Bajaber na Simba kwishinei
Klabu ya Simba SC imefikia makubaliano rasmi ya kuvunja mkataba na kiungo mshambuliaji raia wa Kenya, Mohamed Bajaber (23).
Uamuzi huo umekuja baada ya mchezaji huyo kuonekana kutokuwa kwenye mipango ya kocha mkuu wa Msimbazi, Steve Barker, jambo lililopelekea pande zote mbili kuridhia kutengana kwa amani. Bajaber tayari ameanza mchakato wa kutafuta changamoto mpya katika klabu nyingine.
