Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2018

SIMBA NA ASANTE KOTOKO HAPATOSHI TAIFA

Picha
Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam Mabingwa wa soka nchini Simba SC wanatelemka uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam jioni ya leo kuumana na Asante Kotoko ya Ghana mchezo wa kirafiki kuadhimisha Simba Day. Asante Kotoko iliwasili jana tayari kwa mchezo huo, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ndiye mgeni wa heshima, kuelekea katika tamasha hilo kikosi cha Simba kiliwasili nchini Jumapili kikitokea Uturuki ambapo kiliweka kambi wiki mbili. Kocha mkuu wa Simba Mbelgiji Patrick J Aussems jana aliwaambia waandishi wa habari kuwa atautumia mchezo huo kupata taswira ya kikosi chake, mchezo huo utaanza saa 10:00 na lengo ni kutambulisha wachezaji wapya na jezi mpya

MOROCCO AIGOMEA SINGIDA UNITED

Picha
Na Saida Salum. Dar es Salaam Kocha mkuu wa klabu ya soka ya Singida United  Hemed Suleiman Morocco ameamua kuigomea klabu yake baada ya kushindwa kumtimizia mahitaji yake kama walivyokubaliana hapo mwanzo. Akizungumza kwa njia ya simu kutoka kwao Zanzibar, Morocco amesema ameamua kugoma kuiongoza timu hiyo kwa sababu hajalipwa stahiki zake hivyo ameshindwa kuambatana na kikosi jijini Mwanza ambapo kimeweka kambi. Morocco ambaye ni kocha wa timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes amedai hawezi kuripoti kambini mpaka pale atakapolipwa stahiki zake kwani ameanza kuingia shaka na viongozi wa timu hiyo kwa kuchelewa kumkamilishia mahitaji yake

Ali Kiba aahidi makubwa Coastal Union

Picha
Na Mkola Man. Tanga Mchezaji mpya wa Coastal Union ya Tanga Ali Saleh Kiba maarufu King Kiba ameahidi kuifanyia mambo makubwa klabu yake ya Coastal Union kwakuwa ndiy pekee iliyoweza kumpa heshima kubwa na kumsajili. Akizungumza na Mtandao hu, Kiba amesema Coastal Union imempa heshima kubwa kwa kumsajili kwa Mara ya kwanza kuchezaLigi Kuu kwani soka alilokuwa akicheza ni lmchangani tu. Kiba amesema kwa kiwango alichonacho atawashangaza Watanzania na kukubali mileanachokifanya, Kiba ni mwanamuziki wa miondoko ya bongofleva na amekuwa akifanya vizuri mno tungo sake