Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA WAPONEA TUNDU LA SINDANO KUFA, BASI LAO LATUMBUKIA MTARONI MIKESE

Wachezaji na viongozi wa Yanga SC wamenusurika kifo baada ya basi lao kuacha njia na kutumbukia mtaroni eneo la Mikese majira ya saa 3:30 asubuhi wakati wakitoka Morogoro kuelekea Dar es Salaam.

Akizungumza ajali hiyo katika eneo la tukio Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizunguti alisema basi lao liliacha njia baada ya dereva wao kukwepa kugongana uso kwa uso na basi lingine lililokuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea mikoa ya bara.

“Hii ajali kama siyo akili ya haraka haraka ya dereva wetu kuacha njia na kuseleleka, basi hapa leo kungetokea ajali mbaya tena ingehusisha majeruhi na vifo, lakini tunamshukuru Mwenyezi Mungu hakuna aliyeumia zaidi ya basi kupata mikwaruzo kidogo.”


Kizuguto aliongeza kwa kusema ajali yao imetokana na dereva wa basi lingine aliyekuwa akiyapita malori akiwa katika mwendo kasi na kulazimisha basi la Yanga liachie njia ili basi hilo liweze kupita na endapo isingefanya hivyo, basi hizo zingegongana uso kwa uso.

Malori yalikuwa katika foleni ndefu yakitokea Dar es Salaam kuelekea Morogoro yakielekea mizani ya Mikese, na kutoa nafasi kwa magari yatokayo Morogoro kwenda Dar es Salaam kupita bila kipingamizi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa