Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MESSI HATOENDA KOKOTE-ROSELL.

Staa matata wa Barcelona, Lionel Messi, hataenda popote katika utawala wa rais Sandro Rosell kiongozi huyo alitangaza Alhamisi.

"Kwa muda wote nitakuwa rais, lolote liwezekanalo au lisilowezekana litatendwa kuhakikisha Messi anasalia kitako hapa," Rosell alihimiza katika hafla ya kuwasilisha mkataba wa ushirikiano baina ya Barca na kampuni kuu ya elektroniki ya Marekani, Intel.

"Ni vigumu sana, au tuseme haitowezekana, kuwa Messi ataondoka timu hapa."

Mshindi mara nne wa tuzo la Ballon d' Or anauguza jeraha na anatarajiwa kurudi uwanjani Januari huku kandarasi yake Barcelona ikidumu hadi 2018 karibu na wakati nyota huyo atakuwa karibu kuadhimisha miaka 31 tangu kuzaliwa kwake.


Tetesi kuhusu hatima yake zilizuka Jumanne pale makamu wa rais wa maswala ya kiuchumi Barca, Javier Faus, alipofichua hakuna haja ya kujadilia kandarasi yake upya.

"Kwanini? Kandarasi yake Ilijadiliwa upya miezi sita pekee iliyopita," Faus aliambia kituo cha redio cha Rac1.

Kulingana na duru Uhispania, Messi ana kipengee cha Euro milioni 250 kwa yeyote anayetamani kumtia huru kutoka minyororo ya kandarasi yake na Barca injawaje timu zenye uwezo wa kutimiza hayo ni chache muno.

Uvumi kuhusu uwezekano wa mazungumzo mapya baina ya mshambuliaji huyu na klabu chake umezuka kutokana na swala la mishahara.

Mtana shari wake Real Madrid, Christiano Ronaldo, alisaini mkataba mpya wenye dhamani ya Euro milioni 17 kila mwaka kulingana na gazetu la Marca kumfanya awe mchezaji kabumbu anayelipwa kiasi kikubwa nchini hiyo.

Jarida la Forbes linashikilia Messi anatia kibindoni Euro milioni 16 kila mwaka kwa ulinganishi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa