Rasmi,Msuva asaini El Jajida

Kiungo wa kimataifa wa Tanzania Simon Happygod Msuva amesaini mkataba wa kujiunga na timu ya Ligi Kuu ya Difaa El Jajida ya Morocco lakini klabu hiyo imefanya siri haijaweka wazi mkataba huo ni wa muda gani.

Taarifa iliyotolewa na klabu hiyo mchana wa leo imesema kwamba, Difaa El Jajida imemalizana na mchezaji huyo na tayari imeshamtambulisha kwa mashabiki wake.

Aliyekuwa katibu wa Yanga Sc, Dk Jonas Tiboroha anahusika katika usajili huo akianza kupatana na kumuuza pia, inasemekana Yanga itapatiwa Dola 150,000 ambazo ni sawa na shilingi Milioni 300 za Kitanzania.

Msuva anaungana na winga mwingine wa Tanzania, Ramadhan Singano "Messi" ambaye alikuwa anaichezea Azam FC, Msuva alijiunga na Yanga mwaka 2012 akitokea Moro United ambayo nayo ilimchukua akitokea Akademia ya Azam FC

Simon Msuva ameondoka Yanga
Simon Msuva (wa pili kutoka kulia, akitambulishwa kujiunga na Difaa El Jajida, wa kwanza kulia ni meneja wake Jonas Tiboroha

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA