Bodi ya Ligi Tanzania na Mali waenda kujifunza Yanga
Uongozi wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania ukiambatana na wageni wao kutoka Bodi ya Ligi ya Mali, umefika katika Klabu ya Yanga kwa ziara yenye lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu namna klabu inavyojiendesha.
Katika ziara hiyo, wageni hao wamepata fursa ya kufahamu mifumo ya uendeshaji wa klabu, usimamizi wa shughuli za kila siku, maendeleo ya biashara na masoko, matumizi ya teknolojia, pamoja na namna Yanga inavyosimamia chapa yake na kuwahudumia mashabiki
Wageni hao wamepokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Yanga SC, Andre Mtine










