Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UKICHEZA SIMBA AU YANGA NDIO UNACHAGULIWA TAIFA STARS- CASILAS

Na Prince Hoza

MLINDA lango wa kutumainiwa wa timu ya Mtibwa Sugar ya Manungu Turiani mkoani Morogoro Hussein Sharrif 'Cassilas' ambaye pia ndiye kipa bora wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara (2013/14) ameponda kauli zinazotolewa na wadau wa soka hasa baada ya yeye kutangazwa kipa bora.

'Mimi ndio kipa bora lakini siwezi kuitwa Stars labda niwe Simba, Yanga au Azam', anasema Casilas.


Casilas amelaani vikali baadhi ya wadau kuponda uteuzi wake wa kuwa kipa bora msimu uliomalizika wakati hayupo kwenye timu ya taifa, Taifa Stars.

Hivi karibuni mchambuzi wa soka na mdau maarufu Joseph Kanakomfumo amebeza uteuzi wake wa kuwa kipa bora wakati hayupo Stars, Kanakomfumo ameshangazwa na uteuzi huo na kudai imekuwa mara kwa mara kutoa tuzo kwa wasiostahili.

Lakini mlinda lango huyo ameipuuza kauli hiyo ya Kanakomfumo ambaye pia ni kocha kitaaluma, Casilas amedai kuwa kuna kasumba katika uteuzi wa timu ya taifa, Taifa Stars tena imeendelea kukithili.

Amesema ili uitwe timu ya taifa basi ni lazima uwe mchezaji wa Simba, Yanga au Azam fc, hivyo inawawia vigumu wachezaji kama wao kuonekana bora.'Nastahili kuwa kipa bora, lakini kuitwa kwenye timu ya taifa labda nichezee Simba, Yanga au Azam', alisema na kuongeza.

'Yamekuwa mazoea ya kuteua kikosi cha timu ya taifa kwa kufuata timu zenye majina makubwa ambazo ni Simba, Yanga na Azam fc, ila kama wangejali ubora wa mchezaji husika nasi wasingepata taabu kwani tupo kibao huku Mtibwa na kwingineko', aliongeza kipa huyo aliyelamba kitita cha shilingi Mil 5.

Kipa huyo ameponda uteuzi wa timu ya taifa ambaounatokana na majina na si uwezo wa mchezaji, na ndio maana maendeleo ya soka nchini yanadolola kutokana na uduni wa wachezaji.

Na ili timu ya taifa iungwe mkono na wengi basi ni bora wachezaji wakatokea Zimba, Yanga au Azam, kwani timu hizo tayari zimeota mizizi kwa mashabiki wengi wa soka nchini, Casilas anawaniwa vikali na Simba ingawa timu yake ya
Mtibwa imegoma kumuuza.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa