lakini haikuwa hivyo na jana ikishinda 2-0 na kujiongezea pointi tatu muhimu. "Nilitabiri Yanga itashinda 3-0 lakini Haruna Niyonzima ameniudhi jana baada ya kukosa goli la wazi, Simba sasa hivi ni wateja wetu hawatiwezi tena na tutawanyanyasa sana", alisikika Muumin ambaye alikuwa Pemba ya Msumbiji na bendi yake. Mashabiki wa Yanga jana walikuwa na furaha hasa baada ya timu yao kuichapa Simba mabao 2-0 mchezo wa ligi kuu bara, magoli ya Yanga yalitiwa kimiani na Donald Ndombo Ngoma raia wa Zimbabwe na Amissi Joselyin Tambwe raia wa Burundi

AZAM FC YAENDELEA KUITAMBIA MBEYA CITY

Picha
Na Salum Fikiri Jr, Mbeya Mabingwa wa Afrika mashariki na kati Azam Fc jioni ya leo imeendeleza wimbi lake la ushindi baada ya kuilaza Mbeya City mabao 3-0 kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya mchezo wa ligi kuu bara. Ushindi huo unaipeleka Azam hadi nafasi ya pili nyuma ya vinara Yanga, Azam imefikisha pointi 45 sawa na Simba lakini ina wastani mzuri wa magoli ya kufunga na kufungwa. Mabao ya Azam ambayo jumla imeibuka mbabe kwa Mbeya City mara nne, yalifungwa na washambuliaji wake Kipre Tchetche, John Raphael Bocco na kinda Farid Mussa. Kocha wa Azam Muingereza Stewart Hall amesema timu yake ilistahili matokeo hayo kutokana na maandalizi mazuri ya vijana wake baada ya kufuta makosa katika mchezo wao dhidi ya Coastal Union ambapo Azam ililala 1-0 Mkwakwani Tanga

SIMBA YAKUBALI KUWA TEJA LA YANGA, RASMI YAREJEA KILELENI, BOSSOU AMPOTEZA VIBAYA KIIZA

Picha
Na Alex Jonas, Uwanja wa Taifa Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara Yanga Sc jioni ya leo imeendeleza undava kwa watani zake Simba Sc baada ya kuichapa mabao 2-0 uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Mabao ya Donald Ngoma na Amissi Tambwe yametosha kabisa kuipa pointi tatu na magoli mawili Yanga na kuifanya irejee kileleni ikiwa na pointi zake 46. Simba iliutawala mchezo kipindi cha kwanza na kuwafanya mashabiki wake kuamini leo wataibuka na ushindi, Yanga haikucheza vizuri kipindi cha kwanza lakini ilitumia vema nafasi iliyoipata. Mlinzi wa Yanga Vincent Bossou raia wa Togo ambaye hivi karibuni alizungumza na blogu hii kuwa hamuogopi kabisa Hamisi Kiiza "Diego" kwani ana uwezo mkubwa wa kuwadhibiti washambuliaji machachari. Bossou leo amemkaba vilivyo Kiiza na kumpoteza kabisa mpaka kocha wa Simba Jackson Mayanja kumtoa, Ibrahim Ajibu naye alidhibitiwa vikali mpaka kutolewa, beki Abdul Banda alionyeshwa kadi nyekundu na kuifanya icheze ikiwa pungufu

NI SIMBA AU YANGA NANI ATACHEKA BAADA YA DAKIKA 90

Picha
Na Alex Jonas Ni pambano la kihistoria linatarajia kupigwa jioni ya leo katika uwanja wa Taifa Dar es salaam ambapo miamba ya soka nchini Simba na Yanga itakapepetuana. Timu zote zimejiandaa kuelekea mchezo huo ambapo kila moja iliweka kambi nje ya jiji kwa ajili ya kujiandaa na mchezo huo. Simba ambao ni vinara wa ligi hiyo wakiwa na pointi 45 waliweka kambi yao mjini Morogoro, Simba ina kumbukumbu nzuri ya kushinda mechi sita mfululizo. Kikosi cha Simba kinachonolewa  na Jackson Mayanja kina hali nzuri ya kuibuka na ushindi katika mchezo huo, Simba inajivunia washambuliaji wake wanne Hamisi Kiiza, Ibrahim Ajibu, Danny Lyanga na Mwinyi Kazimoti. Bila shaka nashabiki wake wanajipa matumaini ya kuondoka na ushindi mbele ya Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa ligi kuu bara. Yanga wao waliweka kambi yao Pemba ambapo wana kumbukumbu napo kwani katika mchezo wao wa kwanza na Simba walikaa eneo hilo na wakashinda mabao 2-0. Hivyo mashabiki wake wanaaminj leo watatoka na ushindi, Yanga

STAA WETU: ELIA DANIEL, MSANII WA FILAMU MWENYE NDOTO ZA KUMFIKIA KANUMBA

Picha
Na Prince Hoza KABLA hajaingia rasmi kwenye tasnia ya filamu alikuwa akimuhusudu sana Steven Kanumba (sasa marehemu), Elia aliamini Kanumba ndio msanii bora kwake. Lakini hilo halizuiliki kwani majuzi tu mwenyekiti wa chama cha wasanii wa filamu Simon Mwakifamba naye alisema hakuna msanii yoyote wa filamu hapa Tanzania aliyemfikia Kanumba hadi sasa. Elia Daniel naye anatamani japo siku moja anamfikia Kanumba, hilo kwake linahitaji juhudi na maarifa kwani hakuna libaloshindikana  chinj ya jua, Elia Daniel ni muigizaji wa filamu za kibongo ama Bongo Movie, ni mzaliwa wa mkoani Mbeya miaka 28 iliyopita mwezi Agosti, tarehe 27. Katika mazungumzo yake na blogu hii, Elia (pichani, kulia akiwa na Masinde) alianza rasmi kujikita kwenye filamu mwaka 2002 mkoani Mbeya na anasema amekutana na changamoto nyingi mpaka kufikia hapo halipo sasa. Ameshashiriki filamu nyingi za wasanii wenzake kipindi hicho akiwa bado hajaweza kumudu vema sanaa hiyo, 'Nilikuwa bado sina uwezo wa kutengeneza fi

ETOILE DU SAHEL YAILIPA SIMBA MILIONI 600 ZA OKWI

Picha
KLABU ya Etoile du Sahel ya Tunisia imesema kwamba imekwishaweka fedha benki kwa ajili ya kuilipa Simba SC dola za Kimarekani 300,000 zaidi ya Sh. Milioni 600 za Tanzania. Mwenyekiti ya Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amekutana kwa mazungumzo na Katibu wa Etoile, Adel mjini Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) leo na amehakikishiwa kupata fedha zao wakati wowote. "Baada ya kumaliza suala la Mazembe na samatta, leo nimekutana na katibu wa Etoile, Adel ambaye ameniambia jumatatu waliweka fedha benki kwa ajili ya kutulipa, sasa wajkati wowote mzigo utaingia dar es Salaam,"amesema Poppe juu ya fedha hizo, ambazo ni mauzi ya mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi kwenda Etoile du Sahel ya Tunisia mwaka 2013. Etoile, mabingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika wapo Lubumbashi kwa ajili ya mchezo wa kuwania taji la Super Cup ya CAF dhidi ya wenyeji, TP Mazembe ambao ni mabingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika utakaofanyika kesho Uwanja wa Mazembe mjini humo. Han

MICHANO: NEY WA MITEGO ANAJIPUNGUZIA MASHABIKI AU!

Picha
Na Mkola Man Mwanatanga Yap yap yap leo nachana kuhusu nyimbo ya Ney wa Mitego iitwayo "Shika adabu yako" ambayo ndiyo habari ya mjini na vijijini. Kutokana na utandawazi, Ney wa Mitego amejiongezea mashabiki, pia amejipunguzia mashabiki, vijana wengi wa kiume tumeweza kumpongeza kwa ujasili wake, ila imekuwa tofauti na dada zetu. Dada ,zetu wao asili yao huruma na kupenda mambo mazuri tuu, kiukweli amewagawa mashabiki wake huku akijua ana mtaji mdogo wa mashabiki. Pia wale anaowachana kwenye nyimbo zake wana mitaji mikubwa ya mashabiki, kwa mfano Ray na Ommy Dimpoz, sijajua ana mbinu gani kutokana na mitego yake. Ney wa Mitego anawagawa mashabiki wake yeye mwenyewe nyimbo zake za kuwachana wenzake, Mkola Man "Mwanatanga" sina makuu ila namchukulia kijana huyu mwenye asili ya mkoa wa Kilimanjaro sawa na mfugaji mpumbavu. Samahani sana Ney wa Mitego kukufananisha na mfugaji mpumbavu aliyemtegea kuku wake mayai viza kisha akishangaa kwanini kuku wake atot

NILIMDHIBITI DIDIER DROGBA, SEMBUSE KIIZA- BOSSOU

Picha
Na Mwandishi Wetu, Pemba Beki wa kati wa Yanga Vincent Bossou raia wa Togo, ameshangazwa na kauli za mashabiki wa soka nchini wakishindwa kumuamini na kutamka maneno kuwa hana uwezo wa kumdhibiti mshambuliaji wa Simba Hamisi Kiiza "Diego" raia wa Uganda. Akizungumza kwenye mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea kwenye uwanja wa Gombani Pemba amedai anashangazwa na kauli hizo na amewataka eajitokeze kwa wingi wakamshuhudie atakavyomdhiboti mshambuliaji huyo anayeongoza kwa mabao. Kiiza anaongoza kwa magoli hadi sasa ameshatupia magoli 16 akifuatiwa na mshambuliaji wa Yanga Amissi Tambwe mwenye mabao 14. Beki huyo amedai kuwa hsmuogopi Kiiza wala pacha wake Ibrahim Hsjibu na anawachukulia kama wachezaji wa kawaida, Bossou amewakumbushia mashabiki hao wanaombeza kuwa aliwahi kumdhibiti mchezaji bora wa Afrika Didier Drogba wa Ivory Coast. Pia amewahi kumdhibiti mshambuliaji bora mwingine wa Afrika Mcameroon Samuel Eto'o "Fills"

TFF YAPINGA MATOKEO YA GEITA, POLISI TABORA, SASA KAMATI YA NIDHAMU KUAMUA

Picha
Na Mrisho Hassan Kamati iliyokutana masaa 72 jana ya shirikisho la kandanda nchini TFF ineyapinga matokeo ya kundi C ligi Daraja la kwanza Tanzania kati ya Geita Gold na JKT Kanembwa iliyochezwa uwanja wa Lake Tanganyika na ule kati ya Polisi Tabora na JKT Oljoro uliofanyik uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora. Kamati hiyo ya masaa 72 imepinga vikali ushindi wa Geita Gold wa mabao 8-0 dhidi ya JKT Kanembwa na ule wa Polisi Tabora kuifunga JKT Oljoro mabao 7-0. Madai ya kamati hiyo kupinga ushindi huo imegundua kuwepo kwa mazingira ya upangwaji matokeo, hivyo kamati hiyo imeshindwa kutangaza timu iliyopanda ligi kuu na sasa imepeleka suala hilo kwenye kamati ya nidhamu ya TFF. Ikithibitika timu hizo zilipanga matokeo zitashushwa daraja na kutozwa faini kubwa ili iwe fundisho kwa wengine

KWA YANGA HII TAIFA! SIMBA WAKAROGE

Picha
Na Alex Jonas Yanga ililazimishwa sare na Mwadui Fc mjini Shinyanga ya kufungana mabao 2-2 tena ikinusurika kipigo, lakini pia ilipata ushindi kiduchu dhidi ya African Sports ya Tanga uwanja Mkwakwani. Yanga ikipata bao lake dakika za lala salama, inaonekana Yanga ikicheza nje ya uwanja wa Taifa inakuwa kwenye wakati mgumu msimu huu. Raundi hii ya pili Yanga ilicheza mechi mbili mfululizo zote ugenini, ilianza kucheza na Caostal Union uwanja Mkwakwani na Yanga ikapokea kipigo chake cha kwanza cha mabao 2-0, pia ikaenda sare na Prosons ya mabao 2-2 uwanja wa Sokoine Mbeya. Bado imebakiwa na mechi tano za ugenini bila shaka ina kazi ngumu kutetea mwali wake msimu huu, lakini jeshi hilo la Wanajangwani noma sana wakicheza uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Baada ya Yanga kupoteza mechi yake jijini Tanga na kulazimishwa sare jijini Mbeya watu wengi wakahusisha na mgogoro wa chini kwa chini ndani ya kikosi hicho na kupelekea katibu wake mkuu Dk Jonas Tiboroha kujiuzuru. Lakini il

YONDANI AWAUMIZA VICHWA YANGA

Picha
Na Alex Jonas Kufuatia shirikisho la kandanda nchini TFF kumfungia mechi tatu beki wa Yanga Kevin Yondan tayari kumeanza kuwaumiza vichwa baadhi ya wapenzi na mashabiki wa Yanga. Yondani alifungiwa mechi tatu na TFF baada ya kuonyesha utovu wa nidhamu katika mchezo wa ligi kuu kati ya Yanga na Coastal Union uliofanyika uwanja wa Mkwakwani Tanga. Beki kisiki wa Yanga alimrushia box la dawa daktari wa Coastal Union anayefahamika kwa jina la Mganga, kitendo hicho kilipelekea kuonyeshwa kadi nyekundu. Yondan amefungiwa mechi tatu na kutozwa faini ya shilingi laki tano, hata hivyo tayari ameshatumikia mechi mbili dhidi ya Prisons ya Mbeya na JKT Ruvu. Mchezaji huyo ataukosa mchezo dhidi ya Simba hivyo Wanayanga wameanza kuingiwa kiwewe wakiamini fowadi ya Simba inayoongozwa na Hamisi Kiiza na Ibrahim Hajibu itawasumbua mara kwa mara. Yanga kwa sasa imekuwa ikiwatumia Vincent Boosou na Mbuyu Twite na umekuwa ukiruhusu magoli ya kizembe, Nadir Haroub "Cannavaro" ambay

MWANAMAMA KUAMUA MTANANGE WA WATANI JUMAMOSI, VIINGILIO VYATAJWA

Picha
Na Mrisho Hassan Mwamuzi wa kike Jonnesia Rukyaa ndiye atakayepuliza kipyenga jumamosi katika mpambano wa watani wa jadi Simba na Yanga uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Mwamuzi huyo ndiye aliyechezesha wakati miamba hiyo ilipokutana nwaka juzi mchezo wa Nani Mtani Jembe Simba ikishinda 2-0 magoli yakifungwa na Awadh Juma na Elius Maguli. Wakati Baraka Kizuguto akiwatangazia waandishi wa habari leo, pia alitaja viingilio katika mchezo huo ambapo kwa upande wa walalahoi itakuwa shilingi 7000 na kule wanapokaa matajiri yaani V.I.P shilingi 30, 000. Simba na Yanga zinatarajia kupambana siku ya jumamosi mchezo wa ligi kuu bara, katika mchezo wa raundi ya kwanza Yanga iliifunga Simba mabao 2-0

JOHN WOKA AFARIKI DUNIA

Picha
Na Saida Salum Msanii wa zamani wa kundi la Wagosi wa Kaya John Woka aliyekuwa akiimba muziki wa kizazi kipya amefariki dunia alfajiri ya leo katika hospitali ya Muhimbili. Akizungumza na mwandishi wa blogu hii, kaka wa marehemu Omari Milley amesema mdogo wake amefariki dunia leo alfajili baada ya kupata ajali jana. John Woka aliyetamba kwa staili yake ya kilevi alipatwa na umauti baada ya jana kuangukiwa na kitu kizito wakati alipokuwa geteji Sinza akitengeneza gari lake. Marehemu wakati akitengeneza gari lake aliangukiwa na kitu hicho kilichopelekea kulipuka kwa gesi ambayo ilimuathili kichwani kwake baada ya kitu hicho chenye ncha kali kuingia ndani ya ubongo wake na kuchanganyika na damu. Milley amesema taratibu za mazishi zinapangwa na Mambo Uwanjani itakuwa ikiwajulisha kile kinachotolewa na wafiwa, R.I.P John Woka

SIMBA WASHITUKIA KAMBI YA ZANZIBAR, SASA WAAMUA KUBAKI MOROGORO, WADAI YANGA AKITOKA JUMAMOSI WAKATAMBIKE

Picha
Na Prince Hoza, Morogoro Vinara wa ligi kuu bara Simba Sc wameamua kujichimbia mjini hapa na kuachana na kambi ya Zanzibar wakidai imezingirwa na ushirikina mwingi. Mmoja kati ya viongozi wa timu hiyo aliyeambatana na timu tangia mjini Shinyanga ameamua kufichua kilichopelekea timu yao kujificha Moro na kuikacha Zanzibar. Kiongozi huyo aliyekataa kutaja jina lake akidai yeye si msemaji wa klabu amethibitisha kuwa ile kambi yao ya Zanzibar tayari imezingukwa na watu wa Yanga hivyo hawataweza kwenda "Simba kwa sasa itaendelea kujificha Moro na vijana wako katika hali nzuri na jumamosi Yanga lazima afe" alisema kiongozi huyo anayekubalika na wanachama wa klabu hiyo kongwe hapa nchini. Simba na Yanga zinakutana jumamosi katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam mchezo wa ligi kuu bara. Yanga wameweka kambi yao Pemba, katika mchezo wa kwanza Yanga iliweka kambi yake Pemba na Simba walijificha Unguja, lakini zilipokutana uwanja wa Taifa, Yanga ilishinda mabao 2-0.

MAONI: NITASHANGAA SANA KAMA TFF ITAZIACHIA GEITA GOLD NA POLISI TABORA BILA KUZIFUNGIA

Picha
Na Prince Hoza NI dhahili kabisa matokeo yamepangwa, hakuna ligi yenye ushindani mkubwa kama ligi Daraja la kwanza Tanzania bara (FDL). Lakini cha kushangaza timu zinapigwa 8-0 na nyingine 7-0 halafu mechi za mwisho ambazo zinaamua nani apande ligi kuu bara, Geita Gold Mine inayonolewa na nchezaji wa zamani na kocha msaidizi wa Simba Sc Seleman Matola iliitungua JKT Kanembwa ya Kigoma mabao 8-0. Huo ulikuwa mchezo wa mwisho ambao umeiwezesha Geita Gold kupanda ligi kuu bara, wakati Geita ikiichapa Kanembwa, Polisi Tabora nayo ikaichapa JKT Orjolo mabao 7-0. Polisi nayo ilihitaji ushindi mkubwa kama huo ili iweze kuungana na Ruvu Shooting na Aftican Lyon ambazo tayari zimeshapanda ligi kuu bara. Ushindi mkubwa wa Geita Gold na ule wa Polisi Tabora si kwamba naupinga kwa chuki binafsi, hapana, Geita Gold naifahamu sana ni timu yenye uwezo mkubwa wa kusakata kandanda na inao uwezo wa kushinda mabao mengi kama hayo. Si mara ya kwanza klabu za ligi kuu kukubali vipigo kama hi

AZAM FC YASHINDWA KUKWEA KILELENI, YAPIGWA 1-0 NA COASTAL UNION

Picha
Na Saida Salum, Tanga Mabingwa wa soka Afrika mashariki na kati Azam Fc jioni ya leo imepokea kichapo toka kwa wenyeji wao Coastal Union katika uwanja wa Mkwakwani Tanga. Azam ambayo sasa inakamata nafasi ya tatu ikiwa na pointi 42 imeshindwa kukwea kileleni hivyo inawafanya Wekundu wa Msimbazi kuendelea kukaa kileleni na pointi zao 45 ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 43. Coastal Union ambao wamekuwa wakifanya vibaya wanapocheza na timu dhaifu lakini imekuwa ikitoa vipigo kwa vigogo ambapo ilianza kuitandika Yanga Sc. Goli la ushindi la Coastal Union limefungwa na muuaji wake yule yule aliyeiua Yanga Miraji Adamu, hata hivyo nahodha wa Azam alitaka kurushiana makonde na wenzake wa Coastal. Kwa maana hiyo Azam itakuwa na kazi ngumu ili iweze kurejea tena kileleni kwani jumamosi ijayo itacheza na Mbeya City iliyorejea katika makali yake baada ya kupata kocha mpya raia wa Malawi Kinah Phiri

WACHEZAJI YANGA WAWANYOOSHEA SIMBA VIDOLE VITANO

Picha
Na Alex Jonas, Pemba Tayari mabingwa wa soka nchini Yanga Sc wamewasili Pemba kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wake wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara utakaochezwa jumamosi ijayo na mtani wake Simba Sc katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Yanga jana ilikuwa katika ardhi ya Mauritius ambapo saa 9:30 ilipepetana na Cercle de Joachim katika uwanja wa Curepipe mchezo wa ligi ya mabingwa barani Afrika. Katika mchezo huo Yanga imechomoza na ushindi wa bao 1-0 ambapo itakuwa na kazi nyepesi katika mchezo wa marudiano jijini Dar es salaam majuma mawili yajayo. Donald Ngoma ndiye mfungaji pekee wa goli la ushindi la Yanga, lakini hesabu zote za Yanga zimeelekezwa kwenye mchezo wa jumamosi dhidi ya Simba na iliamua kukodi ndege ya kuwapeleka Mauritius kisha kuwapeleka Pemba kabla ya kuwaleta Dar es salaam. Walipotua kisiwani Pemba muda huu, wachezaji wa Yanga waliwaonyeshea vidole vitano mashabiki wa Simba, hiyo ina maana kwamba Yanga itawafunga Simba mabao matano. Ama ishara h

CHIFU PANDUKA KATIKA MAHUSIANO YA MAPENZI, ANAMRUDISHA MPENZI ALIYEPOTEA

Picha
Na Juma Mwema Leo ni siku spesho kwa wapendanao yaani Valentine Day ambapo watu wote huwajali wenza wao, kona hii nayo inawaletea darasa tosha wapendanao. Chifu Panduka tabibu na mnajimu wa nyota Afrika mashariki na kati anawaletea dawa yake inayorejesha mahusiano yaliyovunjika. Kuna wapendanao wanaachana aidha kwa kufarakana ama kutokewa na jini mahaba na hatimaye mapenzi kufa. Lakini vilevile mapenzi yanaweza kufa kama mvuto umepotea, Chifu Panduka mwenye kituo chake Tabata Relini anayo dawa ya kumrudisha mchumba au mpenzi aliyekupotea. Ama anaweza kumrudisha mchumba wako ambaye amepunguza mahusiano nawe, fika kliniki yake iliyopo Tabata Relini jirani na ukumbi wa Hai Bar , shuka Tabata relini ama waweza kumpigia simu namba 0715281162. NYOTE MNAKARIBISHWA

HAMISI KIIZA AIPELEKA SIMBA KILELENI

Picha
Na Prince Hoza, Shinyanga Wekundu wa Msimbazi Simba Sc kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa ligi kuu bara wamefanikiwa kukamata usukani wa ligi hiyo baada ya kuilaza Stand United mabao 2-1 uwanja wa Kambarage Shinyanga. Hamisi Kiiza 'Diego' raia wa Uganda amekuwa na bahati msimu huu akifanikiwa kufunga mabao yote mawili ambayo yanaiweka timu yake kileleni. Kiiza amefunga mabao hayo kila kipindi na kumfanya afikishe magoli 16 akimuacha nyuma mpinzani waks mkuu kwenye mbio hizo Mrundi Amissi Tambwe wa Yanga mwenye mabao 14. Stand United nao walijipatia bao la kufutia machozi lililofungwa na David Assuman. Simba sasa iko kieleni ikiwa na pointi 45 ikiiacha nyuma Yanga yenye pointi 43 lakini ina mechi moja mkononi. Hata hivyo Simba inaweza kupokwa uongozi na Azam Fc ambao kesho wanacheza na Coaatal Union katika uwanja wa Mkwakwani Tanga, Azam itahitaji kushinda mabao mengi ili kuipoka uongozi Simba kwani yenyewe inatambia mabao ya kufunga

DONALD NGOMA AIPAISHA YANGA KIMATAIFA, YASHINDA 1-0

Picha
Na Alex Jonas, Curepipe Mabingwa wa soka Tanzania bara Yanga Sc jioni ya leo imeanza vema michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika baada ya kuilaza 1-0 timu ya Cercle de Joachim ya Mauritius katika uwanja wa Curepipe. Mabingwa hao ambao leo wamepokwa uongozi wa ligi kuu bara na mtani wake Simba watakuwa na kazi nyepesi katika mchezo wa marudiano utakaofanyika jijini Dar es salaam wiki mbili zijazo. Mshambuliaji Donald Ngoma raia wa Zimbabwe aliifungia Yanga bao la ushindi na kuifanya itoke kifua mbele. Yanga sasa inarejea na ndege yake ya kukodi na moja kwa moja itaelekea Pemba kuweka kambi kujiandaa na mchezo wake wa ligi kuu bara dhidi ya hasimu wake mkubwa Simba katika uwanja wa Taifa Dar es salaam

STAA WETU: JERRY TEGETE WA MWADUI FC YA SHINYANGA

Picha
Na Salum Fikiri Jr Ni mchezaji wa Mwadui Fc anayecheza nafasi ya ushambuliaji, mpaka sasa ameshafunga jumla ya mabao matano, na ana kiu ya kuibuka mfungaji bora wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara. Jerry Tegete alikuwa mitaa ya Jangwani akiichezea Yanga Sc kwa mafanikio makubwa hasa akichangia kuipa mataji manne, mawili ya kombe la Kagame. Mshambuliaji huyo mrefu aliibuliwa na aliyekuwa kocha wa timu ya taifa, Mbrazil Marcio Maxinmo. Mara ya kwanza Maximo alilaumiwa na wadau wa soka nchini hasa pale alipoonekana akimkumbatia Tegete, lakini baadaye nyota yake ilianza kung' ara na ndipo Simba na Yanga zilipopigana vikumbo kumwania. Jerryson Johnson Tegete alijiunga na Yanga na alidhihirisha makali yake na wala Maximo hakukosea kumchukua kutoka shule ya sekondari ya Makongo High School. Tegete alifanikiwa kuitungua Simba zaidi ya mara mbili na kumfanya azidi kuogoewa, mshambuliaji huyo mbali na kutegemewa na Yanga, pia alikuwa tegemeo kwenye timu ya taifa. Tegete ni

SIMBA ILIVYOJIFUA JANA KAMBARAGE, STAND WAKINUSURIKA KIPIGO WAKAOMBE KWA BABU

Picha
Na Prince Hoza, Shinyanga Wachezaji wa Simba Sc jana waliendelea na mazoezi ya nguvu katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga ambapo leo jioni watachuana na wenyeji wao Stand United. Simba inahitaji pointi tatu muhimu katika mchezo huo wa ligi kuu bara na endapo itaibuka na ushindi mojs kwa moja itakwea kileleni kwa mara ya kwanza tangia kuanza kwa msimu huu. Kocha mkuu wa Simba Jackson Mayanja anaonekana hataki mzaha awapo kazini na alikuwa akiwapigisha tizi la nguvu wachezaji wake. bila shaka jioni ya leo Simba itachomoka na ushindi na endapo itatokea bahati mbaya Stand United ikanusurika kipigo basi wakaombe kwa babu