Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA YAIENDEA AZAM FC PEMBA

Na Ikram Khamees, Pemba

Vinara wa ligi kuu bara Yanga Sc inatarajia kuwasili visiwani Pemba tayari kabisa kujiandaa na mchezo wake wa ligi jumamosi ijayo uwanja wa Taifa Dar es Salaam dhidi ya waoka mikate wa Azam Fc.

Yanga imeamua kuijia Azam Pemba ni kutokana na ushndani wake unapokuwa mkubwa hivyo imeamua kuijia Pemba kama ilivyofanya hivyo dhidi ya Simba Sc.

Yanga iliijia Simba Pemba na ikafanikiwa kuichapa mabao 2-0 uwanja wa Taifa Dar es Salaam mchezo wa ligi kuu bara.

Vinara hao wa ligi kuu ndio mabingwa watetezi wa ligi hiyo na safari hii inataka kuhakikisha inachukua tena ubingwa, Akizungumza jana na blogu hii msemaji wavYanga Jerry Muro amesema Yanga itaweka kambi yake Pemba ili kujiandaa na Azam.

Muro amedai Pemba ni sehemu tulivu hivyo panafaa kwa kambi, ameongeza Azam inawakamia sana hasa wanapokutana nao lakini safari ya Pemba itakuwa mwisho wao.

Amedai kikosi chao lazima kiibuke na ushindi katika mchezo huo ili iendelee kuongoza ligi kwa uwiano wa pointi, kwa sasa Yanga inaongoza ligi kwa uwiano wa magoli kwani yenyewe ina pointi 46 sawa na Azam

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa