Peter Manyika atolewa kwa mkopo

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

Mlinda mlango Peter Manyika Jr anatolewa kwa mkopo wakati kipa mwingine Dennis Richard ametemwa rasmi.

Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu ya Simba, Zacharia Hanspoppe amesema leo kuwa wameamua kumtoa kwa mkopo Manyika Jr kwakuwa akarejeshe kiwango.

Manyika ameonekana kushuka kiwango na ndio maana hakuwa akianza katika kikosi cha kwanza, pia Hanspoppe amesema Simba imewaacha Novat Lufunga, Hamad Juma, Pastory Athanas, Janviel Bokungu na Dennis Richard.

Mwenyekiti huyo amesifu usajili walioufanya na kudai umezingatia mahitaji ya mwalimu Joseph Omog na msaudizi wake Jackson Mayanja

Peter Manyika ametolewa kwa mkopo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI