Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA KUTIBUA NDOTO ZA AZAM KUTWAA UBINGWA WA BARA JUMAMOSI

Majaliwa ya Yanga na Azam FC kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara yapo mikononi mwa Simba ambayo imebakiza mechi na vigogo hivyo vinavyofukuzana kwa karibu katika msimamo wa ligi hiyo inayotarajiwa kumalizika Aprili 19, mwaka huu.

Azam ambayo ipo kileleni ikiwa na pointi 47, nne zaidi ya Yanga inayoshika nafasi ya pili, imebakiza mechi nne huku wapinzani wao wakibakiza tano, lakini zote zitalazimika kukutana na Simba, hivyo kupoteza dhidi ya Kikosi hicho cha Zdravko Logarusic kwa timu hizo kunaweza kupeperusha ndoto za kutwaa ubingwa.

Hata hivyo, Azam italazimika kuanza kushinda Jumamosi dhidi ya Simba kabla ya kujipanga kuibuka na ushindi itakapokutana na Ruvu Shooting ugenini na baadaye kuikabili Mbeya City kabla ya kumaliza na JKT Ruvu.


Wakati Yanga yenyewe itakuwa na kibarua kigumu dhidi ya  Tanzania Prisons kesho Taifa na Jumamosi kuifuata Mgambo JKT Uwanja wa Mkwakwani na baadaye kurudi Taifa kuialika JKT Ruvu.

Baada ya mechi hiyo, itasafiri kuifuata Oljoro JKT katika Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid na kisha kumaliza na Simba Taifa.

Hata hivyo, kikwazo kingine cha Azam kinaweza kuwa Mbeya City ambayo ina kumbukumbu ya kupoteza mechi moja tu katika Uwanja wao wa Sokoine.

Tayari mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, Yanga, jana jioni waliingia kambini katika jengo la makao makuu ya klabu hiyo yaliyopo mtaa wa Jangwani na Mafia kwa ajili ya kujiandaa na mechi yao ya kesho dhidi ya Prisons kutoka jijini Mbeya.

Yanga imeamua kurejea kwenye makao makuu badala ya Bagamoyo kama ilivyotangaza kuwa ndiyo kambi yao ya kudumu msimu huu.

Kocha Msaidizi wa Yanga, Boniface Mkwasa, alisema kikosi hicho sasa hakitakuwa na mapumziko kwa sababu mechi zote zilizobakia ni ngumu na wao wanahitaji ushindi.Mkwasa alisema katika mbio za ubingwa hawapo peke yao, hivyo hawatakiwi 'kushangaa'.

"Hakuna kulala, tunajua kwamba sio peke yetu tunaotaka kikombe cha ubingwa, tunaendelea na mazoezi hakuna kupumzika," alisema kocha huyo wa zamani wa Ruvu Shooting.

Alisema kwamba Yanga imejiandaa kukutana na changamoto mbalimbali na ushindani kutoka kwa timu pinzani.
Aliongeza kuwa ligi ni ngumu na kila mchezaji anapaswa kujituma ili waweze kufikia malengo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa