STRAIKA LA MABAO LA GHANA HILI HAPA MSIMBAZI

Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam

Simba SC sasa imepania kwenye suala la usajili kwani imeamua kusajili wachezaji wote nyota ndani ya nje ya Tanzania, Nicholaus Gyan raia wa Ghana ndiye straika mpya anayetarajia kutua katika klabu hiyo.

Gyan ameonyesha uwezo mkubwa katika Ligi Kuu ya Ghana huku akifanikiwq kufunga mabao 12, straika huyo unaambiwa ni hatari kinoma  na Wekundu wa Msimbazi wamepanga kumshusha hivi karibuni.

Hadi sasa Simba imeshasajili wachezaji 12 na inadaiwa kuna wengine wawili watasajiliwa, Gyan ameshawekwa katika orodha ya watakaosajiliwa na kitu kinachosubiriwa kwa sasa ni ujio wake tu, Gyan atasimama namba tisa na anasifika kwa mashuti

Nicholaus Gyan, straika mpya Simba

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI