Ivo Mapunda aanzisha kituo chake cha michezo, lengo kuondoa Panya Road

Na Prince Hoza, Dar es Salaam

Kipa wa zamani wa Yanga, Simba na Taifa Stars, Ivo Philip Mapunda, ameamua kuanzisha kituo chake cha michezo kitakachojumlisha vijana kuanzia umri wa miaka 8- 18.

Akizungumza jana, Mapunda amesema amefikia maamuzi hayo hasa baada ya kuona vijana wengi wakijihusisha na vitendo vya kihuni kama 'Panya Road' na makundi mengineyo.

Kipa huyo aliyewahi pia kuzichezea Tukuyu Stars, Prisons, Moro United, African Lyon, Bandari Mombasa, Gor Mahia, St George na pia Azam FC, kipa huyo amedai bado hajaamua kustaafu soka na amevitaka vilabu vinavyomuhitaji yupo tayari kujiunga nazo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI