GIANNY INFONTINO RAIS MPYA FIFA

Na Mwandishi Wetu

Shirikisho la kandanda duniani FIFA leo limempata rais wake mpya atakayerithi nafasi ya Seppt Blatter ambaye ameenguliwa baada ya kuhusishwa na ufisadi mkubwa uliozingira taasisi hiyo kubwa ya soka duniani.

Gianny Infontino ndiye aliyetawazwa kuwa bosi mpya wa shirikisho hilo baada ya kumshinda Al Salman, Infontino alipata kura 115 akimzidi kura 27 mpinzani wake huyo aliyekuwa akiungwa mkono na bara la Afrika.

Infontino alikuwa katibu mkuu wa shirikisho la soka barani ulaya (UEFA) na anakuwa rais wa tisa wa FIFA baada ya Blatter aliyedumu kwa miaka 18

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA