Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KOCHA WA GHANA ATUA LIVERPOOL


Kocha Kwessi Appiah
Kocha wa timu ya taifa ya Ghana, Kwesi Appiah yuko ziarani nchini Uingereza kupata uzoefu kutoka kwa klabu ya soka ya Liverpool.

Appiah pamoja na kocha wa golkipa Nassam Yakubu, watajionea Liverpool inavyofanya maandalizi kabla ya michuano yoyote.
Zaidi ya hayo kocha huyo wa Black stars, atakutana na maafisa wa shirikisho la mameneja katika uwanja wa St. George, kituo cha mazoezi ya timu ya taifa ya soka ya England.


Ziara hii inalenga kusaidia maandalizi ya timu ya taifa ya Ghana kabla ya kushiriki michuano ya kombe la dunia.
Ujumbe huo unajumuisha naibu wa Appiah, Maxwell Konadu, Yakubu, daktari wa kikosi hicho, Adam Baba na mdadisi Michael Okyere.

Wanatarajiwa kuondoka Accra hii leo kwa ziara hiyo itakayodumu siku kumi.
"hii ni fursa nzuri sana kwetu kuweza kutembelea Liverpool,moja ya vilabu mahiri vya soka duniani kujionea wanavyojiandaa kabla ya michuano,'' alisema Rais wa shirikisho la soka nchini Ghana Kwesi Nyantakyi.
"bila shaka fursa hii itakua muhimu sana kwa kikosi cha Black Stars na itawasaidia kuleta nyumbani ushindi.''
Sio mara ya kwanza kwa Appiah kuzuru England ili kuboresha uzoefu wake na wa wachezaji, amewahi kutembelea Manchester zaidi ya mara moja.

Ghana iko katika kundi G katika michuano ya kombe la dunia pamoja na Brazil na Ujeumani , Ureno na Marekani.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa