Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIRI YAGUNDULIKA KINACHOMUONDOA MANJI YANGA.

Na Salum Fikiri Jr

HATIMAYE siri imegundulika kwamba kinachomuondoa mwenyekiti wa mabingwa wa soka Tanzania bara Yanga Yusuf Manji kufuatia kauli yake aliyoitoa jana wakati viongozi wa timu hiyo walipokutana na kujadili mambo mbalimbali ikiwemo kuteua wajumbe wengine katika kamati mbalimbali zilizoundwa.

Siri iliyogundulika na kuelezwa Mambo Uwanjani kuwa mwenyekiti huyo atogombea tena Uenyekiti katika uchaguzi ujao na kuwapisha wengine wenye nia ya kutaka kuiongoza Yanga, lakini inasemekana Manji amekimbia kivuli chake huku suala la mheshimiwa Rage na klabu yake ya Simba moja kati ya sababu zinazomuondoa mapema Yanga.

Mbali na hilo msimamo wa baraza la wazee la klabu hiyo linaloongozwa na mzee Ibrahim Akilimali ambalo lilipinga waziwazi ajira ya Mkenya kuwa katibu mkuu wa Yanga pamoja na mtunza fedha ambaye alikuwa Mhindi, wazee hao waliendelea na msimamo wao na kupinga wazo la kuanzishwa kwa kampuni.


Inadaiwa wazee hawakutaka Yanga igeuzwe kampuni kitendo ambacho kilitaka kufufua mgogoro mkubwa kama ule wa mwanzo ambao ulizaa Yanga kampuni na Yanga asili, Hivyo Manji akaona Yanga haitawaliki na ni bora atangaze kujiondoa mapema na kuwapisha wengine kuongoza.

Chanzo chetu cha habari ambacho kipo karibu na watu wa timu hiyo kimesema kuwa maamuzi ya Manji yanatokana na sababu hizo, 'Manji alitaka Yanga iwe kampuni ili yeye aweze kununua hisa nyingi na kuimiliki timu hiyo kama ilivyo kwa timu nyingine kubwa za huko Uingereza ambazo zinaendeshwa na mfanyabishara mmoja tajiri.

Man United inaye Glazzer, wakati Chelsea inaye Abramovich, na Yanga ilitakiwa iwe na Manji, kilisema chanzo hicho, Aidha mwenyekiti huyo wa Yanga amekasirishwa na mambo mengi yanayofanyika klabuni hapo ikiwemo wazee kujifanya wao ndio wasemaji wa klabu badala ya mwenyekiti ambaye ni yeye na afisa habari wao.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa