Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MRISHO NGASA FITI KUIVAA AZAM KESHO, KASEJA AAHIDI MAKUBWA GOLINI

MRISHO Ngassa amefanya mazoezi vizuri na kumaliza kuashiria yuko tayari kwa mchezo wa Jumatano dhidi ya Azam FC Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Ngassa aliyewasili kwenye kambi ya timu yake, Yanga SC katika hoteli ya Kiromo, Bagamoyo mkoani Pwani alikosekana katika mchezo uliopita wa ligi hiyo dhidi ya Mtibwa Sugar mjini Morogoro kwa sababu ya majeruhi.

Ngassa alitoka uwanjani kipindi cha pili Jumapili ya wiki iliyopita baada ya kuumia Yanga SC ikimenyana na Al Ahly ya Misri mjini Alexandria katika mchezo wa marudiano Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika na kutolewa kwa penalti 4-3 kufuatia sare ya jumla ya 1-1.

Na baada ya kutua Dar es Salaam Jumatano, alikwenda Mwanza mapumzikoni, huku wenzake wakiingia kambini kujiandaa na mechi dhidi ya Mtibwa Sugar mjini Morogoro Jumamosi iliyoisha kwa sare ya bila kufungana.

Ngassa anatarajiwa kucheza dhidi ya timu yake ya zamani, Azam FC kwa mara ya kwanza msimu huu baada ya kukosa mechi mbili, ya Ngao ya Jamii Yanga ikishinda bao 1-0 na wa Ligi Kuu mzunguko wa kwanza, Azam FC wakishinda 3-2.


Yanga iliyomleta Ngassa Dar es Salaam kwa mara ya kwanza kutoka Kagera Sugar ya Bukoba mwaka 2007, ilimuuza mchezaji huyo Azam FC mwaka 2009, ambao nao mwaka 2012 wakamtoa kwa mkopo Simba SC kumalizia Mkataba wake.

Baada ya kumalizana na Simba SC,
msimu huu Ngassa amerudi timu yake iliyomuingiza mjini na Jumatano anatarajiwa kukutana na Azam kwa mara ya kwanza tangu arejee Yanga.

Ngassa alikosa mechi za awali dhidi ya Azam FC msimu huu kwa sababu alikuwa anatumikia adhabu ya kufungiwa mechi sita kwa kosa la kuhamia Yanga SC akiwa ana Mkataba na Simba SC.

Mtoto huyo wa kiungo wa zamani wa Pamba FC ya Mwanza na Simba SC, Khalfan Ngassa ‘Babu’ anatarajiwa kuwa kivutio kikubwa kwenye mchezo wa Jumatano iwapo atacheza.

Kipa anayeonekana kuwa chaguo la kwanza Yanga chini ya kocha Mholanzi, Hans van der Pluijm, Deo Munishi ‘Dida’ aliyedaka mechi zote dhidi ya Al Ahly na kupangua penalti mbili Uwanja wa Border Guard, aliumia mkono siku moja kabla ya mechi na Mtibwa na Juma Kaseja akaziba vyema pengo lake.

Wazi sasa Kaseja ndiye atakayepewa jukumu la kuzuia michomo ya Azam Jumatano. Mchezaji mwingine atakayekosekana kwenye mchezo wa keshokutwa ni majeruhi wa muda mrefu, kiungo Salum Telela aliyefunga bao pekee katika mchezo wa Ngao.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa