Mtibwa Sugar yamrejesha Kado

Na Ikram Khamees. Dar es Salaam.

Timu ya Mtibwa Sugar imefanikiwa kumrejesha mlinda mlango wake wa zamani, Shaaban Kado ambaye alikuwa anaichezea Mwadui FC ya Shinyanga.

Kocha wa timu hiyo Zuberi Katwila amesema baada ya kuondokewa na kipa wao chaguo la kwanza, Said Mohamed Nduda ambaye amesaini mkataba wa miaka miwili, alimpendekeza Kado.

Uongozi wa Mtibwa Sugar umeona ni bora umrejeshe Kado ambaye alikuwepo hapo kabla hajaenda kujiunga na Yanga SC, Kado ameamua kurejea kwani hadi sasa Mtibwa imemnyakua mlinzi wa Mwadui, Salum Kanoni, Kado amesaini mkataba wa miaka miwili

Shaaban Kado anarejea Mtibwa Sugar
Kado akisaini mkataba mbele ya mratibu wa timu hiyo, Jamal Bayser

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI