Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Simba na Yanga hakuna kuremba

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

Watani wa jadi wa soka la Tanzania Simba SC na Yanga SC leo jioni zinaumana katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuwania Ngao ya Jamii, miamba hiyo inakutana kila mmoja ikiwa imetokea Visiwani Zanzibar ambako ilikwenda kuweka kambi.

Kwa upande wa Yanga, walielekea katika kisiwa cha Pemba lakini walianza kufikia Unguja ambapo walicheza mechi moja ya kirafiki na Mlandege na kushinda mabao 2-0, kisha wakaelekea Pemba ambapo pia walicheza mechi mbili za kirafiki.

Yanga ilicheza na Chipukizi na kushinda bao 1-0 kisha ikainyoa Jamhuri pia bao 1-0, itashuka uwanjani leo ikimtegemea zaidi mshambuliaji wake mpya Ibrahim Ajibu ambaye katika mechi hizo aliweza kufunga.

Simba nao walifikia Unguja ambapo wao walicheza mechi mbili za kirafiki ambapo walilazimishwa sare na Mlandege 0-0 kisha wakaichapa Gulioni mabao 5-0, Laudit Mavugo anapewa nafasi kubwa ya kuiongoza Simba kutokana na kuifungia mabao mawili Simba ilikuwa Zanzibar, ingawa kutakuwa na kivutio toka kwa Haruna Niyonzima na Emmanuel Okwi kwa upande wa Simba na Donald Ngoma na Amissi Tambwe kwa Yanga.

Mchezo huo unatarajiwa kuanza saa 11:00 za jioni na timu zote zinanolewa na makocha wa kigeni ambao watahakikisha wanalinda vibarua vyao, Ligi Kuu itaanza rasmi Jumamosi ya Agosti 26

Simba na Yanga wanaumana leo Uwanja wa Taifa Dar es Salaam

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa