Simba nje Kagame Cup ikishinda 2-1
Timu ya Simba SC imefanikiwa kuambulia ushindi kwenye kombe la Kagame Cup baada ya kuifunga Singida Black Stars mabao 2-1 uwanja wa Amahoro jijini Kigali Rwanda.
Mabao ya Simba yamefungwa na Ibrahim Doumbia dakika ya 27 na Elie Mpanzu dakika ya 66 wakati goli la Singida lilifungwa na Mathew Tegisia Momanyi dakika ya 55 na timu zote zimeaga mashindano hayo kufuatia pointi zao hazikuivuka Jamus ambayo imeingia nusu fainali kwa kufikisha pointi 7
