Okwi aanza balaa lake, apiga bonge la bao

Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam

Mabingwa wa kombe la FA, Simba SC jioni ya leo imechomoza na ushindi wa bao 1-0 mchezo wa kirafiki Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Goli la ushindi limefungwa na Mganda, Emmanuel Okwi aliyepokea pasi murua kutoka kwa John Bocco "Adebayor", huo ni ushindi wa pili mfululizo baada ya Jumanne iliyopita kuichapa Rayon Sports bao 1-0.

Okwi alitoa pasi nzuri ambapo Mohamed Ibrahim "Mo" aliifungia Simba bao la ushindi, Simba inaendelea kukisuka kikosi chake ambapo itacheza na Ruvu Shooting kabla haijaivaa Yanga Agosti 23 mwaka huu kuwanjia Ngao ya Hisani katika Uwanja hup huo wa Taifa

Emmanuel Okwi (Kushoto) akishangilia sambamba na Shiza Kichuya

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI