Ronaldo wa Ndondo Cup atua Mbeya City

Na Exipedito Mataruma. Mbeya

Wagonga Nyundo wa Mbeya City ya jijini Mbeya imeendelea kujiimarisha baada ya kufanikiwa kuwasainisha wachezaji wawili kwa mkupuo.

Wagonga nyundo hao jana wamekamilisha usajili wa Antony Mwingira na kiungo mshambuliaji wa zamani wa Ashanti FC na KCM zote za Dar es Salaam, Iddi Seleman maarufu kama Ronaldo.

Ronaldo anasifika sana kwa uchezaji wake katika michuano ya Ndondo Cup inayochezwa jijini Dar es Salaam, kiungo huyo amekuwa akizivhezea timu mbalimbali ikiwemo Faru Jeuri, wachezaji wote hao wamesaini mkataba wa miaka miwili

Iddi Seleman "Ronaldo" amejiunga na Mbeya City

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI