Kilomoni asema ajafutwa uanachama, na afuti kesi

Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam

Aliyekuwa Mdhamini wa klabu ya Simba, mzee Hamisi Kilomoni amesema atambui kufutwa uanachama kama ilivyotangazwa na klabu hiyo na pia hawezi kwenda kuondoa kesi yake akiyoifungua mahakamani.

Akizungumza na mtandao huu, Kilomoni amesema yeye bado kiongozi wa bodi ya wadhamini wa klabu ya Simba na amedai maamuzi ya kumsimamisha uanachama wameyafanya wao tu ili kudanganyana na kamwe hakuna atakayeweza kumsimamisha wala kumfuta uanachama.

Kilomoni amedai hawezi kwenda kuifuta kesi aliyoifungua katika mahakama ya mkazi ya Kisutu na amesema ataendelea kuushinikiza uongozi juu ya mpango wake wa kutaka kumuuzia klabu mfanyabiashara Mohamed Dewji

Hamisi Kilomoni, amesema afuti kesi na hakuna wa kumfuta uanachama

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI