BOSSOU KUIBURUZA YANGA FIFA

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

Beki wa zamani wa mabingwa wa soka nchini, Yanga, Vincent Bossou ametishia kuiburuza FIFA klabu yake ya zamani ya Yanga endapo itashindwa kumlipa mishahara yake ya miezi miwili.

Bossou amesema anaidai Yanga na imeshindwa kumlipa kwani alianza kudai fedha zake tangia Yanga ikiwa chini ya kaimu katibu mkuu, Baraka Deusdetit na sasa Charles Boniface Mkwasa na wote wamekuwa wakimpiga danadana.

Katika taarifa yake aliyoitoa, beki huyo amedai mashabiki wa Yanga wasimlaumu pale atakapowasilisha madai yake FIFA, wakala wa mchezaji huyo Mganda, Gibby Kalule amesema Yanga watalazimika kumlipa pesa zake za mishahara ama sivyo watafikishwa FIFA

Vincent Bossou, anaipeleka Yanga, FIFA

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI