Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UJUMBE WA FIFA KUTUA QATAR



Waandalizi wa kombe la dunia mwaka 2022 nchini Qatar wanatarajiwa kukutana na mchunguzi wa shirikisho la soka duniani FIFA, Michael Garcia hii leo huku kukiwepo wito kwa taifa hilo kunyimwa haki ya kuandaa mashindano hayo.

Jumapili, gazeti la SUNDAY TIMES la Uingereza, liliripoti kwamba mamilioni ya pauni zilitolewa kama malipo kwa maafisa waliounga mkono ombi la Qatar kuandaa michuano hiyo mwaka 2022, tuhuma ambazo Qatar imepinga vikali.
Habari zinazohusiana

Fifa imesema ombi jipya linapaswa kuruhusiwa iwapo tuhuma hizo za rushwa zitathibitishwa. Makamu wa Rais wa Fifa, Jim Boyce, anasema kuwa ataunga mkono hatua ya kupiga kura tena ikiwa madai hayo yatathibitishwa ili kuteua nchi nyingine.

Bin Hammam afisa wa soka Qatar ndiye anadaiwa kuwalipa hongo maafisa wa FIFA

Afisaa mmoja wa kamati ya FIFA, Lord Goldsmith, alisema kuwa ''Ikiwa itathibitishwa kuwa uamuzi wa kuipa Qatar idhini ya kuandaa kombe la dunia mwaka 2022 ulitokana na hongo kulipwa maafisa wa shirikisho la FIFA, basi uamuzi wa kuinyima nchi hiyo haki hiyo lazima uchukuliwe. ''

Aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa FA Mark Palios, anadhani kwamba rais wa FIFA Sepp Blatter anajitahidi kulinda kazi yake.

Garcia anatarajiwa kukutana na maafisa wa FIFA nchini Qatar. Wakili huyo anachunguza madai mengine ya tuhumza dhidi ya maafisa wa FIFA kuhusiana na kombe la dunia mwaka 2018 na 2022.

Jarida la Sunday Times, linadai kuwa maafisa wa soka walipokea hongo ya kima cha pauni milioni 3 ili waweze kuunga mkono azma ya Qatar kutaka kuandaa kombe la dunia mwaka 2022.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa