USHAHIDI WA PICHA: MASHALI KUMBE ALISILIMISHWA NA SHEIKH SHARIFU

Picha/Habari na Salum Fikiri Jr

Bondia Thomas Mashali ambaye jana alizikwa katika makaburi ya Kinondoni kwa dini ya Kikristo dhehebu la Katoliki kumbe siku za hivi karibuni alibadili dini na kuingia Uislamu.

Mbaruku Heri ambaye naye ni bondia na kocha wa mchezo huo, amethibitisha kuwa Thomas Mashali ni muislamu lakini anashangaa kuzikwa kikristo, bondia huyo aliamua kusilimu yeye mwenyewe na Sheikh aliyehusika kumbadili ni Sharifu.

Heri anadai kuwa bondia huyo aliamua aitwe Mohamed Mashali, lakini anasikitika kuona akizikwa kwa dini ya Kikristo aliyoikataa marehemu mwenyewe, Heri anasema iko wapi haki ya Waislamu mbona wapo Waislamu walioamua kuingia Ukristo na wakifa wanazikwa Kikristo, Heri anasema kuna kaubaguzi kidogo hapa nchini

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI