Ruka hadi kwenye maudhui makuu

IVO MAPUNDA AIGEUKA SIMBA MWISHONI, AMWAGA WINO MWAKA MMOJA GOR MAHIA.

Wakati Simba ikieleza kuwa wameshamalizana na kipa chaguo la kwanza la timu ya Kilimanjaro Stars, Ivo Mapunda, na kilichobaki ni kusaini tu, mlinda mlango huyo amekanusha vikali na kuweka wazi kuwa anasaini mkataba mpya wa kuitumikia Gor Mahia.

Ivo, ambaye ni kipa namba mbili katika klabu hiyo mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Kenya na akiwa ameonyesha uwezo wa hali ya juu akiwa na timu yake ya Kilimanjaro Stars, amesema anatarajia kusaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuichezea Gor Mahia.

Akizungumza jana, Ivo alisema tayari viongozi wake wa Gor Mahia wamemfuata na kumueleza wanataka kumpa mkataba mpya.


Kipa huyo ambaye aliwahi kuichezea Yanga na Prisons zote za Tanzania Bara, akizungumzia suala la kuzungumza na viongozi wa Simba, alisema hajawahi kufanya mazungumzo nao.

Kadhalika alisema, amefurahi kuona ameitumikia vizuri timu yake ya Kilimanjaro Stars licha ya kutofika fainali ya mashindano ya Kombe la Chalenji.

"Nitabaki Gor Mahia kwa mwaka mwingine mmoja, walinipigia viongozi wangu wakataka kuja kambini nisaini, lakini nikawaambia wasubiri nimalize mashindano ya Kombe la Chalenji," alisema kipa huyo.

Hata hivyo, kipa huyo ambaye mashabiki wa Gor Mahia wamekuwa wakiushinikiza uongozi wa timu hiyo kumsajili, hakuwa tayari kutaja dau ambalo atapatiwa na klabu yake hiyo.

Mkataba wa awali wa Mapunda na Gor Mahia unatarajiwa kumalizika Desemba 16, mwaka huu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa