Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SUAREZ AFURAHIA KUIWEKA LIVERPOOL KILELENI.

Luis Suarez alisherehekea mkataba wake mpya kwa kuiweka Liverpool kileleni Ligi ya Premia kwa kufunga mabao mawili na kutamba uwanjani wakati wa ushindi wa 3-1 Jumamosi dhidi ya klabu ya Cardiff City inayokabiliwa na mzozo.

Manchester City walisonga hadi nambari mbili licha ya bao la kujifunga la Vincent Kompany wakati wa ushindi wa 4-2 dhidi ya wanyonge Fulham nao mabingwa Manchester United, walio nambari saba, wakacharaza West Ham United 3-1 kupitia magoli ya Danny Welbeck, Adnan Januzaj na Ashley Young.

Suarez ambaye kwa sasa hashikiki, na aliyekuwa ameonekana kama ataondoka Anfield kipindi cha kuhama wachezaji kilichopita baada ya kupigwa marufuku kwa kumuuma mchezaji mwingine, alifunga bao la kwanza kwa ustadi mkali kasha akamwandalia Raheem Sterling la pili baada ya kupokea mpira mzuri kutoka kwa Jordan Henderson ambaye sasa ameamka.


Muda mfupi baadaye, mambo yalikuwa 3-0 baada ya Suarez kufunga bao lake la 19 ligini msimu huu kipindi cha kwanza kikiisha. Alilifunga kwa kupinda kombora kutoka nje tu ya eneo la hatari baada ya kupewa mpira wa kisigino na Henderson.

Liverpool walirarua Tottenham Hotspur 5-0 ugenini wikendi iliyopita na wangepata mabao mengi dhidi ya Cardiff kwani Suarez nusura afunge lake la tatu lakini akapokonywa na mlingoti wa goli.

"Nina furaha kutokana na mkataba mpya lakini macho yangu yote yalikuwa kwenye mechi. Tulicheza vyema kipindi cha kwanza,” straika huyo wa Uruguay aliambia kituo cha televisheni cha BT Sport.

"Ni mapema kusema (kwamba tunaweza kushinda ligi). Ni muhimu kwetu kuendelea kuangazia mechi inayofuata. Tunapocheza nyumbani, tumekuwa imara.”

Ushindi huo dhidi ya Cardiff ambao wamo nambari sita kutoka mwisho, na meneja wao aliye matatani Malky Mackay, uliwapeleka Liverpool alama moja juu kwenye jedwali wakiwa na alama 36 utoka kwa mechi 17.

Arsenal (alama 35), ambao wako nambari tatu, wanaweza kutwaa tena nambari ya kwanza wakishinda nyumbani dhidi ya Chelsea (33) walio nambari nne Jumatatu (2000 GMT).

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa