Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MALINZI AIKATAKATA YANGA, APINGA MANJI KUONGEZEWA MWAKA MMOJA

Wakati Shirikisho la Soka nchini (TFF) likiwa halijapokea rasmi maamuzi ya kusogeza mbele Uchaguzi Mkuu wa Klabu ya Yanga, Rais wa shirikisho hilo, Jamal Malinzi, amesema katika uongozi wake hataruhusu kuona wanachama wanafanya maamuzi yaliyo kinyume na katiba za vyama na klabu zao.

Wanachama wa Yanga waliokutana Juni Mosi, mwaka huu katika mkutano wa marekebisho ya katiba, pia walikubaliana kusogeza mbele uchaguzi mkuu wa klabu hiyo hadi Juni 15, mwakani.


Hata hivyo, baadhi ya wanachama wa Yanga wakiongozwa na Juma Magoma mwenye kadi namba 2319, wamepinga maamuzi hayo na kumuandikia Malinzi barua ya kutaka asaidie klabu yao ifanye uchaguzi ndani ya siku 90 na ili katiba yao isivunjwe.

Akizungumza kwa njia ya simu kutoka nchini Brazil jana mchana, Malinzi, alisema bado hajaiona barua hiyo ya wanachama wa Yanga iliyondikwa tangu Juni 5, mwaka huu na kupelekwa katika ofisi ya kiongozi huyo.

Malinzi alisema licha ya kutoipata barua hiyo kutokana na yeye kuwa nje ya nchi, uongozi wake muda wote utahakikisha wanachama wake wanafuata taratibu, kanuni na katiba zao.

"Kuhusiana na barua ya wanachama wa Yanga siwezi kusema chochote, niko kwenye mikutano ya CAF/Fifa, sijaiona barua hiyo," alisema kwa kifupi Malinzi.

Wanachama hao katika barua yao walisema kuwa kuruhusu viongozi waliopo kuendelea kuwaongoza kwa kipindi cha mwaka mmoja ni kudhihirisha wazi wote hawaifahamu Katiba ya Yanga, TFF na Baraza la Michezo la Taifa (BMT).

Alisema kwa mujibu wa Katiba ya Yanga uongozi unapomaliza muda wake madarakani na kulazimika kuongezewa, wanatakiwa kuongezwa muda wa siku 90 na baada ya hapo kuitishwa uchaguzi mkuu na si vinginevyo.

Naye Goefrey Mwaipopo (2481), alisema wanashangaa kuona Mama Fatma Karume anaitwa mdhamini wakati jina lake haliko kwenye orodha ya wadhamini wa klabu hiyo.

Viongozi wa Yanga ambao wanamaliza muda wao kikatiba wa miaka minne waliingia madarakani katika uchaguzi uliofanyika mwaka 2010, hivyo kwa kauli hiyo ya Malinzi kama ataitekeleza ni wazi Yanga watalazimika kufanya uchaguzi baada ya siku 90 na si mwakani kama walivyopitisha katika mkutano mkuu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa